Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 18

BIBLIA KWA TASWIRA, AGANO LA KALE, KITABU CHA 25

Wafalme, Mambo ya Siku ya Siku, Manabii wadogo, sehemu ya 3

BWANA NI MUNGU

(VISUALIZED BIBLE, Vol 25, OT The Lord He Is God)


Author: Katherine E. Hershey, Gertude LaQdis
Artist: Vernon Henkel
Imegeuzwa kwa Swahili Congo na watumishi wa Mungu katika DR Congo

© Bible Visuals International


PO Box 153, Akron, PA 17501-0153
6LPX: 717-859-1131
www.biblevisuals.org

SOMO 1 – MUNGU HABADILIKE

Kwa mwalimu kujifunza mbele: 2 Mambo ya Siku 22:11-24:25; 2 Wafalme 11:2-12:21; Yoeli 1:1-3:21

Shabaa ya somo: Onyesha kama Mungu hawezi badirika kamwe


Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kujua: Mungu anaheshimu wale wanaomuheshimu,
anaadibisha wale wanaoenda mbali naye.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kutambua: Hamu ya kuishi maisha mazuri kwa Mungu.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kufanya: Kutubu na kukataa zambi zote zinazojulikana.

Somo kwa kifupi: (kuandika ndani ya buku ya mwalimu na za wanafunzi.)


1. Mungu anakumbuka taifa l ake (2 Mambo ya Siku 22:11-12; 2 Wafalme 11:2-3)
2. Mungu anaheshimu taifa lake (2 Mambo ya Siku 23:1-21; 2 Wafalme 11:4-21)
3. Mungu anatumia taifa lake (2 Mambo ya Siku 24: 4-14; Wafalme 12:4-15)
4. Mungu anaadibisha taifa lake (2 Mambo ya Siku 24:2,17-27; Yoeli 1:1-3:21)

Shairi la kujua kwa ufahamu: “… geukeni kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa mwenye neema yeye,
anayejaa na huruma, si mwepesi kwa kukasirika, na mwenye rehema nyingi, mwenye kujuta ya mabaya”
(Yoeli. 2:13)

Somo:
1. Mungu anakumbuka taifa lake (2 Mambo ya Siku 22:11-13; 2 Wafalme 11:2-3)

Yoasi alikuwa na mwaka moja alifichwa katika hekalu kubwa ya Yerusalema. Watu wamoja walifahamu
kama alikuwa mule.
Mujomba wa Yoasi, Yehoyada na shangazi (Yoheba) walimuchunga. Mujomba Yehoyada alikuwa kuhani.
Alifundisha Yoasi kupenda Mungu sababu yeye mwenyewe alipenda na kutumika Mungu.
Onyesha taswira 1: Nyuma ya miaka mingi, mujomba Yehoyada alishituka Yoasi. “Yoasi, wewe ni mutu
mumoja anayebaki katika jamaa la mufalme Daudi. Kumepita siku nyingi Mungu alifanya ahadi kwa Mufalme
Daudi: “Jamaa yako na ufalme wako vitakuwa vya milele.” (Angalia Samueli 7:16). Tati yako (Atalia) ni
malkia kwa sasa. Lakini yeye haiko wa nyumba ya mufalme Daudi. Sababu alitaka awe malkia alifanya kitu
kibaya sana. Alianza kuua wana wake wakubwa. Wewe Yoasi alikuwa mutoto muchanga na shangazi yako
aliyekupenda alikuponyesha kwa mujiza. Ulifichwa ndani ya hekalu na uliishi humu ya hekalu la Mungu. Tati
yako mwovu alikusahau kabisa lakini Bwana anakutambuka siku, Yoasi utakuwa mufalme wa Yuda. Na
alifikiri kama wewe ulikufaka vilevile.
Mungu alikumbuka Yoasi. Anatukumbuka na sisi.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 1


2. Mungu anaheshimu Taifa lake (2 Mambo ya Siku 23:1-21; 2 Wafalme 11:4-21)

Siku moja waongozi wa Yuda walikusanyika katika hekalu la Mungu. Kuhani Yehoyada akaeleza: “Yoasi
alikuwa na umri wa miaka saba ni yeye mufalme wa kweli wa Yuda. Yoasi ni wa nyumba ya Daudi na Mungu
atatimiza ahadi yake kwa Daudi. Yoasi alitawala sawa mufalme.
Waongozi walishangaa. Mumoja wa nyumba ya Daudi alikuwa hai! Walimuona na macho yao. Ikawa
wakati wa kijana Yoasi kuwa mufalme!
Yehoyada akatoa amri kwa waongozi: “Katika siku ya sabato, mujigawanye katika kundi tatu. Kundi moja
litachunga nyumba ya kifalme. Kundi lingine litachunga hekalu. Kundi la tatu litachunga lango pembeni ya
hekalu. Walinzi katika hekalu watachunga mufalme Yoasi. Kama mutu anaingia ndani ya hekalu, mumuuwe.
Mubaki karibu ya mufalme mahali pote atakwenda.”
Siku ya Sabato, waongozi walienda kwa kundi na kuzunguka hekalu. Wote walisimama kila mutu kwa
nafasi yake ya ulinzi, akiwa na mikuki na ngao.
Kisha Yehoyada alileta kijana Yoasi na kumuvika taji oya ufalme: “Muone, Yoasi ni mufano wa sheria ya
Mungu.” Yehoyada akasema. Yeye na watoto wake wakamwanga mafuta juu ya kichwa cha Yoasi. Kisha
Yehoyada akasema: “Yoasi wewe ni mufalme wa Yuda!” Makutano wakapiga mikono na kusema: “mufalme
aishi milele!”
Onyesha taswira 2: Mwovu malkia Akalia aliposikia fujo akakimbilia hekaluni. Wajemadari na wapiga
muziki walikuwa pamoja naye. Watu waliimba kwa furaha wakati wanaume walichezea vyombo vya muziki.
Kila mutu alifurahi kupata mufalme mupya. Muzee Atalia lipasua mavazi yake na kusema: “Fitina! Fitina!”
[“Uligeuka mbali nami. Uliniasi! Haukusema kweli kwangu!”]
Yehoyada akaamuru: “Munitoe inje! Kama mutu ye yote ambaye anamfuata mumuue.”
Mwovu Atalia alipwa inje ya hekalu na kuuawa. Ilikuwa azabu juu ya uovu na kuabudu kwake sanamu).
Yehoyada akaambia watu: “ninyi ni wa Mungu mutii ya Mungu.”
Makutano waliahidi kweli kwa Mungu. Walienda mara moja kwa hekalu ya miungu na kubomoa, Nyuma
ya hayo mufalme Yoasi alipelekwa kwa nyumba ya kifalme. Pale ambapo walimuketisha juu ya kiti cha
kifalme. Mungu akaheshimu kijana Yoasi.
Mwenye umri wa miaka saba hangeliweza kukataa shauri za maana za mufalme. Ni mojomba yake
Yehoyada na wengine wakamusaidia kuongoza Yuda, ufalme wa kusini. Nyuma, wakati Yoasi alikomaa,
aliongoza.

Maelezo kwa mwalimu:


Masomo mane katika sehemu hii yanatia mukazo juu tabia za ajabu za Mwenyezi Mungu. Yeye
muumbaji ulimwengu, yeye ni juu ya Mambo ya Siku yote. Sisi watu wake tunapashwa kumuabudu.
Acha heshima yako kwa Mungu uwe mufano kwa wanafunzi wako.

Katika sehemu hizi juu ya vitabu vya wafalme na Mambo ya Siku ya siku kunakuwa ingine tano
iliyowekwa ndani juu ya unabii wa manabii wadogo. Mwanainchi Ivan Allbut (Mwanamemba wa
Conseil Editorial anayeheshimiwa) aliandika:

“Vitabu kumi na viwili vya mwisho vya Agano la Kale vinaitwa mra kwa mara manabii wadogo. Ni
vya lazima vilevile na hakika vilevile vilifunuliwa na Mungu sawa vitabu vingine vya manabii. Vyote
vinasema juu ya hukumu ya Mungu: (1) juu ya Israeli na Yuda, (2) juu ya jirani zao na (3) juu ya dunia
nzima. Vinaonyesha vyote neema ya Mungu katikati ya hukumu. Na kwa hali ingine, vinakazisha
kurudi kwa Bwana Yesu Kristo duniani. Vinasema vilevile juu ya kuwekwa kwa ufalme wake na
Yerusalema muji mukubwa wa dunia. Na vinasema juu ya utaratibu mupya katika dunia nyipya
inayokuja tena. Pamoja vinatuonyesha maono ya neema nyipya kupitia hukumu.”

Si lazima kutumia majina yote ya wote waliohuzuria katika masomo haya. Mwalimu: Majina
yanayokuwa (entre parenthèse) ni kama musaada. Wanafunzi wako hawahitaji kuwajua.

Fasirio: Taswira ni ndani ya jalada, onyesha wanafunzi mahali panapotajwa katika masomo.
CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 2
3. Mungu anatumia Taifa lake (2 Mambo ya Siku 24: 4-14; Wafalme 12:4-15)

Mufalme Yoasi alikusudia hekalu la Mungu lijengwe karibuni miaka 150 ilipita kwa kujenga hekalu nzuri.
Wafalme wamoja waliotawala katika miaka hii hawakupenda Mungu. Maana yake hekalu halikujengwa.
Mufalme alikusanya makuhani: “Mwende katika miji ya Yuda!” Akaamuru: “Kusanya mali ambayo watu
wanapashwa kulipa Mungu. Mali yale itatumiwa kwa ujenzi wa hekalu.”
Wakati makuhani hawakutii mara moja mufalme Yoasi, alitoa mupango mupya: “Tutaweka sanduku kwa
mazabahu ndani ya hekalu. Watu wataweka zawadi katika sanduku wakati watakuja kuabudu.”
Kwa amri ya mufalme Yehoyada alifanya sanduku. Alichimba tundu katika mulango. Aliiweka ngambo
ya kuume ya mazabahu. Kisha mufalme Yoasi alituma kwa watu wote: “Mulete zawadi zenu za pesa hekaluni
wakati munakuja kuabudu.”
Onyesha taswira 3: Mara moja watu walitii kwa furaha. Walileta mali yao na kuyaacha kuanguka ndani ya
sanduku. Walitoa hadi sanduku ilijaa mara nyingi. Watu walifurahi! Sisi vilevile tunafurahi wakati tunajitoa
kwa kazi ya Mungu.
Kulikuwa mali nyingi. Waseremala, wajengaji, wapasuaji wa mawe na wengine walianza kazi. Hekalu
lilijengwa na watumishi wote wakalipwa. Hekalu lilitukiwa upya kwa kuabudu Mungu. Biblia inasema: “Watu
walitoa sadaka za kuteketeza katika nyumba ya Mungu kila siku bila kuacha muda wa maisha ya Yehoyada, 2
Mambo ya Siku 24:14). Mungu alitumia taifa lake kwa kufanya kazi yake. Mungu angali anatumia tena watu
wake kwa kazi yake.
Yehoyada, kuhani mukubwa alikuwa muzee ( alikufa kwa miaka 130). Nyumba ya kufa kwake Mambo ya
Siku maovu yalitokea.

