Professional Documents
Culture Documents
Kuheshimu Hitilafu1
Kuheshimu Hitilafu1
WANACHUONI
NA
JITIHADA ZAO
30/04/2023 Ce - 10/Shawwal/1445 Ah
YALIYOMO
1. Shukrani
2. Neno la wafasiri
3. Dibaji
4. Kujipamba na adabu za kuhitilafiana na kuvumiliana katika
jitihada za wanachuoni
5. Mazingatio katika maneno ya wanachuoni wakubwa.
6. Haifai 'kumkhalifu' imamu kwenye swala katika masuala ya
jitihada baina ya wanachuoni
7. Haifai kulazimishana misimamo katika mambo ya jitihada
8. Mambo wanayohitilafiana wanachuoni
Kusoma bismillah katika swala
Kusoma kunuti katika swala ya alfajiri
Kumfuata imamu katika kunuti
Kutikisa kidole katika Tahiyyatu
Kunyanyua mikono wakati wa kusoma dua.
Kusoma dua baada ya swala za faradhi
Hukumu ya kupangusa uso kwa mikono baada ya dua
9. Hitimisho
10. Rejea
1
SHUKRANI
Bismillah Rahmaan Rahiim
Wabillah taufiiq
2
NENO LA WAFASIRI
Bismillah Rahman Rahiim
Sifa zote njema anastahiki Allah mtukufu mwingi wa rehema na
tunamtakia Rehma na Amani Mtume wetu Muhammadi
Hivyo tumejitahidi kadiri ya uwezo wetu katika kufanikisha kazi yetu hii,
huku tukiamini kuwa kitabu pekee kisichokuwa na makosa ni kitabu
cha Allah mtukufu.
*Wafasiri*
Abdillah Masawe.
Bashiri Shabani Dule
*Wahakiki*
Shaaban Ibrahim
Wenge Mohamadi Wenge
Maulid Hussen Maulid
3
DIBAJI
KATIKA majukwaa mbalimbali ambayo Shekhe Abdulqadir Muhammad
Al-Ahdal ameendesha mihadhara na kutoa fat-wa; misikitini au kwenye
vyombo vya habari, amekuwa akiulizwa maswali mbalimbali
yanayotokana na Waislamu kuhitilafiana katika mambo kadha wa
kadha.
4
KUJIPAMBA NA ADABU ZA KUHITILAFIANA NA KUVUMILIANA
KATIKA JITIHADA ZA WANACHUONI
Kundi la kwanza:
Kuna wale ambao hawakubali hitilafu yoyote ile hata ambayo
inakubalika kisheria, isipokuwa kauli na msimamo wao tu ndiyo
wanaoukubali. Msimamo huo huwa chanzo cha mijadala yenye kuleta
migogoro katika jamii ya kiisilamu.
Kundi la pili:
Hili lipo kinyume na kundi la kwanza kutokana na kukubali kila aina za
hitilafu hata kama inakwenda kinyume na misingi ya kisheria ambayo ni
Qur-an na Sunnah pamoja na makubaliano ya wanachuoni.
5
Makundi yote haya mawili yakipimwa katika misingi ya dini utagundua
kuwa kuna sehemu wanapatia na kuna sehemu wanakosea.
Kwa nini tunasema hivyo?
ً ً
منصوصا ّبينا لم
ُ أو عىل لسان نبيه ملسو هيلع هللا ىلص، "كل ما أقام هللا تعاىل به الحجة ف كتابه: قال الشافع رحمه هللا
ي ي
1
".....يحل اإلختالف فيه لمن علمه
6
hawana namna ila kufuata tu, na hawaruhusiwi kwenda kinyume
nacho."2
Imamu anaendelea kusema kwamba ikitokea wamepinga, basi upingaji
huo ndio ambao Allah anaulaumu kwao.
