Professional Documents
Culture Documents
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI I M
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI I M
MWANGA
wa
Kwa Shule Za Upili
i
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
ISBN 978-9966-100-13-9
Mpangilio na Uchapishaji
Ingawa kila juhudi imefanywa kuhakikisha kuwa kitabu hiki kimeboreshwa zaidi, makosa machache yanaweza kutokea.
Hivyo basi usisite kutufahamisha ili tufanye marekebisho.
ii
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Yaliyomo
Shukrani…………………………………………………….................….….…. iv
Dibaji…………………………………………………………….................….… vi
Sura ya kwanza
Mapisi ya ushairi wa Kiswahili…………………………………................…….. 1
Dhana ya ushairi……………………………….………………..............………. 3
Sifa za ushairi…………………………………..…………………..............……. 3
Umuhimu wa ushairi………………………………………………............….… 3
Changamoto za ufundishaji na usomaji wa ushairi……………….................…. 4
Jinsi ya kutatua changamoto hizi……………………………………..............… 4
Sura ya pili
Istilahi mbalimbali zinazotumika katika ushairi…………………….................. 5
Sura ya tatu
Migao/kategoria kuu za ushairi……………………………………...............….. 8
Mashairi ya jadi…………………………………….………………................…. 8
Mashairi huru………………………………………………………...............…. 9
Sura ya nne
Bahari za mashairi………………………………………………….............….. 11
Sura ya tano
Uhakiki wa mashairi…………………………………………….............…….. 26
Sura ya sita
Idhini/uhuru wa kishairi…………………………………………...........……. 31
Sura ya saba
Mkusanyiko wa mashairi……………………………………………............… 34
Msururu wa maswali ya KCSE tangu 2008- 2016
KCSE 2016..................................................................................................... 66
KCSE 2015……………………………………………………………........… 70
KCSE 2014……………………………………………………………........… 72
KCSE 2013…………………………………………………………….......…. 74
KCSE 2011…………………………………………………………….......…. 76
KCSE 2010……………………………………………………………........… 79
KCSE 2009……………………………………………………………............ 80
KCSE 2008…………………………………………………………...........…. 83
Marejeleo………………………………………………………………....… 102
iii
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shukrani
Natoa shukrani za dhati kwa wazazi wangu Silas Were na Pamela Adhiambo,
kwa kuenzi masomo, mke wangu Wanjiru, kwa uvumilivu wake, Dkt. George
Lutomia na mwandani Binti Elvera Tumaini, ushauri walonipa ulinifaa pakubwa.
Jamii ya Shule ya Upili ya Wasichana ya St.Mary’s Mumias, hususan Mwalimu
Mkuu Bi. Kwendo Adema Rosemary. Sitowasahau Bw. Ofunya Charles Wangatia,
Mkuu wa Idara-Shule ya Upili ya Wasichana ya St. Mary’s Mumias na Bw. Issa
Barasa- St. Peter’s Mumias Boys, kwa kukubali kupitia na kukihakiki kitabu hiki,
na wengine wote mlochangia katika kukifanikisha kitabu hiki, Karima awajalie!
iv
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Tabaruku
Toleo hili ni tunu maalum kwa mamangu Pamela Adhiambo.
v
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Dibaji
Kwa miongo kadhaa iliyopita, waandishi wengi wa vitabu vya Kiswahili
wamekuwa wakishughulikia kipengele cha sarui na kusahau kazi za kifasihi,
ushairi ukiwa mojawapo. Kuikia leo hii, ushairi haujatiliwa maanani mno licha
ya kuwa ni sehemu mojawapo inayotahiniwa katika hadhi ya kitaifa katika
karatasi ya tatu. Utanzu wa ushairi umepitia mabadiliko mengi tangu uanze
kufanyiwa utaiti.
Vipo vitabu ambavyo hutumiwa katika kufundishia ushairi wa Kiswahili katika
shule za sekondari, ingawaje ni dhahiri shahiri kwamba bado pana haja ya
kitabu ambacho kitaoana na kazi za waandishi wengine ili kukidhi mahitaji ya
wanafunzi katika udurusu wao wanapojiandaa kufanya mitihani ya kuhitimu
masomo ya sekondari.
Mwanga wa Ushairi kwa Shule za Upili ni kitabu ambacho kimeandikwa ili
kuziba mwanya ulioshamiri katika ufunzaji na ujifunzaji wa ushairi. Kitabu hiki
kinaangazia masuala yote muhimu yanayohitajika katika uwanja huu wa ushairi.
Kitabu hiki kimeandikwa kwa utaalamu wa kutosha ili kuwawezesha wanafunzi
kufanya maandalizi bora wanapojitayarisha kwa mtihani wa Kiswahili hasa
ushairi katika KCSE. Kitabu hiki vilevile ni cha kipekee kwa kuwa kinashirikisha
maswali na majibu ya mitihani ya K.C.S.E tangu mwaka wa 2008-2016, hivyo
basi kumpa mtahiniwa nafasi bora zaidi ya kujiandaa vilivyo kabla ya mtihani.
Ni matumaini yangu kuwa kitabu hiki kitachangia pakubwa katika kuendeleza
ubunifu wa kutunga mashairi na vilevile kuboresha usomi na ufundishaji wa
ushairi wa Kiswahili kwa ujumla.
Duncan M. Were
Idara ya Kiswahili
Shule ya Upili ya Wasichana ya St. Mary’s, Mumias
Januari, 2017
vi
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
MWANGA WA USHAIRI
Uga ninaufungua, niruhusu ukumbini,
Kishairi nafungua, walio bara na pwani,
Ushairi kuangua, na kutopendwa barani,
Ugumu wake ni upi, ushairi kutopendwa?
vii
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Nina Wahasiri
Nimekwepa Penzi
Manung’uniko Kote
Silalamiki Nidatie
Kamwe Mtetezi
Moyoni Wangu
Kinyongo Kweli
Sina Kesharudi
Naapa Nitulie
Mimi
viii
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
1
DHANA YA USHAIRI
Shabaha
1
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Katika kipindi hiki pia, nyingi ya mashairi yalikuwa yenye maudhui ya kidini
hasa dini la Kiislamu. Watunzi wengine wa kipindi hiki ni Bwana Mataka, Ali
Koi, Muhammad Kijumwa na Hemedi Abdallah.
b) Kipindi cha utasa (1885-1945)
Huenda kipindi hiki killitwa hivi kwa sababu maandishi machache yaliandikwa
wakati huu.Huu ulikuwa ni wakati wa vita vya dunia, na mataifa mengi
yakigawana Afrika. Sheria za utunzi wa mashairi zilianza kutozingatiwa.
c) Kipindi cha urasimi mpya (1945-1960)
Mashairi yaliyotungwa katika kipindi hiki aghalabu yalikuwa yanafuata kanuni/
arudhi. Washairi waliotawala kipindi hiki ni Amini Abedi, Shabaan Robert,
Mathias Mnyampala miongoni mwa wengine mashuhuri. Wao walikuwa na
itikadi kuwa ili utungo uitwe shairi, sharti liweze kuimbwa, hivyo lazima liwe
na urari wa vina, mizani inayolingana pamoja na masuala mengine ya kiarudhi.
Kipindi hiki pia kilishuhudia washairi chipukizi wapya kuanza kuibuka.
d) Kipindi cha sasa (1967 kuendelea)
Hiki ni kipindi cha leo hii ambapo pana mgogoro kati ya wanamapokeo na
kundi nyingine la wanamapinduzi.Wanamapokeo wanashikilia mitazamo ya
jadi kuwa shairi lazima lifuate arudhi, nao wanamapinduzi wanapinga suala hili.
Kulingana na wao, muhimu ni ujumbe ambao shairi linabeba bali si muundo wa
shairi. Mashairi mengi wanaotunga wanamapinduzi ni mashairi huru. Washairi
wa kipindi hiki ni pamoja na Euphrase Kezilahabi, Kithaka wa Mberia, Alamin
Mazrui, Mugyabuso Mulokozi kati ya wengineo.
Mwandishi Kezilahabi pia ametoa maoni sawa na haya kuhusu hatamu
mbalimbali ambazo Ushairi wa Kiswahili umepitia. Naye vipindi hivi ameviita
muhula katika Diwani yake. Kezilahabi anaeleza kuwa katika muhula wa
sasa, uhuria umetawala. Idadi ya washairi imeongezeka, idadi ya mashairi pia
imeongezeka na ubora wa mashairi kuimarika. Katika kipindi cha sasa, ushairi
umekuwa sanaa ya umma na mambo yafuatayo yanabainika wazi:
Mashairi huru ni mengi
Mashairi yanahusisha drama/maigizo
Ushairi wa vijana unaosaili yaliyopo katika jamii
Ushairi umebadilika kuendana na hadhira, hivyo basi unachanganywa
na ngoma
Ushairi umeendelea katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
(TEKNOHAMA)
2
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Dhana ya Ushairi
Wanafunzi wengi hushindwa kueleza maana ya ushairi. Dhana ya ushairi
inaweza kufafanuliwa kwa njia kadhaa.
