Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 4

KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA

DAYOSISI YA KUSINI

JIMBO LA CHIMALA – USHARIKA WA RUIWA

MTAA WA MOTOMOTO

IBADA YA TAREHE 19 MEI 2024


SIKU YA KUKUMBUKA KUSHUKA KWA ROHO
MTAKATIFU (PENTEKOSTE)
WAZO LA WIKI: ROHO MTAKATIFU NGUVU
YETU
ZABURI 143:1-12; EFESO 1:13-14
SOMO LA MAHUBIRI: YOHANA 20:19-23
WIMBO: TMW 136

Tofauti na injili nyingine, injili ya Yohana


inaeleza habari za kufufuka kwa Yesu na jinsi
alivyoendelea kujidhihirisha kuwa yupo hai. Katika
Sura hii ya 20:1-10 ni habari za kufufuka kwa Yesu.
Yohana 20:11-18 ni habari za Yesu kumtokea Mariamu
Magdalena. Ambaye anaonekana kuwa ni shuhuda
wa kwanza kumwona Yesu mara tu baada ya
kufufuka! Yohana 20:19-23 ambalo ndilo somo letu la
mahubiri, ni habari za Yesu kuwatokea wanafunzi
wake 10: Yuda Iskariote akiwa alishajinyonga, na
Thomaso hatuambiwi alikwenda wapi. Yohana 20: 24-
25 ni habari za Thomaso ambaye hakuwepo wakati
Yesu anawatokea wanafunzi wengine anarudi na
kusimuliwa kuwa Yesu amewatokea, alikataa na
kusema hataamini mpaka aguse maeneo
yaliyoumizwa wakati akiwa msalabani. Hayo yote
yalitokea siku ya kwanza ya juma, yaani Jumapili.

Yohana 20:26-29, siku nane baadaye Yesu


aliwatokea wanafunzi wake na Thomaso akiwepo.
Hapa Yesu alimpa Thomaso fursa ya kwenda kugusa
makovu ambayo alisema angeamini ikiwa atagusa.
Lakini Thomaso alikataa na kudhihirisha kuwa
ameamini. Na Yohana 20:30-31 ni jumlisho juu ya
sababu au lengo la kuandikwa kwa injili ya Yohana,
na lengo kuu likiwa ni kusisitiza juu ya Uungu wa
Yesu.

Katika somo letu la mahubiri tulilopewa


kutafakari siku ya leo, tunapata habari za Yesu
kuwatokea wanafunzi 10: Yuda Iskariote
alishajinyonga, na Thomaso hatuambiwi alikwenda
wapi. Tukio hili lilitokea siku ile ile ya kufufuka kwa
Yesu, jioni wanafunzi wakiwa wamejifungia kwa hofu
ya Wayahudi kwamba baada ya kusulibiwa kwa Yesu
wangeendelea kuwatafuta wanafunzi wake. Yesu
aliwatokea chumbani humo ingawa milango ilikuwa
imefungwa. Jambo hili liliwashtua sana wakifikiri
kwamba walio na pepe aliyeweza kupita ukutani,
lakini Yesu aliwatuliza hofu yao baada ya
kuwaonesha mikono yake na ubavu wake. Kisha
tunaona Yesu akiwakabidhi wanafunzi wake huduma
ya kupeleka ujumbe wake kwa mataifa yote. Yaani
baada ya kupokea roho Mtakatifu wangekuwa
wajumbe wake duniani kote.

Wapendwa, Siku hii ya kwanza ya Juma, siku


ya kufufuka kwa Yesu ni siku ambayo kanisa lilipewa
uvuvio wa Roho Mtakatifu. Yesu aliahidi kuwa akija
huyo atawafundisha, atawakumbusha sio tu maneno
bali hata matendo ya Yesu. Na leo ni sikukuu ya
Pentekoste, siku ya kukumbuka kushuka kwa Roho
Mtakatifu. Pentekoste ya mwaka jana (28/05/2023)
tulitafakari juu ya Roho Mtakatifu msaada wetu.
Mwaka huu wazo tulilopewa, linatuongoza
kumtazama Roho Mtakatifu kama nguvu yetu.
Matendo ya Mitume 1:8 Lakini mtapokea nguvu
akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu. Bila
shaka huu ni upako wa utumishi unaokuja juu yetu.
Maana yake bila Roho Mtakatifu, hatuna nguvu za
kufanya huduma ambayo tumepewa. Efeso 3:20 Kwa
sababu ya nguvu ya Roho Mtakatifu ndani yetu
inamfanya Mungu afanye mambo makubwa kuliko
tuombayo, na tuwazayo.

Rumi 8:26 Roho Mtakatifu ndani yetu


anatuwezesha kuomba kama atakavyo Mungu. Roho
Mtakatifu ndani yetu anatupa nguvu ya kuishi maisha
matakatifu (Rumi 8:8-9, 14). Hutushuhudia kuwa sisi
ni Watoto wa Mungu (Rumi 8:16). Roho Mtakatifu
ndani yetu ni msaidizi (Yohana 16:7). Anatupa nguvu
ya kutambua dhambi (Yohana 16:8). Roho Mtakatifu
juu yetu ni kwa ajili ya utumishi, kudhihirisha uweza
wa Mungu (Mdo 1:8).

Wapendwa; ni jambo la kushangaza nyakati za


leo, yapo mafundisho potofu ya kutaka Roho
Mtakatifu aonekane kama nguvu ya kummiliki, na
kumweka katika vitu na vitu hivyo kusimama badala
yake, mfano maji ya upako, mafuta ya upako, chumvi
ya upako, mchanga wa upako. Hivi ni vitu ambavyo
havitakiwi kuchukua nafasi ya Roho Mtakatifu. Na
kwa bahati mbaya mahali pengine vitu hivi vinauzwa.
Watu wamenunua na vikachukua nafasi ya Yesu au
Roho Mtakatifu.

Kwahiyo wapendwa; ni muhimu kuwa


tunapokumbuka kushuka kwa Roho Mtakatifu,
tukumbuke kumwomba Mungu atufumbue macho ili
tutambue kweli yake na hatimaye tuishi katika kweli
hiyo. Mungu atubariki. Amen

Mchg Wito Kinyamagoha

KIONGOZI WA USHARIKA WA RUIWA

You might also like