Professional Documents
Culture Documents
Barua Pepe
Barua Pepe
com
Kutoka kwa: brighton.onyango@koderobara.ac.ke
Kuhusu: Jinsi Matukio Katika Matini Yameathiri Utambulishi Wangu.
Hujambo bwana,
Natumai ujumbe huu wangu utakufikia salama.Ningependa kukuarifu kuwa nilikipenda
kitabu kile cha hadithi fupi ya damu nyeusi uliyeandika.Sifa tele tele zikufikie huko
uliko.Mola aendelee kukupa ujuzi wa kuandika vitabu vinginevyo ili kutuelimisha jinsi
ulimwengu wa kisasa ulivyokumbwa na ubaguzi.Sisi Waafrika tu hapa kukupa moyo ili
uendelee kutuwakilisha katika mashindano hayo mengi ya waandishi bora.
Matukio katika matini hayo yameathiri utambulisho wangu kwani yamenifundisha mambo
mengi.Hapo awali, sikuwa na fununu ya kwamba sisi kama Waafrika tunaweza kufanyiwa
unyama kama ule.Hakika ,hapo mwanzo nilikuwa na hamu ya kuenda nchi za ng’ambo lakini
kutokana na matukio yale ambayo Fikirini alitendewa nimeweza kubadili mienendo
yangu..Kwani sisi Waafrika tunachukuliwa kama binadamu hafifu ambao hawafai kuwa
ulimwenguni.Licha ya sisi kuwa weusi,haimanishi kuwa hatufai ,ni Mola aliyetuumba kwa
upendo wake na ni kwa nehema na rehema zake akaona ilikuwa vyema kuwaumba watu
weusi.Kwani hawa wazungu wanafikiria wao ni nani?
Bwana Ken,ningependa kukupa sifa kedekede kwa kuwa umenijuvya kwa mambo ambao
mimi sikuyajua.Ningependa uandike vitabu vingine vingi ili niweze kupata maarifa mengi
kuhusu tabia za wazungu na jinsi wanavyo wanyanyasa Waafrika.Jalali akujalie na akulinde
pia.
Wako mwaminifu,
Brighton.
Usipigwe na butwaa kwa yale ambayo Fikirini alitendewa kwani alienda nchi za ng’ambo
kufanya nini ilhali yeye ni Mwafrika? Mtu akiwa kiherehere mwache ajionee kwa kuwa
mwenye macho haambiwi tazama.Anaenda Marekani kufanya nini? Nina uhakika ya
kwamba hapo kwenu kuna mtu ambaye anataka kuenda nchi za ng’ambo.Mwambie kuenda
nchi za ng’ambo si mbaya ila wajihadhari kabla ya hadhari.
Ikiwa siku moja utaenda huko, tafadhali kuwa na heshima na usisahau kwenu kwa kuwa
hakuna pahali pazuri kama kwenu.Watu wanaoenda nga’mbo aghalabu huwa na matatizo
mengi.Usishangae kuwaona wakiwa nusu uchi.Wengine huenda kwa kiwango cha
kuwatukana wazazi.Juzi nilimwona mmoja akikataa katakata kula ugali ati atapata ugonjwa
wa Waafrika.Nilikuwa ninajiuliza ikiwa kuna ugonjwa wa Waafrika na wa Wazungu.Ama
kweli, dunia rangi rangile ina vituko vyake.Mtu kama huyo enzi zile zetu angenyoroshwa
viboko sawasawa.Huo ni utovu wa nidhamu.
Nikimalizia, ningependa uwahimize wenzako wakinunue kitabu hiki ili wao pia waweze
kupata nafasi ya kukisoma kwa kuwa kina mafunzo mengi.Kitabu hicho cha damu nyeusi ni
cha tukio cha kweli ambacho kilitendeka.Natumai ulikipenda kitabu hicho.Tofauti na damu
nyeusi,kuna vitabu vingine kama siku njema ,kufa kuzikana,ndoto ya alhamasi na vinginevyo
ambavyo pia ni wa kuelimisha, tafadhali pata nafasi na uvisome.
Wako mwaminifu,
Ken.