Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 26

NENO LA AWALI

Naitwa Mohamed Bassanga wengi hunifahamu kama Coach Bassanga Kwa


jina la kazi,ni mtaalamu wa maswala ya fedha,ujasiriamali na uchumi,ni
mkurugenzi na muanzilishi wa Taasisi ya YEMCO,ni mkurugenzi wa YEMCO
MICROFINANCE,ni mkurugenzi wa YEMCO PRODUCTION na ni Rais wa
VICOBA ENDELEVU TANZANIA. Nimekuwa nikiwasaidia watu wengi
kutimiza ndoto zao na malengo yao kwa kutumia mfumo wa YEMCO
VICOBA ENDELEVU.

Ndugu Msomaji wa e-book hii ya mfumo wa vicoba,kwanza nikupongeze


kwa kutenga muda wako kusoma e-book yangu hii maana ungeweza
kabisa kuwekeza muda wako kwenye mambo mengine,lakini pia
nikupongeze kwa maana muda unaouwekeza kwa madini ambayo utaanza
kuyasoma sekunde chache zijazo kutoka kwenye e-book hii hautaujutia
kabisa siku zote za Maisha yako maana utakayokwenda kujifunza kwenye
e-book hii yatakuongezea kitu kikubwa sana kwenye Maisha yako.

Nikusihi uisome e-book hii mwanzo hadi mwisho na ukiweza uisome tena
na tena maana utakapokuwa umeimaliza basi utakuwa umeshakuwa
mtaalamu wa mfumo wa vicoba,ambaye hakuna mtu yeyote ambaye
atakudanganya chochote kuhusu mfumo wa vicoba.

Nakutakia safari njema yakuanza kusoma kitabu hiki naamini kabisa


utaimaliza salama na utakuwa miongoni mwa watu wachache washindi.

karibu
YALIYOMO

1.KUHUSU TAASISI YA YEMCO

2.DIRA, DHAMIRA, MALENGO, KAZI NA NYANJA ZA UONGOZI.

3.KAZI NA WAJIBU WA VIONGOZI.


4.MADARAJA KATIKA VIKUNDI VYA VICOBA

5.MIKOPO NA UKOPESHAJI

6.MIFUKO YA KUWEKA AKIBA KWA KILA MWANACHAMA

7.TARATIBU ZA KIKUNDI KUFUNGA MWAKA NA KUGAWANA


FAIDA

8.HISTORIA YA MFUMO WA VICOBA


MUONGOZO KUHUSU TAASISI
KUHUSU TASISI
YEMCO VICOBA TANZANIA ni iliyoanzishwa, kwaajili ya kuwawezesha kiuchumi vijana,
wanawake na walemavu.Taasisi ya YEMCO VICOBA TANZANIA ni Taasisi Mwamvuli wa
vikundi vya vicoba endelevu,ambapo hufanya kazi ya kuanzisha,kufundisha na kulea
vikundi vya vicoba endelevu Tanzania nzima.Taasisi hii makao yake makuu yapo sinza
white inn,lakini taasisi ya YEMCO VICOBA TANZANIA Inavikundi maeneo mbalimbali
nchini ambayo unaweza kujiunga na vikundi vyetu popote ulipo tofauti na makao makuu.

DHAMIRA YA TAASISI
Kuwa na vikundi bora vya VICOBA ENDELEVU, Vitakavyokuwa na wanachama wenye
maisha bora na ya furaha.
MALENGO YA TAASISI
1. Kuhamasisha ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi kwenye shughuli za uzalishaji
mali na shughuli mbalimbali za maendeleo.
2. Kuwawezesha wanavicoba wote kiuchumi ili kuongeza uwezo wao wa kipato kwa
kupitia ujasiriamali na vipaji walivyonavyo.
3. Kuhamasisha na kutoa elimu ya Vicoba endelevu.
4. Kuwawezesha wananchi kupambana na tatizo la changamoto za ajira ili wajiajiri

KAZI ZA TAASISI
1. Kutoa mafunzo ya kujitambua, ujasiriamali na fedha
2. Kuhamasisha, Kuanzisha, kufundisha na kuvisimimamia vikundi vya vicoba
endelevu
3. Kutafuta fursa mbalimbali kutoka kwa wadau binafsi na serikali na kuzipeleka kwa
wanavikundi
4. Kuhamasisha ushiriki na ushirikishwaji wa wanavicoba katika shughuli za
maendeleo
5. Kuandaa na kuendesha semina na mafunzo mbalimbali kwa wanavikundi ili
kufungua fikra zao za mafanikio
6. Kutatua changamoto mbalimbali zinazotokea kwenye vikundi

Mitandao yetu ya kijamii


instagram@yemco.vicoba

facebook@Yemco Tanzania
Twitter@ YEMCO TANZANIA
Linkedin@ YEMCO TANZANIA
Website: www.yemcotanzania.com
MUONGOZO WA MFUMO WA VICOBA

Watu wengi wamekuwa wanasikia tu kuhusu mfumo wa vicoba lakini hawafahamu kwa undani
juu ya mfumo wa vicoba kupitia ukurasa huu sekunde chache zijazo utakwenda kujifunza kwa
undani juu ya mfumo wa vicoba

VICOBA NI NINI?
VICOBA
Hiki ni kifupi cha maneno Village Community Bank
VICOBA ni benki za kijamii, ambazo zinamilikiwa na wanajamii wenyewe wakiwa kama wabia
na pia wakiwa kama wateja wanaopata huduma kupitia benki hizo. Kwa sera ya huduma ndogo
za fedha ya mwaka 2018 vikundi vya vicoba vimepewa jina la COMMUNITY
MICROFINANCE GROUP

mfumo huu unaundwa na kikundi cha Kuanzia watu 15-50 wenye malengo ya kuwezeshana
kiuchumi, mfumo huu huwawezesha wananchi kujiunga katika kikundi na kuanzisha mfuko wa
kuweka akiba na baadae kuweza kukopeshana kwaajili ya kuanzisha biashara, kuendeleza
biashara au kuanzisha miradi ya kuwaingizia kipato na kutatua matatizo ya dharura
yanayowakabili wananchi husika ya kila siku. mfano magonjwa,vifo,ada za shule,kodi za
pango,shere n.k.
Ndani ya kikundi cha watu 50 watu hawa wanaweza kuwa wanatoka sehemu moja au wanatoka
sehemu mbalimbali lakini wanakuwa na sehem moja ambayo hukutana kila wiki,na wale ambao
ni wafanyakazi au wanafunzi watakuwa wanakutana kila mwezi mara moja kwasababu ya
majukumu yao na kwa watu ambao wanajiunga kwenye kikundi husika lakini wapo mbali na
kikundi kama mkoani au nje za nchi basi wao watakuwa wanahudhuria mara moja kwa mwezi
na wale wan je ya nchi wanahudhuria mara moja kwa mwaka au wanapopata nafasi ya kurudi
nchini kwao,lakini watakuwa wananunua tu hisa zao kwenye kikundi kila wiki.Kwahiyo kama
wewe leo ukijiunga kwenye kikundi cha vicoba utaunganishwa kwenye kikundi ambacho kiko
tayari na utaanza rasmi kufahamiana na wanachama wenzako.Na kama unajiunga na vicoba
lakini uko nje ya nchi au mkoani ukishasajiliwa kama mwanachama utaungwa kwenye grupu la
watsap la wanachama wenzako ili kufahamiana nao na kuanza taratibu za kununua hisa.
Ndani ya kikundi cha watu 15-50 hutengenezwa vikundi vidogovidogo vya watu watano watano
kwaajili ya kudhaminiana wakati wa kuchukuwa mikopo. Vikundi hivi vidogovidogo
huchaguliwa kwa watu wanaofahamiana ambao wanakuwa wameletana kwenye kikundi au
kiongozi wa kikundi ambaye ni mwenyekiti atawapanga tu kwenye makundi yao bila kujali
kufahamiana kwao.Na kama kikundi wanachama wakizidi 50 basi kikundi kimoja cha vicoba
kinaweza kutengeneza vikundi vingine ndani yake na kuvipa majina sawa na kikundi cha
kwanza lakini kwa kuvitenganisha kwa namba au herufi.Kwa mfano MALEZI DAIMA
VICOBA “A”,MALEZI DAIMA VICOBA “B” na kuendelea
Mfumo wa vicoba rasmi umeingia Tanzania mwaka 2002 kutokea India ambako ndio uliasisiwa
na mtu mmoja anaitwa Mohamed Yunus.Baada ya kuona matokeo makubwa ya mfumo wa
vicoba India ndipo ukaingia Tanzania kwaajili ya kuokoa Maisha ya watu masikini sana.

