Professional Documents
Culture Documents
Faru Script
Faru Script
Faru Script
Written by
NDOVU FILMS
S.L.P 16833
ARUSHA
0765823120
ii.
Address
Phone Number
1 EXT: PORINI &NDANI YA GARI 1
(Drone Shot)
SIMBA
"Tanzania Tanzania, Nakupenda kwa
Moyo wote"
CHUI
"Inchi yangu Tanzania, Jina lako Ni
Tamu Sana"
NYATI
"Nilalapo Nakuota wewe"
TEMBO
"Niamkapo ni heri mama weee"
FARU
"Tanzania Tanzania, Nakupenda kwa
Moyo Wote"
WOTE
"Tanzania Tanzania, Ninapokwenda
Safarini, kutazama Maajabu Biashara
Nayo makazi, Sitaweza Kusahau mimi,
Mambo Mema ya Kwetu Kabisaa,
Tanzania Tanzania Nakupenda kwa
Moyo Wote".
KARAKAL
"The Big 5,Wanyama Watano Ndani ya
Hifadhi yenu Amani Ya Mungu Ipo
Pamoja Nanyi"
SIMBA
"Kitambo kirefu hatukuona karakal"
TAI
Hao unaowaona Ndio Askari Ambao ni
Hatari Sana Ndani ya Hifadhi hii,
ni Askari Hodari na wenye Akili,The
Big 5, yule ni
Simba,Chui,Tembo,Faru na Nyati
SIMBA
"Karakal kitambo kirefu kaka"
TEMBO
"Leo upo na wageni Gani?"
KARAKAL
"Kaka kaka, Mambo sio Mambo ndo
maana hatuonani, Nipo na Ndugu
wangu Tai na yule Mwingine Ni
Jaguar Ndugu yetu Amekuja
Kututembelea vivutio vya Tanzania"
TAI
"The Big Five,Vipi hali zenu Mpo
sawa?"
FARU
"Vipi tena Mbona Mmemuudhi Mgeni
wetu, Au hajafurahia Uzuri wa
Hifadhi yetu?"
KARAKAL
"Jini kisirani kamuingia, akimaliza
kununa atacheka tu"
TAI
"Muda sio mrefu vivutio vya Hifadhi
yetu Vitamfurahisha, (Hii ndio
Serengeti bwana")
SIMBA
"Sisi Tuwaache muendelee na
Matembezi, wacha tukaendelee na
Kujenga Taifa".
KARAKAL
"Sawa kaka Tutaonana tena"
3.
TAI
"Kwaheri kaka"
KARAKAL
"Sasa Tutawezaje kumaliza Safari
kwa uzuri kama kuna kununiana?"
JAGUAR
"Nina Kisasi Cha Kulipa Ndani ya
Hifadhi Hii"
KARAKAL
"Sio Kazi Ndogo,Tunahitaji Umakini
Mkubwa Na Kazi inahitaji Muda wa
Kutosha"
TAI
"Kazi Hii Haitawezekana Kwa Siku
Ulizopanga wewe Maana Sio kila
Utakalo litatimia Mengine ni Kama
Bahati Nasibu"
KARAKAL
"Faru ni wachache Sana Na pia wengi
wao wapo katika Uangalizi Hivyo
wamefungwa Viashiria Na
wanajulikana wapo wapi Ndo maana
Kabla Hatujaua Lazima Tumkague kama
Kafungwa Kiashiria cha usalama"
JAGUAR
"Mnaongea Upumbavu
Mtupu,Nimewapatia Pesa Nyingi sanaa
Ili mkamilishe Hili,Mtafanya Vile
Nitakavyo"
TAI
"Sio kila jambo Unalipeleka kwa
Hisia Na Kwa Nguvu ya Pesa Mengine
Ni akili Na Uzoefu"
4.
KARAKAL
"Wewe Ni Mgeni Katika Hifadhi
Hii,Tulia Na Lazima Utumie akili
kubwa Maana Moja ya Nguvu Kubwa Ya
serikali ipo Katika Hifadhi Hii"
KARAKAL (CONT'D)
"Ama kweli Nimeamini Bangi sio Mama
yako Useme Itakuonea Huruma"
2 EXT:PORINI 2
JAGUAR
"Nakusikia Ongea!"
TANZANITE
"Kua na Adabu! Mimi ni Baba
yako,Ujisahaulisha kua Baba yako ni
Kaka Yangu?"
