Professional Documents
Culture Documents
Maswali Ya Mapambazuko Ya Machweo
Maswali Ya Mapambazuko Ya Machweo
Maswali Ya Mapambazuko Ya Machweo
Swali 1
Kifo cha Suluhu maswali na majibu
...iwapo penzi hili litatia doa,basi nirudishie mfuko huu kama ishara ya kulitupa penzi langu
kama jongoo na mti wake..."
Majibu
"...iwapo penzi hili litatia doa, basi nirudishie mfuko huu kama ishara ya kulitupa penzi langu
kama )ongoo na mti wake...
'Ni muasherati - japo ana mke ana wapenzi wa kando kama Abigael.
'Ni katili alifikiria namna ya kumuangamiza mkewe abaki na Abigael.
'Ni msaliti - anaisaliti familia yake kwa kuitelekeza.
.Ni mlezi mbaya- anamwachia mkewe Bi. Suluhu mzigo wa kuwalea
watoto wao na kumwambia ni wake pekee.
.Ni kiongozi mbaya - haleti maendeleo katika eneobunge lake kw alitumia
pesa za umma kuwalipa mabinti wa Chuo kikuu kwa kula uroda nao.
d. EIeza umuhimu wa msemewa wa hadithi hii katika kujenga ploti. (alam 6)
Msemewa ni Abigael.
Kupitia kwa Abigael tunaonyeshwa namna Bw. Suluhu alivyokuwa
ameoza kitabia kwa kula uroda na mabinti wa Chuo kikuu.
Kupitia kwa Abigael tunajua kuwa Bwana Suluhu alikuwa tajiri mwenye
mali na pesa nyingi zilizosababisha utovu wa amani kwa mkewe.
Kupitia kwa Abigael kuisoma barua ya Bi. Suluhu tunajua kuwa Bwana
Suluhu alikuwa ameitelekeza familia yake na kumtwika Bi. Suluhu mzigo
wa kuwalea wanawe.
Kupitia kwa barua aliyoisoma Abigael, tunajua kuwa Bwana Suluhu
alinyakua shamba la mamake Abigael na kumuua.
Kupitia kwa Abigael kuisoma barua ya Bi. Suluhu kwa bwanake tunajua
Suluhu alikuwa na nakama.
KupitiakwaAbigael tunaonyeshwabaadhiyamatatizoyanayowakumba
wanafunzi wa Chuo kikuu kama ukosefu wa chakula, uozo wa jamii,
utegemezi n.k.
Swali 2
Sabina maswali na majibu
Swala la elimu limepewa kipaumbele katika hadithi ya Sabina. Jadili (alama 20)
Majibu
Swali 3
Fadhila za Punda maswali na majibu
“Isije ikawa mwenye nyumba kuja na yeye mpangaji akachelewa kumfungulia mlango;
itakuwa balaa bin beluwa”
i. Eleza muktadha wa dondoo hili (ala 4)
ii. Jadili umuhimu wa mwenye nyumba anayerejelea (ala 6)
iii. Maisha yalikuwa balaa bin beluwa kwa mpangaji. Thibitisha ( ala 10)
Majibu
“Isije Ikawa mwenye nyumba kuja na yeye mpangaji akachelewa kumfungulia mpangaji
itakuwa balaa bin beluwa.”
Swali 4
Msiba wa Kujitakia Maswali na Majibu
Kwa muda mrefu, Machoka na Zuhura walikuwa kama fahali wawili hawakai katika
zizi moja. Kisa na maana, ni wafuasi wa watu wawili tofauti. Leo hii kinachowaleta
pamoja Machoka na Zuhura ni udhikinifu, hali ngumu ya maisha, mfumuko wa bei za
bidhaa muhimu na kutozwa ushuru wa kiwango cha juu na serikali hiyo hiyo ya ‘watu
wao’. Zuhura alisuta nafsi yake.
Alikuwa akiitazamia nchi nzuri na maisha bora baada ya uchaguzi. Alitazamia ‘watu
wake’ wangezitimiza ahadi walizozitoa wakati wa kampeni zao. Leo hii imebakia
kujuta. Kujuta ghya ya kujuta! Tayari alikuwa amekwishafanya kosa. Kosa ambalo
alifahamu lilikuwa la kujitakia. Ulikuwa mwiba wa kujidunga usiokuwa na kilio wala
kuambiwa pole. Maji yalikuwa yashamwagika, katu hayangeweza kuzoleka…”
Chambua maudhui katika dondoo hili. (ala 12)
b. Eleza sababu nne zinazochangia jimbo la Matopeni kutoshuhudia maendeleo ya
kisiasa tangu nchi kupata uhuru . (ala 8)
Majibu
Swali 5
Msiba wa Kujitakia Maswali na Majibu
Majibu
a.
