Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 18

MNYAMA WA KITABU CHA UFUNUO

Watu wengi hawafahamu kuwa mnyama ni nani, na wengi wamejihusisha


naye bila wao wenyewe kujua kama wanashiriki na mnyama. Lakini Mungu
hajatuacha gizani, hivyo, kwa kupitia neno lake (Maadiko Matakatifu)
tunaweza kumfahamu mnyama huyu aliyelezwa katika kitabu cha Danieli
na Ufunuo. Tunapaswa kuyaacha maandiko yajitafisiri yenyewe; kwa
maana “hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo
mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa popote kwa mapenzi ya
mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu,
wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” 2Petro 1:20-21. Hatupaswi kumuacha
mtu flani atafsri unabii kwa jinsi yake mwenyewe, badala yake tunapaswa
kuiacha Biblia ijitafsiri yenyewe.

Katika Danieli 7 wametajwa “wanyama wanne” ambao wanawakilisha


falme nne. Kumbuka mmyama wa 4 aliyetajwa katika Danieli 7 ndiye
mnyama aliyetajwa katika kitabu chote cha Ufunuo. Hivyo hapa tutaangalia
sifa za mnyama wa nne wa kitabu cha Danieli, na mnyama wa kitabu cha
Ufunuo, kisha tutaangalia ni wapi hapa duniani ambapo sifa za mnyama
zinatimizwa kikamilifu.

1. Mnyama atakuwa na uwezo wa kisiasa na kidini (kanisa na serikali).

Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona


MWANAMKE, AMEKETI JUU YA MNYAMA mwekundu sana, mwenye kujaa
majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.”

Mwanamke au bibi-arusi katika unabii huwakilisha kanisa.

Ufunuo 21:2 “…Yerusalemu mpya…umewekwa tayari, kama bibi-arusi


aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.”

Ufunuo 21:9 “…Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa


Mwana-Kondoo.”

Mnyama huwakilisha taifa au ufalme

Danieli 7:17 “Wanyama hao…wanne ni wafalme wanne watakaotokea


duniani”

Danieli 7:23 “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya


dunia…”

Kutokana na Ufunuo 17:3, mnyama huyu ana mwanamke aliyeketi juu yake,
na kwa sababu unabii unatafisiri mwanamke kama kanisa, na mnyama
kama taifa. Je kuna taifa au serikali ambayo imechanganywa pamoja na
kanisa kama kitu kimoja? Ndiyo! Vatican, ni serikali au taifa ambalo
limechanganywa pamoja na kanisa la Romani Katoliki kama kitu kimoja, na
kuongozwa na mtu mmoja ambaye ni Papa.

2. Mnyama atakuwa na kanisa & serikali vimekaa juu ya milima 7.

Ufunuo 17:3 “Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke,


ameketi juu ya mnyama mwekundu sana…mwenye VICHWA SABA na
pembe kumi.”

Vichwa saba katika unabii vinawakilisha milima saba.

Ufunuo 17:9 “Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni
milima saba anayokalia mwanamke huyo.”

Je hapa duniani kuna kanisa na serikali vimekaa juu ya milima saba?

“Ni ndani ya mji wa Roma, uitwao Mji wa vilima saba, hivyo eneo lote la
Serikali ya Vatican limewekewa mpaka kikamilifu.” –The Catholic
Encyclopedia, p 529.

“Je vilima saba vya Roma ni nini?

Roma inajulikana kuwa imejengwa juu ya vilima saba. Roma ilisemwa


imepatikana wakati Romulus na Remus, wana mapacha wa Mars, walifika
katika futi ya kilima Palatine na wakauanzisha mji, Vilima sita vingine ni
Capitoline (kiti cha serikali), Quirinal, Viminal, Esquiline, Caelian, na
Aventine.” –Geography.about.com

ENCYCLOPÆDIA BRITANNICA

Vilima saba vya Roma

“…kundi la vilima juu au kuhusu ambapo mji wa Roma wa zamani ulijengwa.


