Professional Documents
Culture Documents
Kitabu Cha Dua Na Adhkar-66006ee471ba7
Kitabu Cha Dua Na Adhkar-66006ee471ba7
Katika makala hii utajifunza baadhi ya dua za kila siku lakini pia utajifunza swala na
namna ya kuswali. Endelea kusoma kitabu hiki uapate kuijua swala, na mafunzo yake,
na zijue duamba mbalimbali ambazo inakupasa kuzijua.
" Sub-hanallahi wabihamdihi." (mara mia) Ametakasika Allah na sifa zote njema ni
zake.
“Laailaha illallahu, wah-dahu laa sharikalahu, lahul-mul-ku walahul-hamdu wahuwa
'alaa kulli shay-in qadiiru" (mara mia) “Hapana Mola ila Allah, mpweke, asiye na
mshirika, ni wake ufalme na ni zake sifa njema zote, na yeye yuko juu ya kila kitu.
11. Kuomba Msamaha na Kutubia Amesema Mtume (s.a.w): “Naapa kwa Mwenyezi
Mungu hakika mimi ninamtaka msamaha Mwenyezi Mungu na ninatubia kwake
katika kila siku zaidi ya mara sabini." (Al-Bukhari).
“Astagh-firu llaha waatuubu ilahi." (mara mia) “Namuomba msamaha Allah na
ninatubia kwake."
Amesema Mtume (s.a.w): "Hakuna mja yeyote yule anayefanya dhambi kisha
akatawadha vizuri na akaswali rakaa mbili, kisha akamtaka Mwenyezi Mungu
msamaha ila atasamehewa". (Abu Daud na Tirmidh) 12. Dhikri ya kuleta baada ya
kupatwa na janga au balaa “Laailaha illa llahul-'adhwiimul-haliimu, laa ilaha illa llahu
r a b b u l - ' a r - s h i l ' a d hwi imi , L a a i l a h a i l l a l l a h u rabbussamaawaat
warabbul-ardhwi,warabbul-'ar-shilkariimi. “Hapana Mola ila Allah, aliye mtukufu
mpole, Hapana Mola ila Allah, Mola wa arshi tukufu, Hapana Mola ila Allah, Mola
wa mbingu na ardhi na Mola wa arshi tukufu. “Laailaha illaa-anta Sub-hanaanaka
inny kuntuminal Dhw- Dhwaalimiina." Hapana Mola ila Wewe, Utukufu ni wako,
hakika mimi ni miongoni mwa waliodhulumu nafsi zao. 13.Unapokutana na adui au
mtawala dhalimu “Hasbunallahu wani'imal-wakiilu" “Allah anatutosheleza Naye ni
mbora wa kutegemewa.
21.Dua ya kuleta wakati mvua inanyesha “Allahumma Swayyiban naafia'n “Ee Allah
ijaalie iwe mvua yenye manufaa."
26. Dua ya kuleta baada ya kupiga chafya Unapopiga chafya hunabudi kusema:
“Al-hamdulillaahi" “Sifa zote anastahiki Allah." Kisha ndugu zako Waislamu
watasema: “Yar-hamuka llahu." “Allah akurehemu." Kisha utajibu kwa kusema:
"Yah-diykumullahu wayusw-lihi baalakum." "Allah akuongozeni na kuwasahilishia
mambo yenu." Kama anaeambiwa ni mwanamke
“Utasema yar-hamuki llahu”
28. Dua ya kuleta unapoanza kufanya tendo la ndoa “Bi smi l lahi A l lahumma
jannib-nashshay - twaana wajannibish-shytwaana maarazaq-tanaa". “Kwa jina la
Allah, Ee Allah muweke shetani mbali nasi na muweke shetani mbali na hicho
ulichoturuzuku."
31. Dua unayomuombea yule aliyekufanyia jambo zuri “Jazaka llahu khayran"
“Allah akulipe kheri."