4. Mungu anaadibisha Taifa lake (2 Mambo ya Siku 24:2,17-27)

Watu wamoja waovu waliyoongoza Yuda wakasema kwa mufalme Yoasi. Watu waovu wana tabia ya
kusema uovu. Mufalme aliwasikia kwa mushangao na kugeuka mbali na Mungu. Kuliko kuwa mwenye nguvu
kwa Bwana, mufalme Yoasi alienda mbali maye. Mufalme Yoasi aliacha kuabudu kwa hekalu la Mungu
ambalo yeye mwenyewe alijenga tena. Kuliko aongoze watu wake kwa Mungu, Yoasi aliwafuata hadi kwenye
sanamu. Mufalme alifanya zambi na Mungu anachukia zambi.
Bwana Mungu alikasirikia mufalme na taifa la Yuda. Lakini aliwapenda tena. Kwa hiyo alituma tena
manabii kwa kupima kuwarudisha kwake (tazama 2 Mambo ya Siku 24:19). Nabii Yoeli, alisema maneno ya
aya yetu: “…geuka kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa mwenye neema yeye, anayejaa na huruma si mwepesi
kwa kukasirika na mwenye rehema nyingi.” (Yoeli 2:13) (Sukuma wanafunzi kurudilia aya hii).
Nabii akatoa agizo hili: “Musikie haya; Waee! Mutege sikio, ninyi wote wenyeji wa inchi! Hakuna kitu cha
namna hii kilichofikilia kwa wakati na baba zenu?” Kisha, akasema kwa jeshi la ajabu la nzige. Walikula
mashamba yote. Mbegu, zabihu, miti yote iliharibiwa na nzige. Hata nyama waliteswa, kulibaki tu maji
(Angalia 1:4,11-12). Sababu gani Mungu aliruhusu uharibifu huu? Sababu watu walifanya zambi na kuwenda
mbali na Bwana.
Onyesha taswira 4: Yoeli anasema mengi katika unabii huu. Alisema: “Siku ya Bwana – siku kubwa.
(Magumu makubwa yanakuja! (Tazama Yoeli 2:1). Nabii Yoeli alisema maneno haya kumepita miaka mingi
(Karibuni miaka 800 mbele ya kuja kwa Yesu duniani). Lakini “Siku ya Bwana haiyakuja, hapana.” “Siku
hii”, Yoeli anasema: “Itakuwa siku ya giza. Hakuna siku ya giza na mvua. Jeshi kubwa na la nguvu litakuja
(Jeshi la nguvu kushinda nzige). Mbele jeshi hili likuje, inchi itakuwa nzuri kama bustani ya Edeni. Nyuma ya
kwenda kwa jeshi hakutabaki kitu. Yote yatakuliwa na moto mukali.” (Tazama Yoeli 2:2-3) Yoeli aliendelea
na agizo lake akisema: “Siku ya Bwana ni ya hatari. Nani ataweza kuivumilia? Musikie maneno ya Mungu:
“Rudi kwangu kwa moyo wako wote.” (Angalia Yoeli 2:11-12). Mungu aliendelea kuomba taifa lake
kumurudilia. Anahitaji sana kuhurumia taifa lake.
Wewe ni mumoja wa jamaa ya Mungu? Kama ndio, hautakuwa juu ya dunia muda wa siku hii ya hatari ya
Bwana. Utakuwa katika ulinzi ndani ya paradiso.
Yoeli alimaliza unabii wake na habari njema za kufuata siku ya Bwana. Mungu anasema: “Yuda na
Yerusalema wataishi milele. Nitawasamehe” (Tazama Yoeli 3:20-21).
CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 3
Mufalme Yoasi na watu wake walisikia maagizo ya manabii. Lakini walikataa kurudilia Mungu. Kwa
mwisho, Bwana alituma Zakaria, mwana wa mujomba Yehoyada. Zakaria akasimama mbele ya watu na
kusema: “Haya ni maneno Bwana anasema: “Sababu gani hamukutii maagizo ya Bwana? Hamutasitawi
kamwe. Sababu mulienda mbali na Bwana, na aliwaacha” (Tazama 2 Mambo ya Siku 24:20).
Wafalme na rafiki zao waovu hawakupenda unabii wa Zakaria. Mufalme Yoasi akaagiza: “Auawe na
mawe!” Na akafanyiwa vile.
Fikiri juu ya ile! Mufalme Yoasi aliishi sababu baba yake na Zakaria Yehoyada, alimuchunga. Yoasi
hakukumbuka tena wema wa mujomba Yehoyada. Kwa hiyo aliuwa mwana wa yehoyada, Zakaria. Vilevile,
katika maisha ya mujomba yake Yehoyada, Yoasi alitumikia Bwana (Angalia 2 Mambo ya Siku 24:2). Lakini
watu wabaya waliacha Mungu.
Ni kwepesi kupendeza Mungu wakati uko pamoja na wakristo wengine. Lakini namna gani unaishi wakati
wewe ni pamja na watu bila Mungu? Kwa mufano wanataka kutosha wakristo katika musingi na wanacheka
Biblia. Utasema nini? Utafanya nini wakati wanaapa, wanasema uwongo ao kuiba? Utageuka mbali na Mungu
kama vile Yoasi alifanya?
Sababu ya zambi zake, Bwana aliazibu mufalme Yoasi; alileta kundi ndogo la jeshi la Suria kutembelea
yerusalema (Yerusalema ulikuwa muji mukuu wa Yuda. Onyesha Yerusalema na Suria juu ya taswira. Pale,
Wasuria wakapiga jeshi kubwa la Yuda. Wasuria wakaua waongozi waliopeleka Yoasi mbali na Mungu
(Angalia 1 Mambo ya Siku 24:23-24). Mungu akapatia Wasuria ushindi juu ya taifa lake. Sababu gani?
Sababu mufalme Yoasi na Yuda walienda mbali na Mungu.
Mufalme Yoasi alitaka Wasuria watoke Yerusalema. Kwa hiyo, alikamata hakiba ya zahabu takatifu ya
hekalu la Mungu na nyumba ya kifalme. Yoasi akaamuru Wasuria: “Twaeni hii kwa mufalme wenu.” Jeshi la
Suria likaenda na vitu vile vya lazima vya zahabu mara moja, na kurudi kwao haraka. Hakiba nzuri ya Mungu
ikaenda inchini mwa adui! (Tazama 2 Wafalme 12:18)
Watumishi wa Yoasi waliua Yoasi sababu aliua mwana wa Yehoyada. Mwana wa Yoasi (Amazia) akawa
sasa mufalme mupya. Hivi mumoja wa nyumba ya Daudi alikuwa tena juu ya kiti cha ufalme, sawa vile Mungu
aliahidi.
Sababu mufalme Yoasi alienda mbali na Mungu, akamuazibu. Bwana habadilike. Angali anaazibu wale
wanaoenda mbali naye. (Mwalimu: Mungu hatumie tu kifo sawa azabu. Lakini 1 Wakorinto 11:27-31, 1 Yoane
5:16).
Umekwisha kwenda mbali na Mungu? Umekwisha kufanya kisichopendeza Mungu? (Mwalimu: Unahitaji
kusoma Waefeso 4:30-32). Biblia inasema: Ni jambo la kuogopesha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye
hai, (angalia Waebrania 10:31). Usione kama ni kitu cha heshima kwa Bwana kukuadibisha. Anakupenda na
anataka kukusamehe kwa makosa uliyoyafanya. Unataka kutubu zambi zako kwa wakati huu (Mezali 28:13; 1
Yoane 1-9).
(Mwalimu: Toa muda wa kimya kusudi Bwana aseme kwa kila mumoja).

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 4


Biblia AK Kitabu 25

SOMO 2 – MUNGU ANAFANYA MEMA MARA KWA MARA

Kwa mwalimu kujifunza mbele: 2 Mambo ya Siku 24:1-26:23; 2 Wafalme 14:1-21; 15:1-7,32; Amosi 1:1-
9:15

Shabaa ya somo: Kuonyesha kama Mungu anafanya vizuri kwa kuhukumu wenye kiburi.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kujua: Hatuna sheria hata moja ya kuwa na kiburi sababu jinsi
tulivyo na yote tuliyo nayo inatoka kwa Mungu.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kutambua: Hali ya unyenyekevu, sababu wema wa Mungu ni
neema.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kufanya: Kutubu kiburi chote kwa Bwana. Acha kuabudu
sanamu. Shukuru Mungu kwa ahadi zake za mapendo.

Somo kwa kifupi: (kuandika ndani ya buku ya mwalimu na za wanafunzi.)


