Asili Yako

You might also like

Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 9

Kwa kawaida kila unachokiona huwa kina asili yake au kilipotoka.

Kila
mwanadamu amezaliwa na mwanamke na wanyama huzaliwa na wanyama
weyewe. MWANZO 1:26-28 Imeandikwa, “Mungu akasema, Na tumfanye mtu
kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa
angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho
juu ya nchi. Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu
alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia,
Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha;
mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye
uhai kiendacho juu ya nchi.” Mungu aliwabarikia wakaze na kuongezeka
wakaijaze nchi. Maana yake ukazae na kuongeza, na si kuzaa tu bali uzae na
kuongezeka. Chochote unachokishika kizae na kuongeka. Kuongezeka kimasomo,
mtaji, biashara, familia na ustawi.

MWANZO 3:1-6 Imeandikwa, “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama


wote wa mwitu aliowafanya Bwana Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati!
Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani?
Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula;
lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala
msiyaguse, msije mkafa. Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa,
kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo,
mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.
Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho,
nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake
akala, akampa na mumewe, naye akala.”
Baadhi ya Makutano wakifuatilia neno la Mungu wakati wa Ibada ya Leo.
Nyoka alikuwa mwerevu akawaambia mkila mtafanana kama yeye. Baada ya kula
uwepo wa Mungu ukaondoka. MWANZO 3:12-15 imeandikwa, “Adamu akasema,
Huyo mwanamke uliyenipa awe pamoja nami ndiye aliyenipa matunda ya mti
huo, nikala. Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya?
Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala. Bwana Mungu
akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko
wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo
utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka
uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo
utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” Mungu aliweka uadui kati
ya uzao wa mwanamke na nyoka. Leo tutawaponda kwa jina la Yesu, uzao,
masomo, biashara, afya itakombolewa.

Hapa Mungu ametupa uhalali wa kuwaganyaga uzao wa nyoka kwa jina la Yesu.
Kazi iliyomezwa, ndoa, masomo leo atatapika kwa jina la Yesu. Hata wewe
umezaliwa na mwanamke bila shaka umefungwa kwenye magereza, kwenye
mashamba leo utatoka kwa jina la Yesu.UFUNUO 12:13-17 imeandikwa, “Na joka
yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule
aliyemzaa mtoto mwanamume. Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya
tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo
alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama
mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.”

Platform Ministry wakiongoza kipindi cha Sifa na Kuabudu.


Nyoka alipomuuzi mwanamke akatupwa mpaka nchi, na mwanamke alipokuwa
akijifungua nyoka akafungua kinywa ili ammeze. Lakini mwanamke alipewa
mabawa mawili ili alombowe uzao wake. Nyoka alitoa maji ili mwanamke
akasombwe na mto ule. MATHAYO 18:18 imeandikwa, “Amin, nawaambieni, yo
yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote
mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni.” Leo tutafunga
balaa zote, mikosi yote kwa jina la Yesu.

KUTOKA 2:15-19 imeandikwa, “Basi Farao alipopata habari, akataka kumwua


Musa; lakini Musa akakimbia mbele ya Farao, akakaa katika nchi ya Midiani;
akaketi karibu na kisima. Basi kuhani wa Midiani alikuwa na binti saba, nao
wakaja wakateka maji, wakazijaza birika maji, wapate kunywesha kundi la
baba yao. Wakasema, Mmisri mmoja alituokoa katika mikono ya wachungaji,
tena zaidi ya hayo, akatutekea maji, akalinywesha kundi.”

Farao alijua mtawala atakuwa mwanaume, akaamua kuongea na wazalishaji


mtoto akizaliwa wa kiume auwawe lakini wa kike wamwache aishi. Lakini
wakunga hawa hawakufanya matakwa ya mfalme. Mfalme akatafuta njia nyingine
ya kuwaaangamiza, katikati ya tangazo Musa alizaliwa, Musa akaokotwa na mtoto
wa Farao. Mama yake Musa alipewa kazi ya kumnyonyesha Musa na akawa
analipwa. Katikati ya magumu Mungu anaonekana.

Waamuzi 13:2-5 imeandikwa, “Palikuwa na mtu mmoja wa Sora, wa jamaa ya


Wadani; jina lake akiitwa Manoa; na mkewe alikuwa tasa, hakuzaa watoto.
Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, wewe
sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto
mwanamume. Basi sasa, jihadhari, nakuomba, usinywe divai wala kileo, wala
usile kitu kilicho najisi; kwani tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto
mwanamume; na wembe usipite juu ya kichwa chake; maana mtoto huyo
atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli
na mikono ya Wafilisti.” Kuna uwezekano mtu akabeba mimba kwa uwezo wa
kishetani/kijini/mganga kienyeji. Na mtoto alipozaliwa wakaenda kunyoa na
kumkata kitovu. Unapokuwa wanaweza kufuatilia unachokifanya kwa sababu
wanavitu vyako. Unawezekana unapata matatizo kwa sababu umetokana na uzao
wa mganga wa kienyeji.
Mchungaji Mwandamizi Daktari Hapiness Muhimbula akimfungua mtu.

