Professional Documents
Culture Documents
Mambo Ya Ndoaa5
Mambo Ya Ndoaa5
Mambo Ya Ndoaa5
Saimon
MAISHA YA NDOA
MAMBO YA KUZINGATIA ILI KUWA NA NDOA
YENYE FURAHA
EDWARD B. SAIMON
1
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
2
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
MAISHA YA NDOA
© Edward B. Saimon
Kimechapishwa na
Mpango Mkakati Technologies Co. LTD
P. O. BOX 5562 Dar es salaam, Tanzania
www.mpangomkakati.co.tz
info@mpangomkakati.co.tz
+255 715403214/ +255 767238675
3
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
YALIYOMO
SHUKRANI 7
DIBAJI 9
SURA YA KWANZA 1
KUSUDI 1
Kuhusu kuumba 8
SURA YA NNE 33
KUCHAGUA MARAFIKI 33
Mambo ya kuzingatia 34
SURA YA SITA 54
4
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA NANE 75
6
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SHUKRANI
Kwanza kabisa ninapenda kutumia nafasi hii kumshukuru Mungu
wetu wa Mbinguni ambaye alinitambua kabla sijazaliwa kwa
mafunuo yake kwangu kupitia Roho Mtakatifu ambaye
ameniwezesha kupata maneno ya kuzungumza na wewe juu ya
maisha ya ndoa; na hasa mambo unayopaswa kuyafahamu ili kuwa
na ndoa yenye furaha. Ninaamini maneno yaliyomo katika kitabu
hiki yatatengeneza kitu kipya ndani yako. Heshima na utukufu apewe
yeye tu, maana bila yeye nisingeliweza kitu.
Pili nina mshukuru sana mke wangu mpenzi Bi Leah Lukios pamoja
na wanangu wapenzi Jenivela, Saimon na Saraphina kwa moyo
wao wa uvumilivu kwangu pamoja na kuwa nami bega kwa bega
wakati wote na hasa wakati nikiandaa kitabu hiki. Kuna wakati
nilikata tamaa na kuvunjika moyo lakini kila nilipowatazama nilitiwa
moyo na kupata nguvu za kuendelea zaidi. Kuna wakati mke wangu
alikesha pamoja nami mezani nilipokuwa ninaandika na mara zote
alisikika akisema “kazana mume wangu Mungu analo kusudi la
kuponya ndoa za watu kupitia wewe”. Maneno hayo yamekuwa
yakinisukuma kuendelea.“Kitu pekee ninachoweza
kukuhakikishia mke wangu ni kwamba ninakupenda sana na
mara zote ninakuombea, nami ninaamini kwamba wewe na
watoto wetu mnaniombea maana ninauona ulinzi wa Mungu juu
yangu”.
7
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
DIBAJI
Kiini cha ustawi wa jamii ni ndoa. Tangu awali Mungu aliweka ndoa
kuwa taasisi ambayo inaamua ustawi na mustakabari wa ulimwengu.
Ni katika ndoa Mungu aliagiza kuzaa, kuongezeka, kuijaza nchi na
9
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Deogratius Sukambi
Mwalimu, Mshauri na Mchambuzi wa Mahusiano na Ndoa
11
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
UTANGULIZI
Kitabu hiki kinahusu mambo ya ndoa ambayo unatakiwa
kuyafahamu ili kuwa na ndoa yenye furaha.Nimesukumwa
kuandika kitabu hiki kwa sababu mambo yanayohusu ndoa kwa
walio wengi yanaonekana kutofahamika kwa sehemu kubwa kama
ilivyotazamiwa. Hatari kubwa inayolikabili kanisa la sasa na jamii
ni pamoja na vijana kutokujua nini wanatakiwa kufanya
wanapofikia hatua za kutaka kuingia kwenye ndoa.
13
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
14
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
15
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA KWANZA
KUSUDI
1
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
1.1.1 Kujitambua
2
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
a) Kimwili
b)Kiroho
Kujitambua kiroho inajumuisha mambo yanayohusiana na imani
kama vile kumwamini au kutokumwani Mungu, masuala ya toba na
kusamehewa dhambi, kuokoka, kuliamini neno la Mungu, kuwa
mtakatifu, kuongozwa na Roho Mtakatifu, kumwabudu na kumsifu
Mungu, kwenda kanisani kusali (kanisa gani), huduma yako kanisani
(mwimbaji, mwinjilisti, kukarimu wageni, mwombaji, mwalimu,
n.k.), ufahamu wako kuhusu nafasi ya Mungu katika maisha yako,
uongozi wa Mungu, kujilinda na dhambi n.k. Kabla ya kuingia
kwenye ndoa hakikisha unaujua upande uliosimama kiroho na hata
wale wanaokuzunguka wakikutazama wathibitishe hilo.Ukiamua
kuwa rohoni lazima kujijua kiroho umesimama kiasi gani,unaelewa
nini juu ya mpango wa Mungu. Unatakiwa kuzithamini ibada za
kanisa huku ukiiogopa dhambi.Amini juu ya uwepo wa Mungu ma
ana ukiamini utaona mafanikio makubwa.
c) Kiakili
4
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
5
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
juu kuliko zetu. Mipango yake iko juu kuliko yetu na kadhalika
mikakati yake kuliko yetu Yeremia 29:11. Maana nayajua mawazo
ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani wala si
ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
d) Kijamii
e) Kiuchumi
9
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
11
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA PILI
15
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
16
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
17
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
18
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
20
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
26
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
28
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
29
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA TATU
32
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA NNE
KUCHAGUA MARAFIKI
Rafiki ni mtu unayemfahamu, unamwamini na unayempenda sana
katika maisha yako ambaye mara nyingi si mtu wa familia yako.
Wataalam wanasema; watu wawili hawezi kuwa marafiki isipokuwa
75% ya tabia na mwenendo wao vimefanana. Biblia inasema watu
wawili hawezi kutembea pamoja isipokuwa wamepatana Amos 3:3.
33
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
37
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
4.2.2 Anayejiheshimu
38
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kuwa kielelezo ni ile hali ya kuwa mfano bora katika jambo fulani
kiasi kwamba watu wanatamani kuwa kama wewe, unaelekeza njia
na watu wakiifuata wanafika bila kupotea. Rafiki mzuri mwenendo
wake unatakiwa kuwa na mwelekeo mzuri, sio lazima awe kiongozi
au mtu maarufu ndani ya jamii lakini anatakiwa kuwa mtu ambaye
anajua kwamba anaishi ndani ya jamii ambayo inahitaji kujifunza
kutoka kwake. Kuwa kielelezo ni kitu muhimu sana kwa kuwa
atakuachia mambo mazuri ambayo utayatumia katika maisha yako.
