Professional Documents
Culture Documents
Tangzo La Nafasi Ya Kazi - Tag Maswa
Tangzo La Nafasi Ya Kazi - Tag Maswa
KITUO CHA KAZI: TAG EBENEZER CHRISTIAN CENTER – MASWA MJINI, SIMIYU.
Kanisa la Tanzania Assemblies of God (T.A.G), Ebenezer Christian Center liliolpo wilayani Maswa
Mkoa wa Simiyu limekuwa likitoa huduma kwa watoto wanaotoka kwenye kaya maskini kupitia
kituo cha Huduma ya maendeleo Jumla ya Mtoto (Holistic Child Development Ministry) kwa
kushirikiana na Shirika la Compassion International Tanzania (CIT). Kanisa kupitia Program za
maendeleo jumla ya mtoto linalenga kuwafungua watoto katika umaskini kwenye maeneo ya Kiroho,
Kiuchumi, Kijamii na Kimwili (ambao ndio ujumla wa mtu), kwa shabaha ya kuwawezesha wawe
watu wazima wanaojua wajibu wao na wanaojitosheleza. Mchungaji kiongozi, anakaribisha maombi
kwa Watanzania wenye sifa na uwezo wakujaza nafasi tajwa hapo juu.
1. SIFA ZA MUOMBAJI:
Mratibu wa Kituo cha Huduma ya Mtoto na ni mwajiriwa wa kanisa. Katika utendaji wake wote wa
majukumu /wajibu atawajibika moja kwa moja kwa Mchungaji kiongozi na kusimamiwa na Kamati
ya huduma ya mtoto kwa kushirikiana na Huduma ya Mtoto ya Compassion International Tanzania
(CIT).
xxiv. Kuhakikisha kuwa taarifa zote za watoto na Kanisa zilizoko katika mfumo wa taarifa wa
Compassion connect ni sahihi na zimehuishwa.
xxv. Kuhakikisha zawadi zilizotumwa na wafadhili zinawafikia walengwa kwa wakati na kwa
asilimia mia moja.
xxvi. Kushiriki katika mafunzo yanayoandaliwa kwaajili ya huduma ya mtoto na vijana.
xxvii. Kuwasaidia watenda kazi wengine wa Kituo na kushirikishana wajibu wao pale
inapohitajika. Hii ni pamoja na kuhakikisha watenda kazi wapya wanajua majukumu yao
katika Kituo cha huduma ya mtoto.
xxviii. Kutoa taarifa kwa kamati ya Huduma ya Mtoto, juu ya ubadhilifu wa fedha au tabia
isiyoridhisha kwa mmojawapo wa Watenda kazi wengine wa Kituo.
xxix. Kuhakikisha watoto walioandikishwa katika Kituo kwaajili ya ufadhili ni wale tu
wanaokidhi vigezo vilivyowekwa katika Ushirika-wenza.
xxx. Kuendesha vikao vya watenda kazi mara moja kwa mwezi au zaidi pale inapobidi.
xxxi. Kushiriki kikamilifu ibada za kila siku asubuhi pamoja nawatenda kazi wote kabla ya
kuanza kazi.
xxxii. Kuratibu vikao na mafunzo kwa wazazi kwa kushirikiana na uongozi wa Kanisa pamoja na
kamati ya wazazi kwa lengo la kuhamasisha watu hao kuhusika na maendeleo ya watoto.
xxxiii. Atafanya kazi nyingine za kiofisi kama atakavyopangiwa na uongozi wa kanisa.
Waombaji wenye sifa watume maombi yao kabla ya tarehe 15/8/2019 kwenye anuani zilizopo
hapo chini. Kila mwaombaji aambatanishe barua ya maombi pamoja na CV, nakala za vyeti vya
taaluma, Cheti cha kuzaliwa na barua ya utambulisho kutoka kwa Mchungaji wa kanisa analoabudu.