Professional Documents
Culture Documents
Lishe Ya Kuku
Lishe Ya Kuku
LISHE YA KUKU:
Ili kuku waweze kuishi, kukua vizuri, kunenepa na kutaga mayai mengi ni lazima wale chakula kingi na
chenye ubora unaotakiwa. Uwingi na ubora wa lishe ya kuku unaweza kuainishwa katika makundi ya
vyakula kama ifuatavyo:
5. Maji.
Makundi ya vyakula:
b. Nafaka kama vile mtama , chenga za mahindi ,chenga za mchele, uwele , na ulezi
c. Mimea ya mizizi kama vile muhogo, viazi vitamu na magimbi. Kabla ya kulisha kuku hakikisha mizizi
hiyo inalowekwa kwa muda wa saa moja au kupikwa kabla ya kukausha ili kuondoa sumu ambayo kwa
asili imo katika vyakula vya aina hii.Inashauriwa kuwa mizizi hiyo ilishwe kwa kiasi cha asilimia 10% ya
chakula chote anacholishwa kuku.
Katika kundi hili la kutia nguvu ,vyakula vya mafuta kama vile mafuta ya kutoka kwenye vyakula vya
mafuta kama mashudu ya mimea ya mafuta, mafuta ya samaki husaidia kuongeza nguvu na joto mwilini.
Vyakula vya kutia nishati huchangia asilimia 60-70 ya mchanganyiko wote wa chakula.
Ø Damu ya wanyama iliyokaushwa (waliochinjwa na kukaguliwa), hii inafanywa ili kuepusha uwezekano
wa kuku kupata magonjwa ya kuambukiza .
Ø Vyakula asilia kama vile minyoo, mayai ya mchwa, Masalia ya nyama toka kwenye ngozi/mifupa,
wadudu walioteshwa kutokana na damu au nyama iliyooza na vyakula vya aina nyingine.
Ø Vyakula hivi huchangia asilimia 20 hadi 30% ya mchanganyiko wote wa chakula cha kuku.
2. Vyakula vya kuimarisha mifupa(madini): a)Hivi ni vyakula vya madini ambavyo huhitajika kwa ajili ya
kujenga mifupa, maganda ya mayai, kukua na kuuweka mwili wa ndege (kuku) katika hali ya afya njema
kwa ujumla.
b) Madini ya muhimu ni madini ya chokaa (calcium) na fosiforasi (phosphorus). Ili kuku watage mayai
yenye ganda gumu ni lazima wapate madini ya chokaa maganda ya konokono na mayai yaliyosagwa
vizuri. Lakini inapendekezwa kwamba unapoongeza madini ya fosforasi inakubidi uongeze pia madini ya
chokaa kadri inavyopasa ,kwasababu kiwango cha aina moja kikizidi kuliko cha aina nyingine
husababisha upungufu wa kile kidogo
Ø Chumvi ya jikoni
Ø Magadi (kilambo).
Ø Mchicha, samadi ya ng’ombe ambayo haijakaa muda mrefu baada ya kunyewa, mchicha pori, Chinese
kabeji n.k.
Ø Chakula cha kuku wanaofugwa ndani ni lazima kichanganywe na vitamini zinazotayarishwa viwandani.
Kuna njia kuu mbili za kuchanganya chakula cha kuku, nazo ni;
o Njia hii hutumika viwandani kuchanganya chakula kwa ajili ya kuku wanaofugwa katika mashamba
makubwa.
Ø Kuchanganya chakula majumbani (home made ration): Hii ni njia inayotumika kuchanganya chakula
kwa ajili ya kulisha kundi dogo la kuku na njia ambayo inaweza kutumiwa na wafugaji wadogowadogo.
VIFAA; Beleshi /koleo(spade), Turubai/sakafu safi, Viinilishe , Viroba/Magunia kwa ajili ya kuhifadhia
chakula kilichochanganywa.
Chakula kilichochanganywa kinaweza kuwekwa katika uzani wa kilo 25-kilo 50, au kilo 100.
