Jifunze Forex Kwa Lugha Ya Kiswahili Toleo La Pili

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 81

G Online Trading and Financial Markets (gotafima)

MAFUNZO YA FOREX KWA LUGHA YA KISWAHILI – TOLEO LA PILI

IMEANDALIWA NA: GOTAFIMA


WhatsApp: +255 755 264 229
Telegram Chanell: @gotafima
Telegram Group: @gotafima1
Instagram: @gotafima1
Twitter: @gotafima
Facebooke: https://web.facebook.com/gotafima1
Website: www.gotafima.com
Jinsi ya kufungua account ya forex fungua lingi hii www.deriv.com

UTANGULIZI
FOREX NINI?
Forex inasimama badala ya neno FOREIGN EXCHANGE, Ambapo unakuwa unabadili
sarafu moja toka sarafu nyingine. Mfano kama ukitoka Tanzania unatumia TSH
ukaenda Kenya ambapo wanatumia KSH itakubidi ubadilishe sarafu yako ya
kitanzania kwenda katika saafu ya kikenya. Kwa zoezi hilo unakuwa umeshafanya
FOREX.
Hapo kinachofanyika ni hiki, TSH/KSH kwamba unauza sarafu ya kitanzania kwa
kununua sarafu ya kikenya. Hili tutaliona katika platform hii. utakutana na vitu kama
USD/CHF GBP/JPY EUR/USD
kwa wakati mmoja ambapo fedha hizo zinakuwa katika pair moja.
Fedha hizo zinakuwa katika pair ambayo tunaita CURRENCY PAIR ambayo inakuwa
na fedha mbili za nchi tofauti,mfano wa currency pair unaweza kuwa USD/TSH hii ni
pair ya United State Dollar (Fedha ya Marekani) na Tanzania shilling (Fedha ya
Tanzania).
Kubadilisha hela huku mtandaoni ni biashara ambayo inazungusha hela nyingi kupita
aina yoyote ya biashara ulimwenguni kwa siku. Kwa siku biashara hii mzunguko wake
wa hela ni zaidi ya $5 TRILLION. Wakati stock exchange ya New

<<<BONYEZA HAPA KUFUNGUA ACCOUNT YA FOREX (DERIV.COM)>>>


York kwa siku ni $22.4billion, Tokyo ni $18.4 billion na London ni $7.2 billion kwa
siku. Na hizo ni stock exchange kubwa duniani, hivo FOREX ONLINE ni kubwa kuliko
hizi stock exchange.

NANI WAHUSIKA KATIKA FOREX? (KEY PLAYER IN THE FOREX MARKET)


Soko la Forex awali lilikusudiwa kwa ajilli ya Ma benki makubwa na taasisi kubwa za
kibiashara,ila kutokana na mabadiliko makubwa ya technologia haswa kwenye
'internet',wafanyabiashara wadogo pia (retail traders) nasi tumepata uwezo wa
kuingia sokoni kupitia kwa dalali ama broker.
Wahusika wakubwa kwenye soko ( Key player)
1. Benki kubwa duniani (super bank) , ambazo hizi hufanya biashara hii kwa kiasi
kikubwa sana na huchangia sana uelekeo wa soko hili, bank hizo ni kama Citi
Bank, JPMorgan, UBS, Deutsche Bank and HSBC

2. Kampuni kubwa za kibiashara duniani (Large commercial companies), kampuni


hizi hufanya biashara hii kwa ajili ya biashara Zao, mfano kampuni kama
Toyota katika kuagiza vifaa nchi nyingine hulazimika kubadilisha fedha yao
kwenda kwenye fedha ya nchi ambako vifaa hivyo vinaagizwa.

3. Serikali na Bank za nchi (government and central bank)

4. Speculators

Je, hii biashara ina muhimu wowote kwako? Jibu linategemea wewe
unahitaji nini
1. Kama unataka soko ambalo halilali.
2. Kama unataka fursa ya kufanya biashara mda wowote katika siku.
3. Kama unataka kutengeneza kiasi kikubwa cha pesa. Basi nadhani FOREX ni mahala
sahihi kwa hayo yote
NB: Kama utaweza tengeneza kiasi kikubwa cha pesa ndani ya mda mfupi, pia
unaweza kupoteza kiwango cha fedha ndani ya mda mfupi huohuo
4. FOREX ni biashara kama biashara zingine kama vile biashara ya nguo,biashara ya
duka,biashara ya madini, biashara ya mazao na zinginezo unazozifahamu na kila
biashara inamtindo wake wa kuifanya na hapo ndipo biashara zinatofautiana na hili
biashara uweze kuifanya na kukuletea faida lazima uhifahamu biashara hiyo na ni
jinsi gani unaweza kuifanya.
Watu gani wanaokuwepo/wanaoshiriki katika hii biashara?
1. Benki kuu (Central banks)
2. Serikali (Government)
3. Umoja wa wawekezaji(investment coorperation)
4. Wafanyabiashara wa duniani kote(businessies worldwide)
5 Wafanyabiashara wadogo(Retail trader)
Maeneo vitovu katika hii biashara duniani ni:
1. NEW YORK (United States Dollar USD)
2. LONDON (Euro EUR and Pound GBP)
3. FRANKFURT (France franc CHF)
4. TOKYO (Japanese YEN JPY)
5. SYDNEY(Austarlian dollar AUD)
VIPINDI VYA FOREX MARKET (SESSIONS)
1.SYDNEY SESSION
Hii ni session ambayo inaanza saa 6:00 usiku mara baada ya soko kufunguliwa na
inaisha saa2 asubuhi,hapa unaweza ukafanya biashara sarafu zote lakini unashauriwa
kufanya biashara zaidi sarafu zenye NZD na AUD kwasababu zinakuwa na mzunguko
mkubwa kwa wakati huo sokoni.
2.TOKYO/ASIAN SESSION
Hiki kipidi kinaanza saa 8 usiku masaa 2 mara baada ya Sydney session kuanza na
inaenda mpaka saa 4 asubuhi, hapa unaweza kufanya biashara sarafu zote lakini
unashauriwa zaidi kufanya biashara sarafu zenye JPY kwasababu zinakuwa na
mzunguko mkubwa kwa wakati huo sokoni.
3.LONDON SESSION
Hiki kipindi kinaanza saa 4 asubuhi saa 1 kabla ya kipindi cha Tokyo na kufungwa
na kwenda mpaka saa 12 jioni, hapa unaweza kufanya biashara sarafu zote lakini
unashauriwa kufanya biashara sarafu za EUR,GBP,USD na JPY kwa sababu zinakuwa
na mzunguko mkubwa kwa wakati huo sokoni.
4.NEW YORK SESSION.
Hii inaanza saa 9 mchana na kufanya muunganiko na kipindi cha London(London
session) kwa mda wa masaa 4,yenyewe inaenda mpaka saa 5 usiku ambapo kipind
cha sydney kinaanza tena hapa unaweza ukafanyia biashara sarafu zote lakini
unashauriwa kuafanya biashara zaid sarafu za USD,CAD,EUR na GBP kwasababu
zinakuwa na mzunguko mkubwa kwa wakati huo sokoni.

NB:-Masaa yote hapo ni kutegemeana na masaa ya AFRIKA MASHARIKI.(EAT


+3GMT)