JAGUAR
"Sina Muda wa kusikiliza hayo,Toa
Melekezo ya kazi"
TANZANITE
"Mmmh Natumaini Umewaona Hao vinaja
wawili,La muhimu kwa sasa ni kazi
iliyowapeleka,Mteja amepiga simu na
leo ndio atatoa malipo ya awali ya
mzigo wake hivyo fanya hima ,kuhusu
kisasi tutapanga baadae"
JAGUAR
"Nimekuelewa ila kuhusu kisasi
usinipangie muda wa kukilipa"
5.
3 EXT:PORINI 3
CHUI
"Faru, Ungeanza kumpa kaka yako
Tembo,kisha Tukafuata wengine."
TEMBO
"Chui Wewe pia ni kaka Yetu ndio
maana Ameanza na wewe"
CHUI
"Sikia Tembo,Ningeringa sanaa
ningekua Na Undugu na nyinyi, Hivi
kwanini mliamua kujiunga na jeshi
hatari kama hili tena Ndugu wa
Damu?"
FARU
"Baba yetu alikua Askari wa kulinda
wanyama pori, Hivyo tumerithi kazi
ya Baba yetu"
NYATI
"Baba yenu Alikua Hodari kama
Nyinyi?"
SIMBA
"Wanaonekana wanafuata Nyendo za
Baba yao"
TEMBO
"Hatujamfikia Hata theluthi ya
Uhodari wake Afande"
CHUI
"Mnaweza kumfikia na Kumpita kama
Mtamuuliza mama yenu vizuri kuhusu
uhodari wa Baba yenu"
6.
FARU
"Chukua zawadi ya Kunipa siri ya
Kua Hodari kama Baba yangu"
REDIO
"kikosi cha Big 5 Rudia kama
mnanisikia"
SIMBA
"Big 5 Tumekupata Rudia kama
unatusikia"
RADIO
"Natumaini upande huo upo salama
over"
SIMBA
"Tupo salama na kila mahali kupo
shwari over"
RADIO
"Mwelekeo wa leo Kusini mashariki
Over"
SIMBA
"Tumekunakili over"
4 EXT:KIJIJINI 4
JANGILI
"Haloo,vipi hali yako?"
KARAKAL
"Salama kaka, vipi kila kitu kipo
Tayari au bado"
7.
JANGILI
"Safari hii mnabahati kweli kwa
maana mitego yetu imenasa mapema
sana,mteja wa safari hii ana Baraka
kweli".
KARAKAL
"Acha hadithi nyingi tupe maelekezo
tunaupataje maana Hatuna muda wa
kutosha,hapa tulipo tunatamani
kupaa tukufuate ulipo"
JANGILI
"Ndo nilikua nakaribia kuingia
kijijini, japo njaa inaniuma ila
naona bora niwasubiri maana ingia
toka ingia toka kijijini sio salama
kwa kazi zetu na siku hizi hali sio
shwari saana,tuapambana kiuzoefu"
KARAKAL
"Sawa tukutane upande upi? Usalama
wote upo juu yako".
JANGILI
"Ondoa shaka mimi sina tofauti na
mbwa mwitu,yoyote anayejichanganya
mbele yangu sijawahi kumuacha
salama, tukutane upande wa
mashariki kwenye kituo chetu."
KARAKAL
"Vizuri,Usiogope kuhusu njaa wala
kiu nina chakula na maji."
5 EXT:NYUMBANI 5
MKE
"mama mwanao mpaka sasa hapatikani
na mimi leo hali yangu najiona
kabisa sio nzuri,huwenda Mgeni
akaja leo in shaa Allah"
8.
MAMA
"Pole mwanangu,muda mwingine
wapaswa kua jasiri, hata mimi
ujauzito wangu wa kwanza ulikua
unampenda sana baba yenu, hivyo
sikuweza kumkosa machoni mwangu"
MKE
"Kama ni hivyo basi na jina
tumwandalie kabisa huwenda
nikamleta baba"
MAMA
"Inshaa Allah, sote tunategemea
itakua hivyo."
MKE
"In shaa Allah"
6 EXT:PORINI 6
JANGILI
"Habari ndugu yangu"
SHUSHUSHU
"Salama kaka, vipi mbona unatoka na
kuni kijiji unazirejesha tena
porini?"
