Professional Documents
Culture Documents
Justine Kasusura
Justine Kasusura
Mnamo tarehe 02 August 2001, Dada aitwaye DOREEN alimpigia simu ndugu
JUSTINE KASUSURA ambaye alikuwa ni Dereva wa gari ya kampuni ya ulinzi
ya KNIGHT SUPPORT akimwelekeza afike ofisini kwani kuna maagizo
anatakiwa apewe.
Polisi mbeya walimfatilia na kubaini jamaa yupo anakata kilaji hoteli ya MOON
DUST na kafikia nyumba ya wageni ya THREE IN ONE Chumba namba
101K,wakaona ni vizuri kuingia chumbani kwake na kumsubiri akirudi kulala
wamkamate. Aliwekewa ulinzi wa siri kote alikokuwa.
KASUSURA akiwa hajui lolote alitoka bar na kwenda kulala ambapo alikamatwa
kiulaini sana "KUMYATIA KIZIWI" ilikuwa sio rahisi kuamini mtu
aliyetangazwa kuwa ni jambazi sugu angedakwa kiulaini bila purukushani
yoyote. Walipomsachi walimkuta na TSHS 256,000 tu.
Siku mbili tu baada ya kesi hii kusomwa, Tarehe 9 jan 2002 aliibuka IGP
OMARI MAHITA na kudai wanawashikilia askari wake nane wakiwemo watatu
waandamizi kwa kusaidia kumtorosha mtuhumiwa kila alipokamatwa(mara
tatu Dar na mara nyingine mikoa ya Arusha na Tanga)
Baada ya kauli hiyo Mkurugenzi tarehe 15 jan 2002 wa makosa ya jinai ADAD
RAJAB alitoa taarifa ya kuwaachisha kazi askari watano wa chini na
kuwafungulia mashtaka wote nane mahakamani.
Pia alikana kumiliki bastora siku ya tukio kama ushahidi ulivyowasilishwa. Hata
hivyo Mh. Hakimu SILVANGILWA MWANGESI alimkuta na hatia na tarehe 30
March 2007 alimhukumu jela miaka 30 kwa unyang'anyi na miaka 5 kwa wizi
CONSECATIVELY (hivyo jumla miaka 35)pamoja na viboko 12.
Katika hukumu Jaji alisema Wangeweza kuitupilia mbali rufaa hiyo tangu
mwanzoni kwani ilikuwa nje ya muda,hata hivyo waliisikiliza ili kurekebisha
adhabu kwani wanahisi hakimu alipotoka alipohukumu CONSECATIVELY
badala ya CONCURRENTLY yaani sio kifungo kwa KUFUATANA bali PAMOJA.
Kati ya hoja TISA za KASUSURA ni hoja TATU ziliwashawishi majaji hawa nazo
ni;
1. Kiapo chake cha kukiri kosa na Onyo kilichotolewa mahamani
kilipandikana nje ya muda wa kisheria ya mwenendo wa makosa ya jinai.
Alikamatwa Dec 24 akachukuliwa maelezo 26 Dec 2001
2. Muda waliodai ametenda kosa hilo,Mabadiliko ya Sheria ya KANUNI ZA
ADHABU inayoelekeza kifungo cha MIAKA 30 kwa anayekutwa na hatia
ARMED ROBBERY yaikuwa hayajaanza kutumika. Je, NI KWA NINI
HAKIMU ALIMUHUKUMU KWA SHERIA AMBAYO HAIKUWEPO?
3. KASUSURA alidai hadi wakati anahukumiwa,Upande wa Mashtaka
haukuwahi kumleta shahidi yoyote ambaye ni mmiliki wa mzigo unaodai
kuibiwa(CITIBANK) Pia kiasi kinachodaiwa kuibiwa hakikufanana kati ya
HATI YA MASHTAKA na kiasi walichotaja MASHAIDI. CITIBANK tu
ndio wangetoa utata.
Baada ya hoja hizi majaji waliwabana vilivyo mawakili wa serikali
TUMAINI KWEKA na CECILIA MKONONGO ambao walikosa kabisa
hoja kinzani. Majaji wakapanga siku ya hukumu iwe tarehe 09 May 2016