Soko la FOREX hufunguliwa jumapili saa 6 usiku na kufungwa Ijumaa saa 5:59 usiku
hivo ndani ya huu mda una uwezo wa kufanya biashara
FAIDA ZA FOREX
1. Una uwezo wa kufanaya biashara sehemu yeyote ulipo na kwa mda wowote ndani
ya siku tano za week ndani ya saa 24 (24/5)
2. Unaweza kutoa faida hela zako mda wowote ndani ya week au hata weekend
kulingana tu na broker unayemtumia
3. biashara hii ya forex imewekewa Sheria rahisi sana ukilinganisha na biashara
zingine.
5. Uwiano mzuri kwa kiasi kidogo unaweza ingiza faida kubwa. (Leverage)
HASARA ZA FOREX
1. Upatikanaji wa HASARA kubwa na kwa muda mfupi.unapotegemea kupata faida
basi pia utegemee kupata hasara kubwa pia
2. Hii sio biashara ambayo kila mtu anaweza kuifanya.
SWALI:Je unafikiri forex ni biashara kama zilivyo biashara nyingine na kama hapana
kwanini na kama ndio kwann?
AINA ZA WAFANYABIASHARA KATIKA FOREX
Hii ni eneo muhimu sana kulijua na wewe kufanya maamuzi unataka uwe
mfanyabiashara wa aina gani. Hivyo kabla hujaanza ni bora kujitathmini wewe ni
mfanyabiashara wa aina gani na utumie njia zipi katika kufanya biashara yako.
Ni muhimu kujua wewe ni mfanyabiashara wa aina gani katika forex ,hiyo itakusaidia
kuweza kupanga muongozo wa kibishara(trading plan) yako ili uweze kufanya
biashara hii kwa kwa mafanikio makubwa.
Forex inajumuisha wafanyabiashara wa aina zifuatazo:-
1. DAY TRADER
Huyu ni mfanyabiashara ambae huingia katika biashara katika siku husika na kutoka
katika trade siku hio hio. Uzuri wa kuwa day trader ni mda wa kutosha wa kufanya
zako analysis. mara nyingi huwa na mda maalum wa kuingia katika trades zake. Na
mda ukifika wanasubiri fursa ijitengeneze na kuingia katika biashara(traders) zao,
Mara nyingi hutumia chart za dk 30, liasaa 1 hadi saa 4 katika kufanya
uchambuzi(analysis).
2. SCALPER
Huyu ni mfanyabiashara anaekuwa katika soko kwa mda mfupi sana. Mara nyingi
anaingia na kutoka katika trade na dakika kadhaa tu. Kivutia kikubwa kwa trader wa
aina hii huona faida au hasara ndani ya mda mfupi tu. Msingi mkubwa wa scalper ni
kuwa na uwezo wa kufikiri haraka na kuweza kumantain pressure. Kulingana na mda
mfupi wa fursa scalper huamua aingie katika hio fursa au aache,huwa anadumu
sokoni kwa muda mfupi tu na hutumia chart ya dk 5,dk15 mpaka dk30 kufanya
uchambuzi (analysis).
3. SWING TRADER
Huyu ni trader ambaye anaingia na kukaa sokoni kwa muda mrefu kulingana na na
target yake ,anaweza akakaa kwa masaa 5,week mpaka mwezi.tunaweza kusema ni
mfanyabiashara wanaoweza kukaa sokoni mda mrefu kuliko aina nyingine ya trader
kulinga na mtiririko wa soko ukitokea wa kupanda au wakushuka wanakuwa
wanaenda nao.
FOREX TERMINOLOGIES
Kama nilivyotangulia kusema ya kwamba katika FOREX tunahusika na jozi za sarafu
mbalimabali(currency pair), Misamiati hii kama utaweza kuielewa vizuri basi nina
hakika kutakuwa hakuna shaka ya wewe kuwa katika soko.

1. BASE CURRENCY
Hiki ni kiini msingi katika kununua au kuuza katika forex. kama utabuy EUR/USD Hii
ni kumaanisha unanunua euro ya ulaya na wakati huohuo unauza dola ya kiamrekani
2. QUOTE CURRENCY
Hii ni ile sarafu ya pili katika pair ya sarafu husika unapofanya trade. Mfano
EUR/USD, USD ndio quote currency.

3. LONG/BULLISH/BUY
Hii ni termonology ambayo unasikia watu wakiiongelea. kama imepatikana fursa
(opportunity) ya long/bullish hapa maana yake NUNUA. Bull ni aina za mnyama
ambae anakula majani hivo candlestick zake nyingi zinakuwa zikiwakilishwa na rangi
ya kijani. Huyu mnyama akitaka kukudhuru huinamisha kichwa chini na
anakunyanyua kwa kukuchota kukupeleka juu. Hivyo katika Forex hapa inamaanisha
soko linatoka chini linapanda juu.
4. SHORT/BEARISH
Kama imepatikana fursa (opportunity) ya short/bearish hapa maana yake UZA. Bear
ni aina ya mnyama ambae anakula nyama, hivo candlestick yake huwakilishwa na
rangi nyekundu. Huyu mnyama anavyokudhuru huruka juu kisha hukushusha chini.
Hii katika forex inamaanisha soko linatoka juu kushuka chini.
5. PIP (PERCENTAGE IN POINT)
Hiki ni kiasi cha thamani kinachocheza kulingana na mzunguko wa sarafu husika
katika biashara. Au tunaweza kusema ni mzunguko mdogo wa bei ambao currency
pair unaoufanya kwa kupanda au kushuka.Mfano Thamani ya USDCAD imetembea
kutoka 1.34286 hadi 1.34984 itakuwa imetembea kwa 66pips,Hii tunaipata kwa
kuchukua 1.34286 – 1.34948 ambapo tutapata 0.00662 na katika FOREX thamani ya
pip tunaanza kuhesabu kuanzia desimali ya nne hivyo basi kwa hapo USDCAD
itakuwa imeshuka kwa 66pips,na hiyo 2 tunaita micropip.kwa hiyo ni sawa na useme
imemove pips 66.2,
Lakin kwa pair za Japanese Yen kama vile USDJPY,GBPJPY kwa hizi thamani ya pip
tunaanza kuhesabu kuanzia desmali ya tatu.
6. LOT SIZE
Hii ni thamani inayotumiwa kujua faida na hasara.
Standard Lot size: 1.00 = $10 kwa pip moja
Min Lot size: 0.10= $1 kwa pip moja
Micro Lot size: 0.01= 10 cent kwa pip moja

7. TAKE PROFIT (TP)(chukua faida)


Hili ni eneo ambalo utaamua kutoka nje ya soko baada ya faida. Eneo ambalo utaona
faida uliyopata inakutosha au ni eneo ambali price inaweza kugeuka na kukuingizia
hasara.
Unapoingia kwenye soko analysis zako zinakuonesha sarafu itapanda/kushuka mpaka
eneo Fulani baada ya hapo itageuka trends Ila haujui itachukua mda gani mpaka
kufika katika hio bei(price) unaweza ukafunga mannualy au automatically lakini mda
mwingine huwezi kukaa kwenye screen yako mda wote kuisubiri hio point.
Unachokifanya unaset bei ikifika katika hilo eneo trade yake ijifunge automatically na
kisha wewe ukirudi au ukimaliza mambo yako kama itakuwa ilifika katika hio point
uje ukutane na profit yako. Hapo ndo panaitwa TAKE PROFIT.
8. STOP LOSS (SL)(kata hasara)
Hili ni eneo ambalo utaamua kutoka nje kwa hasara ama kwa kuona
uchambuzi(analysis) wako ulikuwa na makosa au unaamini upande wa hasara uliopo
utaongezeka zaidi hivyo badala ya kupata hasara kubwa unaamua kuchukua hasara
kidogo. Wanasema kama hutakubali hasara basi jiandae kupokea mama wa hasara
kwa lazima.
Kwenye market ukishafanya analysis unaona kuna fursa ya kupanda kwa sarafu hivo
unaamua kuinunua ikiwa chini ili ikifika juu uiuze na ile tofauti ya bei ulonunua na
utakayokuja kuuza ndo inakuwa faida Na wewe uliingia sokoni kwa hio sarafu labda,
Sasa baada ya kufanya hio uchambuzi inatokea (habari)news mfano ya kushuka kwa
ajira mfano marekani So kwa namna yoyote sarafu baada ya kupanda
itashuka.Maana itakuwa hafifu(week).Sasa unakuta na wewe ulishaingia kwa hiyo
unagundua itashuka sana hivyo unaamua kutoka katika soko katika hasara ndogo ili
usipate hasara zaidi kwani haujui hio sarafu itashuka mpaka wapi. Hio ndo inaitwa
STOP LOSS,unaweza kutoka mannualy au kwa set ijitoe automatically kama utakuwa
busy au mbali na kifaa chako.
AINA ZA ORDER KATIKA SOKO LA FOREX
Kuna aina mbalimbali za order katika soko la Forex ila za muhimu kuzifahamu ni:-
1. Market order/Instant order
2. Pending order
MARKET ORDER
Hii ni order ambayo unaifungua hili uweze kununua (buy) au kuuza(Sell) kwa bei
iliyopo sokoni wakati huo.Mfano umeenda dukani ukakuta kiatu kinauzwa elfu sabini
bila hata ya kutaka punguzo au kusubili bei ishuke unaamua kununua apoapo bei
kama ilivyo utakuwa umefungua instant order ya kubuy.(INSTANT ORDER)
PENDING ORDER
Hii ni order ambayo unaiweka sokoni kabla bei yako ya kuuza au kununua bado
haijafikiwa ,hivyo unakuwa kama unatega ili price ikifikiwa hiyo bei uliyoiweka basi
order ifunguke na uingie sokoni.(order zinakuwa zinaingia automatically katika soko)
Mfano,kama nyumba inauzwa milion 19 lakini wewe hautaki kununua kwa bei hiyo
hivyo unasubiri bei ikishuka na kufika million 15 ndipo ununue hivyo basi million 15
ni pending order yako ya kununua nyumba hiyo.Mfano mwingine ni kama una gari
unataka kuuza lakini bei unayoweza kuuza
wakati huo ni million 2 ambapo kwako wewe unaona sio stahiki hivyo unasubiri
thamani ya gari ipande na ikifika million 8 ndipo uuze hivyo basi million 8 ndio
pending order yako ya kuuza gari.
AINA ZA PENDING ORDER
1. Buy stop
2. Sell stop
3. Buy limit
4. Sell limit
SELL STOP
Ukifanya analysis katika soko utagundua kuna fursa Fulani ya kurudi chini(kushuka
chini) inatokea katika soko. Au imeonesha dalili za kutokea. Lakini sio mda wote
utakuwa katika kioo chako cha kompyuta. Hivo unaweka pending order ya kuuza(sell
stop) kama price itafika eneo fulani. Hivo utaweza kuendelea na shughuli zako kisha
price ikifika pale itajiuza na kukuingiza kwenye market.
BUY STOP
Ukifanya analysis katika soko utagundua kuna fursa fulani inatokea katika soko. Au
imeonesha dalili za kutokea. Lakini sio mda wote utakuwa katika kioo chako cha
kompyuta. Hivo unaweka pending order ya kununua kama price itafika eneo fulani.
Hivo utaweza kuendelea na shughuli zako kisha price ikifika pale itajinunua na
kukuingiza kwenye market.
SELL LIMIT
Hii ni order ambayo utaweka sokoni baada ya kufanya analysis na kugundua kuwa
price inapanda lakini ikifika price flani itaanza kushuka hivyo basi unaweka SELL
LIMIT katika price hiyo na mara baada ya price kufikiwa order yako itafunguka na
utakuwa umeingia sokoni kwa order ya kuuza (sell).
BUY LIMIT
Hii ni order ambayo utaweka sokoni baada ya kufanya analysis na kuona kwamba
price inashuka lakini ikifika price flani itaanza kupanda hivyo basi unaweka BUY LIMIT
katika price hiyo na mara baada ya price kufikiwa order yako itafunguka na utakuwa
umeingia sokoni kwa order ya kununua (buy).

