Professional Documents
Culture Documents
Mbinu Za Kupata Pesa Nyingi Hadi Kuwa Tajiri 01102020 09 48
Mbinu Za Kupata Pesa Nyingi Hadi Kuwa Tajiri 01102020 09 48
SURA YA KWANZA1
VYANZO VYA UMASIKINI TANZANIA .......................................................1
SURA YA PILI
MIRADI 66 INAYOWEZA KUKULETEA PESA NYINGI HADI KUWA
BILIONEA ................................................................................................19
SURA YA TATU
MAMBO 34 AMBAYO NI MWIKO KWA MATAJIRI ..................................88
SURA YA NNE
MBINU ZA KUPATA MTAJI ....................................................................108
SURA YA TANO
MAWAZO POTOFU KUHUSU PESA NA UTAJIRI MKUBWA. ..............121
HITIMISHO ............................................................................................130
REJEA ...................................................................................................134
Hongera kwa kuanza kusoma sura hii. Hapa ndipo sasa nitaanza kukueleza
kiini cha kitabu hiki. Kwa kusoma sura hii yote nina hakika utaamua vyema
kuwa siyo milionea tu bali kuwa bilionea pia. Sura hii inaeleza miradi
ipatayo 66 ambayo ina mawazo chanya na ufafanuzi wa wazi unaoweza
kukufanya upate pesa nyingi sana kwa muda mfupi hadi kufikia kuwa
bilionea. Ukiamua kwa dhati, hakika utakuwa bilionea mkubwa.
Miradi iliyoelezwa katika sura hii imefafanuliwa kwa msisitizo mkubwa wa
kimahesabu ambapo ukiifanya kwa umakini, kwa utafiti, upelelezi na ujasiri
mkubwa, ukafanya kwa bidii bila woga wala uvivu, ni hakika utakuwa bilionea
ndani ya miaka mitatu au chini ya hapo. Ninakupa ahadi (Guarantee) ya
miaka 3 kama utachukua moja ya mradi au wazo lililofafanuliwa ndani ya
kitabu hiki, hakika utakuwa bilionea.
Ifuatayo ni Miradi iliyofafanuliwa kwa kina na kwa mifano ambayo inaweza
kukufanya ukapata utajiri mkubwa ambao utadumu hadi kwa watoto wako
na watoto wa watoto wako mpaka watoto wa watoto wa watoto wa watoto
wako.
1. Mradi wa Miti ya Mbao
Mradi huu ni mradi ambao mtu akiufanya kwa muda wa miaka 5 mfululizo
baada ya miaka kumi ataanza kuvuna pesa. Unaweza kupanda miti ya
Kumbuka kuku wapatao 5000 unaweza kuwafugia hata katika eneo dogo
tu la nusu heka kwa kujenga mabanda matano yanayofuga kuku 1000 kwa
kila banda. Huu ni ufugaji wa kuku wengi na ndio ufugaji wa kibiashara
(large scale chicken farming). Ukiamua inawezekana kabisa. Je, hupendi
Kupata mshahara wa milioni ishirini na saba kwa mwezi? Kama unapenda
unangoja nini sasa kuchukua hatua ndugu yangu?
Aidha, waweza kuamua kufanya biashara ya Kununua na kuuza kuku
wa kienyeji kutoka vijijini kwenda kuuza mijini kwa faida zaidi. Badala ya
wewe Kufuga kuku unachofanya ni kwamba wewe unanunua kwa wafugaji
wa vijijini kisha unaenda kuuza mijini kwa faida zaidi. Kwa mfano kama
ukinunua kuku 40 vijijini kwa bei ya Tshs 7,000 kisha ukawaleta kuku hao 40
kuwauza mjini kwa bei ya Tshs 10,000 maana yake ni kwamba utakusanya
Tshs 400,000 ambapo wewe faida yako itakuwa Tshs 3000 x 40 = 120,000
kwa siku moja. Mtaji wa kufanya biashara hiyo utaona kwamba ukiwa
na Tshs 280,000 unaweza kuanza biashara hii. Hata tukisema tuongeze
gharama ya nauli kwenda vijijini na kurudi ukaongeza gharama ya matenga
ya kubebea kuku; hapa ina maana kwamba utaanza na Mtaji wa Tshs
350,000 tu.