Yeremia 15:1-3 imeandikwa, “Ndipo Bwana akaniambia, Hata wangesimama


mbele zangu Musa na Samweli, moyo wangu usingewaelekea watu hawa;
watupe, watoke mbele za macho yangu, wakaende zao. Kisha itakuwa, hapo
watakapokuambia, Tutoke, tuende wapi? Utawaambia, Bwana asema hivi,
Walioandikiwa kufa, watakwenda kufa; au kufa kwa upanga, watakufa kwa
upanga; au kufa kwa njaa, watakufa kwa njaa, au kutekwa nyara, watakuwa
mateka. Nami nitaamrisha juu yao namna nne, asema Bwana; upanga uue, na
mbwa wararue, na ndege wa angani, na wanyama wakali wa nchi, wale na
kuangamiza.” Tunaona Samsoni alipozaliwa alikuwa na asili yake. Aliponyolewa
nywele zake asili yake ilipotea.

1 Samweli 1:1-6 imeandikwa, “Palikuwa na mtu mmoja wa Rama, Msufi, wa nchi ya


milima milima ya Efraimu, jina lake akiitwa Elkana, mwana wa Yerohamu, mwana wa
Elihu, mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu naye alikuwa na wake wawili;
jina lake mmoja akiitwa Hana, na jina lake wa pili aliitwa Penina; naye huyo Penina
alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na watoto. Na mtu huyo alikuwa akikwea
kutoka mjini kwake mwaka kwa mwaka, ili kuabudu, na kumtolea Bwana wa majeshi
dhabihu katika Shilo.”

Pamoja na Pennina kumchokoza Hana, Hana hakukata tamaa. Siku moja kuhani
alimkuta Hana midomo yake ikichezacheza akamuuliza kwa nini umelewa asubuhi
hii yote. Hana akamjibu mimi naumimina moyo wangu kwa Bwana. Siku chache
zilizofuata Hana akamzaa shujaa wa Bwana Samweli. Unapochelewa kuzaa usife
moyo Bwana amekuandalia jambo kubwa, endelea kuomba utapokea sawasawa
na haja ya moyo wako. Inawezezkana umepewa taarifa mbaya kutoka kwa
madaktari, hizo ni taarifa za wanadamu lakini leo yupo Yesu atakayerudisha vyote.
Mungu anasema njia zenu sio njia zangu, yeye anatuwazia mema.

1 Samweli 1:10-18 imeandikwa, “Naye huyo mwanamke alikuwa na uchungu rohoni


mwake, akamwomba Bwana akalia sana. Akaweka nadhiri, akasema, Ee Bwana wa
majeshi, ikiwa wewe utaliangalia teso la mjakazi wako, na kunikumbuka, wala
usinisahau mimi mjakazi wako, na kunipa mimi mjakazi wako mtoto mume, ndipo
mimi nitakapompa Bwana huyo mtoto siku zote za maisha yake, wala wembe
hautamfikilia kichwani kamwe. Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini?
Achilia mbali divai yako. Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni
mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina
roho yangu mbele za Bwana. Basi huyo mwanamke akaenda zake, naye akala
chakula, wala uso wake haukukunjamana tena.” Hana alipokuwa anaomba, Kuhani
akamwambia Bwana akupe sawasawa na haja yako. Hii inatufundisha kuwa neno
la Kuhani ni la muhimu wakati wa uhitaji wako. 1 SAMWELI 1:20 Imeandikwa,
“Ikawa, wakati ulipowadia, Hana akachukua mimba na kuzaa mtoto
mwanamume; akamwita jina lake Samweli, akisema, Kwa kuwa nimemwomba
kwa Bwana.” Mungu alimpa mtoto wa kiume na Hana alitimiza nadhiri kwa
kumtoa Bwana.

Vita ya uzao ni vita ya kufa na kupona, ndo maana shetani ameachilia waume na
wake wa kipepo. Unapokuwa umelala unaingiliwa kwenye ndoto. Inawezekana
una watoto baharini au unanyonyesha ndotoni, katika hali ya kawaida huwezi
kupata ujauzito katika ulimwengu wa mwili. Dalili za mtu aliyefunga ndoa za
kipepo Kiuno, mguu wa kushoto unakufa ganzi, ukiota unatoka bichi (out). Shetani
anafanya hivi kwa sababu anataka uzao wake uchanganyike na uzao wa
mwanadamu ili aweze kutenda kazi kwa urahisi.