JANGILI
"Hahahaha Maisha ya siku hizi bila
simu yaani unaonekana hujaendelea
na chaajabu zaidi, ukiipoteza simu
ndo Matokeo yake haya kuonekana
mwendawazimu, Hata sijafika
nyumbani imebidi nirejee maporini
kuitafuta"
SHUSHUSHU
"Pole sana ndugu yangu,simu
imerahisisha maisha ila simu nayo
inaangamiza maisha,naomba
nikusindikize maana pia wanyama
wakali wapo kila mahala"
9.
JANGILI
"Hapana ndugu yangu,usijisumbue
nitaitafuta mwenyewe,na kuhusu
wanyama, wenyewe wakiniona
wanakimbia kama vichaa,usighairi
safari yako kisa mimi bwanaa."
SHUSHUSHU
"Sawa ila kuna dharura hata za
maradhi kutembea wawili ni bora"
7 EXT:PORINI 7
FARU
"Jamani ukweli mimi sina imani na
Yule jamaa aliyekua na kina
karatai,sijui kwanini hajanitoka
kwenye akili yangu,wasiwasi
unaniambia sio mtu mwema kabisa."
NYATI
"Una maanisha nini?"
CHUI
"Ina maana hauwaamini pia karatai?"
FARU
"Naona muda wa swala umeingia ni
bora tuswali kwanza,Huwenda ni
wasiwasi wangu tu,pia ni kawaia ya
ibilisi kutia wasiwasi katika nyoyo
za watu. "
8 EXT:OFISINI 8
TANZANITE
"Ingia"
KIJANA WA WILD
"Habari Bwana Tanzanite,nimeagizwa
na bwana Wild nikuletee mzigo wako"
TANZANITE
"Karibu ukae,utahitaji kawaha au
chochote"
KIJANA WA WILD
"Hapana Asante Nipo sawa."
TANZANITE
"Hello Mr Wild"
WILD
"Hope you receive it Mr Tanzanite"
TANZANITE
"Received"
MKE
"Asante Mungu afadhali inaita sasa"
KARAKAL
"Asante Mungu Afadhali amepiga"
KARAKAL (CONT'D)
"Haloo,halooo,netiweki sio nzuri
kabisaaa"
MKE
"Haloo Mume wangu Kipenzi"
FARU
"Haloo mke wangu Mzuri"
MKE
"Assalaam aleykum mume wangu"
FARU
"Waaleykum salaam mke wangu"
MKE
"Nimekutafuta sana hupatikani mpaka
nikawa na wasiwasi,na leo najionea
tafrani tu,sijui ndo baba yako
anataka kuja."
FARU
"In shaa Allah, Nitafurahi ikiwa
hivyo,msiwe na wasiwasi ni netiweki
tu inasumbua baadhi ya maeneo"
MKE
"Mama mwanao nimepata njoo uongee
nae,Ngoja kwanza umsalimie mama
maana netweki inaweza kututoroka
tusikupate tena."
FARU
"Sawa mke wangu."
MAMA
"Haloo Mwanangu,Hamjambo? Poleni na
kazi"
FARU
"Hatujambo mama shikamoo"
MAMA
"Marahaba mwanagu,kaka yako nae
hajambo? Maana nae simu yake
haipatikani"
12.
FARU
"Sote tupo sawa Dua zenu tu."
MAMA
"Mungu awalinde wanangu na Mungu
awafanye muwe mahodari kama baba
yenu"
FARU
"Amiin"
MAMA
"Halooo,halooo"
10 EXT:PORINI 10
KARAKAL
"Haloo,hapo nakusikia,hili ndo
tatizo nalichukia huku kwenu."
JANGILI
"Pole ndo kazi uliyoichagua,jikaze
acha kudeka"
KARAKAL
"Mimi sina tatizo ila kuna kitinda
mimba tupo nae ndo tatizo,najuta
kuja nae kabisaa"
JANGILI
"Njaa inaniuma sana naomba mfanye
haraka"
JAGUAR
"Kuzungushana maporini tuu mwisho
tuliwe na fisi ndo akili zitatukaa
vizuri"
TAI
"Hahahah jikaze wewe, acha kutia
huruma,ulilia jeshi wala ujionee
mwenyewe"
KARAKAL
"Haya safari iendelee".