Ushairi ni mojawapo wa utanzu wa fasihi andishi unaoelezea mawazo mazito
kuihusu jamii na ulio na mpangilio mahsusi wa maneno yenye mtiririko, lugha
ya mkato na urembo fulani wa aina yake.
Ni sanaa inayotambulishwa na mpangilio maalum wa vifungu ambao una
mdundo maalum na aghalabu hutumia lugha ya mkato.
Shairi ni utungo wa kisanaa ambao hutumia lugha teule na kushirikisha
mpangilio maalum wa maneno ili kuwasilisha ujumbe uliokusudiwa. Ni tungo
za kishairi zenye maudhui maalum yanayomhusu mwanadamu na tabia zake.
Sifa za ushairi
Sifa ni upekee fulani unaojitokeza katika kazi yoyote ile. Ushairi huwa na upekee
wa aina yake ukilinganishwa na kazi nyinginezo za fasihi. Hivyo basi utanzu wa
ushairi huwa na sifa kuu zifuatazo:
Hutumia lugha teule na ya mkato.
Hutumia tamathali tofauti tofauti za usemi.
Sio lazima ufuate kaida za kisarui.
Lugha iliyotumiwa huweza kuibua hisia, yaani hugusa moyo wa
anayesoma.
Huwa na mpangilio maalum kuanzia kwa vina, mizani, mishororo na
beti.
Huweza kukaririwa ama kuimbwa
Huelezea mambo yanayohusiana na imani za watu katika jamii.
Umuhimu wa ushairi
Mashairi huwa na umuhimu anuwai katika jamii. Baadhi yazo ni pamoja na:
3
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
4
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
2
ISTILAHI ZA USHAIRI
Istilahi mbalimbali zinazotumika katika ushairi
Tumeeleza chini ya sifa za ushairi kuwa utanzu huu huwa na upekee fulani. Hili
vilevile linadhihirika tunapoangazia istilahi za kishairi. Mwanafunzi bora ni
yule anayeweza kutumia istilahi za kishairi anapochambua na kuyajibu maswali.
Istilahi za kishairi ni misamiati bainifu ambazo hutumika kurejelea masuala ya
ushairi. Istilahi hizi ni kama zifuatazo:
Mizani – ni idadi ya silabi au sauti zinazotamkika katika kila mshororo wa
ubeti. Mashairi mengi ya arudhi aghalabu huwa na mizani 16 ingawaje huwa
siyo lazima. Rejelea mifano inayofuata inayoonyesha mizani katika mshororo.
Ku ru ki a si ku zu ri, ma ne no mu si ru ki e, (mizani 16)
1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16
Mu ta ku ja zu sha sha ri, ma ko nde mu ya bu gi e, (mizani 16)
Vina – ni silabi za mwisho wa kila kipande cha mshororo. Huainishwa kama
vina vya ndani/kati ama vina vya nje/mwisho. Vina huweza kufanana ama
kutofautiana. Iwapo shairi lina vipande ziadi ya viwili, vina huainishwa kutegemea
vipande kwa mfano vina vya ukwapi, vina vya utao, vina vya mwandamizi na
6
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
7
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
3
KATEGORIA ZA MASHAIRI
Migao/Kategoria kuu za mashairi
Mashairi huweza kugawika katika kategoria mbili kuu:
1) Mashairi ya jadi
2) Mashairi huru
Mashairi ya jadi.
Mashairi haya pia huitwa mashairi ya kimapokeo au ya kiarudhi. Aina hii ya
• urari wa vina
mashairi hufuata kaida za utunzi wa mashairi. Kanuni hizi ni kama vile:
•
•
Lina mishororo sawa (minne) katika kila ubeti
•
Mizani inajitosheleza katika kila mshororo (mizani 16)
•
Vipande ni sawa (viwili, yaani ukwapi na utao) katika kila mshororo
Lina beti tatu zinazojitosheleza.
Mashairi huru/za kisasa
Ni kategoria ya mashairi yasiyozingatia kanuni za utunzi. Hii ina maana ya
kwamba kanuni zilizoorodheshwa chini ya mashairi ya kimapokeo siyo lazima
zifuatwe. Aghalabu mashairi haya huzingatia maudhui kwa kina. Kila malenga
huwa na mtindo wake tofauti wa kuwasilisha kazi yake. Wanaoshikilia msimamo
huu nao huitwa wanamapinduzi. Mashairi haya pia huitwa mapingiti/mavue/
masivina/zuhali/za kimapinduzi. Hebu tazama shairi lifuatalo.
Nimeyaandika maneno haya
kwa niaba ya,
Mamilioni wasio malazi
Wazungukao barabarani bila mavazi
Wabebao vifurushi vilivyo wazi,
… milki yao ya maisha.
Kwa niaba ya:
Maelfu wanaovuma bila haki
Wiki baada ya wiki
Leo sumu au spaki
Leo kamba au bunduki
Na kwa wale wanasubiri kunyongwa
Kwa niaba ya
Vijana walio mtaani
Wale mayatima na maskini
Wazungukao mapipani
Kila pembe mjini
Kuokota sumu kutia tumboni
Kujua bila kujua
’ili kupata kuishi.
Kwa niaba ya:
Wakongwe wasiojiweza
Walao chakula kilichooza
Wachukuao choo wakijipakaza
Pole pole wakijiangamiza
Katika vyumba vyao
Baridi na giza
Kwa saba hawan watazama
Wala wauguza
9
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
10
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
4
BAHARI ZA MASHAIRI
Mojawapo wa maswali yanayotahiniwa katika ushairi ni kueleza bahari ya
shairi. Je nini maana ya bahari? Bahari za mashairi ni neno ambalo hutumiwa
kurejelea zile mikondo mbalimbali za mashairi kwa kutegemea sura ya shairi
lenyewe. Bahari ni aina mojawapo ya tungo za mashairi ambazo huainishwa
kwa mujibu wa sifa zake. Uainisho wa bahari za mashairi hutegemea pakubwa
vigezo mbalimbali ambavyo vimeangaziwa hapa chini. Vigezo hivyo ni kama
vifuatavyo:
Kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti
Kulingana na idadi ya vipande katika mshororo
Kulingana na vina
Kulingana na mpangilio wa maneno
Kulingana na mizani
Kulingana na idadi ya mishororo katika ubeti
Aina za mashairi
Mashairi huwa ni ya aina mbalimbali. Ili kueleza shairi ni la aina gani, kigezo cha
idadi ya mishororo katika kila ubeti ndicho hutumiwa. Kwa kuzingatia kigezo
hiki, tunapata aina zifuatazo za mashairi.
Tathmina/umoja – ni shairi lenye mshororo mmoja kaika kila ubei.
Mashairi ya aina hii hayapaikani kwa wingi. Vielelezo vifuatavyo vinaashiria
aina hii ya shairi.
1._________________________, _________________________
2._________________________, _________________________
3._________________________, _________________________
4._________________________, _________________________
5._________________________, _________________________
Tathnia/uwili – ni shairi lenye mishororo miwili katika kila ubeti. Mashairi
haya ingawaje yapo, lakini pia kwa uchache. Tazama vielelezo vifuatavyo;
1_________________________, _________________________
_________________________, _________________________
2_________________________, _________________________
_________________________, _________________________
3_________________________, _________________________
_________________________, _________________________
11
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
4_________________________, _________________________
_________________________, _________________________
Mfano huo unaonyesha shairi la beti nne, mishororo miwili katika kila ubeti na
kisha vipande viwili katika kila mshororo.
Tathlitha/utatu/wimbo – ni shairi lenye mishororo mitatu katika kila ubeti.
Shairi la aina hii wakati mwingine pia huitwa wimbo. Tazama shairi lifuatalo;
1. Wakale metenda mengi, milele ya kukumbuka,
Walioanzisha misingi, ambayo yaaminika,
Waleo hutupingi, baadhi tungekenka.
Malenga wa Vumba
B. Amana Uk.63,O.U.P 1982
12
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
14
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Sababu tumezidia,
Kuacha ya asilia,
Kazi ilotimilia,
Ambayo imetukuka.
15
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Ukishajijua wazi,
Kuwa wewe huna kazi,
Yapunguze matembezi,
Kuzurura ni mashaka,.
