Professional Documents
Culture Documents
Kitini Cha Mwongozo Wa Ujasiriamali - Kozi Fupi - MWL Shadrack PM
Kitini Cha Mwongozo Wa Ujasiriamali - Kozi Fupi - MWL Shadrack PM
Kitini Cha Mwongozo Wa Ujasiriamali - Kozi Fupi - MWL Shadrack PM
KOZI FUPI
1
KUHUSU MWANDISHI:
UTANGULIZI:
Kitabu hiki cha mwongozo wa Elimu na Mafunzo ya Ujasiriamali kinatoa elimu, kanuni na
mafunzo yote muhimu ambayo ni lazima sana wajasiriamali kuyajua na kuyafanya kwa
uyakinifu ili kupata faida wanayoitamani. Kinatoa mwongozo wa nadharia za Ujasiriamali,
Elimu ya kujiajiri, namna ya kubuni mawazo ya biashara na kuyageuza fursa nzuri za biashara,
kuanzisha biashara kwa mafanikio na kufanya biashara kupitia mpango kazi wa biashara hiyo.
Hadhira kubwa inayotegemewa kupitia kitabu hiki ni wanafunzi hasa wa vyuo vya kati
ikiwemo wa mafunzo ya kozi fupi kutoka chou cha vet ana vijana shiriki kutoka taasisi
mbalimbali.
Mwongozo huu umejiegemeza sana kutoka misingi ya maelezo ya chuo cha VETA, Mwl Aliko
Mmongele, Mwl Christopher Mbagwa, Mwl Winnie Nguni (CKD) na wengine kibao.
Walimu na wakufunzi wanahimiza sana kupata kitabu hiki kama mwongozo kwa kila
mwanafunzi ili kufanya vyema katika Maisha ya kijasiriamali sasa na baadae.
2
YALIYOMO
1. Dhana ya mjasiriamali na Ujasiriamali…………………………………………..3
2. Uanzishaji wa biashara…………………………………………………………...9
3
1.0: DHANA YA UJASIRIAMALI NA MJASIRIAMALI
UTANGULIZI
Umuhimu wa kuwa na jamii ya Kijasiriamali.
Tangu mwanzoni mwa miaka ya tisini kumekuwa na mwamko mpya wa ujasiriamali
katika jamii. Mwamko huu unaonekana katika: -
• Kuongezeka kwa idadi ya wajasiriamali
• Ujasiriamali kupewa kipaumbele katika nchi (tafiti, majarida mbalimbali ya biashara,
mafunzo maalumu ya ujasiriamali, sera za nchi n.k)
• Kukubalika kwa ujasiriamali katika jamii.
Mwamko huu wa ujasiriamali unatokana na muonekano chanya wa tabia za
kijasiriamali. Inaaminika kuwa msingi mkuu wa ujasiriamali upo katika ubunifu.
Katika jamii ya sasa, sifa hii si tu inaendana na uendeshaji wa biashara ndogo ndogo
bali pia inamanufaa makubwa katika maisha ya mtu mwenyewe na utendaji kazi wa
jumuia (kampuni kubwa au serikali). Tabia hii mpya imekuwa muhimu katika utendaji
kazi katika dunia hii ya leo.
1.1: MAANA YA UJASIRIAMALI NA MJASIRIAMALI
Maana ya ujasiriamali
“Ujasiriamali” ni hali au kitendo cha mtu au watu kuthubutu kuanzisha biashara au
kuboresha biashara iliyokuwepo na kusimamiaa kwa lengo la kupata faida.
Maana ya mjasiriamali
Mjasiriamali ni mtu mwenye uwezo wa kuchunguza mazingira yake, kugundua fursa
zilizopo, kukusanya rasilimali, kuanzisha na kuendesha biashara kwa faida. - Ni mtu
ambaye ana ari, msukumo na nia ya kufanikiwa katika malengo aliyonayo.
Vipengele vya ujasiriamali
i. Ufahamu wa mazingira uliyomo
ii. Kunga’amua ufanye nini katika hayo mazingira ili ufaidike nayo (kutafuta fursa)
iii. Kuainisha na kukusanya rasilimali zinazohitajika katika kufanya hiyo shughuli.
iv. Kuanza kuifanya hiyo shughuli maandalizi yanapokuwa yamekamilika.
v. Kuanza kunufaika na hiyo shughuli
Tabia au Sifa zitakazomfanya mjasiriamali afanikiwe
i. Kutafuta fursa na kuzifanyia kazi ; • Unatakiwa kuzishika na kuzitumia fursa
zisizoonekana na wengine na kuanzisha biashara mpya pale unapoona pana manufaa.
ii. Kuthubutu; Mjasiriamali anatakiwa kujaribu kufanya kazi bila woga mara tu baada
ya kupima hatari ambayo haitakiwi kuwa chini ya wastani.