Ni kwa nini wanaume au wanawake wa kipepo, sababu ni kama zifuatazo,


inawezekana nyota yako inang’aa. Inawezekana nyota yako ya uzao wako. Hivyo
wanakuchukua ili ukazae kule kuzimu. Kuna mwanaume kakupenda kwa sababu
ya nyota yako, anapokuingilia kimwili usiku yeye anafanikiwa katika kazi zake.
Katika ulimwengu wa roho mnaoneka ni mwili mmoja ni kwa sababu ya agano.
Ukiingia katika siku zako unapatwa na maumivu makali, hii hali si ya kawaida
unatakiwa ushughulikie. Leo hii wanatumia kucha, mawigi na kope za bandia.
Kucha na kope zimetolewa kwa maagano ya kuzimu ili wapate malikia wengi
duniani.
Mchungaji Godfrey Mwakyusa akimfungua mtu
MWANZO 11:30 Imeandikwa, “Na Sarai alikuwa tasa, hakuwa na mtoto.”
MWANZO 25:21 Imeandikwa “Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake,
maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua
mimba.” Baba alichelewa kuzaa na mtoto alichelewa pia. Kumbe ukichelewa
unatakiwa uendelee kuliitia jina la Bwana na ukipokea Baraka zako jina lako
linabadilika. LUKA 1:5 Imeandikwa, “Zamani za Herode, mfalme wa Uyahudi,
palikuwa na kuhani mmoja, jina lake Zakaria, wa zamu ya Abiya, na mkewe
alikuwa mmojawapo wa uzao wa Haruni, jina lake Elisabeti.” Alipojifungua
mtoto aliitwa Yohana, jina limebeba Baraka za mtu.

ISAYA 14:29b imeandikwa, “Maana katika shina la nyoka atatoka fira, Na uzao
wake ni joka la moto arukaye.” Zaburi 22:10 imeandikwa, “Kwako nalitupwa
tangu tumboni, Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.” Unakuta
tangu tumboni wengine washaanza kunywa makombe, dua. Unakuta mtu anakula
mkaa, udongo kumbe mama yake alivyokuwa mjamzito alikuwa anakula udongo.
Ukiona mtu anakula udongo ujue tumboni kwake kuna joka. Leo ukatae kula
vyakula vya kipepo kwa jina la Yesu.

ZABURI 58:3 imeandikwa, “Wasio haki wamejitenga tangu kuzaliwa kwao;


Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.” Unakuta mtu anaongea uongo
kumbe ni asili yake tangu tumboni. Kataa kila asili ambayo umeipata kutoka kwa
mama yako ambayo si nzuri kwa jina la Yesu. LUKA 1:13 -15 Imeandikwa, “Lakini
yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na
mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.
Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa
kwake. Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala
kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.”
Namna Yohana alivyopokea Roho mtakatifu tangu tumboni.

LUKA 1:39-43 Imeandikwa, “Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata
nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, akaingia nyumbani
kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia
kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti
akajazwa Roho Mtakatifu; akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa
wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?” Kumbe
mtu anaweza kupokea roho kupitia sauti ya mtu. Mtu anaweza kupata matatizo
au Baraka kupitia salamu. WAEBRANIA 1:7 imeandikwa “Na kwa habari za
malaika asema, Afanyaye malaika wake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa
miali ya moto.” ZABURI 104:4 imeandikwa, “Huwafanya malaika zake kuwa
pepo, Na watumishi wake kuwa moto wa miali.” Unakuta unapata fursa nzuri
lakini zinapotea, umenyang’anywa kinywa.

Mchungaji Kiongozi Daktari Godson Issa Zacharia akimfungua mtu na uzao wake umekuwa
salama kwa jina la Yesu.
ISAYA 6:8 imeaandikwa, “Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume
nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa,
nitume mimi.” Mungu alikusudia kuokoa uzao kwa kumtoa mwanawe wa pekee.
YOHANA 6:16-17 imeandikwa, “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda
ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee,
bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni
ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.” Mungu
aliupenda ulimwengu, kutoa kunaendana na kupenda. Mungu alimtoa mwanawe
ili upate uzima tele. Kazi, ndoa, masomo, biashara yako iwe na uzima tele.
Lazimisha ulimwengu wa roho ukuachilie ili uongezeke. Kila unachokianza maana
yake kizae na kuongezeka.7

You might also like