Na ikitokea mtu anauliza kwamba ipo wapi hiyo lawama ya Allah, basi
atajibiwa kwamba Allah amesema:
٤ :ﭧﭐﭨﭐﱡﭐ ﲠ ﲡ ﲢ ﲣ ﲤ ﲥ ﲦ ﲧ ﲨ ﲩ ﲪ ﲫ ﱠ ابلينة
2
Tazama "arisala" (1/560), Aalamul-muwaqiyna (2/263)
3
Rejea iliyopita.
4
Taarekh Baghdadi (13/352)
5
Taarekh Baghdadi (13/352)
7
Amesema mwanachuoni Yunus Aswadafiy, akimzungumzia Imamu
Shafii ambaye alifariki dunia mwaka 204 hijiria (Allah awarehemu):
"Sijapatapo kumuona mtu mwenye akili kuliko lmamu Shafii. Nilijadiliana
naye siku moja katika mambo ya dini na hatukuafikiana kisha
tukaachana halafu tukakutana siku nyingine, basi lmamu Shafii
aliponiona akanishika mkono kisha akasema:
6
Siyaru a’laami nnubalaa (10/16-17)
8
Amesema mwanachuoni Ibun Qudamah (Allah amrehemu): "Haimpasi
yeyote kumkemea mtu yeyote ambaye anafanyia kazi kauli ya
madhehebu yake.
11
Rejea kitabu Majumua Fatawa, Juzuu 23, uk 115 - 116.
9
Na akasema tena: "Mtu yeyote ambaye amefikia daraja ya jitihada
inayoruhusiwa kisheria basi haifai kumlaumu na kumwona kuwa
amepata dhambi, kwani hakika ya Allah amemsamehe alipokosea
kwenye hiyo jitihada yake, bali inapasa kuwa naye pamoja na kumpenda
kwa kuwa ana imani na uchamungu, na ni mwenye kusimamia yale
ambayo Allah amewajibisha katika haki za huyo mwenye kujitahidi.
Miongoni mwa hizo haki ni kumpongeza na kumwombea dua pamoja na
haki nyingine…. "12
Na amesema tena: "Ikiwa kauli inakwenda kinyume na Sunnah
(mwenendo na mafundisho ya Mtume yaliyo wazi) na makubaliano ya
wema waliotangulia, basi ni lazima akemewe huyo mtu, ikiwa si hivyo
atakemewa kwa kubainishiwa udhaifu wa hoja zake.
14
Rejea kitabu Majumua Fatawa juzuu 20 uk 207.
15
Rejea kitabu Likaati Babu Maftuuh, juzuu ya 3, uk 79.
10
17
Rejea kitabu Majumua Fatawa, Juzuu ya 35, uk 212.
11
(ii) Hoja za wanaosoma bismillah kwa siri.
SWALI
Kuna maimamu ambao wanaposwalisha hudhihirisha Bismillah
na wengine hawadhihirishi, Ni upi usahihi wa hilo?
MAJIBU:
Wanachuoni wamehitilafiana juu ya kusoma bismillah kwa sauti au kwa
siri katika swala. Na jambo hili halitakiwi kuleta mfarakano katika
umma, kwani kila mmoja ana mashiko (ushahidi) wake.
18
Rejea Sahihi Bukhari, hadithi namba 89.