FAIDA ZA KUJIUNGA KWENYE KIKUNDI CHA VICOBA

Unapojiunga kwenye kikundi cha YEMCO VICOBA tarajia kupata faida zifuatazo
q Kujengewa uwezo na desturi ya Kujiwekea akiba.Kuweka akiba sio tabia za watu
wengi ndio maana watu wengi wanabakia masikini hivyo unapojiunga na YEMCO
VICOBA tunakujengea tabia ya kuweka akiba kwasababu kuweka akiba kwetu ni jambo
la lazima na usipoweka akiba utatozwa faini hivyo huo ulazima unakuweka wewe
kwenye nafasi ya kujenga tabia ya kuweka akiba tabia ambayo itakupelekea kuwa
Tajiri.Kwahiyo hata ukiwa na malengo yako ni rahisi kuyatimiza lakini pia hata ukipata
dharula au changamoto yeyote ni rahisi sana kuitatua.
q Kupata fursa ya mafunzo,ukijiunga na yemco vicoba utapata mafunzo ya
kujitambua,mafunzo ya ujasiriamali na fedha.Kwahiyo hautakuwa tena na changamoto
ya kukuza biashara yako au kwa wale ambao hawana biashara hautakuwa tena na tatizo
la kukosa biashara
q Kupata mikopo kwa urahisi,ukijiunga na yemco vicoba utapata faida ya kupata mikopo
kwa urahisi Zaidi na isiyokuwa na riba.Yemco vicoba tunatoa mikopo kwa wajasiriamali
na wafanyabiashara ya kuanzisha biashara na kuendeleza biashara lakini pia mikopo ya
dharula.Kwahiyo hautakuwa tena na tatizo la kukuza biashara zako na kufikia malengo
yako.
q Kupata fursa za kukutana na watu mbalimbali katika vicoba,serikalini na wadau
binafsi.yemco itakukutanisha na watu ambao ulikuwa hujawahi kukutan anao kwenye
Maisha yako ambao wengine watakusaidia kutimiza ndoto zako na wengine watakuwa
wateja wako
q Kutimiza malengo yako kwa urahisi, yemco inakusaidia kutimiza malengo yako ambayo
ulikuwa siku nyingi unatamani kuyatimiza.
MADHUMUNI YA KUANZISHWA KWA MFUMO WA YEMCO
VICOBA
I. KUWAJENGEA UWEZO NA DESTURI YA KUWEKA AKIBA WANANCHI
Mfumo wa YEMCO VICOBA umeanzishwa maalumu kwaajili yakuwajengea watu wapenda
maendeleo desturi na tabia ya kujiwekea akiba.ambapo kila mwanachama ambaye atajiunga
kwenye kikundi cha YEMCO VICOBA atatakiwa kuweka akiba kila wiki.Kwa wafanyakazi
ambao wanataka kuweka akiba kwa mwezi watatakiwa kuweka mwisho wa mwezi lakini
wataweka akiba zao za mwezi mzima.pia hata kwa ambao sio wafanyakazi lakini watataka
kununua akiba zao kwa mwezi wanaruhusiwa lakini utaratibu ni kuwa unanunua hisa za mwezi
ujao na sio mwezi uliopita.Katika mfumo wa YEMCO VICOBA Tunajiwekea akiba katika
maeneo yafuatayo.
(A) MFUKO WA HISA

HISA NI NINI?
Hisa ni akiba ambazo kila mwanachama atakuwa anajiwekea kwenye kikundi kwaajili ya
maendeleo yake binafsi, ambapo hisa hizi mwanachama atakuwa anajiwekea kwaajili ya
kuanzisha biashara, kuendeleza biashara, kujenga au kuboresha makazi au kununua magari
Mwanachama atakuwa anaruhusiwa kununua kuanzia hisa moja mpaka kadri ya uwezo wake
kulingana na malengo yake na ndoto zake mwenyewe kwa kila wiki ambayo mwanachama
anajiwekea akiba. Katika mfumo wa YEMCO VICOBA ununuaji wa hisa utakuwa kwa viwango
tofauti tofauti kulingana na kila mwanachama.Ambapo utaratibu wa kununua hisa Upo kama
ifuatavyo

DARAJA “A” PREMIUM MEMBER


Hili kundi la kwanza la wanachama ambao wananunua hisa Tsh 50000/= kima cha chini
kwa kila wiki.Aambapo kama mwanachama akiamua kuanza uwanachama wake kwa
kiwango hiki haruhusiwi kununua hisa chini ya kiwango hiki

FAIDA ANAZOPATA MWANACHAMA AMBAYE ATAKUWA KWENYE DARAJA HILI


i. Atapewa kipaumbele wakati mikopo
ii. Atapewa zawadi (recognization)mwisho wa mwaka
iii. Atakuwa na beji maalum itakayomtambulisha kama premium member
iv. Ataingizwa kwenye group la preum taifa
v. Atapewa nafasi ya kukutanishwa na watu waliofanikiwa ili kumuongezea mbonu na
maarifa yakuzidi kufanikiwa

DARAJA “B” GOLD MEMBER


Hili ni daraja la wanachama ambao wanaweka hisa kuanzia Tsh 30000/= kila wiki bila
kushuka.

DARAJA “C” DIAMOND MEMBER


Daraja hili ni la wanachama ambao wananunua hisa kuanzia Tsh. 20000/= kila wiki na
hazishuki ila wanaweza kununua Zaidi kadri ya uwezo wao
DARAJA D: SOIL MEMBER
Hawa ni wanachama ambao wananunua hisa kuanzia Tsh 10,000/= kila wiki kwa kima cha
chini na wanaweza kununua Zaidi kulingana na malengo yao.

IJULIKANE KUWA VIWANGO HIVI VIMEWEKWA KWAAJILI YA KUWEKA NAFASI NZURI ZA


UNUNUAJI WA HISA NA UKUAJI WA MWANACHAMA.HAYA MADARAJA KILA MTU ANACHAGUA LA
KUANZA NALO NA ANAWEZA KUBADILISHA DARAJA MUDA WOWOTE AMBAO ANAONA INAFAA
KWAKE KUBADILISHA.