Japokuwa wapo watu wenye maadili mema katika jamii lakini bado
unamhitaji Mungu ili akuwezeshe kudumu katika kuwa kielelezo
maana katika dunia ya sasa unaweza kujikuta uko katikati ya jamii
iliyomomonyoka kimaadili wakabadilisha mfumo wako wa maisha
kwa ujumla wake. Hivyo rafiki uliyenaye hakikisha wakati wote
anaongea mambo ambayo yanajenga na yenye manufaa kwa jamii
inayo mzunguka, sio mtu aliyejaa majungu na visasi ndani yake.
39
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
40
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
41
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA TANO
MAANA YA NDOA KWA MUJIBU WA
SHERIA ZA NCHI
Hii ni sheria inayotoa miongozo kuhusu haki na wajibu wa
wanandoa kwa upande mmoja, malezi, haki na maslahi ya watoto
katika ndoa kwa upande mwingine. Kwa mujibu wa sheria ya ndoa,
ndoa ni muungano wa hiari kati ya mwanamume na mwanamke
unaokusudiwa kudumu kwa maisha yao yote. Sheria hii imeainisha
aina mbili za ndoa ambazo ni: Ndoa ya mke mmoja na Ndoa ya wake
wengi.
43
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
1.Kidini:
Hii ni ndoa inayofungwa baina ya wanandoa wakristo, waislamu au
dini nyingine kwa taratibu za dini na madhehebu yao. Hii ina maana
kwamba ili ndoa ya aina hii itambuliwe ni lazima ifungwe kwa
majibu wa kanuni na taratibu za dhehebu husika. Mfungijishaji wa
ndoa hiyo lazima awe mwenye mamlaka ya kufungisha ndoa
anayetambulika kwa majibu wa sheria. Ndio maana wachungaji
wetu wanapofungisha ndoa wanasema kwa mamlaka niliyopewa na
Mungu na kwa mamlaka niliyopewa na Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ninakuuganisha wewe na wewe kuwa mke na mume tangu
sasa.
2.Kimila
Ndoa hii ni ile inayofungwa kwa kufuata mila na tamaduni za jamii
husika. Ifahamike wazi kuwa msichana kuishi kinyumba na mvulana
sio ndoa ya kimila. Ili ndoa itambulike kama ndoa ya kimila kuna
utaratibu ambao ni lazima ufuatwe. Kwenye kila jamii kuna wazee
waliotambuliwa na kupewa mamlaka ya kufungisha ndoa hizo.
Sheria inasema ili ndoa hiyo iweze kutambuliwa kwamba ilifungwa
kimila yule mfungisha ndoa hutakiwa kutoa taarifa juu ya kusudio la
44
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
kufunga ndoa hiyo kwa afisa tarafa ambapo atamwalika afisa tarafa
ili kuwepo siku ya tukio. Ndoa ya namna hii pia inaweza
kuandikishwa na kupewa cheti.
3.Kiserikali:
Ndoa hii hufungwa mbele ya afisa wa serikali mwenye mamlaka ya
kufungisha ndoa kwa kufuata taratibu zilizoainishwa na sheria ya
ndoa. Siyo kila afisa wa serikali anaweza au ana mamlaka ya
kufungisha ndoa ya aina hii, usije ukaamka asubuhi na kwenda ofisi
ya kata kwamba unakwenda kufunga ndoa. Ofisi yenye mamlaka ya
kufungisha ndoa za namna hii ni ofisi ya mkuu wa wilaya. Ndoa zote
hizi kisheria zinatakiwa kutangazwa kwa kipindi kisichopungua siku
21 ili kutoa nafasi kwa pingamizi kama lipo.
45
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
1. Maradhi ya zinaa
46
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
47
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
48
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
49
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
2.Hiari:
Lazima kila mmoja awe ameridhia kwa hiari yake bila hila kutumika
kupata hiari, kulaghaiwa au kulazimishwa na mtu yoyote. Hii ina
maana kwamba wanaofunga ndoa lazima wawe wamekubaliana wao
wenyewe, baada ya makubaliano ya watu hawa wanapokusudia
kufunga ndoa ndipo taratibu zingine zinazokubalika kwenye jamii na
kanisani zinafuata.
3.Jinsi:
Watu hao wanaokusudia kufunga ndoa lazima wawe watu wawili
wenye jinsi tofauti, mmoja awe mwenye jinsi ya kiume na mwingine
awe mwenye jinsi ya kike.Hii ina maana kwamba kwa sheria zetu
ndoa za watu wenye jinsi moja ni kosa na hazikubaliki
4.Wasiwe maharimu:
Maharimu ni watu wenye undugu wa karibu wa damu ambao
hawaruhusiwi kuoana. Kwa hiyo muungano huo usiwe wa watu
wenye undugu wa karibu ambao sheria imekataza watu wa uhusiano
huo kuoana. Watu wenye uhusiano wa kindugu waliokatazwa kuoana
wameelezwa katika kifungu cha 14. Kifungu hiki kinakataza mtu
kuolewa/kumuoa dada, kaka, baba, mama, babu, bibi, shangazi,
mjomba au mtoto aliyemuasili. Hao wanaokusudia kufunga ndoa
wanatakiwa wasiwe na undugu wa damu, kwa mujibu wa sheria zetu
watu wenye undugu wa damu hawaruhusiwi kuoana.
50
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
5.Pingamizi:
Kwa mujibu wa kifungu cha 18 sheria inatamka kwamba kabla ya
ndoa kufungwa ni lazima tangazo litolewe juu ya kusudio la kufunga
ndoa. Kifungu cha 26 kinatamka kwamba tangazo hilo liwe la siku
21 kabla ya ndoa kufungwa. Hata hivyo, kifungu cha 23 kinaruhusu
msajili wa ndoa kufungisha ndoa bila tangazo la siku 21 kama kuna
sababu za msingi. Lengo la tangazo ni kutoa nafasi kwa mtu mwenye
sababu ya kuzuia ndoa hiyo isifungwe kuweka pingamizi dhidi ya
ndoa hiyo kama inavyotakiwa katika kifungu cha 20(1). Kama
pingamizi limewekwa, basi mfungishaji ndoa hawezi kuifungisha
ndoa hiyo hadi pingamizi hilo litakapoondolewa.