Ni kalamu mfukoni,
Suti na tai shingoni,
Twautaka ukarani,
Mashamba twayaepuka.
Tunapokaa mezani,
Shamba atalima nani,
Kisha tutakula nini,
Inataka kukumbuka.
Ni bure wanaosema,
Kudharau ukulima,
Na hali dunia nzima,
Ukulima wasiika.
(Limenukuliwa)
b) Mathnawi
Ni bahari ambapo shairi huwa na vipande viwili katika kila mshororo yaani
ukwapi na utao. Shairi lifuatalo linaonyesha mfano wa bahari hii ya shairi.
KILA MCHIMBA KISIMA
1. Tenda utendapo tendo, tenda tendo kwa hekima,
Lindamane mwenendo, sawa na yakio kalmia,
Kalmia yenye upendo, kufurahisha mtima,
Kila mchimba kisima, budi hungia mwenyewe.
16
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
c) Ukawai
Ni bahari ambapo shairi huwa na vipande vitatu katika kila mshororo yaani
ukwapi, utao na mwandamizi. Tazama mfano ufuatao.
HAKI
1. Haki watutisha, tusikuandame, kwa matendo yetu,
Watukoroisha, tusikuandame, kila penye kitu,
Mbona watugwisha, miba ituchome, kwenye huu mwitu,
Tutokwe na utu!
2. Hatutakufanya, mwana kwa mvyele; aliyemzaa,
Haki watunyima, machumi ya mbele, na nyingi hadaa,
Tuchumayo nyanya, uchungu umbele, hatuna wasaa,
Haki twashangaa!
3. Na kambi nzima, kunaiyenea, hasa hapa petu,
Tunakutazama, kwa kuulizia, kuweza thubutu,
Na kwenye milima, ilotueka, kupandia watu,
Usifanyekatu!
(Suleiman A. Ali)
4. d) Bantudi/Tuo
Ni bahari ambapo shairi lina vipande vinne katika kila mshororo yaani ukwapi,
utao, mwandamizi na ukingo. Hebu tazama vielelezo vifuatavyo vinavoonyesha
mfano wa bahari hii ya shairi.
(ukwapi) (utao) (mwandamizi) (ukingo)
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
______________,________________,_______________, _______________
17
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Kulingana na vina
Vina ni silabi za mwisho wa kila kipande cha mshororo. Huainishwa kama vina vya
ndani/kati ama vina vya nje/mwisho. Vina huweza kufanana ama kutofautiana.
Kutokana na kigezo hiki, bahari zifuatazo za mashairi zinadhihirika wazi.
a) Mtiririko
Katika bahari hii, shairi huwa na vina vya kati/ndani na vilevile vina vya nje
ambavyo havibadiliki katika utungo mzima. Hii ina maana kuwa vina vya ndani
vinafululiza katika beti zote na vilevile vina vya nje pia vinafululiza katika beti
zote. Shairi lifuatalo linaelezea mfano wa shairi katika bahari hii.
Ndege akiwa angani, usiseme wangu mie
Mngoje atuwe chini, na ndipo mgombanie
Lakini yupo hewani, tama isikwingie
Sigombee kivulie, ndege apaa angani.
Ndege apaa angani, sigombee kivulie
Mnapigana machoni, mwagombea uzurie
Mwalizana kama nyani, matunda mwagombeae
Sigombee kivulie, ndege apaa angani.
Shika awe mkononi, ndipo ukajivunie
Umshikapo mwilini, chukua kajifugie
Kama utavyo moyoni, kufuga ama mwachie
Sigombee kivulie, ndege apaa angani.
(Mathias Mnyapala)
b) Ukara
Bahari hii ya shairi huwa na vina vya kipande kimoja ambavyo havibadiliki
katika utungo mzima, lakini vina vya kipande kingine vinabadilika kutoka ubeti
hadi mwingine. Hebu tazama vielelezo vifuatavyo.
_________________________sa, ________________________ta
_________________________sa, ________________________ta
_________________________sa, ________________________ta
_________________________sa, ________________________la
_________________________sa, ________________________la
_________________________sa, ________________________la
Katika hicho kielelezo cha hapo juu, vina vya ndani ambavyo ni ‘sa’ ndivyo
havibadiliki lakini vina vya nje vinatofautiana kutoka ubeti hadi ubeti. Zingatia
mfano huu wa pili hapa chini ambapo sasa vina vya kati vinabadilika kutoka
ubeti hadi ubeti ilhali vina vya nje havibadiliki.
18
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
19
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Mke________________________ _ , _____________________________
_____________________________ , _____________________________
_____________________________ , _____________________________
_____________________________ , _____________________________
20
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Mzigo______________________, ________________________
___________________________, ________________________
___________________________, _____________________beba
Beba_______________________, ________________________
___________________________, ________________________
___________________________, ____________________cheza
21
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
22
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
__________________________, _________________________
__________________________, _________________________
__________________________, _________________________
__________________________, _________________________
__________________________
__________________________
__________________________
__________________________
__________________________
__________________________
Hapa, ubeti wa kwanza una mishororo mitatu, ubeti wa pili una mishororo
mitano, ubeti wa tatu mishororo ni minne ilhali ubeti wa nne una mishororo
sita. Hivyo basi kuna bahari mbalimbali katika utungo mmoja.
Ngonjera
Ni shairi la majibizano. Tofauti na tungo nyinginezo, ngonjera hukaririrwa,
haziimbwi. Ngonjera hutambuliwa kwa kuwepo kwa wahusika wanaojibizana
katika utungo. Pia huambatana na vitendo. Kwa mfano, ubeti wa kwanza mzazi
akazungumza kisha ubeti unaofuata mwanawe akamjibu. Zingatia shairi hili.
Babu: Jina hili limevuma , mjini shambani pia
Gazetini wanasema, mara nyingi hutokea
Nashindwa pa kutuama , makelele yamejaa
Ukimwi ninauliza , kitu hiki kitu gani?
Bibi: Sihangaike bwanangu, jambo hilo kutuhusu
Dunia ina mizingu, shika yanayotuhusu
Mambo mengi chunguchungu, ni vigumu kudurusu
Ukimwi nimesikia, kila mtu yuataja
Babu: Nikifungua radio, matangazo yazagaa
Kenya nayo hata hio, Tanzania yaongea
Jihadhari na kinoo, Ukimwi ukisambaa”
Ukimwi ninauliza, Kitu hiki kitu gani?
Bibi: Jambo umeshikilia , Ukimwi sijui nini?
Shika njia kimbilia , Uliza wanake nini?
Mashaka yamezidia , Waweweseka ndotoni?
Nyuma tusijiachie , mashaka kujiwekea
Babu: Ni vyema tuutambue, twende kwa wanaojua
Akili watufumbue, tufahamu ya dunia.
Nyuma tusijiachie, mashaka kujiwekea.
Ukimwi ninauliza, kitu hiki kitu gani?
23
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
24
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Togoo
Ni aina ya shairi ambalo limetungwa kwa kusudi la kusiia uzuri wa mahali, mtu
au kitu fulani.
Kumbukizi
Ni aina ya shairi ambalo huwakumbusha watu kuhusu matukio mahsusi katika
jamii. Matukio haya yaweza kuwa ya kihistoria, kidini au hata kishujaa. Kwa
mfano ujio wa Rais wa Marekani nchini Kenya, ujio wa Papa Mtakatifu (2015)
ni matukio ya kihistoria.
25
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
5
UHAKIKI WA MASHAIRI
Uhakiki wa mashairi (Namna ya kuchambua mashairi)
Ili kuyachambua mashairi, ni lazima kuzingatia mambo muhimu yafuatayo;
Dhamira
Maudhui
Muundo
Lugha
a) Dhamira
Mara si haba, wanafunzi hukumbana na swali hili…‘Eleza dhamira ya shairi hili.’
Dhamira ni lengo kuu ambalo malenga huwa nalo anapoitunga kazi yake. Lengo
la mtunzi linaweza kuwa kuelimisha jamii, kuikosoa jamii, kutahadharisha,
kufariji, kuhamasisha n.k Maneno mengine ambayo huweza kutumika badala
ya dhamira ni kama vile lengo, nia, kusudi, azma.
b) Maudhui
Suala la maudhui ni muhimu sana katika uchambuzi wa mashairi na hata kazi
nyinginezo zozote za fasihi. Maudhui ni ujumbe mkuu unaowasilishwa katika
kazi ya fasihi. Maudhui huweza kuwa kama vile ya ndoa, migogoro, elimu,
matabaka, ukengeushi n.k
c) Muundo
Ni kawaida vilevile wanafunzi kuulizwa…‘Eleza muundo wa hili shairi.’
