Professional Documents
Culture Documents
769 Grade 4 End of Term 3 Kiswahili Exam 2021 Word Format 2 3x7dm8
769 Grade 4 End of Term 3 Kiswahili Exam 2021 Word Format 2 3x7dm8
SHUGHULI ZA KISWAHILI
GRADE YA NNE
SEHEMU YA KWANZA
Mtoto tiifu ni mwema. Si mjeuri. Si mtukuku. Ana heshima na adabu njema. Akiitwa huitika
vizuri na kwa heshima. Akitumwa hakatai. Akikanywa asifanye kosa hutii.
Mtoto tiifu huwapenda wazazi wake. Huwasaidia wazazi wake kwa kazi zote za nyumbani.
Hazururi ovyoovyo na kuenda na watoto wengine watukutu. Yeye akitaka kutoka nyumbani
kwenda mahali huomba ruhusa kwa wazazi. Nao wazazi wakikataa asiende, hakasiriki wala
hanuni na kuvimba mashavu kama paka.
Mtoto tiifu hupenda masomo shuleni, hachelewi kuingia darasani. Hufanya kazi zote za
shuleni na huwasikiliza walimu wake kwa makini. Pia, hagombani na watoto wengine shuleni.
Yeye ni mfano mwema shuleni na nyumbani. Je, wewe ni mtoto mtukutu au tiifu?
SEHEMU YA PILI
UFAHAMU (alama 10)
RAFIKI YANGU
Rafiki yangu anaitwa Fatuma. Yeye ni msichana mwenye rangi ya kahawia . Yuko katika
darasa la nne katika shule ya Msingi Tumaini. Anaishi katika mtaa wa Mali pamoja na wazazi
wake.
Fatuma ana umri wa miaka kumi. Ana bidii sana katika masomo yake na somo
analolipenda sana kuliko yote ni Kiswahili. Husema ya kwamba Kiswahili ni lugha ya taifa na
kimataifa na hivyo anataka Waafrika wajivunie lugha yao ya Kiswahili. Hapendi jinsi waafrika
weusi wanavyofurahia lugha ya Kiingereza na kubeza Kiswahili. Yeye anataka kuwa mtangazaji
na pia mwandishi wa vitabu vya Kiswahili.
Rafiki yangu ni mzuri sana kwa sababu ni mpole, mnyenyekevu na mcheshi. Anapenda
sana kufurahi kila wakati. Mimi nampenda kwa sababu hunihimiza kutia bidii katika masomo.
Pia hunisaidia masomo mengineyo kama vile Hesabu na Sayansi. Tukiwa na shida husaidiana na
ndio sababu tunapendana sana.
Maswali
1. Rafiki ya mwandishi anaitwa _____________
SEHEMU YA TATU
1. Kanusha
(a) Mama ameenda sokoni.
___________________________________
(b) Mkulima alinunua mbegu nyingi
________________________________________
(c) Tunaenda shuleni
____________________________________________
(d) Mwalimu atawaadhibu wanafunzi watukutu.
__________________________________________________
(e) Kesho nitasafiri mjini.
___________________________________________________
2. Tambua aina ya neno lililopigiwa mstari katika sentensi zifuatazo.
(a) Mkeka umeliwa na panya.
(b) Kufuli mbaya imetupwa.
(c) Gari liliendeshwa polepole.
(d) Msichana mrembo amepotea.
(e) Wao ni warefu sana.
3. Jaza nafasi kwa msamiati sahihi
(a) Tunatumia _____ kuchanja kuni.
(b) Anayefanya kazi ya ukulima ni ___________
(c) Mimea ambayo haihitajiki shambani huitwa _______
(d) Mmea mchanga huitwa ___________
(e) Huwa tunapanda ________ ambayo huota mimea tofauti.
4. Andika kinyume cha neno lilopigiwa mstari
(a) Mzee yule amepatikana akiwa amechapwa.
(b) Shangazi alinitembelea jioni.
5. Jaza mwanya kwa kiulizi -pi
(a) Mvulana ______ alichelewa shuleni?
(b) Kiatu _______ kilichoshonwa na fundi?
(c) Matunda ________ yaliyooza?
(d) Mti _______ ulioanguka?
(e) Mikoba _______ iliyonunuliwa?
6. Andika kwa idadi
(a) Watoto 8 _____________________________
(b) Vijiko 13 _____________________________
SEHEMU YA NNE
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________
___________________________________________________________________________