35.Dua ya Safari “Allahu akbaru, Allah akbaru, Allahu akbaru, sub-haana lladhiy
sakh-kharalanaa hadhaa wamakunnaa lahu muqriniyna, wainnaailaa rabbinna
lamunqalibuuna. Allahumma innaa nas-aluka fiy safarinaa hadhal-birri wa-ttaqwa,
waminal-a'mali maatar-dhwaa, Allahumma hawwin a'laynaa safaranaa hadha wat-wi
a'nnaa budahu, Allahuumma antasw-swaahibu fiy ssafari, wal-khaliyfatu fiyl-ahli.
“Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, Allah ni mkubwa, ametakasika ambaye
ametudhalilishia sisi hiki (chombo au mnyama), na hatukuwa sisi kwako ni wenye
uwezo, na sisi kwa Mola wetu tutarejeshwa. Ee Allah, hakika sisi tunakuomba katika
safari yetu hii wema na ucha Mungu, na katika matendo unayoridhia, Ee, Allah ifanye
nyepesi safari yetu hii na ufupishe umbali wake. Ee Allah, wewe ndie mwenzangu
katika safari na mchungaji wa familia yangu.
Jabir Ibn Abdullah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Hakika dua
kubwa ni kusema: “Al-hamdulillaahi" “Shukurani zote anastahiki Allah." Na hakika
namna bora ya kumkumbuka Allah (dhikri) ni kusema: “Laailahailla llaaha." “Hapana
Mola ila Allah." (Ahmad)
41.Dhikri ya kuleta wakati wa kulala Alikuwa Mtume (s.a.w) akienda kulala usiku,
akiweka pamoja viganja vyake kisha akivipulizia na akivisomea suratul-Ikhlas,
suratul Falaq na Suratun-Naas, kisha akipangusa kwa hivyo viganja vyake kiasi
anachoweza katika mwili wake, akianza kichwani, usoni na mbele (akifanya hivyo
mara tatu.) (Bukhari na Muslimu)
Mwenyezi Mungu, hakuna Mola ila yeye, ndiye mwenye uhai wa milele, msimamia
kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala. Ni vyake (peke yake vyote)
vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na nani huyo awezaye kuombea mbele
yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yaliyo) nyuma yao;
wala (hao viumbe) hawalijui lolote katika ilimu yake ila kwa alipendalo. Enzi yake
imeenea mbinguni na ardhini, wala kuvilinda hivyo hakumshindi; Na yeye (pekee)
ndiye aliye juu na ndiye aliye mkuu." (2:255)
Alikuwa Mtume (s.a.w) akitaka kulala, anaweka mkono wake wa kulia chini ya shavu
lake, kisha anasema: "Allahumma qiniy a'dhaabaka yaumatab-a'thu i'baadaka." "Ee!
Allah nikinge mimi kwa adhabu yako siku utakapowafufua waja wako."
Pia Mtume (s.a.w) wakati wa kulala alikuwa akisema: “Allahumma Bismika amuutu
wa-ahyaa. “Kwa jina lako, Ee Allah ninakufa na nina kuwa hai." uzi na ndiye
Mwenye hikima (2:32)
DUA ZA SWALA
SWALA
Umuhimu wa Kusimamisha
Swala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.a) tuliyoirejea mwanzoni, kusimamisha
swala ni nguzo ya pili ya nguzo za Uislamu. Katika kuonyesha umuhimu wa
kusimamisha nguzo hii Mtume (s.a.w) amesema: Swala ndio nguzo kubwa ya Dini
(Uislamu) mwenye kusimamisha swala amesimamisha dini (Uislamu) na mwenye
kuiacha swala amevunja Dini . (Uislamu)
Katika Hadithi nyingine, amesimulia Jabir (r.a) kuwa Mtume wa Allah amesema:
Tofauti yetu sisi (Waislamu) na ukafiri ni kuacha swala h. (Muslim) Pia Mtume
(s.a.w) amesema: Tofauti iliyopo kati yetu (Waislamu) na wengine (wasiokuwa
Waislamu) ni swala (Ahmad, Abu Daud, An-Nasai, Tirmidh) Kutokana na hadithi
hizi, tunajifunza kuwa mtu ambaye hasimamishi swala, hatakama anajiita Muislamu
si Muislamu bali ni kafiri kama makafiri wengine. Anakuwa kafiri kwa sababu
amekanusha amri ya Allah iliyowazi kama inavyobainika katika aya zifuatazo:
Waambie waja wangu walioamini, wasimamishe swala. (14:31) Basi simamisheni
swala, kwa hakika swala kwa waumini ni faradhi iliyowekewa nyakati makhsusi. h
(4:103) Na waamrishe watu wako kuswali (kusimamisha swala) na uendelee
mwenyewe kwa hayo... h (20:132).