Muundo ni mjengo, umbo au sura ya shairi. Umbo hubainishwa kwa kuonekana
bayana kama alivyoandika mtunzi. Mwanafunzi anapolijibu swali hili anastahili
kuangalia shairi na kuandika tu anayoyaona. Hastahili kuikiria kwa kina ili
kuandika anayoyaona.
Ili kueleza muundo wa shairi, mwanafunzi anafaa kuzingatia mambo
yafuatayo;
•
•
Je shairi lina beti ngapi?
•
Je shairi lina mishororo mingapi katika kila ubeti?
•
Je shairi lina vipande vingapi katika kila mshororo?
Je shairi lina vina vya kati na vya nje, na kuna urari wa vina au
la?
26
•
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
•
Je idadi ya mizani ni ngapi katika kila kipande au mshororo?
Shairi lina kibwagizo au kituo? Iwapo lina kibwagizo, basi nakili
kibwagizo moja kwa moja
d) Lugha
Matumizi ya lugha na viambajengo vyake ni muhimu sana katika kufanikisha
uchambuzi bora wa mashairi. Jinsi malenga mmoja anavyotumia lugha ni tofauti
sana na jinsi malenga mwingine atakavyoitumia. Kipengele hiki huchunguza
jinsi mtunzi ametumia tamathali za usemi. Lugha pia huendeleza maudhui ya
shairi. Tamathali hizi ni pamoja na;
Tashbihi/mshabaha- ni mbinu ya lugha ambapo vitu viwili
hulinganishwa kwa njia isiyo ya moja kwa moja. Kwa ufupi,ni ulinganisho
isiyo wa moja kwa moja kwa kutumia vilinganishi kwa mfano: mithili
ya, kama, ja na sawa na. Tazama mfano huu:
Juma ni mrefu mithili ya/ja mlingoti.
Uhaishaji/uhuishi/tashihisi- ni mbinu ambayo vitu visivyo na uhai
hupewa sifa za kibinadamu. Mfano: Kaburi likammeza mzima mzima.
Misemo na nahau- ni kauli fupifupi ambazo hutumika kutoa maana
nyingine pasi na maana iliyotumika. Misemo huwa haitumii vitenzi
kwa mfano: mkono birika- mchoyo, mkono mrefu-mwizi n.k. Nahau
hutambulishwa kwa matumizi ya vitenzi kwa mfano: kula kalenda-
fungwa jela, chungulia kaburi- karibia kifo n.k
Takriri/anafora- mbinu ya kurudiarudia neno,tukio au mawazo Fulani.
Takriri huweza kuwa za aina mbalimbali kama vile
Takriri sauti- sauti fulani hurudiwarudiwa.
Takriri neno- neno/kifungu cha maneno fulani hurudiwarudiwa,
Takriri mawazo- mawazo fulani hurudiwarudiwa.
Takriri muundo/usambamba ambapo muundo fulani wa
kisintaksia hurudiwarudiwa. Malenga hutumia takriri hususan
kusisitiza ujumbe.
Maswali balagha/mubalagha- huwa ni maswali yasiyohitaji majibu.
Tanakuzi- pia huitwa ukinzani. Hapa mawazo yanayokinzana hutumiwa
pamoja katika sentensi moja. Kwa mfano; baada ya dhiki faraja, mpanda
ngazi hushuka, nazama nakuibuka.
Tanakali za sauti- mbinu hii pia hujulikana kama onomatopeia.
Maneno yanayoiga sauti au hali fulani hutumika. Mfano kuanguka
majini chubwi.
Methali- huwa ni misemo ya hekima na ambayo maana yake imefumbwa.
Katika ikisiri yake, Joseph Nyehita anaangazia kuwa matumizi ya
methali yanapozingatiwa, ushairi wa Kiswahili unaweza kuainishwa
zaidi kwa kuzingatia kutumiwa au kutotumiwa kwa methali. Anasema
27
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
kusisitiza ujumbe fulani.
Tasida- ni matumizi ya lugha ya adabu ili kuicha makali ya lugha.
Mfano kujifungua mtoto badala ya kuzaa, kuenda haja badala ya kuenda
chooni.
Kinaya- hapa mtunzi huleta dhana ya kinyume cha matarajio. Kwa
mfano badala ya kiongozi alichaguliwa kutetea maslahi ya watu wake
akawa wa kwanza kuwanyanyasa. Kuna aina kadhaa za kinaya kama vile
kinaya cha kiusemi na kinaya hali. Kinaya cha kiusemi ni hali ambapo
maana inayokusudiwa huwa kinyume cha kile kinachosemwa. Katika
kinaya hali matokeo huwa kinyume cha matarajio.
Jazanda- matumizi ya lugha iche au ya mafumbo. Msomaji huhitajika
kuwaza maana kamili iliyokusudiwa. Kwa mfano paka na panya kwa
maana ya watawala na watawaliwa, Mdudu hatari kurejelea ugonjwa wa
UKIMWI.
Tabaini- matumizi ya neno “si” pamoja na maneno kinzani. Kwa mfano:
Alikuwa si wa maji si wa dawa.
Utohozi- mbinu ya kuswahilisha maneno yasiyo ya lugha ya Kiswahili.
Mfano “school”- skuli, “Class”- klasi
Sitiara/sitiari- huu ni ulinganisho wa vitu au hali mbili kwa njia ya
moja kwa moja kwa sababu vitu hivi vina sifa au tabia sawa. Mfano:
Mwalimu mkuu ni simba, Maria ni twiga.
Taashira/Ishara - mbinu ambapo mtunzi hutumia lugha ya ishara
kuwakilisha ujumbe fulani. Kwa mfano mvi kuashiria mtu mzee.
Taswira- ni mbinu ambapo mtunzi hutoa maelezo ambayo huibua
picha ya kitu au hali fulani akilini mwa msomaji. Kuna aina kadha za
taswira kama vile:
Taswira mnuso/harufu- k.m rihi ya maua
28
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
29
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Mandhari na wakati
Mandhari ni mazingira au muktadha au mahali ambapo shairi fulani hutungiwa.
Mandhari na wakati huenda sambamba. Kutokana na maudhui ya shairi,
tunaweza kubaini ni wapi na ni lini shairi lilitungwa. Mifano ya mandhari ni
kama vile Pwani, mjini, shuleni n.k. Hivyo basi mandhari na wakati husaidia
kuendeleza maudhui ya shairi. Kwa mfano katika shairi la Mnazi na Vuta n’
kuvute, mandhari ni ya Pwani.
Uhusika katika ushairi
Mashairi pia huweza kuwa na wahusika haswa tukirejelea ngonjera na
malumbano hivyo basi ni muhimu kulitilia maanani suala hili. Wahusika huwa
kama sauti ya mwandishi maanake ni kupitia kwao ambapo mtunzi hueleza
mawazo yake bayana.
Tasnifu
Haya ni maelezo mafupi ambayo mwandishi wa kazi ya fasihi huyatoa kuhusu
maudhui na dhamira yake katika utungo.
Lugha ya nathari/Lugha tutumbi/mjalizo
Hili ni swali ambalo aghalabu halikosi kwenye maswali ya ushairi. Mwanafunzi
ataulizwa...Andika ubeti fulani katika lugha ya nathari. Lugha ya nathari ni
lugha ya kawaida. Huwa ni maandishi mfululizo. Ubeti uandikwe kwa aya moja
ama kwa njia ya kiinsha bali si ya kishairi. Mishororo igeuzwe iwe sentensi za
Kiswahili sanifu zinazozingatia kanuni za lugha. Sehemu zilizorudiwarudiwa
ziandikwe mara moja tu. Usitumie lugha ya mshairi.
30
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
6
UHURU WA KISHAIRI
Idhini/Uhuru wa kishairi
Kazi za sanaa huhitaji ubunifu wa hali ya juu. Hali hii hupelekea wakati mwingine
watunzi kuenda kinyume na kaida za matumizi ya lugha kimaksudi. Jambo hili
huibua dhana ya uhuru wa kishairi. Uhuru wa kishairi ni idhini au ruhusa ya
mwandishi kutunga shairi kwa namna fulani bila kuzingatia kanuni za kisarui.
Uhuru wa kishairi huhusisha yafuatayo:
1) Mazida – uhuru huu humruhusu mtunzi kuyarefusha maneno fulani.
Mazida husaidia kuleta utoshelezo wa idadi ya mizani katika kipande
au mshororo na pia urari wa vina.
