Professional Documents
Culture Documents
Notes Kiswahili Iiila
Notes Kiswahili Iiila
Notes Kiswahili Iiila
1. VIRAI VIVUMISHI
Kirai kivumishi ni kundi la maneno ambalo neno laken kuu ni kivumishi. Ifahamike
kwamba,vivumishi hukaa pembeni ya nomino ama kiwakilishi cha nomino ili
kuvifafanua.
Mifano :
-Duka lake kubwa limefungwa.
-Mashirika mengi ya Serikali yatabinafisishwa.
-watoto wake wengi walisajiriwa katika kiwanda cha chumvi
-Yule mrefu sana kuliko wengine ndiye anakimbia sana.
- Vile vyote vipya vinahitajika hapa.
-shule nyingi za kibinafsi zimefungwa na wizara ya Elimu
2. VIRAI VIELEZI
Mifano :
-Ni vizuri kuyasoma maswali vizuri sana ili kuyaelewa.
-Sherehe zilikamilika (zilimalizika) usiku wa manane.
-Watu hawa wamefika leo asubuhi.
-Tutakutana huko sokoni jioni.
N.k
3. VIRAI VIHUSISHI
4. VIRAI VIUNGANISHI
Mifano :
-Amechelewa shuleni kwa sababu anaishi mbali sana.
-Baba na mama pamoja na mjomba wangu wanaishi Umarekani.
-sili wala sinywi chochote kile.
-Umeharibu tena vitabu vyangu ?
N.k.
Somo la XIV. FASIHI
Fasihi ni sanaa inayotumia lugha kwa kuwasilisha ujumbe kwa hadhira (msomaji au jamii
inayonuiwa). Fasihi hutumia lugha kwa kufafanua tabia za watu na athari zake.
Kuna tofauti kati ya fasihi na sanaa. Fashi, hutumia lugha kwa kuwasilisha ujumbe.
Sana nayo hutumia vifaa kwa kuwasilisha ujumbe.
RIWAYA
Katika riwaya,
1. VINYUME (Antonimu)
Mifano :
Neno Kinyume
Msichana Mvulana
Mwanaume Mwanamke
Mjomba Shangazi
Jogoo Koo
Mfalme Malikia
Nyanya/bibi Babu
Furaha Huzuni
Ubaya Uzuri/Wema
Ukubwa Udogo
Faida Hasara
Pata Kosa
Choma Chomoa
Funga Fungua
Kavu Nyevu
Kaa Simama
Chimba Chimbua
Tiifu Kaidi
Safi Chafu
2. VISAWE (Sinonimu)
Haya ni maneno yanawakilisha dhana moja. Visawe huwa na maana sawa au maana
ambayo inakaribiana.
Sinonimu ni muhima katika kuboresha uandishi wa insha kwani hukinga kurudiarudia
neno lile lile mara nyingi.
Mifano ya visawe/sinonimu :
Kizunguzungu = kizunzi
Dalili = ishara
Makini = uangalifu
Wajimu = jukumu
Wasiwasi = shaka. Wahka, tewengu
Shida = tatizo
Hasira = hamaki, ghadhabu
Aibu = soni, haya, tayahuri, izara
Goigoi = mzembe, mvivu, mpetevu
Bendera = beramu
Matata = fujo, ghasia, sokomoko, ugomvi, kimondo
Chelewa = kawia, limatia, ahirika
Gereza = jela, kizimba
Fikiri = waza, dhani, tafakari
Busara = hekima, akili, tabasuri
Mtu = mja, mwanadamu,adinasi
Mwizi = pwangu, mdokozi, pwanguzi
Rika = umri, hirimu
Ugali = sima
Udhi = kirihi
Yapo maneno yenye maana nyingi ambazo zinahusiana na zingine ambazo hazina
uhusiano.
Mifano :
Rai :
-maoni
-sihi
Unga :
-leta pamoja
-kitu kilichosagwa
-tia viungo ndani ya chakula ili kuboresha ladha
Sita :
-namba(ri)
-babaika
Kaa :
-keti
-kipande cha kuni kilichochomwa
Vua :
-toa vazi(nguo,viatu,n.k)
-toa samaki majini
-okoa, toa kwenye matatizo
Chungu :
-isiyo tamu
-mdudu mdogo mweusi
-kifaa cha udongo cha kupikia(pot)
Ua :
-toa uhai wa kiumbe
-ugwe(kamba au waya) unaozunguka nyumba(enclos)
-sehemu ya mmea unaozaa(une fleur)
Kata :
-kifaa cha kutekea maji(ingata)
-tenganisha kitu(couper)
-sehemu ndogo kuliko tarafa(quartier)
Taka :
-hitaji,tamani
-takataka(uchafu)
Tupa :
-kifaa cha kunolea visu
-puuza
-rusha mbali
Jaa :
-furika
-mahali pa kutupa takataka(jalala)
Kinga :
-zuia
-jambo au dawa ya kujikinga na madhara
-kipande cha kuni chenye moto au kilichoungua
Nyanya :
-bibi mzaa mama/babu
-tunda la mnyanya ambalo hutumika kama kiungo.