iii. Kupenda ufanisi na ubora;• Anatafuta njia zitakazomwenzesha kufanya shughuli
zake vizuri zaidi, kwa haraka zaidi na kwa urahisi zaidi lakini bila kuhatarisha ubora
4
iv. Uvumilivu;• Anachukua hatua kukabiliana na vikwazo vinavyojitokeza bila kukata
tamaa
v. Kutii ahadi na mikataba ya kazi; Jitahidi kuwaridhisha wateja wako na kukirimu
kwa ajili ya mafanikio ya siku zijazo kuliko kujali faida ya muda mfupi
vi. Kutafuta taarifa ;• Mjasiriamali anatafuta habari kutoka kwa wateja na wasambazaji
wake
vii. Kuweka malengo;• Weka malengo ya muda mrefu na mfupi ambayo yataleta
matokeo mazuri na pia yanaleta changamoto kwako.
viii. Kupanga utaratibu na kufuatilia;• Malengo ya muda mrefu yaweke kwenye
vipengele vinavyoweza kutekelezeka na kulingana na muda uliopo
ix. Kushawishi na kuwa na mtandao;• Tumia mikakati uliyojiwekea kuwashawishi
wengine ili kuwavuta katika bishara yako
x. Kujitegemea na kujiamini;• Tafuta mamlaka aidha kwa kutumia sheria au kwa
kuwadhibiti wengine ili kulinda hadhi yako ya kibiashara
NYINGINEZO: Ubunifu, uerevu, kuwa na nia, mwenye kupenda kujifunza n.k
MITAZAMO YA MSINGI KWA WAJASIRIAMALI
Uhuru wa mawazo/Fikra
Msukumo wa kubadilika
kutenda
KUTAMBUA NAFASI/UWEZO WA KIJASIRIAMALI
Uwezo binafsi unaelezewa kama ni uwezo ambao mjasiriamali mmoja anaweza
kufanikiwa Zaidi ya mwingine ikiwa wanafanya kazi katika mazingira yanayofanana
na pia wanafanana hali ya mtaji n.k! Wanazuoni walifanya tathmini na kutambua
makundi matatu tu ya uwezo binafsi ya kijasiriamali.
KUNDI LA MAFANIKIO KUNDI LA MIPANGO KUNDI LA NGUVU YA
KIJASIRIAMALI
1. Kutafuta fursa 1. Kutafuta taarifa 1. Ushawishi
2. Kupima hatari 2. Kuweka 2. Mtandao
3. Uhitaji wa ufanisi na ubora mipango 3. Kujitegemea
4. Uendelevu 3. Uwekaji mzuri 4. Kujiamini
5. Kutii ahadi na mikataba ya wa mipango na
kazi/ kujitoa katika kazi kusimamia
5
Maarifa
Muda
FAIDA NA HASARA ZA UJASIRIAMALI
FAIDA HASARA (CHANGAMOTO)
Imeongeza uwekezaji katika teknolojia na ugunduzi Kuchajiwa ushuru
Kikuza uchumi kwa wajasiriamali Ni gharama kuanza
Hukuza masoko mapya Ufinyu wa mazingira ya kutenda
Kukuza umilikaji wa biashara Ushindani
Huongeza elimu, mafunzo na maarifa Kutokuwa na mfumo maalumu
Hutanua uchumi wa nchi Huchukua muda mrefu kusimama
Chanzo cha ajira Mwanzo mgumu huwatesa wengi
Husaidia kukidhi mahitaji madogo Hatari ya kupoteza mtaji wa uwekezaji
Kuinua hali ya Maisha kwa wajasiriamali Kutokuwa na mwendelezo
Tofauti za mapato
Kukosa mshahara
6
DHANA YA KUAJIRIWA (KAZI/ AJIRA YA MALIPO)
KUAJIRIWA
Ni ile hali ya kuwa na kazi yenye kupokea malipo kutoka kwa wamiliki wa biashara hiyo.
Hii husemwa kuwa ajira ya malipo kwani huhusisha mshahara kwa wafanyakazi.
Kampuni na biashara nyingi huajiri watu kufanya kazi kwa manufaa ya wawekezaji ili
kupata faida, kisha hugawa faida kwa ajili ya malipo, uwekezaji na wawekezaji
wenyewe.
TOFAUTI KATI YA KUJIAJIRI NA KUAJIRIWA
KUJIAJIRI KUAJIRIWA
Wewe mwenyewe ndio mmiliki Wewe ni mfanyakazi
Unafanya kazi yako mwenyewe Unafanya kazi ya mtu au kampuni Fulani
Mapato ndio faida yako Mapato ni mshahara wako
Hakuna kikomo cha faida Kuna kikomo cha mshahara
Kazi hubadilika badilika Kazi haibadiliki badiliki
Mmiliki anajisimamia mwenyewe Unasimamiwa na mmiliki
Ni kalinda Maisha Sio kalinda Maisha kama utafukuzwa
Hakuna mafao baada ya kuacha kazi Kuna mafao baada ya kustaafu kazi.
