Professional Documents
Culture Documents
HAYA NDIYO QUR'an IMENIFUNZA-Qur'an Na Uthibitisho Wa Sayansi Ya Karne Ya Ishirini Na Moja
HAYA NDIYO QUR'an IMENIFUNZA-Qur'an Na Uthibitisho Wa Sayansi Ya Karne Ya Ishirini Na Moja
HAYA NDIYO QUR'an IMENIFUNZA-Qur'an Na Uthibitisho Wa Sayansi Ya Karne Ya Ishirini Na Moja
IMENIFUNZA:
(Toleo la Pili)
IbnuRajab Allhassany
1
HAYA NDIYO QUR‟AN IMENIFUNZA:
(Toleo la Pili)
Qur‟an na Uthibitisho wa Sayansi, Teknolojia na Gunduzi
za karne ya Ishirini na moja
ISBN: 978-9912-40-528-8
Kimerejelewa na:
Shaykh Mohamed Abbas,
Mkurugenzi,
African Muslim Agency,
Tawi la Tanga.
Mpiga chapa:
Truth Printing Service
geofreymakula@gmail.com
Ubungo, Dar es Salam, Tanzania.
2
UFUNGUO WA KITABU
3
YALIYOMO:
UFUNGUO WA KITABU............................................................................................... 3
KUHUSU KITABU: .................................................................................................... 6
MAKOSA YA CHAPA NA UANDISHI: ...................................................................... 7
DIBAJI ....................................................................................................................... 8
SHUKRANI............................................................................................................... 10
UTANGULIZI ........................................................................................................... 12
HISTORIA YA KUSHUSHWA KWA QUR‘AN TUKUFU......................................... 16
JE! QUR‘AN IMEPITWA NA WAKATI AU IPO MBELE YA WAKATI .................. 20
UTHIBITISHO NDANI YA QUR‘AN ....................................................................... 21
Qur‘an na Sayansi, Teknolojia na Teknohama .............................................. 22
Qur‘an na Asili ya Ulimwengu (The Big Bang Theory) ............................. 24
Qur‘an na Sayansi ya Anga (Astrology)...................................................... 26
Qur‘an na Uhusiano wa Wakati (Time Relativity) ..................................... 29
Qur‘an na Sayansi ya safari za anga za mbali (Space Travelling) .......... 33
Qur‘an na Sayansi ya asili na maendeleo ya kukuwa kwa Mwanadamu
(Embryolojia) .................................................................................................. 43
Qur‘an na Kalenda (Moon and Solar Calenders) ....................................... 56
Qur‘an na Nguvu ya mvutano (Force of Gravity)...................................... 58
Qur‘an na Kemia ya Mmenyuko (Kutu/Rust) ............................................. 74
Qur‘an na Sayansi ya Milima ........................................................................ 78
Qur‘an na Gunduzi za vyanzo vya Moto ..................................................... 83
Qur‘an na Sayansi Anatomia ya Viumbe .................................................... 85
Qur‘an na Sayansi ya Bahari (Oceanography) .......................................... 91
Qur‘an na Sayansi ya Hyndrolojia (Mzunguko wa Maji) ........................ 101
Qur‘an na Sayansi ya Alama za Vidole ..................................................... 105
Qur‘an na sababu za makatazo ya muziki ............................................... 108
Qur‘an na Sayansi ya Wanyama (Zoolojia) .............................................. 119
Qur‘an na Matokeo ya Sayansi ya Kitabibu ............................................. 125
Qur‘an na Sayansi ya vita vya anga .......................................................... 145
4
Qur‘an na Sayansi ndani ya Tetemeko la Ardhi ...................................... 153
Qur‘an na Sayansi ya Mwisho wa Ulimwengu (The Big Crunch Theory)
....................................................................................................................... 158
HITIMISHO ........................................................................................................... 163
REJEA ZA KITABU: .............................................................................................. 165
5
KUHUSU KITABU:
6
MAKOSA YA CHAPA NA UANDISHI:
7
DIBAJI
8
kufanya upembuzi huu wakakusanya majumui kutoka katika
rejea mama na za msingi.
Mapungufu ya kibinadamu hayakosekani, hivyo tuna waasa
wasomaji wa kitabu hiki wakiona madosari madogo madogo
wajue kwamba ni ya kibinadamu kwani mkamilifu ni Allah
mtukufu pekee.
Wabillahi Tawfiq.
Shaykh Mohammad Abbas
9
SHUKRANI
10
kitabu hiki linafikiwa. Kwa muktadha huo namshukuru sana
Shaykh Mohamed Rajab (Ibnrajab), Al-Akh Mohamed Abdallah
Kifosha, Mudir Mussa Abdallah Amir, pamoja na wote ambao
wamekua ni viungo muhimu katika kila nyanja ya ukamilishaji
wa chapisho hili.
Kwa ujumla, namuomba Allah (Subhanahu) ampe kila mmoja
mema na rehma zake, aweke wema na mchango wao katika
chapisho hili katika mizani ya matendo yao mema. Namuomba
Allah (Subhanahu) awape kila hitajio la nafsi zao, awawaruzuku
afya, hekima, na taqwa ya kuendelea kuitumikia dini na jamii ya
Kiislamu kwa ujumla. Aamin.
Abuu Farheen Farid
11
UTANGULIZI
12
matokeo ya tafiti hizo, yalizalisha makundi manne makubwa.
Makundi hayo akayafafanua na kuyabainisha namna ambavyo
zilijengwa imani zao, na kutakidi juu ya kuumbwa kwa viumbe
na ulimwengu kwa ujumla.
Imam Ibn Jawzy (Rehma za Allah ziwe juu yake) akaeleza kuwa
tafiti hizo zilizalisha kundi la Wasekula (Kundi la Watu wasio na
dini) ambao waliamini kuwa hakuna Mungu wala Muumba, na
vitu vyote vinavyoonekana katika ulimwengu, pamoja na
ulimwengu wenyewe vilikuwepo na vitaendelea kuwepo bila ya
uwepo wa Mungu wala Muumba, na hakuna nguvu yoyote
ambayo imeanzisha na inayoweza kusimamia kuendeleza
matukio ya viumbe na ulimwengu wao.
Kutokana na matokeo ya utafiti wao walikanusha uwepo wa
Mungu kwa sababu walishindwa kumfahamu kwa hisia zao na
wakashindwa kutumia akili zao. Kutokana na imani zao hizo, Ibn
Jawzy (Rehma za Allah ziwe juu yake) alieleza kuwa kwa mtu
mwenye akili timamu sio rahisi kwake kutilia mashaka uwepo wa
Muumba. Kwani katika hali ya kawaida, mtu akipita kwenye
kipande cha ardhi kisicho na majengo, kisha akarudi na kukuta
ukuta umejengwa hapo atagundua kuwa lazima kulikuwa na
mjenzi aliejenga ukuta huo.
Kundi la pili ni kundi la Wanaasili (Naturalist), ambao waliamini
kuwa kila kitu katika huu ulimwengu hakikuumbwa na yoyote,
bali ni matokeo ya uoto wa asili. Wakaamini kuwa ulimwengu na
walimwengu wote umezaliwa na vipengele vinne muhimu
ambavyo ni Dunia, Maji, Mito na Anga. Katika imani yao ni kuwa
vipengele hivyo vinne ndivyo haswa chanzo cha asili ya
ulimwengu na walimwengu kwa ujumla wake.
Ama kwa upande mwengine, Ibn Jawzy (Rehma za Allah ziwe
juu yake) akaeleza kuwa kundi la tatu katika matokeo ya tafiti
za asili, waliamini juu ya ushirika wa uwili (Dualist) waliamini
kuwa ulimwengu umeumbwa na unaendeshwa na nguvu za
miungu wawili ambao ni Muumba mwema na Muumba muovu.
Wakisema kuwa Muumba mwema ni muumba wa mwangaza na
muumba muovu ni Muumba wa giza. Imani yao ikaegemezwa
13
kuwa miungu hiyo miwili ndio miungu ya milele ambayo daima
walikuwa na watakuwa na nguvu juu ya kujua, kusikia, kuona
na mengi mengine ambayo yatahakikisha ustawi mzuri wa
ulimwengu na walimwengu. Dhana na imani hizi, ndizo ambazo
siku zote huwatoa viumbe katika kumtambua na kumjua
Muumba wa hakika na kuwazuia watu kujua ubainifu wa hakika
katika kumtambua Muumba wa kweli.
Kundi la nne ambalo lilizalishwa na jitihada za utafutaji wa
ukweli na hakika ya kuumbwa kwa ulimwengu na viumbe ni
kundi la Wanafalsafa, ambao kwa mujibu wa Ibn Jawazy
(Rehma za Allah ziwe juu yake) ni miongoni mwa waliokumbwa
na hadaa na vitimbi vya ibilisi (Laana za Allah ziwe juu yake).
Aliwahadaa na kuwafanya waamini juu ya maoni, mawazo, fikira
na mitazamo ambayo haitegemei mafundisho ya unabii, Uungu
wala imani yoyote isipokuwa kile wanachokitafakari na kukiwaza
viongozi wao. Wanafalsafa waliamini na kuabudu mawazo na
mitazamo ya viongozi wao, huku kila jambo katika ulimwengu
walilihukumu na kutoa miongozo kwa mujibu wa mitazamo hiyo.
Baadhi ya wanafalsafa, kupitia Imani yao yaliegemea zaidi na
kuamini mawazo na matokeo ya kundi la wanaasili (wasio amini
dini) ya kwamba ulimwengu hauna Muumba wala mwenye
kuusimamia. Kwamfano, miongoni mwa mawazo ya wanafalsafa
walidai kuwa dunia ni sayari iliyo katika utupu wa ulimwengu, na
kwamba kila sayari ina walimwengu wake kama ilivyo sayari ya
dunia. Wote katika wanafalsafa wanaamini kuwa dunia haina
mwisho kama ambavyo haikuwa na mwanzo.
Kutokana na ukweli kuwa dhana zote hizo hazina hakika. Kupitia
Qur‘an tukufu aliyoteremshiwa Mtume wa Allah (Sala na Salam
ziwe juu yake) ambayo ndio inayothibitisha kwa wazi na
ufafanuzi murua ambao unakinaisha juu ya asili ya kuumbwa
kwa Ulimwengu na walimwengu. Vile vile, Qur‘an ndio kitabu
pekee ambacho kadiri miaka na karne zinavyokwenda, ndivyo
mambo kadhaa yanaendelea kuthibitishwa ndani yake. Mbali na
masuala kadhaa kuhusu kuumbwa kwa ulimwengu na
walimwengu, Sayansi na miamala mbali mbali ya kijamii, kitaifa
14
na kimataifa imeendelea kuikiri Qur‘an kwa vitendo na
maandishi.
Kutokana na msingi huu sasa, kila mwenye akili timamu, humili
kuamini kuwa dhana pekee ambayo itahakikisha na kuaminika
kuwa ndio ya hakika ni sharti kuwa, dhana ama imani hiyo iwe
imekamilika na kuaminika kuwa imetoka moja kwa moja kwa
Muumba. Qur‘an ikiwa ndio chanzo kikuu cha Imani ya Kiislamu,
na ndio kitabu kinachofuatwa na kutegemewa na waumini wake.
Waislamu wanaamini kuwa Qur‘an ni muongozo kwa viumbe
wote. Hii ni kwa sababu ujumbe wa Qur‘an unaaminika kuwa ni
wa nyakati zote na unapaswa kuwa muhimu kwa kila zama.
Kutokana na asili ya kushushwa kwa Qur‘an, pamoja na yale
ambayo imejumuisha ndani yake, ni dhahiri kuwa Qur‘an
inatosha kutoa majibu ya uhakika juu ya kila jambo. Jambo hilo
liwe ni la kiimani, kiitikadi, kitabibu, kidiplomasia ama miamala
mengine muhimu ndani ya jamii ya Kitaifa na Kimataifa.
Kutokana na ukweli huo, huenda kama kila mmoja katika
kuutafuta ukweli wa uhakika wa kuumbwa kwa ulimwengu,
wangelijikita katika kutafuta ukweli huo kupitia Qur‘an, basi
kusingekuwa na mapote ya dhana ambazo hazina mashiko.
15
HISTORIA YA KUSHUSHWA KWA QUR‟AN TUKUFU
16
Mola wake kuwa unapatikana katika kumi la mwisho la
Ramadhani. Ni sunnah kwa Waislamu kuzidisha kusoma Qur‘an
katika mwezi mzima wa Ramadhani na kukaa Itiqaf katika kumi
la mwisho, ili kushiriki kikamilifu katika sherehe ya kumbu
kumbu ya kuanza kushuka Qur‘an. Historia ya kuanza kushuka
Qur‘an kwa Mtume Muhammad (Swala na amani ziwe juu yake)
kupitia kwa Malaika Jibril (Alaihi Salam) inasimuliwa vyema
katika Hadith ya bibi 'Aisha (Radhi za Allah ziwe juu yake)
17
kuwa kitu kinaweza kunitokea ". Khadijah alijibu: "Hapana!
Naapa kwa jina la Allah, Allah (Subhanahu) hatakufedhehesha.