51
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
9. Kudumu:
Wanakusudia kufunga ndoa wanathibitisha kwamba Muungano wao
unakusudiwa kudumu kwa muda wote yaani milele, hapatakuwa na
kuachana na kwamba kifo tu ndicho kitakachowatenganisha.
53
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA SITA
54
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
59
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Hatua ya Kuvutia
Kila mtu anapenda hatua hii kwa sababu imejaa nguvu, shauku na
mapenzi. Uko katika mapenzi na uko wazi kuwa unataka kutumia
maisha yako yote na mwenzi wako. Unafikiria juu ya mwenzi wako
siku nzima na unajiona kama wewe ni mmoja! "Katika kipindi hiki
kila kitu kinakuwa sawa, maisha yanaonekana kama ni nusu ya
ufalme wa Mungu. Katika kipindi hiki majina yote mazuri
yanatafutwa na kuwa radhi kuhakikisha kwamba hakuna
anayekwazwa na matendo ya mwingine. Wakati mwenzi wako
anakushirikisha jambo la kufurahisha, linganisha shauku yako na
yake, usiwe mtoa hoja au maoni ya kuua shauku yake.
Awamu ya Kuamka
Hatua ya pili inajumuisha kuishi siku kwa siku na jinsi kila mwenzi
anavyochukua majukumu yake wakati wanaishi pamoja. Katika
hatua hii, unaanza kumjua mwenzi wako vizuri zaidi lakini maswali
yake yanaanza kukukasirisha. Unaanza kugundua kuwa yeye sio
mkamilifu na labda unajaribu kufikiri namna ya kubadilisha tabia
zake ili awe kamili kama wewe kwa kuwa unafikri wewe ni bora
kuliko yeye. Wakati ukifikiri hivyo yeye pia kwa upande wake
anawaza hivyo. Mwishowe huzuni inaweza kukua na kusababisha
kudorora kwa uhusiano huo kwasababu matarajio yako yameanza
kwisha. Katika hatua hii kukatishwa na kukatisha tamaa kunaanza
60
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Hatua ya Machafuko
61
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
62
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Hatua ya Ushirika
Hatua ya Urafiki
63
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Utaratibu wa Utimilifu
64
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA SABA
KUSUDI LA MUNGU JUU YA NDOA
7.1 Mwanzo wa Ndoa
Mungu ndiye mwanzilishi wa Ndoa, yeye ndiye aliyeumba
wanandoa wa kwanza Adamu na Eva kama mume na mke. Maandiko
yanasema katika Mathayo 19:4 “yeye aliyewaumba hapo mwanzo
aliwaumba mtu mume na mke” Mwanzo 2:18 “Bwana Mungu
akasema, si vema mtu huyu aishi peke yake, nitamfanyia msaidizi wa
kufanana naye” Mwanzo 2:22 Mungu alipomaliza kumuumba
mwanamke,alimchukua na kumleta kwa Adamu. Mwanzo 2:24 hapa
kuna maswali kadhaa ya kujiuliza ni kwanini Mungu alipomaliza
kumuumba mwanamke alimleta kwa Adamu? Je hapakuwepo mahali
pengine ambapo ungepswa kumweka? Majibu yake ni rahisi sana,
asingemweka eneo lingine kwa kuwa aliumbwa kwa ajili ya Adamu,
huyu mwanamume adamu ndiye aliyehitaji msaidizi kwahiyo ilikuwa
65
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
68
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
f) Kuimarishana kiroho
69
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
70
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
v. Kujitegemea
72
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
74
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA NANE
MAMBO YANAYOMHUSU
MWANAMUME
8.1 Mwanamume ni nani hasa?
Mwanamume ni mtu yeyote mwenye jinsi ya Me wakati Baba ni sifa
na cheo cha ziada anachokipata huyo mwenye jinsi ya Me
kikiwakilisha uwajibikaji. Jinsi hii ya Me mwanamume anayo
kutokana na maumbile yake kibayolojia ambayo alijikuta yuko nayo.
Laiti kama kungekuwa na vikao kwa ajili ya kupitisha au
kumwondolea mtu hadhi ya kuwa na jinsi ya Me basi kuna watu nina
uhakika wasingalikubaliwa au wangenyang’anywa hadhi hiyo.
1. Mbeba maono
Baba ndiye mwenye maelekezo ya namna ya kuishi maisha bora
hapa duniani kwa wote watokao ndani yake, yeye anawajibika
kuwaelekeza na kuwaongoza kwa kutangulia mbele kama mfano wa
kuigwa. Mwanzo 2:15-16. Hii iko namna hiyo kwa kuwa baba ndiye
mbeba kusudi la Mungu kwa familia, yeye ndiye mwenye patano na
Mungu juu ya namna atakavyomwakilisha kwenye ngazi ya familia.
Kwahiyo kama wewe una familia na huna maono ya wapi
unakoipeleka wewe ni mwanamume siyo baba; ni kwa bahati mbaya
75
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
76
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
77
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Mtu mmoja aliwahi kusema “Mke wako anaendelea kuishi kwako sio
kwa kuwa wewe ni mzuri isipokuwa ni kwa kuwa unaweza kutimiza
mahitaji yake ya msingi, siku utakaposhindwa kuyatimiza basi
unaweza kuumwa hata na mbwa wako mwenyewe”; akasema pia,
“kama unataka heshima toka kwa mke wako, watoto wako na jamii
kwa ujumla fanya mambo matatu, la kwanza fanya kazi, la pili fanya
kazi na la tatu fanya kazi maana kazi ni msingi wa maendeleo na
78
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
4. Mtunza familia
Kama baba kwenye familia Mungu alikusudia wewe ndiwe uwe na
wajibu wa kwanza katika kuitunza familia hiyo; siyo Mungu tu na
hata sisi wengine ambao tunakutazama mategemeo yetu ni kwamba
wewe ndiwe mwenye wajibu wa kuilisha na kuihudumia
familia.Tunaposema familia yako tunazungumza mke na watoto
wengine ni ziada baada ya hawa kuridhika. Kumbuka maandiko
yanasema “utamwacha baba na mama” sasa kuna akina baba
wanajitahidi sana kuwaridhisha marafiki zao, wanakula hoteli huku
wakiwaacha wale walio wa msingi kwao wakihangaika. Hiyo siyo
sawa hata kidogo, 1Timotheo 5:8,“Lakini mtu yeyote asiyewatunza
walio wake yaani wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana imani,
tena ni mbaya kuliko asiyeamini”.