Mji wa awali wa Romulus ulijegwa juu ya kilima Palatine (#1) (Kilatini: Mons
Palatinus). Vilima vingine ni Capitoline, (#2) Quirinal, (#3) Viminal, (#4)
Esquiline, (#5) Caelian, (#6) na Aventine (#7) (Vinavyojulikana kimoja
kimoja kwa kilatini kama Mons Capitolinus, Mons Quirinalis, Mons
Viminalis, Mons Esquilinus, Mons Caelius, na Mons Aventinus).”
–http://www.britannica.com/seo/s /seven-hills-of-rome/

Kwa hiyo unabii huu wa Ufunuo 17:3, unaonyesha wazi kuwa mwanamke
aliyeketi juu ya mnyama, amekaa juu ya vilima saba vya mji wa Roma. Kwa
vyovyote, ni Vaticani na kanisa la Romani Katoliki ambavyo vimekaa juu ya
milima saba, na kutimiza unabii huu. Danieli 7:23 inasema mnyama wa
mwisho (Roma) anatofautiana na wanyama wengine watatu waliopita. Kwa
hakika hakuna taifa wala ufalme mwingine ambao una kanisa na serikali,
harafu kwa wakati huo huo umekaa juu ya milima saba. Ila ni kanisa la
Romani Katoliki pekee.

3. Mnyama atatoka baharini

Ufunuo 13:1 “Kisha nikaona mnyama AKITOKA KATIKA BAHARI, mwenye


pembe kumi, na vichwa saba, na juu ya pembe zake ana vilemba kumi, na
juu ya vichwa vyake majina ya makufuru.”

Bahari katika unabii huwakilisha watu/jamaa, mataifa, lugha.

Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule
kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.”

Ukatoliki wa Romani ulitokea ulaya ya magharibi pamoja na makutano ya


“watu/jamaa, mataifa, na lugha.” Na kwa wakati huu kanisa la Romani
Katoliki lina idadi kubwa ya “watu, mataifa, na lugha,” kuliko kanisa jingine
lolote duniani mwote. Na sasa, baada ya kuanzishwa kanisa moja duniani,
Juni 26, 2000, Papa alichaguliwa kama kiongozi wa makanisa yote ambayo
yameungana na lake. Hii ilifanya kanisa liongezeke mara mbili. Na hivi
karibuni, makanisa yote pamoja na yasiyo ya Kikristo yatatangaza kwamba
Papa ni kiongozi wao mwema.

Na Juni, 2008 mataifa 174 katika mataifa 192 duniani, yana serikali zao
zikiwakilisha Vatican. Hivyo, kanisa la Romani Katoliki linatimiza unabii huu
kwa ukamilifu.

4. Mnyama atatawala miaka 1260. (kabla hajapata jeraha la mauti).

Danieli 7:25 “Naye atanena maneno kinyume chake aliye juu, naye
atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataadhimu kubadili majira
na sheria; nao watatiwa mikononi mwake KWA WAKATI, NA NYAKATI
MBILI, NA NUSU WAKATI.”

Ufunuo 12:6 “Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambapo ana mahali


palipotengenezwa na Mungu, ili wamlishe huko mda wa SIKU ELFU NA MIA
MBILI NA SITINI.”

Ufunuo 13:5 “Naye akapewa kinywa cha kunena maneno makuu, ya


makufuru. Akapewa uwezo wa kufanya kazi yake MIEZI AROBAINI NA
MBILI.”

Danieli 7:25 inaonyesha muda ambao angetawala mnyama, kama wakati,


na nyakati mbili, na nusu wakati. Ufunuo 13:5 inauonyesha mda huu wa
utawala wa mnyama, kama miezi 42, miezi 42 = miaka 3 na 1/2. Hivyo,
ukiangalia kwa makini hapa utaona kuwa, wakati = mwaka 1, na nyakati
mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka.
Kwa hiyo, wakati nyakati mbili nusu wakati = miaka 3 na nusu ya Danieli
7:25, au miezi 42 ya Ufunuo 13:5, au siku 1260. Mahesabu haya
yanathibitishwa katika Ufunuo 12:6 ambapo inasema, “Yule mwanamke
(kanisa) akakimbilia nyikani…wamlishe huko mda wa siku 1260.” Kwa hiyo
miaka 3 na 1/2 = miezi 42 au siku 1260 ambazo mnyama angetawala kabla
hajapata jeraha la mauti.