)399( ) و مسلم343( رواه البخاري عنه19
12
Ushahidi wa wanaodhihirisha bismillah katika swala:
Mosi: Katika Sahihi Bukhari, kwenye kitabu kinachozungumzia fadhila
za Qur-an, pia amesimulia Anas (Radhi za Allah ziwe juu yake) kwamba
aliulizwa juu ya kisomo cha Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
akasema: "Kisomo chake alikuwa anavuta, kisha akasoma Bismillah
Rahmaan Rahiim, yaani alikuwa akivuta neno bismillah na neno
rahmaan na neno Rahiim."20
Pili: Kutoka kwa Abuu Nuaimu (Radhi za Allah ziwe juu yake) amesema:
“Nimeswali nyuma ya Abuu Hurayrah ambapo alianza kusoma Bismillah
Rahmaan Rahiim kisha akasoma Suuratul Faatiha mpaka akafika
“Waladhwaalliin” na akasema “aamiin”, na pindi alipotoa salamu
akasema; Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu ipo mikononi mwake,
hakika yangu mimi nimeswali swala kama alivyoswali Mtume
(Swallallahu Alayhi Wasallam)."21
Tatu: Anas amesema: "Muawiyah (Radhi za Allah ziwe juu yake) alipofika
mji wa Madina aliwaswalisha watu na akaacha kusoma bismillah kwa
sauti, wakampinga wale waliohudhuria swala hiyo katika Muhajirina, na
aliposwali mara nyingine akasoma bismillah kwa sauti."22
Nne: Amesema lbn Kathir katika tafsir yake: "Kwa sababu wanazuoni
wamekubaliana juu ya swala ya mwenye kudhihirisha bismillah na
mwenye kuisoma kwa siri, tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hili."23
20
21
Hadithi hii ameipokea Annasai kwa namba (905), Ibun Khuzaymah namba (499), Alhaakim katika kitabu Mustadrak,
juzuu ya (1/uk 232), Sunanulbayhaqiy, juzuu ya (2/ uk 46), Imamu Shafii katika Al-Ummu, juzuu ya (1/uk 232), Naswbu
Raya, juzuu ya (1/uk 353), Tafsir Ibun Kathiri, juzuu ya (1/ uk 66) na Daarulqutniy kama hadithi namba 14. Daarulqutniy
amesema hadithi hii ni sahihi na wapokezi wake wote ni wakweli.
22
Rejea tafsir lbun Kathir, Juzuu ya 1, uk 66, Chapa ya Daarulhadithi, Cairo.
23
13
Tano: Amesema lbn Qayyim: "Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
alikuwa anadhihirisha bismillah mara chache, na mara nyingi alikuwa
akiisoma kwa siri kuliko alivyokuwa akiidhihirisha."24
Sita: Imamu wetu Shafi (Allah amrehemu) anaona kudhihirisha
bismillah katika swala ni lazima, ingawa alikuwa anaswali nyuma ya
mtu ambaye hadhihirishi bismillah.
24
Rejea Zaadulmaad, Juzuu ya 1, uk 206. Chapa ya
26
Rejea Majumua Alfatawa, Juzuu 23, uk 379.
14
2. KUSOMA KUNUTI KATIKA SWALA YA ALFAJIRI
SWALI:
Ni upi usahii, kukunuti kwenye kila swala ya Alfajiri au
kutokunuti kama wanavyofanya maimamu wengine?
MAJIBU:
Maana ya kunuti:
Neno kunuti lina maana nyingi takriban kumi kama alivyosema Ibun
Hajar katika kitabu chake cha Fat'hu l-baari, juzuu wa 2: uk 491.
Kauli ya kwanza:
Hairuhusiwi kukunuti katika kila swala ya alfajiri isipokuwa kwenye
majanga, tena katika swala zote tano.
27
Amepokea lmamu Tirmidhiyyu hadithi namba 402.
15
Pili: Amepokea Ibn Abii Shayba na wengineo kutoka kwa Abii Makhlad,
akisema: "Nimeswali pamoja na Ibn Omar (allah amridhie) hakukunuti
katika swala ya alfajiri na akasema sijamuona yeyote katika maswahaba
zetu akifanya jambo hilo"28
Nne: Kutoka kwa Ummu Salama (Radhi za Allah ziwe juu yake)
amenukuu kutoka kwa Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam): "Hakika
yake amekataza kukunuti katika swala ya Alfajiri." 30
Tano: Kutoka kwa Ibun Abasi (Radhi za Allah ziwe juu yake) amesema:
"Kukunuti asubuhi ni bida'a (uzushi katika dini)."31
Kauli ya pili:
Msimamo wa pili unasema dua ya kunuti ni jambo lililopo kisheria
katika swala ya alfajiri. Hii ni kauli ya imamu Maaliki na Imamu Shafii.