Unakaa vizuri na kuwafanyia wema ndugu na jamaa zako,
unawasaidia masikini na fukara, unawakirimu wageni na
unawasaidia waliokabiliwa na matatizo. "Kisha Bibi Khadijah
alimchukua Mtume (Swala na amani ziwe juu yake) mpaka kwa
bin-ami yake, Waraqa bin Naufal bin Asad bin Abdul Uzza,
ambaye alikuwa Mkristo. Waraqa wakati huo alikuwa mzee sana
na alikuwa hawezi kuona tena. Khadijah alimuambia Waraqa
"Sikiliza hadithi ya mpwa wako, Ewe Bin-ami yangu" Waraqa
aliuliza, "Ewe Mpwa wangu umeona nini?" Mtume wa Allah
alimuhadithia habari yote kama alivyoona. Waraqa akasema:
"Huyu ni yule mtunza siri (Malaika Jibril) ambaye Allah
(Subhanahu) alimtuma kwa Mussa. Natamani ningelikuwa kijana
na kuishi mpaka wakati huo watu wako watakapokukataa na
kukufukuza." Mtume wa Allah (Subhanahu) akauliza:
"Watanifukuza?" Waraqa akajibu kuwa watafanya hivyo na
akasema, "Yeyote aliyekuja na kitu kama hicho ulichokuja nacho
alifanyiwa uadui na watu wake, na ningejaaliwa kubakia hai
mpaka siku hiyo watu wako watakapokufukuza, ningelikusaidia
kwa hali na mali." Lakini baada ya muda mfupi Waraqa alifariki
na Wahyi mwingine ulikawia kuja kwa kipindi kirefu. (Sahihi
Bukhari)
Tunajifunza kutokana na Hadith hii kuwa kabla Mtume (Swala
na amani ziwe juu yake) hajaanza kushushiwa Qur‘an kupitia
kwa Malaika Jibril (Alaihi Salam) alikuwa akipata Wahy kwa njia
ya ndoto.
Qur‘an yote kwa ujumla imehifadhiwa katika ubao mtukufu wa
Allah (Subhanahu) ulio katika Arshi yake kama
tunavyofahamishwa katika Qur‘an:
18
Malaika Jibril (Alaihi Salam) kwa kipindi chote cha Utume cha
miaka ishirini na tatu.
19
JE! QUR‟AN IMEPITWA NA WAKATI AU IPO MBELE YA
WAKATI
Miaka takribani elfu moja mia nne (1400) imepita tangu Wahy
(ujumbe) wa kwanza wa Qur‘an kuanza kumshukia Mtume wa
Allah (Rehma na Amani ziwe juu yake) kupitia kwa Malaika
Jibril. Karne kumi na nne (14) zimepita tokea karne ya saba
ambayo ndio karne ya Qur‘an, ilishushwa kutoka katika ubao
uliotukuka kumshukia Mtume wa Allah (Rehma na Amani ziwe
juu yake).
Inasemwa kuwa Qur‘an ilishushwa katika karne iliyoitwa ya giza
la elimu, karne ambayo haikuwa na wala haikutegemewa kuwa
na maendeleo makubwa ya kiugunduzi katika masuala kadhaa
wa kadhaa. Tofauti na karne ya ishirini na ishirini na moja
(miaka 1400 baada ya Qur‘an kushushwa) kipindi ambacho
maendeleo makubwa ya Sayansi, teknolojia na teknohama
yamedhihiri, huku yakileta matokeo chanya ya urahisishaji wa
masuala mbali mbali ambayo hapo awali hayakuwepo.
Maendeleo makubwa yakaonekana katika sekta tofauti kama
vile usafiri na usafirishaji (Maji, Anga, Ardhi), tiba, mawasiliano,
na mengine mengi yasiyokuwa hayo. Huku ikionekana kwa
dhahiri kuwa karne za ishirini na ishirini na moja ndio karne za
maendeleo, ndio karne za mwangaza wa kielimu na
kiutandawazi, kutokana na hatua za ugunduzi zilizofikiwa
kulinganisha na karne ya saba (ambayo Qur‘an ilishushwa).
Kutokana na dhana hizo ambazo zimeendelea kuoteshwa ndani
ya fikra za walio wengi, hoja ya msingi ni kwamba; ni kweli
karne ya Qur‘an (Karne ya saba) ndio karne ya kiza cha elimu?
Na Je! Kwakuwa Qur‘an imeshushwa katika kipindi hicho,
tuamini kuwa imepitwa na wakati? Ili kujibu hoja hizi za msingi,
tuangalie baadhi ya nukta ambazo zilitajwa ndani ya Qur‘an
miaka 1400 iliyopita na namna ambavyo iliigharibu Sayansi na
wanasayansi karne kumi na nne (14) kuweza kuyafahamu na
kujifunza ndani yake.
20
UTHIBITISHO NDANI YA QUR‟AN
21
kwakuwa haina mafungamano yoyote ya muda, zama wala jamii
fulani. Kutokana na ukweli huu juu ya Qur‘an, siku zote
imeendelea kukidhi haja na mahitaji ya viumbe katika njanja na
fani mbali mbali.
Wanasayansi na wasomi kadhaa wamekuwa wakijaribu kuipa
Qur‘an changamoto au kufanya tafiti za kutafuta na kubaini
makosa ndani yake, ila wamekuwa wakigonga mwamba
kwakuwa ahadi ya Allah (Subhanahu) juu ya ujumbe uliopo
ndani ya Qur‘an imeendelea kusimama bila kutingishwa kwa hali
yoyote ile. Wapo baadhi ya wanasayansi ambao walihoji juu ya
taarifa za kuumbwa kwa mbingu na ardhi huku wakisema kuwa
wakati muumba anaviumba vitu hivi yeye alikua wapi? Baada ya
miaka kadhaa kupita sayansi ikaja kuthibitisha kuwa kabla ya
kuumbwa kwa ardhi na mbingu, vipo baadhi ya vitu ambavyo
vilishaumbwa, kama vile maji. Walichoshindwa kufahamu ni
kuwa jambo hilo lilishafafanuliwa na Qur‘an katika karne ya
saba.
22
Hili limekuja baada ya kuona mambo mengi ambayo
yamefafanuliwa na Qur‘an katika kipindi hicho, ambayo
iliwachukuwa manguli na wabobezi wa sayansi, takribani miaka
elfu moja kuweza kuyafahamu na kuyatumia. Kutokana na hoja
hii, tunasema kuwa karne ya ishirini na ishirini na moja ni karne
za matumizi ya elimu ambayo ilitolewa na Qur‘an kupitia kwa
Mtume wa Allah (Rehma na Amani ziwe juu yake) karne ya
saba.
Wakati Qur‘an inaanza kushushwa kwa Mtume wa Allah, amri ya
kwanza aliyopewa ni kuamrishwa kusoma, kama ilivyokuja
katika Surat Alaq; baadhi ya wafasiri wa Qur‘an wanasema kuwa
amri ya kusoma imekuja kufungua enzi mpya, enzi ya sayansi
na teknolojia, enzi ya kusoma na kutumia uwezo mkubwa wa
kitafiti na kigunduzi wa kuijua dunia na mifumo yake, kumjua
mwanadamu na utaratibu wake, ili elimu hiyo impelekee kiumbe
katika kumjua Muumba wake na kumpwekesha kwa ibada na
stahiki zake zote.
Hivyo, Mtume wa Allah alitumwa kuufikisha ujumbe huu wa
kielimu, elimu ya juu yenye mkusanyiko wa maarifa ya fani
tofauti. Mtume ambae hakujua kusoma wala kuandika, bali
alifundisha na kufafanua mambo makubwa ambayo yamekuja
kuwashangaza wengi miongoni mwa wanasayansi mashughuri.
Mfano mzuri, ni Dokta Maurice; mwanasayansi na daktari
bingwa wa upasuaji wa binadamu, aliandika katika kitabu chake
„The Bible, the Qur‟an and Science (2004) kuwa; Qur‘an
ndio kitabu pekee katika ulimwengu huu kilichoeleza kwa kina
na ufasaha juu ya habari za kuumbwa kwa mbingu na ardhi,
pamoja na namna ambayo uumbaji ulivyofanyika. Wakati Qur‘an
inaelezea habari za kuumbwa kwa ulimwengu, kitabu chenyewe
hakikuwepo. Aidha, kupitia tafiti yake pia alisema kuwa
alishangazwa kupata taarifa ndani ya Qur‘an juu ya matukio ya
asili ambayo maana yake inaweza tu kueleweka kupitia ujuzi wa
kisasa wa kisayansi.
Allah (Subhanahu) anaelezea ndani ya Qur‘an kauli ambayo
ilimfanya Dokta Mourice kusema maneno hayo kuwa;
23
―Na yeye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Na
kiti chake cha Enzi kilikuwa juu ya maji.‖ (11:07)
Qur‘an inafafanua na kujibu hoja dhaifu za baadhi ya
wanasayansi ambao walihoji juu ya uumbaji wa mbingu na
ardhi. Kauli ya Allah (Subhanahu) inathibitisha kuwa kabla ya
kuumbwa kwa mbingu na ardhi, tayari alishayaumba maji
ambayo ndiyo yalibeba arshi (kiti cha enzi) yake. Ingawaje
ilionekana kuwa ni ajabu maji kuweza kubeba kitu chochote hali
ya kuwa yenyewe ni kimiminika, na yalihitaji kitu cha kuyabeba.
Sayansi inathibitisha kuwa maji yanaweza kuwa katika hali kuu
tatu; kimiminika, gesi, na pia maji yanaweza kuwa na hali ya
mgando. Kwa mujibu wa tafiti za uumbaji wa dunia,
wanasayansi wanathibitisha kuwa hapo awali maji yalikuwa
katika umbile moja kubwa la mgando ambalo lilikuja kuyeyuka
baada ya kuubwa kwa ardhi na mbingu.
Hivyo, kutokana ukweli unaothibitishwa kuwa Qur‘an imebeba
elimu kubwa ndani yake na pia karne ya Qur‘an ndio karne ya
mapinduzi ya kielemu. Zifuatazo ni nukta muhimu na matokeo
kadhaa ya tafiti za Sayansi, teknolojia na teknohama
yakionyesha namna ambavyo Qur‘an imekua ikifafanua masuala
mengi ambayo hawakuyahafahamu hapo kabla.
25
Katika mtazamo huo ambao ulikuja takribani miaka elfu moja
baadae na wengi miongoni mwa wanasayansi wa anga
wanakubaliana moja kwa moja na dhana hiyo ya sayansi. Qur‘an
iliyoshushwa karne ya saba imefafanua na kuweka bayana
jambo hilo na hivyo sayansi ikaifata na kuikiri kwa tafiti na
majaribio mbali mbali. Allah (Subhanahu) anasema ndani ya
Qur‘an;
―Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi
zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabadua? (21:30)
27
Karne ya Qur‘an (karne ya saba) ndiyo ilikuwa karne ya ufunguzi
wa zama za kielimu na ndio karne pekee iliyofungua milango ya
tafiti na gunduzi mbali mbali za Kisayansi na Teknolojia. Kwani
baada ya Qur‘an kueleza kuwa sayari zote pamoja na jua na
mwezi kila kimoja huzunguka katika muhimili wake, ndipo juhudi
za ziada za kigunduzi kuchukuliwa na kisha matokeo yake
yakaja kueleza na kuithibitisha Qur‘an.
28
Allah (Subhanahu) amesema juu ya hilo;
―Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na
vyote vinaogelea katika njia zao.‖ (36:40)
Kauli hii ya Allah (Subhanahu) inathibitisha juu ya mienendo ya
sayari hizo ambazo kila moja huzunguka katika nafasi na wakati
wake. Kutokana na mihimili yake, hazikufanywa kimoja kuenda
mbele ya mwenzake kama ambavyo mchana hauwezi kuingia
katikati ya usiku. Kila kimoja kina wakati wake, safari na njia
zake ambazo vimepangiwa.
﴾٥﴿ن
ْ َن يَ ْعل
ْ ًَسبىَ َهب ل
َ ٱإل
ِ نَ ََّعل
‖Kamfundisha mwanadamu aliyokuwa hayajui‖ (96:05)
29
Akaongeza pia, siku moja ndani ya sayari ya Jupiter ni sawa na
masaa tisa na dakika hamsini na tano (Masaa 9, Dakika 55).
Kwa mujibu wa dhana maarufu ya fizikia ya Einstein inasema
kuwa uwiyano wa muda hutegemea namna ambavyo kitu
kinavyotembea kwa kasi yake. Dhana hii imekuja kuthibitishwa
na gunduzi juu ya namna ambavyo sayari tofauti huzunguka
katika mihimili yake huku kila moja ikiwa na kasi yake.
30
Kadhalika, katika kuthibitisha juu ya dhana ya uhusiano wa
wakati, angalia namna ambavyo nyakati zinavyokuwa na
utofauti mkubwa baina ya nchi na nchi, kulingana na masafa ya
mabara. Tunaona vipimo vya siku (Mawio na machweo)
hutofautiana kwa kiasi fulani kutoka nchi moja ndani ya bara
moja na nchi nyengine iliyo katika bara jengine. Sote
tunakubaliana kuwa idadi ya masaa ya funga ya Ramadhani
hapa nchini sio sawa na idadi ya masaa ya baadhi ya nchi za
bara Ulaya. Zipo nchi ambazo wakati hapa nchini tukifunga kwa
takribani masaa kumi na mbili, wao hufunga masaa zaidi ya
kumi na tano ikiwa ni miongoni mwa visithibitisho kwa uwiyano
wa wakati (Time relativity).
31
Qur‘an inatueleza kuwa elimu na sayansi iliopo ndani ya
uhusiano wa wakati ndani ya ulimwengu huu, ulishatolewa
ufafanuzi wake miaka elfu moja iliyopita, huku baadhi ya
wanasayansi wakiumiza kichwa kujadili yawaje kitabu ambacho
kilishushwa jangwani, ndani ya karne ya giza la elimu,
kilichoshushwa kwa Kiumbe ambae hakuwa na elimu, kiweze
kufafanua masuala mazito yenye kuhitaji ujuzi na vifaa vya
kisayansi ya kisasa!
Qur‘an kupitia Surat Al-Hajj, Allah (Subhanahu) anasema;
―Na hakika siku moja kwa Mola wako Mlezi ni kama miaka elfu
mnavyo hisabu nyinyi.‖ (22:47)
32
Lakini kadiri zama na nyakati zilivyokwenda huku maendeleo
makubwa ya kigunduzi kufikiwa, sayansi imekuja kuikiri Qur‘an
kwamba kwa hakika ―Muda unao mahusiano‖ ndani ya huu
ulimwengu. Mahusiano ambayo hutofautiana kulingana na
umbali wa sayari moja hadi nyengine, mahusiano ambayo
hutegemea na kasi ambayo sayari moja huzunguka katika
muhimili wake, aidha, mahusiano ambayo hutegemea na nani
haswa hupima kiwango hicho cha wakati.
