Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 194

|

|i

|
j

wi

wa aa
wi

UTA
TAA AUA
WA AA WA ADI wa
Wa KA

UA
WA Wa ai
Kaa
Wa
WA
YA
EA
ai
VYA KATAA
Fani ya
Fasihi
kwa shule za Upili

Assumpta K. Matei

OKFORD
UNIVERSITY PRESS
OKFORD
UNIVERSITY PRESS

Osford University Press is a depa


rtment of the University of Ozfo
It furthers the University's obje rd.
ctive of eKcellence in research
and education by Publishing , scholarship,
worldwide. Osford is a register
Ozford University Press in the ed trade mark of
UK and in certain other countrie
s

Published in Kenya by
Ozford University Press East Afri
ca Limited, The Osford Place,
Elgon Road, Upper Hill, PO Bos
72532-00200, Nairobi, Kenya
|
” OAssumpta K. Matei 2011

The moral rights of the author


have been asserted

First published in 2011

All rights reserved. No part of


this
a retrieval system, or transmitted,
in an
DTior permission in writing of
Osford
> OT Under terms agreed with
Tganization. Enguiries concerni
ng
above should be sent to the Righ
ts
t Africa Limited, at the address
above
You must not circul ate this
work in any other form
and you must impose this same
condition on any acguirer

ISBN 978 019 573654 0

14 15 16 17 18 19 20

15 14 13 12

Printed in Kenya by
Icons Printers Ltd, PO Bos 3927
3-00623, Nairobi, Kenya

The publishers would like to


th ank the following publishers
€ekcerpts of their books: Tenzi for allowing us to use
Tatu za Kale (TUKI), Kipendacho
Roho (OUP) , Malenga wa Mvita (OUP
)

Photographs/Illustrations by OUP
Library

While every eftort has been


made to trace the original
source of copyrighted mater
ial, er Tors and omissions can occur.
to us for correction or attribution. Do not hesitate to write
Yaliyomo

Dibaji www... ................................................................”.Tebubasbososososomo vi


Maana na Dhima ya Fasihi.........................s..sse00ees0o0eooooo00oooooooo0ocoooocooooc000 1
Uandii aaa 1
Maana ya Sanaa aaa nili
Dhima ya fasiki kitika Jimi 2
Makutidi ya Kasiki uiiaa. 5
Tofatiti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi.......s..<.ssssssssmsemeesemasssnumamsansasessa 5
Athari za fasihi simulizi katika fasihi andishi.........s........ssss.ssss.mssesmmmmsmensmasmmamamensss
nse 7
Fasihi Simulizi .....................c00e AAA AA AAA 10
Utangulizi Ai . 10
Vipengele muhimu katika uwasilishaji wa fasihi simulizi...............<<<wmmmmmemmeo 10
ITA ZA Ea itikaMtii
iba aaa kaya wamama amazi manaka Mai 11
Dhima ya fasihi ia II, u12
Mambo ambayo huchangia kubadilika kwa fasihi simulizi...............<veswmsewemmee ....14
Wahusika katika Fasihi ili ii... 15
'Tarizu za fasihi simulizi ii... 18

Utanzu wa Hadithi ................s..0sss000000000000000000000000..e.............................. 21