1. Mungu anaongoza taifa lake (2 Mambo ya Siku 25:1-13; 2 Wafalme 14:1-2)
2. Mungu anachukia kiburi katika taifa (2 Mambo ya Siku 25:14-28; 2 Wafalme 14:8-14)
3. Mungu anasaidia taifa lake (2 Mambo ya Siku 26: 1-15; 2 Wafalme 14:21)
4. Mungu anaazibu taifa lake (2 Mambo ya Siku 26:16-23; 2 Wafalme 15:32; Amosi 1:1-9:15)

Shairi la kujua kwa ufahamu: “… geukeni kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa mwenye neema yeye,
anayejaa na huruma, si mwepesi kwa kukasirika, na mwenye rehema nyingi, mwenye kujuta ya mabaya” (Yoeli
2:13).

Somo: Yoasi, aliyekuwa mufalme wa Yuda akiwa kijana, alianza vizuri. Sawa mutu, alifanya kazi kubwa.
Nani atasema kuhusu aliyoyafanya? (Acha wanafunzi wahojeane juu ya utafuti wa mali Yoasi alifanya ao
ujenzi wa hekalu ya Mungu. Kwa maulizo, endelea kuuliza kuhusu maisha ya Yoasi). Kwa mwishi mufalme
Yoasi alikataa kusikia manabii wa Mungu. Hakurudi tena kwa Mungu. Mwisho Mungu aliruhusu auwawe.
Yoasi mufalme wa nyumba ya Daudi alipoteza ufalme na maisha yake. Mwana wake Amazia, mwenye miaka
25 akawa mufalme wa Yuda. Tusome pamoja 2 Mambo ya Siku ya Siku 25:2: Amazia akawa: “Alikuwa
mwema machoni pa Bwana, lakini hapana na roho safi.” Hiyo inasikilika vizuri? Vibaya? Ao yote mbili?
Sikiliza vizuri!

1. Mungu anaongoza Taifa lake (2 Mambo ya Siku 25:1-13; 2 Wafalme 14:1-2)

Wakati ukafika, mufalme Amazia alikusudia kama anahitaji kuwa na jeshi nzuri. Alikusanya watu wote wa
Yuda (Ufalme wa kusini). Katika watu hawa alichagua wanaume wa karibuni miaka 20. Kwa wakati
waliposimama kila mutu kwa fasi yake mufalme Amazia aliwahesabu. Alianza: “moja … wawili … 10 … 20
… 50 … 100 … 5000 … 100.000 …300.000!” Jeshi gani! wote 300.000 walikuwa na uwezo wa kushika
mukuki na ngao. Waaskari wakubwa!
Mufalme Amazia alipanga kutuma jeshi lake kupigana na Edomu. (Mwalimu: Onyesha Edomu ndani ya
jalada). Kwa kuwa hakika na ushindi mukubwa, Amazia alitaka waaskari wengi. Alituma kutafuta katika
Israeli (Ufalme wa kaskazini), wanaume 100.000. kwa wale watu alilipa mali nyingi. Jeshi gani tunalo sasa!
Nyuma ya pale, mutu wa Mungu akafika (nabii). “Ee mufalme Amazia!” Akaanza: “Usiache waaskari wa
Israeli.” Mukumbuke! Israeli ulikuwa na wafalme wabaya walioongoza Waisraeli mbali na Mungu. Mutu wa
Mungu akasema tena: “Kama ukikamata waaskari wa Israeli pamoja nawe, Mungu atakuangusha. Mungu ana
uwezo wa kusaidia ao kuangusha.” Bwana akaongoza mufalme Amazia kupitia nabii wake.
Amazia alikuwa na ulizo kwa nabii: “Nifanye nini na hii mali nililipa kwa wale waaskari wa Israeli?”
Mutu wa Mungu alikuwa na habari njema: “Bwana anaweza kukutolea mengi zaidi ya ile.”
CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 5
Onyesha taswira 5: Mufalme Amazia alisikia nabii na akatii maneno yake. Akarudisha waaskari wa
Israeli kwao. Waaskari waliwaza wataiba mali mingi katika hakiba za Waedomu. Kwa hiyo, walikasirikia
Yuda sana. Hawawezi kusahau ile!
Kisha mufalme Amazia akaongoza jeshi lake la 300.000 kule Edomu. (onyesha kwa taswira). Kule Mungu
akamupa ushindi mukubwa. Hata na lile jeshi ndogo ambalo Amazia alitaka, alishinda Waedomu. Bwana
aliongoza mufalme kupitia nabii aliyemupa ujumbe wa Mungu.

Maelezo kwa mwalimu:


Historia na buku ya yote iliyopita. Unabii unasema lile litakalokuja. Vitabu vine vya Biblia vya
wafalme na Mambo ya Siku ya Siku vinakuwa na historia ya lazima. Taifa la Mungu lingelikuwa na
Mungu mwenyewe sasa mufalme wao. Kuliko kuchagua kuwa na wafalme wa dunia sawa mataifa
jirani. Vitabu hivi vine vinaeleza magumu yaliyoletwa na wafalme wamoja wa dunia. Wafalme
wamoja walianza vizuri. Wengi wao walikataa Mungu na taifa lao.

Mungu alipenda taifa lake na hakutaka kuwaazibu. Kwa hiyo alituma manabii waliwaamuru
yatakayokuja, kama walikosa kumutii. Wakati watu walikataa kurudi kwake, aliwaazibu. Kwa njia ile
unabii ulitimilika. Ndio maana, manabii wamoja walitabiri juu ya Mambo ya Siku fulani ambayo
haijatimilika. Sababu Neno la Mungu ni kweli, kila kitu kilichotabiriwa na manabii kilitimilika.
Bwana anakuwa na mupango wa utaratibu juu ya Mambo ya Siku yote. Yote itatimilika kwa wakati
wake.

Mambo ya Siku ya siku (Ufuatano wa Maelezo na historia ya Mambo ya Siku) ya mufalme huyu wa
Agano la Kale yangelipashwa kuwa mufano kwa wanafunzi wako. Bwana atumie vitu vilivyotabiriwa
na manabii kwa kutuarifu na kututia nguvu sote.

Note: Katika masomo haya kuna maneno sawa: kuteka, kuharibu, kunyanganya, kuteka nyara, nyara
yanaamanisha wizi wa kinguvu. Fasiria na tumia neno moja ambalo wanafunzi wataweza kukumbuka
wepesi.

2. Mungu anachukia kiburi katika taifa lake (2 Mambo ya Siku 25:14-28; 2 Wafalme 14:8-14)

Mufalme Amazia na waaskari wake walishangilia ushindi wao. Walinyanganya vitu katika nyumba za
Waedomu, wakabeba vitu vingi.
Mufalme akaleta sanamu za Waedomu. Akaziweka, akazitolea sadaka na kuziabudu. Fikiri juu ya ile.
Mufalme amazia aliabudu sanamu zilizochongwa ni mikono ya watu. Sanamu zilikuwa na macho lakini
hazikuona zilikuwa na masikio ambayo haikusikia. Zilikuwa na vinywa lakini hazikusema (Angalia Zaburi
135:15-17). Mufalme Amazia hakushukuru Mungu aliye hai kwa ushindi wake, ubaya wake, aliabudu sanamu.
Bwana alikasirika kuhusu ile. Alituma nabii kwa mufalme Amazia kuletea ujumbe: “Sababu gani unaabudu
miungu ya Waedomu? Miungu yao haikuwaokoa kwa Waedomu na jeshi lako” (Angalia 2 Mambo ya Siku
25:15).
Mufalme Amazia akakasirika sana kusikia ujumbe wa nabii. Akasema: “Wakati gani tulikuambia utoe
mashauri kwangu, mimi mufalme? Nyamaza ao nitakuwa!”
Nabii akatabiri polepole: “Sababu haukusikia ujumbe wa Mungu, atakuharibu” (Tazama 2 Mambo ya Siku
25:16).
Mufalme Amazia wa Yuda alihangaishwa zaidi sana jinsi hakuwazia. Waaskari wa Israeli waliorudishwa
kwao walikasirika. Kwa hiyo walishambuliwa muji ya Yuda, akawa watu 3000 (Tazama 2 Mambo ya Siku
25:13). Wakachukua vitu vya nyumba na kupeleka mateka. Kwa hiyo, mufalme Amazia alipiganisha mufalme
wa Israeli (Yoahasi)
Mufalme wa Israeli alijibu: “Sababu ulishinda Edomu, unakua na kiburi: Baki nyumbani, ao wewe na Yuda
mutakuwa katika magumu” (Tazama 2 Mambo ya Siku 25:19).

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 6


Amazia mufalme wa kiburi wa Yuda hakusikia mufalme wa Israeli. Akaanza vita. Sababu mufalme Amazia
alienda mbali na Mungu na kuendea sanamu, Mungu alikataa kuwasaidia. Kwa hiyo, jeshi la Yuda lilipotea
njia na mufalme akashikwa (Angalia 2 Mambo ya Siku 25:23).
Onyesha taswira 6: Jeshi la Israeli lilikamata mufalme Amazia aliyepotea njia ya Yuda pa Yerusalema.
Pale aliangalia uharibifu wa kuta za muji wa Israeli. Aliona wanateka hekalu la Mungu na nyumba ya mufalme.
Hazina kubwa pamoja na wafungwa wa vita wakapelekwa Samaria (Muji mukuu wa Israeli – onyesha taswira).
Hatujui tena kitu kuhusu Amazia ila kuharibiwa kwake. Unabii wa nabii ukatimia.
Neno la Mungu linasema: “Majivuno yanatangulia uharibifu, na roho ya kiburi inatangulia kwanguka”
(Tazama Mezali 16:18). Ilikuwa kweli kabisa juu ya mufalme Amazia. Bwana alipima kumusikilizisha.
Alituma nabii wake kwa kurudisha Amazia asiabudu sanamu na kurudilia Mungu. Maneno ya aya yetu
yanasema jinsi Mungu alitaka awe. (Wanafunzi wataje Yoeli 2:13b). Lakini Amazia hakusikia.
Unakuwa na ujuzi ambao wengine hawana? Kama ndio, shukuru Mungu kwa ukimya. Yeye ni yule
anayefanya wema milele, anapana ujuzi kwa taifa lake. Kiburi kinaweza kuharibu. Mungu anachukia kiburi
(Tazama Zaburi 101:5,6; Mezali 6:16:16-17; 21:4)