Jumla kilo 74
Jumla kilo 22
chokaa(dicalciumphosphate)… kilo 2
Jumla kilo 4
JUMLA 100
HATUA YA KWANZA:
Changanya , chokaa, chumvi na majivu ya mifupa pig mix vizuri - huu utauita mchanganyo Na.1
HATUA YA PILI:
Changanya mchanganyo huo na damu pamoja na samaki waliosagwa - huu utauita mchanganyo Na. 2
HATUA YA TATU:
HATUA YA NNE:
Mchanganyo Na.3 umwage juu ya rundo la pumba iliyochanganywa (pumba ya mahindi na pumba laini
ya mpunga).
o Chukua beleshi /koleo safi lililo kavu na kulitumia kuchanganya rundo la chakula ili kusambaza
viinilishe vizuri.
a) Baada ya kuchanganya chakula kitawekwa kwenye viroba au magunia na kutunzwa ghalani (stoo) hadi
pale kitakapohitajika kwa ajili ya kulisha kuku.
c) Chakula kilichochanganywa ni lazima kiwekwe sehemu kavu ili kisiharibiwe na unyevunyevu kama vile
kwenye chaga mabanzi yaliyotandazwa juu ya mawe yalipangwa vizuri
d) Chakula kilichoharibika hakifai kulisha kuku kwani kinaweza kusababisha matatizo ya afya.
Vilevile vitu mbadala aina ya nafaka vinavyopatikana hutegemea sana aina ya mazao yanayolimwa katika
eneo husika.
Mbinu za kuotesha mchwa na funza: Funza na mchwa ni chakula kizuri na rahisi chenye viinilishe aina ya
protini kwa kuku wanaofugwa kwa mfumo huria unaoboreshwa. Hata hivyo vyanzo hivi vya chakula cha
protini huchangia tu vile ambavyo kuku wanatakiwa kupewa.
a. Inashauriwa uwape vifaranga hao funza na mchwa kwa sababu ndio wanaohitaji protini kwa kiasi
kikubwa na cha kuaminika.
Funza na mabuu yanaweza kuoteshwa kwa njia rahisi na kutumika kuboresha chakula cha vifaranga.
c) Mafunza na mabuu yanaweza kuoteshwa kwa kutumia damu, viungo vya ndani ya tumbo la
ng’ombe pamoja na samadi ya ng’ombe.
d) Chungu kijazwe maji theluthi moja ya ujazo wake, inzi watakuja na kutaga mayai katika
mchanganyiko ambao mafunza walioteshwa wataanza kula mchanganyiko huo.
e) Baada ya hapo vitu hivi vyote vitachanganywa pamoja katika chungu kimoja kikubwa ambacho
kitaachwa wazi wakati wa mchana na kufunikwa wakati wa usiku.
f) Siku tano baadaye maji yatajazwa kwenye mtungi huo na mafunza yatakusanywa wakiwa wanaelea
juu. Baada ya kukusanya waoshe vizuri na maji halafu lisha kuku moja kwa moja.
g) Kumbuka kuweka chungu kinachooteshwa mafunza kuweka mbali na maeneo ya watu ili kuepuka
harufu inayoweza kusumbua watu.
KULISHA KUKU:
Idadi ya
vifaranga
Kiasi kinachotakiwa
100
100
100
100
100
100
§ Ni vigumu kukadiria mahitaji ya chakula cha kuku wanaojitafutia chakula, lakini inakadiriwa kuwa kuku
mmoja mkubwa wa uzito wa kilo 1-2 anahitaji chakula chenye uzani wa gramu 80-160 kwa siku kwa
kuku wanofugwa ndani lakini wale kuku wanafugwa kwa mfumo wa huria nusu huria mahitaji
yanakadiriwa kupungua hadi kufikia gramu 30-50 kwa siku .
§ Ifahamike pia kuwa kiasi cha chakula hutegemea mahitaji kutokana na uzito na uzalishaji, mfano kuku
anayetaga na anayekua wanahitaji chakula kingi zaidi ya wale ambao hawatagi au wamekoma kukua.
§ Hakikisha kuku wanawekewa chakula na maji safi kwenye vyombo safi na kubadilisha kila
vitakapoisha.