Utani ai A. 21
Sifa za Hadithi II... 21
Dhima ya hadithi iii. 22
Usimulizi wa halii AI 23
Vipera vya hadithi wA 25
Nana IIIA... 25
Ngano Za mai... 29
Hai ii ...a. 32
Hekaya wa... 34
Ngano za Mtanzika ii... 36
Ngano za ii Ia 38
Ngano za Mashujaa ii... 39
Ngano za kimafumbo i.........,,
Misha. WAA wahi
Visiki ii .... 48
Visa ia. 49
Vipera vingine vya hadithi ii 51
Via ii .I. Si
Tai 51
Kiba. 52
kayayaeVAYaKa yaaAA AA aa$u$ II AS$AS$A 52
Mbinu za uchambuzi wa hadithi Ua. 52
Bi Ki Wai Ia... 53
Vipo vitabu kadha ambavyo vinatumiwa kufundishia fasihi simulizi katika shule za upili
na vyuo vya ualimu. Hata hivyo, imebainika kwamba bado pana haja ya kitabu ambacho
kitachangiana na kukamilishana na vingine katika kulikabili somo la fasihi simulizi.
Fani ya Fasihi Simulizi kwa Shule za Upili kimeandikwa kukidhi mahitaji ya vitabu vya rejea
. kwashule za upili na vyuo vya ualimu. Kitabu hiki pia kitaweza kutumiwa kama kitangulizi
cha kufunzia fasihi simulizi katika vyuo vikuu.
Masuala yameshughulikiwa kwa njia angavu na nyepesi. Tanzu na vipera vya fasihi simulizi
vimeshughulikiwa kwa kina na mifano ya uchanganuzi wa vipera hivi kutolewa.
Maswali yanayotahini viwango vyote vya utambuzi (ujuzi, ufahamu, matumizi, uchanganuzi,
usanisi na tathmini) yametolewa kwa nia ya kumtayarisha msomaji kwa mitihani. Kadhalika
kumetolewa mazoezi ya marudio na majibu yake mwishoni mwa kitabu ili kumwezesha
msomaji kujitathmini mwenyewe.
Tunatumai kuwa kitabu hiki kitachangia katika ufunzaji na ujifunzaji wa fasihi simulizi, na
kwamba wasomaji wake wataibua mijadala ambayo itasaidia kuboresha, pamoja na kuukuza
usomi na ufundishaji wa somo hili.

Assumpta K. Matei
Kenya High School, Nairobi
Juni, 2010
Maana na Dhima ya Fasihi

Utangulizi
Fasihi ni sanaa ambayo hutumia lugha kwa ubunifu kuwasilisha masuala kuhusu maisha
ya binadamu na mazingira anamoishi. Fasihi huweza kuandikwa au kusimuliwa.

Maana ya sanaa
Sanaa ni ufundi wa kuwasilisha hisia na fikira za binadamu.
Sanaa huwasilishwa kwa mbinu kama vile maandishi,
matamshi, michoro, uchongaji, ususi, ufumaji na ufinyanzi.
Sanaa ni zao la mikono na akili ya mtu na kwa kawaida
huwa na umbo au sura dhahiri. Tunaposema kuwa sanaa
ina umbo dhahiri ina maana kuwa sanaa huchukua maumbo
yanayobainika. Ushairi, kwa mfano, ni utanzu wa sanaa ya
fasihi ulio na umbo dhahiri la beti zilizo na mishororo. Vinyago
na vyungu ni maumbo ya sanaa ya uchongaji na ufinyanzi
mtawalia.
Ufinyanzi
Tofauti kati ya fasihi na sanaa nyingine
(a) Fasihi hutumia lugha kama malighafi ya kuelezea fikira za binadamu. Sanaa nyingine
hazitumii lugha. Mfinyanzi, kwa mfano, hutumia udongo kufinyanga vyungu na
mchongaji hutumia kipande cha mti au jiwe kuchongea vinyago. Fasihi hutumia
lugha yenye mvuto na mguso wa kipekee. Tanzu na vipera vya fasihi hutumia lugha
ya kitamathali kama vile nahau, misemo, misimu, lakabu, kinaya na dhihaka.
(b) Fasihi, tofauti na sanaa nyingine, hujikita katika mazingira au muktadha wa mahali,
wakati na hali maalumu. Kuna methali, nahau na misimu ambayo hujikita katika
mazingira ya shambani. Pia kuna riwaya, mashairi na tamthilia ambazo zinaonyesha
migogoro ya kijamii. Tamthilia ya Kitumbua Kimeingia Mchanga ya Said A. Mohammed,
ni mfano wa tamthlia inayojikita katika mazingira ya jamii ya Waswahili na kusimulia
migogoro iliyojitokeza kati ya vijana na wazee wa jamii hiyo. Mazingira ya kazi ya
kifasihi huweza kuwa ya kubuni au ya kweli. Kinjeketile nayo ni mfano wa tamthilia