79
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kwa wazazi mnaosoma kitabu hiki na kwa bahati nzuri watoto wenu
wameoa au kuolewa ninawasihini sana kwa neema za Kristo Yesu
rizikeni na kile mnachopata kutoka kwa watoto wenu msitake wala
kulazimisha kupata sawa na wenzi wa watoto wenu. Kumbukeni
watoto wenu baada ya kuoa au kuolewa wanaanzisha nyumba na
kwa kawaida nyumba haijengwi ndani ya nyumba nyingine,
kumsomesha mtoto kusitumike kama kigezo cha kumtaka
akuhudumie kuliko yule anayewajibika kwake.
5. Mlinzi wa familia
Kulinda ni kukinga au kuzuia madhara, hasara au uharibifu visitokee
mahali fulani au visimpate mtu au kitu fulani. Mlinzi ni mtu
anayechunga na kulinda mali isiibiwe, ikiwa hivyo ndivyo maana
80
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
6. Tegemeo la familia
Tegemeo maana yake ni “tarajio la kupata kitu au hitaji kutoka kwa
mtu”. Kwahiyo wanafamilia wote wanategemea kupata mahitaji yao
kutoka kwa baba, baba amepewa wajibu na Mungu kuwa tegemeo la
wote walio chini ya uaangalizi wake ili awawezeshe kustahilimili
changamoto za kimaisha, awape mahitaji yao, awakuze ili wafikie
hatua ya kujitegemea na kuendesha maisha yao. Kwa hiyo kila alipo
baba lazima ajue kwamba waliopo nyumbani mwake wanamwona
kama tegemeo. Na unapokuwa tegemeo lazima ujitahidi kujua wale
wanaokutegemea wanakuonaje. Waefeso 6:4. Ili uonekane wewe ni
tegemeo lazima wale wanaokutegemea wafikie hatua ya kujipiga
kifuani kwamba tunaye baba, huyu ndiye hufanya hiki na kile,
ukiona kwenye familia yako mambo ni tofauti na hivyo anza
kujifanyia tathimini.
7. Mtetezi wa familia
Baba anawajibika kuitetea familia yake kwa nguvu na uwezo wake
wote.Hii ina maana kwamba kila mara unapoona mmoja wa
wanafamilia wako anapata shida unawajibika kusimama naye mpaka
mwisho kuhakikisha kwamba haki yake inapatikana.Huu siyo
mlango wa kufanya upendeleo bali ni wajibu wa kuhakikisha
kwamba walio chini ya dari yako hawakumbwi na madhara wala
uonezi. Bila shaka umewahi kusikia watoto wakitambiana mitaani
kwamba “usicheze na baba yangu, yeye ni kiboko” Maana yake ni
82
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
8. Kuhani
Katika agano la kale Kuhani alihusishwa na usimamizi wa utoaji
dhabihu na sadaka katika madhabahu ya Mungu pamoja na
kusimamia ibada ya kumwambudu Mungu.Majukumu haya ya
kikuhani anayo baba kwenye familia maana ni kiongozi
anayemwakilisha Mungu katika mambo yote yahusuyo maisha ya
kiroho ya familia yake.Anawajibika kuijulisha na kuifundisha familia
yake juu ya mapenzi na rehema za Mungu zilivyo kuu kwao kama
familia,masuala ya utumishi ikiwa ni pamoja na kumtolea
Mungu.Mara zote baba usisahau kuomba rehema na neema juu ya
familia yako maana yumkini wamemtenda Mungu dhambi bila wewe
kujua Kumbukumbu 31:12-13. Kwahiyo kama watoto kwenye
familia hawamjui Mungu anayewajibika katika kuwafanya wamjue
ni baba, Kumbukumbu 6:6-9.
9. Mwalimu
Mwalimu ni mtu mwenye ujuzi wa kufundisha jambo, ni mtu
anayemwelekeza mtu mwingine ujuzi, ufahamu au uelewa. Baba
kama mwalimu kwa familia yake anao wajibu wa kuwafundisha
wanafamilia wake kila lililo jema. Kumbuka yeye ndiye mbeba
maono, ndiye aliyepewa kusudi na Mungu hivyo anao wajibu wa
83
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
84
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
10. Mfalme/mtawala
Mfalme/mtawala ni nani?
Huyu ni mtu ambaye anasimamia ufalme au utawala.Kuna
uwezekano wa mtawala kuwa mzuri au mbaya, kuwa mtawala mzuri
mzuri au mbaya haiondoi sifa ya kuwa mfalme/mtawala.
Utawala ni nini?
Ni mchakato unaohusisha taratibu za usimamizi na uendeshaji wa
shughuli za kiserikali au taasisi. Mchakato huo hujumuisha namna
maamuzi yanavyofanywa, ushiriki katika kufanya maamuzi,
utekelezaji, usimamizi, ufuatiliaji na ufanyaji wa tathmini. Mtawala
mzuri ni yule anayetawala kwa kuonyesha mifano yaani kwa
kutangulia mbele kwanza na kuwataka wengine kumfuata na
anapoagiza jambo lifanyike afuatilie kuona limetekelezwa kama
alivyoagiza na kama ni tofauti basi atake kujua visababishi; kama
limetekelezwa vizuri, mtekelezaji apongezwe kwa kufanya kazi
kama alivyoelekezwa.
hilo kwa undani, pata ushauri kwa watu wako wa karibu ili kwamba
usifanya maamuzi ya kukuumiza na kukufanya ujute baadaye.Baba
kama mtawala akianza tabia ya kusikiliza maneno ya uongo kutoka
kwa watu wasiokuwa na nia njema na familia anaweza kusababisha
madhara makubwa kwenye familia Mithali 29:12. Baba awe mfano
wa kuigwa katika mwenendo na usemi, asiwe mtu wa nia mbili, awe
mwenye kuisimamia nyumba yake vema,ajuaye kutiisha watoto
wake katika maadili yampendezayo Mungu na hata wanadamu pia.