2) Inkisari – huu ni uhuru wa mshairi kuyafupisha maneno fulani. Kama
ilivyo katika mazida, inkisari pia husaidia kutosheleza idadi ya mizani
na kuleta urari wa vina.
3) Tabdila – ni uhuru wa mshairi kubadilisha herui au hata sauti ya neno
bila kubadili maana ya neno hilo. Kwa mfano daraza badala ya darasa.
Tabdila husaidia kuleta urari wa vina katika kipande cha mshororo.
4) Kuboronga/kuinyanga/Kubananga sarui – pia huitwa miundo
ngeu/ukiushi wa kisintaksia/ukiushi wa kimiundo. Huu ni uhuru wa
mshairi kutofuata kanuni zinazotawala sarui. Kusudi la kufanya hivi ni
kuleta urari wa vina katika mishororo. Kwa mfano, kunapopambazuka
kila, amka mwanadamu badala ya kila kunapopambazuka,
mwanadamu amka
5) Kikale – ni matumizi ya msamiati wa kale, kwa mfano, nyuni badala ya
ndege, mgunda badala ya shamba n.k
6) Vilugha/vilahaja – ni matumizi ya msamiati wa lahaja za Kiswahili
badala ya Kiswahili sanifu.
7) Utohozi – kutohoa ni kuswahilisha msamiati wa lugha nyingine na
kuwa Kiswahili. Kwa mfano, klasi badala ya class, eropleni badala ya
aeroplane, deski badala ya desk n.k.
32
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Subuhana
f) Andika majina mawili ya Mungu kwa mujibu wa shairi.
Rabana
Jabaruti
g) Kwa kutolea mifano, eleza mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika shairi
Balagha
hili
Tashbihi
- k.v Vipi tungelisongana, tunaoishi tiati?
- ikawa kama ya kuti
33
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
7
MKUSANYIKO WA MASHAIRI
Maswali
a) Onyesha mpangilio wa vina katika ubeti wa nne.
b) hibitisha matumizi ya pindu katika shairi hili
c) Taja, ueleze na utoe mfano wa mbinu zozote mbili za uhuru wa ushairi
zinazodhihirika katika shairi hili.
d) Toa mifano miwili ya uradidi katika shairi.
e) Kuna madhara gani kwa mtu anayerukia maneno?
f) Fafanua dhamira ya mshairi
34
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
35
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
a) Eleza dhamira ya shairi hili.
b) Kwa kutoa mifano, eleza aina mbili za idhini ya kishairi alizotumia
mshairi
c) Kwa kurejelea ubeti wa tatu taja na ueleze tamathali ya usemi na mbinu
ya kimuundo.
d) Huku ukitoa mifano, eleza kwa kifupi mwelekeo wa mshairi kuhusu
vibarua.
e) Andika ubeti wa tano katika lugha ya nathari.
f) Onyesha utata wa maana katika matumizi ya Kibaruwa Manamba.
36
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
a) Lipe shairi hili kichwa mwafaka
b) Shairi hili ni la bahari gani. Toa sababu.
c) Fafanua dhamira za shairi hili
d) Onyesha muundo wa shairi hili
e) Taja na ueleze tamthali tatu za lugha zilizotumika katika shairi hili
f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi
i) fumanizo
ii) mwambuzo
38
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
39
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
40
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
42
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) “Shairi hili ni la kukatisha tamaa”. Fafanua dai hili kwa kutoa mifano
minne.
(b) Eleza umbo la shairi hili
(c) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari
(d) Taja tamathali ya usemi iliyotawala katika shairi zima utoe mifano miwili
ya jinsi ilivyotumika
(e) Onyesha mifano miwili ya ubabadume inayojitokeza katika shairi hili
(f) Eleza maana ya maneno yafuatayo jinsi yalivyotumiwa katika shairi:
(i) mzima utashi
(ii) maungoni
43
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shairi 7, E. Kezilahabi
Dhamiri imenifunga shingoni.
Nami kama mbuzi nimefungwa
Kwenye mti wa utu. Kamba ni fupi
Na nimekwishachora duara.
Majani niwezayo kuikia yote nimekula.
Ninaona majani mengi mbele yangu
Lakini siwezi kuyaikia: kamba, kamba.
Oh! Nimefungwa kama mbwa.
Nami kwa mbaya bahati, katika
Uhuru kupigania, sahani ya mbingu
Nimeipiga teke na niigusapo kwa mdomo
Mbali zaidi inakwenda na siwezi tena
Kuiikia na hapa nilipofungwa
Nimekwishapachafua na kuhama siwezi.
Kamba isiyoonekana haikatiki.
Nami sasa sitaki ikatike, maana,
Mbuzi wa kamba alipofunguliwa, mashamba
Aliharibu na mbwa aliuma watu.
Ninamshukuru aliyenifunga hapa
Lakini lazima nitamke kwa nguvu “Hapa nilipo sina uhuru!”
Maswali
a) Lipe shairi kichwa mwafaka
b) Taja mambo manne ambayo mshairi analalamikia.
c) Kwa nini mshairi haoni haja ya yeye kuwa huru?
d) Eleza maana ya mshororo ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi.
“Kamba isiyoonekana haikatiki.”
e) Taja na utoe mifano ya aina mbili za tamathali zilizotumika katika shairi hili.
f) Kwa kutoa mifano miwili, eleza jinsi matumizi ya mishata yanavyojitokeza
katika shairi hili.
g) Andika ubeti wa pili kwa lugha tutumbi.
44
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
45
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shairi 9, E. Kezilahabi
KISU MKONONI
Wakati miaka inaibwa mmoja mmoja,
Kurudi nyuma, kusimama, kupunguza mwendo
Siwezi, kama gurudumu nitajiviringisha
Mtelemko mkali huu
Lini na wapi mwisho sijui
Mbele chui mweusi, nyuma mwanga
Nionako kwa huzuni vifurushi maelfu ya dhambi
Kisu! Maisha kairi haya
Kama kutazama nyuma na mbele
Ni kufa moyo mzima!
Sasa kama Simba - Mtu shauri nimekata
Ya nyuma sana nisijali, ya mbele sana niyakabili
Kwa ujasiri na uangalifu nitazunguka
Nikifuata kamba kama ng’ombe aliyefungwa,
Kila mpigo wa moyo wangu
Huu mpigo muziki wa maisha
Maswali
a) Hili ni shairi la aina gani?
b) Taja sifa mbili za shairi la aina hii.
c) Eleza toni ya shairi hili.
d) Eleza ujumbe wa mtunzi kwa kifupi
e) Kwa kutolea mifano taja tamathali mbili za usemi zinazojitokeza katika shairi hili.
f) Mhusika katika shairi hili ana matatizo gani?
g) Ni kwa namna gani mhusika katika shairi ananuia kutatua matatizo yake?
h) Mtunzi ana maana gani anaposema
(i) Wakati miaka inaibwa mmoja mmoja
(i) Kama simba – mtu shauri nimekata
46
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Lipe shairi hili anwani mwafaka
(b) Eleza muundo wa shairi hili.
(c) Onyesha maovu yanayoendelezwa na anayerejelewa.
(d) Huku ukitoa mifano miwili eleza uhuru wa kishairi alioutumia msanii.
(e) Mshairi anatoa ushairi gani katika shairi?
(f) Andika ubeti wa 3 katika lugha nathari.
(g) Eleza maana za maneno haya kama yalivyotumika katika shairi.
(i) Lasakama
(ii) Limeota pembe
48
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
50
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Mjukuu
Nyanyangu wanifahamu, toka mwangu utotoni,
Wewe kwangu u mkimu, wa nasaha duniani,
Ela taasubi kamu, chungua wako uneni,
Imepitwa na wakati, na masomo ya kisasa.
Nyanya
Naona nimekwelewa, usemayo mjukuu,
Ni kweli tumechelewa, na dhana yenye mafuu,
Naenda uloamuwa, kwa mamako ninukuu,
Tohara za wanawake, zina madhara makuu.
51
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
a) Pendekeza anwani mwafaka kwa shairi ulilolisoma.
b) Fafanua umbo la ubeti wa pili.
c) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu.
d) Eleza bahari mbili za shairi hili.
e) Malenga alikuwa na lengo lipi alipolitunga shairi hili?
f) Jadili maudhui makuu yanayojitokeza katika shairi.
g) Fafanua msimamo wa mjukuu kuhusu tohara ya wanawake.
52
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
53
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
54
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
a) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu
55
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Shairi hili ni la aina gani?
(b) Ni nani mzungumzaji katika shairi hili?
(c) Eleza taswira inayochorwa na mzungumzaji katika shairi hili.
(d) Eleza toni ya shairi hili na uonyeshe inavyochangia kuupitisha ujumbe wa
shairi.