33
Walichoshindwa kutambua kuwa Allah (Subhanahu) kupitia
Qur‘an tukufu alishafafanua juu ya mwenye mamlaka ya juu ya
kuwawezesha kufanya safari hizo. Wanasayansi kupitia
majaribio tofauti ambayo hayakuwapa matunda ya mafanikio
walishindwa kutambua kuwa mbali na elimu, sayansi, na
maendeleo makubwa ya kiteknolojia hayawezi kuwawezesha,
bila ya kupata idhini ya mwenye mamlaka ya safari za anga za
mbali. Allah (Subhanahu) anasema ndani ya Surat Ar-Rahman;
―Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye
mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa
madaraka.” (55:33)
Wafasiri wa Qur‘an tukufu wameifafanua kauli ya Allah
(Subhanahu) wakisema kuwa; Allah (Subhanahu)
anawabainishia waja wake kuwa kama wataweza kupenya nje
ya mipaka ya mbingu ama kupenya chini ya mipaka ya ardhi
basi wapenye ili kuikimbia adhabu yake na ufalme wake. Aidha,
wakasema kuwa madaraka yaliyokusudiwa hapa ni ufalme wake
wa utendaji kwa kila alipendalo na kuwa kila jambo lipo kwenye
umiliki wake. Wapo baadhi ya wanachuoni waliofafanua neno
madaraka kuwa ni elimu na upeo wa kuweza kupenya kwa
idhini yake.
Hivyo basi, kutokana na ukweli huo wa Qur‘an, mnamo mwezi
Julai mwaka 1969 baada ya tafiti za kina kufanyika pamoja na
kupewa mamlaka ya elimu na Allah (Subhanahu), safari ya
kwanza ya mwanadamu kutua katika ardhi ya mwezi ilifanyika
huku Kamanda Neil Armstrong na rubani wa mwezini bwana
34
Edwin Aldrin wakiwa ndio binadamu wa kwanza kupewa
madaraka na Allah (Subhanahu) kupaa kufika anga za mbali.
Taarifa katika mtandao wa NASA zinaeleza kuwa upo mpango
mwengine ambao wameuweka kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka
2025 wanatafanikiwa kuwapeleka wanaanga wengine 25 katika
ardhi ya mwezi. Ila bila kusahau kuwa itafanikiwa endapo
watapewa mamlaka na Allah (Subhanahu).
Miaka kadhaa baadae, tumeshuhudia safari nyingi zikifanyika
ambazo baadhi zilifanikiwa na baadhi kupata changamoto, ikiwa
ni pamoja na kugharimu maisha ya wana anga kadhaa. Kupitia
safari ya kwanza ya wanadamu kutua katika uso wa ardhi ya
mwezi ambayo iliwachukuwa wana anga hao kusafiri umbali wa
masafa ya kilomita 376,400, yapo matukio makubwa ambayo
tunapaswa kuyafahamu. Matokeo ambayo wanasayansi hawa
wameyaona na kuyasimulia kwa ulimwengu mara tu baada ya
kurejea ndani ya sayari ya dunia.
Kutokana na taarifa za wanasayansi hawa juu ya yale waliyo
yashuhudia huko pamoja na mlolongo mzima wa safari yao ulio
uwacha ulimwengu mdomo wazi, huku wakiwa na masuali
lukuki, masuali ya kuwa kivipi Qur‘an iliyoshushwa karne ya
saba iliweza kueleza juu ya mambo kadhaa kuhusu mwezi katika
kipindi ambacho hakuna kiumbe aliyeweza kufika katika anga za
mbali.
Nidhamu ya mzunguko wa mwendo wa kinyume cha saa
(kuzunguka kutoka kulia kwenda kushoto) katika
kuufikia mwezi:
Kwa mujibu wa taarifa iliyorushwa mubashara ulimwenguni
kuhusu safari hiyo, inaeleza kuwa chombo ambacho walikitumia
kusafiri katika masafa hayo ya mbali ambacho kilipewa jina la
Apollo 11, mara tu baada ya kutoka na kupenya nje ya sayari ya
dunia kilianza kuzunguka katika obiti (mihimili ya mwezi) kutoka
kulia kwenda kushoto huku kikiendelea kukaribia ardhi ya
mwezi. Wanasayansi wanakiri kuwa sayari zote huzunguka
katika mihimili yake kwa mwendo wa kinyume cha saa yaani
huzunguka kutoka kulia kwenda kushoto.
35
Ilisemwa pia haikuwezekana kuufikia mwezi kwa kufanya
mzunguko mwengine wowote isipokuwa kwa kuzunguka kwa
mwendo wa saa, na jambo hili lilielezwa na wanasayansi kuwa
ni kutokana na maumbile ya sayari zote zimeeumbwa
kuzunguka katika muhimili wake kwa kufata nidhamu hiyo.
36
Nidhamu hii inatuthibitishia kuwa kila umbile ndani ya
ulimwengu limeumbwa na Allah (Subhanahu) kwa kufata
utaratibu maalumu kama ule ambao mahujaji hutufu nyumba
tukufu ya Kaaba kwa kuizunguka kutoka kulia kwenda kushoto.
37
kulia kwenda kushoto, hivyo iliwalazimu kuufuatisha mzunguko
huo ili kuepuka kikinzana nguvu ya mvutano huo ili usilete
madhara kwao na kwa chombo chao. Kwa tafakuri za kina, tukio
hili linathibitisha kuwa wanasayansi hawa hawakuweza kupenya
nje ya mbingu na kuufikia mwezi isipokuwa na mamlaka ya
Allah (Subhanahu) kwani hawakuweza kupata njia yoyote
mbadala ya kuufikia mwezi isipokuwa kwa kufata nidhamu
aliyoiweka Mwenye Mamlaka.
Ushuhuda wa Neil Armstrong kuhusu kupasuka kwa
mwezi:
Allah (Subhanahu) kupitia Surat Al-Qamar amesema katika
karne ya saba;
―Kiama (Saa) kimekaribia, na mwezi umepasuka!‖ (54:01)
Ibn Kathir (Radhi za Allah ziwe juu yake) amemnukuu Anas bin
Malik (Radhi za Allah ziwe juu yake) akisimulia kuwa Imam
Ahmad amepokea kutoka kwa Anas bin Malik akisema; ―Watu
wa Makka walimtaka Mtume wa Allah (Rehma na Amani ziwe
juu yake) awaonyeshe muujiza, ndipo wakashuhudia mwezi
ukipasuka vipande viwili katikati ya mji wa Makka.‖
Qur‘an tukufu inaeleza habari za mwezi kupasuka ikiwa ni ishara
ya kuonyesha kuwa kiyama kimekaribia huku wafasiri wa Qur‘an
wakifafanua aya hii kwa kutumia Hadithi kadhaa sahihi juu ya
tukio la muujiza wa kupasuka kwa mwezi, ikiwa ni miongoni
mwa miujiza mikubwa ya Mtume wa Allah (Rehma na Amani
ziwe juu yake). Wanasayansi wa karne ya ishirini hawakuacha
kupinga na kuona kuwa ni jambo lisilo na mashiko huku kwa
kebehi na dharau wakiwageukia waumini kwa masuali kadhaa
yasiyo na majibu.
Ni kweli, kutokana na maendeleo finyu ya sayansi na teknolojia,
halikuwa jambo jepesi kulithibitisha ingawaje bado suala hili
likaendelea kuwaumiza kichwa watafiti na wasomi wa masuala
ya anga. Kutokana na mamlaka ya elimu na vipawa
walivyopewa watafiti wa masuala ya anga wa karne ya ishirini,
mnamo mwaka 1969 safari ya Neil Armstrong ilikuja kutoa
38
uthibitisho wa kuikiri Qur‘an. Katika taarifa ya Bwana Neil
akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo wa kimataifa
mara tu baada ya kurudi kutoka katika misheni ya mwezi,
aliulizwa na mwandishi mmoja kuhusu faida za safari hiyo.
Bwana Armstrong alisema kuwa miongoni mwa faida kubwa
waliyoipata ni kuthibitisha kuwa ipo athari ya kuthibitisha kuwa
mwezi unawezekana kuwa ulipasuka vipande viwili.
39
kina wa vipande hivyo, ilithibitika kuwa ni miongoni mwa
ushahidi wa athari za mpasuko wa ardhi ya mwezi.
40
Ugunduzi wa Sayari (nyota) yenye sauti ya kugonga:
Katika kuendelea kutoa ufafanuzi kuhusu matokeo ya safari ya
kwanza ya wanadamu katika uso wa ardhi ya mwezi, inaelezwa
kuwa safari hiyo iliweza kugundua kuhusu uwepo wa nyota
kubwa ambayo huonekana duniani nyakati za usiku ambayo kwa
kutumia kifaa maalumu cha kunasa sauti, waliweza kugundua
kuwa inatoa sauti mfano wa sauti ya mtu anae gonga mlango
wa mbao kwa kutumia vidole vyake.
41
sauti kuwa chini ya kiwango ambacho uwezo wa usikivu wa
mwanadamu kuweza kunasa kwa ufasaha. Wakaeleza kuwa
kutokana na matokeo ya safari ya kwanza ya nje ya dunia,
ilipekea wanasayansi kutafiti na kuchunguza kwa kina juu ya
madai ya bwana Neil Armstrong na wenzake. Madai ambayo
yalikuja kuwezesha kugunduliwa kifaa maalumu cha kupima na
kusikiliza sauti za sayari tofauti kwa kutumia mawimbi yake ya
mtetemeko wa sauti.
42
Surat At-Tariq ambayo kwa lugha ya Kiingereza hitwa ‗The night
comer‘ au ‗The Knocker‘
―Naapa kwa mbingu na kinachokuja usiku. Na nini kitakacho
kujulisha ni nini hicho kinacho kuja usiku. Ni nyota yenye
mwanga mkali.‖ (86:01-03)
Kwa hakika Allah (Subhanahu) ni mbora kwenye kuumbwa na
kuyabainisha kwa waja wake ili iwe ni fundisho na muongozo
wa maisha yao.
43
Miongoni mwa mambo ambayo alisema Qur‘an imefafanua
wakati ambao sayansi haijafika katika tafiti zake ni kauli ya Allah
(Subhanahu);
―Amemuumba mwanadamu kwa tone la damu‖ (96:02)
Kwa mujibu wa Dokta Naik, wakati aya hii inapelekwa kwa
mtafiti huyo hakuweza kuthibitisha kwa upande wa sayansi
kwamba mwanadamu katika kuumbwa kwake hupitia hatua ya
pande la damu. Baada ya kulipitia suala hilo, ilimlazimu kufanya
tafiti ya kina juu ya hatua za awali za uumbaji wa mwanadamu,
pamoja na kusoma kwa undani mfumo mzima wa embyolojia ya
mwanadamu huku akishirikiana na wataalamu wenzanke katika
fani hiyo.
44
za baba na mama) kufikia hatua ya kuwa pande la damu na
hadi kuwa kiumbe hai.
46
Qur‘an ilieleza kuwa maji ya uzazi yanatoka baina ya mifupa ya
mgongo na mbavu, ukiangalia katika picha hapo juu sehemu
ambayo imezungushiwa ndio sehemu ambao Qur‘an imeieleza.
Wanasayansi wa fani ya uzazi wa mwanaume wanaeleza kuwa
sehemu hiyo ipo mshipa mkuu wa neva (abnominal aorta)
ambao umeenda moja kwa moja katika ubongo wa
mwanadamu.
47
Wapo baadhi ya wanasayansi wanaosema kuwa uzalishaji wa
mbegu za uzazi huanzia katika ubongo kwa mfumo wa hisia
kisha kusafirishwa katika sehemu hiyo kwa ajili ya kuwekwa
tayari kwa ajili usafirishwaji wa mwisho kuelekea katika tezi
dume kabla ya kutolewa (ejaculation).
―Hebu naajitazame mwanadamu ameumbwa kwa kitu gani?
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa. Yatokayo baina ya
mifupa ya mgongo na mbavu.‖ (86:5-7)
48
Ukiangalia mchoro hapo juu unaweza kuona namna ambavyo
mchanganyiko wa kromosoma unavyo fanyika huku
ukitengeneza na kuamua jinsia ya mtoto kwa kuchanganya
mbegu za baba (X au Y) na zile za mama (X). Maelezo na
ufafanuzi huo umekuja baada ya tafiti na kazi kubwa za
kimaabara kufanyika. Tafiti ambazo zilionekana kuwa ni ushindi
mkubwa uliopatikana ndani ya karne ya ishirini. Walishindwa
kutambua kuwa hivyo hivyo, ndivyo Qur‘an ilivyobainisha juu ya
uzazi na jinsia ya watoto; Allah (Subhanahu) anasema ndani ya
Surat Ash-Shura;
―Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Allah; anaumba apendavyo,
anamtunukia amtakaye watoto wa kike, na anamtunukia
amtakaye watoto wa kiume, au huwachanganya wanaume na
wanawake, na akamfanya amtakaye tasa. Hakika Yeye ni mjuzi
mwenye uweza.‖ (42:49-50)
49
wasomi na watafiti wa masuala haya kuja kuikiri na kuiweka
katika vitabu vyao. Allah (Subhanahu) anasema;
―Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi (pea) mbili, dume na
jike. Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa.‖ (53:45-46)
Tunakubaliana kuwa mbegu za uzazi hutolewa na baba, na
kama Qur‘an ilivyoeleza kuwa ni maji mchupo, yenye
kumiminika kutoka katika mifupa baina ya mgongo na mbavu.