3. Mungu anasaidia taifa lake (2 Mambo ya Siku 26: 1-15; 2 Wafalme 14:21)

Mwana wa Amazia, Azaria aliyekuwa na miaka 16 akawa mufalme wa Yuda. Mufalme Azaria aliabudu
Bwana. Alikuwa muzuri aliyeleta heshima kwa taifa lake. Yuda akawa tena na nguvu. (Ulikuwa kubwa sana
kuliko wakati wote tangu mufalme Solomono). Mufalme Azaria alikuwa shujaa sana. Alikuwa mujengaji
muzuri, mufugaji na mugeuzi muzuri. Alijua namna ya kutoa mavuno mazuri. Aliongoza vizuri jeshi lake
kubwa na kufanya silaha za vita. (Mwalimu: kufuatana na miaka ya wanafunzi wako uwasomee 2 Mambo ya
Siku 26:9-15).
Onyesha taswira 7: Mufalme Azaria alikuwa mutu wa uwezo. Biblia inasema juu yake: “Katika siku
zake alitafuta Bwana, Mungu alifanya asitawi (2 Mambo ya Siku 26:5). Inasema vilevile: “Mungu alisaidia
Azaria (Tazama 2 Mambo ya Siku 26:7). Sababu Azaria alikuwa na jeshi kubwa, Yerusalema ulilindwa juu ya
maadui. Kwa sababu ya ushujaa wa mufalme Azaria akawa mutu mukubwa katika inchi zingine: “Sifa yake
ilienda mbali, sababu alilindwa mpaka alipokuwa na nguvu zaidi” (Tazama 2 Mambo ya Siku 26:15) Nani
alisaidia mufalme Azaria? Bwana alikuwa musaada wake.
Mungu ni wake sababu anafanya wema milele anasaidia watu wake wanaomutafuta. Kama ninyi ni wana wa
Mungu atawasaidia. Munataka kuomba musaada wake.

4. Mungu anaazibu taifa lake (2 Mambo ya Siku 26:16-23; 2 Wafalme 15:32; Amosi 1:1-9:15)

Sikia sasa Neno la Mungu: “Lakini wakati Azaria alipokuwa na nguvu moyo wake ulijaa kiburi,
akajipandisha kwa kupoteza.” Mufalme Azaria akawa na kiburi. Na sababu ya kiburi chake, alifanya mambo ya
kuogopesha.
Mufalme Azaria aliingia ndani ya pahali patakatifu ndani ya hekalu. Alikuwa tayari kuchoma uvumba
katika mazabahu ya uvumba. Mbele sanaMungu aliamuru makuhani tu waliweza kufanya vile (Tazama Kutoka
30:7-9; Hesabu 16:40). Mufalme Azaria hakuwa kuhani na alifahamu sheria ya Mungu.
Zaidi ya makuhani 80 walifuata mufalme mpaka pahali patakatifu. Wakasema kwa nguvu: Si vizuri kwako.
Ee mufalme, kuchoma uvumba kwa Bwana. Mungu aliweka makuhani kwa kuifanya. Toka mahali patakatifu.
Mungu hatakuheshimu.”
Mufalme Azaria alikasirika ndani ya hekalu takatifu la Mungu, alitombokea makuhani.
Onyesha taswira 8: Sawa mufalme alikasirika, ukoma (vidonda vikubwa na vya kuambukia) Ukaonekana
kwa uso wake. Makuhani waliona wakamupeleka inje. Azaria naye alitaka kutoka pahali patakatifu pa Mungu.
Lakini ni nyuma kabIsaya Mungu alikuwa amepiga mufalme. Atakuwa na ukoma katika maisha yake yote.
Hangeweza kuishi tena katika nyumba yake ya kifalme. Alipashwa kuishi katika nyumba mbali na watu.
Ilikuwa sheria ya Mungu kwa wale waliokuwa na ukoma (Tazama Walawi 13:46). Tangu saa ile mpaka kifo
chake, mwana wa Azaria (Yotamu) akafanya ya mufalme.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 7


Kwa muda ule, Mungu aliita muchungaji (wa ngombe), Amosi awe nabii. Mungu akatuma Amosi
Betelehemu ya Israeli. (Onyesha taswira). Kwa kutoa unabii (tazama Amosi 7:12-13). Kwa miaka ya mbele
mufalme Yeroboamu wa Israeli aliwekaka sanamu ya zahabu pa Beteli “Muabudu hapa” Yeroboamu akaamuru
Waisraeli. Kwa hiyo taifa lilienda mbali na Mungu aliye hai wa Mbinguni. Waliabudu sanamu iliyotengenezwa
na mikono ya mutu. Mungu hangeweza ao kutaka kukubali kuabudu sanamu (Tazama Kutoka 20:1-5).
Kuabudu sanamu ni zambi. Zambi inapashwa kuhukumiwa, lakini Mungu ni mwenye haki, yeye ni kweli.
Hangeweza kuhukumu taifa lake bila kuliharifu kwanza juu ya zambi zake. Kwa sababu hiyo Bwana alituma
Amosi pa Beteli.
Onyesha taswira 9: Amosi akasema: “Bwana ananguruma! Kwa mushangao Amosi alianza kusema juu ya
zambi za jirani za Israeli. (Mwalimu: Tumia taswira tia maandiko kwa majina ya mahali kufuatana na jinsi
unaonyesha wanafunzi).
Nabii Amosi alisema waziwazi: “Bwana anasema hivi kwa Domasi, mujlikuwa wabaya kwa wafungwa.
Nitatuma nyumba ya kifalme na ngome zake. Nitavunja lango (kuacha miji bila ulinzi). Wewe taifa la Suria
utapelekwa utumwani.” (Watakamatwa sawa wafungwa kwa inchi ingine).
Amosi akaendelea: “Bwana anasema: “Gaza (katika Filistini) atakamata makabila yote na kuyauza sawa
watuMwanzo Kwa hiyo nitatuma moto wa kuharibu miji ya Filistini (Tazama Amosi 1:6-8).
Muji wa Tiro utasikia maonyo ya Mungu juu ya zambi zao. Hiyo ilifuatana na: “Nitatuma moto.” Mungu
hatafunga macho juu ya zambi zao.
Amosi akasema tena na nguvu ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Edomu, Amoni, Moabu. Zambi zao si
sawa, lakini azabu ya Mungu itakuwa moja. Anasema: “Nitatuma moto.” [Inchi hizi tatu zitakamatwa na
Waasuria].
Amosi akageuka kwa makabila mawili ya Yuda, inchi yake. Mungu anasema: “Mulitupilia sheria ya
Bwana mulipotezwa na miungu ya uongo. Nitatuma moto.”
Waisraeli walifurahi kusikia kuna jirani zao wataazibiwa? Inawezekana Amosi mugeni Israeli, hangesema
kwao kwa makali. Wapi angelipashwa? Mungu alituma Amosi katika Israeli. Kwa hiyo alipashwa kusema
kuhusu ujumbe wa Mungu.
Nabii Amosi akaanza: “Bwana anasema hivi kwa Israeli: “Munakanyaga kichwa cha masikini.
Munaamuru manabii wasitabiri: Nitakuponda. Siku nitahukumu Israeli juu ya zambi zao, nitaharibu
mazabahu” Tazama Amosi 2:6-16; 3:14). Nama ya zahabu haikufichwa mbele ya macho ya Mungu.
Bwana akasema mingi, mingi sana juu ya taifa la Israeli. Kisha akaongeza: “Sababu nitafanya vile kwenu,
mujitayarishe kwa kukutana na Mungu wenu, Ee Mungu.” Mungu akisihi taifa lake: “Unitafute na utaidhi,
usitafute Beteli [fasi ya sanamu] Beteli atashushwa chini sana (Angalia Amosi 5:4-6).
Yote Mungu alisema ilikasirisha kuhani wa Beteli. Akasema kwa Amosi. “Toka! Kwenda Yuda na kufanya
unabii wako kule. Usitabiri tena Beteli … Ni hekalu la Israeli” (Tazama Amosi 7:12-13). Taifa la Israeli
lilipenda sanamu yao ya dama ya zahabu. Hawatarudiliaka tena Bwana anayewapenda.
Mungu akasema kwa Israeli kwa uchungu kupitia nabii wake: “Hakika Israeli wataenda utumwani, mbali
na inchi yao ya kuzaliwa. Sitaweza kusahau yote waliyofanya. Macho ya Bwana ni juu ya ufalme unaofanya
zambi. Nitawaharibu juu uso wa dunia.” Mungu anahukumu wafalme wenye zambi sawa Azaria. Anaazibu
vilevile miji na inchi zinazoishi katika zambi.
Mungu akaongeza habari hii kubwa kuhusu wakati utakaokuja: “… nitasimamisha hema la Daudi.
Nitalitengeneza na kulisimamisha na kulijenga sawa vile lilikuwa” (Amosi 9:11-12). Bwana aliahidi Daudi
(miaka 300 mbele) kama ufalme wake utakuwa wa milele. Mungu alirudilia ahadi yake. Utawala wa Daudi
(Hema) utaendelea, hata kupitia Azaria, wa ukoo wa nyumba ya Daudi aliyefanya zambi. Mungu wa mbinguni
aliye hai hawezi kusahau! Ni yeye Anayeazibu zambi, anakumbuka ahadi zake za upendo. Mungu anaendela
kufanya wema. Umekwisha kupata magumu ya kiburi sawa Azaria? Omba musaada wake kwa kuacha zambi
anayoichukia. Umekwisha kupenda kitu fulani ao mutu fulani kupita Bwana (sawa vile taifa la Israeli
walifanya?) Kama ndio, unataka kuomba musaada wake?
Sisi wote tushukuru Mungu kwa unabii wake wa ajabu. Tumushukuru kusudi yatimilike kwa wakati wake.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 8


Biblia AK Kitabu 25

SOMO 3 – MUNGU ANAKUA NA UWEZO WOTE

Kwa mwalimu kujifunza mbele: Yona 1:1-4:11; 2 Wafalme 15:32-16:20; 2 Mambo ya Siku ya Siku 27:1-
28:8; 16:27; Isaya 7:1-12; Mika 1:1-7:20.