57
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Chambua maudhui ya shairi hili.
(b) Kuna uhusiano gani kati ya muundo wa shairi hili na maana yake.
(c) Shairi la aina hii linaitwaje?
(d) Eleza muundo wa shairi hili.
(e) Toa mifano ya mishata katika shairi hili.
59
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Kwa nini msanii alilitunga shairi hili?
(b) Taja mambo mawili yanayoweza kupelekea kiburi mintaarafu ubeti wa
kwanza?
(c) Nini sababu ya mtunzi kunadi kuwa kiburi hakifai?
(d) Fafanua muundo wa shairi hili.
(e) Yanakili majina ya Mwenyezi Mungu yaliyodhukuriwa shairini.
(f) Tambua methali mbili alilozidokeza mtunzi.
60
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
61
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Beti hizi zimekusudiwa nini?
(b) Nakili
(i) Utao wa mloto wa ubeti wa pili
(ii) Ukwapi wa mleo wa ubeti wa tano
(c) Yaorodheshe matendo manne yanayoonyesha tamaa.
(d) Taja hasara zinazomkabili mja mwenye tamaa.
(e) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu.
(f) Fafanua bahari tatu za shairi hili.
(g) Idhini ya kishairi humruhusu msanii kuitumia lugha pasi kujali sana.
hibitisha kwa kurejelea vipengele viwili kati ya vifuatavyo mintaarafu shairi
hili.
(i) Inkisari
(ii) Tabdila
(iii) Kuboronga sarui
(h) Andika ubeti wa tatu kwa lugha mjalizo.
(i) Eleza msamiati ufuatao kufungamana na shairi.
(i) Uazizi
(ii) Akaivunda
(iii) Dua
(iv) Kasi
62
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
63
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
64
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Maswali
(a) Eleza aina ya shairi hili.
(b) Shairi hili ni la bahari gani? Kwa nini?
(c) Fafanua umbo la shairi hili.
(d) Pendekeza anwani nyingine ya shairi hili.
(e) hibitisha kuwepo kwa matumizi ya udhini ya ushairi katika shairi hili.
(f) Ni vipi sharia za utunzi/arudhi zilivyotumika kwa mujibu wa hili shairi.
(g) Eleza mbinu tatu za lugha alizotumia mshairi.
(h) Ni maudhui yapi yanayojitokeza katika shairi hili?
(i) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha tutumbi.
65
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
66
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
67
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shairi la 2
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
T. Arege: Barabara
Barabara bado ni ndefu
Nami tayari nimechoka tiki
Natamani kuketi
Ninyooshe misuli
Nituliza akili
Lakini
Azma yanisukuma
Mbele ikinihimiza kuendelea
Baada ya miinuko na kuruba
Sasa naona unyoofu wake
Unyoofu ambao unatisha zaidi
Ingawa nimechoka
Jambo moja li dhahiri
Lazima nifuate barabara
Ingawa machweo yaingia
Nizame na kuibuka
Nipande na kushuka
69
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2015
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Daima alfajiri na mapema
Hunipitia na jembe na kotama
Katika njia iendayo kondeni
Kama walivyofanya babuze zamani;
Nimuonapo huwa anatabasamu
Kama mtu aliye na kubwa hamu
Kushika mpini na kutokwa jasho
Ili kujikimu kupata malisho.
Anapotembea anasikiliza
Videge vya anga vinavyotumbuiza
Utadhani huwa vimemngojea
Kwa usiku kucha kuja kumwimbia;
Pia pepo baridi kumpepea
Rihi za maua zikimletea
Nao umande kumbusu miguu;
Na miti yote hujipinda migongo
kumpapasa,kumtoa matongo;
Na yeye kuendelea kwa furaha
kuliko yeyote ninayemjua
Akichekelea ha ha ha ha ha ha …
T. Arege: Mwili
Leo kitaka niike, natamani, ila wauma mwili
Kwa kazi nihusike, samahani, unahiliki mwili
Napenda nihesabike, makundini, ila huwezi mwili.
Vitisho kamwe kelele, ninavicha, kwa nafsi na mwili
Ila ugonjwa utimile, umechacha, na kuudhili mwili
Msikose simile, magalacha, si gurudumu mwili.
Vingekuwepo viraka, kuutia, ngeushuruti mwili
Kifundi kivipachika, kuingia, hata kuridhi mwili
Upya ukaungilika, kuvutia, roho na wake mwili.
Lakini kamwe haiwi, kuvipata, vipande vyake mwili
Sihofu kupata mawi, sitajuta, kupigania mwili
Hata kufutwa sikawi, nitakita, kidete nao mwili.
Kazi ninaithamini, ni hakika, akilini na mwili
Ila kamwe siamini, kusagika, damu, jasho na mwili
Uwele hususani, kioneka, nguvu hitishi mwili.
a) Eleza dhamira ya mtunzi wa shairi hili. (alama 4)
b) Fafanua mbinu nne za lugha zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 8)
c) Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
d) Ni nani anayezungumziwa na nafsineni katika shairi hili? (alama 1)
e) Eleza bahari ya shairi hili kwa kurejelea vipande. (alama 2)
f) Andika ubeti wa mwisho kwa lugha ya nathari. (alama 3)
71
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2014
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Amiri A. S. Andanenga: Sauti ya Kiza
1 Ngakua na mato, ya kuonea 6 Kwa yangu mabega, nikathubutu
Ngalisana kito,cha kuchezea Ngabeba maiga, yalo matatu
Kilicho kizito, cha kuelea Bila hata woga, kwenye misitu
Kikamuenea, akivae. Simba tembo chatu, sinitishie.
2 Makusudi yangu,ngaliandaa 7 Miti yenye pindi,na jema umbo
Ngainyanga chungu, cha mduwaa Ngajenga ulindi, mwema
Ngatia vitangu,vinavong’aa wimbombo
Ili ziwe taa, kwa apikae. Fundi aso fundi, penye kiwambo
Moyo wenye tambo, apekechae.
3 Mkungu wa tano, wa mduwara
Ulo bora mno, kisha imara 8 Singaajiri, ngachimba mimi
Ulo na maono, kuwa ni dira Kisima kizuri, cha chemchemi
Kwenye barabara, itindiae. Maji ya fahari, ya uzizimi
Jua la ukami, siyaishae
4 Ngaomba Baraka, kwake Rabana
Punje za nafaka, kila aina 9 Tamati nafunga, kwa kuishia
Chunguni kuweka, kwa kulingana Mato ndo malenga, kanikimbia
Hajaangu suna, yule alae. Nahofu kutunga, mabeti mia
5 Ngafanya bidii, kwenda mwituni Asije chukia, ayasomae.
Sio kutalii, kukata kuni
Ya miti mitii, huko jikoni
Isio na kani,ni iwakae.
(a) Eleza ujumbe wa shairi hili. (alama 2)
(b) Kwa kurejelea ubeti wa pili, eleza umuhimu wa aina mbili za uhuru wa
kishairi aliotumia mshairi. (alama 4)
(c) Andika ubeti wa saba kwa lugha ya nathari. (alama 4)
(d) Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
(e) Fafanua aina tatu za urudiaji zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 6)
(f) Bainisha nafsi neni katika shairi hili. (alama 2)
72
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
73
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2013
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Sinongi aushi yangu, hii leo, kwa ukungu wa ujana,
Nikaiga rika langu, kwa vileo, na mbio za wsichana,
Kiwa ni riziki yangu, mapokeo, kuoa na kuona,
Ni wakati utanena.
Nashukuru kwa ugumba, wenye ndimi, wanipazao nao,
Wapitao wakiimba, eti mimi, ningapenda hali zao,
Haupandiki mgomba, wana nyemi, isadi wa hadhi zao,
Eti ni kwa raha zao.
Ni lipi lenye kukera, kwa Muumbi, marufuku kwenye misa,
Ni mtu kuwa hawara, wa vitimbi, ama alozawa tasa?
Ugumba na ukapera, sio dhambi, wala haujawa kosa,
Waama sina makosa
Bora tungeni vitabu, magazeti, mutangaze kwa rediyo,
Muwaite watribu, kina Siti, watuzwa ilimu hiyo,
Na zaidi muhutubu, kwa umati, muwambe ambayo siyo,
Kwalo sichafuki moyo
Hidhuru yote ni bure, sio kitu, kudhiki asodhikika,
Siwi nikaona ghere, lailatu, nyota njema itaika,
Kwa shangwe na njerejere, kila mtu, mdomo utafumuka,
Akiri amejibika.