Tukumbuke kuwa hawi Muumini yule anayekuwa na hiari katika kutekeleza amri ya
Allah na Mtume wake kama tunavyokumbushwa katika aya ifuatayo: Haiwi kwa
mwanamume aliyeamini wala kwa mwanamke aliyeamini, Mwenyezi Mungu na
Mtume wake wanapokata shauri, wawe na hiari katika shauri lao. Na mwenye
kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amepotea upotofu ulio wazi h.
(33:36)
Kutokana na aya hii tunajifunza kuwa lengo la kusimamisha swala ni kumtakasa mja
na mambo machafu na maovu. Kwa maana nyingine, tunajifunza kuwa swala
ikisimamishwa vilivyo, humfanya msimamishaji awe mtu mwema mwenye
kutakasika na mambo machafu na maovu na mwenye kuendea kila kipengele chake
cha maisha kwa kumtii Allah (s.w).
Labda tujiulize swali: Ni nguvu gani au ni msukumo gani uliomo katika swala
unaomfanya mwenye kuswali atakasike na maovu na awe na tabia njema anayoridhia
Allah (s.w) Linaloleta mabadiliko haya makubwa katika tabia na utendaji wa
Muumini, ni lile kumbuko la Allah (s.w) lililomo ndani ya swala. Kwa hiyo lengo hili
la swala litapatikana tu pale mwenye kuswali atakapokuwa na mazingatio na
kumkumbuka Allah (s.w) katika kila hatua ya swala.
Maana ya Swala
Maana ya Swala
(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua.
Katika Qur-an tunaamrishwa kumswalia Mtume, yaani kumuombea dua Mtume
(s.a.w) katika aya ifuatayo: Hakika Mwenyezi Mungu na Malaika wake
wanamswalia Mtume (wanamtakia Rehema). Basi, enyi mlioamini mswalieni
(muombeeni au mtakieni Mtume) Rehema na muombeeni amani (33:56)
Vile vile katika Hadith, Mtume (s.a.w) anatuambia: Yule atakayealikwa kwenye
karamu ya harusi aitikie wito huo, kama hataweza kuitika amswalie (amuombee dua)
aliyemkaribisha. (Muslimu).
(b) Kisheria Katika sheria ya Kiislamu, swalaa ni maombi maalumu kwa Allah (s.w)
yanayofanywa kwa kufuata utaratibu maalumu uliowekwa na Allah (s.w) na
kufundishwa kwa matendo na Mtume wake. Katika maombi haya maalumu mwili
mzima huhusika katika maombi haya kwa kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu,
kukaa na kuzingatia yale yote anayosema katika kuleta maombi haya.
Kusimamisha Swala.
Maana ya Kusimamisha Swala Kusimamisha swala ni tofauti na kuswali. Kuswali ni
kufanya vitendo vya swala kama vile kusimama, kurukuu, kuitidali, kusujudu, n.k.
Kusimamisha swala ni kuitekeleza swala kwa kuchunga na kutekeleza kwa ukamilifu
yafuatayo:
Mtu akiswali bila ya kuzingatia na kutekeleza kwa ukamilifu mambo haya matatu,
ataonekana kuwa kaswali, lakini atakuwa hajasimamisha swala na atastahiki
kuadhibiwa vikali na Mola wake kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo: Basi
adhabu kali itawathibitikia wanaoswali, ambao wanapuuza swala zao (kwa
kutozisimamisha), ambao hufanya ria (107:4-6).