Bado, wengine watakataa na kusema, hapana, miezi 42 haiwezi kuwa sawa


na siku 1260, kwa sababu miezi mingine haina siku 30. Lakini katika unabii
mwezi 1 = siku 30. Mwanzo 7:11 inasema, mvua za garika zilianza siku ya
17 ya mwezi wa pili, na Mwanzo 8:3, 4. inasema kuwa maji yakapunguka
mwishoni mwa siku 150, harafu safina ikatua siku ya 17 ya mwezi wa saba.
Hizo ni miezi 5 tangu mvua zilipoanza. Kama ukigawanya siku 150, kwa
miezi 5, utapata siku 30 kwa kila mwezi. Hivyo, miezi 42 ikizidishwa kwa 30
jibu litakuwa 1260. Kwa hiyo wakati, nyakati mbili, na nusu wakati, ni sawa
na miaka 3 na nusu, au miezi 42, au siku 1260. Kwa hakika, Ufunuo 12:6
inathibitisha mahesabu haya inaposema kuwa watoto wa Mungu
watakimbilia nyikani kwa muda wa siku 1260 wakati wa utawala wa
mnyama (upapa).

Katika unabii siku 1 ni sawa na mwaka 1,

Ezekieli 4:6 “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.”

Hesabu 14:34 “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…”

Kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni


sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha
watakatifu. Je hii ilitokea? Je unabii huu ulitimia? Au Je kuna ushahidi
wowote unaothibitisha kuwa unabii huu ulitimia?

Kwanza kabisa tunatakiwa kujua ni lini kanisa la Romani Katoliki lilipata


nguvu zote za kutawala kama “mwanamke juu ya mnyama” (kanisa na
serikali), na kutawala kisiasa na kidini kwa wakati mmoja kama Ufunuo
17:3 inavyosema.

“Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la


Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327

Hiistoria inathibitisha kuwa upapa umeanza utawala wake kama “kanisa na


serikali” mwaka 538 B.K. juu ya amri ya mfalme Jastinian, na chini ya ulinzi
wa jeshi la Belisarius. Na unabii unasema mnyama (upapa) atatawala
miaka 1260 kabla haujapata jeraha la mauti.

Ukiongeza miaka 1260 katika mwaka ambao kanisa la Romani Katoliki


lilianza kutawala kisiasa na kidini, mwaka 538 B.K., utapata 1798 B.K. Hivyo,
unabii unasema utawala wa kwanza wa mnyama ungeisha 1798 B.K. Je
utawala wa mnyama uliisha mwaka huo 1798 B.K?

“Katika mwaka 1798 Generali Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa


utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica
1941 edition

Kwa hakika, hizo ni miaka 3 na 1/2 au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati,
ambazo ni miezi 42 au siku 1260 za unabii ambazo mnyama angetawala
kisha angepata pigo la mauti au kuchukuliwa mateka. Je mnyama alipata
pigo la mauti mwaka huo 1798 B.K?

5. Mnyama atapokea jeraha la mauti.

Ufunuo 13:3 “Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa
jeraha la mauti, na pigo lake lake la mauti likapona…”

Ufunuo 13:10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua


kwa upanga, atauawa kwa upanga…”

Kama tulivyoona huko nyuma baada ya mnyama kutawala miaka 1260


angepata jeraha la mauti na kuuawa kwa upanga (upanga = vita). Baada ya
mnyama kumaliza utawala wake wa miaka 1260, ambao ulianza 538 B.K.
hadi 1798 B.K., Napoleon alimtuma Generali/Jemedari wake Berthier
pamoja na jeshi lake, kwenda Roma kuuondoa utawala wa upapa.

“Katika mwaka 1798 Generali Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa


utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica
1941 edition

Napoleon alipomtuma Generali wake Berthier kwenda kumuondoa Papa


madarakani, hapo ndipo jeraha la mauti lilipompata mnyama, na mwaka
uliofuata 1799 B.K. Papa alikufa. Hii ndiyo sababu watoto wa kikatoliki
katika parokia hufundishwa kuwa Napoleoni alikuwa mpinga Kristo.

“Nusu ya Ulaya walidhani…kwamba pamoja na papa upapa ulikuwa


umekufa.” –Joseph Rickaby “The Modern Papacy” Lectures on the History
of Religion, Lecture 24, (London Catholic Truth Society, 1910), p. 1

Lakini unabii ulisema kuwa jeraha hili lililompata mnyama lingepona. Je


jeraha hili lilipona? Je utawala wa upapa ulipoondolewa madarakani na
Generali Berthier ulipata nguvu zake tena?
6. Mnyama atapona jeraha lake la mauti.

