Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 5

Fonolojia na fonetiki za Kiswahili

Education (Meru University of Science and Technology)

Studocu is not sponsored or endorsed by any college or university


Downloaded by Akandwanaho Fagil (akandwanahofagil4@gmail.com)
SURA YA KWANZA
1:0 FONOLOJIA NA FONETIKI
1: 1 Fonolojia (Phonology)

Fonolojia ni nini?
Ni tawi mojawapo katika taaluma ya isimu linalojumuisha vipengele vya matamshi,
mkazo,kiimbo, lafudhi, toni, mfuatano wa sauti katika kuunda silabi, mfuatano wa sauti
katika kuunda mofimu, mfuatano wa mofimu katika kuunda maneno na tahajia / otografia
zake.
Fonolojia ni tawi la taaluma ya isimu linaloshughulikia uchunguzi, uchambuzi, na
uanishaji wa sauti pambanuzi katika lugha mahususi. Tawi hili hujishughulisha na
sauti ambazo hutumika kutofautisha maana za maneno katika lugha maalum /
mahususi. Fonolojia hujihusisha na sheria / kanuni zinazoandamana na utoaji wa sauti
pamoja na utumiaji wa sauti hizo pambanuzi.
Fonolojia imejikita katika lugha maalum ikichunguza namna binadamu
anavyotamka sauti na kuziunganisha ili kuleta maana katika lugha maalum inayohusika.

1:2 Fonetiki (Phonetics )


Ni taaluma inayoshughulika na sauti zinazotumika katika lugha mbalimbali duniani. Ni
tawi la isimu linaloshughulikia uchunguzi, uchambuzi wa taratibu zote zinazotumika au
zinazohusiana na utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikiaji na ufasiri wa sauti za lugha za
binadamu kwa ujumla.
Fonetiki huchunguza maumbo mbalimbali ya sauti zinazoweza kutolewa au
kuzalishwa na alasauti za binadamu. Tawi hili huchunguza namna maumbo hayo
yanavyotolewa, yanavyomfikia msikilizaji na jinsi yanavyofasiliwa au yanavyotafsiriwa
katika ubongo wa binadamu bila kujali sauti hizo zinatumika katika lugha ipi.
Fonetiki imegawanyika katika matawi manne katika uchunguzi wake wa sauti hizo
zinazotolewa na alasauti. Matawi hayo ndiyo yanayokamilisha kazi ya fonetiki katika
isimu.

1:2:0 Matawi ya Fonetiki


1:2:1 Fonetiki Matamshi (Articulatory Phonetics )
Hili ni tawi la isimu ambalo linashughulikia jinsi sauti mbalimbali za lugha
zinavyotamkwa kwa kutumia alasauti za lugha za binadamu. Tawi hili huchunguza
namna utamkaji wa sauti unavyofanyika na mahali pa kutamkia sauti hizo. Mchakato wa
tawi hili unaonekana kupitia jedwali la Alfabeti za Kifonetiki la Kimataifa
( International Phonetiki Alphabet <IPA>). Jedwali la konsonanti la alfabeti za
kifonetiki la kifamataifa lipo kama ifuatavyo. Thorne (1997).

Downloaded by Akandwanaho Fagil (akandwanahofagil4@gmail.com)


Kielelezo na: 1
Jedwali la Konsonanti la Alfabeti za Kifonetiki la Kimataifa

JINSI YA
MATAM MAHALI PA KUTAMKIA / MATAMSHI
SHI
Mido Mido- Meno,Uf Kipind Kaak Kaak Kaak Kida Mido- Mido- kishi Korom
m oMenomo izi- uka gumua gumua laini ka kaakaam kaakaam mo oe
Meno,Ba a -ufizi a aa Tong o gumu o laini
ada ufizi e-aak
aaK
laini

Nazali ɲ
m ɱ n ɳ
ŋ N
Vipasuo ɢ ʔ
p b t d ʈ ɖ k g q
c ɟ
Vikwamiz β θ ðs ẕ Ʒ j ʍ ʕ
i ɸ f v z s ʃ ç x ɤ χ ᴚ ħ h ɦ
Vizuio- ɥ
Kwamizi υ ɹ ɻ j ɰ
w
Vitambaz
a-
Kwamizi
ɺ ʙ
Vitambaz ɭ ʎ
a l
Vimadend
e
r ʀ
Vipigo ɾ ɽ ʀ
Ijektivu ῤ ť ḱ
Implosivu ɖ ɠ
ɓ
Vidoko- ͽ ʇ c
Kati
Kitambaz ʖ
a-Kidoko

