Professional Documents
Culture Documents
MAARIFA SHOP - Ufunguo Wa Pesa
MAARIFA SHOP - Ufunguo Wa Pesa
Mengineyo
MAARIFA SHOP
MAARIFASHOP ni mtandao unaokupa maarifa mengi ya kukuwezesha kushinda changamoto nyingi za kiuchumi na maisha kwa ujumla. Kumbuka
maandiko yanasema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa Maarifa"
Home Motisha wa Kazi nani Anapaswa Kutoa? Vitabu Wajasiriamali Kaya na Uchumi Ufunguo wa Pesa
MUSHONGI
View my complete profile
"Pesa ni Mwakilishi Shughulika na Anayewakilishwa" ~ CYPRIDION MUSHONGI
* indicates required
Email Address
*
First Name
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 1/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Last Name
Subscribe
Popular Posts
Unaposikia Uwekezaji
Katika Hisa Unapata
Picha Gani?
“Mtu anayeuza hisa ni
sawa na mtu anayeuza
kuku wakati anapenda mayai” ~
Cypridion Mushongi Neno "hisa"
limekuwa maaru...
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 2/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Baada ya hapo akili yako inakusukuma ili ukamilishe kazi ya kubadilisha huo
ubunifu uliopo katika hali ya wazo kuwa vitu halisi ambavyo mwisho wake
Blog Archive
hukuletea pesa.
▼ 2023 (4)
Ndiyo maana tunasema PESA ni ishara ya nguvu ya ubunifu ulionao katika hali ya ▼ March (1)
kuonekana kwa macho. Kwahiyo, pesa tunatembea nazo mawazoni mwetu, UZIO WA MJI NANI
tunalala nazo usingizini, tunakuwa nazo kila mahali tunapokua. ANAFUNGUA LANGO
LAKE?
Kazi tunayo moja tu nayo ni kuzitoa huko ndani yetu. Ili tuweze kuzitoa pesa ndani ► January (3)
yetu tunahitaji kuendelea kujifunza namna bora ya kuzitoa nje, maana zikikaa
► 2021 (3)
tutakufanazo.
► 2020 (12)
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 3/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
► 2018 (8)
Binadamu ukishapata kile unachohitaji na ukawa na uhuru wa kuchagua upate nini ► 2017 (36)
na uache nini ndiyo unapata kuishi maisha ya furaha na kuridhika pia.
► 2016 (41)
► 2015 (38)
Unachotakiwa kufahamu ni kwamba wewe umejaliwa nguvu ya ubunifu ndani yako
na hiyo ndiyo hazina ya pesa uliyonayo. Kwahiyo, unatakiwa kuwa mtu mwenye
matumaini na kuhakikisha hofu na mashaka havina nafasi kwako.
JAZA E-MAIL KUPATA MAARIFA
Habari njema ni kwamba leo hii kuna idadi ya watu wengi sana ambao tunakaribia
kuwa watu bilioni tisa hivi.
WATEMBELEAJI WETU
Watu wote hawa wako tayari kulipa pesa ili kukidhi mahitaji yao. Unachotakiwa
kufanya kama wewe ni kukidhi mahitaji ya asilimia ndogo sana ya watu wote 92,303
walioko hapa duniani.
Kwahiyo, ukiona umepata pesa ujue kuwa hiyo ni ishara inayoonyesha nguvu ya MAARIFASHOP
ubunifu ndani yako.
Search
Kila wakati tuzame zaidi katika kutafiti na kufuatilia hitaji hasa la jamii tunayoweza
kuifikia na katika hitaji lao hilo tuone pesa kwa macho yetu ya rohoni.
Tukishaona kwa macho ya ndani tuanze kufanyakazi ya kuitoa ndani kwa maana
ya kufanyakazi kwa vitendo ili kukidhi hitaji lililopo kwenye jamii husika.
Kazi ya nguvu ya ubunifu ikishakamilika, watu wenye uhitaji wataleta pesa kwako
na utaanza kuikusanya kwenye kapu, hapo ndio itaanza kuonekana kwa watu
wengine.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 4/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Baadae, utaanza kusikia watu mtaani wakisema fulani amezipata pesa, sijui
amezitoa wapi wakati wao ndio wamezileta kwako….hivyo ndivyo maisha
yanavyokwenda.
Mpendwa msomaji wa makala hii litafakari sana suala hili la kuitoa nje pesa iliyoko
ndani kwani ni rahisi kuutokomeza umaskini moja kwa moja.
Najua unapenda kufuata njia za mkato lakini ukweli ni kwamba ukae ukijua kuwa
pesa inayopatikana kwa njia za mkato inadumu kwako muda mfupi sana na wakati
mwingine njia inayotumika siyo rahisi kuitumia wakati mwingine.
Kwahiyo, wakati ukiendelea na njia zako za mkato anza taratibu kufuata kidogo
kidogo njia hii ya nguvu ya ubunifu ili kutengeneza mfereji wa pesa zitiririkazo kuja
kwako bila kikomo.
Kupata mafunzo ya kila siku na makala mpya kwa njia ya whatsap bonyeza
neno MAFUNZO.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 5/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 6/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 7/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 8/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Sasa umeyajua haya! Ni lazima tuanze pamoja kutafuta pesa bila sababu
zitokanazo na shida/matatizo.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 9/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Pesa ambayo huwa tunapata mara zote utoka kwenye mifumo mikuu
miwili ambayo ni “mfumo wa mshahara” na “mfumo wa FAIDA”. Kati ya
mifumo hiyo, mfumo wa mshahara ndio unaotegemewa na kuaminiwa na
watu wengi. Lakini pia ndio mfumo ambao unazalisha maskini wengi, na
ni mfumo ambao watu wake uhangaika sana kutafuta pesa ya kujikimu.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 10/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Wakati huo huo, mfumo wa faida unakuwezesha wewe kupata pesa kila
siku. Unapoweza kupata mapato (pesa) kila siku inakusaidia kufikia
ulinganifu wa mapato na matumizi.