i. Takriri - watu, wapiga kura.
ii. Nidaa/siyahi - hawajui leo wala kesho!
iii. Tashbihi - Maisha ya Wanamatopeni yalikuwa kama mchezo wa karata.
iv. Msemo - asubuhi ya majogoo.
v. Mbinu rejeshi - Zuhura anakumbuka namna yeye na wenzake walivyotunga
foleni ndefu.
vi. Methali - Wajinga ndio waliwao.
mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.
vii. Jazanda - Mzigo mzito wa maisha. (zozote 6 x 1 =6)
b.
i. Maisha ya udhikifu
ii. Mfumuko wa bei
iii. Kutozwa ushuru wa kiwango cha juu na serikali.
iv. Uamuzi wa mpiga kura hauheshimiwi.
v. Kupewa mishahara duni.
vi. Mishahara inachelewa kulipwa
vii. Wanatawaliwa na viongozi wasio na sera bora.
viii. Shughuli za uchaguzi zinaendeshwa kwa njia isiyo huru wa haki.
ix. Ndoto na nia za vijana zimebanwa, zikafinywa na kuzimwa.
x. Njaa - Machoka hajatia chochote kinywani tangu asubuhi kiasi matumbo yake
kushindwa kuhimili makali ya njaa.
xi. Ukosefu wa ajira - Machoka anatafuta kibarua mchana kutwa bila mafanikio.
xii. Ukabila – Zuhura anampigia kura Sugu Junior kwa sababu ni wa kabila lao.
xiii. Viongozi waliochaguliwa hawawatimizii raia ahadi walizotoa.
xiv. Ufisadi - wapiga kura wanahongwa kwa kupewa khanga, sukari, unga wa
sima, mafuta na visenti vya kununua tembo.
(zozote 7 x 2 = 14)
Swali 6
Fadhila za Punda Maswali na Majibu
. “Katika hali ile ya uchungu, kilio na mtanziko wa mawazo, akaiona simu yake imeanguka
chini ya kitanda….. Haidhuru hata kama atamuunga mkono mwanawe.”
Majibu
i. Msemaji ni mwandishi.
Anayerejelewa ni Lilia
Mahali ni nyumbani kwa Luka/Lilia.
Ni baada ya kupigwa na mumewe kwa kumripoti katika kituo cha polisi.
(alama 4)
ii. Taswira (hisi) - hali ya uchungu/ kilio /mtanziko
Nahau/msemo - unga mkono (alama 2)
iii. Sifa za Lilia
Mwenye mapenzi ya dhati - anampenda mumewe
Ni mtiifu - anawacha kazi baada ya kushauriwa na mumewe.
Ni mwaminifu - mbele ya mumewe
Ni mwenye heshima - anamwita mama mkwe kwa heshima.
Ni mwenye huruma - anamtetea mumewe kupewa ufadhili.
Mtulivu - hapendi ugomvi.
Mwenye bidii - anasoma hadi chuo.
(za kwanza 4 x 1 =4)
iv. Taasubi ya kiume
Luka anampiga mkewe Lilia kwa ngumi, teke, kofi na hata kumfokea.
Baada ya kuanza uzinzi na hawara zake, Luka anakuwa mkali kwa mkewe.
Luka anashinikiza Lilia kuacha kazi kwa madai kuwa anamhitaji kudhibiti
fedha za kanisa.
Lilia hana usemi nyumbani mbele ya Luka.
Luka anampuuza Lilia anapomshauri asiingilie siasa.
Luka analiuza kanisa lao bila kumshauri wala kumwuliza mkewe Lilia.
Luka kurithi mali ya babake Lilia badala ya bintiye (Lilia)
Luka haoni umuhimu wa kuandamana na mkewe; anamwacha kijijini.
Luka kutaka miadi kabla ya kutembelewa na mkewe.
Wanawake hawafai kuwastaki waume zao. Lilia anahofia kujulikana kwamba
alikuwa na nia ya kumshtaki mumewe.
Luka kuwa na hawara. Kitendo hiki kinamkosesha Lilia hadhi yake katika
ndoa.
(zozote 5 x 2 = 10)
Swali 7
Fadhila za Punda Maswali na Majibu
“Yu wapi kirukanjia wako? Wajua yuko wapi? Uliacha mbachao kwa msala upitao.
Atakutunza nani, maana kwako fadhila za punda ni mashuzi!”
Majibu
“Yu wapi kirukanjia wako? Wajua yuko wapi? Uliacha mbachao kwa msala upitao.
Atakutunza nani, maana kwako fadhila za punda ni mashuzi!”