7
1.4: KUWEKA VIPAUMBELE
Maana ya Uwekaji Vipaumbele:
Ni kitendo cha kuchambua shughuli muhimu Zaidi kuwahi kufanyika kuliko shughuli
nyingine,
KUWEKA VIPAUMBELE Vipaumbele husaidia:
• Kazi hufanyika katika mpangilio unaoeleweka
• Kazi za haraka hukamilishwa kwa wakati
• Bughudha hudhibitiwa
• Uharaka unahakikiwa
• Fursa mbamblimbali mbadala hubainishwa (kwa kufanya hesabu za kuzidisha)
• Ratiba za kazi huzingatiwa
• Mtiririko na matokeo ya kazi yanakuwa ya kuridhisha
• Wafanyakazi wenzako, viongozi wanaridhishwa na utendaji
JIKUMBUSHE KWA MASWALI HAYA MUHIMU!!!!!
1. Eleza maana ya maneno yafuatayo:
A) Ujasiriamali
B) Kujiajiri
C) Mjasiriamali
D) Vipaumbele
E) Utunzaji Muda
2. Suala la kujua ni zipi shughuli zinazopaswa kufanyika kwanza ni jambo la msingi sana
kwa wafanyabiashara wa sasa. Eleza kwanini.
3. Kazi ya kudhibiti kazi yako kufanyika kwa wakati sahihi na uzalishaji bora ni bure
kama hakuna nidhamu ya kujali muda.
4. A) Taja rasilimali tano muhimu kwa wajasiriamali
B) Fafanua faida 5 za kujiajiri
5. ‘Dhana ya kujiajiri na kuajiriwa ni kama maji na mafuta katika ndoo moja, ni rahisi
sana kutambua baina zao. Tenganisha dhana hizo kwa hoja sita
8
2.0: UANZISHAJI WA BIASHARA
Maana ya neno “Biashara”
Biashara ni neno pana sana hapa ulimwenguni ambalo kila mtu anaweza kudhani na kutafakari
kwa aina yake, wapo wanazuoni mbalimbali waliowahi kujadili na kuhitimisha kwa maana ya
jumla. Inasemekana kuwa Biashara ni shughuli yeyote ile afanyayo mtu ambayo inauwezo wa
kumuingizia kipato,
Hivyo, BIASHARA ni shughuli yeyote ambayo mtu au kundi Fulani hufanya kwa
kubadilishana bidhaa/huduma (mazao) kwa fedha ili kujiingizia kipato. Shughuli hiyo lazima
ihusishe utoaji wa bidhaa au huduma ili kupata fedha. Mfano, Mama mmoja akifungua duka
kila siku ili kuuza bidhaa na nafaka za dukani ili kupata faida baada ya kurejesha gharama zote.
TOFAUTI KATI YA BIDHAA NA HUDUMA
Bidhaa ni vitu ama vifaa vyenye thamani ambavyo hununuliwa ili kutimiza jukumu Fulani.
Mfano, peni, mchele, msanii, n.k
Huduma ni jumla ya shughuli zote ambazo hufanywa ili kutoa bidhaa au kusaidia
ubadilishanaji wa fedha. Mfano, msanii anaweza kutoa huduma ya uimbaji ili kupata fedha.
BIDHAA HUDUMA
Huonekana Haionekani
Hushikika Haishikiki
Huweza kuhifadhika Haihifadhiki
Haibadiliki badiliki Hubadilika kutokana na mazingira
Hufanana Hazifanani
Hutenganishwa hazitenganishwi
9
AINA YA BIASHARA WAAJIRIWA MTAJI/MAUZO
Ndogo ndogo 1-4 0-Hadi milioni 5
Ndogo 5-49 5m-200m
Za kati 50-99 200m-800m
Kubwa Zaidi ya 99 Juu/Zaidi ya 800m
10
Huwezesha vijana na makundi maalumu
Kuchochea kukua kwa masoko
11
2. 3: TAASISI ZA KUSAIDIA BIASHARA
Ni mashirika au makundi ya watu yanayotoa fedha ili kufadhili ama kudhamini biashara
nyingine ili kufikia lengo.
-Taasisi za huduma za kuendeleza Biashara ni taasisi ambazo kwa namna moja ama nyingine
hutoa huduma ambazo husaidia kuanzisha na kuendeleza tasnia/biashara. Kutokana na taasisi
kama hizo wajasiriamali hupata msaada au taarifa mbalimbali ambazo huwaongoza namna ya
kuanziasha biashara zao. Taasisi zimewekwa katika aina tofauti kutokana na aina na upekee
wa huduma maalumu ambayo husaidia biashara.
AINA YA TAASISI ZA KUSAIDIA BIASHARA
A. Vyama vya kibiashara kama Asasi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), chama cha
Biashara , Viwanda na kilimo Tanzania, (TPSF) , shirikisho la wenye Viwanda Tanzania
(CTI) Jumuiya ya Vibindo.
B. Wataalam Washauri ambapo hujumuisha washauri wanaojitegemea, kampuni
binafsi na jumuiya za wanataaluma na washauri wa mambo ya biashara.