Shabaa ya somo: Kuonyesha kama Mungu ni Muweza yote.


Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kujua: Mungu hakutukazaka tumutii.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kutambua: Hamu ya kutii Mungu.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kufanya: Kuomba Mungu awasaidie kumutii.

Somo kwa kifupi: (kuandika ndani ya buku ya mwalimu na za wanafunzi.)


1. Mungu anaamuru kila mara (Yona 1:1-4:11)
2. Mungu anaweza kufanya kila kitu (2 Wafalme 16:5-6; 2 Mambo ya Siku 28:5-8,16-19)
3. Mungu ana uwezo wa kulinda taifa lake (2 Mambo ya Siku 28:8-15; Isaya 7:1-9)
4. Mungu ni mwenye uwezo (2 Wafalme 16:7-19; 2 Mambo ya Siku 28:20-25, Isaya 7:10-12; Mika 1:1-7:20).

Shairi la kujua kwa ufahamu: “… Geukeni kwa Bwana, Mungu wenu, kwa kuwa mwenye neema yeye,
anayejaa na huruma, si mwepesi kwa kukasirika, na mwenye rehema nyingi, mwenye kujuta yale mabaya
(Yoeli 2:13).

Somo: Mara kwa mara watu wanafurahi kuwa manabii wa Mungu aliye hai. Elisa, Elia, Obadia, Yoeli, Amosi
wote walisema juu ya Mungu. Walitabiri juu ya maonyo kwa azabu kama watu wanaendelea kufanya zambi.
Mara ingine, waliosikia, walikubali ujumbe wa Mungu. Mara nyingi, walikataa na hata waliua manabii wa
Mungu. (Tazama Matendo 7:52).
Kwa kawaida, manabii walitabiri juu ya Yuda na juu ya Israeli. Mungu alichagua watu hawa kwa ajili yake
mwenyewe. Sababu hiyo, Mungu alitumia nabii Amosi kuarifu miji na inchi jirani. Tana uliyokuwa mbali ni
Ninawe muji mukuu wa Asuria (Onyesha taswira).
Waovu, wakali (Waasuria) walikuwa wenye kuabudu sanamu. Bwana alitaka wafundishwe naye.
Atasamehe zambi zao nyingi wakimugeukia.

1. Mungu anaamuru siku zote (Yona 1:1-4:11)

Siku mumoja Bwana akasema kwa Yona: “Kwenda katika muji mukubwa wa Ninawe na kuwaambia kama:
Uovu wako unapanda hadi kwangu. (Yona 1:2) Ninawe (muji mukubwa wa Asuria). Ulikuwa mbali na muji
wa Yona, Gati wa Eferi (Mwalimu: Onyesha majina ya mahali juu ya taswira). Mungu aliambia Yona awe
nabii.
Yona alijua lile alipashwa kufanya. Kuliko kutii Mungu na kuenda Ninawe, alienda Yofa (muji uliyokuwa
karibu na Bahari ya Kati). Pole, aliingia ndani ya merikebu (mashua) kwa kuenda na watu na kuenda Tarsisi
(karibuni 2000 km. ngambo ya magaribi). Katika mashua, Yona alilala.
Kisha Mungu alituma upepo mukubwa. Watu waliokuwa ndani ya mashua walifikiri mashua itazama. Kila
mutu alianza kuomba mungu wako! Hakose ataona linalotendeka na kutusaidia.

Maelezo kwa mwalimu:


Mungu akapatia watu wake aliyowachagua sheria kamili. Sheria yake ya kwanza ni: “Hautakuwa na
miungu mingine mbele yangu.” Sheria ya pili ni “Hautajifanyia sanamu ya kuchongwa …” (Tazama
Kutoka 20:1-4). Bila kuchoka, Bwana alirudilia sheria hizi. Wakati watu wake walimutii, walishiriki
baraka zake. Lakini wasipomutii, kasirani yake iliwaka juu yao (2 Mambo ya Siku 28:25). Lakini
Mungu hakasiriki siku zote (Zaburi 103:9). Alisamehe wale waliorudi kwake kwa kweli.
CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 9
Muda wa utawala za wafalme, taifa la Mungu halikutii Mungu. Sababu ya upendo wake, Mungu
alituma manabii wengi kwa kuwaagiza. Manabii walifanya Mambo ya Siku mengi kinyume na
maagizo ya taifa juu ya vinyume vya zambi. Mara kwa mara walisema juu ya Mambo ya Siku
yatakayokuja. Unabii zingine zilitimilika. Katika somo hili, Mika anasema juu ya jinsi Samaria
utakuwa: “maziwa mengi.” Unabii huu ulitimilika muda wa utawala wa mufalme (Ahazi) Yuda.
“Mufalme wa Asuria alizunguka inchi yote na kushinda Samaria, aliukamata muda wa miaka mitatu”
(2 Wafalme 17:5). Kisha, Waasuria walikamata Israeli yote na kupeleka Waisraeli kama watumwa
kule Asuria.

Yote Mungu anayoisema inatimilika, itatimilika. Anakuwa na uwezo wote na atachunga Neno lake
bila uchafu. Kfundisha Neno la Mungu na uhakika na ulazima.

Onyesha taswira kwa jalada ya nyuma: Yona akaagiza: “Munitupe inje ya mashua!” Watu waliokuwa
ndani wakatii na Yona akatupwa ndani ya maji. Mungu alituma samaki kubwa iliyomeza Yona. Muda wa
muchana tatu na usiku tatu, Yona alikuwa ndani ya tumbo ya samaki. Kwa mwisho, Yona aliomba Bwana na
Mungu alimujibu.
Onyesha taswira ndani ya jalada: Mungu akaagiza samaki kutapika Yona kwenda udongo kavu na
samaki ilitii. Mungu akasema tena kwa Yona: “Uende Ninawe, uape ujumbe ninayokupa.” Kwa wakati ule
Yona alitii Bwana. Pale Ninawe alitabiri ujumbe wa Mungu: “Nyuma ya siku 40 Ninawe utaharibiwa.” Katika
muji huu mukubwa Yona alieleza unabii ule ule mara kwa mara.
Wakati habari zilifikia mufalme, alitosha nguo yake ya kifalme. Alivaa gunia (vazi nzito ya kutengeneza
gunia), akakaa katika vumbi, mufalme akahakikisha kama alifanya zambi. Mufalme akaagiza: “Watu wote
walililia Mungu, kama wanaacha njia zao mbaya na jeuri yao. Hakose Mungu atatusamehe na kwa hiyo
hatutaaongamia tena.”
Mungu aliona kama watu wake waitubu zambi zao. Aliwasamehe mara moja na hakuangamiza tena muji
wao. Tendo hili likaletea Yona huzuni. Mungu angaliharibu Ninawe sawa vile alivyotabiri. Yona aliazibiwa
juu ya kutokutii kwake. Alitaka watu wa Ninawe waazibiwe juu ya uovu wao. Yona akasahau kama watu wa
Ninawe walitubu zambi zao.
Mungu muzima wa mbinguni ana uwezo wote. Anaweza kutuma upepo mukubwa. Anaweza kutayarisha
samaki kubwa kwa kumeza mutu. Anaweza kuita mara ya pili nabii asiyetii. Anaweza kusamehe watu waovu
wanaomurudi. Mungu anaamuru kila siku.

2. Mungu anaweza kufanya kila kitu (1 Wafalme 16:5-6; 2 Mambo ya Siku 28:5-8; 16-19).

Mungu ana uwezo juu ya manabii sawa Yona. Ana uwezo juu ya wafalme sawa Azaria wa Yuda. Azaria
alikuwa mufalme muzuri kwa mwanzo, aliweza kufanya hakose Mambo ya Siku yote. Lakini alifundishwa
kama kulikuwa kitu ambacho hangeweza kufanya. Aliingia na kiburi katika pahali patakatifu katika hekalu.
Makuhani tu ndio waliingia. Lakini mufalme Azaria mwenye kiburi aliingia pahali patakatifu, tayari kuchoma
uvumba. Makuhani walipima kumukataza lakini mufalme Azaria hakusikia. Mara moja katika hekalu, Mungu
alimuazibu na ukoma wa ajabu.
Mwana wa Azari (Yotamu) akawa na “alifanya wema machoni mwa Mungu.” Ukoma wa baba yake
ulimukumbusha azabu ya Mungu juu ya kiburi. Mwana wa Azaria akawa na nguvu sababu alitii Mungu.
Nyuma ya kufa kwa mwana wa Azaria, mujukuu wa Azaria, Ahazi akawa mufalme wa Yuda. Sawa vile
baba yake na tati yake, Ahazi alikuwa wa nyumba ya Daudi. Lakini mufalme Ahazi hakufanana na mufalme
Daudi. Ahazi hakufanya yaliyo mema machoni mwa Mungu. (Tazama 2 Wafalme 16:2-4; 2 Mambo ya Siku
28:1-4) Alifanya miungu na kuiabudu. Alitoa hata sadaka watoto wake. Mufalme Ahazi hakufanya angalisho
kwa Mungu wa kweli anayeishi mbinguni. Na taifa la Yuda lilifuata mufano wa mufalme wake. Mungu alijua
yale mufalme Ahazi alifanya? (Kuhusu wanafunzi watoe mawazo yao). Mungu aliweza kufanya kila kitu
kuhusu Ahazi na Yuda? Kama kawaida, aliweza. Anayeweza yote anaweza kufanya yote.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 10


Mungu aliweka mufalme Ahazi na Yuda katika mikono ya wafalme wa Suria na Israeli (Tazama 2 Mambo
ya Siku 28:5).
Onyesha taswira 10: Mungu aliahidi kwa majeshi jirani, ya Suria na Israeli (ufalme wa kaskazini)
kupiganisha Yuda (Ufalme wa kusini). Kwa siku ile waaskari 120.000 shuja wa Yuda wakakufa. Na 200.000
ya wanaume, wanawake na watoto wakakamatwa na kupelekwa sawa watuMwanzo Sababu gani Yuda
ilizarauliwa sana? “Kwa sababu Yuda waliacha Bwana Mungu.” (Tazama 2 Mambo ya Siku 28:6). Tungeweza
kusema kwa mufalme Ahazi maneno ya aya yetu. (Wanafunzi warudilie: Yoeli 2:13).