4. VITATE
Vitate ni maneno ambayo hutatiza wakati wa kuyatamka. Maneno hayo, kwa kawaida
huundwa kwa sauti tatanishi. Sauti tatanishi hukaribiana kimatamshi.
Mifano :
Mifano :
Fahamu vema(F.V) : Vitenzi vinavyoishia kwa irabu –u, -i, -e havichukui kiambishi cha
ukanushi –i.
Mifano :
Mtoto anaharibu nepi => mtoto haharibu nepi
Baba anasamehe mama => baba hasamehe mama
Ule upepo unarudi tena => ule upepo haurudi tena
2. Hali timilifu
Hali timilifu au wakati mtimilifu unaonyesha na kiambishi (njeo ya wakati) –me- katika
kitenzi. Kiambishi hicho hubadiliki –ja- katika hali kanushi.
Mifano :
Barabara imefungwa hivi punde => barabara haijafungwa hivi punge
Nimesahau funguo zangu => sijasahau funguo zangu
Mti umeanguka leo asubuhi => mti haujaanguka leo asububi
3. Wakati uliopita
Kiambishi ama njeo ya wakati –li- ndicho kinachotambulisha . Kiambishi hicho hugeuka na
kuwa –ku- katika hali kanushi.
Mifano :
Nilimletea pesa zako jana => sikumletea pesa zake jana
Magari haya yaligongana wiki jana => magari haya hayakugongana wiki jana
Viatu vyake vilichanika sana => viatu vyake havikuchanika sana
4. Wakati ujao
Wakati ujao unaonyesha na njeo –ta-. Katika hali kanushi ta hubaki kuwa –ta-.
Mifano :
5. Hali ya mazoea
Hali ya mozea huonyeshwa na kiambishi ama silabi hu- mwanzoni mwa kitenzi.
Ukanushi wake hufanywa kama ule wa wakati wa sasa.
Mifano :
Wanafunzi huvaa sare za shule => wanafunzi hawavai sare za shule
Nguo za watoto huchafuka sana => nguo za watoto hazichafuki sana
Hali zingine zinastahili kukanushwa :
Hali ya kuamuru
Mifano :
Angalieni picha hiyo kwa makini ! => msiangalie picha hiyo kwa makini !
Ondoka hapa sasa hivi ! => Usiondoke hapa sasa hivi !
Mifano :
Watoto wanakula mikate => watoto hawali mikate
Wamekunywa maji machafu => hawajanywa maji machafu
Mjomba atakuja kesho asubuhi => mjomba hatakuja kesho
Ng’ombe walikula majani mengi jana => ng’ombe hawakula majani mengi jana.
Vitenzi-jina
Mifano :
Kuchelewa kwake shuleni kulitushangaza sana => kuchelewa kwake shuleni
hakutushangaza sana.
Kulima kunanufaisha => kulima hakunufaishi
- Kiini cha insha : hii ni sehemu kuu ya insha. Mawazo hupangwa kwa mtiririko sahihi.
Insha ya wasifu : hueleza sifa za watu, na vitu kama vile wanyama, majengo, milima, mahali
fulani, n.k
Insha ya kisanaa : huwa na lugha yenye mvuto na misemo kama vile nahau, methali,
tamthilia za semi
Insha ya hoja : huletea mawazo ya aina fulani na kupinga mawazo mengine kwa uthibitisho
ulio dhahiri.
Kumbusho :
Sentensi ni utungo au kundi la maneno ambalo hueleza dhana (maana) iliyokamiliko. Sentensi
ni kundi la maneno ambalo lina muundo wa kiima na kiarifu na ambalo huleta maana kamili.
1. Sentensi za taarifa : sentensi hizi hutoa taarifa tena huishia kwa nukta.
Mifano :
Dada yangu ameumwa maleria.
Darasa letu lina wanafunzi wachache kuliko mengine.
Tunasoma Kiswahili kwa vipindi vinne.
Mama yangu hawezi kuosha vyombo.
2. Sentensi ulizi : hizi huuliza swali kuhusu jambo fulani. na huishia na alama ya kuuliza.
Mifano :
-Watu hawa wanahitaji nini ?
-Miti hiyi iliangukaje ?
-Kwa nini unachelewa kila asubuhi kazini ?
3. Sentensi agizi : sentensi agizi hutoa amri na huishia kwa alama ya hisi (alama ya
kushangaa.
Mifano :
-Nenda taratibu usianguke !
-Kaeni wawili wawili !
-Ondoa uchafu huo haraka haraka !
-Andika maswali hayo katika madaftari yenu
4. Sentensi hisihi : Hizi ni sentensi ambazo huonyesha hisia kama vile huzuni, uchukivu,
mshangao, n.k
Mifano :
-Ajabu ! Tarafa nzima kukosa zahanati !
-Lo ! Bikizee kaendesha gari kweli !
5. Sentensi za masharti : katika sentensi hizi, kuna masharti. Yaani jambo fulani ni lazima
litimizwe ili mafanikio yapatikane.
Mifano :
-Kama mvua ingenyesha mapema mavuno yangekuwa mengi
-Ningekuwa na pesa ningenunua gari la kifahari.
-Ukifika mapema tutaondoka pamoja.
Kumbusho :