C. Taasisi za serikali zinazohusika na utafiti, ubunifu na uendelezaji wa teknolojia ;
taasisi za elimu na mafunzo ambazo hutoa taarifa kwa umma. Mf. SIDO, BRELA,
VETA, TRIDO n.k
D. Asasi zisizokuwa za serikali (NGOs) ambazo husaidia na kuendeleza jitihada za
sekta binafsi kiuchumi katika programu zao za maendeleo . Mf. SNV ( uholanzi )
E. Taasis zinazotoa huduma za kifedha; Benki kama CRDB, NMB, NBC, TPB,
VICOBA, PRIDE, FINKA
MAWAKALA WANAOSAIDIA WAFANYABIASHARA
12
Mafunzo na elimu VETA, CBE, ILO, AGRA
13
Uzoefu katika kazi
Ujuzi binafsi ulionao
Biashara inayoshabihiana
Matakwa binafsi/utashi wa mtu (hobbies)
Uvumbuzi
Maonyesho
Utafiti
Tafakari na malalamiko.
SIFA ZA MAWAZO MAZURI YA BIASHARA
Ni ukweli usiopingika kwamba kuwa na wazo la biashara ni suala moja na kulibadili wazo
husika kuwa biashara ni suala jingine. Hivyo basi, wazo husika liwe mahususi linajibu maswali
yafuatayo
• Je kuna soko?-Upatikanaji wa soko
• Je linarahisisha maisha au kutatua tatizo?-Suluhisho la changamoto
• Je linatekezeleka ? –Ni rahisi kutekelezeka
• Je linaweza kuleta faida? –Huleta faida
• Je upo uwezekano wa kukua?- Kukua kwa masoko na biashara
Kuwepo kwa ushindani?- Ushindani ni maendeleo kwa biashara
Kuwepo kwa wateja halisi?-upatikanaji wa wateja muhimu.
2.5: KUBAINISHA FURSA ZA BIASHARA
Maana ya fursa ya biashara
Fursa ya biashara inafafanuliwa kama ni kuvutia uwekezaji au mapendekezo yanayotoa
uwezekano wa marejesho mara baada ya mtu kuthubutu kufanya biashara. -FURSA YA
BIASHARA: Ni wazo zuri la biashara linalovutia uwekezaji na lenye uwezo wa
kurejesha faida katika biashara.
SIFA ZA FURSA NZURI YA BIASHARA
1. Kuwepo kwa mahitaji halisi, yaani kuitikia utashi ambao haujahudumiwa au mahitaji
ya wateja ambao wanauwezo wa kununua na ambao ni chaguo lao
2. Rejeshao la uwekezaji, kupata faida au rejesho ambalo ni imara, kwa wakati husika
na lililoendelevu kutokana na uthubutiu na juhudi inayohitajika.
3. Yenye ushindani, yaani nafasi sawa au bora zaidi katika muonekano kwa mteja kuliko
mwengine..
4. Upatikanaji wa Rasilimali, na umahili, yaani ndani ya uwezo wa mjasiliamali katika
rasilimali, umahili, vigezo vya kisheria,nk.
Zifikie malengo yaani zifikie malengo na maono au mtu au taasisi inayofanya uthubutu.
14
TOFAUTI KATI YA FURSA NA WAZO LA BIASHARA
WAZO FURSA
??? ???
UWEZO FURSA
15
MAPUNGUFU TISHIO
16
2.8: UCHAMBUZI WA MASOKO
Je,Masoko ni nini?
Masoko ni shughuli yoyote afanyayo mjasiriamali kuanzia uzalishaji wa bidhaa hadi mtumiaji
anapotumia bidhaa hiyo zenye lengo la kuongeza mauzo kwenye Biashara yake.
MJUMUISHO WA VIPENGELE VYA MASOKO
Kumbuka kwamba kitu muhimu katika biashara ni kuuza bidhaa/huduma, hivyo mteja ni mtu
muhimu sana katika biashara! Kwa hiyo ikiwa mjasiriamali anapenda wateja kununua
bidhaa/huduma anayotoa ni lazima kutekeleza yafuataya:
Kuwa na bidhaa/huduma sahihi (BIDHAA)
Kuuza bei nzuri kwa pande zote (BEI)
Kuwepo eneo sahihi (BANDA)
Kutumia njia inayokubalika kutangaza (BANGO)
2.9: KUJENGA MTANDAO
Mjasiriamali anapofanya biashara anategemea sana mtandao alionao kufanikisha
biashara zake hasa kumwezesha kupata wateja wa bishara zake. Kadili mitandao yao
inavyokuwa mikubwa, ndivyo wanavyokuwa na fursa Kubwa katika kufanikiwa.
Mjasiriamali anatakiwa kufanya kazi kwa umakini sana kuelekea kujenga (kuimarisha)
mitandao yao binafsi. Tafsiri ya Mtandao (usiyorasmi). Tafiti mbalimbali kuhusu maana
ya neno mtandao zinaonyesha kutofautiana.Kuna tafsiri za aina nyingi.
