Professional Documents
Culture Documents
01 Kiswahili - Maelekezo Kwa Msimamizi
01 Kiswahili - Maelekezo Kwa Msimamizi
01 KISWAHILI
(i) Hakikisha unasoma hadithi kwa sauti na taratibu kwa mara ya kwanza huku
ukizingatia alama zote za uandishi zilizopo katika hadithi hiyo. Unaposoma kwa
mara ya pili ongeza kidogo kasi ya usomaji.
(ii) Muda utakaotumia kuwasomea watahiniwa hadithi ni dakika tano (05) na muda
utakaotumika kwa watahiniwa kujibu maswali ni dakika tano (05). Sehemu hii
itafanyika kwa dakika kumi (10).
2. Nikisoma hadithi kwa mara ya kwanza, sikiliza bila kujibu maswali na nikimaliza
kusoma kwa mara ya pili, jibu swali la 1 hadi 5 kisha endelea kujibu maswali
mengine (6 hadi 45).
HADITHI
Hapo zamani za kale palikuwa na kijiji kiitwacho Faru. Faru ni kijiji kilichokuwa
karibu na msitu mkubwa wenye wanyama wakali. Wanakijiji wa Faru waliishi maisha
ya raha sana. Kiongozi wao aliitwa Adabu, alikuwa kiongozi shupavu na mzalendo.
Ukurasa wa 1 kati ya 2
SIRI
SIRI
Wanakijiji walimpenda kwa sababu alikuwa anajitoa kwa ajili ya kijiji chake,
alipenda haki na alipigania maendeleo ya kijiji chake.
Siku moja Adabu akiwa nyumbani kwake alisikia kelele nje ya nyumba yake.
Alipotoka nje aliona kundi kubwa la wanakijiji wameshikilia silaha mbalimbali kama
vile rungu, sime na magongo, hakujua ni ya kazi gani? Akauliza kwa shauku “kuna
nini?” Mzee Funzi akajibu kwa hofu “tumevamiwa! tumevamiwa! na simba.
“Simba?” Adabu aliuliza huku akikimbia kurudi ndani, akatoka na mshale. Punde si
punde ilisikika ngurumo nyuma ya nyumba yake.
Ukurasa wa 2 kati ya 2
SIRI