28
Al-majmui ya nnawawiy (3/466) المجموع للنووى
29
766 ومسلم4904 البخاري
30
Al-majmui ya nnawawiy (3/466) المجموع للنووى
31
Rejea iliyopita ( )المصدر السابق
16
“Zilindeni swala, na hasa swala ya kati na kati na simameni kwa ajili
ya Allah nanyi ni wenye kukunuti (kunyenyekea).”32
Pili: Ni hadithi ya Anasi ibun Maaliki (Radhi za Allah ziwe juu yake)
ambaye amesema: "Hakuacha Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
kukunuti katika swala ya alfajiri mpaka alipoondoka duniani." 33
Kauli ya tatu:
32
Suratul-Baqarah (2/238)
33
Hadithi hii ameipokea Imamu al-Bayhaqiyyu kwa namba 3105, Daar-kutuniyyu kwa namba 1694, Imamu Ahmad kwa
namba 12657, Ibun Abii Shayba kwa namba 312, Abdulrazzaki kwa namba 4964, Bazaar kwa namba 556 na Atwahawi
1:143 na Al-Hakim 2:201. Na ameisahihisha Imamu Maaliki na Imamu Shafii, Daar-kutuniyyu, Al-Haakim, Bayhaqiyyu na
Nawawiyyu na Al-balkhiyyu…. Tazama kitabu Al-majmuua ya Imamu Annawawiyyu 3:465-467.
34
Rejea Al-Majmuu ya lmamu Annawawiyyu 3:465-467.
35
Rejea Al-majmuua 3:465-467
36
Rejea al-Majmuua ya Imamu Annawawiyyu 3 :465-467.
17
Kunuti ni jambo ambalo limefutwa na halipo kisheria katika hali zote,
iwe katika majanga au laa. Na hii ni kauli ya baadhi ya watu wa
madhehebu ya Hanafi na baadhi ya watu wa lraq.
SWALI:
Kama mimi nimekinaishwa na msimamo wa kwamba Mtume (Swallallahu
alayhi wasallam) hakukunuti, ninaweza kumfuata imamu anayekunuti
katika swala?
MAJIBU:
37
Faslul-khitwab (7/456), فصل الخطاب في الزهذ والرقائق واآلداب.
18
katika utekelezwaji wake. Hivyo maamuma anatakiwa kumfuata imamu
kwa utaratibu atakaoufanya hata kama yeye haoni hivyo. 38
38
Al-ikhtiyaaraatul-Fiq-hiya (uk:68).
39 Maj-muu fataawa wamaqaalaatu mutanawia, juzuu (14/177).
40
Majmoo' Fataawa wa Rasa'il al-'Uthaymeen (14/144).
19
Jibu ni ili pasitokee tofauti baina yake na imamu ndani ya swala. Kwa
kuthibitisha hilo huu hapa ushahidi mwingine wa Hadithi: “Hakika
amefanywa imamu kuwa ni wa kufuatwa katika swala, basi msipingane
naye.”
SWALI:
Kama imamu haoni kufaa kwa kusoma kunuti katika swala ya alfajiri,
lakini anaswalisha watu wanaoona kufaa kwa kunuti. Ni lipi jambo
sahihi analotakiwa kufanya?
JIBU:
Endapo imamu akiwaswalisha watu wanaoona kusoma kunuti ya alfajiri
inafaa, basi asome kunuti ili kuepuka kuwagawanya.
41
Kaseti No. (262) yenye kichwa cha habari. “Fataawa kwa njia ya simu”
20
kutokana na jitihada za wanachuoni. Hivyo imamu akikunuti naye
maamuma aitikie "Aamiyn" na ikiwa imamu hakukunuti maamuma
naye hatokunuti.
