Professional Documents
Culture Documents
Safari Ya Bulicheka Na Mke Wake - USER
Safari Ya Bulicheka Na Mke Wake - USER
Safari Ya Bulicheka Na Mke Wake - USER
MKE WAKE
ALFONSO LOOGMAN
YALIYOMO
Safari ya Bulicheka na mke wake
Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu
Safari ya Bulicheka na mke wake
Akasokota kamba ndefu sana, akaivuta juu ile meza, akailaza vizuri sana
katikati ya magogo, halafu akaifunga kwa kamba yake. Kazi hii ilikuwa
ngumu sana kiasi cha kumchosha kabisa, hata hivyo, hakukubali
kushindwa, mwishowe akafaulu.
Lizabeta akasema, “Je, Bulicheka, nitawezaje kuupanda mti hadi nifike
nyumba yetu?”
Bulicheka akajibu, “Wewe usiwe na hofu, nitatengeneza ngazi ya kamba
itakayokuwezesha kupanda kwa urahisi. Nyumba yetu ikiisha kuwa tayari
utaona ajabu kweli kweli. Siyo watu wengi duniani walio na nyumba kama
hii yetu sisi. Tena ni nyumba yenye usalama kamili. Wanyama hawawezi
kutuingilia usiku. Leo ukiwa na njaa huna budi kula nazi tena, kesho
nitakwenda kuwinda paa.
Bulicheka akatengeneza kuta za nyumba kwa kutumia makuti ya mnazi,
akayasukasuka vizuri. Akawahi hata kufanya dirisha ukutani ili wapate
kuyatazama mambo ya nje; mwishowe, ikawa nyumba ndogo, lakini nzuri,
mahali pa kuwatosha watu wawili. Akatengeneza pia ngazi ya kuteremkia
chini. Alichukua vijiti, akaviunganisha kwa kamba toka juu mpaka chini;
bali wakati wa usiku alikuwa akiipandisha juu ili isiwepo hatari ya mtu
kuingia upande ule.
Bulicheka akafikiri: Sasa nitakwenda kuwinda paa. Lakini sina silaha
yoyote. Haidhuru, nitajitengenezea silaha vilevile. Akalitafuta tawi
litakalofaa kuwa upinde, akalichonga vizuri, likawa na ncha mbili. Halafu
akalifungia kamba likawa uta.
Lakini uta peke yake hautoshi. Akakata na mishale pia, akaichonga, ili
zile ncha zake ziwe kali sana kama sindano, hapo akawa mata tayari.
Bulicheka alitaka kuwinda paa. Akatafuta kila mahali asimpate paa, awe
mkubwa awe mdogo. Wanyama aliowahi kuwaona ni mbuni, wale ndege
wakubwa wenye miguu yenye nguvu, kazi yao kutembe chini chini ardhini
bali hawawezi kuruka angani. Akajisemea, “Ikiwa siwezi kumpata paa,
basi, haidhuru, nitajaribu kumpata mbuni. “
Lakini, kumbe, ilikuwa ni kazi. Kwa maana yeye Bulicheka akakaribia,
mbuni humwona na kutoroka.
Akafanya jambo moja. Kwanza alijificha nyuma ya mti. Akajifungia
majani nyuma mithili ya manyoya ya mbuni, akachukua fimbo mkononi juu
yake ikiwa ina tunda linalofanana na kichwa, halafu akajitokeza hivi akiwa
kama mbuni. Ndege wale wakimwangalia kwa mshangao! Mbuni wa
namna gani huyu? Wala hawakutoroka. Hata Bulicheka alipomkaribia zaidi,
akampiga mmoja wao, akamwua.
Kwa furaha kubwa, alimshika shingoni kwa mkono wake, kwa sababu
hakuweza kumbeba kwani alikuwa mzito mno. Akashika njia kurudi
nyumbani akiwa amejaa furaha moyoni, na wimbo mdomoni. Kumbe, mzee
mamba naye alimwona akipita. Yeye pia alikuwa na njaa, akatamani kumla
yule mbuni. Akamnyemelea polepole, akienda taratibu nyuma ya
Bulicheka, kama ilivyo desturi yake, alimkamata yule mbuzi kwa ghafla,
hata akawahi kummeza karibu wote mara moja tu.
Hapo akashtuka zaidi kiasi cha kukata tamaa ya kutoka salama kutokana na
hatari hizo nyingi. Kwa ajili ya hofu kubwa, aliuachilia ule mti, akaanguka
chini. Yule faru alikuwa ameendelea mbele na safari yake, wala
hakumwona. Basi Bulicheka hakuwa na hamu ya kuendelea kuwinda
wanyama tena, badala yake, kwa siku hiyo, alitamani tu kurudi nyumbani.
Wakati huo huo, Lizabeta alikuwa akimngojea Bulicheka arudi, kwani
aliona ya kwamba alikuwa anakawia: Bulicheka huyu alikuwa ameondoka
asubuhi na mapema, na sasa ni saa kumi ya jioni bado hajarudi. Yuko wapi,
maskini? Labda ametumbukia shimoni, au labda amekumbwa na simba.