SURA YA TISA
MAMBO YANAYOMHUSU
MWANAMKE
Kuna mambo muhimu yanayomhusu mwanamke ambayo
mwanamume anatakiwa kuyajua kabla hata hajafikiria kumtafuta
kama msaidizi au mwenza wa maisha, miongoni mwa mambo hayo
ni pamoja na mwanamke ni nani? Ni upi mwenendo na msingi wa
kutenda au kutotenda kwake? Kwa nini aliumbwa? Na aliumbwa
kwa kusudi gani? Utakumbuka Mungu anasema “si vema mtu huyu
aishi peke yake” Kwahiyo ina maana ili majukumu aliyopewa
mwanamume yatimizwe vizuri ni lazima mwanamke awepo. Hivyo
basi kila kitu alichonacho mwanamke alipewa ili kumsaidia
mwanaume kutimiza wajibu wake ndio maana kuna msemo kwamba
“kwa kila maendeleo ya mwanamume nyuma yake yupo mwanamke”
86
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
1. Msaidizi wa mwanamume
Ndani ya mama Mungu ameweka nguvu na uwezo wa kumsaidia
baba kutimiza majukumu yake kuelekea kulitimiliza kusudi na
majukumu ndani ya familia kama ulivyo mpango wa Mungu. Uwezo
huu aliopewa mama ni muhimu ukitumika vizuri kwa makusudi
yaliyokusudiwa na siyo kule kutaka kuwa sawa na baba.Wakati
mama akijua na kujali kuwa yeye ni msaidizi mwanamke atataka
kuwa sawa na mwanamume, hakubali hata kidogo kuitwa msaidizi
wa mwanamume, kwake hilo analiona kama ni kushuka thamani, na
mara zote anapigania haki sawa kati yake na mwanamume.
Miongoni mwa usaidizi wa mama kwa baba ni pamoja na:-
2. Kushawishi
Inaaminika kwamba theluthi moja ya siku za maisha ya mwanadamu
yeyote aliyezaliwa duniani huitumia akiwa mikononi mwa mama,
mama ndiye humfundisha mtoto mambo mengi ya awali kuliko mtu
mwingine yeyote, Ezekiel 16:44 hapa ndipo penye umakini sana.
Kama mama akishindwa kushika nafasi yake kubaki na nafasi kama
mwanamke basi tegemea watoto wako kuwa katika mazingira
ambayo si yale uliyoyatazamia. Maandiko yanathibitisha kwamba
mwanamke/mama ana maneno yenye nguvu kubwa ya ushawishi,
yaani ni kwamba mwanamke/mama akiamua kukukamata kwa
maneno yake hakuna anayeweza kufurukuta, lazima unasalimu amri
Mithali 7:21,“Mategemeo yangu ni kwamba uwezo huu mama
atautumia kuwafundisha watoto wake na sio kinyume chake”.
3. Mzalishaji wa mali
88
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
4. Mvumilivu
Kwa namna mwanamke alivyoumbwa ni mwenye uwezo mkubwa
wa kuvumilia hali na changamoto mbalimbali anazopitia. Mama ana
uwezo mkubwa wa kuchukuliana na hali yoyote hata watu wale
ambao kwa macho ya kawaida unaona kwamba hawakustahili na
haiwezekani kuwavumilia lakini anavumilia kwa kuamini kwamba
ipo siku watabadilika. Mfano mzuri wa uvumilivu ni pilikapilika za
ujauzito pamoja na kujifungua. Manesi na madaktari wanajua hili,
mama anapojifungua anaapa viapo vyote vya kutorudia lakini baada
ya miezi au miaka kadhaa unamkuta na mimba nyingine. Mambo
haya na mengine mengi yanaonesha uwezo mkubwa wa uvumilivu
alionao mwanamke. Uwezo huu wa uvumilivu kama ukithaminiwa,
kutunzwa na kulindwa unaweza kumsaidia mwamume katika
kutimiza wajibu wake.
5. Mtunza uhai
Kwa kawaida mama ni mwangalifu sana linapokuja suala la kutunza
uhai wa mtoto. Mama anayenyonyesha kwa mfano akisikia mtoto
analia akiwa ndani anaweza kujua kilio hiki mtoto kakojoa, ana njaa
89
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
6. Kunyonyesha
Afya na kukua kwa mtoto hutegemea maziwa ya mama. Maziwa ya
mama ndicho chakula pekee, bora na kamili kwa ajili ya makuzi ya
mtoto. Wataalam wanasema mama anatakiwa kumnyonyesha mtoto
wake ndani ya lisaa limoja baada ya kujifungua na aendelee
kumnyonyesha maziwa bila kumpa kitu kingine chochote ndani ya
miezi sita ya mwanzo.Maziwa ya mama ndiyo yanayosaidia
kutengeneza ubongo wa mtoto,kinyume chake kama mtoto
hatanyonyeshwa ipasavyo ubongo wake hautakuwa kwa kiwango
kinachotakiwa na madhara yake ni kwamba ubongo wake hautakua
katika kiwango kilichotazamiwa.
7. Mbembelezaji na mfariji
Mama kwenye familia tunategemea akitaka jambo kutoka kwa baba
atumie uwezo wake wa kubembeleza kwa kuwa ndani yake Mungu
ameumba uwezo huo Isaya 66:12-13 lakini akina mama wengi
wameshindwa kufanya hivyo badala yake wanatumia nguvu na
ubabe ambao kimsingi Mungu hajawapatia. Hatutegemei mama awe
mkali kama moto wa kiangazi ndani ya nyumba,mama anategemewa
kuwa mfariji ili kwamba baba anaporudi akiwa amevurugwa apate
faraja kutoka kwake.Ukweli ni kwamba wanawake wengi
wamewapoteza na kuwafukuzia mbali kinababa kwasababu ya ukali.
Hii ni kwasababu hakuna mwanamume ambaye yuko tayari
kudhalauliwa. Na akikuponyoka kutokana na ukali wako kumrudisha
utahitaji nguvu ya ziada. Lakini jiulize, kwanini utumie nguvu kubwa
wakati uwezo wa kumweka chini ya himaya yako kwa
kumbembeleza na kumfariji unao?
91
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
8. Mpole
Upole katika biblia lina uhusiano wa karibu na unyenyekevu pamoja
na uvumilivu. Hii ni tabia yenye nguvu sana ambayo iko kinyume na
ubinafsi na kiburi, upole humsaidia mtu kuvumila lawama hata kama
hakuzistahili huku akisamehe na kuachilia. Mama anayejitambua na
ambaye anaijua nafasi yake kama mama hii ndiyo silaha na nguo za
kuijenga ndoa yake.Mke ananyenyekea kwa mumewe kwa kuwa
anajua kuwa mume ni kichwa cha familia, anatii kama kumtii Kristo
lakini mwanamke wakati wote anataka haki sawa, ulinganifu,
kulingana na kuwa sawa jambo ambalo kwenye ndoa linaifanya
isambalatike. Mwanamume ukitaka kupima urefu na upana wake
mguse kwenye hili eneo la kutaka kuwa sawa naye, hapo utaona na
kugundua rangi zote alizonazo, usijaribu wala kuruhusu kujaribiwa
katika eneo hili kwa kutaka kuwa sawa na mumeo.Wataalamu
wanasema sura nzuri ya mwanamke inampa 75% za kuolewa lakini
upole na unyenyenyekevu zinampa 100% za kudumu kwenye ndoa.
