Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa.
Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,
Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea. Zaburi 23
BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
Naam, nijapopita kati ya bonde la kivuli cha mauti,
Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele. IMANI YA MITUME
Namwamini Mungu Baba Mwenyezi, Muumba mbingu na nchi na Yesu Kristo
mwana wake pekee, Bwana yetu aliyechukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu akazaliwa na bikira Mariamu, akateswa zamani za Pontia pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashuka mahali pa wafu, siku ya tatu akafufuka, akapaa mbinguni, ameketi mkono wa kiume wa Mungu Baba Mwenyezi. kutoka huko atakuja kuwahukumu walio hai na watu wafu,
Namwamini Roho Mtakatifu. kanisa takatifu ushiriki wa watakatifu, ondoleo la