KAZI ZA KUHUSU HISA

a) Hisa hukusaidia kupata mkopo kwaajili ya kuanzisha biashara,kuendeleza


biashara,kujenga au kuboresha makazi au kununua gari.Unapokuwa umekuwa
mwanachama kwa miezi mitatu unakuwa unaweza kukopa kuanzia mara moja mpaka
mara tatu ya hisa zako.Maelezo Zaidi ya kukopa utayapata ukifika kwenye mada ya
mikopo na ukopeshaji
b) Mwanachama anaruhusiwa kununua hisa kuanzia kiwango cha daraja lake mpaka
kadri ya uwezo wake,kwenye mfumo wa yemco vicoba hauna kikomo cha kununua hisa
kwa kila wiki,kila mtu anaweza kununua hisa kadri ya uwezo wake kwa kila wiki hakuna
ukomo na ununuaji wa hisa sio lazima uwe wa aina moja bali leo unaweza kununua hisa
nyingi na kesho ukanunua kidogo.
c) Kwenye gawio mwenye hisa nyingi atapata gawio kubwa,kwenye mfumo huu wa
yemco vicoba mwenye hisa nyingi mwisho wa mwaka atapata faida kubwa,faida
zinapatikana kwenye faini ambazo tutakuwa tunazitoza,faida zinapatikana kwenye miradi
ya kikundi na pia faida zinapatikana kwenye mikopo ya faida ambayo tutakuwa
tunakopeshana
d) Ni lazima mwanachama anunue hisa maana ndio msingi wa kikundi na kama hatanunua
hisa atatozwa faini ya kutokununua hisa.hata kama mwanachama atakuwa hajafika
kwenye kikao atanunua hisa kupitia akaunti ya kikundi na baadae atatuma muamala kwa
muhasibu na muhasibu atamuandikia kwenye kitabu chake.Mwanachama ambaye
atashindwa kununua hisa kwa wiki husika kwa sababu za msingi atapaswa kutoa taarifa
mapema kwa mwenyekiti wa kikundi ili asitozwe faini.
e) Hisa ni mali ya mwanachama na anapotaka kujitoa atarudishiwa kwa utaratibu
maalum,Mwanachama akitimiza malengo yake au akifika mwisho wa kuwa kwenye
kikundi anaruhusiwa kujitoa kwenye kikundi ambapo kama mwanachama atataka kujitoa
kwenye kikundi ataandika barua kwa mwenyekiti kutaka kujitoa kisha,atasubiri siku
tisini kurudishiwa hisa zake,wanachama wote watatakiwa kujitoa mwisho wa mwaka wa
kikundi kinapofunga mahesabu na mwanachama atapewa akiba zake zote na faida zake
zote.Kama mwanachama atajitoa katikati yam waka atakatwa 15% ya akiba zake kama
faini ya usumbufu.Na hisa zake zitarudishwa ndani ya siku tisini na endapo kikundi
kitakuwa na mradi ambao kinafanya basi mwanachama atasubiri fedha irudi ndio
arudishiwe.
f) Kama mwanachama amefariki mrithi wake anaweza kurithi hisa zake na akaendelea na
kitabu chake kama kikundi kitamkubali,ikitokea mwanachama amefariki kwenye fomu
ya kujiunga na kikundi kuna taarifa za mrithi ataitwa mrithi kwaajili ya kupewa stahiki za
mwanachama aliefariki lakini pia kama mrithi atapenda kuendelea na kikundi kama
kikundi kitamruhusu basi anaweza kuwa mwanachama na akaendelea na kitabu
husika,kama kikundi kitaona kuwa hawamfai basi watamrudishia stahiki zake.
FAIDA ZA KUNUNUA HISA NYINGI KWENYE VIKUNDI VYA VICOBA
1.Kupata gawio kubwa, ikumbukwe kuwa unaponunua hisa nyingi kila mwisho wa
mwaka unapata gawio kubwa kulingana na hisa zako kwasababu faida hugawiwa
kulingana na idadi ya hisa zako,
2.Kupata mikopo mikubwa, ukiwa na hisa nyingi unaweza kupata mikopo mikubwa
kwasababu ukumbuke kuwa mkopo wa kwenye vicoba ni kuanzia mara moja mpaka
mara tatu ya hisa zako kwahiyo jinsi hisa zako zilivyo ndivyo utakavyopata mkopo
kwahiyo kama unamalengo makubwa nunua hisa nyingi.

3.Kufanya mambo makubwa (Malengo makubwa kutimiza),manunuzi ya hisa nyingi


hukuweka kwenye nafasi ya kutimiza mambo makubwa na malengo makubwa hivyo
unachotakiwa kufanya kama unamalengo makubwa nunu hisa nyingi zikuweke kwenye
nafasi nzuri ya kupata mkopo utakaokuwezesha kutengeneza mambo makubwa.

4.Hisa nyingi ni dhamana kwa mikopo midogo midogo,ukiwa nah isa nyingi
inakusaidia unapokopa mkopo mkubwa zinakuwa kama dhamana ya mkopo wako.Mfano
unahisa za milioni moja unataka mkopo wa laki tis abasi hisa zako ndio dhamana yako.

(B) MFUKO WA JAMII


JAMII NI NINI?

Jamii ni akiba ambazo mwanachama anaweka kwenye kikundi kwaajili ya kumsaidia kwenye
mambo ya dharula ambayo yanaweza kumkuta mwanachama akiwa hana pesa.Mfano
Kuuguwa,kuuguza,kifo,ada ya shule ya watoto,kodi n.k.Kila mwanachama ataweka jamii kila
wiki Pamoja na hisa kulingana na uwezo wake.Kwenye uwekaji wa hisa kule juu tumeweka
madaraja ya uwekaji wa hisa lakini kwenye jamii hakuna madaraja kwahiyo jamii yenyewe kima
cha chini kwa wiki ni Tsh 2000/= Tu ambapo mwanachama anaweza kununua jamii kwa wingi
ambao anaweza kununua.Kwenye uwekaji wa akiba jamii na hisa mtu anaweza kununua sawa
lakini hawezi kununua jamii nyingi kuliko hisa.Kwahiyo sasa kama wewe ni mwanachama wa
daraja la 10000 kwa wiki la hisa na jamii shilingi 2000 kima cha chini utakuwa unanunua hisa na
jamii tsh 12000/=.Unaweza kununua kwa kiwango kikubwa uwezavyo.
q Mfuko wa jamii pia ni mali ya mwanachama na anastahili kurejeshewa pindi atakapojitoa
kwenye kikundi kwa utaratibu maalum,mfuko wa jamii kama mtu anajitoa kwenye
kikundi basi atachanga kwenye hisa zake na kukatwa 10% kama kawaida kama atakuwa
amejitoa katikati yam waka na zitakazobakia basi atarudishiwa kama kawaida.
q Mwanachama atakaefariki na jamii zake pia atapewa mrithi wake kama alikuwa ahana
deni la mkopo wa jamii.Kama atakuwa na deni basi atakatwa deni lake kwanza kisha
ndio atarejeshewa jamii zake
q Jamii hizi kila inapofika mwisho wa mwaka huwa tunarudishiana kama mtu hadaiwi deni
lolote.zinaonganishwa na faida za mwanachama husika

HUO NDIO UTARATIBU WA KUWEKA AKIBA KWA


MWANACHAMA YEYOTE AMBAYE ATAJIUNGA NA KIKUNDI
CHA YEMCO VICOBA
II. KUJIPATIA MIKOPO ISIYOKUWA NA MASHARTI MENGI LAKINI
KWA URAHISI ZAIDI
Dhumuni la pili la kuanzishwa kwa kikundi cha yemco vicoba ni kupata mikopo.Ukiwa
mwanachama kwenye kikundi cha YEMCO Vicoba na ukawa umetimiza miezi mitatu unakuwa
na uwezo wa kukopa kupitia hisa zako na jamii zako ambazo unakuwa umeziweka kwenye
kikundi.Ambapo utaratibu wa kukopa ni kuanzia mara moja ya hisa ambazo unakuwa umeweka
mpaka mara tatu.Kwa mfano kwenye kikundi umeweka hisa za laki moja basi utaweza kukopa
kuanzia hiyo laki moja mpaka laki tatu,lakini mkopo wa kwanza kwa mwanachama yeyote ni
kiasi alichoweka kwenye kikundi,mkopo wa pili atakopa mara mbili na mkopo wa tatu sasa
anaweza kukopa mara tatu ya hisa zake au jamii zake isipokuwa mwanachama ambaye anakopa
kwaajili ya kununua kiwanja,nyumba au kununua vyombo vya moto kama gari n.k,huyu
anaweza kukopa mara tatu ya hisa zake hata kama ni mkopo wake wa kwanza na dhamana
zinakuwa nyaraka za hivyo vitu ambavyo amenunua zinawasilishwa kwenye kikundi,kwahiyo
kama mwanachama kanunua gari basi kadi itabakia kwenye kikundi.Mwanachama anaweza
kukopa mara nyingi awezavyo kama atakuwa mrejeshaji mzuri kwenye kikundi.Na utaratibu wa
mikopo upo kama ifuatavyo

MIKOPO NA UKOPESHAJI
Kwenye mfumo wa YEMCO VICOBA tuna mikopo ifuatayo
A.MIKOPO YA NDANI YA KIKUNDI
Hii ni mikopo ambayo mwanachama atakuwa anakopa kwa kulingana na akiba zake ambazo
yeye anakuwa ameziweka kwenye kikundi,mikopo hii huanza kutolewa kwa mwanachama baada
yakuwa ametimiza miezi mitatu kwenye kikundi.ambapo katika sehemu hii ya mikopo tuna
mikopo miwili ambayo ni
1. MKOPO WA HISA