9. Mwalimu
Maana na fasili ya mwalimu tumekwisha kuieleza katika kipengele
kilichotangulia hapo juu, hivyo mama anatakiwa kuwa na sifa za
mwalimu ambazo ni pamoja na zifuatazo:-
a. Mzazi/mlezi
b. Hakimu/mwamuzi
c. Daktari
d. Mshauri
Mama kwenye nyumba (ndoa) anatakiwa kuwa na sifa hizi, sio kila
mara mama atakuwa hakimu, na sio mara zote atakuwa daktari.
Anatakiwa kuuvaa uhusika kulingana na mazingira. Lazima ajue
mazingira aliyomo na kujua aina gani ya sifa ifanye kazi katika
92
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
10. Malikia
Malikia ni nani?
Ni mke wa mfalme, anastahili heshima kwa kiwango sawa na cha
mfalme. Anatumikiwa na wakati mwingine huwaamrisha walio chini
yake ili kutekeleza matakwa yake au yale ya mfalme. Mama kwenye
nyumba ipo siku na wakati anavaa hiki cheo, muda huo kutenda
kwake lazima kufanane na malkia.Sio anakuwa malkia halafu
anatenda kama muuza matembele, haiwezekani.Maana yake ni
kwamba kwenye nyumba unakaa na kutumikiwa,unaagiza
unachotaka kifanyike kisha unafuatilia kuona kama kimefanyika
kama ulivyoagiza.Bahati mbaya sana hiki ndicho cheo pekee
mwanamke anakitamani na kukipenda kuliko vyeo vingine. Anataka
kuamrisha kila mtu ndani ya nyumba mpaka na mfalme; hii ni ajabu!
93
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
SURA YA KUMI
TOFAUTI ZA KIMAUMBILE KATI YA
MWANAMUME NA MWANAMKE
Kimaumbile mwanamume na mwanamke wametofautiana sana.
Utofauti huo wa kimaumbile unahusu pia utofauti katika mahitaji
yao, jambo ambalo linaonekana kuwa la muhimu kwa mwanamume
linaweza lisiwe na umuhimu ule ule kwa mwanamke. Ni muhimu
kwa mwanamume na mwanamke pia kujifunza na kuzijua tofauti hizi
za kimaumbile zilizopo kati yao. Kuzijua kunakusaidia kuishi kwa
amani maana jambo likifanyika utakuwa unajua huyu ndivyo
alivyoumbwa na Mungu hakuna namna ninavyoweza kumbadirisha
ila naweza kumwombea.
94
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
95
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
96
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
100
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
102
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
103
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
11.4 MSAMAHA
Ndoa nyingi zina shida kwasababu ya wanandoa kushindwa
kusameheana. Ni kweli kwenye ndoa kuna mambo mengi ambayo
katika hali ya kibinadamu yanaweza kukufanya ushindwe kusamehe,
nami kama Mwalimu sinabudi kukufundisha kile ambacho neno la
Mungu limeelekeza kwamba tafuteni kwa bidii kuwa na amani na
watu wote, Waebrania 12:14.Watu wote ukianza na mumeo,
hatutegemei uwe na mahusiano mazuri na watu wa nje, wakati mume
wako hutaki kumsamehe, utakuwa unajidanganya nafsi yako. Hivyo
bila kujali mumeo/mkeo amefanya kosa gani ni lazima ujifunze
kusamehe na kusahau. Hii ni kwasababu kutokusamehe ni kumpa
110
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
112
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
114
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Nafsi:
Kwenye nafsi ndipo kuna nia, hisia na maamuzi juu ya maisha,
kufikiria kwetu juu ya maisha kunatokea kwenye nafsi; kwahiyo basi
ikitokea Shetani akakamata nafsi mojawapo kati ya mume au mke;
119
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Tamaa:
Tamaa ni moja ya vitu vinavyoleta shida katika ndoa.Asili ya
mwanamke ni kutamani Mwanzo 3:6, tamaa hii ipo katika vitu.
Hivyo Mungu alipokuwa anatoa adhabu kwa mwanamke,
alimwambia na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye atakutawala.
Mwanamume mara nyingi tamaa yake inakuwa kwa wanawake siyo
kwenye vitu. Hii ni kutokana na asili ya mwili wa mwanamume
ambao uwezo wake wa kuzaa haufungwi katika majira na nyakati
kama ilivyo kwa wanawake.Kwa lugha nyingine mwanamume
anaweza kuzalisha saa yeyote lakini mwanamke inategemeana na
majira.Na kwa kuwa Mungu alitwambia zaeni mkaongeze Mwanzo
1:28, dhambi ilivuruga na kuliweka hilo kwenye tendo la ndoa. Ndio
maana Yesu alisema “Kila amtazamaye mwanamke kwa kumtamani,
amekwisha kuzini naye moyoni mwake” Mathayo 5:28
Kutoondoka kwenu:
Kwasababu hiyo mtu atamwacha baba na mama yake naye
ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja
Waefeso 5:31.Huu msitari ukiusoma haraka unaweza kudhani
123
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kutoilinda imani:
Hiki ndicho kipengele cha muhimu kuliko vyote kwani maandiko
yanasema tunaishi kwa imani.Hivyo hata katika ndoa tunatakiwa
tuishi kwa imani. Kwa kuwa maisha yetu yanategemea imani yetu
kwa Kristo, vita kubwa iliyopo kati yetu sisi na shetani ni kile
kilichopo ndani yetu ambacho ni imani, siyo ndoa. Ndoa ni mlango
ambao Shetani anautumia kukutenga na imani kwa Yesu. Unapoona
ndoa imevunjika au ina misukosuko ujue kwamba kuna kiwango
fulani cha imani ambacho kimepungua au hakipo kabisa. Maandiko
yanatueleza kwamba pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu,
matatizo mengi kwenye ndoa ni matokeo ya kile kilichokosekana
125
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kutokuwa na Maombi:
Maombi ni muhimu sana katika ndoa, ni muhimu kwa kuwa suala la
ndoa pia ni la kiimani, changamoto kubwa ambayo inazikabiri ndoa
nyingi kwa sasa ni wanandoa kuanza maombi wakishapatwa na
matatizo ila wanapokuwa kwenye raha wakiitana majina yote mazuri
huoni wala kusikia maombi; kumbe kwa kufanya hivyo inakuwa ni
sawa na kulala wakati milango ikiwa wazi. Ni mhimu kuomba kwa
sababu maombi ndio nguzo inayozuia matatizo yasitokee.Usisubiri
umepigwa na adui ndipo uingie kwenye maombi.