Kutokana na kauli hii ya Allah (Subhanahu) tunaweza
kuthibitisha kuwa mbegu ya uzazi inayomiminwa kutoka kwa
baba, na ndio maji ambayo wanasayansi wanakiri kuwa
yamebeba kromosoma za kike na kiume ambazo ndizo hizo
zilizotajwa na Qur‘an kuwa ni jozi mbili.
50
matabaka matatu ambayo ni ngome dhidi ya madhara mbali
mbali ya ndani. Akafafanua kuwa matabaka hayo ni pamoja na;
a) Ukuta wa tumbo la mama
b) Ukuta wa Uterasi
c) Utando wa amniochorionic unaojumuisha amnioni
iliyounganishwa na chorion
51
hadi kufikia karne kadhaa baadae. Jambo hili linanipa ushahidi
kuwa Muhammada ni mjumbe wa Mungu/Allah.‖
52
Allah (Subhanahu) amesema pia;
―Mna nini hamueki heshima kwa Allah? Na hali Yeye
kakuumbeni daraja baada ya daraja.‖ (71:13-14)
Pili; Profesa Marshal alisema kuwa kama hivyo sivyo, basi elimu
juu ya hatua hizo ambazo mwanadamu anapitia katika tumbo la
mama yake ilikuwa ni elimu ya kubahatisha ambayo ilikuja
53
kuendana na matokeo ya kisayansi. Hoja hii haikuwa na uzito
kwakuwa kadiri matokeo ya sayansi yalivyokuwa yanashamiri,
ndivyo iliendelea kuthibitishwa kuwa Qur‘an ilishatangulia
ugunduzi wao. Hivyo Mtume wa Allah (Sala na Amani ziwe juu
yake) asingeweza kubahatisha na kupatia kila kitu.
Tatu; kama sio hayo yote mawili, basi lazima Muhammad atakua
ni Mtume na Mjumbe wa Allah (Subhanahu) na amepewa elimu
na mwenye elimu zaidi ya mambo. Hii ndio hoja ya yenye nguvu
na inayoonyesha ukomavu wa elimu na ambayo inampasa kila
mtu aweze kuibeba na kuiamini.
54
Profesa Moore akaendelea kueleza kuwa baada ya hatua hiyo,
mwanadamu hupitia katika hatua za kuwa ni pande la nyama
ambalo mwanzo wake huwa na pingili kama za mgongo ama
shanga (mchoro A), kisha katika siku ya ishirini na nane ndipo
mabadiliko ya pande hilo la nyama huanza, tayari kwa ajili ya
kuwekwa mifupa (mchoro B)
55
Profesa Moore akaendelea kueleza kuwa hatua inayofuata
baada hiyo ni ile hatua ya makuzi ya kasi na mabadiliko ya
haraka kwa mtoto. Hatua ambayo viungo vyote muhimu tayari
vimeshapandikizwa kuanzia macho, pua, mikono, miguu, na
vyengine. Na ndio hatua ambayo kiumbe anaweza kuzaliwa na
kuwa salama hata kama ikitokea kuzaliwa kabla ya muda wake
kufika. Akaongeza kuwa hatua hii ndio ile ambayo Qur‘an
iliposema kuwa “Kisha tukamfanya kuwa kiumbe
mwengine mpya”
56
ya karne ya ishirini na ishirini na moja, ni vipimo vya masiku,
miezi, na miaka ambayo hupimwa na kuhesabiwa kwa ustadi
kwa kutumia kalenda za kisasa.
Allah (Subhanahu) amesema ndani ya Surat Al-Kahf;
﴾٢٥﴿سعب
ْ ِي َوٱ ْش َدادو ْا ت ْ َولَبِثى ْا فًِ َك ْه ِف ِه
ِ ن ثَالثَ ِهئَة
َ سٌِي
―Na walikaa katika pango lao miaka mia tatu, na wakazidisha
tisa‖ (18:25)
Kauli hii ya Allah (Subhanahu) inawazungumzia waja wake
ambao walikimbia katika mji wao kwa kuogopa fitna na uadui na
kuamua kwenda kujificha katika pango ambalo kwa mujibu wa
Qur‘an tukufu walikaa ndani yake kwa muda wa miaka mia tatu
na wakaongeza miaka mengine tisa. Kauli hii ni miongoni mwa
maajabu makubwa ya Qur‘an ambayo ilishushwa karne ya saba.
Ndani ya kauli hii juu ya idadi ya miaka kuna elimu kubwa
ambayo imefunganishwa ndani yake, elimu ambayo kwa undani
unaelezea utofauti wa hisabu za kalenda ambazo huhesabiwa
kufuata mwenendo wa jua na zile ambazo hufuata mwenendo
wa mwezi (muandamo).
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) akifafanua maana ya
kauli ya Allah (Subhanahu) juu ya; “Miaka mia tatu, na
wakazidisha tisa” amesema katika tafsiri yake ya Qur‘an
kuwa; Urefu wa muda ulikuwa miaka mia tatu pamoja na tisa
katika miaka ya mwezi mwandamo, ambayo ni miaka mia tatu
katika miaka ya jua. Tofauti kati ya miaka mia moja ya
mwandamo na miaka mia ya jua ni miaka mitatu, ndio maana
baada ya kutaja mia tatu, Allah (Subhanahu) anasema
akaongeza tisa.
57
Wasomi na wanasayasi wa hisabati, hawakulijua jambo hili hadi
ilipofika karne ya ishirini na ishirini na moja, ndipo walipokuja
kujua kuwa kwa kufuata mwezi mwandamo mwaka unakuwa na
siku mia tatu hamsini na nne tu, na kwa kufuata mwezi
unaofuata mwenendo wa jua, mwaka huwa na siku mia tatu na
sitini na tano. Ambapo tofauti ya mwaka wa mwezi mwandamo
na mwaka wa jua ni siku kumi na mbili. Hivyo, miaka mia tatu
kwa mwaka wa jua ni sawa na miaka mia tatu na tisa kwa
mwaka wa mwezi mwandamo. Hii ni miongoni mwa dalili kuwa
Qur‘an ipo mbele ya muda na itaendelea kuwa mbele ya muda.
58
Allah (Subhanahu) ametumia kiapo katika kueleza juu ya uwepo
wa vitu vingi ndani ya ulimwengu ambavyo vyengine amewapa
wanadamu uwezo wa kuviona kwa macho yao ya kawaida, na
vipo miongoni mwa vitu hivyo ambavyo havionekani kwa macho
ya kawaida. Mara zote Allah (Subhanahu) anapotaka kuelezea
mambo makubwa ambayo yanahitaji umakini wa viumbe,
hutumia viapo akiashiria uzito wa ujumbe huo.
Miongoni mwa vitu visivyoonekana, wanasayansi wa karne ya
ishirini na ishirini na moja wamekuja kugundua kuwa upo
mwangaza ambao hauonekani kwa macho ya mwanadamu
(Invisible light) wakasema kuwa; Urefu wa mawimbi ya
mwangaza hupimwa kwa nanomita. Nanomita moja ni sawa na
bilioni ya mita. Mwangaza unaoonekana una urefu wa mawimbi
kuanzia takribani nanomita 400 hadi nanomita 700. Mawimbi
mafupi kuliko nanomita 400 au zaidi ya nanomita 700,
hayaonekani kwa macho ya binadamu. Utafiti huu ni kwa mujibu
wa jarida la Discovering the Universe la mwaka 2002.
Kutokaana na ufafanuzi huo si shaka kuwa ugunduzi huu
umeikiri Qur‘an kupitia aya ya 38-39 ya Surat Al-Haaqqa
iliyoshushwa karne kumi na nne zilizopita.
59
Kadhalika, katika kuthibitisha kuwa Qur‘an ipo mbele ya wakati,
na kwamba wanasayansi ya karne ya ishirini na ishirini na moja
kuna mambo mengi ambayo hawakuyajua kabla, hali ya kuwa
Qur‘an ilishayashiria na kuyafafanua katika karne ya saba. Allah
(Subhanahu) kupitia Surah Luqman amesema;
ِ ًَ أَى ت
وي َد َ س ِ ود تَ َس ْوًَ َهب َوأَ ْلقًَ فًِ ٱألَ ْز
ِ ض َز َوا َ وب َواتِ بِ َغ ْي ِس َع
َ ٱلس
َّ َ َ خل
ق َ
﴾١١﴿نْ بِك
―Ameziumba mbingu bila ya nguzo mnazo ziona; na ameweka
katika ardhi milima ili isikuyumbisheni.‖ (31:10)
Ibn Kathir (Radhi za Allah ziwe juu yake) katika tafsiri yake
amesema juu ya kauli ya Allah (Subhanahu); “Ameziumba
mbingu bila ya nguzo mnazo ziona” kuwa kauli hii ni
ushahidi wa Tawhid ambao Allah (Subhanahu) anaeleza nguvu
zake za hali ya juu katika kuumba mbingu na ardhi na vyote
ambavyo vimo katikati yake. Akiendelea kufafanua juu ya kauli
kuhusu nguzo zisizo onekana, Ibn Kathir (Radhi za Allah ziwe
juu yake) amewanukuu Al-Hasan na Qatadah (Radhi za Allah
ziwe juu yao wote) wamesema kuwa; Mbingu haina nguzo
zozote, zinazoonekana wala zisizo onekana.
As Saadi (Rehma za Allah ziwe juu yake) katika kutafsiri kauli ya
Allah (Subhanahu) kuwa; ―Ameziumba mbingu bila ya
nguzo mnazo ziona” amesema kuwa; Allah (Subhanahu)
anapambanua nguvu na ukuu wake kwa waja wake
kuwaonesha baadhi ya ishara zake na miongoni mwa maajabu
ya uumbaji wake na ukarimu wake.
Hiyo ni Qur‘an iliyoshushwa kwa Mtume wa Allah (Subhanahu)
miaka 1400 iliyopita, ambapo baada ya karne kadhaa kupita,
wanasayansi wa kisasa waliipitia na kuitumia aya hii katika
nidhamu za kitafiti. So hivyo tu, bali matokeo ya tafiti zao katika
karne ya kumi na nane yakaja pia kubaini kuwa baina ya
mbingu na ardhi ipo nguvu ya asili ambayo kazi yake kubwa ni
kuzuia maumbile yote ya mbingu na vile vilivyobebwa,
visianguke katika mgongo wa ardhi. Uthibitisho wa hili ulitolewa
na mwanasayansi mashughuri Issac Newton alipokuja na
60
dhana yake ya ―Nguvu za Mvutano‖ kitaalamu inaitwa
“Gravitational Force”
Kwa mujibu wa ugunduzi wa mwanasayansi Issac Newton
anahoji kuwa; umewahi kujiuliza jinsi sayari hulizunguka jua?
dunia inavyouvuta mwezi katika mzunguko wake, na mwezi
unaivutia dunia, kwa hivyo zote hazipaswi kugongana? kwanini
mwezi hauanguki? kwa nini inaendelea kuizunguka dunia? Hoja
hizi zote zinajibiwa na nguvu ya mvutano kati ya mbingu na
ardhi ambazo ndizo hufanya kila kitu kuenda katika utaratibu
ambao Allah (Subhanahu) ameuweka na kuvifanya viwe na
utulivu kwa amri na matakwa yake.
61
halipo kwenye baadhi ya sayari nyengine. (Ndio maana
mara zote wana anga huonekana kuelea bila kugusa chini
wawapo nje ya dunia kwakuwa hakuna nguvu ya
mvutano yani zero gravity)
62
―Je! Huoni jinsi Mola wako Mlezi anavyo kitandaza kivuli. Na
angeli taka angeli kifanya kikatulia tu. Kisha tumelifanya jua
kuwa ni kiongozi wake. (25:45)
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) katika kutafsiri kauli
ya Allah (Subhanahu) aliposema kuwa; “Je! Huoni jinsi Mola
wako Mlezi anavyo kitandaza kivuli.” Amewanukuu Ibn
Abbas, Ibn Umar, Mujahid na wengine wakisema kuwa; Kivuli
katika aya hii kinakusudiwa ni kipindi cha kuanzia mwanzo wa
machweo hadi jua linapochomoza.
63
(Picha kwa hisani ya mtandao wa Science Friday)
64
baada ya Qur‘an kushushwa, kwa hakika angetaka basi
angekifanya kivuli hicho ni chenye kubaki moja kwa moja.
Kwa mfano, ikiwa uko kwenye gari ambalo linatembea kwa kasi
ya kufanana kwenye barabara iliyonyooka, huwezi kujisikia
mwendo mwingi. Walakini, gari linapoongeza kasi au
kupunguzwa kwa mwendo kwa kuzuia breki, unahisi mwendo na
mabadiliko hayo.
65
Qur‘an. Miongoni mwa thibitisho hizo ni kama vile ugunduzi wa
nguvu mvutano (gravitational forces).
66
ْ ج َعل لَّه
ن ِهي ْ َّطلع َعلًَ َق ْىم ل
ْ ًَ ن ْ َ هب ت
َ ج َد
َ س َو
ِ و
ْ ٱلش
َّ ع
َ ط ِل َ َح َّتً إِذَا َبل
ْ غ َه َ
﴾٣١﴿س ْتسا ِ دوًِ َهب
―Hata alipo fika matokeo ya jua aliliona linawachomozea watu
tusio wawekea pazia la kuwakinga nalo.‖ (18:90)
Baadhi ya wafasiri wa Qur‘an (wa karne za sasa) wameitafsiri
aya hii kuashiria maeneo hayo ambayo jua kwa takribani miezi
mitano halizami na kusema kuwa kutokuzama kwa jua ndio
pazia ambalo hawakuwekewa. Ingawaje, wafasiri wengine
wanasema kuwa pazia lilokusudiwa ni nyumba za makazi na
nguo za kujistiri. Hizi zote ni dalili kuwa Qur‘an imeitangulia
sayansi kwa kipindi kikubwa. Maana ni dhahiri kuwa bila ya
uwepo wa utandawazi, ingekuwa vigumu kujua kuwa ipo
sehemu ndani ya dunia hii ambayo wanapitia katika kipindi
ambacho hakuna usiku wenye kiza, kutokana na jua kutozama.