42
Mjmuu fatawa (23/115-116).
43
Majmuu fatawa (14/159)
44
Ahkamul-qurani (4/194)
21
Amesema shekh wetu Abdulqadir (Allah amhifadhi) : Kwa masikitiko
makubwa, mwenye kuutazama umma wa kiislamu leo hii, atakuta kuna
misingi mingi imekengeukwa isipokuwa wale ambao wamerehemewa na
Mola. Utakuta sababu za nusra zimeachwa, na kuchukua sababu za
migawanyiko na mifarakano.
45
Majmuu fatawa (20/24)
22
5. KUTIKISA KIDOLE KATIKA TAHIYATU
SWALI:
Kuna hili la kutikisa kidole kwenye swala na wengine hawatikisi. Ni
yapi mafundisho sahihi kuhusu hili?
ّ … ( حديث وائل بن ُحجر رض هللا عنه عندما يصف صالة النب ملسو هيلع هللا ىلص قال
فرأيته، ثم قبض ثنتي من إصبعه ي ي
46
" يحركها يدعوا بها
47 ّ
"يشي بإصبعه إذا دعا وال يحركه
النب ملسو هيلع هللا ىلص كان ر
"أنه ذكر أن ي: رض هللا عنه
الزبي ي
حديث عبدهللا بن ر
46
363 وصححه االلبانً فً اإلرواء الغلٌل، ٨٨9 ًأخرجه النسائ
47
ذكرالبٌهقً بإسنا ٍد صحٌح عن ابن زبٌر ورواه ابو داؤود بسن ٍد صحٌح:545/3 قال الحافظ النووي رحمه هللا فً المجموع
48
Rejea kitabu Raudwatu Atwaalibiin juzuu ya 1 uk 443-1444
23
6. KUNYANYUA MIKONO WAKATI WA KUSOMA DUA KATIKA
KHUTBA
SWALI:
MAJIBU:
Wanachuoni wamehitilafiana juu ya jambo hili katika kauli mbili tofauti.
Kauli ya kwanza:
Inasema haifai kwa khatibu kunyanyua mikono wakati wa kusoma dua.
49
Angalia hii katika Sahihi Muslim, hadithi namba 874.
24
Na vilevile Mtume (salallah alyhu wasallam) alikuwa hanyanyui mikono
akiomba dua kati ya sijida mbili na kwenye tahiyyatu (tashahudi) ya
mwisho kabla ya salamu.
Na hivihivi pia baada ya kutoa salamu katika swala tano alikuwa akivuta
nyiradi zilizothibiti kisheria na alikuwa hanyanyui mikono.
Nne: Amepokea Imamu Bukhari kutoka kwa Anasi (radhi za Allah ziwe
juu yake)” akisema: “Siku moja Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
aliingia nyumbani kwa Ummu Suleym, akamletea Mtume (Swallallahu
Alayhi Wasallam) tende na samli, kisha Mtume (Swallallahu Alayhi
Wasallam) akasema: "Rejesheni samli katika chombo chake na tende
katika mfuko wake, kwani mimi nimefunga” kisha akasimama akaelekea
kwenye upande wa nyumba, akaswali swala isiyo kuwa ya faradhi, kisha
akamwombea dua Ummu Suleym na watu wa nyumbani kwake.
50
Rejea kitabu Majumua Fatawa ya shekh Ibun Baazi Juzuu ya 6 UK 158.
25
Kauli ya pili:
Hii inasema inafaa kwa khatibu kunyanyua mikono yake anapoomba
dua.
26
Hili jambo la kunyanyua mikono ni katika sababu za kujibiwa dua
isipokuwa katika maeneo ambayo Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
hakunyanyua mikono basi nasi hatunyanyui katika maeneo hayo.