2. MKOPO WA JAMII

B. MIKOPO YA NJE YA KIKUNDI

Kwenye kikundi cha yemco kuna mikopo ya nje ya kikundi,mikopo hii hutolewa kutoka makao makuu ya
taasisi ya YEMCO,mikopo hii ni mikopo ambayo wanachama watakuwa wanakopa bila kuangalia hisa
zao au jamii zao,mikopo hii huanza kukopeshwa kwa kikundi ambacho kinakuwa kimetimiza mwaka
mmoja wa kusimamiwa na taasisi ya YEMCO.Mikopo hii huwa na masharti mbalimbali kulingana na
aina ya mkopo ambapo kikundi kikishatimiza miezi sita sasa kitaanza kuelekezwa aina ya mikopo ya nje
na taratibu zake kama kikundi kinakuwa ndio kimeanza wanachama watatakiwa kusubiri mpaka
watakapoelekezwa kuhusu mikopo ya nje baada ya miezi sita ya kuanzishwa kwa kikundi husika.
MIKOPO YA HISA

v Mikopo ya hisa ni mikopo ambayo hutolewa ndani ya kikundi kutoka kwenye hisa
za mwanachama ambapo mwanachama anaanza kukopa kuanzia mara moja ya
hisa zake mpaka mara tatu ya hisa za mwanachama.lengo la mkopo huu nikuanzisha
biashara,kuendeleza biashara au kufanyia mradi wa maendeleo kwa
wanachama.Mwanachama anapokopa mkopo wa hisa ni lazima atambue kuwa hayo ndio
maeneo ambayo atatakiwa kupeleka mkopo huo na sio maeneo mengine.Mkopo wa hisa
umegawanyika katika sehemu mbili ambazo ni zifuatazo
i. MKOPO WA UWEZESHWAJI.
Mkopo huu ni mkopo ambao mwanachama atakopa kutoka kwenye hisa zake kwa madhumuni
yaleyale ya mkopo wa hisa lakini mwanachama atakopeshwa pesa taslimu kutoka kwenye
kikundi,ambapo kama mwanachama atapewa pesa taslimu basi atarejesha kiasi hicho hicho cha
pesa bila kuongeza kiasi chochote cha fedha.Kiasi alichokopa ndio atakachorejesha,isipokuwa
atalipa Bima tu ya mkopo ya 2% ya mkopo wake ambapo bima zote zinalipwa makao makuu ya
Taasisi ya YEMCO na mwanachama akifa na mkopo basi taasisi italipa deni lililobakia la mkopo
husika kwenye kikundi.Kikomo cha mkopo huu ni Tsh 400,000/= Tu

ii. MKOPO WA MAENDELEO:

Mkopo huu ni mkopo ambao mwanachama atakopa kwenye hisa zake kwa utaratibu ule ule wa
mkopo wa hisa lakini mkopo huu mwanachama anakuwa anakopa Zaidi ya 400,000/= ambapo
mwanachama anakuwa anataka mkopo wa kuanzia 500,000/= na kuendelea,mkopo huu sasa
mwanachama hatapewa fedha cash atalipiwa vifaa ambavyo yeye anataka au vitu ambavyo yeye
anataka kukopa,yeye mwanachama atatafuta hivyo vifaa atakubaliana bei na muuzaji halafu
kikundi kitamlipia yeye atakopeshwa vifaa na kikundi.Kwa mfano Mwanachama AMINA
anataka mkopo wa milioni moja,lengo la mkopo ni kwenye kununua madera kwasababu ndio
biashara ambayo anafanya amina.Hivyo amina ataomba mkopo kwenye kikundi wa milioni moja
kisha amina atatafuta duka ambalo anaenda kununua hayo madela kikundi kitamlipa muuzaji na
amina atachukuwa madera,mkopo huu amina akikopeshwa atarejesha na faida ya 10% hiyo ni
faida ya kikundi ambayo kikundi kitagawana mwisho wa mwaka.Endapo mkopaji akiwa
anakopa lakini ananunua bidhaa kutoka kwa wauzaji wengi atajaza fomu ya uwakala ambapo
mwanachama atafanya kazi yakwenda kununua bidhaa hizo kwa niaba ya kikundi.Hapa kikundi
kitampatia fedha AMINA na atakwenda kununua bidhaa,akishanunua atapeleka vithubitisho vya
kununua bidhaa zake kwenye kikundi husika.
TARATIBU ZA MAREJESHO YA MKOPO WA HISA
Mwanachama ambaye anakopa mkopo wa hisa atarejesha kama ifuatavyo
v Mwanachama atapewa mwezi mmoja bila kufanya marejesho na mwezi unaofata
lazima aanze kufanya marejesho.hii huwa inaitwa grace period.Mwanachama akikopa
atakaa mwezi mmoja halafu mwezi wa pili ndio ataanza kurejesha kwa tarehe ile ile
ambayo yeye atakuwa amekopa kwa mfano mwanachama amekopa tar 1/2/2023 ataanza
kurejesha tar 1/4/2023 huo mwezi mmoja anapewa kwaajili ya kukusanya
marejesho,ambapo utaratibu wa kisheria wa marejesho utakuwa kwa mwezi kwa tarehe
ambayo aliombea mkopo,ijapokuwa mwanachama anaweza kurejesha kwa wiki kama
yeye atakuwa anataka kurejesha hivyo.Mwanachama anapokopa marejesho yake
yatagawanywa kulingana na mkopo wake ijapokuwa anapokopa kama anakopa mkopo
wa maendeleo atakatwa kabisa 10% ya faida ya mkopo wake halafu kitakachobakia ndio
atapewa,kwa mfano mwanachama akikopa 1,000,000/= laki moja ya faida itakatwa
kabisa atapatiwa laki tisa halafu marejesho yake yatakuwa ya milioni moja tu.kwahiyo
itachukuliwa hiyo milioni moja na itagawanywa kwa muda wa mkopo wake ambao yeye
anataka kurejesha litaandikwa rejesho lake rasmi.
v Mikopo ya hisa hutolewa kwa miezi mitatu,sita au mwaka,mwanachama ambaye
anakopa laki nne kushuka chini atarejesha kwa miezi mitatu,mwanachama ambaye
atakopa laki sita kushuka chini atarejesha ndani ya miezi sit ana mwanachama ambaye
atakopa mkopo wa kuanzia laki sab ana kuendelea atarejesha ndani yam waka mmoja.
v Mkopo wa hisa unabima ya mkopo ya 2% ambayo na yenyewe hulipwa kabla
mwanachama hajapewa mkopo.Bima hii ya mkopo humsaidia mwanachama atakapokufa
au atakapopata ulemavu wa kudumu.mkopo utalipwa na bima yake na bimah ii hulipwa
moja kwa moja makao makuu ya YEMCO.
v Kila mkopaji atatakiwa kujaza fomu ya mkopo ambayo itasainiwa na wadhamini wake
wanne,ili kama atashindwa kulipa hisa za wadhamini zitakatwa atakapomalizia mkopo
wake.Mwachama ambaye anakopa mkopo wa hisa kuna fomu ya maombi ya mkopo
lazima ajaze ambapo fomu hiyo itakuwa na taarifa zake,taarifa za biashara yake na taarifa
za wadhamini wa mwanacama ambapo wadhamini wanne wanatoka kwenye kikundi na
mdhamini mmoja anatoka nje ya kikundi,ambapo anaweza kuwa mume au mke wa
mwanachama au ndugu wa karibu.
MFANO WA TARATIBU ZA MAREJESHO YA MIKOPO KULINGANA NA MUDA WA
MKOPO

Katika MFUMO WA VICOBA utaratibu wa mikopo upo kama ifuatavyo


1.MKOPO WA KUANZIA 100000 - 400,000 Unarejeshwa ndani ya miezi mitatu na muda wa
mapumziko wa mwezi mmoja .Kwahiyo itakuwa miezi minne
2.MKOPO WA KUANZIA
500,000 - 3,000,000 UNAREJESHA KWA MIEZI 12 na mwezi mmoja wa
mapumziko.Kwahiyo inakuwa miezi 13
3.MKOPO WA KUANZIA
6,000,000 NA KUENDELEA unaweza kurejesha ndani ya miezi 18 mpaka miaka miwili.
HUo ndio utaratibu wa mikopo na MAREJESHO Nikila mwezi Kwa tarehe ulioomba mkopo.

TARATIBU ZA KUOMBA MKOPO WA HISA


Mwanachama anapotaka kuomba mkopo wa hisa ataenda kwenye kikundi ataomba fomu
ya mkopo atajaza kisha atairejesha fomu ile ya mkopo,kikundi kitaisoma na kuijadili na
baada ya hapo fomu yake itatumwa makao makuu ya yemco kwaajili ya kujiridhisha na
baada ya hapo mkopo wa mwanachama utatoka,kama kikundi kiko mkoani viongozi wa
vikundi watasimama kwa niaba ya taasisi lakini pia wanaweza kutuma fomu za mikopo
kwa njia ya watsap na zikakaguliwa.mkopo wa hisa ni mkopo ambao unachukuwa wiki
mbili hadi wiki tatu kuanzia siku anayoomba mkopo mpaka kukamilika kutolewa kwa
mkopo ijapokuwa kama mwanachama atakuwa amekamilisha fomu yake mapema na
amekidhi vigezo basi anaweza kukopesha hata chini ya muda huo wa mkopo.