Hali hii ndiyo inatufanya wengi hasa waajiriwa kushindwa kupata mitaji
ambayo ingetuwezesha kuingia kwa urahisi kwenye “mfumo wa faida”.
Kwa maana nyingine ni kwamba tayari tumejenga tabia au utamaduni wa
kula bila ya kuwa na pesa.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 11/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Siku zote waajiri wako wanakata pesa yao kwanza, alafu wanakupangia
kiasi utakachotumia kuendesha maisha ambayo wao wanaona ni
muhafaka kwako. Kimsingi maisha yako yote yanadhibitiwa hadi unakosa
kuifurahia dunia hii yenye maziwa na asali.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 13/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 14/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Binadamu ili apate kufahamu kitu fulani lazima picha iliyoko kichwani
ilingane na kufanana na kitu unachotafuta. Endapo picha zikipishana
lazima itakuwa vigumu sana kupata hicho unachotafuta. Mara nyingi, tizo
hili la kupishana kwa picha linatokea zaidi kwa vitu vingi ambavyo siyo....
halisi, kama vile PESA. Katika suala la pesa, watu wengi wanapicha
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 15/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Inatosha kusema kuwa katika utafutaji wetu wa pesa tuko katika makundi
makuu mawili ya watu. Kundi la kwanza ambalo ndilo la wengi ni lile
linaloichukulia pesa kuwa ni kitu halisi na mara nyingi hawa wanatumia
HISIA zaidi katika kufanya maamuzi mbalimbali juu ya utafutaji wake.
Kundi la pili ni lile la watu wachache ambao wanaitambua pesa kama
“kitu ambacho SIYO HALISI ~ ni WAZO” na mara nyingi wanatumia
ukweli katika kupanga na kuchagua njia za kuitafuta pesa.
Hatari ya kuiona pesa kama KITU HALISI ni pale unapoifunga akiri yako
isiweze kuona na kujua kile kinachosababisha pesa kuingia mfukoni.
Kwakuwa akiri yako itakuwa tayari imejifunga basi mwisho wake ni
kwamba hautajali kuboresha au kuendeleza kile ambacho
kinakuwezesha wewe kupata pesa hiyo unayoifurahia sasa.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 16/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 17/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Watu wengi wakizidi kuamini kuwa pesa ni kitu halisi, ni wazi kwamba
siku zote wataendelea kuamini kuwa pesa walizonazo ni kidogo na
mwisho kujikuta wakijenga wivu na chuki dhidi ya wale wanaowadhania
kuwa wanazo pesa nyingi.
Falsafa yangu katika hili ni kwamba “Ukidhania pesa ni kitu halisi, basi
ujue kuwa hata njia na mbinu utakazotumia kutafuta zitakuwa
zinafanana na zile za kutafuta vitu halisi”.
Mfano: Ukitaka nyanya moja kwa moja ama utaenda shambani kwako au
utaenda gengeni hayo yakifanyika unapata nyanya kwa dakika chache.
Ukihisi njaa moja kwa moja unatafuta kitu halisi ambacho ni chakula –
ama utakwenda nyumbani au hotelini, michakato hiyo ikifanyika tayari
tatizo lako la njaa litakuwa limekwisha.
Vitu ambavyo siyo halisi kama ilivyo pesa, navyo vina utaratibu wake na
mbinu zake katika kuvitafuta. Pia ni vizuri kukumbuka kuwa, pesa yoyote
unayoiona siyo halisi bali ni kitu kilichopewa thamani na binadamu,
japokuwa pesa ni muhimu sana katika maisha lakini akili, afya na
ufahamu wako ni muhimu kuliko PESA. Maana pesa ulipwa baada ya
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 18/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 19/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Kwasasa wapo watu wengi wanaodhani kuwa wao wanazo pesa kidogo
na wangependelea Mungu awaongezee. Pia kuna wale wachache
ambao wanadhani wanazo pesa nyingi lakini na hawa wangependelea
Mungu azidi kuwapa pesa nyingi zaidi. Ki-ukweli hakuna pesa kidogo
wala pesa nyingi.
Kama nilivyotangulia kusema hapo awali kuwa watu wengi bado wana
machungu na wanalalamika kila wakati kwamba wao hawafanikiwi
kupata pesa ya kutosha. Kuwepo kwa hali ya malalamiko juu ya pesa
kidogo kunaonyesha dhairi kuwa ufahamu uliopo ni kidogo, kwasababu
mfumo wa elimu ya darasani hauna ajenda ya kufundisha pesa. Na pia
watu wengi tumefanya utafutaji wa pesa kuwa wa HISIA zaidi kuliko
ukweli ulivyo.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 21/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Kwahiyo, wale ambao ndani ya nafsi zao wana sababu nzito ya kutafuta
pesa ndio wanapata kiasi hicho ambacho kwako wewe uliye na sababu
nyepesi unaona wamepata pesa nyingi. Napenda kurudia tena kusema
kuwa “hakuna aliye na pesa nyingi bali kila mtu anacho kiasi ambacho ni
hitaji lake kwa wakati huo”.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 22/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 23/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 25/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 26/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 28/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
E-mail: mchumieconomist2009@gmail.com
Tovuti: http://maarifashop.blogspot.com
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 29/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Kila kitu unachokifanya sasa hivi kimeanza kama wazo kutoka ndani
yako. Hakuna matendo utakayotenda bila kuanzia kwenye fikra
(mawazo).
Kwahiyo, ukiwaza kwa namna fulani, basi ujue kwamba utapata utajiri wa
namna fulani sawa na ulivyowaza mwanzoni kabla ya kupata utajiri huo.