1:2:2 Fonetiki Akustika / Fonetiki Mawimbisauti / Safirishi


(Acoustic Phonetics)
Ni tawi ambalo hushughulika zaidi na jinsi ya mawimbi ya sauti za lugha
yanavyoweza kusafirisha sauti hizo. Fonetiki Akustika hushughulikia jinsi mawimbi ya
sauti yanavyosafirisha sauti kutoka katika kinywa cha msemaji kwenda kwenye sikio la
msikilizaji na akili ya msikilizaji na kufanya masikilizano kuwepo.
Sauti husafirishwa na mawimbi kutoka kwa msemaji na kumfikia msikilizaji .
Massamba na wenzake (2004)

Downloaded by Akandwanaho Fagil (akandwanahofagil4@gmail.com)


1:2:3 Fonetiki Masikizi (Auditory Phonetics)
Ni tawi linaloshughulikia jinsi ya utambuzi wa sauti mbalimbali za lugha
unavyofanyika. Fonetiki Masikizi huonesha uhusiano uliopo kati ya sikio, neva masikizi
na ubongo. Huchunguza jinsi sikio, neva msikizi na ubongo vinavyohusiana na kufanya
kazi katika mchakato wa utambuzi wa sauti Thorne (1997).

Mifano na: 1
Sauti [b] [a] [r] [g]
[+kons ] [+sil ] [+ghun ] [+ghun ]
[+ghun ] [+ghun ] [+kont ] [+kor ]
[+mid ] [+chin ] [+mad ] [+kons ]
[-kont ] [+son ] [+ant ] [- kont ]

1:2: 4 Fonetiki Tibamatamshi / Majaribio (Experimental Phonetics)

Fonetiki tibamatamshi ni tawi linaloshughulikia matatizo yanayoambatana na


usemaji au utamkaji wa sauti na jinsi ya kuyatatua. Mfano tatizo la mtu kuzaliwa na paa
la kinywa / kaakaa lililogawanyika ambalo huathiri matamshi katika usemaji wake. Vile
vile watu wanaozaliwa na tatizo la mdomo juu kugawanyika hushindwa kutamka
vizuri sauti zinazotamkiwa katika midomo.
Lengo kuu la tawi hili ni kujaribu kuchunguza na kutafuta jinsi ya kuwasaidia watu
wenye matatizo hayo. Massamba na wenzake (2004)
1: 3 Usuli wa neno Fonetiki (Background of Phonetics)
Fonetiki ni sayansi ya lugha inayoshughulikia sauti za lugha mbalimbali zinazotolewa
na kinywa cha binadamu. Tunapozungumzia usuli wa fonetiki tuna maana ya usuli wa
jedwali la alfabeti za kifonetiki za kimataifa (International Phonetic Alphabet <IPA>).
Alfabeti za Kifonetiki za Kimataifa (AKK) ni wazo la kuunda alfabeti za kifonetiki
ambalo lilifikiwa baada ya kugundua kuwa alfabeti za lugha ya Kirumi zilizotumika
kurekodi lugha ya maandishi ya Kiingereza hazikukidhi au hazikuakisi uhalisia wa lugha
hiyo. Wanaisimu waliamua kuunda au kutengeneza kielelezo kingine cha alfabeti
kiitwacho Alfabeti za Kifonetiki za Kimataifa ambacho kinajaribu kuonesha kila
tofauti ya sauti hizo. Kielelezo hicho kilipendekezwa kwa mara ya kwanza na Otto
Jespersen kati ya mwaka 1860 – 1943. Mwaka 1886 mchakato wa kuandika kielelezo
hicho ulianza. Mwaka 1888 kielelezo cha kwanza cha Alfabeti za Kifonetiki za Kimataifa
(AKK) (International Phonetic Alphabet <IPA> ) kilichapishwa.
Lengo la mfumo au mchakato huo lilikuwa ni kuunda maumbo au viwakilishi vya
sauti ambavyo vinawakilisha sauti husika. Maumbo hayo ya sauti hutofautiana kutoka
sauti moja kwenda sauti nyingine, ambayo pia yataweza kutumika katika lugha yoyote ile
ambamo sauti husika inatumika. Thorne (1997)