MIKOPO YA JAMII

o Mkopo wa jamii hutolewa kwa wanachama ambao wamepata shida za


dharura.Mkopo huu sio kwaajili ya kufanyia biashara bali kwaajili ya kufanyia mambo
ya dharura ambayo yanakulazimu wewe kuyatafutia ufumbuzi wa dharura kwa mfano
magonjwa au kulipia kodi au ada ya mtoto shule,japo wapo wanavicoba ambao sio
waaaminifu huchukuwa mikopo ya jamii na kupeleka pasipohusika pia.
o Mikopo ya jamii hukopa mara tatu ya jamii za mwanachama na atarudisha bila ziada ya
mkopo kwa mfano mwanachama anajamii za laki moja anaweza kukopa laki tatu na
atarejesha hiyo hiyo laki tatu bila ziada yeyote
o Mikopo ya jamii hurejeshwa ndani ya miezi mitatu tu,hakuna kupitisha miezi mitatu
kwenye mikopo hii.ambapo mwanachama anaweza kurejesha kila mwezi au akaa nao
huo mkopo mpaka miezi mitatu ndio akarejesha
o Mkopo wa jamii hauna wadhamini wa nje,dhamana za mkopo huu ni hisa za
mwanachama husika,kwahiyo mwanachama haweza kukopa Zaidi ya hisa zake
o Mkopo wa jamii hauna bima ya mkopo kwasababu sio mkopo ambao unazalisha.
o Mkopo wa jamii wenyewe mwanachama anaweza kuomba siku hiyo hiyo kwenye
kikundi na ukatoka siku hiyo hiyo.anachotakiwa mwanachama akiwa na tatizo ni kuwahi
kwenye kikundi kujaza fomu mapema na mkopo wake utasomwa kwenye kikundi na
kukopesshwa,mkopo huu hautegemei idhinisho la makao makuu.

MAMBO YA KUZINGATIA WAKATI WA KUCHUKUWA MKOPO WA HISA

Mwanachama wa kikundi anapaswa kuzingatia mambo yafuatayo anapotaka kuomba mkopo au


anapokuwa amepata mkopo kwenye kikundi
1) JUA KIASI HALISI CHA MKOPO AMBAO UNAUHITAJI

Kabla hujaomba mkopo lazima uwe umeshafanya mahesabu yako vizuri na ukajua kabisa kiasi
halisi ambacho unahitaji,usiombe mkopo ukiwa hujui kiasi halisi cha mkopo ambao
unahitaji.kwa mfano mtu anakuwa anahitaji laki tano lakini kwasababu anahisa nyingi anaomba
mkopo mkubwa hivyo mwanachama anapaswa kujua kiasi halisi cha mkopo ambacho
anahitaji.Na uhitaji uendane na kitu anachokwenda kufanya.Pamoja na hayo mwanachama
anatakiwa kuangalia hisa zake kwanza zinamruhusu kukopa kiwango hiko ambacho yeye
anakitaka?
2) JUWA NAMNA UTAKAVYO UREJESHA MKOPO WAKO

Kabla hujachukuwa mkopo kaa chini ujue kabisa namna ambavyo utarejesha mkopo wako na
kama umekopa kwaajilii ya kuanzisha biashara lazima ujiulize kuwa kwa mfano hii biashara
ikifa nitatoa wapi marejesho ya mkopo,mwachama ajiridhishe atakavyorejesha kabla ya kukopa
kuepusha usumbufu kwenye marejesho
3) KUPELEKA MKOPO SEHEMU AMBAPO UMEOMBEA MKOPO WAKO

Wapo watu huwa wanadanganya sana kwenye vikundi mtu anakwambia nataka mkopo kwaajili
ya biashara lakini sio kweli kwamba anapeleka kwenye biashara wengine huwa wanapeleka
kwenye mambo yao.Ukiomba mkopokwaajili ya biashara peleka kwenye biashara ili usisumbuke
4) FAHAMU KAMA UNATAKA MKOPO WA KUANZISHA BIASHARA AU WA
KUENDELEZA BIASHARA

Kama unataka kuchukuwa mkopo kwaajili ya kuanzisha biashara ni bora kukopa mkopo kidogo
ili usipate shida kurejesha.
5) CHUNGUZA KAMA NI WAKATI SAHIHI WA WEWE KUCHUKUWA MKOPO

Katika vikundi vya vicoba wapo watu huwa wanachukua mikopo kwasababu wamewaona watu
wengine wanachukuwa mikopo,sasa kila mwanachama anapaswa kufahamu kuwa lazima ajue
kama ni wakati sahihi yeye kukopa kama muda bado bora usikope tu.
6) KUWA NA NIDHAMU YA FEDHA

Hakika hili ni jambo la kuzingatia sana unapokuwa umechukuwa mkopo kwenye kikundi cha
vicoba endelevu kama unamatumizi mabaya ya fedha nakushauri kwanza jifunze kuyapunguza
kisha ndio uanze kufikiria kukopa,kwasababu kama huna nidhamu ya fedha halfu ukachukuwa
mkopo lazima utautumia ndivyo sivyo na mwisho wa siku ni majuto ndio yatafatia.Nidhamu ya
fedha nikutumia pesa inapopaswa kutumia hata kama unauwezo wa kutumia ambapo hakupaswi
kutumika,kwa mfano unaweza kabisa kunywea pombe pesa ya mkopo lakini kwasababu
unanidhamu ya pesa unajizuia,kwahiyo lazima uwe na nidhamu ya hali ya juu sana kabla ya
kuchukuwa mkopo kwasababu pesa inavishawishi sana.

MAMBO YA KUZINGATIA KWA KIKUNDI KABLA YA KUTOA MKOPO KWA


MWANACHAMA

Kikundi huzingatia mambo yafuatayo kabla yakumpatia mkopo mwanachama.Kutokukamilika


kwa vitu hivi kunawea kusababisha mwanachama asipate mkopo kwenye kikundi
A. FOMU YA KIKUNDI IJAZWE KWA UFASAHA MKUBWA SANA

Mwanachama anapaswa kuhakikisha fomu yake ya mkopo imejazwa kwa ufasaha kabla ya
kuwasilishwa kwenye kikao cha kikundi kwaajili ya kusoma fomu yake,endapo fomu ya mkopo
itakuwa na kipengele ambacho hakijajazwa ipasavyo basi mwanachama hatapatiwa mkopo
mpaka kipengele husika kiwe kimejazwa vzr.
B. KUJIRIDHISHA KWA BIASHARA HUSIKA AMBAYO INAPELEKEWA HUO MKOPO

Mwanachama akiomba mkopo wa kufanya jambo Fulani kikundi kitafanya uchunguzi wa kina
kujirisha juu ya biashara ambayo mwanachama anaombea mkopo na kiwango cha mkopo
ambacho mwanachama anaomba,kama sio biashara basi kitu chochote ambacho mwanachama
anaombea mkopo haswa kwenye mikopo ya hisa lazima kikundi kujiridhisha juu ya pesa na
mahali pesa zinapopelekwa.ikiwa biashara inayofanywa ni kidogo kulingana na mkopo ambao
anoomba mkopo utapunguzwa.kwa mfano mwanachama anaomba mkopo wa milioni moja lakini
biashara inahitaji laki sab abasi mkopo utakaopitishwa ni laki saba tu.
C. KUWA NA WADHAMINI WA MKOPO

Kila mwanachama anapotaka mkopo atapaswa kuhakikisha wadhamini wa mkopo wake wamejaza fomu
vizuri.kwenye kila mkopo kutakuwa na wadhamini wanne wa ndani ya kikundi na mdhamini mmoja wan
je ya kikundi.