Oo
inayojikita katika mazingira ya ukweli. Inasawiri mapambano kati ya Watanzania na
Wajerumani na vita walivyopigana katika enzi za ukoloni.
(c) Fasihi ni sanaa tendi. Fanani (mwasilishaji wa fasihi simulizi) anaweza kuigiza yale
anayowasilisha na pia akashirikisha hadhira yake kwa kuigiza. Pia hadithi katika riwaya
na tamthilia huweza kuigizwa. Sanaa nyingine, kama vile ufinyanzi na uchongaji,
haziigizwi.
(4) Fasihi hutumia wahusika kuwasilisha maudhui. Ngano, riwaya, tamthilia, baadhi ya
mashairi na hadithi fupi ni mifano ya kazi zinazotumia wahusika kuwasilisha maudhui.
Sanaa nyingine, kama vile uchongaji, ni maumbo yanayomithilisha watu, hali na vitu
mbalimbali katika jamii.
(e) Fasihi huwasilisha ujumbe kwa kutumia maudhui na fani pamoja, tofauti na sanaa
nyingine ambazo hutumia sura au maumbo ya vitu.

Fasihi kama sanaa


Ingawa fasihi inatofautiana na sanaa nyingine, ni sanaa kwa sababu zifuatazo:
(a) Inatumia lugha kwa ufundi. Ngano, riwaya na tamthilia kwa mfano, huwasilisha
maudhui kwa lugha ya kitamathali. Lugha ya kitamathali ni lugha inayotumia
tamathali za usemi kama vile methali, chuku, tashihisi na kinaya.
(b) Fasihi ina umbo (sura) mahususi. Kila kipera cha fasihi huwa na umbo maalumu.
Shairi, kwa mfano, hugawika katika beti, mishororo, vipande, mizani na vina.
(c) Fasihi husawiri mandhari (mazingira) mahususi kwa ufundi mkubwa.
(d) Fasihi hujenga wahusika kwa ustadi mkuu ili waweze kusawiri tabia na matendo ya
watu katika jamii.

Dhima ya fasihi katika jamii


Fasihi ina majukumu manne ya kimsingi:
(a) Kuchora au kusawiri mazingira ya binadamu. Fasihi ni kitambulisho cha jamii. Hii ina
maana kuwa fasihi huchota maudhui au mambo ya kuzungumziwa kutoka kwa jamii
inayohusika. Kupitia kwa fasihi, itikadi na mielekeo ya jamii hueleweka.
(b) Kukuza au kujenga tabia. Katika kuisoma, kuitazama au kuisikiliza kazi ya kifasihi,
binadamu hujenga tabia yake. Mathalani, kupitia kwa tungo kama vile hadithi,
binadamu huweza kuiga matendo ya wahusika na kujifunza kwayo.
(c) Kumburudisha na kumstarehesha binadamu. Msomaji, mtazamaji au msikilizaji wa
kazi ya kifasihi hujituliza na kusisimka kimwili na kiakili anapoisoma, kuitazama ama
kuisikiliza kazi ya kifasihi. Vilevile, fasihi humpumzisha binadamu na kumtuliza baada
ya shughuli za kazi.
(4) Kuichochea na kuielimisha jamii. Fasihi hueneza mawazo na falsafa za jamii kwa
wanajamii. Huuchochea na kuufumbua macho umma ili kupiga vita mazingira ya
njaa, maradhi, umaskini, ujinga na hali nyingine za uozo katika jamii. Pia huwapa
wanajamii maarifa na stadi za kukabiliana na mazingira ambamo wanaishi.
au

Kutokana na misingi hii, ni wazi kwamba fasihi ina dhima kubwa katika jamii:

(a) Fasihi ni kitambulisho cha jamii za binadamu. Fasihi hufungamana na miktadha


fulani ya kiuchumi, kijiografia na kitamaduni. Kwa hivyo, dhima mojawapo ya fasihi
ni kusawiri hali ya binadamu, mazingira anamoishi, mahusiano na mtagusano wake
na watu, hisia, imani na mitazamo ya watu katika jamii. Haya huwasilishwa kupitia
kwa tanzu na vipera vya fasihi. Methali kama Mke ni nguo mgomba kupalilia inaonyesha
imani ya jamii husika ambayo humchukulia mwanamke kama kiumbe anayestahiki
kutunzwa na kwamba akivishwa vizuri atakuwa mrembo. Mke anafananishwa na
mgomba ambao ukipaliliwa utanawiri na kuzaa ndizi nzuri.