126
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Hivyo akina mama watumie karama hiyo na kubeba ndoa zao katika
maombi kwani bila maombi ndoa haitaenda.Tusisubiri kufanya
maombi wakati tukiwa na matatizo, ukweli wenyewe ni kwamba
ukiwa na matatizo huwezi kuomba badala yake utalalamika kwa nini;
kwasababu kila utakapokuwa unajitahidi kusema unaomba utaiona
sura ya yule aliyesababisha tatizo husika na kama kulitokea maneno
basi sauti ile itakuwa ikijirudiarudia masikioni.Ni vema wanandoa
wakawa na utaratibu wa kufanya maombi ya shukrani katika yale
mengi ambayo Bwana amewatendea bila kusahau ulinzi kwenye
ndoa na familia kwa ujumla wake na kila mwanandoa ahakikishe
analo neno la Mungu kwa wingi ndani yake.
12.3Mambo ya kukumbuka
Wazia nyumba ambayo imeachwa bila kutunzwa kwa muda mrefu
kidogo hali iliyopelekea rangi yake kuanza kubanduka banduka, paa
yake imeharibika na nyasi zilizoota hazijakatwa, kwa kuitazama
nyumba hiyo imepigwa na dhoruba kwa miaka mingi nayo
imechakaa. Je kuchakaa huko kumeifanya ibomolewe? Si lazima,
ikiwa msingi wake ni imara na muundo wake ni thabiti, nyumba hiyo
inaweza kurekebishwa.Je hali ya nyumba hiyo inakukumbusha ndoa
yako?Kwa miaka mingi, huenda dhoruba za mfano zimeiathiri ndoa
yako, inawezekana mmoja wenu au nyote wawili mmeiachilia ndoa
yenu kwa kiasi fulani. Hata kama hali katika ndoa yako iko
hivyo,usiende haraka kwamba inapaswa kuvunjwa.Ndoa yako
inaweza kurekebishwa.Mengi yanawategemea wewe na mwenzi
wako mnavyotimiza wajibu wenu katika ndoa.Kufanya hivyo
kunaweza kuimarisha ndoa yenu wakati wa majaribu.
Wajibu
Wajibu katika ndoa humaanisha kulazimika kutimiza au kujiwekea
masharti ya jambo fulani.Ni ile hali ya kusurutishwa kutimiza jambo
fulani kwa mwenzako hata kama kunaonekana ugumu fulani katika
128
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Ushirikiano
Siyo kwamba wanandoa hawatofautiana mawazo na mtazamo,
hapana hata vyombo vikiwa pamoja kwenye kabati vinagongana
itakuwa binadamu.Wanapogombana/kutofautiana wanapaswa
kujitahidi kutatua tatizo hilo, si kwasababu ya nadhiri walizofanya
bali kwasababu wanapendana.Yesu alisema hivi kuhusu mume na
mke wao si wawili tena, bali mwili mmoja.Inamaanisha nini kuwa
mwili mmoja na mwenzako? Paulo aliandika kwamba wanaume
wanapaswa kuwawapenda wake zao kama miili yao wenyewe
Waefeso 5:28, 29.Hivyo basi, kuwa mwili mmoja humaanisha
kuhangaikia hali njema ya mwenzako kama unavyohangaikia hali
yako mwenyewe.Wanandoa wanatakiwa kubadili mtazamo wao,
129
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kutokuwa na Ubinafsi
Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho
kutakuwa na nyakati za hatari. Kwa maana watu watakuwa wenye
kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye
kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na
shukrani, wasio watakatifu, wasio na upendo,wasiopenda
kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili,
wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao
anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu.Inaonekana watu wengi
kwenye ndoa hujifikiria wenyewe zaidi kuliko kuwafikiria wenzi
wao.Katika ndoa nyingi, kujitoa kumfanyia mwenzako jambo fulani
bila kuwa na hakika kwamba atakufanyia vivyo hivyo,huonekana
kama ni udhaifu.Hata hivyo ukweli umejidhihirisha kuwa ndoa
nyingi zilizofanikiwa ni zile ambazo wanandoa wote wameonyesha
130
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
132
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kuna sehemu kuu tatu katika mawasiliano ya ana kwa ana miongoni
mwa binadamu sehemu hizo ni pamoja na: - miondoko ya mwili, toni
ya sauti na maneno. Kulingana na utafiti imethibitika kwamba 55%
ya athari hulingana na miondoko ya mwili. Kwa mfano: jinsi mtu
alivyokaa, ishara za uso, mikono na macho, 38% hulingana na toni
ya sauti, na 7% hulingana na maudhui (ujumbe au maneno)
yaliyotumika katika mawasiliano. Kwahiyo mwanandoa
unapowasiliana hakikisha unazingatia asilimia hizi, upo uwezekano
mkubwa wa kuwa unaeleza kitu fulani lakini msikilizaji akikutazama
anapata ujumbe tofauti na ule unaousema.
134
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
136
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
137
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
138
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Mawasiliano binafsi
Haya ni mawasiliano yanayofanyika kwenye akili yako mwenyewe
bila kushirikisha upande wa pili. Mara nyingi mawasiliano haya
hufanyika kimya kimya ingawa wakati fulani yanaweza hufanyika
kwa sauti. Hapa ndipo penye kituo cha hisia zetu, imani zetu,
misimamo yetu na maamuzi yetu, hii ni dhamiri inayotushuhudia
kwa ndani, mtu wa nje yako hawezi kuisikia ingawa kwako muda
wote unakusurutisha. Luka 15:18 “Nitaondoka, nitakwenda kwa
baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele
yako.” Mawasiliano haya Mungu huyatumia anapotaka kukuelekeza
kitu cha kufanya, lakini pia hata shetani huyatumia kukushawishi
kufanya yaliyo kinyume na mapenzi ya Mungu.