Swali 8
Huku ukirejelea hadithi zifuatazo tano jadili maudhui ya migogoro kwa kutoa mifano
maridhawa. (alama 20)
a. Fadhila za punda
b. Msiba wa kujitakia
c. Mapambazuko ya machweo
d. Harubu ya maisha
Majibu
Huku ukirejelea hadithi zozote tano jadili maudhui ya migogoro kwa kutoa mifano
maridhawa.
a. Fadhila za punda
Lilia na Luka wana mgogoro unaosababisha vita k.m anapojitazama
kwenye kioo anaona kovu shavuni na donda.
Mapenzi ya Lilia na Luka yanaleta mgogoro kati ya Lilia na babake-
hapendi uhusiano ule.
Kuna mgogoro wa kinafsia kwa babake Lilia anayemshuku Luka kuwa
na uhusiano na mwanawe Lilia.
Luka kumvamia mkewe na kumvuta nywele kumwelekeza kwenye
chumba cha kulala, ambapo anampiga ngumi na mateke.
Luka anamtawisha Lilia na hata kumlazimisha kuandamana naye
kwenye kampeni na hii inawafanya wakosane – Luka anamwambia
wanawake ni wengi.
b. Msiba wa kujitakia
Kati ya viongozi na raia ambao wako tayari kupigania haki zao-
hawapewi huduma na viongozi.
Zuhura na Machoka-Zuhura angependa kumchagua kiongozi kwa
misingi ya kikabila kinyume na Machoka.
Sugu Junior na Fumo Matata – Fumo anaona dai la serikali kwamba
kuna maendeleo ni porojo tu.
Mgogoro kati ya tume ya uchaguzi na wananchi.
Mgogoro wa ushindi wa Sugu Junior dhidi ya Fumo matata.
Kati yam zee Sugu Senior na Zuzu Matata; ambapo mzee Sugu senior
alitwaa uongozi baada ya kuondoka kwa wakoloni.
c. Mapambazuko ya machweo
Mzee Makutwa kumtifulia mzee Makucha vumbi na kumdhihaki
kuhusiana na kazi yake.
Bi Macheo anajikuta katika mgogoro na mumewe kwa vile hapendi jinsi
mzee Makutwa anavyomfanyia stihizai mumewe.
Mzee Makucha anakuza mgogoro anapomwitia polisi mzee Makutwa
kwa kuwahujumu vijana.
Mzee Makutwa ana mgogoro na sheria kwa vile anaendesha biashara
haramu.
Migogoro kati ya vijana waliosoma na serikali kwa mfano Sai alidai kuwa
vijana wanaachiwa kazi za hadhi ya chini.
Mzee Makutwa na polisi wakijaribu kumwingiza pangoni.
Mzee Makucha na shirika la reli-kukataa kumlipa pesa.
d. Harubu ya maisha
Mama Mercy amtaka mumewe aeleze sababu ya kutofika ilhali motto
anaelekea kulala. Mama Mercy analalamika kuwa mumewe hatimizi
wajibu wake.
Familia ya Kikwai ina mgogoro na fundi wa nyumba hajalipwa kwa
mwezi mzima.
Kikwai anagongana na Bosi kwa kuacha gari nyumbani kwa kukosa
mafuta.
Nilakosi ana mgogoro wa mpangishaji wake kwa vile hajamlipa na mwezi
unaenda kuisha.
Kikwai kutoleta chakula.
Kikwai kufika amechelewa.
Mercy kulalamikia njaa na upweke.
Swali 9
Nipe Nafasi Maswali na Majibu
a. Eleza tafsiri mbalimbali za kichwa cha hadithi hii, ‘Nipe Nafasi’ (alama 7)
Pupa (F. M. Kagwa)
b. Fafanua umuhimu wa mandhari ya Chenga-ways katika kujenga hadithi Pupa. (alama
5) Toba ya Kalia
(Douglas Ogutu)
c. “Ni kutokana na mchango wako kupitia twitter na facebook katika maswala
mbalimbali ambapo iliamuliwa upewe fursa ya kuzungumza moja kwa moja na
watazamaji wetu.”
Eleza nafasi ya vijana kwa mujibu wa hadithi Toba ya Kalia. (alama 8)
Majibu
a. Eleza tafsiri mbalimbali za kichwa cha hadithi hii, ‘Nipe Nafasi’ (alama 7)
Kuchukua nafasi ya kuboresha maisha yake. Kazili anapoona mumewe
amemdhalilisha vya kutosha, anaamua kuondoka. Hajali kuomba ruhusa
kama anavyotakiwa.
Kuchukua hatua wanapoona waume zao hawawajibiki. Bi. Kazili
anajisemea kuwa atarudi kufanya kazi kuwakimu, na siku hiyo lazima
wale chajio.
Nafasi ya kuishi atakako. Kazili anawakumbusha wanaume kuwa yeye ni
raia halali wa Lesotho kupitia kwa ndoa, na hakuna anayeweza
kumlazimisha kurudi Swaziland, hata mumewe.