AINA ZA KUFANYA BIASHARA.


Katika forex kuna aina mbili za kufanya biashara, hapa nitazielezea mbili za msingi
ambazo wewe ungependa kuchagua ni ipi itakuwa nzuri kwako.
1. Technical analysis
2. Fundamental analysis
TECHNICAL ANALYSIS
Huu ni aina ya uchambuzi wa soko kwa kuangalia mwenendo wa bei kupitia charts
ambapo tunaangalia jinsi bei (price) ilivyotembea wakati uliopita na tabia ilizoonesha
na tunahusianisha na wakati huo inavyotembea ili tuweze kutabiri/kutambua wakati
ujao itaelekea wapi.
FUNDAMENTAL ANALYSIS
Huu ni ufanyaji wa biashara kwa kuliangalia soko kulingana na shughuli za
kiuchumi,kisiasa na kijamii ambazo hupelekea kuleta madhara katika suala zima la
demand and supply
SUPPORT NA RESSISTANCE
Haya ni maeneo muhimu sana ambayo mfanyabiashara yoyote wa forex anatakiwa
lazima kuyajua. Support na Resistance ni maeneo ambayo ,price ya sarafu husika
huwa na tabia ya kugeukia mara nyingi hapo na hivyo wauzaji na wanunuzi kutafuta
fursa ya kuuza au kununua katika maeneo hayo.
Support - hili ni eneo ambalo bei(price) ya sarafu imefika katika kiwango chake cha
chini na pia ni maeneo ambayo wanunuzi pia hujiandaa kwa ajili ya kupandisha bei ya
sarafu husika kwenda juu.,na ni maeneo ambayo price imegusa kuanzia mara 2 na
kuendelea na kugeuzia hapo.
Resistance - hili ni eneo ambalo bei(price) ya sarafu imefika katika kiwango chake
cha juu na pia ni maeneo ambayo wauzaji(sellers) pia hujiandaa kwa ajili ya
kushusha bei ya sarafu husika kwenda chini.,na ni maeneo ambayo bei imegusa
kuanzia mara 2 nakuendelea na kugeuzia hapo.
MUHIMU:
1. Support iliyotobolewa na bei(price) kuzidi kushuka chini zaidi hii hugeuka na kuwa
resistance mpya.
2. Resistance iliyotobolewa na bei(price) kuzidi kupanda juu zaidi hii hugeuka na
kuwa support mpya. Unaweza kuangalia mchoro hapo juu na kuona jinsi ambavyo
resistance na support hugeuka pale bei (price) inapotoboa na kuweka level mpya.
Jinsi ya kuchora Support na Resistance:
Namna nzuri ambayo unaweza kuchora support na Resistance ni kwa kutumia Line
chart, kama unatumia simu au computer badili chart yako kama iko kwenye
candlestick chart iwe kwenye Line chart.Kisha baada ya kubadili kwenye line chart
weka mstari wa horizontal seheme ambayo unaona bei imegeuka hapo zaidi ya mara
2,yani sehemu ambayo bei(price) imegusa zaidi ya mara 2 na kugeuza ilikotoka.

Support na Resistance hutumika kwa mtindo huu,


• Nunua (buy) wakati bei(price) inapofika kwenye eneo support,
• Uza(Sell) wakati bei(price) inapofika kwenye eneo resistance,
• Nunua (buy) wakati bei(price) imetoboa resistance na kupitiliza kwenda juu zaidi,
• Uza(Sell) wakati bei(price) imetoboa support na kuzidi kushuka chini.tutaona hapo
ni namna gani ikitoboa utakaiwa kuingia sokon
MUHIMU;
Kama utaona bei(price) imefika maeneo ya support na resistance kabla ya kuafanya
uamamuzi kuingia sokoni kununua au kuuza sarafu husika hakikisha umepata
'signal' au alama ya kukuonyesha kuwa sasa bei inageuza .kuelekea unapotaka
kuingia
CANDLESTICK PATTERN.
Candlestick patern ni moja ya kitu muhimu kutumia unapofanya analysis yako(kati ya
kuuza au kununua) kwasababu kitakupelekea kufanya maamuzi sahihi na kuleta
matokeo chanya. CANDLESTICK pattern ni lugha ambayo hutumiwa na
wafanyabiashra wa forex(forex traders)endapo utajua kuitumia vizuri itakusaidia
kujua kujua soko linakutaka ufanye nini.
Kwa sasa nitaelekeza jinsi ya kuzitambua candlestic pattern na ujumbe unaotoa jinsi
kuzitumia katika kufanya biashara.
1. ENGULFING.
Hii ni candlestic pattern ambayo inajumuisha candlestick mbili candlestick ya kwanza
huwa fupi na candle ya pili huwa ndefu kuzidi candlestick ya kwanza.

KUNA AINA MBILI ZA ENGULFING


• BULLISH ENGULFING (BULLISH MOVEMENT)
Hii ni aina ya pattern ambayo hutokana na kuwa na candle moja dogo ya sellers
(wauzaji) ikafuatiwa na candle kubwa moja ya wanunuaji (buyers), candle kubwa ya
buyers umbo lake huanzia chini kidogo ya candle ndogo ya sellers na kufungia juu ya
candle hiyo ya sellers.
Pattern hii hutokea baada ya sellers (wauzaji ) kuanza kupoteza nguvu ya kuendelea
kuwepo sokoni na hivyo buyers(wanunuaji) kuanza kuchukua nafasi.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
1. Tafuta pattern hii ikiwa kwenye movement ya chini amabapo ni eneo la support
2. subiri candle inayofuata kufunga juu ya candle kubwa ya buyers ili kuhakiki uwepo
wa buyers(wanunuaji) sokoni. uhakiki huu ukitimia unaweza kuweka order zako za
kununua.katika soko na ukawa salama
• BEARISH ENGULFING (BEARISH MOVEMENT)
Hii ni aina ya pattern ambayo hutokana na kuwa na candle moja dogo ya
buyers(wanunuaji) ikafuatiwa na candle kubwa moja ya wauzaji(sellers), candle
kubwa ya sellers umbo lake huanzia juu kidogo ya candle ndogo ya buyers na
kufungia chini ya candle hiyo ya buyers.Pattern hii hutokea baada ya
buyers(wanunuaji) kuanza kupoteza nguvu ya kuendelea kuwepo sokoni na hivyo
sellers(wauzaji) kuanza kuchukua nafasi.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.
1. Tafuta pattern hii ikiwa kwenye movement ya juu amabapo ni eneo la resistance
2. subiri candle inayofuata kufunga chini ya candle kubwa ya sellers ili kuhakiki
uwepo wa sellers sokoni. uhakiki huu ukitimia unaweza kuweka order zako za kuuza
sarafu husika.katika soko na kuwa salama
2.DOJI CANDESTICK
Hii hutokea pale ambapo bei ya kuuza na kufungua imekuwa ni moja
AINA ZA DOJI CANDLESTICK
• DRAGONFLY DOJI (BULLISH MOVEMENT)
Candle hii huonekana kama herufi ya T, hapa ni kuwa bei ya sarafu ya kufungua na
kufunga ni sawa,haina ule mwili kamili kama candlestick ya kawaida bali una mkia
mrefu wa chini