3. Mungu anakuwa na uwezo wa kuchunga taifa lake (2 Mambo ya Siku 28:8-15; Isaya 7:7-9)

Mufalme Ahazi na watu walikuwa na woga na waliyumbayumba sawa miti wa upepo (Tazama Isaya 7:12).
Mungu akatuma nabii Isaya kwa kusema na mufalme Ahazi: “Uwe mwangalifu” Isaya akaanza: “Tulia,
Usiogope”. Wafalme hawa, wa Israeli na Suria walipanga kuharibu. Wakasema: “Tutakata Yuda vipande na
kugawanyana. Tutaondoa Ahazi na kuweka mutu wetu juu ya kiti cha ufalme.” (Tazama Isaya 7:36)
Kisha Isaya alipana Habari njema. “Lakini Mungu akasema yale haitatokea.” Mungu ana uwezo wote.
Anaweza kuchunga watu wake. Hataruhusu mufalme wa inchi ingine kuketi juu ya kiti cha ufalme wa Yuda.
Onyesha taswira 11: Bwana aliahidi kuchunga kiti cha ufalme cha Daudi katika mikono yake. Mungu
hataruhusu ufalme uondoshwe katika nyumba ya Daudi. Ahazi alikuwa muovu, lakini alikuwa wa nyumba ya
Daudi. Na Mungu atachunga ahadi yake mpaka Daudi (Tazama 2 Samweli 7:116-16).
Mufalme Ahazia alifurahi juu ya habari njema kwa Yuda. Lakini alipenda miungu kuliko Mungu.

4. Mungu ni muweza yote


(2 Wafalme 16:7-19; 2 Mambo ya Siku 28: 20-25; Isaya 7:10-12; Mika 1:1-7:20)

Muda ulifika (Wakati mufalme Ahazi alihitaji musaada). Aliweza kutubu zambi zake na kurudi kwa Mungu.
Mungu muweza yote anakuwa na uwezo wote. Aliweza kusaidia Ahazi. Mufalme Ahazi aligeukia kwa
mufalme wa Asuria. (Nabii Yona alihubiri katika Ninawe muji mukuu wa Asuria).
Mufalme Ahazi aliingia katika hekalu takati ya Mungu. Akatoa katika hazina ya Mungu vitu na kuvituma
kwa mufalme wa Asuria, (Angalia 2 Wafalme 16:7-8), “Kuja unisaidie!” Ahazi akasihi mufalme wa Asuria.
Kuliko kutafuta musaada, mufalme Ahazi akachanganikiwa (Tazama 2 Mambo ya Siku 28:20). Muda wa
magumu yake: “Mufalme Ahazi akawa muovu sana mbele ya Bwana.” (Tazama 2 Mambo ya Siku 28:22) Fikiri
kuhusu ile!.
Kisha mufalme Ahzai akatembelea Damasiki muji jirani. (Onyesha taswira). Pale akaona mazabahu ya
kipagani. Ahazi alitaka moja inayofanana na ile na hata kupata moja sawa na ile. Akaitumia kuhani wa hekalu
takatifu la Mungu pa Yerusalema. “Unifanyie mazabahu sawa na hii.” Ahazi akaamuru. Na kuhani ambae
Mungu alichagua aliwekwa wakfu kwake, akatii mufalme mwenye zambi.
Mufalme Ahazi akaondoa mazabahu ya Mungu hekaluni. “Tangu sasa” Ahazi akasema kwa kuhani.
“Tumia mazabahu haya mapya”, Mufame Ahazi alifanya mengine mabadirika katika hekalu la Mungu.
Alifanya haya yote kwa kufurahisha mufalme wa Asuria (Tazama 2 Wafalme 16:17-18).
Kwa mwisho Ahazi alifunga hekalu la Mungu. Akajifanyia yeye mwenyewe mazabahu kila mahali katika
Yerusalema. Katika kila muji wa Yuda, alijenga fasi kubwa. Katika mahali pale, watu wa yuda waliteketeza
sadaka kwa miungu mingine. Mufalme aliongoza kuhani na watu mbali na Mungu muzima. Kwa hiyo
mufalme Ahazi akakasirisha Mungu! (Tazama 2 Mambo ya Siku 28:25).
Mungu, Muweza yote, angeliazibu mara moja mufalme Ahazi. Lakini alituma mwengine nabii kuonya
mufalme. Mika akaanza: “Sikiliza, ee watu wote! Sikiliza ee dunia, na wote wanaoishi duniani. Bwana
ataazibu Samaria, Israeli yote, Yerusalema na Yuda yote!” Bwana anasema: “Nitashusha Samaria kama vipande
vya majiwe. Miungu yake yote itavunjwa vipande vipande (Tazama Mika 1:3; 3:7). Mimi Mungu mitatuma
musiba Yerusalema. Watoto munaowapenda watapelekwa utumwani katika inchi ingine (Tazama Mika 1:12-
16).

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 11


Mika akaambia watu: “Muko na tamaa, muko na pupa (mukipenda kitu cha wengine kiwe chenu). Ona lile
Mungu anasema: “Nilipanga kukuletea musiba wewe taifa langu. Hautaweza kujiokoa wewe mwenyewe”
(Amosi 2:1-3).
Nabii akasema na nguvu kwa viongozi wa taifa “Munachukia mema na kupenda mabaya. Sababu yenu,
Yerusalema utakuwa kipande cha majiwe” (Tazama Mika 3:1-12). Uzuri wake utaharibiwa. Sababu gani?
Sababu mufalme na watu waliacha Mungu wao muzima. Na Mungu alikasirika sana.
Onyesha taswira 12: Nabii alaongeza haraka habari njema: “Katika siku za mwisho, mulima wa Bwana
utatengenezwa … watu watarudi humo. Mataifa mengi watakuja na kusema: “Muje, tuende mulimani mwa
Mungu, nyumbani mwa Mungu … Atatufundisha njia zake kusudi tuweze kutembea katika njia zake.” Neno la
Mungu litatoka Yerusalema. Hakutakuwa vita. Mungu muweza yote alisema. Tutatembea kwa jina la
Mwenyezi Mungu wetu milele na milele.”(Tazama Mika 4:1-5). “Siku hizi za mwisho” ambazo Mungu
anasema hazijatimia bado. Lakini kila kitu kitatimia kwa wakati wake. Maana yeye ni Mwenyezi Mungu.
Bwana alikuwa na habari njema nyingi. Mika akahubiri juu ya Betelehemu, muji ambao mufalme Daudi
alizaliwa. Akasema: “Wewe Betelehemu, mudogo katika Yuda. Lakini ndani mwako mutatoka mufalme
atakayetawala juu ya Israeli. Ufalme wake ni wa milele.” Mufalme Ahazi hakupenda kusikia unabii ule.
Lakini sisi tunaweza sababu nusu yake imekwisha kutimilika. Mungu alisema kama Mwana wake wa milele
atazaliwa Betelehemu. Mwana wa Mungu, Bwana Yesu alikuwa wa pamoja na Mungu siku zote. Mika
akatabiri kama atatokea Betelehemu.
Yesu akakuja (miaka 700 nyuma) lakini watu hawakupomukea kama mufalme. Kisha wakamuua Yesu
hakubaki anakufa. Alifufuka na kuenda mbinguni. Muda atakuja wakati Bwana Yesu atatawala hapa duniani.
Kisha kwa muda wa Mungu, unabii unaobaki utatimilika.
Watu wa Mungu wakaanza kufahamu namna gani Mungu ni mwema na jinsi walikuwa wenye zambi.
Walitaka kusamehewa. Wakaomba! “Mungu atakubali elfu za kondoo dume? Ao uwingi wa mafuta?
Atakubali muzaliwa wa kwanza kama sadaka? Hapana! Mungu hahitaji sadaka zile juu ya zambi zao.
Anataka utii. Anasema: “Muache zambi, mufuate haki. Penda juruma. Tembea na unyenyekevu pamoja na
Mungu wako” (Tazama Mika 6:1-8).
Kwa wakati wa Mika Mungu alitaka watu wake watumikishe haki. Atawasaidia yeye mwenyewe. Lakini
hatukaze kutumikisha haki: Mungu hakukaza mufalme Azaria, Yona ao mufalme Ahazi kutumia haki. Lakini
aliwaazibu juu ya matendo yao mabaya.
Bwana anataka vilevile watu watembee mbele yake k wa unyenyekevu, hapana ona kiburi. Hata kama
tunakuwa nayo ao munakuwa nayo, tunapashwa kuwa wanyenyekevu mbele ya Mwenyezi Mungu. Unataka
kumuomba akusaidie kutumia haki kwa kumutii? Kumbuka kama Mungu anaweza yote sababu yeye ni
Mwenyezi.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 12


Biblia AK Kitabu 25

SOMO 4 – MUNGU NI MUTAKATIFU

Kwa mwalimu kujifunza mbele: 2 Wafalme 17:1-14; Osea 4: 1-14:2

Shabaa ya somo: Kuonyesha kama wale wanaoasi Mungu wataazibiwa.


Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kujua: Kama kila kitu kinachokuwa kwa nafasi ya Mungu
(nafasi ya kwanza) katika maisha yao kinaweza kuwa sanamu.
Yale ambayo wanafunzi wako wangelipaswa kufanya: Mugeukie Mungu Mutakatifu na kuacha miungu.

Somo kwa kifupi: (kuandika ndani ya buku ya mwalimu na za wanafunzi.)


1. Mungu ni (Yoeli 2:13; Osea 4:1-2; 11:1-8; 13:16; 14:12)
2. Mungu ni wa rehema (2 Wafalme 17:4-6)
3. Mungu hakasirike haraka (2 Wafalme 17:7-23)
4. Mungu ni mwema (2 Wafalme 17:24-41)

Shairi la kujua kwa ufahamu: “… geukeni kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa mwenye neema yeye,
anayeja na huruma, si mwepesi kwa kukasirika na mwenye rehema nyingi, mwenye kujuta yale mabaya (Yoeli
2:13).