Fikra au mawazo, ndio kitu pekee ambacho huweza kukusukuma
kufanya vitu fulani fulani ambavyo ndivyo huweza kukuletea utajiri.
Maeneo hayo yote matatu ni muhimu sana katika kuishi maisha yenye
mafanikio na furaha. Ni lazima mwili uwe na utajiri, akili iwe ya utajiri na
roho pia iwe na utajiri, hapo ndipo itawezekana wewe kuifikia ndoto yako
ya utajiri.
Kama kila kitu kwenye maisha kinakazana kuwa zaidi ya kilivyo sasa,
iweje wewe leo uendelee kuwa pale pale miaka yote? Mti unakazana
kukua zaidi ya ulivyo sasa.
Na wewe binadamu pia ni lazima ukazane kuwa bora zaidi ya ulivyo sasa
katika maeneo yote muhimu ya maisha yako.
Nyakati zinaonekana kuwa ngumu kwa wale wote walio katika usawa
wakushindana na wenzao. Lakini, wewe unayetafuta utajiri wako
hunabudi kuanza kujifunza maisha yale ambayo unashindana na
malengo yako au ndoto zako basi.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 33/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
“Ukipata pesa na ukaitumia kabla ya kutenga akiba, basi ujue
umelipa watu wengine kwanza na wewe umesahau kujilipa”
Tajiri mkubwa na mashuhuri duniani, Bwana Warren Buffet aliwahi kusisitiza kuwa, kama unataka
kujenga mtaji kutoka kwenye akiba yako binafsi ni sharti ujitahidi kuacha tabia ya “kuweka akiba
baada ya kutumia na badala yake utumie kile kinachobaki baada ya kutenga pesa ya akiba”. Katika
maisha ya umilikaji pesa duniani, kuna makundi ya ina mbili.
Kundi la Kwanza ni la wale wanaoweka akiba ya kile kinachobaki baada ya wao kutumia na kundi la
pili ni wale wanaoweka akiba kabla ya kutumia. Kwa mfumo wetu wa mapato na matumizi ya pesa,
tunaona kuwa kundi la waweka akiba baada ya kutumia ni wengi sana na ndilo kundi la watu ambao
ni walalamikaji juu ya ukosefu wa mitaji ya kufanyia biashara au shughuli nyingine za kiuchumi.
Katika ulimwengu wa biashara, mtaji ndilo suruhisho la uwekezaji wowote wenye tija. Hatahivyo, mtaji
umekuwa ni adimu kuupata na umekuwa ni kikwazo namba moja cha watu wengi kushindwa
kuwekeza na hatimaye kuwa wajasiriamali. Ili kuweza kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa
mitaji, watu wengi wamezidi kuhamasishwa kujiweea akiba binafsi kidogo kidogo kutoka kwenye
mapato wanayopata.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 34/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Lakini pamoja na kwamba njia hii ya akiba binafsi ni rahisi na ya uhakika, bado suala la kuweka akiba
limekuwa gumu kutekelezeka. Sababu kubwa ya kushindwa kujiwekea akiba ni kwamba watu wengi
tumejenga utamaduni wa “kutumia kwanza na akiba baadae”.
Ukweli ni kwamba, pindi tunapopata pesa, kitu cha kwanza kufanya ni kutumia kwanza kwa lengo la
kumaliza eti shida zilizopo. Hapa kipaumbele kinakuwa ni kumaliza shida na siyo kuweka “akiba”.
Uzoefu umeonyesha kuwa, ukipata pesa na ukaanza kutumia kabla ya kutenga akiba, inakuwa siyo
rahisi kubakiza pesa yoyote kwasababu shida ni nyingi na mahitaji ya wakati huo ni mengi,
ukilinganisha na kiasi cha pesa unachokuwa umepata.
Ukipata pesa na ukatumia kabla ya kutenga akiba, basi ujue umelipa watu wengine kwanza kabla ya
kujilipa wewe. Utamaduni wa kulipa watu wengine kwanza pindi tupatapo pesa umezidi kukua siku
hadi siku na tumeendela kuulithisha kwa watoto wetu. Pesa yoyote unayojilipa kwanza ndiyo hiyo
hugeuka kuwa “akiba”. Tunahitaji kujenga utamaduni wa kujilipa kwanza kabla ya kufikiria kununua
kitu chochote kile pindi tunapoingiza pesa mifukoni mwetu.
Hatahivyo, utumiaji wa mikopo kama chanzo cha mitaji, bado haujaweza kuwanufaisha kwa kiwango
walichotarajia. Hii ni kutokana na upungufu mkubwa wa elimu juu ya mtiririko wa pesa (inayoingia na
kutoka) au uelewa mpana juu ya mapato na matumizi ya pesa.
Kukosekana kwa uelewa wa kutosha juu ya utunzaji na utumiaji wa mikopo, wanufaika wengi wa
mikopo, wamejikuta wakigeuka kuwa mawakara wa kudumu wa mabenki ya biashara. Hii ni kutokana
na ukweli kwamba, mikopo mingi imekuwa ikitumika zaidi kununua vitu ambavyo si vya kuingiza pesa
mfukoni (assets), bali vimekuwa ni vitu vya kupeleka pesa nje ya mfuko.
Wapo watu wengi ambao tumeshuhudia wakishindwa kabisa kurudisha mikopo na hapa wakopeshaji
wa pesa, wanalazmika kunadi mali zao na hivyo kujikuta wakifirisika ghafla. Lakini chanzo cha
kushindwa kurejesha mikopo kukosekana kwa nidhamu ya matumizi ya pesa ambayo haikujengeka
huko nyuma. Bila kuwa na nidhamu na tabia ya kujilipa kwanza kutokana na mapato yako binafsi,
huwezi kuwa na nidhamu ya kutumia pesa ya mkopo (ambayo siyo ya kwako) kwa umakini
unaostahili.