Maana halisi ya hili umbo ni nini?


wakati soko linapofunguliwa wauzaji(sellers) huvuta chini zaidi bei ya sarafu husika
lakin baada ya muda wanunuaji(buyers) huongeza nguvu zaidi kuipandisha bei ya
sarafu hiyo juu,na mwisho wanunuaji(buyers) hufanikiwa kuirudisha bei mahali
ilipofungulia.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
kwanza ili uweze kuingia sokoni kwa kutumia candle hii, hakikisha haya yafuatayo
1. Imetokea wakati bei ya sarafu husika iko uelekeo wa chini. (downtrend
movement(in support areas), hivyo hutuashiria kuwa uelekeo wa soko unabadilika
kuanza kuelekea juu (bullish movement)
2.Subiri candle inayofuata baada ya dragonfly ifunge juu ya hii dragonfly ili kuhakiki
uwepo wa uelekeo mpya wa juu, ukishahakiki hivi unaweza kununua sarafu husika..
3. Jinsi mkia unavyokuwa mrefu zaidi,ndio uhakika zaidi wa wanunuaji kutawala
soko.
• GRAVESTONE DOJI (BEARISH MOVEMENT)
Candle hii huonekana kama herufi ya T iliyogeuzwa kichwa chini, hapa ni kuwa bei ya
sarafu ya kufungua na kufunga ni sawa,haina ule mwili kamili kama candlestick ya
kawaida bali una mkia mrefu wa juu.

Maana halisi ya hili umbo ni nini?


wakati soko linapofunguliwa wanunuaji(buyers) huvuta juu zaidi bei ya sarafu husika
lakin baada ya muda wauzaji (sellers) huongeza nguvu zaidi kuishusha bei ya sarafu
hiyo chini,na mwisho wauzaji(sellers) hufanikiwa kuirudisha bei mahali ilipofungulia.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
kwanza ili uweze kuingia sokoni kwa kutumia candle hii, hakikisha haya yafuatayo
1.Imetokea wakati bei ya sarafu husika iko uelekeo wa juu. (uptrend movement (in
resistance area)), hivyo hutuashiria kuwa uelekeo wa soko unabadilika kuanza
kuelekea chini (bearish movement)
2.Subiri candle inayofuata baada ya gravestone doji ifunge chini ya hii gravestone
doji ili kuhakiki uwepo wa uelekeo mpya wa chini, ukishahakiki hivi unaweza kuuuza
sarafu husika..
3.Jinsi mkia unavyokuwa mrefu zaidi,ndio uhakika zaidi wa wauzaji kutawala soko.
3.SHOOTING STAR (BEARISH MOVEMENT)
candle hii huonekana kama nyundo inayoning'inia hewani na mkia mrefu, hutokea
wakati bei ya sarafu husika iko kwenye uelekeo wa juu zaidi.candle hiz huwa
zinajitengeneza upande wa resistance kuashiria kuuza(sell)

Maana halisi ya umbo hili ni nini.?


Kama ilivyo kwa Gravestone Doji candle hii pia wakati soko linapofunguliwa
wanunuaji(buyers) hupandisha bei ya sarafu juu zaidi,lakini wauzaji(sellers)
hupigania kurudisha bei chini,hivyo kupelekea kutengenezwa kwa umbo la mraba.
Jinsi mkia wa juu unavyokuwa mrefu zaidi basi ndivyo inavyotoa uhakika wa sellers
kuchukua nafasi zaidi.

Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?


1. imetokea wakati bei ya sarafu husika iko kwenye uelekeo wa juu (resistance )
2. subiri candle inayofuata ifunge chini ya hii shooting star ili kuwe na uhakika zaidi
wa sellers(wauzaji) sokoni, ikitokea hivi basi unaweza kutafuta nafasi ya kuingia
sokoni kuuza.
4.HAMMER (BULLISH MOVEMENT)
Candle hii huonekana kama pipi ya kijiti ya mraba au nyundo, huwa na umbo dogo
sana ambalo husababishwa na bei ya kufungia kuwa juu kidogo au chini kidogo ya bei
ya kufungulia
Maana halisi ya umbo hili ni nini.?
Kama ilivyo kwa Dragonfly doji candle hii pia wakati soko linapofunguliwa
wauzaji(sellers) huvuta bei ya sarafu chini zaidi,lakini wanunuaji(buyers) hupigania
kurudisha bei juu,hivyo hufanikiwa kuirudisha juu kidogo au chini kidogo ya bei ya
kufungulia.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
1. Imetokea wakati bei ya sarafu husika iko uelekeo wa chini. (downtrend
movement(in support), hivyo hutuashiria kuwa uelekeo wa soko unabadilika kuanza
kuelekea juu (bullish movement)
2. Subiri candle inayofuata baada ya hammer ifunge juu ya hammer ili kuhakiki
uwepo wa uelekeo mpya wa juu, ukishahakiki hivi unaweza kununua sarafu husika..
3. Jinsi mkia unavyokuwa mrefu zaidi,ndio uhakika zaidi wa wanunuaji kutawala
soko.
5.HARAMI.
Hii ni candlestic pattern ambayo inajumuisha candlestick mbili candlestick ya kwanza
huwa kubwa aundefu na candle ya pili huwa ndogo kuliko ile candlestick ya kwanza.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
1. Tafuta pattern hii ikiwa kwenye movement ya chini amabapo ni eneo la support
2. subiri candle inayofuata kufunga juu ya candle ndogo ya buyers ili kuhakiki uwepo
wa buyers(wanunuaji) sokoni. uhakiki huu ukitimia unaweza kuweka order zako za
kununua.katika soko na ukawa salama
3. Tafuta pattern hii ikiwa kwenye movement ya juu amabapo ni eneo la resistance
4. subiri candle inayofuata kufunga chini ya candle ndogo ya sellers ili kuhakiki
uwepo wa sellers sokoni. uhakiki huu ukitimia unaweza kuweka order zako za kuuza
sarafu husika.katika soko na kuwa salama

6.HANGING MAN
huonekana kama pipi ya kijiti ya mraba au nyundo, huwa na umbo dogo sana ambalo
husababishwa na bei ya kufungia kuwa juu kidogo au chini kidogo ya bei ya
kufungulia.
Maana halisi ya umbo hili ni nini.?
Candle hii ni wakati soko linapofunguliwa wanunuji(buyers) huvuta bei ya sarafu juu
zaidi,lakini wauzaji(selers) hupigania kurudisha bei chini,hivyo hufanikiwa kuirudisha
chini kidogo au juu kidogo ya bei ya kufungulia.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
1. wakati bei ya sarafu husika iko uelekeo wa juu. (uptrend movement(in
ressistance), hivyo hutuashiria kuwa uelekeo wa soko unabadilika kuanza kuelekea
chini (bearish movement)
2. Subiri candle inayofuata baada ya hanging man ifunge chini yake ili kuhakiki
uwepo wa uelekeo mpya wa chini, ukishahakiki hivi unaweza kuuza sarafu husika..
3. Jinsi mkia unavyokuwa mrefu zaidi,ndio uhakika zaidi wa wauzaji kutawala soko.
7. INVERTED HAMMER.
candle hii huonekana kama nyundo inayoning'inia hewani na mkia mrefu, hutokea
wakati bei ya sarafu husika iko kwenye uelekeo wa chini zaidi.candle hizi huwa
zinajitengeneza upande wa support kuashiria kununua(kubuy)
Maana halisi ya umbo hili ni nini.?
candle hii pia wakati soko linapofunguliwa wauuzaji(sellers) hushusha bei ya sarafu
chini zaidi,lakini wanunuaji(buyers) hupigania kurudisha bei juu,hivyo kupelekea
kutengenezwa kwa umbo la mraba. Jinsi mkia wa juu unavyokuwa mrefu zaidi basi
ndivyo inavyotoa uhakika wa wanunuaji(buyers) kuchukua nafasi zaidi.
Jinsi gani unaweza ingia sokoni na candle hii.?
1. imetokea wakati bei ya sarafu husika iko kwenye uelekeo wa chini (support )
2. subiri candle inayofuata ifunge juu ya hii inverted hammer ili kuwe na uhakika
zaidi wa wanunuzi (buyers) sokoni, ikitokea hivi basi unaweza kutafuta nafasi
ya kuingia sokoni kununua.
8. SPINNING TOP
Hii ni candlestick moja yenye umbo dogo na mkia mrefu juu na chini. Ikitokea katika
ya eneo la RESISTANCE na SUPPORT huashiria kubadilika kwa trends,

9. RAILWAY TRACK
Hii ni candlestick pattern ambayo huwa na candlestick mbili zinazofuatana zenye
urefu na umbo sawa.hivi pia zinapoonekana eneo la support and resistance uashiria
kujeuka kwa soko
AINA ZA RAILWAY TRACK
• BULLISH RAILWAY TRACK:Katika hii candlestick ya kwanza inakuwa ni
bearish na ya pili ni bullish lakini zenye urefu na umbo sawa.Hii huashiria soko
litageuka kuelekea juu kwenda kununua(buy) endapo ikitokea kwenye
support.