Kupinga maamuzi kuhusu maisha yake ambayo hajahusishwa kufanya.
Mama Kazili anakana maamuzi ya wanaume kwenye kraal ambayo awali
yanachukuliwa kuwa sheria isiyoweza kupingwa.
Wanawake kupewa nafasi na nyadhifa. Kazili anaeleza jinsi wanawake
wanavyohiniwa nafasi na wadhifa katika jamii kwa kusingizia Biblia,
kuwa mwanamke anafaa kuwa mnyenyekevu.
Nafasi ya kuheshimiwa. Kazili anapinga swala la mwanamke
kuchukuliwa kama mtoto ambaye anafaa kuomba ruhusa kwa kila kitu
kutoka kwa mumewe.
Nafasi ya ajira na kazi. Mwisho wa mwaka huo, Kaizili anafanya kazi ya
ualimu bila ruhusa kutoka kwa yeyote, na wanawe wanapata chakula kila
siku.
Kupatiwa nafasi ya usemi. Wanawake wa makamo wanakubaliana na rai
ya Kazili, wanaona kuwa amaesema ukweli mchungu. Wako tayari
kubadili mkondo huu wa dhuluma dhidi yao.
Kufanya maamuzi ya kibinafsi. Mama Kazili anawambia wanaume
kwamba aliondoka bila kuomba ruhusa kwa mumewe kwa sababu alijua
hangekubaliwa. Anawajuza kuwa hawezi kukaa tu kuwatazama wanawe
wakihangaika kwa njaa.
Nafasi ya kusema ukweli. Wanaume wanahisi kwamba Kazili amewatusi,
na kwamba lazima arudi kwao Swaziland kwa kuwakosea heshima.
Hatarajiwi kusema ukweli.
Pupa (F. M. Kagwa)
b. Fafanua umuhimu wa mandhari ya Chenga-ways katika kujenga hadithi Pupa. (alama
5)
Kufichua mitandao ya uhalifu inavyofanya kazi / biashara haramu
zinazoendeshwa katika jamii na madhara yake.. Ni danguro.
Kusawiri maudhui ya masaibu yanayoandama mtoto wa kike katika
jamii.
Kuendeleza ploti. Baadhi ya matukio yanatokea katika mandhari haya.
Kuwaibusha wahusika na sifa zao kama Mashaka.
Kuchimuza matabaka katika jamii. Kuna tabaka la wateja matajiri na
wanyonge kina Mwakuona, Mashaka ambao ni bidhaa ya matajiri
Toba ya Kalia (Douglas Ogutu)
c. “Ni kutokana na mchango wako kupitia twitter na facebook katika maswala
mbalimbali ambapo iliamuliwa upewe fursa ya kuzungumza moja kwa moja na
watazamaji wetu.”
Eleza nafasi ya vijana kwa mujibu wa hadithi Toba ya Kalia. (alama 8)
Kukuza vipaji. Jack na Siri wanashiriki katika shindano linaloandaliwa
na wahandisi kutoka Uchina na kuibuka katika nafasi tatu za kwanza.
Jack anaandaa kazi ya kupigiwa mfano na hata fomyula zake zinaingizwa
kwenye vitabu, japo kwa jina la Siri
Kuendeleza lugha na utamaduni. Jack akiwa Uchina anaendeleza elimu
ya lugha ya Kiswahili kwa wakazi wa huko, na anasema kwamba baadhi
yao wanapata umilisi hata kuliko wazungumzaji wa nchi yake ya
nyumbani.
Ujasiriamali. Jack anapokamilisha masomo yake ya shule ya upili kukosa
karo anaanzisha biashara ya kuuza nguo.
Siri huwasiliana na wazazi wake kupitia skype, na Jack ndiye
huwaunganishia mitambo kuhakikisha mawasiliano yanafaulu vizuri.
Wanapatana naye vyema akiwa Uchina.
Urafiki wa dhati. Urafiki wake na Siri ni wa kipekee. Wanasaidiana sana,
hata wanawafikiri kuwa ndugu. Hata kuhiniwa fursa yake na kupewa
Siri hakuwatenganishi.
Usamehevu. Anawasamehe wote waliomkosea mwishoni.
Kukuza teknolojia kupitia kwake Jack , nafasi ya teknolojia na
mawasiliano inabainika.
Kukuza uzalendo. Siri anakipigania Kiswahili na kukifunza Uchina.
Ushauri. Mwishoni mwa kipindi, Siri anawapa watazamaji wosia kuwa
wasiwadhulumu mayatima na maskini
Siri na Jack wanawakilisha teknolojia ya mawasiliano na umuhimu wake
katika kuunganisha jamii.