Na hivi hivi baada ya kutoa salamu katika swala tano alikuwa akivuta
nyiradi zilizothibiti kisheria na alikuwa hanyanyui mikono, basi
hatutanyanyua mikono yetu katika maeneo hayo kwa kumuiga Mtume
(Swallallahu Alayhi Wasallam). Ama kuhusu maeneo ambayo Mtume
(Swallallahu Alayhi Wasallam) amenyanyua mikono yake basi ni sunnah
kunyanyua mikono miwili katika maeneo hayo, kwa sababu jambo hili ni
katika sababu za kujibiwa dua.
51
Rejea kitabu Majumua Fatawa Juzuu ya 6 UK 158.
27
7. KUSOMA DUA BAADA YA SWALA ZA FARADHI:
SWALI:
Sheria ya dini inasemaje kuhusu kusoma/kuomba dua baada ya
swala ya faradhi?
MAJIBU:
Wanachuoni wamehitilafiana pia kuhusu kusoma dua baada ya swala ya
faradhi kwa mtu mmoja mmoja au kwa pamoja katika kauli mbili.
HOJA ZAO:
Mosi: Hoja ya kwanza wanasema: “Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam)
hakufanya wala maswahaba zake hawakufanya hilo na kama jambo hilo
lingekuwa ni kheri basi wangetutangulia kulifanya.
(52)
Hadithi hii ni sahihi kaipokea Imamu Tirmidhiy kwa Namba 289.
28
Tatu: Watu wa kundi hili wanasema kila baada ya swala kumalizika
huwa hakuna dua bali ni dhikri maalumu (nyiradi).
Amesema Allah Mtukufu wakati anasimulia kisa cha nabii yusuf (alayhi
salaam) :
٨٥ :ﱼ ﱠ يوسف
ﱽ ﭧﭐﭨﭐﱡﭐ ﱳ ﱴ ﱵ ﱶ ﱷ ﱸ ﱹ ﱺ ﱻ
"Na wote wawili wakakimbilia mlangoni na mwanamke akairarua
kanzu yake Yusuf kwa nyuma.”54
Hii ina maanisha nabii Yusuf ( Amani zimfikie ) alikuwa ameivaa kanzu
yake na ndiyo maana ikaweza kuraruliwa (kuchanwa) kwa nyuma.
(53)
Ameipokea lmamu Tirmidhiy kwa namba 3499 na lmamu Annasai kwa namba 9936. Na ameisahihisha Sheikh al-Albaan
katika Sahihi Tirmidhiy kwa namba 3499.
(54)
Suuratu Yusuf (12:25)
29
1. Sheikh lbun Baaz.
2. Sheikh lbun Uthaymin.
3. Sheikh Al-Albaaniy (Allah awarehemu).
4. Vile vile ndiyo kauli ya Sheikh Fauzan (Allah amhifadhi).
Kauli ya pili:
Wanachuoni wa kauli hii ya pili wao wanaona dua husomwa ndani ya
swala na hata baada ya kutoa salamu, yaani baada ya kumalizika kwa
swala.
HOJA ZAO:
Mosi: Ni hadithi ya Mtume (Swallallahu Alayhi Wasallam) isemayo:
Mnamsabihi (Sub-haana Allah) na mnamshukuru (Alhamdulillah) na
mnatukuza (Allahu Akbar) nyuma ya kila swala mara thelathini na
tatu.55
٧ :ﭧﭐﭨﭐﱡﭐﱓﱔﱕﱖﱠ الرشح
Imethibiti kutoka kwa lbun Abbasi pale alipotafsiri aya hii akasema:
"Ukipata faragha (muda) katika swala zako fanya juhudi maana yake ni
(55)
Hadithi ameipokea lmamu Muslim katika sahihi yake kwa namba 595
56
Hadithi hii ameipokea lmamu Annasai katika Sunanulkubraa kwa nambari 9848
30
kuzidisha dua na kumwomba Mola wako shida zako (iwe ndani ya swala
au nje).57
Tatu: Ama hoja yenu ya aya ya suratu annisai (103) kuwa hakuna dua
baada ya swala ila kuna dhikri (nyiradi) tu siyo sahihi, kwasababu aya
hii allah alikuwa anawazungumzia watu walioko vitani, Amesema sheikh
Assaadiy katika tafsiri ya aya hii: "Mtakapomaliza swala zenu (swala ya
khofu/vita) na swala nyingine basi mtajeni Allah katika kila hali zenu.