Kama kila tikitimaji utaliuza kwa Tshs 1000 shambani utakuwa na uhakika
wa kupata Tshs 7,200,000 kwa msimu mmoja. Kwa jinsi tikiti zilivyo, kwa
mwaka unaweza kuvuna mara mbili. Hii ni kwa sababu, tikitimaji hukomaa
ndani ya miezi 3. Kama umetumia ushauri wa watalaam wa kilimo, na
kutumia mbolea za kukuzia na kuimarishia mazao utavuna siyo chini ya
mara mbili kwa mwaka na waweza kujipatia zaidi ya Tshs 14,400,000 kwa
mwaka ambayo ni takribani Tshs 1,200,000 kwa mwezi. Mahesabu haya
siyo ndoto za usiku wala za mchana, bali ni maelezo yaliyo ya uhakika,
ukiyafanyia kazi hautabaki maskini maishani mwako.
12. Mradi wa Kulea watoto wadogo (Day care centre)
Kutokana na utandawazi, siku hizi wazazi wote wa kike na kiume
wanakimbizana kutafuta riziki. Hapo kale, mzazi wa kiume tu ndiye
aliyekimbia huku na kule kitafuta riziki ya familia. Siku hizi wote wanakimbia
kutafuta riziki kuanzia asubuhi hadi jioni. Athari hizi za utandawazi na usawa
wa kijinsia zimeleta fursa nyingine kwa wajasiriamali. Wazazi wengi ambao
ni vijana ambao bado wanazaa watoto wanahitaji mtu makini ambaye
anaweza kuwalelea watoto asubuhi hadi jioni wanaporejea nyumbani.
Mbinu za kupata Pesa nyingi hadi kuwa Bilionea, 2014 37
Ukianzisha kituo cha kulelea watoto na ukakitangaza vyema utapata wateja
wa kukutosha hasa kwa wanaoishi mijini hasa miji mikubwa. Kama ukiweza
kujenga kituo cha kutosha kulea watoto wasiopungua 30 kwa siku wenye
umri wa kuanzia miezi 3 hadi miaka 5 unaweza kujipatia kipato kizuri zaidi.
Kama kila mtoto atatunzwa kuanzia saa moja asubuhi hadi saa 12 jioni kwa
gharama ya Tshs 5000 kwa siku, utakuwa na uhakika wa kujipatia zaidi ya
Tshs 150,000 kwa siku sawa na Tshs 4,500,000 kwa mwezi. Kwa Mwaka
utakuwa na uhakika wa kukusanya pesa isiyopungua Tshs 54,000,000.
Wazazi wengi wanaweza kulipa pesa hiyo endapo tu watahakikishiwa
usalama wa watoto wao kuanzia asubuhi wanapoenda kazini hadi jioni
wanaporudi nyumbani. Wengi wanaweza kupenda mfumo huu kuliko wa
kuajiri msichana/mvulana wa kazi kwani siku hizi watu wengi hawawaamini
tena wafanyakazi wao wa majumbani. Mtoto akishafikisha umri wa miaka
5 sasa anaweza kuanza shule ya awali ambapo sasa mzazi atamhamishia
shuleni mtoto wake na akaendelea kusoma sasa akitunzwa na shule.
13. Mradi wa Kuuza Chakula
Mradi wa kuuza chakula kwenye Mgahawa wako waweza kukutoa kwenye
umaskini endapo utaufanya kwa umakini na ushindani. Kwa mfano kama
unafungua mgahawa kwenye miji mikubwa sana hata ile inayochipukia
kama vile Nzega, Tinde, Bariadi, Kakonko, Uvinza, Tunduma, Gairo,
Runzewe, Tarime, Rorya, Kyaka, Katoro, nk unaweza kuuza chakula kwa
wateja wasiopungua 20 kwa siku. Kama kila mteja utamuuzia chakula kwa
bei ya Tshs 2,000 utaweza kupata siyo chini ya Tshs 40,000 kwa siku. Na
endapo utakuwa na wateja wanaofikia 40 kwa siku utaweza kupata Tshs
80,000 kwa siku. Kama mgahawa wako utazingatia viwango vya usafi wa
hali ya juu, ushindani, viwango vikubwa vya kuwajali wateja; utakuwa na
uhakika wa kupata kipato zaidi ya hicho kwa siku. Je, kama utafanya kazi
kwa siku 7 kwa kila wiki utakosa Tshs 2,400,000 kwa mwezi? Je utakosa
Tshs 28,800,000 kwa Mwaka? Kama mugahawa wako utakuwa kwenye
miji mikubwa ambapo kuna idadi kubwa ya watu na ukawa na uhakika wa
kuuza sahani angalau 150 za chakula kwa maana ya wateja 150 wanaokula
kwa bei ya mjini ya Tshs 3000 au 4000 kwa sahani moja ya wali/ugali kwa
nyama, utakuwa na uhakika wa kuuza zaidi ya Tshs 450,000 au 600,000