Kwahiyo, tabia ya kutenga akiba kabla ya kutumia (kulipa watu wengine), ndio inatuwezesha kujenga
nidhamu ya matumizi stahiki ya pesa yetu binafsi na hata ile ya mkopo.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 35/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Akiba binafsi imeshindikana….! Wengi wetu tunashindwa kabisa kujiwekea akiba binafsi licha ya
kwamba tunapata pesa ya kutosha. Kila wakati tunapopata pesa kitu cha kwanza tunachowazia na
kukipa kipaumbele ni “MATUMIZI” yaani kununua mahitaji (kuwalipa wengine) na pesa inayobaki
ndiyo mara nyingi watu ukumbuka kujiwekea akiba. Haipiti wiki moja, ile akiba tuliyoweka mwanzoni
baada ya kutumia nayo tunaitumia kwa mambo mengi ambayo ufanyika kwa mtindo wa dharura.
Suala la kupenda kutumia haliishii hapo bali watu wengine uenda hatua ya mbele zaidi ambayo ni ya
kutumia vitu kwa mkopo ambapo mtu ulipa pesa baadae baada ya kupata pesa. Unapomkuta mtu
yuko busy anatafuta pesa, husidhani mtu huyo anasukumwa na kutaka kutoka kimaisha laasha! Bali
huyo mtu anatafuta pesa za kulipia madeni ya vitu alivyokwisha tumia siku za nyuma.
Kwahiyo, itoshekusema kuwa mtu huyo alikula bila kufanya kazi, na adhabu yake ni kwamba
matunda yote ya kazi yake, lazima yalipe madeni tu maana hamna namna nyingine.
Unapanga mipango ya kutumia baada ya kupata pesa? Tabia hii ya kutumia kwanza na akiba
baadae ndiyo inawafanya watu wengi kuamini kwamba huwezi kupanga mipango yoyote kabla ya
kupata pesa.
Watu wa namna hii kwa kipindi ambacho hawana pesa wanakaa tu bila kupanga na kufanya
chochote cha maana. Kwa maana nyingine, watu hawa bila kusukumwa na pesa waliyonayo mifukoni
hawawezi kufanya jambo lolote la maendeleo. Hii ni hatari na lazima umaskini huwe halali yako.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 36/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Waliofanikiwa wanaweka akiba kwanza kabla ya yote: Kwakuwa akiba binafsi ndiyo chanzo cha
uhakika wa kupata mtaji binfsi, ni lazima tuanze kubadilika kwa kuanza kujifunza tabia ya wale watu
waliofanikiwa.
Watu waliofanikiwa, mara nyingi wanapopata pesa yoyote hile, kitu cha kwanza kwao huwa ni
kutenga kwanza asilimia fulani ya pesa kama akiba na baada ya hapo ndipo ufikiria suala la matumizi
mengine. Unapoweka akiba kwanza kabla ya kitu chochote ndipo unaweza kudhibiti tamaa yako, kwa
maana utatakiwa kuwa na nidhamu ya kutumia kulingana na kile kilichobaki.
Kwahiyo, jijengee tabia ya kutanguliza kujilipa kwanza kabla ya kulipa watu wengine; kwani kwa
kufanya hivyo, utapata mtaji wa kutosha na hatimaye kufikia mafanikio makubwa maishani.
Ili kuendelea kupata makala hizi moja kwa moja kupitia e-mail yako bonyeza “KUPATA MAKALA”
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 37/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
asubuhi. Zamu hii, alikuwa akihojiwa kiongozi mmoja wa dini, ambaye alikuwa
akijaribu kuelezea jinsi walivyojipanga katika kuandaa na kukamilisha siku ya
mkesha wa kuombea uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka huu, na akasisitiza
kuwa maombi yatafanyika mkesha wa 8/8/2015. Katika mazungumzo yake
akagusia jambo moja muhimu kuwa kwa sasa watu wengi wanatanguliza pesa
mbele hata kabla ya kufanya kazi na wengine wanadai walipwe pesa, ndipo
wapige kura za ndiyo kwa wagombea, hasa katika kipindi hiki tunapoelekea
uchaguzi mkuu. Kiongozi huyu, alitumia fursa hiyo kuwahasa watanzania
kujiepusha na tabia ya kupenda kutanguliza pesa mbele. Katika kuweka msisitizo
wa kuonyesha ni kwa jinsi gani pesa siyo kitu halisi; alirejea maandiko kutoka
katika vitabu vitakatifu yanayosema kuwa “Pesa ni Sanamu”. Kitendo cha watu
wengi kushindwa kutambua usanamu uliopo juu ya pesa, ndicho chanzo cha
kuwepo kwa changamoto nyingi zinazotukabili leo hii kama watu binafsi na taifa
kwa ujumla.
Dhana hii ya “pesa ni sanamu” ni muhimu tukaijua na kuielewa vizuri, ili hatimaye
mimi na wewe tupate kujinusuru kwa kutoka kwenye kundi kubwa la watu
wanaotafuta pesa kama “sanamu”. Yawezekana leo hii hatupati pesa ya kutosha
na unaangaika sana, kwasababu fikra na mitazamo yako ni ile ile ya kudhania
kuwa pesa ni kitu halisi kumbe ni “sanamu”. Tafsiri ya neno “pesa ni sanamu”
inamaanisha kwamba, pesa siyo kitu halisi bali ni mfano au kivuli cha bidhaa na
huduma mbalimbali, ambazo hazionekani kwa macho yetu ya kawaida. Kwa
maana nyingine, pesa ni kitu ambacho husimama badala ya bidhaa na huduma
mbalimbali hasa wakati wa zoezi zima la ubadilishanaji vitu kati ya muuzaji na
mnunuzi.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 38/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
tuna vitu tofauti tofauti. Mfano: utakuta mtu mwingine kwenye wallet yake
ameweka huduma ya mapambo, usafiri, ufundi, elimu, kuchangia mawazo kwenye
vikao n.k. Wengine wallet zao utakuta bidhaa kama vile chakula, nguo, dawa, jiko,
taa, simu, mafuta n.k. Ukiamua kutumia macho ya ubongo wako utakubaliana na
mimi kuwa, pesa tulizonazo kwenye wallet zetu hazifanani.