Watetezi imara wa haki na ukweli. Siri
Kukuza mahusiano ya kimataifa na umuhimu wake katika jamii
unadhihirika. Siri
Swali 10
Nilitamani (Phibiana Muthama) na Kifo cha Suluhu – Dominic Maina Oigo
Majibu
Swali 11
Mume wangu, hebu zivute fikra zako miaka kumi na mitano iliyopita tulipoingia katika
mkataba wa ndoa. Kwa nini unataka kujitia hamnazo kuhusu ahadi ulizozitoa? Umesahau
namna tulivyohangaika, tukachekwa na watu, tukakosa hata marafiki na hatimaye
tukabandikwa majina ya ajabu? Umesahau, mume wangu? Umesahau namna kazi yako ya
kuuza makaa ilivyofika hatima ya ghafla baada ya serikali kupiga marufuku ukataji wa miti
katika eneo la Dafrao? Naomba ukumbuke. Ninaamini huenda umesahau! Ama cheo chako
cha ubunge ulichokipata kwa mbinu nizijuazo mimi kimekulevya na kukufanya uisahau
familia yako?
Majibu
Swali 12
“Wewe mke sampuli gani usiyetaka kumuunga mkono mmeo?”
Kwa kurejelea hadithi hii na nyingine zifuatazo, jadili changamoto anazopitia mnenewa
pamoja na wahusika wa jinsia yake. (alama 20)
Ahadi ni deni.
Hadithi ya Nipe nafasi
Majibu
a. Fadhila za punda
Mwanamke kutawishwa, lilia anaachishwa kazi ya umeneja na mwishowe
kutawishwa. Anaishia kukaa nyumbani na kutishwa asidhubutu kutoka nje ya
lango.
Mwanamke anatishiwa – Lilia anapodhubutu kumshtaki mumewe
anakumbushwa kuwa yeye ndiye Gavana na ana uwezo wa kufanya haki kuwa
batili na batili kuwa haki.Utajua kichomtoa kanga manyoya.
Mwanamke anapokezwa vipigo. Lilia anapokea mapigo kutoka kwa mumewe
anapoenda kuripoti kwa polisi.
Mwanamke kutusiwa: Lilia anaambiwa amenona kama nguruwe.
Mwanamke kudhalilishwa. Lilia annambiwa kuwa ana umbo kama nguruwe
kwani kazi yake ni kula na kulala tu.
Mwanamke kuendewa kinyume na mumewe, katika ndoa, Luka anasemekana
kuwa na kiruka njia ambaye waliandamana naye kila mahali. Lilia anapouliza
ni nani anapokea kipigo kinachomlaza kitandani siku mbili.
Kuachishwa kazi. Lilia anaachishwa kazi na mumewe ili awe mpokezi wa
wageni nyumbani.
b. NIPE NAFASI
Wanawake kutosaidiwa katika malezi na waume zao. Mama Kazili hatumiwe
pesa na mumewe yeye na watoto wake wanataabika kwa njaa.
Mwanamke kutosikilizwa. Wazazi wa mama Kazili wanadinda kusikiliza
malalamishi yake kuwa mumewe ana mke mwingine migodini.
Kutopatiwa pesa za mahitaji – nyanyake msimulizi anakosa kumpa mamake
pesa zinapotumwa na babake.
Kufiwa na jamaa zao. Mama Kazili anafiwa na mwanawe Mkhathini wakiwa
katika safari yao kwenda Makongeni.
Wanawake kulaumiwa/kusingiziwa kusababisha kifo. Mama Kazili
analaumiwa kusababusha kifo cha Mkhathini kwa sababu hakuomba ruhusa.
Wanawake kuuawa – mwanamke katika kijiji cha Habelo anatoroka na
mwishowe maiti yake kufukuliwa na mbwa kondeni mwake. Hii ni baada ya
kumuita mumewe mzembe.
Wanawake kudhalilishwa – wanawake wanaketi sakafuni nao wanaume
wanaketi vitini.
Mwanamke kutopewa nafasi ya kujitetea. Mama Kazili ananyamazishwa na
Matweba anapojitetea kwa wazee.
Kutengwa kwa misingi ya kitaifa. Mama Kazili anaambiwa lazima arudi kwao
Swaziland.
Mwanamke kuchukuliwa kama mtoto anayetarajiwa kuwa chini ya uelekezaji
na utunzi wa mwanamume katika jamii ya Belo.
Jamii na serikali imewanyima wanawake uhuru. Wanahitajika kuomba ruhusa
kwa kila jambo wanalolihitaji kufanya.
c. Ahadi ni deni
Kutoonana na jamaa zao kwa muda mrefu. Fadhumo anakaa kwa muda wa
mihula mitatu bila kuonana na wazazi na jamaa zake.
Kufiwa na wazazi, Fadhumo anafiwa na babake katika ajali na mamake pia
anafariki baadaye.