11 EXT:PORINI 11
FEDHA
"Karibu Bwana Tanzanite,
hatujaonana kitambo,vipi biashara
zako"
TANZANITE
"Nipo Salama kabisa Bwana
Fedha,kuhusu biashara sio nzuri
sana kwa sasa, ndo kuna mdeni wangu
mmoja ndo amenilipa leo nimeona
nilete mapema maana nina mambo
mengi na yanahitaji pesa"
FEDHA
"Bado upo na just tanzanite au una
biashara ingine,maana watu wakubwa
mnawekeza kwenye mambo mengi"
TANZANITE
"Ni kweli kabisa ,uwekezaji ndio
jambo muhimu sana,kwa sasa bado
nipo na just tanzanite".
FEDHA
hakuna tabu tutaifanyia kazi muda
sio mrefu,Kkaribu tena bwana
Tanzaniate.
TANZANITE
"Asante Bwana Fedha,nawe siku moja
upite ofisini kwetu uone biashara
zetu,sio sisi pekee ndo tunakufuata
kila siku"
FEDHA
"Nitakuja kukutembelea ondoa shaka"
TANZANITE
"Nitafurahi kukuona"
EXT:PORINI
Wanaonekana askari wa hifadhi
wakiwa wanatembea kwa mstari na
huku gari yao ikifuata
polepole,simba anaonekana kushika
simu yake na kupata ujumbe,anatoa
ishara ya kusimama,wanasimama.
SIMBA
"Askari,kuna Taarifa ,kijiji cha
Fisi upande wa mashariki kuna
kiashiria cha ujangili,sote
tunaelekea huko"
WOTE
"Ndio Afande!"
12 EXT:PORINI 12
KARAKAL
"Tumekosea njia tupite ile ya kule
tumebakiza kilometa 2 tu tutakua
tumefika"
JAGUAR
"Mnachekesha sana kumbe hata
hamapajui mnapokwenda?"
TAI
"Ungebaki nyumbani kunyonya
kitindamimba wa watu"
JAGUAR
"Unasemaje?"
KARAKAL
"Haya sasa mnataka kufanya nini?
Kimyaa! Mnajua fika kazi hii ni
hatari lakini bado mnataka kuanza
upuuzi wa kutiliana uchuro."
TAI
"Samahani kaka, alisema kisha
akampiga bega"
15.
13 EXT:PORINI 13
SIMBA
"Natumaini sote tunajua cha kufanya
na jisi ya kuliendea hili jambo"
WOTE
"ndio afande!"
SIMBA
"Nawakumbusha kua hii ni vita,sote
tuna haki ya kuipigania nchi yetu
na urithi wetu,tunapokwenda kila
mmoja wetu ana ulazima wa kujilinda
na kumlinda mwenzake,tunakwenda
watano na tutarudi
watano,mmenielewa"
WOTE
"Ndio Afande!"
14 EXT:PORINI 14
MWANAKIJIJI
"Mwituu!"
MWANAKIJIJI (CONT'D)
"Samahani kama nimekuudhi mwitu,
nimekuona haupo sawa hivyo
nimekuhofia ndugu yangu usije
ukapatwa na matatizo,na sisi ni
wanaume hata kama una matatizo
niambie takusaidia"
MWITU
"Ama kweli wewe ni nyumbu kama jina
lako,hiyo tabia yako ya
kujisahaulisha mbaya sana, kama mtu
hataki kitu wewe unalazimisha cha
nini? kuna siku itakuponza Haki
nakuambia"
16.
MWITU (CONT'D)
"wewe ni mwema sana,jumuika
nami,ukweli wanawake wanaudhi sana
majumbani mwetu,unaweza kuamini
nafika nyumbani badala mtu anipokee
na akushukuru anaanza maneno eti
kuni nyembamba nataka nene mara
sitaki fupi nataka ndefu yaani
ilimradi tu kusiwe na amani ndani
ya nyumba,ndo maana ulishangaa
natoa kuni kijiji na kuzirejesha
mwituni"
NYUMBU
"Pole sana ndugu yangu,mwanamke
anaweza sababisha hata mtu
ukajinyonga buree,eeeeh Mungu
epushia mbali"
MWITU
"Muda mwingine hua nakuja huku
mbali kutazama uzuri wa mandhari
yetu ili kuwa sawa,Hebu anagalia
kunavyopendeza"
MWITU (CONT'D)
"Wewe ni nyumbu tu,hujawahi kua
makini na maisha yako,hatimaye
mikononi mwa mbwa mwitu,puzika kwa
amani rafiki"
15 EXT:PORINI 15
JAGUAR
"Ongea!"