Wote tunaweza kuwa na noti ya shilingi elfu kumi za kitanzania, ambazo kwa
macho ya kawaida zinafanana, lakini kwa macho ya ubongo, wallet zetu
hazijabeba pesa bali zimebeba vitu tofauti mtofauti kabisa. Kwahiyo, ikiwa wewe
biashara yako ni kufuga na kuuza kuku basi elfu kumi yako ni kuku; kama wewe ni
mwandishi basi elfu kumi yako ni habari, gazeti au kitabu na ikiwa wewe ni
mshereheshaji basi elfu kumi yako ni ushereheshaji, ualimu, uchoraji n.k. Mifano
hii michache inatuonyesha kuwa, pesa zote tulizonazo hazifanani kabisa,
isipokuwa bidhaa na huduma tunazozalisha ndizo hubadilika na kuwa kitu kimoja
ambacho ni sanamu yaani “pesa” inayoonekana kwa macho yetu ya kawaida.
Kwa wale wote wanaoamini kuwa pesa siyo sanamu, maana yake ni kwamba vitu
vyote vinavyotengeneza pesa waliyonayo, hawawezi kuviona kwasababu macho
yao ya ubongo yamepofuka na hivyo wamebakia kutumia macho ya kawaida peke
yake. Ukiangalia pesa kwa macho ya kawaida (kwa mujibu wa kinachonekana),
kiukweli wewe utaishia tu kuona noti za elfu 10, 5, 2, 1 n.k. ikiwa kuona kwako
kutaishia hapo, basi na wewe ni mmojawapo wa watu hawaoni pesa bali wanaona
“sanamu”. Mtu anayeona sanamu kila wakati, hawezi kujua mahali kitu halisi kilipo
na wala hatajua hiyo pesa ilikotoka. Ndiyo maana inapotokea mtu akapata pesa
na baadae kuishiwa, ni vigumu kuzipata tena kwa haraka kwasababu, anakuwa
tayari ameishasahau zilikotoka. Na kwa yule anayetambua kuwa pesa aliyonayo
kwenye wallet ilitokana na mkusanyiko wa bidhaa na huduma mbalimbali; ni rahisi
sana kwake yeye kuzipata pesa kwa muda mfupi, kwasababu chanzo chake
kinajulikana na kimekuwa kikitunzwa na kuimarishwa mara kwa mara.
Kwenye jamii yetu kwasasa, bado watu wengi wanaishi kwenye ulimwengu wa vitu
vinavyoonekana kwa macho ya kawaida. Tunahitaji kujifunza kutumia macho yetu
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 39/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 40/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
yeyote, bali unakuwanayo kwa kuzaliwa ilimradi, uwe na utaratibu wa kujali afya yako
basi!.
Kwakuwa kila mmoja wetu anamiliki na kuitawala nguvukazi yake mwenyewe, maamuzi
ya kutumia nguvukazi yako kwa mtu mwenyewe. Kuna kundi la watu wanaotumia
nguvukazi yao zaidi kwenye “Uzalishaji Pesa” na kuna wengine wanaitumia zaidi kwenye
shughuli ambazo siyo za uzalishaji wa pesa (Non Income Generating Activities ~ NIGA).
Hapa Tanzania, bado watu wengi wanawekeza nguvukazi kubwa zaidi kwenye shughuli
zisizo za uzalishaji pesa. Shughuli nyingi ambazo siyo za uzalishaji pesa, zinatumia sana
pesa, hali inayopelekea watu wengi kutumia kuliko wanavyozalisha pesa. Kama nguvu-
kazi yetu nyingi inawekezwa zaidi kwenye shughuli ambazo siyo za uzalishaji, basi tujue
kabisa kuwa tutapata bidhaa/huduma kidogo, na hatimaye tunaishia kupata pesa kidogo.
Watu wengi tunataka na tunatamani sana “maisha bora”; maisha ambayo tutakuwa na
uwezo endelevu katika kupata chochote tunachohitaji kama lilivyo kusudio la Mungu
kutuweka hapa duniani. Kwakuwa, maisha bora ndiyo kusudio la watu wengi, basi
inatupasa tubuni mchakato wa maisha bora badala ya hali ya sasa ambayo tumejikita
kwenye shughuli za kutafuta pesa ambazo hazina mpangilio. Kwa sasa ukichunguza
harakati nyingi za kutafuta pesa, unagundua kuwa kila shuguli inajitegemea kiasi kwamba
kukamilika kwa shughuli moja hakuna uhusiano wowote na shughuli nyingine. Jambo hili
la kufanya shughuli ambazo hazina mpangilio maalumu unaolenga kupata maisha bora,
ndiyo linatufanya tukose mwelekeo na hatimaye kushindwa kuyafikia maisha ya ndoto
yetu. Kwahiyo, zoezi la kutafuta pesa na hatimaye maisha bora ni lazima kulifanya kuwa la
ki-mchakato zaidi kuliko ki-shughuli zaidi. Kupitia fikra, utafiti, vitabu na hitoria za watu
waliofanikiwa; nimejifunza kuwa, ili uweze kuyafikia maisha ya ndoto yako (maisha bora)
ni muhimu upitie mchakato maalum. Mfano ni kama huu hapa chini:
Ukichunguza mchakato wa kupata pesa hapo juu unaona moja kwa moja kuwa pesa siyo
matokeo ya mwisho ambayo binadamu anayatafuta bali pesa ni sehemu tu ya mchakato wa
maisha bora. Katika mchakato wa kupata maisha bora, pesa ipo katika nafasi ya nne kati ya
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 41/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
vitu sita muhimu ambavyo vinahitajika kupewa kipaumbele kama unataka kufanikiwa.