Kuacha masomo – Fadhumo anaacha masomo yake kwa sababu ya ukosefu
wa karo. Anaachia kidato cha pili.
Kulazimishwa kuwa kimada. Jamaa ya babake Fadhumo anamwambia kuwa
ikiwa anataka kusoma sharti awe kimanda wake.
Mwanamke kulazimishwa kuolewa akiwa mchanga Fadhumo anaolewa na
Adan akiwa mchanga.
Mwanamke kutwikwa majukumu. Fadhumo anajukumika kuwalea na
kuwasomesha nduguze ingawa ni mchanga.
Mwanamke kufanya kazi kunachukuliwa kama kuzurura. Adan anaulizwa na
watu kwa nini mkewe anaenda kazini ilhali anafaa kukaa nyumbani na
kutunza nyumba na watoto.
Mwanamke kutoruhusiwa kusoma; mjombake Adan anamwambia kuwa
masomo yatamfanya mkewe kuwa jeuri.
Mwanamke kusingiziwa; mjombake Adan anamwambia Adan kuwa Fadhumo
anaweza kutoroka na walimu wake au wanafunzi wenzake (zozote 20 x 1 =
20)
Swali 13
Nipe Nafasi Maswali na Majibu
Majibu
a.
i. Nafsi ya kwanza
Vidole vyangu vya miguuni..
Nikatamani tufike kwa jamaa ya baba yetu.....
Kututafuna kadri tulivyokazana...nk. (Nafsi-1, Mfano-1)
ii. Umuhimu wa nafsi ya kwanza:
Swali 14
Fadhila za punda
Majibu
a. Muktadha: Pastor Lee Imani akijiwazia mwenyewe baada ya kupata shinikizo la kuoa
mkw mwingine baada ya kifo cha mkewe. Anaeleza kuwa hangeoa kwa kuwa hayupo
anayelingana na marehemu mkewe 1x4 = 4
b.
Mcha Mungu - anaanzisha na kuendeleza kanisa
Mkarimu - anampa mamake Luka ajira
Mdadisi - Anamwita Luka na kumuuliza nia yake kwa bintiye
Mwenye mapenzi - Alimpenda marehemu mkewe pia bintiye
za kwanza 2x3=6
Tanbihi"
i. Ndoa na mapenzi
ii. Kifo/mauti za kwanza 2x2=4
Alama 1 kutaja, 1 ufafanuzi wa kweli
d.
i. Swali balagha
ii. Tashbihi
za kwanza 2
Atoleee maelezo ya kila mbinu, asipoeleza asituzwe chochote.
Swali 15
Sabina
Majibu
a.
i. Ayasemayo mhusika
ii. Matendo ya mhusika
iii. Wayasemayo wahusika wengine
iv. Maelezo ya mwandishi kuhusu mhusika mwenyewe
v. Uhusiano wake na wahusika wengineMbinu za kimtindo
b.
i. Taswira – athari kujiandika
ii. Msemo- kajishika tama
iii. Tashbihi- mithili ya msafiri
iv. Balagha- angefeli je?
v. Mbinu rejeshi- aliyakumbuka maneno ya mwalimu mkuu
vi. Jazanda- mizizi ya elimu
vii. Methali- mtaka cha mvunguni sharti ainame
viii. Tashihisi- maswali yakamwacha…
ix. Takriri- mtihani, mtihani
c. Aina za taswira kwenye kifungu
i. Oni- usoni mwake
ii. Mwendo- msafiri aliyefika salama
iii. Hisi- kujishika tama
iv. Usikivu- alifikiria
v. Onji- mizizi ya elimu ni michungu (Za kwanza2x1)
d. Matatizo yanayomkumba mwanamke
i. Mimba za mapema- Nyaboke
ii. Kukatiza masomo- Nyaboke
iii. Kufanyishwa kazi nyingi- Sabina
iv. Kukataliwa na wanaowadunga mimba- Nyaboke kukataliwa na janadume
lililompachika mimba
v. Kujukumizwa ulezi wa mapema- Nyaboke
vi. Kukatisha wazazi tamaa
vii. Kukosa malezi ya baba mzazi- Sabina
viii. Kufanya kazi za sulubu ili mtoto apate mahitaji ya kimsingi
ix. Kifo cha mzazi-Sabina
x. Kifo cha walezi- babu na nyanyake Sabina
xi. Kutelekezwa na wanakijiji –Wanakijiji kuapa kukaa mbali naye baada ya
kushuku familia hiyo imelaaniwa.
xii. Kutengwa – Sabina anatengwa na watoto wa mjomba wake (Ombati)
xiii. Dhiki za kisaikolojia-Sabina anapoitwa na mwalimu mkuu
xiv. Kushukiwa- mwalimu mkuu anamshuku Sabina anapinga adhabu ya
kuchelewa kufika shuleni.
xv. Kuchapwa/kuteswa- Sabina anapigwa na shangazi yake.(Yunuke)
xvi. Matusi- Sabina anatusiwa kiokote na Yunuke
xvii. Kunyimwa vifaa vya kimsingi vya matumizi- Yunuke anamzimia Sabina
kibatari alipokuwa akisoma, rinda la Sabina ni kuukuu.