31
swala, na kumalizika kwa dhikri/nyiradi za baada ya swala, kuomba
hali ya kuwa umenyanyua mikono yako juu, kwa sababu kunyanyua
mikono ndiyo asili na ni katika sababu za kukubaliwa kwa hiyo dua.
59
Hadithi hii ameipokea lmamu Tirmidhiy na ameisahihisha Sheikh al-Albaani katika Sahihi Tirmidhiy kwa Nambari 3556.
60
Hadithi hii ameipokea Abuu Dauud na ameisahihisha Sheikh al-Albaani katika sahihi ya Abi Dauud kwa nambari 1522.
32
hilo. Ama kuhusu kupangusa uso hakuna isipokuwa hadithi moja au
mbili (zisizo sahihi) ambazo huwezi kusimamishia hoja, na Allah
ndiyo Mjuzi zaidi."
1. Madhehebu ya Hanafi
Kupangusa uso baada ya dua kwao ni Sunnah kwa kauli iliyo sahihi.
Angalia kwenye kitabu cha Sherhe Al-haswkafiy, juzuu ya 1, ukurasa
507.
2. Madhehebu ya Maliki
3. Madhehebu ya Shafii:
33
4. Madhehebu ya Hambali
Kwa hivyo basi katika jambo hili kumekuwa na kauli tatu baina ya
Wanazuoni (Allah awarehemu).
1. Kauli ya kwanza wao wanaona kuwa jambo hili ni Sunnah kwa kuwa
hadithi hiyo wanaiona kuwa ni sahihi.
3. Kauli ya tatu wao wanaona wala siyo bida'a (uzushi) bali ni Mubah
(inapendeza). Ukifanya hatuwezi kusema kuwa umefanya bida'a (uzushi)
na ukiacha inapendeza zaidi, lakini mwenye kupangusa hatutamlaumu
kwa kuwa anategemea hadithi iliyotajwa na ameiona kuwa kwake ni
34
sahihi. Na jambo hili ni katika mambo ambayo wanazuoni
wamehitilafiana.
35
HITIMISHO
Amesema mwanachuoni, sheikh Ibn Uthaymin kwamba "Baada ya
kubainisha kuwa dua baada ya swala za faradhi ni bida'a (uzushi) na
wala haifai, akauliza muulizaji: “Itakapokuwa mwenye kufanya hivi ni
mtu mzima (imamu) je, nimchukie? Akajibu Sheikh lbun Uthaymin
kwamba msemeshe kwa hekima na wala usimchukie kwa kuwa si
haramu, bali kinyume chake (kuacha) ni bora zaidi.
36
REJEA
Qur-ani tukufu.
Hadithi za mtume Muhammad (Swallallahu alayhi
wasallam)
Tafsir Ibun Kathir (Ibun Kathir)
Tafsiri al-Qurtubiy (Imamu Qurtubiy)
Fat-hul baary (Ibun Hajar al-As-Qalaniy)
Al-ummu cha (lmamu Shafii).
Taarikhu Baghdadi (Al-Khatwib Baghadad).
Siyar A’alam Annubalaa (Imamu Dhahaby).
Majumua Fatawa (Ibun Taymiyah).
Al-Adabu Sharia (Ibun Taymiyah).
Liqaati Babu Maftuuh (Ibun Uthaymin).
Zaadulmaad (Ibun Qayim).
Al-majmuua (Imamu Annawawiyyu) .
Raudwatu Atwaalibiin (imamu Nnawawiy)
37