Download as doc, pdf, or txt
Download as doc, pdf, or txt
You are on page 1of 2

Sintaksia na Semantiki kama Mihimili katika Utunzi wa kazi za Fasihi

Winne Mtega
Mtegawinnie19@gmail.com

Sintaksia ni nini?

Sintaksia ni taaluma inayohusu namna maneno yanavyoungana kuunda sentensi na vilevile


sharia ambavyo husimamia uundaji wa sentensi (Richard, 1995).

Aidha, Habwe na Karanja (2004) wanaeleza kuwa sintaksia kuwa utanzu wa isimu
unaoshungulikia muundo wa sentensi na elementi zingine zinazounda sentensi kategoria za
maneno, vikundi ann vishazi.

 Sintaksia ni utanzu wa sarufi au kiwango cha isimu ambacho hujishungulisha na


uchanganuzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi ikiwa ni pamoja na uhusiano na
vipashio vyake.
 Huzingatia sharia ambavyo hufuatwa katika kupanga maneno ya lugha katika mfuatano
unaokubalika na kuleta maana. Isitoshe huchunguza uhusiano wa maneno katika tungo na
kubainisha jinsi yanavyoweza kumilikina kutawala zingine.
 Kwa mintarafu tunapata uhusiano uliopo baina ya isimu na sintaksia vilevile isimu na
mantiki , tunaishia kuwa sentensi ni isimu nayo sinyaksia uchunguza jinsi maneno
yanavyounganishwa ili kuunda tungo zenye maana katika lugha ya mwanadamu kwaivyo
sintaksia inakuwa kiwango cha isimu.
 Mantiki inatubainishia kuwa isimu ni uchunguzi wa lugha ya mwanadamu kisayansi.
 kuwa sarufi ni taaluma inayojumuisha viwango vyote vya uchanguzi wa lugha mahususi
yaani, fonolojia,mofolojia, sintaksia na semantiki basi inafuatia kuwa sintaksia ni sehemu
ya sarufi.

MAWANDA YA KISINTAKSIA

 Katika kutekeleza majukumu ya kuchanganua tungo, sintaksia hujishungulisha na


maswala yafuatayo :
 Uainishaji wa kategoria za maneno na viambajengo vingine vya sentensi
 Uchunguzi wa mpangilio wa maneno katika sentensi
 Uchanganuzi wa miundo ya sentensi.
 Uchambuzi wa nadharia na sharia zinazotawala miundo ya sentensi.
 Uchunguzi na uhusiano wa maneno na vipashio vingine vya sentensi.

Semantiki
Semantiki hujikita kuchunguza lugha ya kitamathali na miundo ya lugha ambayo ni sifa muhimu
ya kuchunguza matini ya kifasihi tunapotumia nadharia ya Umitindo. Ni jinsi matumizi ya lugha
yanavyoathiri maana kwa njia fulani. Ukiushi wa aina hii unahusu matumizi ya maneno na jinsi
maana hiyo inavyofasiriwa katika hali za kawaida. Mara nyingi huhusisha matumizi ya maneno

Huchunguza maana kwa njia ambazo si za kawaida kimaana. Darajia hii hujikita katika matumizi
ya tamathali za usemi: Mbinu za kinaya, kejeli, mbinu ya kweli-kinzani (paradoksi,) sitiari,
balagha, ndoto, majazi, jazanda , taswira, taharuki, kisengere nyuma, kisengere mbele, takriri,
kejeli, chuku, sadfa, tashhisi, tashbihi

Vilevile, huhusisha matumizi ya jazanda, yaani lugha ya picha aidha za kimaelezo au za kiishara.
Maelezo haya ni kulingana na; (Leech na Short 2007:101, Wamitila 2008:518).
• tawi la semantiki kwa sababu ndilo tawi huchunguza lugha katika kiwango cha maana.
Huchunguza maana ya maneno yanayopatikana katika lugha husika, iwe ya kifasihi au ya
kiisimu. Pia tulizingatia viwango vingine viwili vya ukiushi ambavyo ni: Kiwango cha
maandishi/grafolojia na kiwango cha umbo.

• Kiwango hiki kilitufaa sana kwa sababu kama tulivyoeleza, mtindo ni jinsi lugha
ilivyotumiwa na kuathiri maana kama inavyotumika kwa njia ya kawaida.

• Kwa muhtasari mtindo unaweza kuelezwa kama mazoea ya matumizi ya lugha ya mtu au
jamii-lugha fulani. Nayo nadharia ya Umitindo hujihusisha na uhakiki na fasiri ya matini
katika mtazomo wa Kiisimu kama taaluma ambao una uhusiano wa karibu na mtazamo
wa Kifasihi.

You might also like