Ufunuo 13:3 “Nikaona kimoja cha vichwa vyake kana kwamba kimetiwa
jeraha la mauti, NA PIGO LAKE LA MAUTI LIKAPONA. Dunia yote
ikamstaajabia mnyama yule.”

Kama tulivyoona, upapa ulipata jeraha la mauti mwaka 1798 B.K. Vaticani
ilibaki kama kanisa tu bila nguvu za kisiasa, na unabii ulisema jeraha hili
lingepona. Je jeraha la mauti lilipona? Baada ya jeraha la mauti kutokea
miaka kadhaa badaye katika mwaka 1929 B.K. Italia ikautambua mji wa
Vaticani kama serikali ya kujitegemea, hii ilimfanya papa kuwa na nguvu
tena kama mtawala wa kisiasa na kidini. kama unabii ulivyosema kwamba
jeraha la mauti lingepona, na upapa ungerudishiwa tena uwezo wake wa
kanisa na serikali kwa pamoja. Hebu angalia magaziti yaliyotoa taarifa hiyo
jinsi waandishi wake walivyotumia lugha ya unabii bila ya wao wenyewe
kujua.

Kusaini kwa Mussolini na (Kadinali) Gasspari mkataba wa kihistoria wa


Romani

“Suala la Romani usiku huu lilikuwa ni jambo lililopita, na Vaticani ilikuwa


katika amani na Italia…katika kuweka sahihi kwenye mkataba wa
kukumbukwa kuponya jeraha la miaka mingi, uchangamfu wa kupindukia
ulionyeshwa na pande zote.” –The San Francisco Chronicle. Feb. 11, 1929

Papa Amekuwa Kiongozi Wa Serikali Tena

“Roma, Juni 7.–Kutoka saa 5 kamili asubuhi hii kulikuwa na mtawala


mwingine wa serikali ya kujitegemea duniani. Katika mda huo waziri mkuu
Mussolini, kama waziri wa mambo ya nje Italia akimuwakilisha mfalme
Victor Emmanuel–waziri mkuu wa kwanza Italia kuvuka kizingiti cha chini
cha mlango wa Vaticani–akibadilishana na kadinali Gasspari, wakala wa
serikali ya upapa, akimuwakilisha papa Pius XI, makubaliano ya mikataba
yalisainiwa katika ikulu ya Lateran Feb. 11. Kwa kitendo hicho rahisi
mtawala wa serikali ya kujitegemea ya mji wa Vaticani amekuwepo.” —
New York Times July 7, 1929

Hivyo, unabii huu ulitimia kikamilifu na jeraha la mauti lililoupata upapa


1798 B.K. lilipona kabisa tangu 1929 B.K. mpaka leo kanisa la Romani
Katoliki lina nguvu za “kisiasa na kidini” au “mwanamke juu ya mnyama.”
Kwa kumaliza sehemu hii tunagundua kwamba mnyama huyu ndiye
aliyekuwako, naye hayuko, na sasa yupo.

7. Mnyama aliyekuwako, naye hayuko, naye yuko.

Ufunuo 17:8 “Yule mnyama…alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari…”


Mnyama aliyekuwako: ni kanisa la Romani Katoliki tangu lilipoanza
kutawala kama “kanisa & serikali” 538 B.K. na likaendelea mpaka.
Napoleon alipomtuma Berthier kwenda kuuondoa utawala wa upapa. 1798
B.K.

…naye hayuko tokea 1798 B.K. mpaka kusaini kwa mkataba uliofanyika
katika ikulu ya Lateran katika mwaka 1929 B.K. Vaticani ilikuwa kanisa tu
bila uwezo wa kiserikali.

…naye yu tayari kutoka 1929 B.K. mpaka leo kanisa la Romani Katoliki lina
nguvu za kisiasa na kidini, “kanisa & sesikali” au mwanamke juu ya
mnyama.