Downloaded by Akandwanaho Fagil (akandwanahofagil4@gmail.com)


Alfabeti za Kifonetiki za Kimataifa zimeweza kutumika katika lugha mbalimbali, na
matumizi yake kupanuka mara nyingi sana hususani mwaka 1989 katika isimu ya lugha.
Hadi hivi sasa bado wanaisimu duniani kote wanatumia kielelezo hiki na ndicho
hukubalika zaidi katika miaka ya sasa katika isimu.
Kazi ya kielelezo hiki cha Alfabeti za Kifonetiki za Kimataifa au IPA ni:
a) Kupambanua kila sauti kulingana na jinsi inavyotamkwa
b) Kurekodi sauti za maneno kiuhalisia, kitu ambacho huwasaidia wanaisimu
kutofautisha maneno yanayoonekana katika tahajia ya kifonetiki lakini sauti
zinatofautiana
Maneno hupambanuliwa kifonetiki kwa kuyafungia katika mabano ya mraba ili
kuonesha kwamba mkazo uko kwenye sauti hizo na jinsi zinavyoundwa wakati wa
utamkaji.
Mifano na: 2
(i) Anacheza [anaʧεza] au [anačεza]
(ii) Ngugu [ndugu ]
(iii) Ghala [ɤala ]
(iv) Dawati [dawati ]

Fonetiki kama taaluma ya sayansi inayochunguza namna ya sauti zinavyoweza


kuzalishwa kusafirishwa na jinsi zinavyoweza kufasiliwa ama kutafsiriwa kwa
kutegemea alasauti za binadamu ambazo ndizo huzalisha sauti hizo. Alasauti hizo ni
midomo, meno, ulimi, kaakaa gumu kaakaa laini, ufizi, koromeo, kidaka tonge
nakadhalika.

1:4 Alasauti za Lugha.(Speech Organs)

Alasauti za lugha ni viungo mbalimbali maalum vya mwili wa binadamu. Viungo hivi
ni muhimu sana katika sayansi ya lugha hususani katika tawi la fonetiki na fonolojia.
Viungo hivi hutumika kuunda au kuzalisha sauti mbalimbali ambazo hushughulikiwa
katika tawi hili la fonetiki katika isimu ya lugha. Massamba na wenzake (2004)
Alasauti hizi ni mapafu ambayo hufanya kazi ya kuvuta hewa ndani na kutoa nje ya
kifua cha binadamu kupitia katika chemba ya kinywa au chemba ya pua. Umio ,koromeo
ni aina nyingine ya alasauti ambayo huwa na namna fulani ya kambakamba ya nyama
laini zinazoitwa nyuzisauti. Nyuzisauti zina uwazi katikati unaoruhusu hewa kutoka nje
ya kifua cha binadamu na kuingia ndani ya mapafu ya binadamu. Nyuzisauti zinapokuwa
zimeachana hewa hupita kwa urahisi kwenda nje na hivyo kusababisha sauti
zinazotamkwa kutokuwa na mtimbwiliko mfano sauti [t],[p] nakadhalika. Lakini
zinapokuwa zimekaribiana au zimegusana hewa kutoka mapafuni hulazimika
kuzisukuma ili kuziachanisha na kusababisha sauti zinazotamkwa kuwa na mtimbwiliko
mfano sauti [r], [b] nakadhalika.
Alasauti nyingine ni kinywa ambacho kinajumuisha ulimi, kaakaa gumu, kaakaa
laini, ufizi, na meno. Ulimi una sehemu kuu tatu; sehemu ya mbele ambayo inajumuisha
incha ya ulimi ambayo hukutana na alasauti ama viungo vingine kama meno, ufizi,kaakaa
gumu,kaakaa laini ili kutamka sauti [t], [d], [θ], [i] na kadhalika. Kiwiliwili au bapa la

Downloaded by Akandwanaho Fagil (akandwanahofagil4@gmail.com)

You might also like