Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 5

THE KENYA NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL

SCHOOL BASED ASSESSMENT

KISWAHILI
SEHEMU A
Zoezi la 1 na la 2

Gredi ya 5
NAKALA YA MWALIMU

School Based Assessment © 2023 The Kenya National Examinations Council


Gredi ya 5
2

Sehemu A inatathmini Stadi ya Kusikiliza na Kuzungumza. Inajumuisha mazoezi matatu:


i. Mazungumzo ya ana kwa ana
ii. Ufahamu wa Kusikiliza
iii. Kusoma kwa sauti

Maagizo ya jumla
1. Mwalimu awafahamishe wanafunzi wote kwamba mazoezi yote katika sehemu hii
yatakuwa tathmini ya ana kwa ana. Kila mwanafunzi atakuwa na zamu yake ya
kutathminiwa; mmoja baada ya mwingine.
2. Mwalimu awafahamishe wanafunzi wote kwamba karatasi hii ina mazoezi matatu:
i. Mazungumzo ya ana kwa ana
ii. Ufahamu wa Kusikiliza
iii. Kusoma kwa Sauti
3. Mwanafunzi aandaliwe kiti au dawati kutazamana na mwalimu.
4. Mwalimu atangulize kila zoezi na amfahamishe mwanafunzi matarajio ya kila zoezi.
5. Mwalimu amfahamishe mwanafunzi kukamilika kwa kila zoezi.
6. Mwalimu atathmini umilisi wa mwanafunzi kwa mujibu wa mwongozo wa kutathminia
pamoja na kuweka rekodi.

School Based Assessment © 2023 The Kenya National Examinations Council


Gredi ya 5
3

ZOEZI 1A: MAZUNGUMZO YA ANA KWA ANA


Maagizo maalum
i. Andaa mazingira mazuri ya tathmini kwa kumkaribisha mwanafunzi.
ii. Mwamkue na kumwomba akae.
iii. Jitambulishe kwake kwa kusema, ‘Mimi ni mwalimu________________’.
iv. Muulize jina lake.
v. Anza tathmini kwa kusema,

‘Leo ningependa tuzungumze kuhusu mazingira.’


1. Nina hakika umejifunza kuhusu mazingira. Nitajie baadhi ya vitu vinavyopatikana
katika mazingira ya nyumbani.
(Mwanafunzi ajibu)

2. Tunapata faida nyingi kutokana na mazingira. Hebu nieleze faida moja ya


mazingira.
(Mwanafunzi ajibu)

3. Je, unafikiri ni nini kitafanyika tukichafua mazingira yetu?


(Mwanafunzi ajibu)
4. Kufuta vumbi ni kuondoa vumbi kwenye sehemu fulani. Je, kupiga deki ni
kufanya nini?
(Mwanafunzi ajibu)

School Based Assessment © 2023 The Kenya National Examinations Council


Gredi ya 5
4

ZOEZI 1B: UFAHAMU WA KUSIKILIZA


Maagizo maalum
i. Msomee mwanafunzi kifungu kifuatacho mara mbili.
ii. Mjulishe kuwa atajibu maswali baada ya kusomewa kifungu mara ya pili.

Mbuni ni ndege mkubwa sana. Mbuni ndiye ndege mkubwa zaidi ulimwenguni. Ndege huyu
anaweza kukua hadi kufikia uzito wa kilo mia moja arubaini. Ana miguu mirefu na shingo ndefu.
Ni ndege mwenye mbio za ajabu. Anaweza kukimbia kwa kasi ya kilomita sabini kwa saa moja;
utadhani ni gari. Hata hivyo, mbuni hawezi kupaa juu kama wafanyavyo ndege wengine.
Mbuni ana manufaa mengi. Yeye hutaga mayai makubwa ambayo huliwa. Nyama yake vile vile
ni chakula. Aidha, mbuni huwavutia watalii ambao huleta pesa za kigeni nchini.
Ukija kwetu utaona picha maridadi ya mbuni kwenye ukuta sebuleni. Picha hiyo nimeichora
mimi mwenyewe. Niliichora baada ya kumwona mbuni tulipozuru mbuga ya wanyama ya
Maasai Mara. Hakika mbuni ni ndege anayependeza.

5. Kifungu nilichokusomea kinamhusu ndege yupi?


(Mwanafunzi ajibu)

6. Kulinga na kifungu, unafikiri kwa nini mbuni hawezi kuruka?


(Mwanafunzi ajibu)

7. Kama ungezuru mbuga ya wanyama ya Maasai Mara unadhani ungeona ndege yupi
mwingine?
(Mwanafunzi ajibu)

8. Kulingana na kifungu, maana ya kasi ni?


(mwanafunzi ajibu)

School Based Assessment © 2023 The Kenya National Examinations Council


Gredi ya 5
5

ZOEZI 2 : KUSOMA KWA SAUTI


Maagizo maalum
i. Mfahamishe mwanafunzi matarajio ya Zoezi la Kusoma. (Zingatia mwongozo wa kutathminia
Kusoma kwa sauti).
ii. Mpe mwanafunzi nakala atakayoisoma kwa sauti.
iii. Mwanafunzi anaposoma, sikiliza na kurekodi idadi ya maneno anayosoma kwa muda wa
dakika moja.
iv. Onyesha kwa mshazari (/) mahali mwanafunzi alipofikia kusoma dakika moja ikikamilika.
v. Mruhusu mwanafunzi kusoma mpaka mwisho wa kifungu.
vi. Pigia mstari maneno yote ambayo mwanafunzi atashindwa kuyasoma au kuyatamka vizuri.
vii. Rekodi idadi ya maneno ambayo mwanafunzi ameweza kusoma kwa usahihi kwa dakika moja.
(Baada ya kuondoa yaliyotamkwa vibaya au/na aliyoshindwa kutamka)
viii. Rekodi viwango vya umilisi wa mwanafunzi kwa kuzingatia mwongozo uliopewa.
ix. Hakikisha una nakala ya kurekodia tathmini hii. (Iwe na majina ya wanafunzi wote.)
x. Ukiwa tayari kuanza tathmini, sema,
‘‘Sasa naomba unisomee kifungu hiki kwa sauti.’’

Mwalimu amwambie mwanafunzi asome kifungu kifuatacho kwa sauti.


Tangu jadi, binadamu amekuwa akitumia mapambo kuongeza urembo. Mapambo haya
10 20
ni ya aina nyingi. Kuna yale yanayovaliwa mikononi kama vile bangili, saa na pete.
30
Yapo yanayovaliwa shingoni kama vile mkufu na kidani. Masikioni nako huvaliwa
40
herini au vipuli. Kwenye miguu huvaliwa njuga na vikuku.

50
Mbali na mapambo ya kuvaliwa, kuna yale ya kujipaka. Katika kundi hili, kuna poda
60 70
na wanja. Mtu hujipaka poda usoni na wanja machoni. Hina nayo hupakwa

mikononi, kuchani, miguuni na kwenye nywele.

80
Ni muhimu kutumia mapambo haya kwa namna ambayo inafaa. //Usijipambe kupita
90
kiasi ukauharibu urembo wenyewe. Huna budi kujihadhari usije ukatumia mapambo
100
ambayo yanaweza kudhuru ngozi yako. Ukifanya hivyo utakuwa umejiletea hasara.
107

School Based Assessment © 2023 The Kenya National Examinations Council


Gredi ya 5

You might also like