8. Mnyama atabadili majira na sheria za Mungu.

Danieli 7:25 “…naye ataadhimu kubadili majira na sheria…”

Unabii huu ni ushahidi ulio wazi sana ambao karibu kila mtu hawezi
kusumbuka kuelewa kwamba ni kanisa gani hapa duniani lililobadilisha
sheria za Mungu. Ni kanisa moja tu la Romani Katoliki ndilo lililobadilisha
sheria za Mungu kama Danieli 7:25 inavyodai kuwa. Kanisa la Katoliki
limebadilisha sheria ya pili inayozuia kuchonga sanamu ya kitu chochote
kile (angalia Kut 20:4). Katika katekism kanisa limeirarua amri ya 2 kisha
likaigawa amri ya 10 katika sehemu mbili ili kuonyesha amri 10 zote. Lakini
Je ni nani hapa duniani anayedai kuwa anauwezo wa kubadili amri za
Mungu?
“Papa anauwezo wa kubadili majira, kubadili sheria, na kuachana na
mambo yote, hata maagizo ya Kristo!” “Papa anayo mamlaka na mara
nyingi ameyatumia, kuachana na amri ya Kristo.” –Decretal, de Tranlatic
Episcop. Cap. (The Pope can modify divine law.) Ferraris’ Ecclesiastical
Dictionary.

“Papa ni wa mamlaka kuu na nguvu kiasi kwamba anaweza kurekebisha,


kuelezea au kutafsiri hata sheria za Mungu…Papa anaweza kurekebisha
sheria ya Mungu, kwa sababu nguvu zake si za mwanadamu, bali ni nguvu
za Mungu, na hutenda kama mwakilishi wa Mungu juu ya dunia.” –Lucius
Ferraris,Prompta Ribliotheca, “Papa,” art. 2, translated.

Tangu kwamba papa ana mamlaka na maranyingi ameyatumia kubadili


majira na sheria za Kristo, Je alibadili sheria ya Sabato? Je kanisa katoliki
liliibadili Sabato ya siku ya saba ya wiki kwenda siku ya kwanza ya wiki?
Kwa hakika kanisa lenye linakubali!

“Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi
kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya
mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –H.F. Thomas, Chancellor of
Cardinal Gibbons

“Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na


uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.”
–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

“Swali: Siku ipi ni siku ya Sabato?


Jibu: Jumamosi ni siku ya Sabato.

Swali: Kwanini tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi?

Jibu: Tunatunza Jumapili badala ya Jumamosi kwa sababu kanisa katoliki,


katika balaza la Laodikia (364 BK) liliihamisha kutoka Jumamosi kwenda
Jumapili.” –The Convert’s Catechism of Catholic Doctrine,p. 50, 3rd ed.

“Kanisa la Romani (Katoliki) liliigeuza amri ya nne kwa kuiondolea mbali


Sabato ya neno la Mungu, na kuanzisha Jumapili kama siku ya
mapumziko.” –Nicholas Summerbell, History of the Christian Church, 3rd
edition, 1873, p. 415 [Christian Church (Christian Connection)].

“Na ni wapi tumeambiwa katika maandiko kwamba tutunze siku ya kwanza


kabisa? Tumeamriwa kutunza siku ya saba; lakini hakuna sehemu yoyote
tuliyo amriwa kutunza siku ya kwanza. Sababu ya kutunza siku ya kwanza
ya wiki kitakatifu badala ya siku ya saba ni kwa sababu ile ile kwamba
tunatunza mambo mengine mengi, siyo kwa sababu ya Biblia, lakini kwa
sababu kanisa, limeyaingiza [limeyaamuru].” –Isaac Williams, Plain
Sermons on the Catechism, vol 1, pp. 334, 336 [Anglican].

Hivyo, kanisa la Romani Katoliki liliibadili sheria ya Sabato na kuwaamuru


watu watunze jumapili badala yake. Na mwaka 1582. Papa Gregory XIII,
alianzisha kalenda mpya. Kwa vyovyote, ni Vaticani ndiyo ilitimiza unabii
huu kwa ukamilifu kabisa, hakuna jumuiya, wala shirika, wala sehemu
yoyote ya kidini au isiyo ya kidini ambayo imetimiza unabii huu, kama ilivyo
Vaticani. Ni kanisa la Romani Katoliki pekee ambalo lilibadili sheria, na
majira, na kuamuru siku ihesabiwe kuanzia saa sita usiku kinyume na
Maandiko yanayothibitisha kuwa siku huanza kuhesabiwa jioni.
Mwanzo 1:5 “Mungu akaiita nuru Mchana, na giza Usiku. Ikawa jioni ikawa
asubuhi, siku moja.”