17
v. Taasisi au mashirika ya fedha yanayofanya biashara ya kukopesha fedha (Mfano PRIDE,
FINCA, FAIDIKA n.k.)
vi. Wakala wa serikali aliyeteuliwa kuwakopesha wajasiriamali kwa kupewa fedha za
Serikali (Mfano; Mfuko wa raisi – PTF).
vii. Benki za biashara. Lakini mjasiriamali unatakiwa kuwa makini sana na mikopo ya
benki kwa kuelewa vizuri masharti yake kabla ya kusaini mikataba ya mikopo
MATUMIZI MAKUU YA MTAJI WA BIASHARA
Fedha taslimu au kianzishio cha biashara
Kununua vifaa
Kulipa mishahara
Kodi
Soko
N.k
JIKUMBUSHE KWA MASWALI HAYA MUHIMU!!!!!
1. Ibrahim Bacca amekuwa fundi wa magari kiasi kwamba hajui kabisa maana ya
UMAFUTI, anahitaji kujua vitu vya msingi vinavyounda UMAFUTI, hasara na faida
zake. Unaweza kumsaidia?
2. Mawazo ya biashara, mara chache hutokea yakiwa yamejitenga na mtu kuokota, kwa
kawaida huambatana na vigezo ambavyo ndivyo vyanzo vya mawazo hayo. Jadili.
3. Ni ukweli usiopingika kwamba kuwa na wazo la biashara ni suala moja na kulibadili
wazo husika kuwa biashara ni suala jingine. Hivyo basi, wazo husika liwe mahususi ni
lazima kukidhi vigezo vya fursa. Taja sifa tano za fursa za biashara.
4. ‘’Kumbuka kwamba kitu muhimu katika biashara ni kuuza bidhaa/huduma, hivyo
mteja ni mtu muhimu sana katika biashara!’’Alisema Bw.Matagiri. Kwa hiyo ikiwa
mjasiriamali anapenda wateja kununua bidhaa/huduma anayotoa ni lazima kutekeleza
mambo muhimu katika soko. Fafanua msomo huo kwa hoja NNE.
5. Wote tunatambua kuwa taarifa zina thamani, lakini si taarifa zote zina thamani kwa
wajasiriamali. Fafanua taarifa muhimu kwa biashara.
18
3. Ufadhili
3.1: AINA ZA UMILIKI WA BIASHARA
Umiliki pekee (binafsi) (Mmoja)
Ushirikiano
Shirika/ Kampuni
1. UMILIKI PEKEE (MMOJA)
Huu ni umiliki wa biashara ambapo mtu mmoja anawekeza mtaji wake, ujuzi, maarifa na nguvu
kazi binafsi katika kusimamia biashara. Mfano; duka la nyumbani, n.k
2. USHIRIKIANO
Hii ni aina ya umiliki wa biashara ambapo watu au makundi mawili na Zaidi huungana
kutengeneza biashara yao kwa lengo la kupata faida, faida yao hugawanywa kutokana na zao
la uwekezaji.
Mfano: A + B = AB CO.
3. SHIRIKA/KAMPUNI
Hii ni ain aya umiliki wa biashara ambayo huwa na kikomo cha madeni ya uwekezaji. Biashara
huwa na utofauti wa umiliki kwa watenda kazi wake, huweza kuwa ya kutengeneza faida au
kwa ajili ya jamii.
KAMPUNI; Hii ni biashara inayomilikiwa kwa uwekezaji mkubwa wa hisa za watu
mbalimbali, huanzishwa na kuendelezwa kwa sheria za nchi husika.
19
USHIRIKIANO - Rahisi kuanzisha - Deni halina kikomo
- Gharama ndogo kuanza - Hakuna mwendelezo
- Mtaji huongezeka - Mamlaka ya pamoja
- Uongozi wa kushirikiana. - Ugumu wa kuongeza mtaji
- Uwezekano wa faida za kodi - Ugumu kupata washirika
wazuri.
Mtu mmoja au kundi moja Hugawana faida kwa Huweza kuwa ya kutaka faida
humiliki asilimia za uwekezaji
Hupata hasara yote Hufanya maamuzi kwa Kugawana faida kutokana na uwekezaji
ruhusa ya wote wa hisa
20
Hakuna sheria nyingi Mmoja akifa au Ni kubwa, hulindwa na serikali
kuchizika huvunja
ushirika
21
5. hupelekea ukweli na uhalisi wa wafanyakazi wawapo kazini
6. husaidia wafanyakazi kufikia malengo yao kazini
7. huleta matokeo
3.3: UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU KATIKA BIASHARA
MAANA YA UTUNZAJI KUMBUKUMBU:
Ni kitendo cha kuhifadhi, kujali na kuweka taarifa zote za maandishi katika vitabu muhimu
vya biashara.
AU; Ni kitendo cha kuandikisha taarifa za biashara kwenye vitabu vya kampuni.
AINA ZA UTUNZAJI KUMBUKUMBU:
1. Kumbukumbu za kifedha
2. Kumbukumbu zisizo za kifedha
A) UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZISIZO ZA KIFEDHA.
Ni utunzaji wa kumbukumbu zisizohusiana na fedha kabisa, yaani zinahusika na
kuendesha biashara lakini si kutokana na fedha. Mfano, bidhaa, majina ya waajiriwa,
rushwa n.k
22
Kuna aina nyingi zaa vitabu zinatumika kuwekea kumbukumbu, hujulikana kama vitabu vya
ziada. Hutofautiana kati ya biashara moja na nyingine. Hata hivyo kuna baadhi ya vitabu
ambavyo hutumika katika biashara zote.