(Mwalaa M. Nyanje)
(a) Eleza jambo ambalo mzungumzaji (nafsineni) katika shairi hili anasingiziwa.
(alama 2)
(b) Fafanua mambo matano ambayo mzungumzaji (nafsineni) anapinga katika
shairi hili. (alama 5)
(c) Eleza umuhimu wa viishio vya beti za shairi hili. (alama 2)
(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha ya nathari. (alama 4)
(e) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 5)
(f) Bainisha matumizi mawili ya tafsida katika shairi hili. (alama 2)
74
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
2. Japo aula kushufu, na machoni vyavutia, 6. Nambie faida gani, nambie ipi idi?
Dunia wana dhaifu, waugua nisikia, Upatayo hatimani, waja wakikufukia,
Vijana nawasarifu, falau mkisikia, Ilakufa kama nyani, kasoroyako mkia,
Ukiona vyang’aria, tahadhari vitakula. Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.
3. Jepusheni na zinaa, mlale penye sheria, 7. Kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia,
Msije andama baa, makaa kujipalia, Ujifanye kama kwamba, u jiwe huna hisia,
Jepusheni na zinaa, madhara kukadiria, Wakwambe watalokwamba, kwa lolote vumilia,
Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula. Uonapo vyang’aria, tahadhari vitakula.
75
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2011
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
KUJITEGEMEA
1 Nchi ni ile ambayo, imekita ardhini 3 Twaishije tujihoji, wanachi humu nchini
Siyo ile iombayo, ghaibu na majirani Kila tunachohitaji, kupatakwe ugenini
Taratibu siyo hiyo, wanachi twambizaneni Hiyo ni tete haviji, tongo tupangusaneni
Daima hukaa chini, maganja ya mpewaji Daima hukaa chini, maganja ya mpewaji
2 Chumo lote na mitaji, leo lirao maganjani 4 Kuomba wataalamu, ni mwendo hauh’ngani
Bepari na wanyonyaji, wasalie maguguni Tupate wa humu humu, wajuzi wa kila fani
Shime utekelezaji, vingine havifanani Mbele washike hatamu, kwa mapimo na makini
Daima hukaa chini, maganja ya mpewaji Daima hukaa chini, maganja ya mpewaji
76
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
HAKI
1. Haki watutisha, tusikuandame, kwa matendo yetu,
Watukoroisha, tusikuandame, kila penye kitu,
Mbona watugwisha, miba ituchome kwenye huu mwitu,
Tutokwe na utu!
2. Hatutakufanya, mwana kwa mvyele; aliyemzaa,
Haki watunyima, machumi ya mbele, na nyingi hadaa,
Tuchumayo nyanya, uchungu umbele, hatuna wasaa,
Haki twashangaa!
3. Na kambi nzima, kunaiyenea, hasa hapa petu,
Tunakutazama, kwa kuulizia, kuweza thubutu,
Na kwenye milima, ilotueka, kupandia watu,
Usifanyekatu!
4. Sio hao mabwana, waloteuliwa, kupata mwangaza,
Haki wakubana, lilotarajiwa, kwenye hichi kiza,
Ndevu kuchomana, wengine kuliwa, tukijiingiza,
Kambi yatuviza!
5. Haki buna njia, kizuizi mali, ndio njia panda,
Tukiifatia, hatuiki mbali, wengi tunaganda,
Sio yetu nia, lakini akili, mali ishapenda,
Haki yatuponza!
6. Wala hutasemwa, sababu ni nyoyo, kwisha haribika,
Ya mali kuchumwa, vyovyote iwavyo, itavyopatika,
Wakati mtumwa, ushatumwa ndivyo, na ushatuika,
Kwetu nimashaka!
7. Haki hufanyiki, papitapo mambo, na vikubwa visa,
Watu hawataki, kutenda kijambo, tunu yao pesa,
Sisi kwetu dhiki, yatunisha tumbo, wao hata hisa,
Nandio ya sasa!
8. Haki husimami, kwa viumbe sisi, tuvyojaaliwa,
Na huna ulimi, kuweza tukisi, tukageukiwa,
Zama za uchumi, zishashika kasi, nguvu zishapewa,
Haki wauliwa!
9. Iwe hivi haki, hakuna mmoja, akukumbukae,
Hatuna ashiki,kuvutalahaja,haki ituvae,
Mbona hatutaki, twalia na tija, haki iambae,
Haki tamati!
(Suleiman A. Ali) Malenga Wapya
77
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
78
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2010
Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata.
Dhamiri yangu
Dhamiri imenifunga shingoni.
Nami kama mbuzi nimefungwa
Kwenye mti wa utu. Kamba ni fupi
Na nimekwishachora duara.
Majani niwezayo kuikia yote nimekula.
Ninaona majani mengi mbele yangu
Lakini siwezi kuyaikia: kamba, kamba.
Oh! Nimefungwa kama mbwa.
Nami kwa mbaya bahati, katika
Uhuru kupigania, sahani ya mbingu
Nimeipiga teke na niigusapo kwa mdomo
Mbali zaidi inakwenda na siwezi tena
Kuiikia na hapa nilipofungwa
Nimekwishapachafua na kuhama siwezi.
Kamba isiyoonekana haikatiki.
Nami sasa sitaki ikatike, maana,
Mbuzi wa kamba alipofunguliwa, mashamba
Aliharibu na mbwa aliuma watu.
Ninamshukuru aliyenifunga hapa
Lakini lazima nitamke kwa nguvu
“Hapa nilipo sina uhuru!”
(E. Kezilahabi)
(a) Taja mambo manne ambayo mshairi analalamikia. (alama 4)
(b) Kwa nini mshairi haoni haja ya yeye kuwa huru? (alama 2)
(c) Eleza rnaana ya mshororo ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi.
“Kamba isiyoonekana haikatiki.” (alama 2)
(d) Taja na utoe mifano ya aina mbili za tamathali zilizotumika katika shairi hili.
(alama 4)
(e) Kwa kutoa mifano miwili, eleza jinsi matumizi ya mishata
yanavyojitokeza katika shairi hili. (alama 4)
(f) Andika ubeti wa pili kwa lugha nathari. (alama 4)
79
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2009
Soma shairi kisha ujibu maswali yanayofuata:
KIBARUWA: Abdilatif Abdalla
Kwenye shamba hilo kubwa asilani hakunyi mvuwa!
Ni kwa mitilizi ya jasho langu ndiyo hunweshezewa
Kwenye shamba hilo kubwa sasa imeshaiva kahawa
Na bunize ni matone ya damu yangu niliyotowa
Ndipo mte ukatipuza!
Buni hiyo itakaangwa buni hiyo itapondwapondwa
Buni hiyo itasagwa na buni hiyo itafyondwafyondwa
Bali itabaki nyeusi kama ngozi yangu Kibaruwa
Waulize ndege kwa nyimbo nyanana watutumbuizao
Iulize na mito kwa furaha maji itiririkao
Uulize na upepo mkali kwa ghadhabu uvumao-.
Viulize: Ni nani araukaye na mapema kuzitema mbuga na kuzilaza?
Viulize: Ni nani akweaye minazi tangu kuchapo hadi lingiapo giza?
Viulize: Ni nani abebeshwaye mizigo hadi maungo yakageuka shaza?
Halfuye hana faida moja apatay wala malipo yanayotosheleza-
Isipokuwa kusundugwa na kutupiwa matambara na vyakula viliyooza?
Viulize: Ni nani huyo ni nani!
Viulize: Ni nani aliyemaye mashamba na kuyapoliliya?
Na mimea kochokocho ikajaa kwa uzito ikajinamiya?
Hatimaye nani atajirikaye mali yakammiminikiya
Akatoa na kitambi kama mja mzito wa miezi tisiya
Na akaongeza magari na wanawake kutoka na kuingiya?
Viulize: Ni nani huyo nani1
Na hao ndege kwa nyimbo nyanana watutumbuizao
Nayo hiyo mito kwa furaha maji itirikao
Na huo upepo mkali wenye ghadhabu uvumao
Vyote hivyo vitatu vitakujibu kawa umoja wao
“Ni Kibaruwa Manamba ndiye mtendaji hayo!”
a) Eleza dhamira ya shairi hili. (alama 2)
b) Kwa kutoa mifano, eleza aina mbili za idhini ya kishairi alizotumia mshairi
(alama 4)
c) kwa kurejelea ubeti wa tatu taja na ueleze tamathali ya usemi na mbinu ya
kimuundo mshairi (alama 4)
d) Huku ukitoa mifano, eleza kwa kifupi mwelekeo wa mshairi kuhusu
vibarua. (alama 4)
80
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
81
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
82
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2008
Soma shairi hili kisha ujibu maswali yanayofuata.