Mafanikio makubwa yameshindikana kufikiwa na watu wengi, kwasababu ya kutilia
mkazo zaidi kitu kimoja tu! ambacho ni PESA. Michakato yetu mingi ya kutafuta pesa,
haitilii mkazo vitu vingine kama “afya, nguvukazi na bidhaa”. Kwa maana nyingine
tunaweza kusema kuwa hatupati pesa kwasababu mara nyingi mchakato wa kutafuta pesa
na hatimaye maisha bora “tunauanzia katikati”.
Unapopanga mkakati au mchakato wa kutafuta pesa na wakati huo huo ukaacha kuzingatia
na kujali afya yako, basi ujue kuwa uwezekano wa wewe kupata maisha bora ni mdogo
sana. Kumbuka afya bora ndio chimbuko la nguvu ulizonazo ambazo ndio hukupatia
rasilimali “nguvukazi”. Unapoamua kuwekeza nguvu kazi yako kwenye shughuli za
uzalishaji ndipo unapata bidhaa au huduma ambazo hugeuka kuwa pesa. Unapokuwa na
bidhaa/huduma ndipo watu wengine sasa huamua kutoa na kutuma pesa zao kwako, ili
kujipatia bidhaa/huduma husika. Kwahiyo, iwapo utakuwa umezalisha bidhaa nyingi
utapata pesa nyingi na ni pesa hiyohiyo ambayo na wewe utaitoa na kuituma kwa watu
wengine ili kupata bidhaa/huduma na hatimaye kukidhi mahitaji yako mbalimbali.
Unapofikia hatua ya endelevu wa kupata kile unachohitaji kwa muda muhafaka, ni wazi
kwamba unakuwa tayari umefikia maisha bora ambayo ni ya ndoto yako na hapa ndipo
unaanza kupata vitu vile ulivyokuwa ukivipenda lakini ulilazimika kuviacha kwa muda ili
kuruhusu mchakato wako wa maisha bora ukamilike.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 42/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 46/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 47/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Wenzao ambao ni matajiri wao, mara tu pesa inapoingia, kitu cha kwanza
ujiuliza ni kitu gani wanaweza kukitoa ili kuondoa kero kwenye jamii ikiwemo
le iliyowazunguka. Kwahiyo, wao uweza kuiachia pesa yao kutoka lakini kwa
malengo ya kuituma malighafi ambayo pengine ikiunganishwa na mambo
mengine uweza kurudi na bidhaa au Huduma ambayo ni hitaji muhimu
kwenye jamii. Kwa kufanya hivyo, hata wale maskini walioogopa kuiachia
pesa yao mwanzoni, wakati huu uweza kuituma kwa matajiri hao na
mzunguko uendelea hivyo hivyo na mwisho ni umaskini uliokithiri.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 48/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Watu wengi hasa waajiriwa pamoja na wakulima, huwa pesa zao zikishatoka
kwa mwenyewe, mara nyingi huwa hazirudi kwasababu ya kutumwa vitu
ambavyo wewe ndiye mtumiaji wa mwisho. Sababu kubwa ya waajiriwa
ufanya hivyo ni kwasababu ya kutegemea mshahara mwisho wa mwezi. Hali
hii humfanya mtumishi pamoja na mkulima kuishi maisha ya kawaida sana
ambayo huwa hayabadiliki miaka nenda rudi. Baadhi ya vitu ambavyo pesa
ikitumwa kuvifuata yenyewe hairudi ni vingi sana; mfano: Runinga Redio,
Karo za wanafunzi, gari la kutembelea, n.k.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 49/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 50/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
ya maana pana ya pesa upo kwa watu wengi, na hali hii ni kwa wote waliokwenda
shule na wale ambao hawakwenda kabisa.
Katika kutafuta pesa kunakuwa na dhamira tofauti kati ya maskini na tajiri; “Watu
maskini wanawekeza muda na nguvu yao kwa dhamira ya kutafuta pesa lakini
watu matajiri wanawekeza muda, akili na nguvu yao kwa dhamira ya kutafuta “vitu
na huduma”. Kwasababu maskini wengi waliamini kuwa mwisho wa utafutaji wao
ni pesa, basi ndipo ugundua kuwa sio mwisho, kumbe mwisho wao ni kupata vitu
na Huduma (chakula, dawa, mavazi; usafiri, elimu, utaalam, nguvukazi n.k.).
Kwahiyo, pamoja na kutafuta pesa hiyo kwa kutumia nguvu kubwa na muda
mrefu, mtu huyo ujikuta akilazimika kuzipeleka mwenyewe kwa tajiri ambaye
wakati huo ana vitu na huduma fulani fulani. Kwa maana nyingine tunaweza
kusema kuwa watu hawa wanaishi kwa kutafuta pesa na kisha kulipa bill! au
madeni basi.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 51/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
hapo juu, ndiyo maana siku zote pesa itakwenda kule kulipo na vitu au huduma
hakuna sehemu nyingine.