(b) Fasihi hueneza itikadi zinazotawala jamii husika. Methali na vitendawili ni mifano
ya semi ambazo hutumiwa kutilia nguvu itikadi fulani kwa kuzipitisha kutoka kizazi
kimoja hadi kingine. Fasihi pia inaweza kupinga itikadi zinazotawala, ikachukua
msimamo wa kuwatetea wanyonge. Vipera vya fasihi, kama vile nyimbo, hutumiwa
kueneza propaganda za kisiasa na kupinga utawala dhalimu. Katika fasihi andishi,
maandishi mengi yamepinga ukandamizaji wa wanyonge na kueneza siasa za
ukombozi. Baadhi ya kazi za aina hii ni pamoja na tamthilia ya Kinjeketile, ambayo
pamoja na kupinga unyonyaji wa mabepari kwa tabaka la wafanyakazi, inawachochea
kuungana kupigania uhuru wao wakiongozwa na Kinjeketile mwenyewe.
(c) Fasihi hupumzisha, huburudisha na huliwaza. Nyimbo za kazi husaidia kupunguza
hisia za uchovu. Aidha, usomaji wa riwaya, tamthilia na mashairi hupumzisha akili
na kuiliwaza. Vivyo hivyo, watu wanapotazama michezo ya kuigiza huchangamka na
kujisahaulisha kwa muda matatizo yao.
(d) Fasihi huhifadhi na kurithisha maarifa au elimu ya jamii. Fasihi simulizi na andishi
huhifadhi maarifa ya kijamii na kuyapitisha kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kupitia
kwa tungo, kama vile nyimbo na vitabu (riwaya, ushairi, tamthilia na hadithi fupi),
maarifa hupitishwa kwa wanajamii. Amali za jamii (mila, imani, historia) na sherehe
za kijadi (jando, matambiko, ibada na sherehe za kutawazwa) huhifadhiwa katika
tanzu na vipera vya fasihi simulizi na andishi na kupitishwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine.
(e) Fasihi husaidia kukuza lugha. Lugha ndiyo malighafi ya fasihi. Kila fanani au mwandishi
ana upekee wake wa matumizi ya lugha. Kadiri lugha inavyotumiwa na fanani na
waandishi mbalimbali, ndivyo nayo inavyofinyangwa upya na kupevuka, na hivyo,
matumizi yake kupanuka. Halikadhalika, misimu inapokubalika kama semi katika
lugha hukuza lugha kwa kuiongezea msamiati. Maneno yaliyokuwepo katika lugha
hupewa maana mpya.
(f) Fasihi humwezesha binadamu kujenga tabia ya kudadisi na kutafakari kuhusu
Masuala yanayomkumba. Katika kusoma kwa makini na hata kuhakiki kazi za
kifasihi kama vile riwaya, hadithi fupi na tamthilia, pamoja na tanzu za fasihi
Simulizi za ngano, semi na vipera vyake, binadamu huimarisha mazoea ya kusoma

