Professional Documents
Culture Documents
Hulka Za Watu
Hulka Za Watu
(TEMPERAMENTS)
Hulka ni tabia ya asili ya mwanadamu isiyoonekana kwa macho bali kwa matendo. Tabia
hii inategemea mtu na mtu, na kwamba kila mmoja ana sehemu/kundi lake. Yakobo 2:17
hutueleza kuwa Imani iendane na matendo hii itatusaidia kujua hulka ya mtu isiyojulikana.
Mungu pekee ndiye ajuaye kila kitu hatuwezi kumficha chochote. Katika utendaji kazi wa
kanisa Mungu alichunguza hulka ya kila mtu na ndio maana wengine ni wachungaji,
wainjilisti, walimu, wafalme,mitume na manabii, Mfano Daudi. Kama tusipojua nafasi ya
hulka katika utendaji kazi wa kanisa/ biashara/ kazi yoyote huduma hiyo inaweza
kudidimia. Kwa nini? (aliyepewa nafasi hana hulka ya uongozi/ hamasisha).
Mfano:-
1. Sanguine
2. Choleric
3. Melancholy
4. Phlegmatic
ii. Je huwa mimi ni mwepesi wa kutenda mara moja au huwa nabaki mtulivu na kusubiri?
iii. Je huwa natunza kwa muda mrefu hisia kwa jambo lililotendwa kwangu au natunza
kwa muda mfupi tu na kisha kutoweka?
Ikiwa majibu yatakuwa yafuatayo basi mtu huyo ana hulka ya Choleric au Melancholy.
a) Kwa kawaida siwezi kusahahu matusi niliyotukanwa nayakumbuka kwa muda mrefu
na ninapoyakumbuka na kuyafikiria najisikia vibaya.
b) Naweza kuwa na kinyongo dhidi ya aliyenikosea kwa muda mrefu kwa siku nyingi
na kwa majuma mengi
Baada ya kugundua kuwa yeye anaweza kuwa na hulka aina ya choleric au melancholy,
anapaswa kujibu maswali yafuatayo ili ajue hulka yake hasa ni ipi kwamba ni choleric au
melancholy.Maswali hayo ni:-
a) Je, huwa ninaonyesha kwa haraka hali ya kutaka kupambana dhidi ya mabaya
niliyotendewa?.
d) Je, huwa ninapotendewa mabaya nabakia mtulivu kwa nje lakini kwa ndani nikiwa
nahangaika na kuumia?
e) Je, huwa naogopa kupoteza tumaini kiasi kwamba nakosa maneno yafaayo na ujasiri
kwa kujibu na hivyo kuamua kunyamaza kimya?
f) Je, inatokea mara kwa mara ya kwamba sijisikii vibaya muda ule ule ninapotendewa
ubaya lakini baada ya saa chache au kesho yake ndiyo naanza kuwa na hisia kwa
ubaya niliyotendewa?
Kama jibu ni ndiyo kwa swali la (a)-( c) basi mtu huyo ana hulka ya Choleric
Na kama jibu la swali la (d)-(f) ni ndiyo basi mtu huyo ana hulka ya Melancholy
Jibu likiwa ni ndio kwa maswali yafuatayo basi mtu huyo ana hulka ya Sanguine. Maswali
hayo ni:-b
Kama jibu kwa maswali yafuatayo ni ndiyo basi mtu huyo ana hulka ya Phlegmatic.
Ni mtu wa kujitolea:Ni wepesi kujitolea kufanya kazi hata kama ni ngumu haiwezi
Ni muhamasishaji mkubwa : Hushawishi wengine kufanya kazi hata kama hawaziwezi
Huanza kazi kwa mbwembwe: Akianza kufanya kazi utadhani itaisha kwa muda mfupi
kwa sababu ya madoido yake
Hakati tamaa mapema na hufanya uamuzi haraka sana
Kwenye kikao anapenda kujua agenda mapema
Anahitaji kusimamiwa: Muda mwingi anautumia kuongea na kutafuta wapi kuna kundi
la watu wamejikusanya.
Mwepesi kusahau majukumu yake:Kazi inaweza isiishe kwa muda uliopangwa na yeye
haoni tatizo.