• BEARISH RAILYWAY TRACK:katika hii candlestick ya kwanza inakuwa ni


bullish na ya pili ni bearish lakini zenye urefu na umbo sawa .Hii huashiria soko
litageuka kuelekea chini kwenda kuuza(sell) endapo ikitokea kwenye
resistance.

10. PIERCING
Hii ni candlestik pattern ambayo huashiria kugeuka kwa soko kuelekea juu kwenda
kununua (buy) endapo ikitokea kwenye support.Kwenye Piercing candlestick ya
kwanza inakuwa ni bearish ikiwa na kiashiria kuwa soko lilikuwa linashuka chini na
candlestick ya pili huwa ni bullish na inafunga katikati ya candlestick ya
kwanza(middle at the past candle) kuonesha soko limefika katika eneo la kugeuka.
11. DARK CLOUD COVER
Hii ni candlestick pattern ambayo huashiria kugeuka kwa soko kuelekea chini kwenda
kuuza (sell) endapo ikitokea kwenye resistance,Kwenye Dark cloud cover candlestick
ya kwanza inakuwa ni bullish kuonesha soko lilikuwa linapanda juu na candlestick ya
pili huwa ni bearish na inafunga katikati ya candlestick ya kwanza kuhashiria kugeuka
kwa soko.kuelekea upande wa kuuza(kusell)

AINA ZA CHART KATIKA FOREX


Katika forex tuna chart kuu 3, amabazo ni
• Bar chart
• Line chart
• Japanese candlestick chart
BAR CHART
Chart hii hutumika kwenye kufanya tathmini (analysis),ambapo kila bar moja
huonyesha bei ya juu na ya chini ya sarafu husika kwa muda husika,kama ni dakika 1
au hata wiki 1, ambapo kila bar moja katika chart inawakilisha muda huo, iwe ni saa1
,saa 4 au hata siku.kutegemea na wewe mda uliyoweka katika chart yako.tuone
mafano chi wa 4hr chart
LINE CHART
Hii ni chart inayounganisha point mbalimbali za bei katika sarafu husika kwa kutumia
mstari (line). Line hii inakupa mwangaza jinsi ambavyo bei inabadilika kila baada ya
muda husika amabao utakuwa umeuset katika platform yako, na kukupa rekodi
sahihi ya historia ya bei za nyuma zilivyofungwa katika market

JAPANESE CANDLESTICK CHART


Hii inafanana kidogo na bar chart,tofauti yao kubwa huwa kwenye kufunga na
kufungua bei ya sarafu husika,ambapo tofauti na bar chart ,candlestick chart
inaonyesha zaidi uhusiano wa bei ya kufungua na kufunga wa sarafu kwa siku husika.
Ambapo chart hii pia huonyesha uhusiano wa Bears(wauzaji) na bull (wanunuzi)
katika soko la forex.
MUHIMU;
Chart hizi zote kwa pamoja tunaweza kuzifanyia analysis katika muda tofauti tofauti
sokoni kuanzia dakika moja,dakika 5,dakika 15,dakika 30,lisa 1, ma saa4, siku 1
,wiki 1 au mwezi.kutegemea na wewe unataka nini,ni muhimu kuanalyse muda
tofauti ili kuwa na uhakika zaid pale unapochukua fursa.
CHART PATTERN
Hii ni mifumo ambayo hutuwezesha kuingia sokoni na kufanya biashara kwa urahisi
zaidi na maamuzi yenye usahihi zaidi wa ama kununua au kuuza sarafu husika.
Kuna aina mbili za charts patterns ambazo ni::
1. REVERSAL PATTERN
2. CONTINUATION PATTERN
1. REVERSAL chart pattern
Pattern hizi zina Kazi ya kutoa kiashiria(signal) kuwa soko linaelekea kubadili uelekeo
wake,kama lilikuwa na uelekeo wa chini(downtrend) basi linaanza kwenda
juu(uptrend) nakadhalika. Hivyo humfanya mfanyabiashara wa soko hili kujiandaa na
mabadiliko yanayofuata ya soko husika.kw wakati huo.
Mfano wa reversals chart pattern ni kama ifuatavyo
• Double tops
• Doubles bottoms
• Triple tops
• Triple bottoms
• Head and shoulder
• Inverted H & S
• Ending diagonal
• Ascending triangle and
• Descending triangle
kuna pattern nyingine nyingi sana,ila kwa reversa pattern l hizi ndizo maarufu na
rahisi kuonekana kwa haraka kwenye chart yako
2. CONTINUATION CHART PATTERN
Pattern hizi zina Kazi ya Kuonesha kuwa soko bado linaendelea na uelekeo wake ule
wa awali ,kama lilikuwa na uelekeo wa chini(downtrend) basi litaendelea kwenda
chini zaidi na kama lilikuwa na uelekeo wa juu basi litaendelea kwenda juu na zaid.
Mfano wa continuation chart pattern:
• Rectangle chart pattern
• Triangle chart pattern
• Flag chart pattern
• Cup and Handle chart pattern
TRENDLINE
Hii ni tool inayofanya kazi kama support and resistance, asili ya kuitwa Trendline
ni namna inatumika tu katika trending market.
Je trending market ni nini?.
Trending market ni aina ya market inayokua na muundo wa higher highs and
higher lows lower highs and lower lows!
• Uptrend ni trend inayoundwa kwa higher high(HH) and higher lows(HL) ambapo
market huwa inapanda juu.
• Downtrend inaundwa kwa lowerhighs(LH) and lowerlows(LL) hivyo basi katika
trend market huwa inaelekea chini.

Channels
hii nayo inafanana saana na trendlines na hata katika mazingira yake ni vile tu kama
trendline ila tofauti yake na trendiline yenyewe ina mistari miwili kwa pamoja juu na
chini yaani mfano wa reli hivi kwa hiyo mstari wa juu utakua resistance na wachini ni
support kwa maneno mepesi kabisa.au unawezea kusema ni njia ambayo bei
huifuata na hujenga kingo ambapo bei inakuwa inatembea ndani yake ila baada ya
mda inavunja kingo mojawapo kutegemea ilikuwa ni ya kupanda(uptrend) au
kushuka(downtrend).

AINA ZA CHANNEL
• Downtrend channel(chaneli ya kushuka)
• Uptrend channel(chaneli ya kupanda)
• Sideway channel(chaneli msambamba)

Downtrend:hizi ni channel za kushuka


Uptrend ni channel za kupanda juu
Sideway channel:hizi ni channel msambamba

CHANNEL INAPOVUNJWA INABIDI USUBIRI IFANYE RETEST AU PULLBACK NDO


UTAFUTE FURSA YA KUINGIA KATIKA SOKO HAPO MBELE NTAELEZEA RETEST AU
PULLBACK NINI?
OK NDUGU ZANGU KABDA YA KUFNDISHA NAMNA YA KUTUMIA MT4 ANGALAU TUWE
NA DEMO ACOUNT KWA AJILI YA KUITUMIA KWENYE MT4 YETU NA ILI UWE NA
DEMO ACCOUNT NI LAZIMA UJISAJILI KWA BROKER SASA KAMA HAUJAJISAJILI
TUMIA LINK CHINI KUJISAILI
BROKER NI NANI?
BROKER ni mtu wa kati anayetuunganisha kwenye soko la FOREX,kwa hiyo
tunatakiwa kufungua akaunti kwake ili tuweze kufanya hii biashara hii.
wapo brokers tofauti na wengi tyu zaid ya 1000 ni wewe kuamua kucagua broker
mzuri na trusted tyu\
Vitu muhimu kuwanavyo ili kuweza kujisajili n broker
1. Kitambulisho
- Cha mpiga kura
- Cha utaifa
- Leseni ya udereva
- cha mkazi wa zanzibar
- passport
(uwe nacho kimojawapo kati ya hivi)
2.Active Email addres.
3.Namba ya simu
4.kuna broker wengine wanahiaji na wengine sio lazima Bank statement, document
inayoonesha bill ya maji au umeme vyote vikiwa na jina lako kama lile unalotumia
kwenye kitambulisho na vikionesha anuani ya makazi note sio kila broker anaihitaji
5. Namba 4 ni muhimu kama unataka kutumia BANK ( VISA card) kwenye kuweka na
kutoa Pesa ,lakini kama hauna unaweza ukatumia no 1 mpaka 3 na ukafanikiwa
kufungua akaunti
ntakupa link ya broker ambae atakuwa ni vepes kwa wewe kujisajili kwa sasa
https://track.deriv.com/_UsOk4XulkfC2vdm9PpHVCmNd7ZgqdRLk/1/
Tumia link hiyo juu kujisajili, click hiyo link hapo juu
Tumia majina kama yalivyo kwenye vitamblisho
Ukishajisajili hapa nadi ya hiyo portla tafuta download then minya dashboard then
chagua MT5 kulingana na kifaa chako
TUTAJIFUNZA KUTUMIA MT4 / MT5 AINA MBILI ZILE ZA KWENYE SIMU NA YA
COMPUTER
TUANZE NA YA SIMU
JINSI YA KUTUMIA METATRADE(MT4 / MT5) KATIKA SIMU AINA YAKO.
Ingia katika playstore au apple store kwenye simu yako na andika META TRADER 4
itatokea kma tunavyoona hapa chini