9. Mnyama atanena maneno ya makufuru juu ya Mungu.

Danieli 7:25 “Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu…”

Ufunuo 17:3 “…nikaona mwanamke ameti juu ya mnyama…mwenye kujaa


majina ya makufuru…”

Ufunuo 13:1 “…nikaona mnyama…mwenye…vilemba kumi, na juu ya vichwa


vyake majina ya makufuru.”

Ufunuo 13:5 “Naye akapewa kinywa cha kunena makuu, ya makufuru…”

Kukufuru katika Biblia inaelezewa kama hali ya mtu kujifanya yeye


mwenyewe kama Mungu.

Yohana 10:33 “Wayahudi wakamjibu, kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa
mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwamadamu
wajifanya mwenyewe u Mungu.”

Je nani hujiita na kujifananisha na Mungu hapa duniani?


“Papa siyo mwakilishi tu wa Yesu Kristo, yeye ni Yesu Kristo mwenyewe,
amejificha chini ya uficho wa mwili.” –Catholic National July 1895.

“Kwa kuwa wewe u mchungaji, wewe u tabibu, wewe u mwongozaji, wewe


u mkulima, hatimaye wewe u Mungu mwingine duniani.” –Labbe and
Cossart’s “History of the Councils.” Vol. XIV, col. 109

“Tunapachukulia juu ya dunia hii sehemu ya Mwenyezi Mungu…” –Pope Leo


XIII Encyclical Letter of June 20, 1894,

Katika “The Bull Unam Sanctam” iliyotolewa na Papa Boniface VIII


inasomeka kama ifuatavyo…

“Papa wa Roma huukumu watu wote, lakini yeye haukumiwi na mtu.


Tunatangaza, kutetea, kuelezea, na kutamka; kutawaliwa na Papa wa Roma
ni kwa kila kiumbe cha mwanadamu muhimu kwa ajili ya wokovu ambao
ulisemwa na Kristo ‘Ameviweka vitu vyote chini ya miguu yake’ inaonekana
vizuri imethibitishwa kwangu…Nina mamlaka ya Mfalme wa Wafalme. Mimi
ni yote katika yote na juu ya yote, hivyo basi, Mungu Mwenyewe na mimi,
kasisi wa Mungu tuna usawa mmoja, na ninaweza kufanya yote ambayo
Mungu anaweza kufanya.”

“Mwokozi mwenyewe ni mlango wa zizi la kondoo; ‘Mimi ni mlango wa


kondoo’. kwenye zizi hili la Yesu Kristo, hakuna mtu anayeweza kuingia
mpaka awe ameingizwa na Papa mtawalawa na ni pale tu kama
wameunganika naye ndipo wanadamu wanaweza kuokolewa, kwa sababu
Papa wa Roma ni kasisi wa Kristo na ni mwakilishi wake kwa nafisi
duniani.” –(Pope John XXIII in his homily to the Bishops and faithful
assisting at his coronation on November 4, 1958).

Kudai kuwa Mungu duniani Biblia inathibitisha kuwa ni kukufuru ju ya


Mungu aliye hai. Kufuru nyingine ni kudai kuwa na uwezo wa kusamehe
dhambi.

Marko 2:7 “Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye


kusamehe dhambi ispokuwa mmoja, ndiye Mungu?”

Je makuhani wa kanisa la Romani Katoliki hudai wana uwezo wa


kusamehe dhambi?

“Kuhani kiukweli kabisa husamehe dhambi kwa uwezo aliopewa na Kristo.”


-Joseph Devarbe’s Catechism, p. 279

“Dhambi zinaweza kusamehewa kupitia sakramenti pekee…wote makuhani


na sakramenti ni vifaa ambavyo Kristo anavitumia kukamilisha msamaha
ndani yetu na neema ya utakaso.” -Catechism of Trent, p. 115.