Swali 16
.“...majira ya magharibi pevu, nilifika tena pale mzimuni. Kama ilivyo ada yangu , nilivaa
guo jeupe lililonifunika kama maiti. Nikaangalia huku na huko, sikuona mtu. Hapo nikasogea
karibu zaidi na ule mzimu. Nilipofika nikauimba ule wimbo wote. Nilipomaliza tu nikajitoma
kichakani mle bila hofu wala kimeme. Mara nikajikuta nimo ndani, kiza tororo! Nikatoa tochi
yangu nikaanza kumulika hukuna huko. Nilichokiona humo, sikuamini macho yangu! Mle
ndani ya mzimu mlikuwa na makanda na makasha ya tumbaku, unga wa kilevi na bang
ikwenye marobota. Kulikuwa na mapipa yaliyojaa chang’aa na tembo ya mnazi. Humo pia,
mlikuwa na kitanda cha besera kilichotandikwa
vizuri. Juu ya kitanda hicho, palitupiwatupiwa asumini na maua ya mlangilangiyaliyonukia
harufu za mahaba kuliko harufuya mapambo ya harusi ya kiharuni! Mle mvunguni mwa
kitanda kile mlikuwa na chetezo kilichojaa udi wa mawaridi. Nikabaki kinywa wazi kwa
bumbuazi na butwaa la uduazi! Butwaa ambalo kwa hakika lilifanya akili yangu isimame
kufikiri kwa muda wa sekunde kadhaa.”
a. Kando na taswira, tambua mbinu zingine za kimtindo katika dondoo hili. (alama 5)
b. Ainisha taswira katika kifungu hiki. (alama 3)
c. Chambua maudhui yanayojitikeza katika kifungu hiki. (alama 4)
d. Eleza umuhimu wa Msimulizi katika mujibu wa hadithi husika. (alama 8)
Majibu
Swali 17
Mzimu wa Kipwerere Maswali na Majibu
…akikiomba radhi kile kitawi cha mti kilichonasa kwenye kazu yake ya rangi ya udongo
iliyoficha kiwingu cha nongo kwa kukosa kuoshwa tangu ainunue! Nikauacha mpambano ule
kati ya mzimu na mwenye dhamana ya mzimu ambao sina shaka ulidumu hadi asubuhi pale
wanakijiji walipofika kushuhudia siri nzito iliyomezwa na mzimu ule waliokuwa wakiogopa
na kuamini kiasi cha kuabudu kwa unyenyekevu na uchaji uliotukuka!
Majibu
Swali 18
“Mike! Mike! Mike! Njoo! Nilijua utafanya vyema mwanangu…”
Swali 19
“Poko! Ukiumwa na nyuki haina haja ya kujitwika jukumu la kuharibu mizinga yote ya asali.
Hujui faida ya nyuki ulimwenguni? Uliamua kurina asali ya nchi.”
a.
i. Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)
ii. Tambua tamathali mbili za usemi zilizotumika katika dondoo hili. (alama 2)
iii. Onyesha matokeo ya kuharibu mizinga yote ya asali ukirejelea hadithi
Mapambazuko ya Machweo.
b. Jadili maudhui ya ukiukaji wa haki za watoto katika hadithi ya;
i. Mapambazuko ya Machweo (alama 10)
ii. Sabina (alama 10)
Majibu
a.
i. Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)
Maneno ya Makucha kwa Makutwa mgodini baada ya MAkutwa
kukamatwa kwa kosa kufuja raslimali ya nchi.
ii. Tambua tamathali tatu za usemi zilizotumika katika dondoo hili. (alama 2)
Taswira fiche. Ukiumwa na nyuki-kuajibishwa kwa kuhujumu uchumi
wa nchi. Dhihaka. kujitwika jukumu la kuharibu mizinga yote ya asali.
Jazanda. Uliamua kurina asali ya nchi - kuhujumu uchumi wa nchi
iii. Onyesha matokeo ya kuharibu mizinga yote ya asali ukirejelea hadithi
Mapambazuko ya Machweo. (alama 7)
Makutwa anafanya biashara ya kimagendo ya kuchimba vito katika
mgodi kisiri. Hii ni raslimali ya serikali ambayo mtu anafaa kupata
leseni ya kuchimba
Ukoloni Mamboleo. Mzee Makutwa anawasomba ijana kwenda
kuwafanyisha kazi ya kusaka vito vya thamani katika mgodi wake.