Somo: Mungu mumoja na wa kweli anayeishi mbinguni ni “Mutakatifu” ni kusema, yeye ni bila kosa, tofauti
na wengine wote. Ni mwenye haki na anatumia haki. Ni Mutakatifu bila zambi.
Kumepita miaka mingi Mungu Mutakatifu, alichagua jamaa moja kwa ajili yake mwenyewe. Aliwachagulia
inchi vilevile. Kwa wakati ule jamaa ilikaa katika inchi ya Mungu. Baba wa jamaa alikuwa Yakobo ambaye
jina lake lilibadirishwa na Mungu kuwa Israeli (Mwanzo 32:28). Kwa hiyo inchi ya watu wa Mungu iliitwa
Israeli, Miaka mingi nyuma, taifa nzuri la Mungu liligawanywa sababu ya zambi ya mufalme Solomono.
Sehemu ndogo sana ya kusini ya taifa iliitwa Yuda. (Ilikuwa jina la kabila yake kubwa). Sehemu kubwa zaidi
ile ya kaskazini ilibaki na jina la Israeli (Tazama tena volume 23, somo la tatu).
Yeroboamu alikuwa mufalme wa kwanza wa Israeli, ufalme wa kaskazini. Sababu mufalme Yeroboamu
alikuwa muovu hata kuweka sanamu katika inchi, akaamuru: “Muziabudu.” Kwa hiyo watu wakaenda mbali
na Mungu kwa kuabudu sanamu za zahabu za mwana wa ngombe. Kwa mwisho Yeroboamu alijulikana kama:
“Mufalme aliyefundisha Israeli zambi” (Tazama kwa mufano 1 Wafalme 12:28-32; 2 Wafalme 13:6,11; 14:24;
15:9; 18:24,28). Ushuhuda gani mubaya! Kila mufalme wa Israeli aliyekuja nyuma ya Yeroboamu alikuwa
mwenye zambi vilevile.

1. Mungu ni mwenye neema (Yoeli 2:13; Osea 4:1-2; 11:1-8; 13:16; 14:1-2)

Mungu anapenda watu wake sana vile sehemu mbili za taifa. Israeli na Yuda. Kwa hiyo wakati walifanya
zambi, Mungu alituma manabii kwa kuwaonya. Nabii Yaoeli akataja maneno ya aya yetu kwa watu wa Yuda.
Akasema: “Geukeni kwa Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa mwenye neema yeye, anayejaa na huruma, si
mwepesi kwa kukasirika na mwenye rehema nyingi, mwenye kujuta yale mabaya.” (Yoeli 2:13).
“Mungu ni mwenye neema”, Yoeli anasema. Maana Yake, Mungu anaonyesha neema, hata kwa wale
wasiostahili. Mungu ni mwenye haki vilevile. Anayekuwa mutakatifu ndiye anapashwa kuazibu wanaofanya
zambi.
Mungu alituma nabii Hosea k wa watu wa Israeli. “Musikie Neno la Mungu, ninyi Waisraeli!” Hosea
akasema: “Mungu anawashitaki ninyi: Hakuna ukweli na rehema. Hamukubali kama Mungu ni Bwana wenu.
Munaapa, kusema uwongo, kuiba na kufanya uzinifu” (Tazama Hosea 4:1-2).

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 13


Watu wa Mungu waliasi sheria hizi tano kati ya sheria kumi. Mungu alitoa sheria hizi wakati alichagua
kuanza Israeli kwa ajili yake yeye mwenyewe. (Tazama Kutoka 1:27). Kwa hiyo taifa lake waliendelea
kufahamu sheria hizi:
Onyesha taswira 13: Mungu akasema kwa watu wake kwa upendo kupitia Hosea: “Wakati Israeli alikuwa
mutoto, nilimupenda … nilifundisha Waisraeli kutembelea nikiwakamatia ku mikono … niliwaongoza katika
wema na upendo” (Tazama Hosea 11:1,3-4). Kama vile baba anapenda mwana wake, ni vile Mungu alipenda
watu wake. Aliwapa sheria kusudi wajue namna kuishi. Aliwapenda, kuwafundisha, kuwalisha. Lakini kwa
uchungu, Mungu alipashwa kusema: “watu wangu wanajitahidi kwenda mbali nami. Namna gani ninaweza
kuwaacha?” (Tazama Hosea 11:7-8).
Kwa mwisho Mungu anasema kupitia nabii wake: “Watu waliasi Mungu. Wataangushwa na upangu,
watoto wao wataangamizwa” (Tazama Hosea13:16) “Ee Israeli, rudi kwa bwana, Mungu wako. Munaanguka
na zambi zenu. Rudi kwa Bwana. Umwambie: “Ondoa uwovu wetu na utupokee kwa huruma” Tazama Hosea
14:1-2).

Maelezo kwa mwalimu:


Kupitia mafundisho haya, mukazo uliwekwa juu ya Bwana Mungu. Wanafunzi wako wanaweza
kupata magumu ya kukumbuka Mambo ya Siku yote kuhusu historia na unabii. Lakini fundisha na
mwangaza huu kama tabia za Mungu zitaendelea kubaki pamoja nao.

“Mungu ni Mutakatifu.” Maana yake, Yeye ni tofauti na wengine wote. Yeye ni bila zambi. Yeye ni
haki na anaendelea kufanya haki. Yeye ni Mutakatifu bila hata zambi moja (Tazama Kutoka 15: 11,
Lawi 19:2, Hab. 1:13; Ufu. 4:8). Kwa kawaida, hatuwezi hata siku moja kuwa atakatifu sawa Mungu
alivyo, ndio maana, Mungu anatuagiza kuishi maisha ya utakaso (1 Pet. 1:15-16). Fanya ile iwe wazo
kubwa la somo yako.

Kitu kinachotuongoza katika somo hili ni maneno ine ya Yoeli 2:13 aya yetu ya kufahamu. Chunga
kweli za haya hii mbele ya wanafunzi wako: Uwasaidie kuitaja kila mara katika siku za kuja.

Katika matayarisho ya kufundisha somo hili, fikiri sana juu kitabu cha Hosea. Alikuwa nabii. Alisikia
uchungu moyoni. Muke wake hakuwa mwaminifu. Kwa hiyo Hosea alifahamu kama Mungu
alivunjika moyo sababu ya kutokuwa mwaminifu kwa Israeli. Mwalimu, moyo wako ushikwe na
mahitaji ya kiroho ya wanafunzi wako. Fundisha na upendo wa neema.

Katika Hosea, Efuraimu imeandikwa mara 30. Efuraimu ilikuwa moja ya makabila makubwa ya Israeli na
jina hili linatumiwa kwa kutaja Israeli. Kwa mwisho wa utumishi wake wa unabii, Hosea alisihi watu wa Israeli.
Akasema: “Ee Israeli, rudi kwa Bwana Mungu wako. Zambi zako zilikuangusha … rudi kwa Bwana.
Umuambie : “Samehe zambi zetu zote, utupokee kwa rehema. Asuria haiwezi kutusaidia. Hatutasemaka tena
juu ya vitu vilivyotengenezwa na mikono ya watu kama Mungu wetu.” (Tazama Hosea 14:1-3)
Kusihi kwa (Hosea hakukubaliwa. Lakini siku moja (tena kwa wakati ujao), Israeli watarudilia Bwana.
Kufuatana na Hosea, Mungu atasema sasa: “Nitasamehe zambi zao na mitawapenda” (Tazama Hosea 14:4).
Mungu alikuwa hajamaliza na Israeli.

2. Mungu ni mwenye rehema (2 Wafalme 17:1-6)

Wakati ulifika ambapo Waisraeli walikuwa na woga. Asuria (400.000 wa kaskazini – mashariki, Onyesha
taswira). Walipata inchi nyuma ya kushinda ingine. Mufalme wa Asuria alienda polepole pamoja na jeshi lake
kwenda Israeli. Kwa mwisho mufalme wa Israeli akawa mutumishi wa mufalme wa Asuria.
Mufalme wa Israeli akaambia watu “Tunahitaji mali mingi kupatia ,mufalme wa Asuria.” Kwa hiyo
Waisraeli walilipa na kulipa tena mufalme wa Asuria. Kwa mwisho, hawakulipa. Kwa hiyo mufalme wa
Asuria alikusudia kama Waisraeli walikuwa biashara.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 14


Onyesha taswira 14a (chunga 14b usionekane): Mufalme wa Asuria akatupa mufalme wa Israeli
gerezani. Kisha, Jeshi la Waasuria likatembea juu ya taifia lote la Israeli. Walishambulia Samaria, muji
mukuu na kuupiganisha muda wa miakia mitatu. Kwa mwisho, Waasuria walikamata Samaria na Waisraeli.
Waisraeli walitembea fasi nyingi za Asuria, mbali sana na inchi yao.
Mungu aliruhusu Waisraeli wauwawe. Lakini aliye mutakatifu na mwenye neema ni mwenye rehema
vilevile. Ni kusema kama yeye ni mwema kwa wale wasiostahili. Mbele sans Mungu akaambia watu wake:
“Kama hamukutii Bwana Mungu wenu, Mungu atawaacha kuangamizwa na adui zenu. Miili yenu ya kufa
itakuwa chakula cha ndege za anga na nyama za duniani (Tazama kumbukumbu 28:15,26). Ndio maana,
Mungu alikuwa mwenye rehema kwa Israeli katika siku zile. Hakuiruhusu, lakini aliwaacha kupelekwa Asuria.
Miaka mingi mbele, Mungu alituma Yona kuhubiri katika muji mukuu wa Asuria. Na waasuria walienda mbali
na Mungu. Hakose sasa, Waisraeli watarudilia Mungu.
Ni ajabu kuona watu wa Mungu kupelekwa sawa watumwa wa vita. Kila mumoja wao alikuwa kama ndege
na bawa moja imevunjwa, ukiruka juu ya udongo.
Onyesha taswira 14b: Lakini kupitia nabii Hosea, Mungu anasema: “Ninyi ni wangu kwa hali maalumu.
Muko na huruma yangu pamoja na rehema.” (Tazama Hosea 2:19). Watu wa Mungu walikuwa mukononi
mwake, hata kama walikuwa wafungwa wa Asuria. Mungu Mutakatifu ni mwenye rehema.