Kila mara Lizabeta alikwenda kuketi dirishani ili apate kuangalia kama
Bulicheka anarudi au hapana. Lakini ni kazi bure tu. Hata akiangalia mara
kumi au zaidi, hamwoni Bulicheka. Anaiona minazi na miti mingine,
anayaona mawingu, anaiona bahari, kwa sababu yupo katika kilele cha
mnazi wake, lakini mtu yeyote alikuwa hamwoni kabisa.
Mpaka ikatimia saa kumi na moja! Lizabeta akachungulia dirishani ndipo
akamwona Bulicheka akija mbio. Upinde na mishale yake yote imepotea,
anakuja kwa haraka sana, wala haangalii nyuma. Lizabeta akamnyoshea
mkono kumlaki kwa furaha, lakini Bulicheka alikuwa haoni kitu,
amekazana tu kuja mbio. Mwishowe, akafika ngazini, akapanda kwenda juu
haraka haraka akaingia nyumbani mwao, akasimama, akiduwaa, asiweze
kusema neno lolote kwanza, ameshtuka mno! Miguu yake inatetemeka
bado. Lakini Lizabeta anamtuliza moyo, anasema, “Usiwe na hofu hivyo,
Bulicheka. Hapa hakuna hatari. Kama huwezi kuwinda paa wala kanga au
kobe, tutaendelea kula nazi tu, au mbata. Hatuwezi kufa kwa njaa.”
Sehemu ya pili
Mtu wa kwanza, akaleta sahani kubwa ya wali, yaani ndicho chakula cha
kwanza. Watu husema, “Wali ni sultani ya chakula, watawazwa katika kiti.”
Wa pili akaleta kikapu kilichojaa vitumbua vya sukari. Wa tatu, akaubeba
mkungu mzima wa ndizi zilizo kubwa sana. Wa nne akaja na kuku, kila
mkono umemshika kuku mmoja. Wa tano, akaleta sahani ya mayai. Basi,
wakala, wakashiba.
Saa za jioni, kukawa na ngoma. Ngoma yao ya ajabu. Watu wote
wakapiga, wakapiga hata kukawa na muungurumo wa kuziba masikio. Mtu
mmoja alikuwa na mbiu moja ndefu sana kiasi cha kushindwa kuuinua kwa
mikono yake, ikalazwa chini, naye akapuliza ndani yake, akiyavimbisha
mashavu yake mithili ya balungi. Tena mtu mwingine alikuwa na namna ya
zeze ambalo lina umbo kama pembe la nyati, mwenyewe akilipiga, linatoa
sauti kama mlio wa ndege.
Ngoma hizo ziliendelea kwa muda wa saa nyingi sana. Giza lilitanda juu
ya nyumba za watu, lakini mwezi ukaonekana katika minazi.
Lakini machozi yake yote yalikuwa ya bure tu. Kwa maana upepo ule
ulipoanza kuvuma na kuikokota ile merikebu, Bulicheka na watu wake
walifanya kazi kubwa sana ya kukiongoza chombo chao vizuri. Wakajaribu
kwa bidii yao yao yote kuirudisha bandarini, bali hawakufaulu.
Kwanza, usukani wenyewe ulivunjika vipande vipande. Halafu, hata
mlingoti ukapasuka kama kijiti kwa ajili ya upepo uliokuwa ukivuma mno.
Mwishowe, wakakagongana na jabali, merikebu ikatoboka, na kuanza
kuzama. Hapo, wakawa hatarini kweli kweli. Merikebu yao ikasukwasukwa
huku na huku mara kwenye jabali, mara baharini. Hapakuwa tena na mtu
aliyeweza kusimama wima.
Mzee akamjibu, “Mimi jina langu Miraji. Nimekaa katika kisiwa changu
kwa miaka kumi na mitatu, na sijawahi kumuona mtu yeyote. Leo
nimekuona katika jabali hili, basi, nimekuja kukuchukua.”
Lo! Bulicheka na wenziwe wakafurahi sana kuokolewa katika taabu yao.
Wakamfuata mzee Miraji katika ngalawa, naye akawapeleka mpaka
nyumbani kwake.
Mzee Miraji alikuwa na nyumba nzuri. Ilikuwa kama pango katika mlima,
lakini mbele yake kulikuwako kiambaza chenye mlango na dirisha moja.
Mara wakausikia mshindo mkubwa sana kama vile ukuta wa nyumba yao
umepasuka.
Wakaangalia, kumbe wakaona ni kweli, upande wa kushoto, jabali
lilipasuka kabisa, na kutokana na kupasuka huko, hazina yenyewe
iliyofichika kwa miaka mingi, ikaonekana, sarafu za fedha na dhahabu
zikatawanyika ovyo chini, zikajifiringisha huku na huku na kuijaza nyumba
nzima.
Lo! Kwanza Bulicheka na mzee Miraji walipigwa na mshangao. Halafu
wakakumbuka, kumbe hiyo ndiyo hazina iliyokuwako, sasa tumeipata.
Wakachukua magunia, kila mtu gunia lake, wakayajaza sarafu tele, kadiri
walivyoweza.