D. MTU MWENYE MAHUDHURIO MAZURI

Kikundi kitazingatia sana mwanachama mwenye mahudhurio mazuri kwenye


kikundi,mwanachama ambaye anakuwa naudhuru nyingi kuhudhuria kwenye kikundi hatapewa
kipaumbele katika mikopo.
III. KUWEKA URAHISI WA UTOAJI MAFUNZO,YA KUJITAMBUA,UJASIRIAMALI NA FEDHA
KWA WANANCHI
Vicoba vya YEMCO sio tu kuweka hisa na kukopa bali kunakuwa na mafunzo kila
wiki,mafunzo haya yapo ambayo yanatolewa kwenye kikundi na yapo ambayo yanatolewa
kupitia mtandao wa watsap.Mafunzo yatakayotolewa ni kujitambua,ujasiriamali nafedha
IV. KUWAJENGEA UWEZO WANANCHI KUWA NA MIRADI YA PAMOJA
Kikundi kitakuwa sehemu ya miradi ya kuingiza kipato,kikundi kikikuwa kinakuwa na miradi ya
kukiingizia kipato miradi hii inatolewa muongozo kutoka makao makuu na namna ya
kuitekeleza.Miradi huongeza chachu ya faida kwa wanachama wanapogawana mwisho wa
mwaka.
V. KUWAWEKA PAMOJA WANANCHI WENYE MAONO SAWA ILI KUSAIDIANA
Kikundi kinakuwa sehemu ya kusaidiana kwenye shida na raha.Kama mwanachama
akifiwa,akiumwa au akiwa na sherehe basi kikundi tunakusaidia kukamilisha changamoto
yako.hii inakusaidia hata kama unakutana na changamoto kwenye Maisha yako unakuwa hauna
wasiwasi kwasababu unakuwa na familia ambayo inakusaidia muda wowote.

WALENGWA WA MFUMO WA VICOBA

WALENGWA WA MFUMO WA YEMCO VICOBA


Walengwa ni watu ambao tunaruhusu wajiunge na YEMCO VICOBA.Hapa nasema hivi mfumo
wa vicoba sio mfumo wa Kila mtu,Bali ni mfumo wa watu Maalum AMBAO wamelengwa
kunufaika na mfumo wa VICOBA na hapa nitawataja walengwa.
1.WATU AMBAO WANATAKA KUINUKA KIUCHUMI KWA KUJIWEKEA AKIBA
LAKINI WAO WENYEWE HAWAWEZI.
Kuna watu ambao WANATAMANI sana Kufanikiwa kiuchumi Kwa Kujenga tabia ya
Kujiwekea akiba lakini kusema ukweli wakisema WAWEKE wao WENYEwe akiba inakuwa
ngumu sana.wengine wanajikuta wanaitumia na wengine wanajikuta wanaweka Kwa muda
mchache tu Kisha wanashindwa kuendelea.kwahiyo watu wa aina hii ni walengwa wa MFUMO
WA VICOBA.
2.WATU AMBAO NI WAJASIRIAMALI AU WAFANYABIASHARA AMBAO WANATAKA
KUBORESHA BIASHARA ZAO

Wapo wafanyabiashara na wajasiriamali ambao Kiukweli wamechonshwa na maisha ya biashara zao


kuwa ndogo nakuwa na biashara za kawaida,Sasa wameamua kuzikuza hizo biashara zao,lakini
changamoto ambayo wanayokutana nayo ni elimu ya kukuza biashara zao.Watu kama Hawa ni walengwa
wa MFUMO WA VICOBA BILA kujali jinsia,Wala dini.Kwasababu mfumo wa vicoba umeanzishwa
kwaajili yao.

3.WATU WANAOTAFUTA FURSA ZA KUWEZESHWA KIUCHUMI BILA MASHARTI MENGI

Moja ya walengwa wa MFUMO WA vicoba NI watu ambao wanatafuta mafanikio Kwa kupitia
uwezeshwaji wa mikopo isiyokuwa na riba na isiyokuwa na masharti mengi.Hawa ni walengwa wa
MFUMO WA VICOBA kupitia taasisi yetu ya YEMCO.Tukubali tusikubali mikopo ni njia pekee
ambayo inaweza kutusaidia katika kuinuka KIUCHUMI lakini BAADHI ya makampuni yanaturudisha
nyuma sana wajasiriamali lakini VICOBA NDIO MKOMBOZI wetu kwasasa..
4.WAFANYABIASHARA AMBAO WANATAFUTA MASOKO

Wafanyabiashara au wajasiriamali ambao wanatafuta MASOKO ya biashara zao ni Moja ya walengwa


wa MFUMO WA VICOBA kutoka YEMCO.YEMCO VICOBA ni sehemu pekee ambayo
unakutanishwa WA wateja wa bidhaa zako na kupata SOKO la pamoja kwahiyo hata kama ulikuwa na
changamoto ya MASOKO basi inakuwa ni rahisi sana kuuza kupitia VICOBA.hivyo watu wote ambao
wanabiashara na wanatafuta MASOKO ni walengwa wa MFUMO WA VICOBA.

5.WATU AMBAO WANATAFUTA KUWEKA PESA YAO MAHALI AMBAPO ITAZAA FAIDA

Watu ambao wanatafuta mahali Ambapo wakiweka akiba zao watapata faida ni walengwa wa MFUMO
WA vicoba.Kuna watu WANATAMANI kuweka fedha zao mahali Ambapo mwisho wa mwaka watapata
faida basi hao ni walengwa wa vicoba

VIKUNDI VYA VICOBA


Katika mfumo wa Vicoba kuna aina mbili za vikundi vya Vicoba ambayo ni yafuatayo
1.VICOBA VUNJA VUNJA
Hivi ni aina ya vikundi vya vicoba ambavyo kila inapofika mwisho wa mwaka wanagawana hisa
na jamii halafu wanaanza upya tena.Kwahiyo kama mwanachama amenunua hisa za laki tano
inapofika mwisho wa mwaka humrudishia hisa zake na jamii zake zote anaanza kununua tena
hisa mwanzo,katika vikundi hivi vya vicoba vunja vunja navyo viko tofauti,viko vikundi
ambavyo wao hugawana pesa yote,na pia viko vikundi ambavyo wanagawana lakini wanaacha
fedha kidogo kwaajili ya kuanzia na fedha hizi huwa hazina mpangilio maalum kila kikundi
hupanga fedha kiasi gani kibaki kwenye akaunti yao wao wenyewe.
Kiuhalisia mfumo huu ulituma tangu enzi za zamani sana ambapo mfumo wa vicoba unaanza
kutumika na wengi ambao walikuwa wanatumia mfumo huu walikuwa wanaweka pesa zao
kwenye masanduku kwahiyo walikuwa wanaogopa kuweka fedha kwa muda mrefu kuhofia pesa
zao kupotea kwasababu pesa zote zilikuwa zinawekwa kwa mtu mmoja ambae alikuwa mtunza
sanduku,japokuwa funguo za sanduku zilikuwa zinachukuliwa na wanachama tofauti lakini bado
usalama wa fedha za wanachama ulikuwa mdogo sana.Katika vikundi ambavyo vinatumia
mfumo huu miaka yote huwa wanaendesha vikundi vyao kwa kwenda mbele na kurudi nyuma
tena,huwa natoa mfano mzuri ni kama wanapiga hatua kumi mbele wanarudi tena kuhesabu moja
wanapiga tena hatua kumi mbele kisha wanarudi tena kuhesabu hatua moja tena,mwisho wa siku
maisha yanakuwa hivyo hivyo

HASARA ZA MFUMO HUU


1. Kutokukuwa kwa mikopo kwasababu wanakuwa wanavunja
2. Kukufikia malengo makubwa kwasababu kwa mwaka kila mtu anatakiwa awe
amerudishiwa fedha zake kwahiyo hawawezi kufanya maendeleo makubwa,hizo akiba
zenyewe zinakuwa chache sana.
3. Kushindwa kumkopesha mwanachama mwisho wa mwaka wa kikundi,ni ngumu sana
kumkopesha mwanachama mwisho wa mwaka kwasababu kikundi kinatakiwa
kuvunjwa.Hivyo hata kama mwanachama anataka kufanya jambo la maendeleo
anashindwa.
4. Kushindwa kufanya miradi endelevu. Kwasababu fedha za kikundi zinarudishwa kila
mwaka hivyo ni ngumu sana kwa wanakikundi kufanya miradi endelevu.
2.VICOBA ENDELEVU
Hivi ni vikundi vya vicoba ambavyo kila inapofika mwisho wa mwaka wanagawana jamii na
faida halafu hisa zinabaki na kuendelea kwenye kila mwaka. Vikundi ambavyo vinatumia
mfumo huu huwa faida na jamii ndio ambayo wanachama wao wanakuwa wanagawana kila
mwaka lakini hisa zote zinabakia kuendelea kwa mwaka mwingine.Mfumo wa Vicoba endelevu
Tanzania ulianzishwa na Muheshimiwa Devotha Likokola Rais wa vicoba endelevu
Tanzania.Hizi hisa zinaendelea mpaka wewe mwenyewe ufike mahali uwe umetimiza malengo
yako ndio unaweza kuzichukuwa na ukajitoa kwenye kikundi.Sisi kama taasisi ya YEMCO
VICOBA TANZANIA Tunatumia mfumo wa vicoba endelevu katika vikundi vyetu.