Ametakasika Allah (Subhanahu).
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) katika tafsiri yake,
amesema juu ya kauli ya Allah (Subhanahu) “Wanavyo
zikunjua mbawa zao na kuzikunja” maana yake ni
kwamba; wakati fulani hutandaza mbawa zao kwa upepo
(kuteleza) na nyakati nyengine huzikusanya na kutandaza
(kupeperusha) mbawa wakati wa kuruka. Aidha akasema
kuhusu kauli ya Allah kuwa; “Hawashikilii ila Mwingi wa
Rehema” kuwa maana yake ni kuwa; Allah (Subhanahu)
67
huwainua juu hewani kwa kuwatiishia upepo kwa REHEMA ZAKE
na upole WAKE.
68
na mifupa michache na isiyo na uzito mkubwa ili kumfanya
alingane na kasi ya upepo na hewa iliopo angani. Na kwa
upande wa ndege ulaya, waundaji wakafata nidhamu hii ya
Qur‘an na kuiunda ndege kwa kutumia mali ghafi nyepesi
ambazo huitwa mali ghafi za teknolojia ya juu, pamoja vifaa
vyengine ambavyo vimetayarishwa maalumu kuwa vyepesi.
Wahandisi wa ndege ulaya wanasema kuwa ndege ili iweze
kuruka na kuelea angani ni lazima iundwe kwa kutumia asilimia
hamsini ya mali ghafi hizo nyepesi, asilimia ishirini ya
aluminiamu, asilimia kumi na tano ya titanium, huku asilimia
kumi ya chuma na shaba (hutumika kuunda dhana za kutuwa)
69
(Picha zimepatikana kwenye mtandao wa Google)
70
Kwa upande mwengine, ndege mnyama pia hutumia miguu
yake miwili kukimbia na kuvuta kasi ya kuruka. Mara baada ya
kuacha ardhi hukunja miguu yake ndani ya tumbo lake kwa
hekima na elimu ya Allah (Subhanahu)
71
Kadhalika, nidhamu hiyo hiyo imetumika katika kuunda namna
ambavyo ndege ulaya hutumia matairi (maringi/landing gears)
kutua na kuiwezesha kutembea katika barabara maalumu
(runway). Namna hiyo pia ndivyo ambavyo ndege mnyama
alivyoumbwa na Allah (Subhanahu) kwamba hutumia miguu
yake miwili kusaidia kutua katika adhri. Ndege mnyama huanza
kuifungua/kuifichua miguu yake kutoka katika manyoya ya
tumbo na mbavu zake mara tu anapokaribia kutua katika ardhi.
Jambo ambalo limefanywa kwa nidhamu sawa na hatua za
kiusalama za kutua kwa ndege ulaya. Kwa mujibu wa hatua za
usalama za kutua kwa ndege, inatakiwa inapokaribia wastani wa
baina ya futi 1000 hadi 500 rubani hupaswa kuanza kufungua
matairi kutoka katika sehemu maalumu na kuyaweka tayari kwa
ajili ya kumsaidia kutua kwenye ardhi.
72
Kutokana na haya yote, Je! Bado tunaweza kusema kuwa
Qur‘an imepitwa na wakati kwa kuwa ilishushwa katika karne ya
saba ambayo haikuwa na uwezo wa kugundua na kufafanua kila
nukta za ishara za kisayansi? Kujibu kauli hii, Allah (Subhanahu)
katika ujumbe wa kwanza wa kushushwa kwa Qur‘an alisema
kumwambia Mtume wake;
﴾٥﴿ن
ْ َن يَ ْعل
ْ ًَسبىَ َهب ل
َ ٱإل
ِ نَ ََّعل
‖Kamfundisha mwanadamu aliyokuwa hayajui‖ (96:05)
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) amesema katika
Tafsiri kuwa; Kuna simulizi inayosema, "Yatunze maarifa (Elimu)
kwa kuyaandika." Vilevile, kuna msemo usemao: "Mwenye
73
kutenda kulingana na anachokijua, Allah (Subhanahu) atampa
elimu asiyoijua." Aidha, amesema pia; Allah (Subhanahu)
alimtukuza mwanadamu kwa kumpa elimu, na ni hadhi ambayo
Baba wa Wanaadamu, alitukuka kuliko Malaika.
74
ya majaribio ya kisayansi ambayo yalikuwa takribani miaka 1400
baada ya Qur‘an kushushwa.
―Hata alipo fika baina ya milima miwili, alikuta nyuma yake watu
ambao takribani hawakuwa wanafahamu lolote. Wakasema:
Ewe Dhul-Qarnaini! Hakika Juju-wa-maajuju wanafanya
uharibifu katika nchi. Basi je, tukulipe ujira ili utujengee baina
yetu na wao ngome?‖ (18:93-94)
Baada ya watu hao kutoa maombi yao kwa mja mwema huyo
aliwajibu kile alichojaaliwa na Allah (Subhanahu) kuwajibu
katika utiifu wake, kisha akawapa mbinu bora zaidi za kumlipa
kuliko ujira walio omba. Hapo ndipo ile sayansi ambayo tulianza
kuifafanua ilitumika na baadae wanasayansi wa karne kadhaa
mbele wakaja kuikiri Qur‘an juu ya sayansi hiyo ya Kemia.
75
Qur‘an, karne ya saba ilikuwa inafundisha matumizi ya shaba
katika kukilinda chuma kisipate kutu.
76
(Picha kwa hisani ya mtandao wa Google)
77
Qur‟an na Sayansi ya Milima
Qur‘an haikuacha jambo lolote ambalo linathibitisha ukuu wa
Allah (Subhanahu), Qur‘an imekuwa ni kitabu ambacho
kushushwa kwake kumeleta mapinduzi makubwa ya kielimu
hapa duniani, ambapo wasomi, watafiti na wagunduzi nguli
wamekuwa wakiisoma na kuitumia katika masuala kadhaa wa
kadhaa. Msomi na mtaalamu nguli wa sayansi ya bahari
(Marine Science) Professor Tom Garrison mwaka 2014 aliandika
kitabu chake “Oceanography” ikiwa ni matokeo ya utafiti
wake kuhusu tabia ya milima.
78
maji maji basi upo ewezekano kuwa milima yote huelea kama
zinavyoelea meli baharini.
79
80
Tafiti hii ikaja kupewa nguvu zaidi na ile kanuni ya Akimidi
maarufu ambayo inaelezea vyema namna kitu kinavyoweza
kuelea na kuzama ndani ya chombo chenye kimiminika huku
ujazo ukipima uzito wa kitu.
82
imara chini ya ardhi kwa kazi maalumu ambayo tulishaifafanuwa
hapo awali.
﴾٥﴿ن
ْ َن يَ ْعل
ْ ًَسبىَ َهب ل
َ ٱإل
ِ نَ ََّعل
‖Kamfundisha mwanadamu aliyokuwa hayajui‖ (96:05)
Imam Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) katika tafsiri
yake alisema kuwa kauli ya Allah; “Yeye ndiye amekujaalieni
kupata moto kutokana na mti wa kijani” maana yake kuwa
ni Ikiwa mtu anataka kuwasha moto, lakini hana kitu cha
kuwashia, basi huchukua matawi mawili ya kijani kibichi kutoka
kwa miti na akasugua mti mmoja dhidi ya mwengine, na moto
hutolewa kutokana na miti hiyo.
83
kupata nishati hiyo. Huku ikiwa ni miongoni mwa dalili za ukuu
wa Muumba wao.
84
Allah (Subhanahu) kutokana na hilo akasema;
―Je! Mnauona moto mnao washa? Ni nyinyi mlio uumba mti
wake au Sisi ndio Waumbaji? (56:71-72)
Hiyo ndiyo Qur‘an, hicho ndicho kitabu kitukufu kilicho shushwa
karne ya saba kikiendelea kuwa ni mfano na ufunuo wa elimu
kwa ulimwengu. Je! Bado tunazo hoja za kusema na
kuthibitishwa kuwa Qur‘an imepitwa na wakati?
85
Wafasiri wa Qur‘an wameiangalia kauli hii ya Allah (Subhanahu)
na kuifafanua kwa kina sana. Wakasema kuwa kila nukta katika
kauli hii ina umuhimu mkubwa wa kila kiumbe kiutafakari mara
nyingi juu ya maisha yake kwa ujumla.
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) amesema kuwa kauli
ya Allah kwamba; “katika upeo wa mbali na katika nafsi
zao wenyewe” maana yake ni Allah (Subhanahu)
anamzungumzia mwanadamu na muundo wake wa mwili. Kama
inavyofafanuliwa katika sayansi ya anatomia, ambayo
huonyesha hekima ya Muumba na mielekeo tofauti na asili iliyo
kinyume ambayo watu wanayo, nzuri na mbaya. Na hukumu za
kimungu ambazo mwanadamu ametiishwa nazo, hana uwezo
wa kuzibadili na ambazo hana uwezo nazo.
86
mwili wa kiumbe hai (haswa mwanadamu) kupungua uwezo wa
kuzalisha melanini. Wakasema kuwa miongoni mwa sababu hizo
ni umri kuwa mrefu, hivyo seli hizo hupungua uwezo wa
kuzalishwa na kufanya viungo hivyo; macho, nywele na ngozi
kupoteza ile rangi yake ya asili.
Kwa mfano kadiri melanini inavyopungua kuzalishwa ndani ya
mwii wa mwanadamu ndivyo nywele zake zinavyofanya weupe
(mvi).
Kwa mujibu wa Makala ya mwana anatomia Bing Zhang na
wenzake ya mwaka 2020, wakiwa wanafanya tafiti ya sababu
nyengine ambazo husababisha uhaba wa uzalishwaji wa melanin
ndani ya mwili wa mwanadamu wamesema kuwa; ―Tunapenda
kukiri kuwa, kutokana na tafiti yetu tumegundua kwamba
msongo mkubwa wa mawazo na hofu ya juu inaweza kupelekea
kupungua kwa kiasi kikubwa sana cha uzalishaji wa melanin
ndani ya mwili wa mwanadamu na hivyo kusababisha nywele
kuwa nyeupe.‖
Aidha, kwa mujibu wa jarida la NIH News in Health lililo
andika juu ya sababu za nywele kuwa nyeupe (kutoa mvi)
amesema Dr. Ya-Chieh Hsu wa Chuo Kikuu cha Harvard
kuwa; ―Tafiti inaonesha kuwa msongo wa mawazo na hofu
husababisha kupungua kwa uzalishwaji wa seli za melanin na
mwisho wake kupelekea nywele kuwa na mvi.‖
Hivyo hivyo, Dr. Chieh akaongezea kuwa; hakutegemea kuwa
msongo wa mawazo na hofu unaweza kuwa na athari mbaya
zaidi kwa mwanadamu, kama hii ya kubadilisha muonekano wa
nywele zake ambao utakuwa ni wakudumu. Katika jarida hilo pia
wakaambatanisha picha hii kufafanua zaidi;
87
Kauli ya Allah (SUbhanahu) aliposema kuwa; “Tutawaonyesha
Ishara zetu katika upeo wa mbali na katika nafsi zao
wenyewe” hizi ndizo miongoni mwa ishara zake katika nafsi
zetu wenyewe na ndizo ambazo zinatupaswa kuifahamu Qur‘an
na zinatupaswa kuikiri kwa kauli na vitendo.
88
Ufafanuzi huu wa kauli ya Allah (Subhanahu) unathibitisha
matokeo ya tafiti mbali mbali za wanasayansi wa karne ya
ishirini na ishirini na moja kuwa inapotokea mshtuko, hofu, ama
hangaiko la moyo, basi hata mtoto mchanga anaweza kuota
mvi. Haidhuru, jambo hili hawakuweza kulikubali wanasayansi
hao kabla ya tafiti na majaribio yao kadhaa ya kimazingira na
yale ya kimaabara.
89
Hud, Surat Al-Waqi‘ah na Surat Al-Mursalat, na Surat Nabai na
Surat Quwirrat.‖
90
Qur‟an na Sayansi ya Bahari (Oceanography)
Bahari na Mwangaza wake:
Allah (Subhanahu) amemsimulia Mtume wake kupitia Qur‘an juu
ya uovu wa makafiri, huku akimpigia mifano kadhaa wa kadhaa
ya kufananisha ukafiri wao huo. Aidha, wakati ujumbe huo
ukiwasilishwa kwa njia hiyo ya mifano, Allah (Subhanahu) ndani
ya ujumbe huo akafunganisha ishara na alama muhimu sana za
kisayansi ambazo hadi kufikia karne ya ishirini ndio undani wa
masuala hayo yamekuja kujulikana. Allah (Subhanahu)
amesema ndani ya Surat An-Nur;
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) ameifafanua kauli hii
ya Allah (Subhanahu) na kusema kuwa; ―Makafiri
wanaowalingania wengine ukafiri wao, wakidhani kuwa wana
vitendo na imani nzuri, na hali sivyo hivyo. Mfano wao ni kama
sarabi inayoonekana katika tambarare ya jangwa, ikitazamwa
kwa mbali kana kwamba ni bahari ya kina kirefu, au sarabi
inayoonekana kwenye eneo kubwa la ardhi lililo tambarare
ambalo ndani yake huonekana kama mfano wa maji.‖ Katika
ufafanuzi wa kauli ya Allah (Subhanahu), kuna nukta ya msingi
sana ambayo tunakusudia kuifafanua kwa uchache.