TANZANITE
"Malipo tushapokea hivyo
wahimize,nakupeni siku mbili mzigo
uwe umekamilika na siku ya tatu
ufike mahala husika"
JAGUAR
"Siku mbili nyingi sana,mzigo upo
tayari ndo tunaenda kuuona kasha
utupatie maelekezo ya kuuchukua"
TANZANITE
"Vizuri,kua makini na usifanye
jambo lolote La kupuuzi,huyo jamaa
unaenda kukutana nae sio mtu wa
mchezo"
JAGUAR
"Nimekuelewa!"
JAGUAR (CONT'D)
"Naombeni tufanye mambo kwa uharaka
maana sitaweza kulala porini,sehemu
hakuna maji wala choo"
KARAKAL
"Kwa safari hii na ulichokifuata
kweli unawaza choo,haya sema
kingine unachoogopa porini?"
TAI
"hahaha alisema anaogopa kuliwa na
fisi"
KARAKAL
"kwa mwendo huu tunaoenda wa kudeka
hivi utaliwa hata na sungura"
JAGUAR
"Wapuuzi"
18.
16 EXT:PORINI 16
SIMBA
"Sio kawaida ya huyu jamaa
kutokupatikana wala kutotuma ujumbe
wake wowote,nahisi kuna tatizo
maana hajawahi toa taarifa ya uongo
wala hajawahi kuchelewa kutoa
mwendelezo wa taarifa"
NYATI
"Mimi pia nina wasiwasi kama
wako,huwenda kapatwa na jambo baya"
FARU
"Siku ya leo nina wasiwasi
sana,Tuombe Mungu iwe salama"
TEMBO
"Tulia ndugu yangu,kaka yako nipo
hapa hakuna litakalokutokea, na
kama ni kuhusu shemeji basi
atajifungua salama."
FARU
"Amin"
CHUI
"Faru toka Asubuhi aliwahisi wale
jamaa vibaya labda ndio bado
anatembea na hisia zile"
SIMBA
"Simama kwanza hapo mbele tujaribu
kuwasiliana nae tena maana maeneo
yao ndo haya"
SIMBA (CONT'D)
"Askari angali kichaka kile kuna
baiskeli imefichwa pekua kila
mahala"
FARU
"Afande kuna simu imevunjwa huku"
CHUI
"Afande, mbona ni baiskeli ya
Askari wetu"
SIMBA
"Pekuweni kila mahali Tafadhali
zote ni ishara mbaya"
NYATI
"Afande,askari wetu huyu hapa
amejeruhiwa vibaya leta maji
haraka"
SIMBA
"Faru,Nyati,Tembo anaglia hali ya
usalama,chui Huduma ya kwanza
Haraka,tembo ongeza nguvu kwenye
huduma ya kwanza"
Majeruhi akiwa amezuia jeraha kwa shati lake ili kuzuia damu
isimtoke kwa wingi,Wanaonekana wanamfanyia huduma ya kwanza
kukagua mapigo ya moyo na mengineyo
CHUI
"Afande,Bado anahema."
SIMBA
"vizuri hakiksha anakua salama
maana taarifa yote anayo yeye"
CHUI
"Sawa Afande"
SIMBA
"Unamjua aliyekufanyia hivi"
SIMBA (CONT'D)
"Nani kakufanyia hivi na kaelekea
wapi?"
20.
SIMBA (CONT'D)
"Amesema nani?"
CHUI
"Amesema Mwitu"
SIMBA
"Ndio Yule tuliyekua tunamfuatilia
kama anajihusisha na ujangili?"
CHUI
"Afande,Askari wetu hakuumia
sana,pia alijizuia kwa tumia nguo
yake damu isimtoke kwa wingi,jua
lilichangia kumchosha hivyo kwa
sasa anaendelea vizuri"
NYATI
"Afande nashauri,Kama askari wetu
anaendelea vizuri tunaweza
kuendelea na mpango kazi"
17 EXT:PORINI 17
SIMBA
"Habari,unaelekea wapi mapema yote
na unajua wanyama wakali wapo kila
mahali?"