Baada ya kuiona app hio click INSTALL na itakuwa kwa simu yako sasa kwa matumizi
Unapokuwa umeingia katika application kwa mara ya kwanza screen itakuonesha
namna ya kusajili akaunti mpya na kulog kama acc utakuwa nayo teyari(log in
existing account)
kwa kuwa utakuwa ulshafungua account kwa broker utaminya ''log in to an existing
account'' mbele yake litakutaka uchague broker utachagua broker unayemtumia na
account uliyojisajili mfano TEMPLER,OCTAFOREX,TICKMILL etc .baada ya hapo
utajaza username na password yako sasa kama hapa chini
QUOTES
Hii ni sehemu ambayo huonesha viwango dhahiri katika muda sahihi vya sarafu
mbalimbali. Quotes ya kawaida huonesha aina ya pair na bei ya kuuza na kununa.
kama utataka kuongeza pair zaid utagusa alama ya kujumlisha inayooneka kwa juu
ili kuongeza pair ambayo haipo katika list na unahitaji iwepo.
Sehemu inayofuata inaonesha chart kam ilivyoandikwa

Haya katika chart tunaona kuna alama tano juu tuue zinawakilisha nini zote
ehemu ya kwanza katika chart inaonesha kimsalaba ambapo hiutwa CROSSHAIR
Sehemu ya pili ni kama herufi F iliyolala. Hapo ndipo huweza kuset indicators yoyote
pamoja na kuchora mistari ya resistance na support na mingineyo.
Sehemu ya tatu $ hapa hutoa nafasi ya kuchange chati kutoka chati ya sarafu moja
kucheki chati ya sarafu nyingine.
Sehemu ya nne ni sehemu ya kubadilisha timeframe za chati husika. Ina alama ya
saa
Na ile sehemu iliopo mwishoni kabisa pale ni sehemu ya kuwekea oda sokoni, kati
buy au sell/sell stop au buy stop/ sell limit au buy limit.
sehemu ya pili katika chart
sehemu ya tatu katika chart
Sehemu ya nne katika chart
Sehemu ya tano na ya mwisho katika chart
Haya tuende na kipengele kinafuta baada ya chart ambacho kinaonesha trades zako
nacho kwanye metratrade 4

Taarifa za akaunti
- PROFIT- faida/hasara iliopatikana baada ya kuclose trade
-BALANCE- kiasi kilichopo katika akaunti yako.
- EQUITY- Kiasi kilichopo katika akaunti yako + matokeo ya trade ulisofungua
zaweza kuwa hasara/faida
- MARGIN LEVEL (%)- Equity/margin * 100
- MARGIN- Kiasi kinachohitajika ili kuendesha position zilizofunguliwa.
- FREE MARGIN- Equity-Margin
Vipengele vilivyowekwa kwa mfumo wa number
1.Aina ya sarafu uliyotrade
2. Aina ya oda uliofanya katika hio sarafu sell/buy

3. Aina ya lot size ambayo umeitumia katika trade yako


4. Bei ambayo umeingia katika trade zako
5. Bei iliyopo katika soko muda huo.
6. Aina ya oda(PENDING ORDERS)
7. Bei ya ambapo order inatakiwa kuingia sokoni (pending oda)
8. Matokeo ya ile trade ulioifungua kat ya faida au hasara
9. Bei iliyopo muda husika kuelekea katika ile pending oda
Window inayofuata katika mt4 ni sehemu inayoonesha history ya akaunti zako, kiasi
ulichoingiza kwa mara ya kwanza, kiasi ulichopata kama faida na hasara, ripoti ya
ulichofanya kwa mwezi, wiki, siku hadi miaka

kufungua trade katika window ya chart


kufungua oda kwa price iliyopo sokoni.

Jinsi ya kufungua pending order


Jinsi ya kubadilisha/kurekebisha oda na jinsi ya kufuta oda.

MWISHO WA SOMO LA MT4 / MT5


TUKAJIFUNZE MBINU MBALIMBALI ZA KUTRADE KATIKA CHART SASA SOMA ELEWA
KILA KITU JAPO ION MASWALI INBOX NAHISI UMEELEWA
Hapa tutasoma vitu kama
1.THE LAST KISS/RETEST
2.THE BIG SHADOW
3.WAMMIES AND MOOLAHS
4.KANGAROO TAILS
5.THE BIG BELT
6.THE TRENDY KANGAROO
7.EXITING THE TRADE nk......
THE LAST KISS.
Wafanyabiashara wanapoona bei haipandi juu wala kushuka chini zaidi, hutambua
kuwa bei ina consolidate na hakuna anaejua itaenda wapi kwa mda huoo. Hivyo
huchora box katika lile eneo ili endapo bei ikitoboa upande wowote wanajua ndipo bei
inaelekea. Lakini bei inaweza ikatoka ndani ya hilo eneo la consolidation lakini kumbe
ikawa ni FAKE BREAKOUT. Matokeo yake unafanya maamuzi kisha bei inageuka na
kurudi tofauti na maamuzi yako.
LAST KISS inakuwa ni mvunjiko wa nje(break out) ambao inatuhakikishia sasa
TREND inaenda upande sahihi. Baada ya bei(price) kutoka katika lile eneo ambalo
umelitenga halafu unaona inarudi(inarudi kutafuta nguvu) tena usawa wa lile eneo la
box kwa kuonesha inaingia lakini CANDLESTICK inafunga kwa kuona ni WICK
imeingia katika eneo lile kisha bei imefunga nje
ya eneo la consolidation basi hiko ni kiashiria cha kuwa huo upande ambao imeenda
ndipo bei itaelekea. Kwa lugha rahisi ni pale price ikitoka katika eneo la consolidation
kisha ikarudi kugusa lile eneo bila kuingia (RETEST) hio ndio LAST KISS.

Sio kila mvunjikoa wa nje(breakout) katika eneo la consolidation ni LAST KISS lakini
kila LAST KISS unayoiona ni BREAKOUTS katika soko.
MUHIMU: pindi uonapo LAST KISS ingia katika trade katika candlestick ya pili kutoa
ya kwanza iliyorudi kwnye box baada ya breakout kulingana na uelekeo.

mfani hapo unaona buy ilipowekwa pale


hiyo ni baadh tu ya mifano vingine unaweza fanya mazoezi kwenye chart yako
mwenyewe
KANGAROO TAIL
Kangaroo tail ni muundo wenye nguvu sana ambao trader wengi wanaotrade chati
tupu(Naked chart) hunufaika. Muundo huu inawezekana huonekana mara nyingi
katika chati kuliko aina yoyote ile.
Chukua mwili wa mnyama Kangaroo ulivyo, umbo dogo halafu mkia mefu. Hivyo
kuna candlestick utaona zina umbo dogo na mikia mirefu. Baada ya kupata uelewa
wa kutosha kuhusu muundo huu naimani utaanza kuuona mara kwa mara, na zaidi
katika maeneo ya REVERSAL.
Kangaroo tail zote lazima ifunguke na kujifungua karibia na mwisho wa
CANDLESTICK iliyopita kbada ya hiyo

bearish kangaro
bullish kangaroo
wick au mkia wa candlestick hii lazima uwe mrefu

angalia kitu gani kinaweza kutoka kama wick ikiwa fupi


inaweza kukutengenezea fake formation katika chart yako kukudanganya kwanza
kabda ya kuende direction ile unayotalka mfano chin hapa