WASAKATONGE
1. Wasakatonge na juakali
Wabeba zege ya maroshani,
Ni msukuma mikokoteni,
Pia makuli bandarini,
Ni wachimbaji wa migodini,
Lakini maisha yao chini
2. Juakali na wasakatonge
Wao ni manamba mashambani,
Ni wachapa kazi viwandani,
Mayaya na madobi wa nyumbani,
Ni matopasi wa majaani,
Lakini bado ni masikini.
3. Wasakatonge na juakali
Wao huweka serikalini,
Wanasiasa madarakani,
Dola ikawa mikononi,
Wachaguliwa na ikuluni,
Lakini wachaguaji duni
4. Juakali na wasakatonge
Wao ni wengi ulimwenguni,
Tabaka lisilo ahueni.
Siku zote wako matesoni,
Ziada ya pato hawaoni,
Lakini watakomboka lini?
(Mohammed Seif Khatib)
(a) “Shairi hili ni la kukatisha tamaa”. Fafanua rai hii kwa kutoa mifano minne.
(alama 4)
(b) Taja tamathali ya usemi iliyotawala katika shairi zima na uonyeshe mifano
miwili ya jinsi iiivyotumika. (alama 3)
(c) Eleza umbo la shairi hili. (alama 5)
(d) Andika ubeti wa tatu katika lugha ya nathari. (alama 4)
(e) Onyesha mifano miwili ya maadiii yanayojitokeza katika shairi hili.
(alama 2)
(f) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi.
(i) Manamba
(ii) Tabaka lisilo ahueni (alama 2)
83
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Inkisari- msamiatiwe
(e)
Utohozi- risavuni
Mazida- Huria
Tabdila- maa- mama
Kilugha/lahaja- kiimanya
(f) Nafsineni ni mwanalugha/mtetezi/mkereketwa wa lugha
(g)
(i) nasongwa- nasumbuliwa/dhulumu/sikitika/nabanwa
(ii) kuriaria- kuzurura/kurandaranda
(iii) adinasi- binadamu/insi/mahuluki
84
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shairi la 2
(a) Toni ya kuhimiza/matumaini/matarajio
(b) Msairi/mwenye matumaini katika maisha
(c) Kuwa tayari kupambana na misukosuko utakayokutana nayo
(d)
Taswira- miinuko
Tasihisi- azma kunihimiza
Tanakuzi- zama na kuibuka
Taashira- barabara- maisha, miinuko- ugumu
Jazanda/stiari- barabara
(e) Nafsineni ni Mcha Mungu- dini
(f)
kuruba- mahangaiko/mateso
barabara yenye ukungu- misukosuko
85
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2015
Shairi la 1
(zozote 4x1=4)
(2x1=2)
Kuhuzunisha/kusikitisha/kuhurumia
linalomridhisha?
(yoyote 1x1=1)
Kuzindua wafanyakazi
(4x1=4)
87
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
88
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2014
Sauti ya kiza
Urudiaji wa silabi ra ra ra /a, a, a, /ngu, ngu, ngu n.k
Urudiaji wa maneno ulo- ubeti wa 3, mato ubeti wa 1, 9
Usambamba/urudiaji wa vishazi/urudiaji wa miundo sawa ya
mistari mf. ngaliinyanga chungu, cha mduwaa.
(Kutaja al. 1, mfano al. 1 za kwanza 3x2=6)
f) Kipofu/mtu asiyeona. Ubeti wa 1 anasema, ngakua na mato.
(Kutaja al.1, kueleza al. 1)
Watafuta riziki
Wenye kujiamini
Waliopuuzwa/hawana makubwa (hawasikiki)
Hawana tamaa
Wenye kupinga ulaghai/wa kweli
89
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Wenye ndoto haizimiki
Hawahini/ huwapa watu haki yao/ waaminifu
Wazalendo
Wanaohangaika/ wanaoteseka kupata/ wanaosumbuka
(za kwanza 5x1=5)
Utohozi- mf.wiki
mizani/kupunguza idadi ya mizani
(3x1=3)
90
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2013
Shairi la 1
a) Mzungumzaji (nafsineni) anasingiziwa ugumba hasa kwa kutoshiriki
mapenzi nje ya ndoa. (1x2=2)
Kiishio kimefupishwa.
mwingine.
91
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Shairi la 2
wanaoingilia zinaa kwa kauli kama vile ‘wawapi leo madume, anasa
Kukejeli/kudharau/stihizai/bezo
anawaambia, ‘kikiki ikaze kamba, u kijana vumilia.’ Ubeti 7
93
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2011
Kujitegemea
a)Umuhimu wa nchi kujitegemea/tatizo la mikopo na uombaji. (alama2)
Ni tarbia/unne
b)
(alama 1)
wa vina.
Kuboronga sarui
AU
(alama 2)
-twaishije tujihoji
-tongo tupangusaneni
-mbele washike hatamu
-shujaa itakiavyo
-kondo tujiamueni.
e) Shughuli zote za kiuchumi ziko mikononi mwa wananchi na wakoloni
pamoja na wanyonyaji wametengwa kando bila kitu kwa hivyo ni muhimu
kufanva bidii maana hakuna njia nyingine ya kujiendeleza kwa kuwa daima
mwombaji wa heshima. Kila siku kuzembea na kukaa/kusubiri kupewa/
kusaidiwa. (Hoja4xl=4)
94
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Haki
a) Ukosefu wa haki ulimwenguni/jinsi haki inavyokosekana maishani
(alama 2xl=2)
Kuweza kuikiri/kusema/kubusu/kutetea
nyuma
(al 2)
95
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2010
Dhamiri yangu
Kufugwa
a)
Kunyimwa uhuru
Alipofungwa pameharibika
Angependa kuhama lakini hawezi
Kuna majani mengi mbele yake lakini hawezi kuyaikia - chakula
Analalamikia upungufu wa chakula/njaa/sahani imeenda mbali
(4 x 1 = 4)
Tashihisi/Uhuishi/uhaishaji
- uhuru!
- Dhamiri imenifunga
- Sahani kwenda mbali
AU
Mshairi analalamika kufungwa kwake kama mbwa. Katika harakati zake
za kupigania uhuru na kufanikiwa kuupata alichotaka hata akizidisha bidii.
Mahali alipofungwa amepachafua na hawezi kupaondoka. (alama 4)
97
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2009
Kibaruwa
a) Maisha ya wafanyakazi na vibarua shambani ni duni na ilhali wanaofaidika ni
wengine. (al.2)
Tamathali mf.
c)
98
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
Mtu humfunza mwana ndipo mwana awe na heshima ili yeyr kama
kujivunjia heshima
99
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
KCSE 2008
Wasakatonge
Tabaka la chini ndio walio wengi katika jamii na ndio tegemeo la jamii
kunyanyua hali za waliowachagua
Kinaya
b)
Taswira
dobi, mayaya, wachapakazi)
Takriri
ix) Mayaya na madobi wa nyumbani (siku zote wako matesoni)
i) wasakatonge
ii) Juakali
iii) Lakini
iv) Wao
v)
Ulingunuzi/ulinganushi
Ni
Kipande kimoja
c)
Beti 4
Mishororo 6 kila ubeti/ tasdisa / usita au kila uneti una kichwa au
101
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
MAREJELEO
Abedi, K.M. (1954) Sheria za Kutunga Mashairi na Diwani ya Amri.
Nairobi: Kenya Literature Bureau.
Arege, T. (2013) Tunu ya Ushairi. Nairobi: Oxford University Press.
Arege, T. (2016) Fani ya Ushairi kwa shule za Upili. Nairobi: Oxford
University Press.
Kezilahabi, E. (1973): “Diwani ya Massamba”, katika MULIKA Na. 13.
Dar es Salaam: TUKI.
Kitula, K na Amata, K. (2001) Taaluma ya Ushairi. Nairobi: Acacia Stantex
Publishers.
Khasiani, D. (2014) Mwongozo wa KCSE Fasihi. Nairobi: Vide- Muwa Publishers
Limited.
Mohamed, S.A. (1980) ’Sikate Tamaa. Nairobi: Longman Publishers.
Mulokozi, M.M. na Kahigi, K.K. (1973) Mashairi ya Kisasa. Dar es Salaam:
Tanzania Publishing House.
Mutali, C.S. na Mbugua, D. (2004) Uhakiki wa Mashairi. Nairobi: JB Publishers.
Walibora, K. (2007) Malenga wa Karne Mpya. Nairobi: Phoenix Publishers Ltd.
102
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
103
MWANGA WA USHAIRI KWA SHULE ZA UPILI
104