MWITU
"Salama,ni kweli uyasemayo,ila
naomba mniwie radhi nina mgonjwa
kijiji cha pili naenda kumuona ni
dharura tu,mimi pia najinea
huruma,nimetoka nimechanganyikiwa"
SIMBA
"unaitwa nani?
21.
MWITU
"Naitwa Mwitu Tambarare"
SIMBA
"Pole kwa kuuguza,uwe na safari
njema"
MWITU
"Asante nanyi pia"
18 EXT:PORINI 18
FARU
"Afande,kuna jambo
nimekumbuka,huwenda likatuongezea
nyama katika mpango kazi wetu"
SIMBA
"Tuambie faru umekumbuka nini? "
FARU
"Asubuhi tulipishana na mtu na
akatuambia anakwenda kumuona
mgonjwa,na ulipomuuliza jina lake
alisema anaitwa mwitu
tambarare,tumuulize Askari wetu
kama ndiye mtu aliyemdhuru
tunayemtafuta"
NYUMBU
"Ndio yeye Afande Anaitwa Mwitu
Tambarare"
SIMBA
"Vizuri"
TEMBO
"Ndugu yangu nakusifu sana kwa
kumbukumbu nzuri"
NYATI
"nashauri wasiwasi wa Faru uwe ni
wa kuzingatiwa"
19 EXT:PORINI 19
MWITU
"Poleni kwa kusubiri,natumaini wote
mnaendelea vizuri"
TAI
"Tupo poa,mbona shati lako na usoni
una damu?"
MWITU
"kuna mzembe alijichanganya
nikamsaidia kumuonyesha njia ya
mbinguni,alale salama tumboni mwa
fisi"
KARAKAL
"Hatuna muda,Pakia baiskel
tuondoke"
20 EXT:PORINI 20
TEMBO
"Afande,alama za tairi za baiskeli
zinaelekea huku"
FARU
"Afande kuna boma za kimasai zipo
hapo mbele,tujaribu kusogea huwenda
kuna mtu wanahusiana nae anaishi
maeneo hayo,au laa basi ndipo
wanapohifadhi nyara zote"
23.
SIMBA
"Askari,wote ndani ya gari
tafadhali"
21 EXT:PORINI 21
MWITU
"Kama nilivyokuambia,safari hii
kila kitu kimekua haraka sana"
MASSAI
"Ndo vizuri maana kukaa na hizi
vitu ndani sio salama,muda mwingine
Askari wanakuja kukagua maboma
zetu,kama metoka huko na meona
hakuna usalama jifanyeni kama
naendelea na safari zenu mtakuja
baadae jua ikizama"
KARATAKAL
"Usiogope Massai,hakuna aliyetuona
wala hatujapishana na mtu"
MASSAI
"Karibuni sana,Jisikieni mpo
nyumbani"
KARAKAL
"Asante sana,sasa sisi sio wageni
tena,tupo nyumbani na tunaimani
hali ni shwari"
MASSAI
"ondoeni wasiwasi"
KARAKAL
"Natumaini wengine unatujua,huyu
anaitwa Jaguar ni Ndugu yetu kama
walivyo wengine,ndo kijana wa Bwana
Tanzanite"
24.
MASSAI
"Karibu Jaguar,Baba zako wote
nimefanya nao kazi muda murefu
sana, na walikua wanalala kwenye
hizi maboma, jisikie upo nyumbani
JAGUAR
"Asante sana nimefurahi"
MAASAI
"Unaweza kufanya malipo sasa"
MASSAI
"Hauna pesa za kitanzania?"
JAGUAR
"Tulihofia zitakua nyingi sana na
ingekua mzigo mkubwa"
MASSAI
"Sawa,twendeni mkaone mzigo wenu"
22 EXT:PORINI 22
SIMBA
"Askari,kama kawaida tutaacha gari
huku kisha tutakwenda kwa miguu
kufanya upekuzi na mjiandae kwa
vita lolote linaweza kutokea"
WOTE
"Sawa Afande"
SIMBA
"Kwa hali yako Utabaki kwenye gari"
NYUMBU
"Sawa Afande"
25.
CHUI
"Si gari ya karatai ile na imebeba
baiskeli?"
