Professional Documents
Culture Documents
Fani Kilio Cha Haki
Fani Kilio Cha Haki
DAR ES SALAAM
KOZI: SHAHADA YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA MAFUNZO
ENDELEVU
1. SADI ISSA
2. TESHA ANTUSA
3. MLINGWA AGNESS
4. MASIMBA SHABANI R.A.
5. HABIBU ABASSI
6. MSHANA EMELINE
7. KISHIMBWE HALIMA
8. GODFREY RENATUSI
9. HAMISI SHABANI
SWALI:
“KILIO CHA HAKI” ni Tamthilia iliyoandikwa na Alamin Mazrui (1981). Tamthilia hii
inaelezea mapambano baina ya wafanyakazi na udhalimu wa makaburu. Tamthilia hii ina sawiri
mapambano ya nchi nyingi za kiafrika kutaka kujikomba kutoka kwa watawala wa kikoloni.
Katika tamthilia hii mwandishi amemchora mwanamke jasiri aliyejikomboa kimawazo na ndiye
aliyekua kiongozi wa mapambano na anadhihirisha udhalimu wa jamii yake unaowapata
wafanyakazi kwa Mwanamke huyu.Alifaulu katika kuwazindua wafanyakazi wenzake ili
wapambane na udhalimu na watetee haki zao. Mapambano haya yanaleta mwamko wa kisiasa
ambao ndio mwanzo wa matayarisho ya vita vilivyoikomboa nchi nzima kutoka na ukoloni.
FANI
“Fani ni ufundi wa mwanafasihi anaoutumia katika uandishi wa kazi yake, ili aweze kufikisha
ujumbe wake kwa wasomaji wake. Katika uchambuzi wa tamlithiliya hii vipengele vilivyo
chambuliwa ni muundo, mtindo, lugha, wahusika, mandhari, maleba, vifaa, matumizi ya
jukwaa, jina la kitabu, kufaulu na kutofaulu kwa mwandishi.
MUUNDO
Msanii AlaminMazrui aliandika tamthiliya hii katika maonyesho kumi, kama ifuatavyo:-
Onyesho la kwanza ukurasa wa kwanza hadi kumi na nne.
Mussa na Dewe wanasoma taarifa toka gazetini zinazo eleza kuwa Kamishina Hunderson
amemkamata Lanina wa Muyaka kwa tuhuma za mauaji ya watu watatu kwenye shamba la
Bwana Delamon.
Lamina kwa mara ya pili tena anahojiwa na makechero kwenye kituo cha polisi kuhusina na
mauaji ya watu watatu kwenye shamba la Bwana Delamon.
Lanina anawajibu makachero kuwa Delamon na wenzake hawakuja kutunufaisha bali kuja
kunyonya nchi yetu ukurasa wa 24.
Lanina alirudi nyumbani lakini alikutana na lawama za mume wake Bwana Mwengo kwa
kumuachia familia kwa muda mrefu. Hata hivyo walisamehana na kutaka waendelee
kushirikiana.
Lanina anakutana na wazazi wake kijijini,baba yake anamlaani na hata kuwapiga yeye na mama
yake kwa sababu Lanina hafuati mila na desturi za kwao na mama yake ndiye aliyepewa
kumfunza.
Hapa wasaliti Matovu, Tereki naPelekha wanajifariji na kuwaona akina Musa na Dewe na
Lanina kuwa ni wajinga, kwa kukataa msamaha wa Bw. Delamon.
Wasaliti hawa wana washawishi Lanina arudi kazini kwa vile wameruhusiwa kuendesha
shughuli za siasa na mshahara unapanda juu kidogo. Lanina anakataa na kuwafukuza nyumbani
kwake.
Onyesho la Nane (uk 56-65)
Lanina yupo kwenye kioski cha mzee Ingeli. Musa, Dewe na Lanina wanakutana kupeana taarifa
kuwa eti Delamoni ameruhusu kuanzisha chama na kumruhusu kurudi kazini.
Hapa Lanina akiwa gerezani anakutana na Askari Malaya aliyekuwa anamtongoza Lanina, lakini
Lanina anamkatalia na kumpiga teke sehemu zake za siri, pia Lanina anaitwa na jaji na
kumsikiliza maelezo yake, uk 77.