Sharti za Swala
Sharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu
ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali. Mambo haya ni:
1. Twahara.
2. Sitara.
3. Kuchunga wakati.
4. Kuelekea Qibla.
Sunnah za Swala
Sunnah za Swala Vipengele vya sunnah katika swala ni vile ambavyo mwenye
kuswali akivitenda husaidia sana kukuza daraja ya swala yake na kuipa nguvu na
msukumo mkubwa wa kuiwezesha kufikia lengo lililokusudiwa kwa urahisi zaidi.
Ama mwenye kuswali akiacha kipengele chochote katika vipengele vya sunnah,
swala yake itakamilika iwapo atatekeleza vipengele vyote vya nguzo. Katika Hadith
tumeona kuwa Mtume (s.a.w) katika swala yake pana vipengele vya ziada ya nguzo
kama ifuatavyo:
1. Kuinua viganja vya mikono mkabala na mabega, usawa wa vigingi vya masikio
wakati wa kuhirimia swala, kwenda kwenye rukuu, baada ya rukuu na baada ya
kutoka kwenye Tahiyyatu ya kwanza.
2. Kusoma dua baada ya takbira ya kuhirimia.
3. Kuanza na a fudhubillaah (kumlaani Shetani) kabla ya kuanza kusoma
suratul-Fatiha.
4. Kuitikia Aamin hbaada ya kumaliza Suratul Fatiha.
5. Kusoma aya za Qur-an baada ya Suratul-Fatiha katika rakaa mbili za mwanzo. 6.
Kuleta Tasbih, Tahmid na dua katika rukuu, itidali na sijda.
7. Kutoa takbira katika kubadilisha kitendo kimoja kuendea kingine isipokuwa tu
kutoka kwenye rukuu kwenda kwenye itidali ndipo tunaposema: Sami fAllahu
liman hamidah - Rabbanaa lakal-hamdu .
8. Kukaa na kusoma Tahiyyatu kila baada ya rakaa mbili, kwa swala zenye rakaa
zaidi ya mbili.
9. Kusoma dua baada ya kumswalia Mtume na kabla ya kutoa Salaam.
Hii tunaipata katika Hadith aliyosimulia Abdullah bin ‘Umar kuwa: “Mtume (s.a.w)
aliposimama kwa ajili ya swala alinyanyua mikono yake mkabala na mabega yake na
kisha kuhirimia (kusema Allahu Akbar). Alipotaka kurukuu alinyanyua mikono kama
alivyofanya kwanza na aliposimama kwa ajili ya itidali alifanya hivyo hivyo na
alisema Allah anamsikia yule anayemsifu. (Bukhari, Muslim na Bayhaqi).
Nafa’a(r.a) ameeleza kwamba Ibn ‘Umar (Abdullah)(r.a) aliposimama kwa ajili ya
rakaa ya tatu alikuwa akinyanyua mikono; jambo ambalo alilihusisha na Mtume
(s.a.w). (Bukhari, Abu Dawud, Nasai).
Naye Wail bin Hijr (r.a) ameripoti: “Niliswali pamoja na Mtume (s.a.w) na aliweka
mkono wake wa kulia juu ya mkono wa kushoto juu ya kifua chake”. (Ahmad na
At-Tirmidh).
Imamu Abu Dawud na Nasai wamepokea kutoka kwa Ibn Khuzaimah kuwa Mtume
(s.a.w) alipokuwa akiswali alikuwa akiweka mkono wake wa kulia juu ya kiwiko
(wrist) cha mkono wa kushoto na sehemu ya mkono inayofuatia kiganja .