91
Kupitia kanuni za kifizikia wakafafanua zaidi na kusema kuwa
katika hali fulani, kama vile sehemu ya lami au hewa ya
jangwani inayochomwa na jua kali, hewa hiyo hupoa kwa kasi
kwa mwinuko na hivyo huongeza msongamano na nguvu ya
kuakisi. Mwangaza wa jua unaoakisiwa kuelekea chini kutoka
sehemu ya juu ya kitu—kwa mfano, sehemu ya juu ya ngamia
jangwani—itaelekezwa kupitia hewa baridi kwa njia ya kawaida.
92
Dr. Philips msomi na mbobezi wa masuala ya mazingira ya
bahari alishangaa na kustaajabu kuona Qur‘an iliyoshushwa
karne ya saba imezungumzia kwa kina juu ya sayansi ya bahari.
Sayansi ambayo iliwaharimu watafiti na wasomi wa sayansi
takribani miaka elfu moja kuifahamu. Baada ya matumizi
makubwa ya vifaa vya hali ya juu huku mamilioni ya fedha
yakitumika katika kuijua na kuitafiti bahari na sayansi yake,
ndipo wakaifahamu kwa uchache.
93
Kwa mujibu wa mtandao huo pia wanasema kuwa; ―Matumizi na
utambuzi wa bahari umeongezeka katika karne ya ishirini na
ishirini na moja, na teknolojia ya kisasa ya kompyuta imesidia
kuwawezesha wanasayansi kupima mali inayopatikana ndani ya
bahari kwa kiwango cha kimataifa.‖ Takwimu zinatuonyesha
kuwa asilimia sabini (70%) ya dunia ni bahari, na wanasema
kuwa bahari ndio sehemu ambayo imehifadhi viumbe hai vingi
zaidi ya ardhi.
94
Bahari ni maji, na maji ni uhai. Allah (Subhanahu) amesema
ndani ya Qur‘an;
―Na tukajaalia kutokana na maji kila kilicho hai.‖ (21:30)
95
Kwa mujibu wa Tom Garrison katika kitabu chake cha Sayansi
ya Bahari amesema kuwa; Katika sehemu kubwa ya bahari,
eneo la uso (au safu iliyochanganyika) yenye joto kiasi, maji
yenye msongamano wa chini hufunika safu inayoitwa
pycnocline. Msongamano unaongezeka haraka na kina katika
pycnocline. Chini ya pycnocline kuna kina kirefu eneo la maji
baridi, mazito - karibu 80% ya jumla ya kiasi cha bahari.
96
chini kwenye tabaka lengine ndivyo ambavyo nuru ya
mwangaza inavyopotea.
97
mwangaza wa asili kabisa. Viumbe wanaoishi katika ukanda huu
ni bioluminescent; yaani wanazalisha na kutoa nuru yao
wenyewe.
99
kwamba yametenganishwa na mpaka usioonekana huku kila
moja ikiwa na aina yake ya viumbe hai na matumbawe. Baadhi
ya wanasayansi wa bahari wanasema kuwa ukuta huo usio
onekana baina ya bahari mbili hutokea pale tu bahari hizo
zinavyotofautiana katika wingi wa chumvi mara tano au zaidi.
Ufafanuzi huu wa Mr. Jacques umekuja kuikiri Qur‘an pale Allah
(Subhanahu) aliposema;
―Nae ndie alie zipeleka bahari mbili, hii tamu mno, na hii ya
chumvi chungu. Na akaweka baina yao kinga na kizuizi
kizuiacho.‖ (25:53)
﴾٥﴿ن
ْ َن َي ْعل
ْ ًَسبىَ َهب ل
َ ٱإل
ِ نَ ََّعل
‖Kamfundisha mwanadamu aliyokuwa hayajui‖ (96:05)
100
Qur‟an na Sayansi ya Hyndrolojia (Mzunguko wa Maji)
Allah (Subhanahu) amesema ndani ya Qur‘an kuwa;
―Na tukajaalia kutokana na maji kila kitu kuwa hai.‖ (21:30)
Nidhamu na Imani juu ya umuhimu wa maji haiwezi kupingika
katika dunia. Viumbe, mimea pamoja na ardhi huhitaji maji
katika ustawi na maendeleo ya makuzi. Maji yamekuwa ni
kiungo muhimu cha uhai wa viumbe wote duniani, kuanzia
wanadamu, mimea, wanyama na hata baadhi ya shughuli mbali
mbali za kiuchumi na kimaendeleo.
Huenda kutokana na umuhimu wake (maji) ndio sababu kubwa
ambayo iliwafanya watafiti na wasomi kutaka kufahamu zaidi
juu ya asili na mzunguko wa maji. Kutokana na jitihada za
kuyafahamu maji kiundani, wasomi na watafiti wakaja na
nidhamu maalumu ya kielimu ambayo itajikita moja kwa moja
katika kuyafahamu maji kuanzia asili, hadi namna ambavyo
yanavyoleta manufaa kwa viumbe kwa ujumla.
Wasomi hao wakaja na fani ya ‗Hyndrolojia‘ ambayo inasemwa
kuwa ni utafiti wa usambazaji na harakati za maji juu na chini ya
uso wa dunia, pamoja na athari za shughuli za binadamu juu ya
upatikanaji wa maji hayo. Kupitia tafiti hizi za hyndrolojia
mnamo mwaka 1580 mtafiti mmoja aliyeitwa Bernard Palissy
alikuwa mtu wa kwanza kueleza dhana ya siku hizi ya
‗mzunguko wa maji‘. Yeye alielezea jinsi maji yanavyovukiza
(Evaporate) kutoka baharini, kupoa na kutengeneza mawingu.
Mawingu yakapandishwa kisha kugandana na kuanguka kama
mvua.
101
Kabla ya hapo hakuna miongoni mwa wanasayansi ambae alijua
kwa uwazi juu ya vyanzo mbali mbali vya maji yatokayo chini ya
ardhi. Wote waliamini kuwa maji yapatikanayo ndani ya bahari
ndio yanayopenya na kutawanyika nchi kavu (barani), cha
kushangaza zaidi hata wale wasomi na manguli wa sayansi
ambao walipewa vyeo na utukufu wa kuwa ni watu wenye
uwezo mkubwa wa kufikiria, pia waliamini katika dhana hizi.
102
Qur‘an kupitia aya hii ilifundisha fani ya hyndrojia ya maji,
ilifungua mwangaza wa kuonyesha namna vyanzo mbali mbali
vya maji vinavyopatikana. Ikiwa ni fani ya elimu ambayo
imekuwa ikisomwa na kufanyiwa tafiti kwa zaidi ya miaka elfu
moja. Allah (Subhanahu) anaeleza pia ndani ya Qur‘an kuwa;
‖Na hukuteremshieni maji kutoka mbinguni, na kwa hayo
huifufua ardhi baada ya kufa kwake. Hakika katika hayo zipo
ishara kwa watu wanao zingatia.‖ (30:24)
103
ardhi kuyahifadhi ndani yake ili mbegu, mimea na chemchem
ziweze kupatikana.
104
Qur‟an na Sayansi ya Alama za Vidole
―Na (taja) aliposema Ibrahim: ―Rabb (Mola) wangu nionyeshe
vipi Unahuisha wafu?‖ (Allah) Akasema: ―Je kwani huamini?‖
Akasema: ―La! (Naamini) lakini moyo wangu utumainike.‖
(Allah) Akasema: ―Basi chukua ndege wanne wazoeshe kwako,
(kisha uwachinje), kisha weka juu ya kila jabali katika hao
(ndege) sehemu yao; kisha waite watakujia mbio (ukiwaona
wanavyoumbika); na jua kwamba hakika Allah ni ‗Aziyzun-
Hakiym (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika - Mwenye hikmah
wa yote)‖. (02:260)
105
wanakuja mbele ya Ibrahim wakitembea haraka kuelekea
kwake, lengo ni ili Ibrahim ashuhudie kwa dhahiri kuhuishwa
kwa ndege hao na apate matumaini ya uweza wa Allah
(Subhanahu).
107
ambavyo kila kiumbe katika huu ulimwengu anao utofauti
kutokana na kiumbe mwengine.
108
Uislamu unatufunza na kututhibitishia kuwa kila jambo ambalo
limekatazwa kupitia mafunzo yake basi huwa na madhara
makubwa kwa viumbe. Hivyo kupitia misingi hiyo tunahimizwa
kujiweka nayo mbali ili tuweze kuwa na mafanikio ya kidunia
pamoja na mafanikio makubwa mbele ya Allah (Subhanahu).
Kutokana na ukweli kuwa Qur‘an ilishushwa na makatazo ya
muziki katika karne ya saba, walio wengi miongoni mwa
wanadamu hawakujua athari zake. Wengi waliamini na
kuchukua nidhamu ya kuacha kila ambacho kimekatazwa na
Qur‘an huku ikiaminika kuwa na athari japo kuwa kwa wakati
huo upeo wa kutambua athari zake haukuwa wazi sana.
109
Tom, akaendelea kufafanua kuwa hisia za mwanadamu,
mawazo na matokeo ya hisia, yote yapo katika mfumo wa
mtetemeko wa sauti ndani ya ubongo. Ndio maana mtu
anapokuwa macho (hakulala) akili yake hutenda kwa mujibu wa
hisia, mawazo ama maelekezo. Bali hali hiyo huwa tofauti
endapo mtu huyo anapokuwa amelala, kwakuwa hakuna
maingiliano ya sauti, hivyo akili ya mtu huyo haiwezi tena
kudhibiti mawazo, hisia na matendo kwa kipindi chote cha kulala
kwake.
110
wa Muziki na Ala Duniani ulitoa mapendekezo ya kubadilisha
masafa ya 432 Hz na kuwa 440 Hz.
111
Kutokana na ufafanuzi huo, Bwana Cross aliulizwa na mwandishi
kuwa; anahisi kwamba mabadiliko ya masafa hayo ya muziki
duniani yanayo mpango maalumu tofauti na wa kitaaluma ya
muziki? Alijibu kuwa; Ukweli ni kwamba kila mtu (wataalamu wa
muziki) anayo dhana yake katika jambo hilo!
112
Kadhalika, wapo miongoni mwa watafiti wa masuala ya muziki
na ala wanaosema kuwa mabadiliko ya masafa ya muziki kutoka
masafa ya 432 Hz kwenda 440 Hz yametokana na kusababishwa
na familia tajiri na yenye ushawishi mkubwa katika dunia ya
Rockefeller. Ambapo inasemwa kuwa walitaka kuutumia muziki
kuhakikisha maslahi yao katika akili za wafuasi wao. Baada ya
ufafanuzi huu, Bwana Cross aliulizwa pia juu ya maoni yake
katika kuutumia muziki kuwashawishi na kuwatawala watu
kihisia na kiakili. Alijibu kwa kusema kuwa miziki unaweza
kutumika kubadilisha matendo na tabia ya mtu. Na kwa
uthibitisho juu ya dhana hiyo, alisema kuwa unaweza kuenda
katika vituo maalumu vya tiba ya akili vinavyotumia miziki
maalumu kuwasaidia wagongwa kupata utulivu akili na nafsi
kutokana na wasiwasi.
113
Ndio maana kila kikosi cha wapiganaji kinao wimbo wa kishujaa
na kujaza morali ya mapigano ama maandamamo. Kwa
kuongeza akasema pia, tunaona hata vikundi vya mazoezi
namna ambavyo hutunga nyimbo kadhaa za kuongeza morali
wakati wa mazoezi kwa kuamsha hisia za ari na kupandisha
kiwango cha nguvu ya mwili na akili. Si hivyo tu zipo nyimbo
ambazo hutumika katika maandamano ambazo zimeundwa
kujenga ujasiri na kuondoa hofu na uoga hata kama kutakuwa
na vizuizi vya nguvu na dola.
114
Mwandaaji mashughuri wa muziki duniani Bwana Guiseppe Vardi
alikuwa ni muungaji mkono mkuu wa masafa ya 432 Hz na ndio
maana masafa hayo pia huitwa ‗Vardi‘s La‘. Inaaminika kuwa
ndio falsafa ya asili yenye mrindimo wa uhakika wa kihisabati
ambao huenda sambamba na mtetemeko wa ulimwengu.
Uwiyano huo, kwa mujibu wa wanasayansi wa Ulimwengu
wanaamini kuwa ndio masafa sawa na masafa ya sumaku
umeme ya dunia.
115
wengi waliamini na kuaminishana hapo awali, bali yanathibitisha
kuwa ni maneno matukufu kutoka kwa mtukufu.
116
(Rehma za Allah ziwe juu yake) amesema “wanao nunua
maneno ya upuuzi” ni wale ambao wanajiweka mbali na kuipa
mgongo Qur‘an, na wasio faidika na maneno ya Allah
(Subhanahu) badala yake, hugeukia kusikiliza zumari na nyimbo
ambazo zimeambatana na ala za muziki.
117
Allah (Subhanahu), na pili hupelekea katika matamanio ya
mambo maovu haswa katika uzinifu. Aliongeza pia; Iblisi alikata
tamaa baada ya kuona waumini wameacha na kujiepusha na
kusikiliza na kuimba nyimbo zenye ala za muziki. Alipoona hivyo,
aliwaletea nyimbo badala yake ambazo hazitumii ala za muziki.
Jambo ambalo liliwasogeza taratibu kutoka katika kusikiliza
nyimbo zisizo na ala za muziki, hadi kuwarejesha tena katika
kuimba na kupiga miziki na ala mbali mbali.
119
Wanasayansi wanakisia kuwa zipo aina takribani milioni 8.7 za
viumbe hai katika dunia. Aidha, inakisiwa pia, kuwa kati ya
milioni moja hadi mbili za viumbe wote hai duniani ni wanyama
na wadudu wengine.
120
ya wanyama ilifafanuliwa katika karne ya saba miaka takribani
elfu moja kabla ya matokeo ya tafiti ya Aristotle ambaye
inaaminika kuwa ndiye „Baba wa Sayansi ya Wanyama‟.
