Professional Documents
Culture Documents
Mualiko
Mualiko
Foundation in RMNCAH
McF - 043
23 Agosti 2023
Kwa heshima, tungependa kutambulisha taasisi isiyo ya kiserikali ya Maternal Care Foundation (McF)
yenye usajili namba 00NGO/R/3226. Taasisi hii inajihusisha na uelimishaji wa afya na imejikita kwenye
kuimarisha afya ya wanawake na watoto kupitia kuchangia kwenye kupunguza vifo na ulemavu
vinavyozuilika kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
Tunatarajia kuwa na hafla jumuishi ya taasisi zinazotoa huduma za afya ya mama na mtoto. Hafla hii ya
maonyesho haya itafanyika tarehe 2 mwezi wa 9, katika viwanja vya maegesho ya gari ya Mlimani City.
Hafla hii imebeba kauli mbiu "Naimarisha Afya ya Mama na Mtoto". Mbali na uelimishaji kwa jamii,
maonyesho haya yatatoa huduma ya upimaji bure na zoezi la uchangiaji damu.
Ndugu Mheshimiwa, tungependa kuwasilisha taarifa hizi kwa ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa mwenye
dhamana ya maswala yote ya afya mkoani.
Tunapatikana kupitia +255 788 272 743 kwa maelezo na maswali yoyote.
Asante.
McF