Kabla ya kuchagua aina ya kitabu unachotaka kutumia, unapaswa kutafuta taarifa unazohitaji
kwa ajili ya kuendesha biashara. Kumbukumbu utakazo andaa lazima ziendane na uendeshaji
wa biashara yako.
USIMAMIZI WA FEDHA
i) Usichanganye fedha za biashara na za binafsi !
(ii) Jilipe ujira (mshahara) kutokana na biashara yako. Wewe mwenyewe uwe
mwajiriwa katika biashara yako.
(iii) Tofautisha fedha zinazotokana na mauzo toka kwenye: fedha za mtaji,akiba na
nguvukazi.
(iv) Tunza kitabu cha fedha taslimu na andika fedha yote inayoingia na kutoka katika
biashara.
(v) Tumia fedha iliyotokana na mauzo kwa madhumuni yaliyokusudiwa na kupangwa
VITABU VYA KUTUNZIA KUMBUKUMBU
Vitabu vifuatavyo vinaweza kuwa muhimu kwa ajili ya kuandikia taarifa za biashara
yako:
• Kitabu cha oda
• Kitabu cha manunuzi
• Kitabu cha mauzo
• Kitabu cha fedha taslimu
• Kitabu cha wadaiwa
• Kitabu cha wanaokudai
3.4: USIMAMIZI WA MAUZO
Mauzo ni neno linaloakisi muamala baina ya pande mbili yaani muuzaji na mnunuzi ambapo
mnunuzi anapokea bidhaa/huduma wakati muuzaji anapokea fedha (dhamana y mauzo) wakati
wa mabadilishano.
Pia, hujulikana kama makubaliano ya pande mbili ambapo bidhaa au huduma
hubadilishwa kwa kiasi cha malipo ya kutoa bidhaa/ huduma hiyo.
Mfano; A; Nahitaji kununua chupa mbili za maji
B; Karibu, chupa moja ni tsh 500
C; Sawa, chukua 1,000, nipe maji.
MBINU/UJUZI UNAOTAKIWA WAKATI WA KUFANYA MAUZO
Kujiamini
Kuwa msikivu
23
Kushawishi
Kutengeneza mahusiano mazuri
Hamasa binafsi
Mtulivu
Kuwa tayari
HATUA ZA KUZINGATIWA WAKATI WA KUFANYA MAUZO
1.UTAYARI/UANGALIFU
Ni lazima wauzaji kuwa waangalifu na kuwa tayari wakati wanataka kufanya mauzo,
ni hatua ya kwanza: Mf. Kusalimiana au kushikana mikono
2. KUTAMANI KUFANYA MAUZO (HAMU)
Muuzaji anatakiwa kutengeneza hamu kwa mteja kutamani bidhaa yake.
3. KUDHIBITI VIKWAZO
Wakati mwingine mteja huwa na vikwazo kabla ya kununua bidhaa, hivyo, muuzaji
hutakiwa kuwa na macho ya kuona na kudhibiti hilo.
4. KUTENDA (KUFUNGA MAUZO)
Baada ya kudhibiti kila kitu, muuzaji anabadilishana na mteja wake bidhaa au huduma
kwa fedha kama namna ya mabadilishano.
SIFA MUHIMU KWA WAUZAJI WENYE MAFANIKIO
Kuwa na mtazamo chanya
Muonekano chanya (utanashati)
Kujiamini
Kuwa msikivu
Kushawishi
Kutengeneza mahusiano mazuri
Hamasa binafsi
Mtulivu
Kuwa tayari
3.5: KUMRIDHISHA MTEJA
Mteja ni mtumiaji wa mwisho wa bidhaa/huduma/mazao.
-Kwa maana nyingine, ni mtu au shirika linalonunua bidhaa au huduma kutoka kwa mtu au
shirika jingine.
Hivyo mteja inabidi aangaliwe kama ndiye uhai wa biashara. Maana ya kumridhisha
mteja Mteja anakuwa ameridhika ikiwa mahitaji, matakwa na matarajio yake
yamekidhiwa.
24
MAKUNDI YA WATEJA
1) Wateja wa ndani: Hawa ni wateja ambao hufanya kazi Pamoja na muuzaji wa
bidhaa/huduma. Ni wafanyakazi wenzi pia!
2) Wateja wa nje: Hawa ni wateja ambao hutokea nje ya sehemu unayofanyia kazi au
kampuni yako.
Umuhimu wa kumridhisha mteja;
Wateja wanaporidhika inakuwa rahisi hata kulipa bei ya juu zaidi na hivyo kuleta
faida zaidi.
Wateja wanaporidhika husambaza sifa nzuri za biashara na hivyo kuleta wateja
wapya.
Wateja wa zamani hurudi tena
Kuongezeka kwa wateja huongeza mauzo na faida pia
Wateja wakiongezeka huongeza ari ya mfanyabiashara na wafanyakazi, na hivyo
kuboresha utendaji wao wa kazi.