Angalia mfano hii kulikuwa na strong trend kisha Kangaroo tail ilivyopinga strong hio
kuigeuza na kutengeneza bearisha kangaro .
Pia wakati mweingine Kangaroo tail zinazojitengeneza katikati ya Trend na zilizo
kinyume na hio trend. Huwa ni uongo zinadanganya ili ufanye maaumizi(fake
formation)
mifano mingine fanya mazoezi utaiona zaid kwenye chart hapo ni baadhi ya mifano
tyu nimetoa

BIG SHADOW
Kama umekuwa mfuatiliaji wa chart utakuwa ushawahi kuona kuna CANDLESTICK ni
ndefu sana na hakuna NEWS au Factor yeyote kubwa. Hii pia lazima itokee katika
eneo la RESISTANCE na SUPPORT. Na inasimama au ni kiashiria kama REVERSAL.
Baadhi ya watu wanaweza kuifananisha hii na ENGULFING, Lakini nataka kukwambia
hii ni zaidi ya ENGULFING.
inapojitengeza katika resistance kama hapa juu tunaita bearish big shadow ikiashiria
kusell
na inapokuwa katika support tunaiita bullish big shadow ikamaanisha kubuy au
kununua
UNAPOAMUA KUFANYA MAAMUZI UNAPOONA BIG SHADOW ZINGATIA HAYA
1. Huu ni muundo wa CANDLESTICK mbili kwa . Candlestick ya pili katika kuundwa
huku ndio tunayoiita BIG SHADOW CANDLESTICK.
2. BIG SHADOW CANDLESTICK lazima iwe kubwa kwa urefu wa juu na chini kuliko
candlestick iliopita nyuma yake.
3. BIG SHADOW lazima itokee kwenye maeneo ya SUPPORT na RESISTANCE.ndo
maeneo ya kufanya maamuzi
4. BIG SHADOW hutokea kwa kwenda juu na chini kulikokithiri zaidi.
5. Kwa BULISH BIG SHADOW, Stop loss huwekwa pips chache chini ya ile BULLISH
BIG-SHADOW CANDLESTICK
6. Kwa BEARISH BIG-SHADOW, Stop loss huwekwa pips chache juu ya ile BEARISH
BIG-SHADOW CANDLLESTIICK
WAMMIES AND MOOLAHS.
Hii ni pale price inapogusa mara mbili kwa kufuatana katika eneo la SUPPORT au
RESISTANCE, ambayo huwa inafuatana.

Wammies and moolahs hutokeaa katika timeframe yoyote, kwa soko la aina yoyote,
Wammies and Moolahs ni kitu cha toleo la kipekee la DOUBLE-TOP and DOUBLE-
BOTTOM. Ukizifuatilia kwa makini aina hii aina ya muundo, unaeza ukawa unatrade
njia hii tu na ikakupa matokeo chanya kwa asilimia nyingi.
Wammies and Moolahs pia ina kaa uzuri katika muundo wa PATTERN zinazoashiria
REVERSAL ya soko.
Traders ambao huingia na kutoka katika trade katika maeneo ambayo wanachukulia
hii kama njia hii ni ya msingi na ya manufaa kwao.kataka ktafuta fursa za kuingia
katika soko
WAMMIES ni pale price inagusa eneo la SUPPORT katika chart yako sokon .
MOOLARS ni pale bei inapogusa katika eneo la RESISTANCE katika chart
yako
SIFA ZA WAMMIES
1. Soko linagusa eneo la Support mara mbili.
2. Kugusa kwa mara ya pili huwa juu zaidi ya mara ya kwanza.
3. Kunakuwa na candlestick zisizopungua sita katikati ya hio miguso miwili.
4. Soko hutengeneza bullish candlestick katika mguso wa pili
5. Stop loss inawekwa pips chache chini ya ile candle iliogusa mara ya kwanza.
SIFA ZA MOOLAH.
1. Soko linagusa eneo la Resistance mara mbili.
2. kugua kwa pili huwa chini ya ule mguso wa kwanza kutokea.
3. Kunakuwa na candlestick zisizopungua sita katikati ya miguso hio miwili
4. Soko hutengeneza bearish candlestick baada ya mguso wa pili.
5. Trader huingia kwa SELL STOP pips chache kutoka katika ile Bearish candlestick.
6.Stop loss inawekwa pips chache juu kidogo ya ile candle iliogusa mara ya kwanza.
BIG BELT
Soko la Forex hukumbwa na nyakati za ajabu wakati mwingine ambzao hata unaweza
usielewe zimetokea vip. Tunaamini kuwa candle inapojifunga ndipo candle nyingine
inatakiwa kufunguka lakini unakuta candle imefunga sehemu nyingine na inayofuata
inafunguka sehemu tofauti. Kwa mtu aliyekuwa nje ya soko hii inakuwa fursa nzuri
sana kwake.
TRENDY KANGAROO.
Hii inakuwa tofauti kidogo sana na Kangaroo Tail. Hii hutokea ambapo soko lipo
katika trend Fulani kisha unakuta soko limetulia linacheza ndani ya eneo Fulani na
candles hazitoki katika hilo eneo kwa mda flani.
na baadae inakuja kutokea cndle ya kangaro tailkufanya maamuzi either ni kusell au
kubuy
EXITING TRADE.
MAMBO YA KUJUA WAKATI UNAINGIA KATIKA SOKO LA FOREX
1.Kutambua fursa ya kufanya trade na hapa unachagua kiasi cha hela unachotaka
kukitoa kwa ajili ya kuingia katika trade hio, Ndipo unaangalia matumizi ya lot size,
idadi ya position na Risk management.
2,Unatengeneza mpango wa kufanya hio trade, kwa kufuata sheria za njia
unayotumia katika kufanya trade.ka ma wewe mwenyewe ulivyojipangia
3.Kuingia katika soko, Ingia katika soko katika kwa bei ambayo unajua ni thamani
yenye kuleta manufaa katika fursa iliyopatikana. ukiona umechelewa kuingia achana
na hiyo fursa na utafute fursa nyinginee
4.Kutoka nje ya soko, Hapa ndipo utahesabu kama umetengeneza faida kiasi gani au
umepata hasara hasara.
5.Kujifunza kutokana na trade unazaokuwa unaingia , Kutambua mapungufu
uliyoyafanya kuanzia hatua ya kwanza mpaka ya tano.
6.kuwa na malengo na kufanya forex na target yako maalam unayojua ikifika
unaweza toka katika market nk.
7.unapoaana kuna kitu kimetokea katika trade yako tofauti na ulivyotarajiamfano
news(habari) na ukaona trend imeahribiwa jifunze kutoka katika hiyo trade

# copide notes

HATUA SITA ZA KUKUFANYA UWE MTAALAM KWA ANAETUMIA CHATI TUPU.