Iwapo utaendelea kujiuliza swali la nitapata pesa wapi ndivyo itakavyozidi kuwa
vigumu kupata jibu ambalo litakuongoza kupata pesa. Kwahiyo, mtanzania
mwenzangu ni wakati sasa wa kubadili swali lako kutoka “nitapata pesa wapi?”
kwenda “Pesa itakuja kwangu kufuata nini?”. Na kila mara utakapojiuliza swali la
pesa itafuata nini kwako, basi jibu jibu lake tu! litakuwa ndiyo pesa yenyewe kwa
maana nyingine utaona watu wakibisha hodi mlangoni kwako, kwaajili ya
kukuletea pesa ambayo miaka yote umekuwa ukikimbia huku na huko kuitafuta
bila mafanikio!. Sasa unachotakiwa kufanya ni utafiti katika mazingira yanayo
kuzunguka na maeneo mengine unayoweza kuyafikia ili kutambua mahitaji, kero
na changamoto zilizopo. Matokeo ya Utafiti yatakusaidia kubuni na kuzalisha vitu
au huduma ili kukidhi mahitaji ya jamii husika, na ukifikia hapo ndipo utaona ndani
muda mfupi watu wakituma pesa ili ikafuate vitu na huduma kutoka kwako.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 52/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
kuwa zipo aina kuu tatu za vipato ambazo ni: Mapato ya Ajira (mshahara); Mapato Hai (kujiajiri);
Mapato yasiyo na kikomo au Tuli, (Passive Income).
1. Mapato ya Ajira (Earned Income)
Haya ni mapato yanayotokana na kufanya kazi ya kuajiriwa (mshahara), ambayo mtu huyapata
kutokana na ajira yake. Katika aina hii ya kipato, vigezo vya kukuwezesha ulipwe ni pamoja na aina
ya kazi na wadhifa au cheo chako. Pia, mapato haya yanajumuisha mapato yoyote yatokanayo na
ajira binafsi (kujiajiri), biashara ndogondogo na shughuli nyinginezo ambazo unapata kipato kutokana
na juhudi na muda uliotumika. Kwa maana nyingine, ni kwamba kama husiposhugulika au
ukasimama kufanya kazi na kipato kinakoma pale pale.
Ø Uzuri wa Mapato ya Ajira
· Mapato yanaongezeka zaidi kulingana na muda na ukubwa wa shughuli inayofanya
· Hauitaji mtaji kuweza kupata mapato haya
· Mtaji ni nguvu au ujuzi wako mwenyewe
Ø Ubaya wa Mapato ya Ajira
· Uwezi kupata utajiri wa kudumu kwa aina hii ya mapato yanayotokana na mshahara.
Kwasababu mshahara unapata, unakula na unanaisha.......Unapata unakula zinaisha.....
· Siyo mapato endelevu, ukiacha kufanya kazi mapato yanakoma.
· Mapato haya ya ajira yanatozwa kodi kubwa kuliko aina nyingine zote za mapato na
Waajiriwa wanalijua vizuri hili.
Mfano; kwa mtu anayelipwa mshahara wa kiasi cha 1,350,000/- anakatwa kodi hivi:
Aina ya Makato Kiasi (TSh)/Mwezi
Kodi (Income Tax) 260,400.00
Bima ya Afya 40,500.00
Chama cha Wafanyakazi 27,000.00
Mfuko wa Pensheni 67,500.00
Jumla 394,900.00
Sasa, ebu fikiria mtu anakatwa karibu Shilingi 400,000/- kila mwezi, kiasi ambacho kwa mwaka
kinafikia karibu shilling 4,800,000/-. Unaweza kukuta mtu ana biashara yenye mtaji upatao shilingi
million 15, siajabu kukuta analipa kodi kiasi kisichozidi shilingi 500,000/- kwa mwaka.
2. Mapato Hai (Active Income)
Aina hii ya mapato, kwa kiasi fulani inafanana na mapato ya ajira yanayo jumuisha mishahara, kwani
mapato haya yanatokana na kuuza na kununua bidhaa kubwa kubwa kama magari, nyumba, kiwanja
n.k. Mchakato huu ni kwamba, unanunua kitu halafu unakiuza kwa faida, halafu basi. Ili uweze kupata
mapato mengine inakubidi, utafute kitu kingine au ununue kitu kingine haraka ndipo upate tena pesa.
Maana yake ni kwamba lazima uwe kazini (active) muda wote huku ukiendelea kuchakarika ndipo
upate mapato. Kama ilivyo kwa mapato ya mshahara, pindi unapoacha kununua na kuuza vitu,
mapato nayo yanakoma mara moja.
Ø Uzuri wa Mapato Hai
· Mapato haya hayahitaji watendaji kazi wengi ili kufanikisha shughuli ni wewe tu mwenyewe.
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 53/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 54/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
kujielimisha zaidi juu ya undani wa mapato haya - "tuli", kupitia mtandao wako wa maarifashop,
tutaendelea kukuletea mafunzo juu ya aina hii ya mapato, ili hatimaye kila mmoja wetu aweze
kuchukua hatua za maksudi tayari kuelekea kwenye maisha ya ndoto zetu.
~TWENDE KAZI PAMOJA~!
Wakati fulani ndani ya mwezi mwaka huu, nikiwa kwa mtoa huduma ya kubrashi
viatu, nilikutana na jamaa mmoja akiwa akiongelea juu ya mambo ya maisha na
mtoa Huduma huyo. Nilipofika waliendelea na stori zao na mimi mara moja moja
nikawa naruhusiwa kuchangia hoja iliyokuwa mezani. Wakati huo wote walijadili
sana juu ya changamoto za kimaisha, ikwemo tatizo sugu la ukosefu wa pesa na
hivyo kufanya maisha kuwa magumu sana. Mimi pamoja ya kwamba nilichangia
lakini nilikwa nasikiliza zaidi mjadala ulivyokuwa ukienda ili niweze kujifunza kitu.