MFUMO WA UONGOZI WA KIKUNDI CHA VICOBA

Katika VICOBA ENDELEVU kikundi kinakuwa na viongozi,viongozi hawa wanachaguliwa na


kikundi au na taasisi makao makuu inategemeana na aina ya kikundi,kwahiyo kama utajiunga
kwenye kikundi ambacho kipo tayari basi unaweza kuwakuta viongozi hawa na
kama,mkianzisha kikundi huko mlipo basi mtawachagua viongozi hawa kusimamia
kikundi.Viongozi hawa wanaweza kuwa na viongozi wengine wa kuwasaidia ambao
watachaguliwa kwenye kikundi
I. MWENYEKITI
II. KATIBU
III. MTUNZA HAZINA
IV. MUHESABU FEDHA
V. MTUNZA NIDHAMU
VI. MTUNZA BEGI/VIFAA

1. WAJIUBU WA MWENYEKITI WA KIKUNDI


Mwenyekiti wa kikundi anawajibu ufuatao
• Kuwa na mtazamo mpana wa kuendeleza kikundi.
• Kufungua mkutano,kuendesha na kusimamia mkutano wa kikundi
• Kutoa taarifa ya maendeleo ya utendaji na taarifa ya fedha za kikundi.
• Kufunga mkutano baada ya majadiliano.
• Kutoa taarifa ya mwanakikundi ya furaha au matatizo.
• Kusimamia utatuzi wa migogoro ya kikundi.
• Kuitisha mikutano yote ya kikundi.
• Kusimamia taratibu zote za kikundi na wajibu wa kila kiongozi
• Kuwa mtia sahihi kwenye akaunti ya kikundi
SIFA ZA MWENYEKITI
ü Awe mwenye uwezo wa kuendesha mikutano
ü Mwenye tabia njema katika jamii
ü Mwenye kukubalika na kusikilizwa katika jamii
ü Muaminifu,mwenye heshina,hekima na busara
ü Mwenye uwezo wa kutatua migogoro katika kikundi
ü Awe mvumilivu,mwenyekupatikana kwenye vikao vya kikundi na mwenye uwezo wa
kusimama na kuzungumza mbele za watu
ü Awe muwajibikaji na mfano wa kuigwa
ü Awe mwenye moyo wa kujitolea kuleta mandeleo ya watu

NB.Kikundi kinaweza kuwa na mwenyekiti msaidizi na yeye anakuwa na sifa kama hizo
hizo.huyu yeye anakuwa anamsaidia mwenyekiti pia anapokuwa hayupo.

2 WAJIBUWAKATIBU
Katibu wa kikundi anawajibu ufuatao
• Kusimamia utekelezaji wote wa kikundi,kwa lugha nyepesi katibu ndio mtendaji mkuu
wa kikundi hatakiwi kukosa kwenye kikundi maana yeye ndio anaweka kumbukumbu za
kila kinachojadiliwa kwenye kikundi.
• Kutunza kumbukumbu zote za kikundi na kuandika mihutasari ya kikundi.
• Kumsaidia mwenyekiti kuongoza vikao vya kikundi.
• Kumsaidia mweka hazina katika shughuli za fedha .
• Kuwaita wanachama kwa namba wakati wa kuita mahudhurio
Na kuweka hisa na mfuko wa jamii.
• Kutoa na kupokea taarifa mbalimbali za mwakikundi kwa mwenyekiti

SIFA ZA KATIBU

ü Ajue kusoma,kuandika na kuhesabu kwa ufasaha


ü Awe mwenye uwezo wa kutoa taarifa sahihi kuhusiana na mwenendo wa kikundi
ü Awe na mahudhurio mazuri kwenye kikundi
ü Asiwe na upendeleo na mwenye kuheshimu wenzake

3. WAJIBU WA MTUNZA HAZINA


• Msimamizi wa fedha zote za kikundi kuhakikisha zinakuwa salama
• Kufuatalia kiingilio ada na michango ya kikundi kwa wanakikundi lazima ahakikishe
wanachama wote wamelipa ada kila mwezi
• Kufuatalia hisa na mfuko wajamii.
• Kuchambua na kuangalia uhalali wa mkopo.
• Kufuatilia marejesho ya mkopo ya wanakikundi.
• Kubuni miradi ya pamoja ya kikundi.
• Kubuni mbinu bora za kuwekeza.
• Kuandika katika leja hisa na jamii zote na kumbukumbu zote za kikundi
• Kupeleka fedha za kikundi benki
SIFA ZA MTUNZA HAZINA
ü Mwenye mahudhurio mazuri kwenye kikundi
ü Mwenye kujua kusoma,kuandika na kuhesabu kwa ufasaha
ü Awe mwaminifu
ü Inashauriwa awe mwanamke
ü Awe tayari kujitolea kwaajili ya wanakikundi

4. WAJIBU WAMHESABU FEDHA


• Kupokea fedha na kurudisha chenji na kupanga fedha kwenye vibakuli.
• Kupokea malipo au risiti na kushughulikia bima za mkopo
• Kuandika kumbukumbu za fedha za wanachama kwenye vitabu vyao
SIFA ZAKE

ü Mwenye mahudhurio mazuri kwenye kikundi


ü Mwenye kujua kusoma,kuandika na kuhesabu kwa ufasaha
ü Awe mwaminifu
ü Awe tayari kujitolea kwaajili ya wananchi

6. WAJIBU WA MTUNZA BEGI


• Kutunza begi la kikundi.
• Kufuatilia usajili wakikundi na kutunza vyeti vya usajili
• Kutunza mali za kikundi.
• Kusimamia ofisi ya kikundi.
SIFA ZAKE

ü Mwenye mahudhurio mazuri kwenye kikundi


ü Awe mwaminifu
ü Awe tayari kujitolea kwaajili ya wananchi

7. WAJIBU WAMTUNZA NIDHAMU


• Ni msimamizi mkuu wa kikundi juu ya utii nidhamu na maadili.
• Kusimamia Usalamawa wanakikundi na mali zao, ana wajibu wa kuhakikisha
kikundi kinastawi vizuri, atatoa adhabu kwa mwanakikundi yeyote
atakayefanya makosa
SIFA ZAKE
ü Mwenye mahudhurio mazuri kwenye kikundi
ü Awe mwaminifu
ü Awe tayari kujitolea kwaajili ya wananchi
UTUNZAJI WA KUMBUKUMBU ZA FEDHA ZA KIKUNDI

Kumbukumbu za kikundi cha vicoba hutunzwa kwenye vitabu vifuatavyo,j

I. PASS BOOK ,hiki ni kitabu cha mwanachama cha kuwekea kumbukumbu zake zote za
ada,kiingilio,hisa,jamii na mikopo,kitabu hiki mwanacha hupatiwa anapojiunga anaweza
kuwa anaenda nacho kwake lakini ili kuepusha kupoteza huwa vitabu vyote hubakia
kwenye begi
II. REJA YA KIKUNDI,hiki ni kitabu kikuu cha kutunzia kumbukumbu za kikundi za
fedha za kikundi kizima na hujazwa na muweka hazina wa kikundi
III. KATIBA
IV. RIPOTI YA MWAKA,kitabu hiki ni kwaajili ya kuandika riporti ya mwaka
V. FOMU YA KUJIUNGA NA KIKUNDI CHA VICOBA,hii ni fomu ambayo inakuwa
na taarifa za mwanakikundi za kutosha na mwanakikundi lazima ajaze yeye mwenyewe
halafu arudishe kwenye kikundi
VI. FOMU YA MAOMBI YA MKOPO WA MWANAKIKUNDI CHA VICOBA
VII. TAARIFA ZA KIKUNDI CHA VICOBA,kitabu hiki hujazwa taarifa za kila siku za
kikundi
VIII. FOMU YA MAREJESHO YA MKOPO
IX. KITABU CHA WAGENI,kama kikundi kinapata mgeni basi atasaini humu
X. REGISTA YA MAHUDHURIO,hiki kitabu kwaajili ya kuandika mahudhurio ya
wanachama ya kila siku
N:B,Pesa zote za kikundi ni lazima ziwekwe benki,hii ni kwa usalama wa kikundi husika
kuepusha upotevu wa pesa lakini wizi wa pesa,lakini pia ni msada wa kikundi kuweza
kukopesheka benki kwa kuangalia miamala yao,maswala ya upotevu wa pesa yamekuwa
makubwa sana kwa vikundi ambavyo vinaweka pesa zao majumbani.Kama hamtaweka benki
basi fedha ziwekwe kwenye m-koba usikubali kujiunga kwenye kikundi ambacho wanaweka
pesa nyumbani kwa mtu.