Qur‘an katika kufafanua taaluma hii, kwanza ilianza kueleza
kuwa wanyama nao ni viumbe na ni mkusanyiko wenye
mchanganyiko wa aina mbali mbali za viumbe wenye aina,
tabia, na maumbile tofauti, Surat Al-An‘am;
―Na hapana mnyama katika hii ardhi, wala ndege anayeruka
kwa mbawa zake mbili, ila ni umma kama nyinyi. Hatukupuuza
kitabuni kitu chochote. Kisha kwa Mola wao Mlezi
watakusanywa.‖ (06:38)
121
inathibitisha juu ya elimu juu ya sayansi ya wanyama (Zoology)
kuanzia chakula cha kila aina ya wanyama, uzazi na makuzi yao.
Na hii ilitosha kuwa ni ishara na ufafanuzi wa kuwawezesha
wanasansi wa karne za sasa kupata mwanzo mzuri wa kigunduzi
katika kujua tabia za wanyama.
123
Kadhalika, akafafanua kuwa kwa kauli ya Allah (Subhanahu)
kuwa; “Na manufaa mengineyo, na baadhi yao mnawala”
amesema maana yake ni kinywaji cha maziwa kinachopatikana
kupitia wanyama hao, na nyama inayopatikana kutokana na
baadhi ya wanyama hao walioruhusiwa kuliwa. Kupitia Aya hizi
pia Allah (Subhanahu) anaendelea kutoa mafunzo juu ya sayansi
ya wanyama katika kubainisha matumizi yao katika kumsaidia
mwanadamu kubeba mizigo mizito ambayo bila ya msaada huo
ingelikuwa tabu kufanikiwa.
124
Unaweza kuona hapa namna ambavyo Qur‘an inaendelea kutoa
ufafanuzi juu ya aina nyengine za wanyama ambao matumizi
yao yametofautishwa na lile kundi la kwanza. Kundi hili likawa
na madhumuni ya kutumika kama msaada wa usafiri kuwabeba
watu na mali zao. Mbali na wanyama hawa wakubwa, Qur‘an
imefafanua pia tawi jengine la zoolojia kwa kuelezea aina tofauti
za wadudu na ndege. Kama ambavyo Qur‘an imemtaja na
kumuelezea kwa kina mdudu Nyuki (16:68), Buibui (29:41),
Mdudu Chungu, mbu (2:26), Nzi (22:73) na hata samaki wa
baharini (5:96, 18:61, 37:142). Na huu ndio Umma wa
wanyama na wadudu na hivyo ndivyo ambavyo Qur‘an
imeifafanua elimu juu ya wanyama na mazingira yao ili iwe ni
ubainifu kwa viumbe na Rehema kwa wenye kutafakari.
126
As-Saad (Rehma za Allah ziwe juu yake) amesema akifafanua
juu ya makatazo ya nyama za mzoga amesema kuwa kusudio la
makatazo haya ni kuwa nyama ya mzoga sio salama kwakua
mtu hajui sababu za kufa kwa mnyama huyo, na huenda sababu
ya kifo ni kutokana na maradhi ambayo huenda yakampata yule
mwenye kula nyama hiyo. Hivyo hivyo, akaeleza kuwa na damu
ya mnyama huwa na madhara makubwa kwa mnywaji.
127
Aidha, wamesema kuwa unywaji wa damu huongeza kiwango
cha madini chuma ndani ya mwili na kufikia kiwango cha juu
ambacho hakihitajiki ndani ya mwili, na hupelekea kusababisha
magonjwa mengi sugu kama vile shindikizo la damu, magonjwa
ya ini, magonjwa ya viungo na uharibifu wa mfumo wa kinga ya
mwili. Matokeo haya yamekuja baada ya kugundulika viini
hatarishi ambavyo hubaki kuwa hai kwa kipindi kirefu ndani ya
damu.
128
huingizwa moja kwa moja katika mishipa ya muhitaji, hivyo
haipiti katika mzunguko wa kawaida wa chakula. Na hata hivyo
inasisitizwa kuwa kabla mtu kuongezewa damu ni lazima
ifanyiwe vipimo vya usalama wa maradhi kadhaa wa kadhaa.
Damu chanzo muhimu sana cha vinasabata vyote vya
binadamu, makatazo yake kwa mujibu wa sayansi ya tiba
yamefafanua athari zake ikiwa ni pamoja na uwezekano wa
kupandikiza vinasabata ambavyo ni huenda vikakinzana na vile
vinasaba vya asili vya mtu. Tunashuhudia wimbi kubwa la
ongezeko la maradhi mengi duniani, huku watafiti wa masuala
ya afya na tiba wakiyaelekeza moja kwa moja kuwa chanzo
chake ni muingiliano wa damu. Matokeo haya ya kitafiti na
kisayansi yamekuja kuonyesha ulimwengu kuwa kila jambo
ambalo limekatazwa na Qur‘an basi zipo sababu za msingi juu
ya makatazo yake kwa viumbe.
129
Kama ambavyo Sayansi imeendelea kuikiri Qur‘an katika
masuala mbali mbali, Mwanasayansi wa tiba ya wanadamu
Profesa Dana Hunnes wa Chuo Cha Nadharia na Vitendo vya
Afya ya Jamii cha Marekani alisema akihojiwa na jarida la ZME
Science (2023) alisema; ―Sitapenda kushauri ulaji wa mazao
ya wanyama, na kwa msisitizo kabisa ulaji wa nyama ya
nguruwe.‖ Akaongeza kuwa miongoni mwa sababu za kusema
maneno hayo ni kwamba nyama ya nguruwe imesheheni
kiwango kikubwa cha mafuta na lehemu.
130
Kwakuwa Allah (Subhanahu) ndio muumbaji wa kila kiumbe hai,
na ndie anaejua kipi ni manufaa na salama kwa waja wake, na
kipi si salama, aliweka muongozo kupitia Qur‘an juu ya ulaji wa
vyakula na wanyama kama ilivyokuja ndani ya Surat An-Nahl;
―Basi kuleni katika vile alivyo kupeni Allah, vilivyo halali na
vizuri.‖ (16:114)
133
kurejesha damu iliyopotea wakati wa kujifungua. Vilevile, tende
inawingi wa madini ambayo huchochea na kusaidia kutatua kuta
za njia za uzazi ambazo huzalishwa kutoka katika tenzi ya
pituitary, pamoja na faida nyingi nyengine ambazo
imefafanuliwa na wanasayansi.
134
135
Amri ya Ibada ya funga na faida zake kiafya:
Mbali na makatazo, Qur‘an imebainisha masuala na mambo
mbali mbali ambayo iliyafanya kuwa ni wajibu kwa kila kiumbe
kuyatekeleza, katika hayo zikawemo ibada, pamoja miamala
mengi mengine ambayo baada ya muda mrefu kupita ndipo
ulimwengu ulikuja kubaini umuhimu na faida zake kwa mtu
mmoja mmoja na jamii kwa ujumla. Kupitia maamrisho mengi,
zilibainika faida lukuki kwa viumbe na umma katika nyanja
tofauti, kama vile kiimani, kiafya na kijamii.
136
na madhumuni makuu ya ibada ya funga ikiwa ni kumuwezesha
mfungaji kuufikia ucha Mungu kupitia kujizuia kula, kunywa na
vyote ambavyo huweza kumfuturisha mfungaji, kama ilivyokuja
ndani ya Surat Al-Baqara Allah aliposema;
―Enyi mlio amini, mumeandikiwa kufunga kama walivyo
andikiwa walio kuwa kabla yenu ili mpate kuwa wacha Mungu.‖
(02:183)
137
Kwa mujibu wa Dokta Eric Berg (DC) mtaalamu wa masuala ya
mfumo wa mmeng‘enyo wa chakula wa mwanadamu, ameeleza
katika Makala yake „My Opinion on Fasting Ramadhan and
Immune system‟ yani „Mtazamo wake juu ya kufunga
mwezi wa Ramadhan na kinga ya mwili‟ alisema; mtu
anapofunga hupelekea kupungua kwa uzalishaji wa cytokines
ambazo hutumika kusafirisha mionzi ya kemikali ndani ya kinga
mwili ya mwanadamu, kemikali ambazo kwa kiasi kikubwa ndizo
husababisha uundwaji wa vivimbe ndani ya mwili.
138
Dokta Eric aliongeza kueleza na kufafanua faida nyingi za funga
ikiwa ni pamoja na kuchochea kwa kiasi kikubwa mmeng‘enyo
wa chakula, kupunguza na kuzuia msongo wa mawazo,
kuusaidia mwili kuzalisha vitoa taka mwili (Anti-Oxidants). Elimu
na ujuzi juu ya faida hizi umekuja baada ya maendeleo ya
sayansi na teknolojia, maendeleo ambayo yaliwezesha kufikiwa
kwa kupitia tafiti mbali mbali za kutambua na kuainisha matokeo
ya funga kwa kiumbe hai.
140
mwanadamu hufanya kazi katika kiwango chake cha juu, kiasi
ambacho hata uchovu wa kufunga huondoka moja kwa moja.
Katika kuthibitisha juu ya ufafanuzi huu wa hatua hizi za
mabadiliko katika mwili wa mwandamu yanayoelezewa na
funga, Imekuja katika Sahihi Bukhari kuwa; ((―Alikuwa Nabiy
(Rehma na Amani ziwe juu yake) linapoingia kumi la mwisho la
Ramadhani; alikuwa akikaza shuka lake. (Yani akijibidiisha
katika kutenda mema) na kujiweka mbali za wake zake, na
akihuisha usiku kwa kufanya ibada na akiamsha ahli zake.‖))
Hadithi hii inaweza kutumika kututhibitishia namna ambavyo
mwili hupata nguvu, kuongezeka kwa umakini katika hatua ya
tatu ya kipindi cha funga.
141
Juhudi hizi zimekua zikilenga kuhakikisha kuwa mtoto anapata
nafasi adhimu ya kunyonya maziwa halisi ya mama kwa kipindi
ambacho wataalamu wa afya wamekipendekeza. Shirika la Afya
Duniani (WHO) wamekua wakitoa miongozo ya mara kwa mara
juu ya unyonyeshaji sahihi wa watoto huku ikilenga maslahi
mapana ya afya ya mtoto na mama kwa ujumla. Shirika hilo
limekua likitumia njia mbali mbali katika kushajihisha, ikiwamo
kuanzishwa kwa siku maalumu ya unyonyeshaji duniani. Lengo
likiwa ni kuueleza ulimwengu juu ya umuhimu wa
kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama kwa kipindi cha miaka
miwili ya mwanzo.
142
uwezekano wa kupata pumu na ugonjwa wa mzio (allergies), na
pia hupunguza uwezekano wa mtoto kupata matatizo ya
masikio, mfumo wa upumuaji na kuharisha.
143
Ulimwengu wa karne ya ishirini na moja umekuwa ukionekana
kuwa na mwanga mkubwa wa kielimu huku ikionekana bila
kuwa na wataalamu na watafiti hawa, faida nyingi zisingeweza
kuonekana.
144
Baadhi ya wanachuoni wakaeleza kuwa sharti la baba wa mtoto
kumtunza mama mwenye kunyonyesha kwa chakula na mavazi
ni kwasababu ya umuhimu wa kitendo cha kunyonyesha kwa
mama kwa mtoto wake. Mbali na kuwa kunyonyesha
kunamfanya mtoto kuchukua vinasaba kadhaa kutoka kwa
mama huku ikiwa ni njia nzuri ya kutengeneza maingiliano ya
kihisia na kinasaba baina ya mama na mtoto.
145
ajili ya kutoa msaada wa haraka na kusambaza wanajeshi na
vifaa mbali mbali. Kutokana sababu kadhaa za kulinda anga
katika uwanja wa vita, mwaka 1914 ndege maalumu za kivita
zilivumbuliwa. Kwa mujibu wa mtandao huo, matumizi ya ndege
za kivita zilianza kuchepua zaidi katika vita ya pili ya dunia.
Ndipo ndege kadhaa za kivita ziliundwa kwa malengo tofauti,
kama vile kulinda anga, kuongeza mbinu na mikakati ya kivita,
hadi kuwa zana imara ya kukubebea mizinga na mitutu ya
maangamizi.
146
(Ndege za kivita zisizo na rubani – Drones)
148
kutumia zana za ulinzi za anga kupigana na adui mwenye zana
nzito za ardhini. Abraha alimiki wanajeshi na akamiliki wanyama
wakubwa na wenye nguvu. Lakini Allah (Subhanahu) akatumia
mbinu ya anga kwa kuwatumia wanyama wadogo (ndege)
wakiwa na silaza nzito za maangamizi.
Allah (Subhanahu) anasema ndani ya Surat Al-Fil;
‖Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyowatenda wale
wenye tembo? Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika? Na
akawapelekea ndege makundi kwa makundi. Wakiwatumia
mawe ya udongo wa motoni, Akawafanya kama majani
yaliyoliwa na kutemwa? (105:1-5)
149
(Ndege za kivita zikiwa zimefatana katika kikundi)
150
Qur‘an inathibitisha kuwa ndege walioshambulia jeshi la ndovu
walitokea baharini. Tunawezaje kupingana na hili wakati mara
nyingi tunashuhudia kwenye mitandao tukiona mipango kadhaa
ya kivita kutumia ndege zikianzia kwenye manuari ya kijeshi
baharini na kuelekea katika uwanja wa vita.
151
Tunafahamu namna ambavyo ndege za kivita zinavyotumika
kushambulia, zote husafiri kuelekea kwenye uwanja wa vita kwa
kasi sana huku zikiwa zimebeba silaha hatari katika tumbo la
ndege hizo. Hutumia kifaa maalumu kuachia na kurusha silaha
hizo katika eneo kusudiwa.