Biashara inaweza kuongeza uhai na kushamiri kwa muda mrefu.
3.6: KUPANGA GHARAMA ZA BIDHAA AU HUDUMA
Kuendesha biashara ndogo kunahitaji kufahamu namna ya kukokotoa gharama na
kupanga bei. Unataka kukokotoa gharama zipi? Utajuaje gharama ya ama kila bidhaa
au huduma? Mbinu zipi zinatumika katika kupanga bei ya kuuzia? Maswali yote hayo
yatashughulikwa katika moduli ya pili.
Maana ya gharama
Gharama ni fedha unayotoa ili kuzalisha/kutengeneza bidhaa/huduma au ni jumla ya fedha
unazotumia katika kuendesha biashara.
Kupanga gharama maana yake ni nini?
Kupanga gharama ni kukokotoa kiasi ulichotumia katika kutengeneza/kuzalisha bidhaa
au huduma ya kuuza.
Aina ya gharama: Katika biashara kuna aina mbili za gharama:
Gharama za moja kwa moja
Gharama zisizo za moja kwa moja.
1. Gharama za moja kwa moja; Gharama za moja kwa moja ni gharama ambazo
zinahusika moja kwa moja katika uzalishaji wa bidhaa au kutoa huduma. Mfano,
gharama za malighafi, na nguvukazi.
2. Gharama zisizo za moja kwa moja; Gharama zisizo za moja kwa moja ni zile
gharama nyinginezo zinazohusu uendeshaji wa biashara na ambazo hazihusiani moja
kwa moja na utengenezaji wa bidhaa au kutoa huduma. Mfano wa gharama zisizo za
moja kwa moja ni: • Gharama ya pango ( nyumba/frame), Kupungua thamani kwa
vifaa, nyumba, mashine, Kukarabati vifaa mashine, Maji na umeme
25
Maana ya Kupanga bei: ▪ Namna unavyotafuta kiasi gani wateja walipe ili wanunue bidhaa
yako au ▪ Namna unavyoamua kuhusu bei ambayo utawatoza kwa ajili ya bidhaa yako.
Kwanini unapaswa kupanga bei ya bidhaa zako? Yakubidi upange bei ya bidhaa zako ili uweze
kufahamu endapo unatengeneza faida au hasara kwenye biashara yako.
MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA KUPANGA BEI
Gharama ulizotumia
Faida unayoitaka
Bei za washindani wako
Bei ambazo wateja wako tayari.
NJIA ZA UPANGAJI BEI
1. Njia ya ongezeko la gharama (Cost-plus) Sehemu au asilimia ambayo unaongeza
kwenye gharama za uzalishaji wa bidhaa/ huduma ili kupata bei ya kuuzia huitwa
kiwango cha faida (profit mark up).
Wajasiriamali wengi huchukua 10 – 50% kama kiwango chao cha faida lakini pia hutegemea
hali ya soko. Bei iliyofanyiwa hesabu ni ile ambayo mjasiriamali anataka kuuza bidhaa yake
au huduma. Lakini vile vile inawezekana siyo bei atakayofanikiwa kuuza! Hii inatagemea hali
ya soko.
2. Njia ya ulinganisho (Comparative method) Njia hii, unalinganisha bidhaa/
huduma yako na soko, kwa kutegemea ubora wake na gharama za uzalishaji, unaweza
kuweka bei rahisi, bei kubwa zaidi au ikalingana na ile ya washindani wako.
3. Njia ya nini soko linaweza kulipa Njia hii inatagemea dhana ya uwingi na uhitaji
wa bidhaa hiyo kwenye soko.
Kwa mfano, iwapo bidhaa haipatikani kwenye soko, basi bei ya bidhaa hiyo inaweza kuwa ya
juu kuliko ile iliyokadiriwa na nyongeza ya thamani
JIKUMBUSHE KWA MASWALI HAYA MUHIMU!!!!!
1. Toa maana ya maneno haya;
A) Bei
B) Gharama
C) Mteja
D) Mauzo
E) Kumbukumbu za fedha na zisizo za kifedha
2. Eleza faida sita za kutunza kumbukumbu
3. “Ni kweli kwamba, si kila mtu ni muuzaji kwani, Maisha ya muuzaji katika soko ni
Maisha yake binafsi”. Thibitisha msemo huo kwa hoja sita.
4. Kwanini tunapaswa kuwaridhisha wateja wetu?
5. Kwa kinagaubaga eleza, namna yua kuwasimamia wafanyakazi katika biashara.
26
4.0: KUANDAA MPANGO (MCHANGANUO) WA
BIASHARA
Ukiwa na wazo zuri la biashara, hatua inayofuata ni kuandika wazo la biashara.
Mpango wa biashara ni nini? Mpango wa biashara ni: Ni waraka/maelezo ya kina
uliotayarishwa na mtu/watu wanatarajia kuanziaha biashara au ambaye tayari yupo
kwenye biashara.