MICHANGO YA MWANACHAMA KATIKA KIKUNDI


Vikundi vya taasisi ya YEMCO VICOBA vyote ukijiunga kuna michango ambayo utakuwa
unalipia kwa mwezi
1. ADA YA KIKUNDI,
Kila mwachama lazima alipie ada ya kikundi Tsh 5000/= kila mwezi,kazi za ada ni
kwaajili ya vitabu vya kikundi ambavyo vinaisha kwa mwaka mmoja,maendeleo ya
taasisi,mafunzo ambayo yanatolewa kutoka kwenye taasisi kwa wanachama,chakula kwa
wanachama wanaohudhuria mafunzo kila mwisho wa mwezi na bima ya Maisha ambayo
mwanachama analipiwa ambapo mwanachama akifariki basi atapewa fidia ya pole ya
msiba ya Tsh milioni moja.
2. MCHANGO WA DHARULA.
Kila mwanachama atatakiwa kuchangia Tsh 2000/= ya dharula,hii ni fedha ambayo
mwanachama anachangia kwenye kikundi ili akifiwa,akioa,au akiuguwa anachangiwa na
kikundi.

3. MCHANGO WA KONGAMANO:
Kila mwaka taasisi hufanya kongamano kubwa la kitaifa na kila mwanachama lazima
kuchangia Tsh 10000/= kwaajili ya kongamano,mchango huu huwa haujalishi kama
mwanachama atashiriki au hatashiriki kwenye kongamano hilo lakini kuchangia ni
lazima.Mwanachama anaweza kupoteza sifa za kuwa mwanachama kama akigoma
kuchangia michango hiyo.

JINSI YA KUGAWANA FAIDA MWISHO MWAKA

Kama tulivyojifunza hapo juu kuwa vikundi vya vicoba endelevu huwa hisa zinaendelea lakini
jamii na faida wanarudishiwa wanachama kwaajili ya kufanya mambo yao,hivyo hapa
tutajifunza kwa pamoja namna ambavyo tutaweza kugawana faida mwisho wa mwaka,katika
safu hii utaweza kujifunza jinsi ya kugawana faida ili uweze kujua ukiwa kwenye kikundi jinsi
ya kukagawana faida.
UNAPOTAKA KUGAWANA FAIDA MWISHO WA MWAKA FATA HATUA ZIFUATAZO

1. Unachukuwa hisa zoote za wanachama halafu unagawanya kwa shilingi 2000 hii ni
thamani ya hisa moja,baada ya kugawanya hapa utapata idadi ya hisa zote kwenye
kikundi.

2. Unajumlisha jumla ya faida zote (faini,ziada za mikopo,faida za miradi kama mtakuwa na


mradi,zawadi kama kuna siku mlipewa zawadi) kisha unagawanya kwa idadi ya hisa
unapata faida ya hisa moja.Utakayopata hapa ndio faida kamili kwa hisa moja. Nb:Faini
za kikundi huchajiwa kwa mwanachama kuvunja sheria za kikundi,ambapo kila kikundi
hukubaliana kiwango cha faini kulingana na makosa husika.

3. Ukishapata thamani ya hisa moja sasa unakuja kwenye hii hatua ya mwisho ambayo sasa
unaanza kuchukuwa kitabu cha kila mwanachama,unaangalia idadi ya hisa za kila
mwanachama unazidisha na thamani ya hisa moja ambayo uliiipata.Hapa unapata faida
ambayo kila mwanachama anatakiwa kuipata.
MFANO WA KUGAWANA FAIDA ZA KIKUNDI CHA YEMCO VICOBA GROUP

Yemco Vicoba group ni kikundi cha watu 30 wanajumla ya hisa za shilingi million 15 kwa
mwaka.kwahiyo hatua ya kwanza utachukuwa million 15 utagawanya kwa sh 2000 ambapo
utapata idadi ya hisa zitakuwa 7500.Kwa maana kuwa sasa kwa mwaka mzima yemco vicoba
group wameweka hisa 7500.
Hatua ya pili unajumlisha jumla ya faida zote walizopata yemco vicoba group ili ugawanye kwa
idadi ya hisa,sasa kwa mfano kwa mwaka mzima yemco vicoba group wamepata faida ya Tsh
750000/= kwaiyo unachukuwa 750000/= unagawanya na idadi ya hisa ambazo ni 7500 unapata
thamani ya hisa ambayo ni Tsh 100/=,hivyo basi faida ya hisa moja ya yemco vicoba group ni
Tsh 100/=
Hatua ya tatu sasa unaanza kuchukuwa kitabu cha kila mtu mmoja unaangalia idadi ya hisa za
kila mwanachama,sasa kwasababu vitabu vitakuwa vimejazwa pesa taslim unachukuwa ile pesa
taslim unagawanya kwa 2000 unapata idadi ya hisa ya kila mwanachama halafu unazidisha na
faida ambayo ni 100 unapata faida ambayo anatakiwa kupata mwanachama.Mfano Juma pesa
zake zote za hisa ni Tsh 2000000 unachukuwa hiyo pesa unagawanya kwa tsh 2000 unapata
idadi ya hisa 1000 kwaiyo Juma anaidadi ya hisa ya 1000 ukizidisha na faida ya tsh 100 unapata
faida ya juma ambayo ni Tsh 100000/= kwaiyo Juma atapata faida ya Tsh 100000/= kama faida
ya mwaka.
HITIMISHO
Napenda nikupongeze kwa kuweza kujipatia maarifa
haya,ambayo kama utayasoma kwa umakini kabisa kuna
uwezekano mkubwa ukawa umeelewa vizuri kuhusu mfumo
wa vicoba na sasa unaweza kuwa mwalimu mzuri kwa
wengine kuhusu mfumo huu,katika kuhitimisha kitabu hiki
nakusihi ukayafanyie kazi yote ambayo umejifunza katika
kitabu hiki yakawe sehemu ya maisha yako,yakabadilishe
maisha yako lakini pia yakabadilishe maisha ya watu
wengine ambao wanakuzunguuka.

VITABU VINGINE VILIVYOANDIKWA NA MOHAMED


BASSANGA

1. Ramani ya Maisha
2. Kanuni 26 za mafanikio
3. Maisha na vyakula jinsi vinavyotuuwa taratibu
4. Umasikini wa waislamu na suluhu zake
5. Siri zilizojificha katika biashara ya mtandao
6. Ujue mfumo wa vicoba vya kiislamu

Vitabu hivi vyote unaweza kuvipata kwa njia ya softy copy kwa kuwasiliana na
mimi kwa simu namba 0715448643
Kuhusu Mwandishi

“Mohamed Bassanga” ni mtaalamu wa maswala ya fedha, ujasiriamali na uchumi, ni mkurugenzi na

Mwanzilishi wa taasisi ya YEMCO, ni mkurugenzi wa YEMCO MICROFINANCE LIMITED, ni mkurugenzi wa


YEMCO PRODUCTION na ni Raisi wa VICOBA ENDELEVU TANZANIA.

Amekuwa akiwasaidia watu wengi kutimiza ndoto zao na malengo yao kwa kutumia mfumo wa
YEMCO VICOBA ENDELEVU.

VICOBA ENDELEVU ni msingi utakaokupeleka katika mafanikio makubwa bila kuwa na msongo
wa mawazo.

You might also like