Baada ya mazungumzo hayo nilipata wazo la kutafakari na kuanza kuandika
makala juu ya “Imani Yako Kuhusu Pesa!” wazo hili lilitokana na ukweli kwamba
watu wawili hawa walihitimisha mjadala kwa kusema kuwa “Fedha ina Siri Kubwa”
wakiamanisha kwamba kanuni au njia ya kupata pesa haijulikani. Ukienda mbele
Zaidi unagundua kwamba, tayari kwenye jamii kumekwisha jengeka imani
kwamba kupata pesa ni kubahatisha, Kiasi kwamba wengi wao wanaotafuta pesa
hawana uhakika kama ipo siku watapata.
Kutokana na hitimisho hilo la kwamba “pesa ina siri kubwa” niwazi kuwa kuna
ombwe la uelewa na ufahamu kuhusu maana halisi ya pesa. Na niseme kuwa
imani iliyopo kwa sasa juu ya pesa yawezekana siyo sahihi (ni potofu). Upotofu
huu wa imani juu ya pesa unajidhihirisha Katika matukio mengi hapa nchini kwetu
Tanzania na nchi za jirani, ambapo kumekuwepo na matukio mengi ya watu
kujaribu kutumia ushirikina ili kupata mafanikio ya haraka na hasa mafanikio ya
kifedha.
Kama ilivyo imani Katika dini kwamba mwanadamu aweza kuwa na imani potofu
juu ya wokovu au akawa na imani iliyo ya kweli kuhusu wokovu na linapokuja
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 55/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
swala la upatikanaji wa pesa ni hivyo hivyo, kwani imani yetu tuliyonayo juu ya
pesa imetokana kiwango cha uelewa tulionao. Lakini niseme kuwa ni bahati
mbaya sana kwamba uelewa wetu juu ya kitu pesa bado ni mdogo sana, licha ya
kuwa “Pesa” ni moja kati ya vitu vichache vinavyopendwa sana duniani. Kama
ilivyo katika dini zetu, kwa waumini wa madhebu yote, ili waweze kuwa na imani
sahihi juu ya muumba wao, wanahitaji kwanza neema ya Mungu, lakini pia
wanahitaji watu ambao wako tayari kujitoa na kufanya kazi ya Mungu ili kusaka
ukweli na kuupeleka ukweli huo kwa watu wote kwa jina la “Habari njema” Hivyo
basi kadili watu wanavyozidi kupata ukweli kuhusu wokovu ndivyo watazidi
kujenga imani ya kweli au sahihi juu ya wokovu au kazi ya Mungu.
Katika kutambua nani mwenye imani sahihi juu ya pesa, unaweza kuangalia
dhana, misemo, methali na nahau juu ya pesa kwa mtu binafsi au kundi la
jamii husika. Hivi vyote, ndivyo vigezo au viashiria tunavyoweza kuvitumia
kupima imani ya mtu aliyonayo juu pesa. Kwa kufahamu imani yake iko wapi ni
rahisi sana kufahamu iwapo huyo mtu ana imani sahihi au imani potofu. Mfano wa
baadhi ya viashiria vya imani ya mtu juu ya pesa ni hivi hapa; ”Pesa ni Sabuni ya
Roho” : Dhana hii ya kuamini kuwa pesa ni sabuni ya roho, inatuonyesha kuwa
ndani ya fikra zetu tunadhani pesa ndilo hitimisho la kazi tuliyokuwa tukifanya bila
kujali tumeifanya na kuumia kwa muda gani. Ukitaka kufahamu nani anaichukulia
pesa kama hitimisho, utamuona tu anavyokuwa amechangamka na kuanza hata
kubadili mfumo wa maisha ikibidi hata vyakula, vinywaji, mavazi, hubadilika
kwasababu mtu huyu anajiona amefika mwisho na roho yake imesafishika. Kama
alikuwa akifuga ng’ombe, sasa ataanza kutokuwajali na baadae mradi utakufa na
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 56/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Kwahiyo, hili tuweze kuiishi imani hii ya “Pesa ni Sabuni ya Roho” ni lazima
kufahamu kuwa ukishapata pesa unafurahi sana, lakini ni vizuri furaha hiyo
isitusahaulishe tunako kwenda na tuendelee kuiona kuwa ni makaratasi ambayo
tunahitaji kuyatuma kwa wengine ili tupate pesa nyingi zaidi kwaajiri ya kuwekeza
kwenye kuzalisha vitu na huduma bila kikomo.
Hili usiendelee kuamini kuwa kupata pesa ni bahati, ni vizuri ukafahamu kwamba
kila mtu amezaliwa na uwezo wa kupata pesa haitakayo. Kinachohitajika kabla ya
kutafuta pesa ni kuchukua muda wako ukafikiri na kutafakari majibu ya maswali
haya; Je? Pesa ni kitu gani?, Pesa hupatikana wapi?, kwanini wengine kipindi
Fulani pesa na baadae kuishiwa?; Je? Pesa inakujaje kwako na inapoteaje? Je?
Wewe unatafuta shilingi ngapi mwaka huu? Kwako fedha itafuata nini? n.k. Kadili
utakavyoweza kujibu maswali haya wewe mwenyewe itakufanya utafakari kwa
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 57/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Ewe mtanzania chunguza imani yako juu ya pesa, ili ujitenge na wale wanaotumia
njia ya mkato na kutafuta utajiri wa haraka. Kama ukikuta imani yako ni potofu,
basi kata shauri leo na kubadili ili uwe na imani sahihi juu ya pesa kabla ya kuanza
kuitafuta.
~KARIBU TWENDE KAZI PAMOJA~
1 comment:
Unknown said...
JAZA NA URUDI
Jina:
Kiasi cha mkopo:
Muda:
Jinsia:
Nchi:
Lengo:
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 58/59
12/1/23, 6:46 PM MAARIFA SHOP: Ufunguo wa Pesa
Nambari ya simu ya rununu:
Home
https://maarifashop.blogspot.com/p/blog-page_75.html 59/59