152
(Ndege za kivita zikishambulia kwa kurusha makombora)
153
Hivyo, kwa mujibu wa wataalamu hao, chanzo kikuu cha
mgawanyiko wa mabara ni tetemeko kubwa la ardhi ambalo
lilitokana na nguvu za asili, ambapo matokeo ya tetemeko hilo
ikaigawa ardhi katika mapande kadhaa ambayo baadae mipaka
ya nchi mbali mbali iliundwa, ambazo kwakutumia mgawanyiko
huo zilitambulika na kutofautishwa na nchi nyengine.
Kwa mujibu wa mtandao wa California Academy of Science
kupitia jarida lake la Plate Tectonics: Shaping the
Continents (2019) wanasema kuwa kwa takribani miaka
bilioni moja, dunia imekua ikiendelea kubadilika kutokana na
mzunguko wa sahani ya dunia ambayo huzunguka na kuigawa
katika matabaka tofuti kwa mujibu wa nguvu ya asili. Mzunguko
huo wa sahani ya dunia ulianza kwa kuigawa ardhi ya dunia
katika bara moja kubwa ambalo lilizungukwa na bahari moja
kuu. Kwa mujibu wa jarida hilo wanasema kuwa baada ya miaka
150, bara hilo kubwa likaendelea kugawika na kuigawa bahari
katika mabara mengine tofauti ambayo yote yalitokana na
mtetemeko wa ardhi.
154
Wataalumu wa masuala ya jolojia wanasema kuwa chanzo kikuu
cha tetemeko la ardhi ni nguvu ya asili ambayo hutokana na
msuguano na msigano wa miamba chini ya ardhi, pale ambapo
muhimili wa ardhi unaposhindwa kuzuia mgandamizo huo, ndipo
hutokea mpasuko na msigano wa sahani ya ardhi na kuzalisha
mtetemeko.
Sayansi inathibitisha kuwa msuguano na msigano wa miamba
ya chini ya ardhi husababisha mtetemeko wa sehemu ya juu ya
ardhi pamoja na mpasuko na uharibifu mwengine kulingana na
kiasi cha mtetemeko huo. Jambo ambalo si katika ugunduzi wa
kushangaza katika jicho la Qur‘an, kwani Allah (Subhanahu)
anasema ndani ya Qur‘an;
―Na ameweka katika ardhi milima ili ardhi isikuyumbisheni.‖
(31:10)
Tunatambua kuwa milimia imefanywa kama ni vigingi yenye
mashina chini ya ardhi ambayo kazi yake kubwa ni kuifanya
ardhi kuwa tulivu na kuhimili misuguano ya miamba chini yake.
Ahadi ya Allah (Subhanahu) juu ya kuifanya milima kuwa ni
mihimili ya ardhi haiwezi kuwa sababu ya kuzuia matetemeko
ambayo yamekadiriwa kutokea na Muumba ambae ameifanya
milima hiyo kuwa mihimi yake.
155
Allah (Subhanahu) anasema ndani ya Surat Az-Zalzala;
―Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake! Na
itakapotoa ardhi mizigo yake!‖ (99:1-2)
Ibn Kathir (Rehma za Allah ziwe juu yake) amefafanua juu ya
tetemeko lililotajwa ndani ya aya hiyo na kusema kuwa hilo ni
tetemeko la mwisho ambalo litaikumba dunia na viumbe kwa
ujumla. Aidha, ameendelea kueleza kuhusu kauli ya Allah
(Subhanahu) “Na itakapotoa ardhi mizigo yake” amesema
kuwa maana yake ni matokeo ya mtetemeko huo ambao
utawatoa maiti na kila kilichozikwa ndani ya tumbo la ardhi.
Qur‘an imelielezea tukio hilo pia katika Surat Al-Hajj na kulitaja
kama ni tukio la hatari na kuogofya kama ilivyokuja;
―Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi. Hakika tetemeko la saa
(Kiyama) ni jambo kuu.‖ (22:1)
Allah (Subhanahu) akasema juu ya matokeo ya tetemeko hilo
kuwa;
―Siku mtapo liona (tetemeko), kila mwenye kunyonyesha
atamsahau amnyonyeshae, na kila mwenye mimba ataharibu
mimba yake. Na utaona watu wamelewa, na kumbe
hawakulewa. Lakini adhabu ya Allah ni kali.‖ (22:2)
Imam Al-Fawzan (Allah amhifadhi) wakati akilolea ufafanuzi juu
ya aya zilizoelezea habari ya tetemeko alisema kuwa; Kauli ya
Allah (Subhanahu) juu ya tetemko hilo, inaelezea kile
kitakachotokea wakati wa tukio la Kiyama, ardhi itatetemeka,
itapasuka na kuangusha mapande mapande, na kutengeneza
nyufa zilizo wazi. Mtetemeko huo utaonekana kwa vishindo
vyake na ardhi kukosa utulivu uliozoeleka. Kadhalika, kuhusu
ardhi kutoa mizigo yake, Imam Al-Fawzan (Allah amhifadhi)
amesema kuwa; ardhi itatoa kila kilichomo ndani ya yake
ikiwamo miili ya wafu na mali (madini) yote yaliomo ndani yake.
Historia za matetemeko ya ardhi duniani inatueleza kuwa tukio
la kwanza la tetemeko ambalo lilishangaza dunia lilitokea
mnamo mwaka 1831 kwa mujibu mtandao wa „Science for
156
Changing World‟ ambao kwa kutumia tafiti kadhaa
zilizowezeshwa na vifaa vya kisasa, waliweza kutambua na
kusoma historia za matetemeko. Kadhalika matokeo kadhaa ya
misuguano ya ardhi yanaonekana katika mgongo wa ardhi. Hivi
karibuni tumeshuhudia mpasuko mkubwa katika bonde la ufa
ambalo unagawa baadhi ya nchi za Afrika mashariki kama vile
Kenya, Tanzania, Uganda na Burundi ukiendelea kutanuka huku
wanasayansi wakisema kuwa ni matokeo ya msuguano wa
ardhi.
157
Hizi zote ni sehemu na mifano wa matokeo ya matetemeko
ambayo yameelezwa ndani ya Qur‘an. Mbali na matukio kadhaa
wa kadhaa ya matetemeko ambayo tunayashuhudia katika
kipindi cha sasa, huku matetemeko hayo yakiacha athari kubwa
za mali na kugharimu uhai wa viumbe wengine. Kila nukta
katika maisha juu ya mgongo wa ardhi ni sehemu ya mazingatio
na funzo ambalo kiumbe hupaswa kujipa tahadhari juu ya
uwepo na ukuu wa Allah (Subhanahu). Matokeo yaliyofafanuliwa
ndani ya Qur‘an karne ya saba kisha sayansi kuja kuyakiri baada
ya karne ishirini kupita, pia ni sehemu ya mazingatio ambayo
kila mwanadamu anapaswa kuzingatia na kuchukua faida ndani
yake.
Qur‟an na Sayansi ya Mwisho wa Ulimwengu (The Big
Crunch Theory)
Sayansi, pamoja na wanasayansi wanakiri na kukubali kuwa
ulimwengu na vilimwengu vyote viliumbwa, kinyume na
mitazamo na dhana zao za awali kuwa ulimwengu ulitokea
kutokana na uoto wa asili usio na muumba wala mwenye
kuusimamia. Kwa mujibu wa tafiti na mijadala ya muda mrefu
ambayo ilionekana kukataa ukweli juu ya umbwaji wa
ulimwengu. Matokeo ya tafiti na mijadala hiyo ikazalisha dhana
maarufu Big Bang ambayo inakubalika na kundi kubwa la
wanasayansi wa karne ya ishirini na ishirini na moja, haswa wale
wabobezi wa masuala ya anga za mbali.
Dhana hiyo inayothibitisha (kwa mitazao ya kisayansi) kuwa
ulimwengu uliumbwa kutoka katika asili ya umbile moja la gesi
mgando, ambayo baada ya kutokea mripuko mkubwa (The Big
Bang) ukalitenganisha umbile hilo na kupatikana mgawanyiko
wa ardhi na mbingu, na baina ya hivyo zikawepo nyota, sayari
na maumbile mengine ambayo yamejenga ulimwengu (The
Galaxy). Dhana hii ikawa ni matokeo makubwa ya kuufahamu
ulimwengu na asili yake, ambayo yalipatikana karne kumi na
nne baada ya kushushwa kwa Qur‘an tukufu. Qur‘an ambayo
ndiyo iliyowafungua macho na maono ya kuweza kuifahamu asili
ya uhakika ya kuumbwa kwa ulimwengu.
158
Allah (Subhanahu) katika karne ya saba, alifafanua masuala
yote ya kuumbwa kwa ulimwengu, huku akieleza kwa kina juu
ya hicho ambacho kimeitwa mripuko mkubwa (The Big Bang)
wakati ambao wanasayansi hawakua na elimu yoyote kuhusu
habari hizo. Allah (Subhanahu) akasema ndani ya Qur‘an kuwa;
―Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi
zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabadua? Na tukajaalia
kutokana na maji kila kitu kuwa hai? Basi je, hawaamini?
(21:30)
Allah (Subhanahu) amesema pia;
―Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi,
vyote katika anga vinaogelea katika mihimili yake‖ (21:33)
Kutokana na uthibitisho wa Qur‘an juu ya kuumbwa kwa
ulimwengu katika maumbile ya ardhi na mbingu, ndiyo ambayo
yaliwafanya baadhi ya wanasayansi kukata shauri na kukiri kuwa
Qur‘an ndio kitabu pekee ambacho kimezungumzia kwa kina juu
ya asili ya kuumbwa kwa ulimwengu. Baada ya Qur‘an
kuwathibitishia hilo, sambamba na matokeo ya sayansi yao,
likazuka suali kubwa na lenye mjadala kuhusu mwisho wa
ulimwengu.
159
Allah (Subhanahu) amesema pia ndani ya Surat Al-Rahman;
―Kila kilioko juu yake kitatoweka. Na atabaki Mwenyewe Mola
wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu. (55:26-27)
160
Wanasayansi hawakuacha kuendelea kufanya tafiti mbali mbali
za kuthibitisha mwisho wa ulimwengu (kutoka na mitazamo yao)
huku vifaa kadhaa vikiundwa kusaidia uchunguzi wa mwenendo
wa ulimwengu. Hata hivyo, duru za kihistoria za kisayansi
zinathibitisha kuwa upo uwezekano kwa ulimwengu ambao
uliumbwa na kuanzisha kwa mripuko mkubwa (The big Bang)
kuwa utamalizika kama ambavyo ulianza. Walichoshindwa kujua
ni kwa namna gani jambo hilo litatokea.
161
Kwa wafuatiliaji wa Qur‘an, wanaweza kuthibitisha kuwa kila
kitu katika fafanuzi za wasomi hawa zilishabainishwa ndani ya
Qur‘an karne kadhaa hapo nyuma. Qur‘an imeelezea mpasuko
na msagiko huu kwa kina kupitia sura mbali mbali, huku
ikibainisha kwa namna tofauti ya matukio ambayo yanaendana
moja kwa moja na matokeo ya gunduzi za big crunch. Allah
(Subhanahu) amesema ndani ya Surat Al-Inshiqaq;
―Mbingu itakapo chanika. Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na
ikapaswa kumsikiliza. Na ardhi itakapo tanuliwa.‖ (84:1-3)
Akasema pia Allah (Subhanahu) ndani ya Surat At-Takwir;
―Jua litakapo kunjwa kunywa. Na nyota zikazimwa. Na milima
ikaondolewa. (81:1-3)
Kadhalika, Allah (Subhanahu) amesema ndani ya Surat Al-
Infitar;
―Mbingu itakapo chanika. Na nyota zitapo tawanyika. Na habari
zitakapo pasuliwa.‖ (82:1-3)
162
HITIMISHO
163
Wasomi na watafiti mbali mbali wa masula ya vitabu vya kale
wanakiri kuwa Qur‘an ndio kitabu pekee ambacho kimekuwa
kikitoa changamoto zisizoweza kujibika kwa viumbe, kisha kutoa
majibu na kubainisha udhaifu mkubwa wa viumbe hao. Kama
hivyo ndivyo, tunapaswa kuisoma Qur‘an kwa mazingatio,
tujifunze na kukimbilia kupata faida zilizomo ndani yake. Hakika
hii ni nuru ambayo Umma wa Kiislamu umeachiwa na kiongozi
mtukufu, na Qur‘an ndio ukamilifu wa dini na mfumo mzima wa
maisha ya mwanadamu.
Qur‘an ndio kitabu kinachorejewa zaidi duniani katika masuala
mbali mbali yanapotatiza vichwa vya wasomi. Tunaona namna
ambavyo Qur‘an imetumika kuwezesha masuala kadhaa ya
kisayansi katika fani mbali mbali kama vile fani za kitabibu,
anga, na mengine lukuki ambayo tunapaswa kuyasoma na
kuyazingatia. Kitabu hiki, kimeeleza kwa kiasi namna ambavyo
Qur‘an imekua mbele ya wakati katika masuala mbali mbali, ili
iwe ni ujumbe kwa jamii na ulimwengu kwa ujumla. Kila
mwenye akili atafakari, kila mwenye macho aone na kila
mwenye kusikia, asikie na kuitangaza elimu na miongozo juu ya
Qur‘an.
Kitabu hiki kimegusa kwa kiwango kidogo sana juu ya
uthibitisho wa sayansi na teknolojia ndani ya Qur‘an, hakika hizi
ni miongoni mwa fursa ambazo kila mwenye nafasi anapaswa
kuziunga mkono kwa hali na mali ili jamii ifaidike na kuelimika
katika kuijua Qur‘an. Hii ni sehemu yetu katika kutekeleza
wajibu wetu wa kuifunza Qur‘an. Haya yote ni neema za Allah
(Subhanahu) kuturuzuku afya na uhai wa kukamilisha kitabu
hiki. Elimu ni bahari kila mmoja huogelea kwa kiwango chake
alichojaaliwa na Allah (Subhanahu) na „HAYA NDIO QUR‟AN
IMENIFUNZA‟
164
REJEA ZA KITABU:
165