Mawasiliano ya wawili
Haya ni mawasiliano baina ya watu wawili. Katika mawasiliano haya
kuna uwezekano wa maana iliyokusudiwa kupotoshwa. Mwanzo
3:10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa
mimi ni uchi; nikajificha. Kwahiyo unapowasiliana na mwenzako
kila mara hakikisha unathibitisha kile alichokisikia kama kinaendana
na kile ulichokisema au kukimaanisha. Hii ni kwa sababu kila mmoja
kati yenu ana namna ya kusikia na kutathimini vitu anavyovisikia,
jitahidini kuzizuia hisia zenu kwenye eneo hili la mawasiliano.
141
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Kusikia na kusikiliza:
Kusikiliza ni kujaribu kuzielewa hisia za mwingine. Ni kukubali kile
kinachosemwa bila kuhukumu mantiki yake ama namna
kinavyosemwa. Kukubali haimaanishi kukubaliana moja kwa moja
na msimamo wa msemaji bali ni kutambua na kuelewa kuwa
kilichosemwa ndicho msemaji anachokihisi na anachomaanisha.
Kusikiliza pia humaanisha uwezo wa kurudia kilichosemwa katika
jitihada za kujiridhisha kama ulichoelewa ndicho kilichokusudiwa na
kilichokuwa kwenye hisia za mzungumzaji. Ni lazima ujiridhishe
kama kile unachokusudia kukiweka kwenye kumbukumbu zako ni
kile kilichomaanishwa na mzungumzaji au ni tafsiri yako tu isiyo
sahihi.
142
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
143
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
Msilipize kisasi
Kulipa kisasi kwenye ndoa ni jambo baya sana, ni nani hasa
unayemlipa kisasi? Kumbuka kwamba mke hana amri juu ya mwili
wake na kadharika wewe pia na katika ulimwengu wa roho miili
yenu mmebadirishana, ikiwa hivyo ndivyo maana yake ni kwamba
kisasi unacholipa unajilipa mwenyewe, maanandiko yanaonyesha
wazi kwamba kulipa kiasi ni dhambi Warumi 12:19-21 wapendwa,
145
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
148
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
150
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
1. Usikate mawasiliano
Kumbuka siku unakutana na mchumba wako kwa mara ya kwanza
mlielewana kwa njia ya mawasiliano, hivyo bila mawasiliano mazuri
kati ya mke na mume fahamu ndoa yenu iko kwenye matatizo.
Kuongea pamoja, kuelezana pamoja kile ambacho kila mmoja
anakihitaji katika maisha yenu ya ndoa huleta maelewano mema kati
yenu. Ni kweli kwamba kadri mnavyozidi kuishi pamoja
mawasiliano yaweza kupungua kwasababu ya kuzoeana sana lakini
151
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
2. Sikilizaneni
Masikilizano mema ni muhimu kwa afya ya ndoa yenu. Kuwa tayari
muda wote kumsikiliza mwenzako. Baada ya ratiba ngumu za siku
kuwa na hamu ya kumsikiliza mwenzako kwa kumuuliza maswali
mbalimbali, lakini kumbuka wakati mwingine hata mke au mume
wako naye anahitaji kukuuliza au kukusikiliza, hivyo epuka kutoa
hitimisho wewe tu! Fungua masikio yako na usikilize kile
anachosema mwenzako. Usitake kuwa mzungumzaji wa mwanzo
mwisho kama mhubiri kanisani, humo ndani ni kuzungumza sio
kuhubiri, hakuna hotuba kuna mazungumzo maana yake unasema
ulichonacho na kutoa nafasi kwa mwenzako naye kusema alicho
nacho huku ukisikiliza.
3. Ucheshi na ukweli
Moja ya kitu muhimu sana katika kuwa na ndoa bora ni ucheshi kwa
wana ndoa. Ni vigumu sana kubaki na hali ya kufurahi na kucheka
pamoja lakini mnaweza kufanikiwa katika hili kwa kutembelea wote
katika maeneo mapya kwa pamoja mkiwa wenyewe tu wewe na
mume ama mke wako. Kuwa muwazi na mkweli ni msingi muhimu
sana kwa wanandoa, hakikisha unakuwa mkweli kwa mke au mume
152
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
4. Onyesha upendo
Hakikisha unatumia muda mwingi kuongea na yule umpendaye.
Unaweza kuwa mbali na mume au mke wako lakini unaweza
kumudu kuongea na umpendaye hata kwa njia ya simu, ili mradi tu
kuonyesha kuwa unampenda na kumjali. Onyesha unampenda sana
mke au mume wako daima. Kila siku hakikisha unadhihirisha
upendo wako kwake usichoke.Mbusu mke au mume wako,
mkumbatie kila mara kama ishara ya upendo. Kama mtapendana kwa
dhati basi bila shaka mtaheshimiana, na kila mmoja atamthamini
mwenzake. kila siku tafakari kwa nini ulimpenda yeye tu na wala si
mwingine, hii itakufanya umpende zaidi.Usijali wengine watasema
nini juu yako, shida kubwa inayotukabili ni kule kushindwa
kuonyesha upendo kwa wake au waume zetu kwa kuogopa macho ya
watu;wanaume wanaogopa kuambiwa wameshikwa na wake zao,
sielewi hivi kushikwa na mke wako ni kosa? Sasa kama hujashikwa
na mke wako ambaye ni nyama katika nyama zako unataka kushikwa
na nani zaidi?
6. Kuvumiliana.
Wanandoa wanaofanikiwa katika maisha yao ni wale wanaopokea na
kutoa msamaha. Ni wale wanaosamehe na kusahau makosa ya
wengine.Hivyo kusameheana ni jambo la muhimu sana katika
mahusiano.Wanandoa wanaofanikiwa kuishi muda mrefu wakiwa na
furaha daima ni wale wanaovumilia hali zote za maisha. Mfano
wakati wa magonjwa, wakati wa utajiri, wakati wa umaskini, wakati
wa afya njema. Kama wanandoa wataweza kuvumiliana katika hali
zote basi wataishi kwa furaha.
156
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
"Hakuna kitu bora au cha kupendeza zaidi kuliko wakati watu wawili
ambao wanaona uso kwa nyumba kama mtu na mke, wakichanganya
maadui zao na kufurahisha marafiki zao." ~ Homer
157
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
158
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
160
Mambo ya kuzingatia ili kuwa na ndoa yenye furaha……….. Edward B. Saimon
KUHUSU MWANDISHI
MWANDISHI
Edward B. Saimon ni mtoto wa kwanza kuzaliwa katika
familia yenye watoto sita ambayo ni ya bwana na bibi
Bihaga Saimon Masela. Huyu ni mwalimu wa malezi ya watoto na
vijana, amekuwa akifundisha semina mbalimbali kwenye jamii na
kanisani.
162