MTINDO
Katika tamthilia hii mwandishi ametumia mtindo wa mwingiliano matini ambapo ameonyesha
mambo mabalimbali yaliyounda kazi hii ya fasihi. Mfanonidialojia, hapa mwandishi aneonyesha
mazungumzo mbalimbali ya wahusika wakijibizana.
Matumizi ya gazeti, pia mwandishi ametumia gazeti lengo lake ni kusambaza habari kwa watu,
hata wale waliogerezani, pia kuonyesha kuwa baadhi ya wahusika ni wasomi, na matumizi ya
gazeti yameonyeshwa katika uk 1 na 2.
Lanina wa Muyuka, mwanamke aliyekuwa mfanya kazi katika shamba maarufu la Bwana
Delamon, ametiwa tena kizuizini.
Pia alitumia lugh ya ushairi. Pia mwandishi ametuamia lugha ya ushairi katika uk 62.
Pia matumizi ya simu.Pia yamejitokeza katika tamthiliya hii ya Kilio cha Haki, pale ambapo
Shindo alipompigia simu kamishna Hunderson. Lengo ni kuonesha uhalisia wa kimazungumzo.
Uchanganyaji msimbo (code mixing); pia mwandishi wa KILIO CHA HAKI ametumia lugha ya
kuchanganya, kama vile Kingereza na Kiswahili, lengo lilikuwa kuonyesha katika matini
palikuwepo na watu tofauti kama vile wazungu na waswahili. Mfano katika uk 10.
Foolish baboons!
Kimbo: Yes…Sa……
MATUMIZI YA LUGHA
Lugha ni ufundi anaotumia mwandishi katika kuandika kazi yake. Ni sifa za kipekee mfano.
Misemo, methali tamathali za semi kama takriri na tashibiha.
NAHAU/MISEMO
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema Nahau ni misemo iliyojegwa kwa kutumia
maneno ya kawaida lakini huwa imesitiri maana tofauti iliyobeba maneno katika hali ya
kawaida.
Katika tamthiliya hii mwandishi ameipamba kazi yake kwa kutumia misemo na nahau kama
ifuavyo:-“Mhitaji ni mtumwa” uk 24. Msemo huu ulijitokeza pale ambapo kachero wa pili
alipomwambia Lanina anyenyekee kwa sababu inaonyesha kuwa unapokuwa na shida lazima
unyenyekee.
Msemo mwingine ulijitokeza pale mama yake Lanina alipokuwa anamwambia mwanawe.
“Mkosa chema haachi kuguna” uk 37. Pia aliendelea kusena “Jicho la hasidi lisimkumbe” uk 37
hapa mama Lanina alikuwa anamwombea mwanawe dua.
“Huyu ni punda tu asiyekuwa na fadhila!” uk 38 msemo huu ulitumiwa na Baba yake Lanina
akimtaka asimsalimie na wala asimwite Baba kwani si Baba yake kutokana na tabia yake.
METHALI
Ni misemo inayotumiwa kuelezea kitu kwa njia ya picha, na kwa ufupi ili itoe maadili au
maonyofulani, methali huwa na sehemu mbili saehemu ya kwana husemwa na mshauri na ya pili
hukamilishwa na mshauriwa. Humfanya msikilizajiawe katika hali ya kufikiri, kuchambua na
kupatanisha ukweli, na hali ili ajue maana ya ndani iliyokusudiwa.
Katika tamthiliya hii ya “KILIO CHA HAKI” mwandishi ameipamba na kuipendezeasha kazi
yake kwa kutumia methali mbalimbali. Mfano katika ukurasa wa 27” ametumia methali “Hasira
hasara” mwandishi ametumia methali hii pale Matovu na Tereki walipokuwa wakimshauri
Lanina akubali kurejea kazini. Hivyo methali hii katika jamii yetu, inatufundisha kuwa tufikiri
kuona ndipo tujue maamuzi.
Methali nyingine ni “Dalili ya mvua ni mawingu” uk 36 pale baba Lanina alipokuwa anaongea
na mama yake Lamina kuhusu mabadiliko ya Lanina na minong’ono ambayo inasemwa kijijini
kuhusu Lanina.
TASHIBIHI
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema tashibiha hutumika kulinganisha kitu kimoja
au zaidi kwa kutumia viunganishi kwa mfano. (Kama, mithili ya).