Maelezo haya huweka bayana biashara husika na mipango yake kwa kipindi maalum (k.m
mwaka mmoja hadi mitano). Kwa maneno mengine Mpango wa biashara ni kiongozi cha
mjasiriamali katika kuendesha biashara.
NI NINI MATUMIZI YA MPANGO WA BIASHARA?
Mpango wa biashara una matumizi makuu mawili. Inatumika (kwa ajili ya biashara yenyewe)
ndani ya biashara au nje ya biashara. yenyewe.
a) Ndani ya biashara Hapa ni pale ambapo mpango hutumika kama kiongozi katika biashara
ili kumsaidia mwenye biashara kuona namna biashara itakavyoanza au inavyoendelea na pia
kuweza kuona matatizo/vikwazo au fursa. Hapa hutumiwa na menejimenti tu Pamoja na bodi
ya wakurugenzi.
b) Nje ya biashara; Wakati Mpango wa biashara unapotumika kupata mkopo kutoka kwenye
vyombo vya fedha (mpango huo huitwa ni nje ya biashara. Mfano; Benki, Serikali, Wadau,
Mikopo, Watafiti, Wateja, Wasambazaji n.k
NAMNA YA KUTAYARISHA MPANGO WA BIASHARA
Kama utaanzisha biashara mpango wako uahitaji kuonyesha yafuatayo:
1. Maelezo kuhusu asili ya biashara husika.
Maelezo hayo ni pamoja na: - Jina la biashara inayokusudiwa kuanzishwa
- Aina ya bidhaa/huduma unayotka kuzalisha/kutoa k.m kutengeneza viti na vitanda
- Tarehe unayokusudia kuanza biashara hiyo k.m tarehe 1 Septemba,2006
- Jina lako ukiwa ni mmiliki wa biashara hiyo k.m Mohamed na Juma
- Uzoefu wako katika kuendesha biashara k.m uzoefu wa miaka 2 kama fundi seremala.
2. Mahali/eneo la biashara
Mahali au sehemu utakapofanyia biashara.
3. Bidhaa/huduma
Elezea aina ya bidhaa/huduma biashara yako itahusika na nini.
4. Mpango wa masoko
Inakubidi kufanya utafiti wa soko kwa kujiuliza mwenyewe maswali yafuatayo:
- Una uhakika wa kuwepo watu watakaohitaji kununua kutoka kwako
27
- Ni kwanini wanunue kutoka kwako? Je, ni kwa kuwa bidhaa/huduma ni rahisi zaidi
au haipatikani katika eneo husika au ni bora zaidi?
- Utawafahamishaje watu/wanunuzi kuhusu bidhaa/huduma yako? Utaweka
matangazo/bango sokoni/mahala pa kuuzia au utawatembelea watu majumbani mwao
na kuwaelezea kuhusu/bidhaa/huduma yako? - Utauzaje? Utauza moja kwa moja kwa
walaji au utawauzia wateja wa jumla?
- Washindani wako watakuwa ni akina nani na bidhaa/huduma zao ni za aina 35ain na
bei zao zikoje n.k?
5. Mpango wa uzalishaji
Hapa unatatakiwa kuonyeha wazi kwamba unafahamu mchakato mzima wa uzalishaji wa
bidhaa/utoaji wa huduma.
6. Uratibu na usimamizi
Hapa unahitajika kuonyesha ni wasaidizi wangapi watahitajika katika kuendesha
biashara.
Unaweza kuanza mwenyewe lakini kadiri muda unavyokwenda na biashara kukua
utahitaji watu wa kukusaidia.
Ni vema pia kuweka makisio ya kiasi cha kujilipa na utakaowaajiri.
7. Ugavi / wasambazaji Hapa unatakiwa kuonyesha :
- Wapi utapata malighafi / bidhaa
- Utahitaji kiasi gani.
- itagharimu kiasi gani.
8. Mashine na vifaa Hapa utatakiwa kuonyesha:
Vifaa utakavyotumia,
Mahitaji ya kiwanda (kama jengo, banda n.k)
Utakakopata vifaa/mashine na gharama yake.
9. Uwekezaji na mpango wa fedha
Hapa utatakiwa kutoa mhutasari wa kiasi cha fedha za kuanzia biashara utakakozipata.
- Kiasi cha fedha unazohitaji (= uwekezaji) na matumizi yake (k.m kununulia
vifaa/mashine, jengo, malighafi)
- Kiasi gani cha fedha zako utawekeza katika biashara
10. Mtiririko wa fedha
Jambo la mwisho ni kutayarisha mtirirko wa fedha/ mapato halisi. Hili utatakiwa
kuonyeha katika kipindi k.m mwaka mmoja: - Kiasi cha fedha unachotarajia kupata
kutokana na mauzo kwa kipindi cha mwezi moja
UMUHIMU WA MPANGO WA BIASHARA:
Huwa ramani katika Maisha ya biashara
Hutumika kufanya maamuzi
28
Huongoza shirika ili kufikia lengo
Huleta matokeo kirahisi na mrejesho wake
Hutumika kama kumbukumbu
Huleta faida kwa wawekezaji
Hukuza mahusiano baina ya biashara na wadau wake. N.k
29