Ingawa inaonekana ni jambo gumu sana kuwa mtaalamu wa hii biashara, lakini
nataka nikuhakikishie ni rahisi. Kama ilivyo kwa mambo mengine katika maisha ya
kawaida, kadri unavoweka nguvu katika jambo Fulani ndipo unajiongezea nafasi
kubwa ya kulimudu jambo hilo jambo hilo katik soko.
1.HATUA YA KWANZA: TENGENEZA ENEO AMBAO HALITAKUPA WASIWASI NA
SHAUKU.
Kwa mfanyabiashara anaetumia chati tupu eneo(zones) ni sehemu pekee ya kufanyia
maamuzi. Hivyo hakikisha umechora zones vizuri katika chati yako
ili pindi bei ya sarafu inavyofika katika eneo hilo, uwe ni wakati sahihi wa kufanya
maamuzi yalio sahihi.
Hii itakufanya usubiri kwa mda mrefu kusubiri bei ifike katika ukanda uliochora. Haina
shida, hii ni sehemu ya kuitwa mfanyabiashara wa chati tupu. Pindi fursa inapotokea
kwa bei kuwa katika zones yako utajikuta umeingia katika trade zenye manufaa
sana.
2.HATUA YA PILI: CHAGUA MUUNDO WA ISHARA AMBAYO ITAKUFANYA UINGIE
SOKONI.
Tumeshasoma mbinu za kufanya biashara katika chati tupu na pattern mbalimbali
katika tabia ya soko. Hapa ushauri ni chagua mbinu moja au mbili ambazo
zitakufanya kila price(bei) ikifika katika zones na utakapona ishara ya muundo uo
imetokea ufanye maamuzi.
Ni lazima uchague kiashiria muundo ambacho umekipa imani kwa kiasi kikubwa.
Muundo kiashiria ambao umeuamini pindi unapotokea huleta matokeo chanya.
3.HATUA YA TATU: FANYA MAJARIBIO.
Fanya majaribio kwa wingi zaidi ili kujua kuwa mfumo wako uliochagua unafanya kazi
kwa matokeo chanya kwa ukubwa wa kiasi gani.Kufanya majaribio ya mara kwa mara
ni hatua pekee itakayokufanya uweze kuelewa kila trade inayokuja mbele yako na
kuwa upande wa matokeo mazuri kwa wingi zaidi. na pia uwe na lengo katika zoezi
unalofanya
4. HATUA YA NNE: ANZA KUTUMIA MFUMO ULIOUCHAGUA.
Baada ya kuufanyia majaribio mfumo wako na kuwa na manufaa kulingana na
matokeo yake, ingiza mfumo huo katika live account kutoka katika demo account.
Kiuhalisia hii itakuwa hatua inayoenda polepole sana. Kwa sababu pindi ukiingia
katika live market kwa live account yako hautaweza kuwa na speed kama wakati
unafanyia majaribia mfumo wako. Hii ni asili yake, Hapo pia ndipo utaona upande wa
pili wa kioo katika live market. Huku ndipo matumizi ya hisia, tamaa na uvumilivu
yanapoanza kuhitajika. Inaweza kuchukua mda mrefu sana kupata kiashiria cha kile
unachokisubiri kitokee ili uingie sokoni. Usilazimishe mambo. Kuwa mtulivu zaidi
unapotaka kufanya maamuzi.
5.HATUA YA TANO: SASA INGIZA MTAJI WA KIASI UNACHOKIHITAJI.
Wafanyabiashara wengi hawapitii hatua hizi nilizokueleza hapo juu. Hivyo itakujenge
ujasiri na kutambua ni nini unachokifanya. Utakuwa umejijengea ujasiri katika hatua
hizo tano zilizopita. Sasa upo tayari kuwa mfanya biashara mwenye manufaa. Kitu
muhimu katika hatua hii ni kuhakikisha unafanya na kufuata kanuni zile zile za
mfumo wako. Unapotrade akaunti kubwa hakuna kikubwa kin achobailika zaidi ya
ukubwa wa balance hivyo nidhamu na ufuataji wa kanuni ni jambo la msingi.
Kufikiria fedha zaidi unapokuwa sokoni kutakufanya utoke nje ya ufuataji wa sheria.
BiaShara haipo kwa ajili ya kutatua matatizo yako, ya familia yako. Biashara inahitaji
kukua ili ilete mafanikio. Jikite katika kuzingatia kanuni za soko faida ni jambo la
mwisho kwako kulifikiria. Hakikisha mpango wako umefuatwa na malengo yako
katika soko yanatimia. Katika chati ako hakuna sehemu imeandikwa pesa hivyo
zingatia vitu vilivyopo kwenye chart hayo mengine yawe ni matokeo.
OKY SASA KAMA BAO AUNA ACCOUNT KWA BROKER UNAWEZA TUMIA LINK HIZI
KUISAJILI ILI UWEZE KUFANYA MAZOEZI ZAID NA ZAIDI
ntakupa link ya broker ambae atakuwa ni vepes kwa wewe kujisajili kwa sasa
https://track.deriv.com/_UsOk4XulkfC2vdm9PpHVCmNd7ZgqdRLk/1/
hapo uwe na kitambulisho kati ya
-TAIFA
-MPIGA KURA
-LESEN
-PASSPORT NK
MPAKA HAPO NIMEMALIZA BASIC YA FOREX MTU YEYOTE ANAWEZA KUSOMA NA
KUINGIA KATIKA MARKET
KIPINDI KINACHOFUTA NTAFUNDISHA KUHUSU ZONES
LEO TUNAENDELE NA PINDI LETU LA ZONES
NA HAPA TUTAANGALIA Supply na demand
SUPPLY AND DEMAND
Supply na demand hizi ni kanda au zone ambazo zinapatikana katika chart ya forex,
hizi zone huwa ndio zinazozingatiwa sana na matrader wote wa aina tatu, ambao ni
seller buyer na institutions, ambao seller na buyer kwa neno moja tunawaita retailer
traders yani wafanya biashara wadogo wadogo na hao walio kwenye taasisi mbali
mbali ambazo zinajihusisha katika biashara hii ndio hao tunawaida wafanya biashara
wakubwa na ndio hasa wenye nguvu katika soko hili la forex.
Kwahiyo kwakua wafanya biashara wote huwa wanaheshimu zones(ukanda) basi hii
inapelekea uhakika zaidi pindi unapotrade kwakutumia zone, maana ndipo jicho la
kila mfanya biashara lilipo duniani kote.
Kama nlivyosema hapo juu kwamba support na resistance huwa hazina utofauti sana
na supply na demand kwa kuziangalia kwa macho ila kiufundi huwa utofauti upo tena
ni wamuhimu sana na ili utrade hii strategy ni lazima uzingatie utofauti huo, maana
usipozingatia huo utofauti utakua umetoka kwenye maana halisi ya supply na
demand na unaingia kwenye support na resistance

Utofauti uliopo kati ya demand na supply ukilinganisha na support na resistance ni


kwamba support na resistance huwa yenyewe inasisitiza sana kwenye idadi ya
candlestick ambazo zinagusa kwenye hizo mistari ya
support na resistance huwa kadri inavyogusa Mara nyingi na kushindwa kuvuka
upande wa pili wa huo mstari basi ndio uimara wa huo mstari wa support au
resistance unavyoongezeka zaid na zaid.
la kwenye supply na demand hii kitu imekataliwa kabisa na kuna sababu nyingi
ambazo zimetolewa zinazofanya hiyo point ikataliwe, huku wanasema kwamba ili
zone ya demand au supply iwe imara basi ni lazima iguswe na candle moja mpaka
tatu zikizidi hapo basi hiyo si ukanda imara kwahiyo achana nao, sasa wakatoa
sababu za kwanini haiwi zone imara ikiguswa na candle ya zaidi ya mbili au
tatu.tutaziona hapo chini
Sababu ya kwanza ya kwanini supply na demand strategy imekataa kwamba idadi ya
miguso mingi kwenye ukanda si uimara wa ukanda huo.
Kwanza tupate picha then tutaenda kwenye sababu moja kwa moja, kama
tulivyowahi kusema huko juu kwamba soko huwa linamove up and down na wakati
mwingine linakua limekaa kwenye usawa na likiwa linapanda juu huwa tunasema
demand wananguvu kuliko supply na likiwa linashuka chini
huwa tunasema supply wananguvu kuliko demand na likiwa katika usawa hapa
tunasema supply na demand wote wako na nguvu sawa .

Kwahiyo ili soko litembee kwenda juu au kurudi chini ni lazima kuwe na kuzidiana
kwa nguvu kati ya demand na supply na endapo wakitoshana nguvu basi soko huwa
linakua linafanya haki, yani watakao nunua watanunua sawa na watakao uza.
Kwahiyo kutokana na sababu hii ya kinachopelekea soko litembee juu chini au chini
juu, ndio sababu ya kwanza inayopelekea supply na demand kukataa ile dhana ya
kwamba eti uimara wa zone unapimwa na idadi ya miguso mingi ya candlestick.
Kwa sababu endapo ukanda utaguswa na candle Mara nyingi hii inamaanisha supply
na demand nguvu zao hazina utofauti sana au ndio zinaelekea kwenye uwiano sawa,
ila endapo itaguswa na candle moja au mbili then reaction ya kwenda juu au chini
ikawa imetokea basi hapo tunasema demand na supply hawako katika usawa na hapo
lazima kutakua na pips nyingi sana.

Kwamfano chukua kitenesi kidundishe kwenye sakafu then kiangalie vile kitakwenda
juu na kurudi kugonga sakafu then kitakwenda baadae
kitapungua kasi na baadae zaidi kitaishiwa nguvu na kitaanza kuroll na hatimae
kitatulia sehemu moja.basi hata
kwenye zone candlestick zitakwenda zitagusa na kugusa tena na tena na baadae
zitatulia hapo kwa muda mwingi bila kushuka sana wala kwenda upande wa pili, so
kadri zone inavyoguswa Mara nyingi ndio udhaifu wake unaongezeka.kwenye mpira
ukiruhusu timu pinzani iwe inakuja kwenye himaya yako Mara kwa Mara lazima
utafanya makosa tu na utaachia na utafungwa goal so miguso ikitokea mingi itafikia
mahali usawa utaonekana na usawa ukitokea basi ukatili utafuata(initiative), hii ndio
tofauti ya hao jamaa na ndio maana kuna watu wanasemaga support na resistance
haina jipya nlimskiaga mtu aliwahi sema hivi pia na marumbano yalikua mengi mno
ingawa sijajua kama na yeye alitumia point hii au alikua na maana nyingine,
anyway tutaendelea na somo baadae now chukua hiko aye.

You might also like