Mfano:- Nyinyi ni kama punda msiyojua fadhila. UK 22 alisema kachero wa kwanza kwa
Lanina pale walipomtia kizuizini.
Anajikunyata kama anayesikia baridi uk 28 hii ni sauti ya msimuliaji ilisikika kutoka nje
Nchi zetu ni kama jaa la bidhaa zinazowazidia uk 24, aliongea Lanina akiwambia
kachero wa kwanza na wa pili.
Kimya kama hayawani uk 76, Lanina alikuwa akijisemea mwenyewe. Hii ina maana
kuwa kunyamaza kama kayawani ni kama kuwa mwendawazimu au mtu
aliyechanganyikiwa na mambo.
TAKRIRI
Ni kujirudia kwa maneno au sauti. Katika tamthilia hii takriri zilizotumika ni kama ifuatayo
“Ndiyo ndiyo uk 16. Hii ina maana kuwa mwandishi alikuwa anakubaliana na jambo hilo
lakini kwa mashaka.
………….. na …………… nauk 16 na uk 17
Kufikiria! Kufikiria! Uk 19
Halafu! Halafu uk 29
La! La! La! Uk 22
Lamina! Lamina! Uk 29
Tafadhari Tafadhari uk 42
Twende! Twende! Nikakupeleke kwa shangazi yako akakufundishe kumtii bwana wako uk.
42.
Alisema baba Lanina akimueleza mkewe.
Haya sema ulilonalo! Sema basi, sema na mimi nisikilize sema! Uk 30
Mwengo aliongea akimwambia mkwewe Lanina.
“Yawache yachache Dewe yawache yachache”
yawache yachache”
Alizungumza musa uk 4
Lamina! Lamina!
Wakili alimuita Lanina uk 76
MDOKEZO
Ni kauli ambazo hazimalizii jambo au ni tamathali ambazo hudokeza kitu Fulani na kukiacha
bila kukimalizia au kukikamilisha kwa maana kwamba kinaweza kukamilishwa na mtu
mwingine kisanaa.
Mfano
SITIARI
Sitiari hulinganisha vitu au watu bila kutumia viunganishi. Hulinganisha vitu kama vinafanana
kabisa.
Katika riwaya hii mwandishi ameweza kuipamba kazi yake kwa kutumia sitiari mbalimbali.
Mfano:“Mimi ndiye simba” Uk 32 hapa baba yake lanina alikuwa na maana ya kuwa yeye ndiye
mkuu wa familia akiomgea kitu hakuna wa kumpinga.
Mfano “Huyu ni punda tu asiyejua fadhila Uk 38 hapa tumemuona baba Lanina alikuwa
akimwambia mwanawe Lanina. Akimaanisha mwanawe hana shukrani maana shukrani ya punda
ni mateke.
TASHIHISI
Ni kuvipa vitu uwezo wa kufanya jambo anbalo halina uwezo au sifa ya kufanya jambo tofauti
na uwezo wa kibinadamu.
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema ridaa ni misemo ambayo kuonyeshwa
kushangazwa kwa jambo fulani. Misemo hii huambatana na matumizi ya alama za mshangao
katika kukubali jambo, kuchukia au kuonyesha heshima maalumu.
Mfano:
WAHUSIKA
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema mwandishi Alamin Mazrui wa tamthilia ya
KILIO CHA HAKI amewatumia wahusika kwa kuwagawa katika makundi mbalimbali ambayo
ni wahusika wakuu, wahusika wasaidizi na wahusika mviringo.
MHUSIKA MKUU
Mhusika nkuu katika tamthilia yaKILIO CHA HAKIni Lanina. Alamini Mazrui alimtumia
Lanina kwa kutumia nadharia ya ufeministi. Lanina amekuwa mwanamke aliyepigania haki na
ukombozi wa mwanamke pamoja na kutetea maslahi ya wafanyakazi wenzake. Hivyo alisimama
kidete bila kukata tamaa katika kupigania haki pamoja na kuwa alipata mateso na manyanyaso
mbalimbali hadi kufikia hatua ya kuwekwa kizuizini.
Mfano
Katika ukurasa wa 14 anasema
Askari anampiga kofi na kusema wacha upuuzi wako huo. Haki! Haki unapigania kitu hata hujui
ukipewa utafanyia nini?