FARU
"Hiyo baiskeli huwenda ni ya Mwitu
ambaye ndo mwenyeji wao"
NYATI
"Hakika huwenda Ndivyo"
23 EXT:BOMANI 23
KARAKAL
"Jaguar tupe muongozo kuhusu
usafiri"
JAGUAR
"Kuna canter tumeiandaa itapita
usiku kuchukua mzigo na
utachanganywa na mahindi hivyo
hawatoweza kugundua barabarani"
TAI
"Vizuri"
MASSAI
"Askari wamekuja"
KARAKAL
"Hapanaa!"
MWITU
Msiogope hawa nawahimili
mwenyewe,kaa tayari kwa vita silaha
yako ndio uhai wako
mwengu
...KIZA...
24 INT:HOSPITAL 24
MAMA
"Daktari nipe taarifa ya mgonjwa
wangu tafadhali"
DAKTARI
"ondoa wasiwasi,Yupo salama pia
hongera amekuleteeni mtoto wa
kiume"
MAMA
"Alhamdulillah, hakika Mungu
hujawahi kumnyima yoyote akuombae"
27.
25 EXT:PORINI 25
Jaguar
TEMBO
"Haloo mama"
MAMA
"Hongera mwangu mkeo amejifungua
mtoto wa kiume"
TEMBO
"Alhamdulillah, samahani mama ni
mimi tembo,faru ana kazi kidogo na
ameniachia simu yake nitampa
taarifa akitoka"
MAMA
"Sawa mwanangu Mungu awalinde na
awape kila hitajio na moyo wenu"
TEMBO
"Amin asante mama kwa Dua,Mbaki
salama" anakata simu na kusema kwa
sauti "Hongera zake majeruhi
amepata mtoto wa kiume"
TEMBO (CONT'D)
"ulisemaje kuhusu kaka yangu"
JAGUAR
"Ningefurahi sana kama angekufa
yeye pamoja na wewe ili kisasi
changu kitimie"
28.
TEMBO
"Kisasi?"
JAGUAR
"Na baba yenu angekua hai ningemuua
kwa mikono yangu Mwenyeweee!"
SIMBA
"Huyo ni mtoto wa marehemu Mzee
FOX,alikamatwa na Baba yako miaka
kumi iliyopita kabla hamjajiunga na
jeshi,Mzee fox alifia magereza
kutokana na maradhi aliyokua nayo"
SIMBA (CONT'D)
"mtoto wa nyoka ni nyoka na vya
kurithi huzidi,pia sikuwahi
kufikiria Karatai mnaweza kua
wahujumu wa hifadhi yetu,ona sasa
mmeishia katika mikono ya sheria"
MWITU
"Mmenikamata kizembe
sana,Hamjanitendea haki kwa
ujangili wangu,nilipaswa kufa kwa
risasi au kuwauwa nyinyi
nyote,ikiwezekana nifungueni
tuchape mkono kiume,Maana risasi
ziliisha na mkanizunguka kizembe
kwa silaha zenu"
SIMBA
"sawa kama utakavypenda bwana
mwitu,Chui una kazi ya kufanya
hapa,Mwitu anataka mapambano ya
kiume"
CHUI
"Ndio Afande"
MWITU
"Sio Chii Tuhata mngeita jeshi zima
msingeniweza"
NYUMBU
"Ukweli ni kwamba ,Naitwa Duma
niliyekua nimevaa ngozi ya Nyumbu"
26 EXT:OFISINI 26
TANZANITE
"Nimewaita hapa kwa haraka maana
kuna dharura imetokea,vijana wetu
tuliowatuma wamekamatwa na askari
wa hifadhi na ushahidi wote
umekamilika,tupo kwenye hatari
kubwa ya kugundulika kua
tunahusiana nao"
WILD
"What about my money?"
TANZANITE
"Nipe mwezi mmoja kuna vijana
nawasiliana nao tutakupa mzigo
wako"
WILD
"No way"
NYIKA
"Mpo chini ya ulinzi"
NYIKA (CONT'D)
"Ushahidi wote umekamilika,ila
walitaka kupigana risasi katika
kuwaweka chini ya ulinzi walijaribu
kunishambulia hivyo nikawahi na
wote wamekufa"
NYIKA (CONT'D)
"sawa Afande"
30.
27 EXT:HOSPITALI 27
MAMA
"Hakika umeniletea mume,sura yake
imelandana sawia na mume wangu,pole
na Hongera sana Binti Yangu"
MWISHO