3. Kupiga Audhu Billah Kabla ya kuanza kusoma Qur-an ni amri ya Allah (s.w)
kujikinga na sheitwani kama inavyodhihirika katika aya ifuatayo: 109 “Na ukitaka
kusoma Qur-an piga Audhu billah (jikinge) kwa Allah (akulinde) na Sheitwani
aliyefukuzwa (kwenye Rehema). (16:98) Hivyo tuanze kusoma Qur-an kwa kusema
“A’udhu-billahi minash-shaytwanir- Rajiim” Najikinga kwa Allah na sheitwan
aliyefukuzwa-kwenye Rehma yako
Tafsri:
(1) Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu: (2)
Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mola wa Walimwengu wote: (3) Mwingi
wa Rehema mwenye kurehemu (4) Mwenye kumiliki siku ya malipo: (5) Wewe tu
ndiye tunayekuabudu, na wewe tu ndiye tunaye kuomba msaada: (6) Tuongoze njia
iliyonyooka: (7) Njia ya wale uliowaneemesha; siyo (ya wale ) waliokasirikiwa, wala
ya wale waliopotea
7.Kuitidal
Kuitidali ni kusimama wima kutoka kwenye rukuu, ni sunnah kusema wakati wa
kunyanyuka maneno haya:“sami’a llahu liman hamidahu” Mwenyezi Mungu
anamsikia kila mwenye kumhimidi. Na baada ya kusimama sawa ni sunnah kusema
“rabbanaa walakal-hamdu”ewe mola wetu sifa zote za ukamilifu ni zako. Pia ni
sunnah kusema maneno haya “rabbanaa walakal-hamdu mil-as-samaawati
wamil-al-ardhi wamil-amashi-ita minshai-in ba’adah”
Ewe Mola wetu sifa zote za ukamilifu ni za kwako, kutoka mbinguni, kutoka ardhini
na katika vitu vyote vilivyo baina yao (mbingu na ardhi) na kutoka katika vinginevyo
unavyo viridhia
8.Kusujudi
Ni nguzo pamoja na kujituliza katika sujudi. Mkusujudi ni kuvituliza chini viungo
saba kwa utaratibu wa swala. Vingo hivyo ni , paji a uso, viganya viwili vya mikono,
magoti mawili na matumbo ya nyayo za vidole vya miguuni.viungo vyote hivi
vinatakiwa vielekee kibla. Paji la uso ni pamoja na pua iguse chini.utasema kwenye
sijda “subhaana rabbiyal-a’alaa” utukufu ni wa kwako Mola uliye tukuka.
10.kikaa tahiyyatu
Katika kukaa Thiyyatu mtume alikuwa akikalia futi la mguu wa kushoto na
kusimamisha futi la mguu wa kulia na katika tahiyyatu ya mwisho alikaa chini na
kuulaza mguu wa kushoto katika uvungu wa mguu wa kulia na alisimamisha futi la
mguu wa kulia, katika vikao vyote hivyo viwili,
Mtume (s.a.w) alivilaza viganja vyake juu ya mapaja karibu na magoti kama
tunavyoelezwa katika hadith ifuatayo: Abdullah bin Jubair(r.a) ameeleza kuwa wakati
Mtume (s.a.w) alipokaa tahiyyatu, alikuwa akiweka kiganja chake cha mkono wa
kulia juu ya paja lake la kulia na kiganja cha mkono wa kushoto juu ya paja la mguu
wa kushoto na alikuwa akinyoosha kidole chake cha shahada (wakati wa k u s e m a ,
“ A s h - h a d u anllaaillaha illallah) na kukiegemeza juu ya kidole gumba na alikuwa
akiweka kiganja chake cha mkono wa kushoto juu ya goti lake (la mguu wa kushoto).
(Muslim).
11. Kusoma Tahiyyatu Kusoma tahiyyatu ni nguzo ya swala. “Tahiyyatu” ina maana
ya “Maamkizi”, ukiwa umekaa kikao cha tahiyyatu unaleta maamkizi kama ifuatavyo:
“Attahiyyaatu lillaah, wasw-swalawaatu, watwa-yyibaatu, assalaamu ‘alaika
ayyuhannabiyyu, warahmatullaahi wabarakaatuhu, assalaamu ‘alay-naa wa-’alaa
‘ibaadillaahi swswaalihiina. Ash-hadu an-llaailaaha illallaahu wa-ash-hadu anna
Muhammadan ‘abduhuu warasuuluhu”. “Maamkizi yote ni ya Allah, na swala zote
na yote mazuri, Amani iwe juu yako, ewe Mtume na Rehma na Baraka za Allah. Na
amani iwe juu yetu na juu ya waja wema wa Allah. Ninashuhudia kuwa hapana Mola
ila Allah. Na ninashuhudia kuwa Muhammad ni Mja na, ni Mtume wake”. (Muslim).