Wasifu mwingine wa Lanina ni mke wa Mwengo. Hii inadhihirika pale ampapo Mwengo
alipokuwa akiongea na Lanina.
Mimi ni mume wako ala!Umesahau? Kwa nini hunijibu? Kwa nini umenipuuza namna hii?
DELAMON
Huyu ni mhusika mkuu pia kwani ameonekana tangu mwanzo wa matukio katika tamthiliya hii
hadi mwisho. Hapa mwandishi ametumia nadharia ya ubada (ukoloni) akiwakilisha jinsi
wakoloni walivyo wagandamiza wafanyakazi wa kiafrika kiuchimi.
Hii imejitokeza katika ukurasa wa 13 pale ambapo Lanina anamjibu Delamon kwa hasira “…..
nyingi hamkuja hapa kwa manufaa/faida yetu…… mmekuja kwa maslahi yenu
wenyewe………… uk 13.
“Katika shamba la Delamon wakati wa mapunziko. Tereki, matuvu, Dewe, Mussa na mfanyakazi
mwingine wanatokeza wamevaa nguo za kazi. Uk 43.
WAHUSIKA WASAIDIZI
Mwandishi amewagawa wahusika wasidizi katika makundi mawili, ambayo ni wale wenye
msimamo wa nadharia ya Ki-Marx na wale wasaliti. Nadharia hii ya kimary huonyesha wahusika
wa kimaendeleo, pia huonyesha matumaini ya juu ya kizazi cha binadamu (tabaka fulani lina
kandamizwa lakini linaonyesha matumaini)
“Mussa (kwa hasira) “wasikilize wapumbavu hawa! Ati Lanina amechochea mgomo
Lanina, Dewe na Mussa walikuwa watu wenye msimamo, hawakukata tamaana waliendelea na
mapambo hadi mwisho katika uk 62 pale Lanina alivyokuwa anaonge na Mussa na Dewe.
“Ndugu zangu, ari yetu ndiyo mwokozi wetu, ari yetu lazima tuisujudie
Mhusika mwingine ni baba Lanina, amechorwa na mwandishi kama mfuasi wa mfumo dume na
kuona kuwa mwanamke hawezi kutetea haki wala kufanya mapinduzi, ukurasa wa 38.
“Mimi ndiye simba wa nyumba hii ningurumapo sitaki kuzisikia sauti zenu za kijinga hapa
(Akimgeukia Lanina)
Mimi si wale wanaume wengine unaochezeachezea. Mimi si kina Mwengo mimi ni dume kweli
kweli umesikia hivyo!
Mtu katili
Hafai kuigwa katika jamii
JUKWAA
Mussa na Dewe wanasoma taarifa tokea gazetini zinaeleza kuwa kamishina Hunderson
amemkamata Lanina wa Muyake kwa tuhuma ya mauaji ya watu watatu wenye shamba la bwana
Delamon.
Lanina anawajibu makachero kuwa Delamon na wenzake hawakuja kutunufaisha bali kunyonya
nchi zetu.
Lanina karudi nyumbani lakini amekutana na lawama za mume wake Bwana Mwengo kwa
kumuachia familia kwa muda mrefu. Hata hivyo walisamehana na kutaka waendelee
kushirikiana.
Lanina anakutana na wazazi wake kijijini, baba yake anamlaani na hata kupigwa yeye na mama
yake kwa sababu Lanina hafuati mila na desturi za kwao na mama yake ndiye aliyepewa
kumfunza.
Onyesho la Sita (uk 43-48)
Hapa wasaliti Matovu, Tereki naPelekha wanajifariji na kuwaona akina Mussa na Dewe na
Lanina kuwa ni wajinga, kwa kukataa ofay a Bw. Delamon.
Wasaliti hawa wana wanamshawishi Lanina arudi kazini kwa vile wamemhusiwa kuendesha
shughuli za siasa na mshahara unapanda juu kidogo. Lanina anakataa na kuwa fukuza nyumbani
kwake.
Lanina yupo kwenye kioski cha mzee Engeli. Mussa, Dewe na Lanina wanakutana kupeana
taarifa kuwa eti Delamon ameruhusu kuendesha shughuli za kisiasa na kuendeleza mapambano
ya kudai haki zao kazini.