3. Mungu Hakasirike haraka (2 Wafalme 17:7-23)

Katika Neno la Mungu, anasema waziwazi sababu gani aliazibu Waisraeli, (Mwalimu: Kufuatana na miaka
ya wanafunzi wako, soma 2 Wafalme 17:9-12).
Angalia lole Mungu mwenyewe anasema: “Ninaazibu Waisraeli sababu waliabudu miungu mingine.
Walifuata mataifa walioishi inchini humu mbele. Waisraeli walijifanya waovu mbele ya Mungu. Walikuwa na
sanamu juu ya kila mulima na chini ya miti mikubwa. Walichoma uvumba kwa sanamu, wakaziita miungu na
kuniletea kasirani. Niliwakataza kuabudu miungu. Lakini hawakusikia. Hawakutii sheria zangu.
Onyesha taswira 15: Mungu anasema zaidi kwa watu wake kuhusu zambi: “Niliwapatia sheria zangu
(ziliandikwa juu ya gombo). Na nilituma manabii na ujumbe wangu. Lakini hawakusikia. Hawakunitii.
Walienda mbali na sheria zangu. Walijifanyia wao wenyewe sanamu mbili kwa namna ya ndama (wana wa
ngombe). Walijiinama mbele ya nyota. Waliabudu Bali. Walitoa wana na binti zao kuunguzwa motoni. Kwa
hiyo nilikasirika sana juu ya Israeli (Tazama 2 Wafalme 17:13-18).
Mungu akatuma haraka nabii wake Hosea, kwa kuonya Israeli, akasema kwa jina la Mungu, Hosea
akasema: Waisraeli wanajifanyia sanamu ya zahabu na feza yao. Ee Israeli. Tupa ndama ya zahabu! “Kasirani
yangu inawaka juu yako. Ndama hiyo ilitengenezwa na mwanadamu, haiko Mungu.” (Tazama Hosea 8:4-6).
Kuabudu sanamu muda wa siku moja inaletea Mungu kasirani kubwa. Lakini Israeli aliabudu sanamu zao
za ndama siku 10 … siku 50 … siku 100 … miaka 10 … miaka 50 … miaka 100 … siku 150 miaka 2000. sawa
vile nabii Yoeli alivyosema hakika katika aya yetu: “Mungu si mwepesi kukasirika”
Kwa hiyo, kwa mwisho Mungu hakutaka watu wake waendelee kufanya zambi. Ndiyo maana, akatuma
Waisraeli mbali na “Uwezo kake” Aliacha adui zao kuwashika na kuwapeleka Waisraeli Asuria. (Onyesha
Taswira). Kule waliishi katikati ya maadui. Mungu si mwepesi kukasirika. Kwa sababu yeye ni Mutkatifu hata
hawezi kuacha zambi bila kuziazibu. Alipashwa kuazibu watu wake.
Kwa hiyo taifa la Israeli waliondoshwa katika inchi yao nzuri. Siku gani ya kutisha kwa watu maalumu wa
Mungu.

4. Mungu ni mwema (2 Wafalme 17:24-41)

Israeli, Inchi ambayo Mungu alichagua kwa ajili ya watu wake, ilikuwa sasa ya Asuria. Kwa hiyo mufalme
wa Asuria alituma watu wake wengi kuishi Israeli. Waasuria hawakuabudu Mungu mumoja wa kweli anayeishi
mbinguni. Walipeleka miungu yao waliyoomba huko Israeli. Kwa hiyo Mungu alituma simba wamoja
waliouwa Waasuria.
Waasuria waliobaki wakasema kwa mufalme haraka sana: “Watu uliotuma kuishi Israeli hawajue kitu gani
Mungu wa inchi hii anaomba. Alituma simba ambao wanaharibu inchi yetu.”
CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 15
Mufalme wa Asuria akaagiza kwa mumoja wa watu wake: “Tafuta kuhani mumoja aliyetoka Israeli.
Umutume Israeli. Anapashwa kuishi kule na kufundisha watu lile Mungu wa Inchi anahitaji.
Onyesha taswira 16: Kwa hiyo, mumoja wa makuhani wa Mungu alienda kuishi Betheli: Munakumbuka
kitu mufalme Yeroboamu alitiaka Betheli, mbele ya zaidi ya miaka 200? (Moja ya ndama za zahabu ambazo
Waisraeli waliabudu). Sasa kuhani alifundisha watu namna gani kuabudu Mungu (Tazama 2 Wafalme 17:28).
Mungu ni upendo na ni mwema. Alitaka Waasuria waweze kumujua. Kwa siku Waasuria walitimiza
mipango ya kuabudu Mungu. Lakini hawakumugeukia kikamilifu. Wale wanaomupenda Mungu
wanamuabudu yeye mwenyewe. Waasuria walipima kuabudu Mungu, lakini waliabudu miungu vilevile.
Kuhani la Mungu alipima kuwafundisha Waasuria sheria ya kwanza ya Mungu: “Hautakuwa ma mungu
mwingine ila mimi tu. Hautajifanyia sanamu ya kuchongwa, ao kitu kinachofanana na kitu kinachokuwa juu
mbinguni ao chini duniani, ao kilicho majini chini ya dunia. Hautajiinama mbele yao na hautawatumikia”
(tazama kutoka 20:4-5). Waasuria walisikia. Lakini hawakutii sheria za Mungu (Tazama 2 Wafalme 17:34).
Leo, Mungu anataka wewe na mimi tumuabudu yeye mwenyewe tu. Unakuwa na miungu inayokamata
nafasi ya upendo wa Mungu? Hauhitaji kuomba kitu fulani kwa kumuabudu. Sanamu ni kila kitu kinachokuw
cha lazima kwako kuliko Mungu, inaweza kuwa mali, wa rafiki ao “kutaka kuwa wa kwanza.” Kitu gni ni cha
lazima katika maisha yako? Kama si Mungu, maana yake unakuwa na sanamu.
Unataka kusema na Mungu saa hii kuhusu sanamu yako? Yeye ni upendo na anataka kukusamehe.
Umuambie kama unataka kumuabudu yeye mwenyewe. (Mwalimu: Tumia 1 Yoane 5:21).

Mwalimu!! Tafazali soma haya

Fuata utaratibu wa vitabu utakapotumia mifululizo ya ufahanuzi wa Biblia. Kwa hiyo fungu (volume) 24,25
na 26 za Agano la Kale zinafundisha kwa kufuatana. Chunguza daftari ifuataYona Mara moja utafahamu
lazima ya manabii wadogo kenda katika fungu hizi.

Utaratibu wa Mambo ya Siku ya Agano la Kale

Namna vitabu vya Agano la Kale vilipangwa haikufuata utaratibu muzuri kufuatana na Mambo ya Siku
yaliyotendeka. Daftari hii inaonyesha vitabu gani vilivyotumiwa karibuni katika muda mumoja.

Mwanzo Yobu
Kutoka Walawi
Hesabu
Yoshua
Waamuzi Ruta
1 Samueli
2 Samueli Zaburi
1 Wafalme 1 Mambo ya Siku, Wimbo wa Solomono, Mezali, Muhubiri
2 Wafalme 2 Mambo ya Siku, Obadia, Yoeli, Yona, Amosi, Hosea, Mika, Isaya, Nahumu, Zefania,
Habakuki, Yeremia, Maombolezo.
Danieli Ezekieli
Ezra Esteri, Hagai, Zakaria
Nehemia Malaki

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 16


VITABU VYA MANABII

Kitabu Mwaka Contexte Wafalme (Nord & Sud


Ecriture
Mbele ya uhamisho Obadia 840 2 Wafalme 8:12 Yoramu, Ahazia, Atalia, Yoasi (Sud) Hukumu juu ya Edomu
Yoeli 835 2 Wafalme 12 Yaosi (5) Pigo ya nzige
Yona 760 2 Wafalme 14 Ninawe, toba
Amosi 755 2 Wafalme 14 Yeroboamu 2 (N) Vidonda vya watu
Hosea 710 2 Wafalme 14-17 Yeroboamu2, Zakaria, Salumu, Menahemu, Upendo maoni ya Mungu
Pekahia, Peka, Hoshea
Isaya 740-612 2 Wafalme 15-21 Yotamu, Ahazi, Ezekia, Manase Wokovu wa Masia
Mika 700 2 Wafalme 15-20 Yotamu, Ahazi, Ezekia (S) Uharibifu na wokovu
Nahumu 663-612 2 Wafalme 21-23 Manase, Amoni, Yoasi (S) Uharibifu wa Ninawe
Zefania 625 2 Wafalme 22-23 Yosia (S) Hukumu juu Yuda
Habakuki 607 2 Wafalme 22-24 Yosia,Yohazi, Yoyakimu (S) Utumwa wa Babiloni
Yeremia 627-585 Yosia,Yohazi, Yoyakimu, Zedekia (S), Hukumu juu ya kuanguka tena
Nebukadeneza wa Babiloni
Wakati wa Maombolezo 586-585 2 Wafalme 25 Nabukadeneza Kilio juu ya uharibifu wa
uhamisho Yerusalema na hekalu
Ezekieli 592-570 2 Wafalme 24-25 Zedekia (S) Mungu anachunga Agano lake
Danieli 537 2 Wafalme 23-25 Yoyakimu (S) Neb ukadeneza, Belsasari, Dario, Mupango wa Mungu kwa siku
Ezra 1-4 Kiro zijazo.
Nyuma ya Hagai 320 Ezra 5-6 Zerubali, Dario 1 Kujenga tena hekalu
uhamisho Zakaria 520-518 Ezra 5-6 Zerubali, Dario 1, Artasasta Tumaini katika kurudi kwa Kristo
Malaki 450-400 Nehemia 13 Artasasta, Dario2 Mashitaki ya Mungu juu ya Israeli.

CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 17


CONGO SWAHILI OT VOLUME 25 – P. 18

You might also like