Wanafanya kazi hii katika mazingira mabovu na kufungiwa mle ndani,
wasiwe na nafasi ya kutokea.
Makutwa analipoka taifa nguzo yake muhimu kwa kuwachukua vijana
mabarobaro na kwenda kuwatumikisha katika mgodi wake. Vijana
hawa wanafaa kuwa wakiendesha shughuli nyingine muhimu za
kujenga jamii.
Ajira ya watoto. Vijana kadhaa, ikiwemo watoto wadogo wanafanya
kazi ya kudondoa vijiwe vidogovidogo vinavyong'aa. Wanasimamiwa
na wanyapara wanaowaamrisha kwa sauti za kutisha.
Mazingira mabovu ya utendakazi. Vijana mgodini wanakumbwa na
hali ngumu ya kimaisha, kwani huko wanakoishi hakuna hali nzuri.
Hewa si safi na kazi wafanyazo ni za sulubu.
Ukosefu wa ajira. Sai na Dai pia wanawakilisha hali ya vijana ambao
baada ya kuhitimu kutoka chuo kikuu, hawajapata kazi wala hawana
matuamini. Wanashinda kuzurura mitaani.
Wafanyakazi kutimuliwa bila fidia. Mzee Makucha anafanya kazi na
shirika la reli ambalo linamtimua kwa ajili ya kupunguza idadi ya
wafanyakazi wake. Baadaye linasambaratika, hivyo anakosa
marupurupu yake.
Umaskini. Mzee Makucha anaanguka kwenye lindi la umaskini baada
ya kuachishwa kazi katika shirika la reli bila marupurupu, kwani
shirika hilo linasambaratika pia.
Kazi duni. Makucha analazimika kuchuuza vitafunio kando ya
barabara kujipatia riziki. Mkewe naye anauza kaimati na vitumbua
kwenye veranda ya nyumba yao.
Kukimbilia ndoa. Riziki, anawatoroka wazaziwe na kuolewa na
Mhindi ili kuepuka urumo.
b.
i.
Swali 20
Siku moja alipokataa katakata kuandamana na mumewe, jungu lilifoka. “Wewe mke sampuli
gani usiyetaka kumuunga mkono mmeo?” Haya kaa nyumbani. Kula na kulala tu, hujui
jingine. Ona umbo lako sasa, kama nguruwe. Si mke mrembo niliyeoa! Wanawake ni
wengi…”
a. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
b. Bainisha vipengele vinne vya kimtindo katika dondoo hili (alama 4)
c. Fafanua nafasi ya mwanamke katika hadithi hii. (alama 12)
Majibu
a.
i. msemaji ni Luka
ii. msemewa ni Lilia
iii. nyumbani kwao
iv. Luka alimtaka mkewe kuandamana naye katika kampeni – taswira ya kiongozi
anayethamini ndoa na familia ili achaguliwe kuwa gavana, (alama 4x1)
b.
i. Balagha – wewe mke sapuli gani?
ii. Nahau = katakata, unga mkono
iii. Taswira – ona sasa
iv. Tashbiha – kama nguruwe
v. Masimango – kama nguruwe
vi. Nidaa – niliyeoa!
vii. Mdokezo – wengi…
c. Fadhila za punda
i. Mwanamke kutawishwa- lilia anaachishwa kazi ya umeneja na mwishowe
kutawishwa.
ii. kukaa nyumbani na kutishwa asidhubutu kutoka nje ya lango.
iii. Mwanamke anatishiwa – Lilia anapodhubutu kumshtaki mumewe
anakumbushwa kuwa yeye ndiye Gavana na ana uwezo wa kufanya haki kuwa
batili na batili kuwa haki.Utajua kichomtoa kanga manyoya.
iv. Mwanamke anapokezwa kichapo cha mbwa- Lilia anapokea mapigo kutoka
kwa mumewe anapoenda kuripoti kwa polisi.
v. Mwanamke kutusiwa- Lilia anaambiwa amenona kama nguruwe.
vi. Mwanamke kudhalilishwa- Lilia annambiwa kuwa ana umbo kama nguruwe
kwani kazi yake ni kula na kulala tu.
vii. Mwanamke kuendewa kinyume na mumewe katika ndoa- Luka anasemekana
kuwa na kiruka njia ambaye waliandamana naye kila mahali. Lilia anapouliza
ni nani anapokea kipigo kinachomlaza kitandani siku mbili.
viii. Kuachishwa kazi. Lilia anaachishwa kazi na mumewe ili awe mpokezi wa
wageni nyumbani.
ix. Ni chombo cha starehe-
x. Wasaliti – kunyanganywa bwana
xi. Kunyimwa uhuru wa kutangamana
xii. Ku