Katika ofisi ya Bwana Delamon wamesikia Sauti za wafanyakazi walipoamua kuimba nyimbo za
kimapinduzi.
Hapa Lanina akiawa gerezani anakutana na Askari malaya,ambaye alimtongoza Lanina lakini
Lanina anamkatalia na kumpiga teke sehemu zake za siri, pia Lanina anaitwa na jaji ili kutoa
utetezi wake katika(uk 77).
MANDHARI
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasema mandhari ni sehemu au mahali ambapo kazi
ya fasihi hutendeka. Katika tamthiliya ya KILIO CHA HAKI mwandishi ametumia mandhari
tofauti tofauti kama vile shambani (kwa bwana Delamon) uk 43 mahamamani, kijijini (kwa baba
na mama wa Lanina) mtunzi ametumia mandhari hayo ili kuonyesha matendo mbalimbali
ambayo yalitumika kuibua dhamira mbalimbali.
MALEBA NA VIFAA
Kutokana na Gerald Njagi Matti. (2001). Anasemamaleba ni mavazi anayotumia msanii katika
Sanaa yake. Kalika kumpamba mhusika. Mavazi yaliyotumika katika tamthiliya hii ni pamoja
na:-
Khanga uk 39, mama alipojifuta machozi kwa kutumia khanga. Khanga katika tamthiliya hii ya
kilio chetu inawakilisha utamaduni wamavazi ya mwanamke wa Kitanzania.
VIFAA
Mfano wa kiko kilichotumiwa na bwana Delamon inaashiria tabia za wakoloni kuvuta kwa
kutumia kiko, (ukurasa wa 10).
Sigara ni kifaa kilichotumiwa na Lanina kuonyesha tabia ya mwanamke huyu jasiri kuwa ni
mvutaji sigara. Pingu nabundiki ni silahazilizotumiwa na wakoloni ili kuwatisha na
kuwagandamiza waafrika ili wawanyonye kwa urahisi (ukurasa wa 14).
TASWIRA NA ISHARA
I. ISHARA
Kutikisa kichwa, katika ishara hii tunaona Lanina akimkatalia Mwengo juu ya mawazo yake
potofu juu ya mkewake Lanina hii inapatikana uk 34. Pia mama yake Lanina alitikisa kichwa
kuonyesha kukubaliana na mumewe. Ishara hizi zinaonyesha matumizi mbalimbali ya viungo
vya mwili vya wahusika wake.
II. TASWIRA
KILIO CHA HAKI, inaonyesha mifadhaiko na manung’uniko yawafanyakazi wakidai haki zao
kama vile, mshara ndogo, mazingira mabovu ya kazi, na vifaa duni vya utendaji kazi.
Wanfanyakazi hii ni taswira iliyokuwa ikiwakilisha umma ulio kuwa ukionewa na kunyanyaswa
na bwana Delamon.
Picha ya jalada la KILIO CHA HAKIni ishara ya mwanamke anayedondosha machozi kwa kulia
kutokana na dhuluma na unyanyasaji anaofanyiwa na jamii yake.
Mwandishi ametumia lugha rahisi inayoeleweka yenye lugha ya kishairi, nyimbo na matumizi
mazuri ya wahusika waliobeba dhamira mbalimbali, hivyo kufanya kazi imvutie msomaji na
kuchangamsha hadhira. Kuna mfano wa shairi (uk 62).
JINA LA KITABU
Jina la kitabu linasadifu yaliyomo. KILIO CHA HAKI, kitaswira linaangalia matatizo na
manung’uniko yaliyokuwa yakiwakumba wafanyakazi katika shamba la bwana Delamon.
Matatizo hayo ni kama vile, ujira mdogo, kufanya kazi kwa muda mrefu, mazingira mabovu ya
kazi pamoja na vifaa hafifu vya utendaji kazi, pia ukosefu wa demokrasia.
Matatizo na manung’uniko hayo ni vilio vya haki ambayo viliwapelekea wawe na vilio kutafuta
ufumbuzi wa matatizo hayo au waweze kujikomboa kutoka kwenye mikono ya makaburu.
“uk 9. Wafanyakazi walivyokuwa wakitoa sauti”. “Nirudishe jasho langu, nirudishe damu yangu,
nirudishe haki yangu, nirudishe utu wangu” (uk 36-42 na uk 8).
REJEA