Hafuati mpangilio: Anaangalia kazi inayombana ndio anahangaika nayo kwanza. Ni
rahisi kutengeneza madeni.
Si mtu wa nidhamu: Ni mtu wa ahadi njoo kesho kila siku kumbe hawezi kufanya, na
ukimkuta kwa bahati mbaya; nilipata dharura, tufanye kesho
SANGUINE KATIKA MARAFIKI
Habebi malalamiko:Ni vigumu kulalamika mbele ya rafiki zake ila hulalamika chini kwa
chini.
Anachukia kuwa peke yake ; Kumkuta akiwa peke yake basi ameshindwa
kabisa.Anapokosekana watu/watoto /marafiki humuulizia
Anapenda kujibu maswali ya wengine:Swali akiulizwa rafiki yake kabla hajajibu yeye
tayari amekwisha msemea/mjibia
HITIMISHO LA SANGUINE
Mfano: Julius Cesar, Hannibal (North Africa), Dikiteta Stalin, Hitler, Mussolini n.k
Anahamasisha familia kutenda: Hapendi kuona familia imekaa bila kazi, kama mtoto
amekaaa bila kazi anajitahidi amtafutie kazi awajibike
Kila wakati anatumia amri: Anaamrisha wakati wote na anatumia sauti ya uongozi hata
kwa mwenza wake, baba/ mama.
Hana uvumilivu kwa utendaji mbovu: Hapendi kuona kazi inafanywa chini ya kiwango
wahusika huwakemea/kuwaonya
Anatazama ukubwa wa kazï: kila kazi inaipa uthamani mkubwa na kujitahidi kuifanya
vizuri
Anatekeleza kwa haraka jambo: sio mtu wa kujivutavuta katika kazi na anasisitiza
uzalishaji
Kosa dogo ni tatizo: Unatakiwa kuwa makini unapofanya kazi na mtu huyu, kosa
kwake ni uzembe unaotakiwa adhabu
Haelezi kazi kwa kina: Anapogawa kazi haielezi kwa kina ambavyo inatakiwa
kufanyika na kwa kiwango gani
Kila wakati yuko sahihi:Katika marafiki zake yeye anafikiri anachokifanya ni bora na
sahihi kuliko wengine wanachokifanya
Anaamua kwa ajili ya wenzake: Anaweza kuamua kwa niaba ya wenzake na uamuzi
huo ni lazima uheshimiwe.
HITIMISHO LA CHOLERIC
Ikitokea ukawa unafanya kazi kwa karibu na choleric unatakiwa kufanya yafuatayo:
Anaweka viwango vya juu: Anaamini katika mafanikio ya kiwango cha juu
Anataka kila kitu kifanyike kwa wakati: Mzazi huyu anapenda familia yake ifanye
mambo kulingana na wakati uliopangwa, hapendi mtu kutoa udhuru
Anaweka nyumba katika mpangilio mzuri: Mwanafamilia akitoka ni lazima atoe taarifa
anakwenda wapi? Na akichelewa vivyo hivyo atoe sababu za kuchelewa
Anashawishi kukuza vipaji: anapenda watoto wake wawe wabunifu kwa kuwafundisha
na kuwapa nafasi ya kufikiri kwanza.
Anakatisha tamaa watoto: Hajui kumtia moyo mtoto , ukifanya vibaya unaambiwa
live.
Anaweka malengo yasiyofikiwa: Malengo ni makubwa kuliko uwezo ulio nao familia
Hufikiria wenzake
HITIMISHO LA MELACHOLY
Ni msikilizaji mzuri
Ana huruma
Hupenda kutazama wengine wakifanya kazi lakini sio yeye kufanya kazi
Anapinga mabadiliiko
Hapendi kujishughulisha
HITIMISHO LA PHLEGMATIC
Ikiwa unafanya kazi na mtu wa jamii ya phlegmatic au ndiye mkuu wako wa kazi,
unatakiwa ufanye yafuatayo:
MWISHO
Yupo mtu mmoja tu anaweza kubadili tabia yako; YESU KRISTO MWANA WA
MUNGU
Chukua hatua umwendee YESU upate kubadilisha tabia yako uwe kiumbe kipya:2
wakoritho 5: 17