“Haya mamlaka ya jaji (Judicial authority) yatajumuisha hata uwezo wa


kusamehe dhambi.” –[The Catholic Encyclopaedia Vol 12, -article “Pope” pg
265]

“Na Mungu mwenyewe analazimika kufungwa na hukumu ya kuhani wake


na ama kutokuomba msamaha au kuomba msamaha, kutokana na kama
wanakataa kutoa ukamilifu, unaotoa toba inayoridhisha.” –Liguori, «Duties
and Dignities of the Priest», p.27

10. Mnyama ana jina lenye namba 666.

Ufunuo 13:17 “tena kwamba mtu awaye yote asiweze kununua wala kuuza,
ispokuwa ana chapa ile, yaani, jina la mnyama yule, au hesabu ya jina lake.”

Ufunuo 13:18 “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili, na aihesabu
hesabu ya mnyama huyo; maana ni hesabu ya kibinaadamu. Na hesabu
yake ni mia sita, sitini na sita.”

Biblia inatuambia kuwa hesabu au namba ya jina la mnyama ni 666


Kanisa la Romani Katoliki hudai kuwa Papa ni kichwa cha kanisa au
mwakilishi wa Yesu.

“Maneno yaliyoandikwa katika kofia (miter) ya Papa ni haya, ‘VICURIUS FILII


DEI’. ambayo ni ya kilatini kwa ajili ya ‘KASISI WA MWANA WA MUNGU’.
Wakatoliki huchukulia kwamba kanisa, ambalo ni jumuiya ya kuonekana,
lazima liwe na kichwa cha kuonekana. Kristo, kabla ya kupaa kwake
kwenda mbinguni, alimteua M.t. Petro kuwa kama mwakilishi wake…hata
hivyo Askofu wa Roma, kama kichwa cha kanisa, alipewa jina ‘KASISI WA
YESU.'” –Our Sunday Visitor, (Catholic Weekly) “Bureau of information,”
Huntington, Ind., April 18, 1915.

Kwa hiyo “VICARIUS FILII DEI” ndilo jina linalotumiwa na mamlaka ya Upapa
na kumthibitisha Papa kama kichwa cha kanisa.

Helufi za kilatini zinaweza kutumika pia kama namba, na siku hizi


hujulikana kama “Namba za Kirumi,” na helufi U inaweza pia kutumika
kama V.

“VICARIVS FILII DEI”

(Kasisi wa Mwana wa Mungu)

V 5

I 1

C 100

A 0
R 0

I 1

V 5

S 0

F 0

I 1

L 50

I 1

I 1

D 500

E 0

I 1

Jumla 666

Vicarius inamaanisha, katika nafasi ya

Filii Mwana

Dei Mungu

Hivyo, kanisa la Romani Katoliki linatimiza unabi huu wa hesabu ya


mnyama 666 kwa ukamilifu kabisa.

11. Onyo la Mungu kwa wote walio katika kanisa katoliki.

Mungu anaoya vikali sana juu ya wale wote ambao wanashirikiana na


mnyama huyu, kama wewe ni mmojawapo unapaswa kuchukua uamuzi
sahihi sasa bila kupoteza muda; kwa maana hukumu itakuja juu ya
mnyama na yule kahaba (kanisa Katoliki) aliyekaa juu mnyama. Hili ni onyo
la mwisho la upendo na la rehema kutoka kwa Mungu.

Ufunuo 14:9-10. “Na mwingine, malaika watatu, akafuata, akisema kwa


sauti kuu, Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na
kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye
naye atakunywa katika mvinyo ya gadhabu ya Mungu iliyotengenezwa,
pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye
atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za
Mwana-Kondoo.”

Ufunuo 19:20 “Yule mnyama akakamatwa, na yule nabii wa uongo pamoja


naye, yeye aliyezifanya hizo ishara mbele yake, ambazo kwa hizo
aliwadanganya watu wale walioipokea ile chapa ya huyo mnyama, nao
walioisujudia sanamu yake; hao wawili wakatupwa wangali hai katika lile
ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti;”

Ufunuo 18:4 “Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema,


Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee
mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika hata mbinguni, na Mungu
amemkumbuka maovu yake…Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja
katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa
moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemuhukumu ni mwenye nguvu.”

IMEANDALIWA NA MG SABATO MASHENENE WhatsApp 0753653270

Email Sabbathmtesigwa@gmail.com

You might also like