“Allahumma swalli ‘alaa muhammad wa’alaa aliy Muhammad kamaa swallaita ‘alaa
ibraahima wa’alaa ali ibraahim innaka hamiidum-majid. Wabaaik ‘alaa muhammad
wa’alaa ali muhammad kamaa barakta ‘alaa ibraahima wa’alaa ali ibraahima innaka
hamiidum-majid”
Muhimu:
Kumbuka kuwa sijda hii Mtume (s.a.w) aliileta baada ya kutoa salaamu na baada ya
kukumbushwa. Abdullah bin Buhaymah (r.a) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w)
aliswalisha swala ya adhuhuri, akasimama baada ya rakaa mbili, alipomaliza swala
akasujudu mara mbili huku akisema: “Allah Akbar” katika kusujudu na katika
kuinuka, wakati amekaa kabla ya kutoa salaam, na watu wakasujudu pamoja naye. Hii
ilikuwa ni kufidia ile tahiyyatu ya mwanzo aliyoisahau”. (Muslim)
(g) Kufanya jambo lisilowiana na swala mfululizo mara tatu. (h) Kuiacha nguzo
yoyote ya swala
(i) Ukizidisha nguzo yoyote ya swala makusudi.
(j) Kumtangulia Imam au kuchelewa kwa nguzo mbili za kimatendo kwa makusudi.
(k) Kutia nia ya kuikata swala au kujishauri moyoni kuwa uikate au usiikate swala.
(l) Kuwa na shaka kuwa umetimiza au hujatimiza sharti au nguzo yoyote ya swala.
(m) Kupotewa na akili au kulala ndani ya swala.
(n) Kutoa Salaam kwa makusudi kabla ya kwisha swala.
(o) Kuswalishwa na asiyekuwa Muislamu.
(p) Kukhalifu utaratibu wa nguzo za swala, yaani kutangulia kutekeleza nguzo ya
swala kabla ya kutekeleza nguzo inayostahiki kutangulia katika utaratibu wa swala.
(q) Kuleta dua ya kuomba kitu haramu au muhali.
(r) Kumshirikisha Allah (s.w) katika kuleta dua yaani kuleta dua ya kuomba kitu cha
halali lakini humuombi Allah (s.w) peke yake.
Baada ya nyiradi hizi, ni vizuri pia kuomba dua yoyote kulingana na haja zako kwa
lugha yoyote. Jambo hili la kuomba dua baada ya swala, umuhimu wake unadhihirika
katika hadithi ifuatayo: Abu Umamah amesimulia kuwa: Iliulizwa: Ee Mtume wa
Allah. ni dua gani ambayo hukubaliwa zaidi? h (Mtume) alijibu: (moja) ni ile ya
katikati ya nusu ya pili ya usiku na (pili) kila baada ya swala ya faradhi . (Tirmidh)
Hivyo ni jambo la msingi mno kuomba dua yoyote kila baada ya swala na dua zilizo
nzito zaidi ni zile zilizomo kwenye Qur-an na hadithi za Mtume (s.a.w). Kwa mfano
ni vizuri kila baada ya swala, au baada ya dhikri zilizotajwa tuombe dua ifuatayo:
Rabii ij’alnii muqiimas-swalaati wamindhurriyyatii Rabbana Wataqabbal du ’aaai.
Mola wangu! Nijaalie niwe msimamishaji swala, na kizazi changu! (Pia kiwe hivi).
Mola wetu! Na upokee maombi yangu mengine... (14:40-41).