o
na kuchunguza makala mbalimbali. Aidha, mtu hupanua mawazo yake na kuweza
kutathmini mambo kwa mitazamo mbalimbali.
Fasihi huhamasisha wanajamii kuhusu masuala ibuka na nyeti katika jamii yao. Kwa vile
fasihi husawiri mambo yanayoathiri jamii mahususi, msomaji, mtazamaji ama msikilizaji
wa kazi ya fasihi hufahamishwa kuhusu mambo mapya au yaliyozuka. Ngomezi, kwa
mfano, ilitumiwa kuarifu watu kuhusu tukio jipya kama kuwepo kwa wavamizi, kifo au
kualika kwenye sherehe.
(h) Fasihi huadilisha. Fasihi hufunza tabia njema inayokubalika na jamii. Huasa jamii dhidi
ya matendo hasi na kudumisha maingiliano mema pamoja na hulka zinazokubalika.
Methali nyingi, kwa mfano, huonya dhidi ya matendo maovu kwa nia ya kukuza
maadili.
(i) Tamaa mbele mauti nyuma - huonya dhidi ya tamaa.
(ii) Mgaagaa na upwa hali wali mkavu —- huhimiza bidii.
(iii) Ndugu mui heri kuwa naye — huhimiza udugu.
Hadithi za kimapokeo pia hutumiwa kufunza maadili. Mathalani, ngano za mhusika fisi
huonya dhidi ya tamaa. Ngano za kiayari nazo huonya dhidi ya ulaghai, usaliti, ujinga
au utegemezi. Katika novela Kipendacho Roho ya Pauline Kyovi, Nyanya anawahadithia
wajukuu wake hadithi ya Kadzo na Mazimwi ili kuwaonya dhidi ya kuhadaiwa kuhusu
mapenzi na ndoa. Hadithi hii pia inawaonya dhidi ya kuwaamini watu wasiowafahamu.
(Gi) Fasihi huunganisha na kuibua hisia za kizalendo au utaifa. Kupitia kwa nyimbo za
kisiasa kama vile wimbo wa taifa, kwa mfano, wanajamii huhamasishwa kuungana
pamoja na kuitetea na kuijenga nchi yao. Ufuatao ni mfano wa wimbo unaohimiza
uzalendo:

Ewe Kenya nchi yangu


Ewe Kenya mama yangu
Ewe Kenya baba yangu
Ewe Kenya kaka yangu
Sitakuacha milele

(Wimbo wa marehemu Kakai Kilonzo)

Wimbo huu unalenga kuibua hisia za kizalendo. Mifano ya tungo zenye dhima hii
huweza kupatikana katika tamthilia, riwaya na vipera vingine vya fasihi.
Na Fasihi huhifadhi historia ya jamii. Tanzu kama vile visakale na visasili hueleza historia
au asili ya jamii na mambo au vitu vinavyopatikana katika jamii hiyo. Tanzu za fasihi
andishi pia huhifadhi historia ya jamii kimaandishi. Mathalani, tamthilia ya Kinjeketile
ni hifadhi ya vita vya Majimaji nchini Tanzania (1905 — 1907) na hali ilivyokuwa chini
ya utawala wa Kijerumani.
mai
(k) Fasihi hupumbaza. Fasihi bora ni ile inayoathiri hisia za binadamu. Fasihi huweza
kuchekesha na kuliza wakati mmoja. Watu wanapotazama au kusoma kazi fulani ya |
fasihi, huathirika na hata wakalia.

1. (a) Fafanua maana ya sanaa.


(b) Taja mifano mingine mitatu ya sanaa mbali na fasihi.
(c) Huku ukitoa mifano, thibitisha kuwa fasihi ni sanaa.
2. Andika mfano mmoja mmoja wa kipera au utanzu wa fasihi unaotumiwa |
kutekeleza dhima zifuatazo:
(a) Kuelezea imani za jamii
(b) Kukuza ujasiri wa kuzungumza hadharani
(c) Kurahisisha kazi.
3. “Jamii ndiyo huipa fasihi sura yake. Jadili.

Makundi ya fasihi
Fasihi imegawanywa katika makundi mawili makuu kulingana na jinsi inavyowasilishwa
na kuhifadhiwa.

1. Fasihi simulizi
Hii ni fasihi ambayo hubuniwa na kuhifadhiwa akilini. Fasihi simulizi huwasilishwa na
kusambazwa kwa masimulizi, mazungumzo ya kisanaa, kuimba, kughani, kuigiza na
kukariri kwa hadhira hai. Fasihi simulizi imegawika katika tanzu zifuatazo: hadithi,
semi, ushairi, maigizo na mazungumzo.

2. Fasihi andishi
Fasihi andishi ni fasihi ambayo huhifadhiwa katika maandishi na kusambazwa kupitia
kwa maandishi. Fasihi andishi imegawanywa katika tanzu zifuatazo: riwaya, tamthilia,
ushairi, novela, hadithi fupi na hadithi za watoto.

Tofauti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi


(a) Fasihi simulizi huhifadhiwa akilini na kusambazwa kwa njia ya mdomo ilhali fasihi |
andishi huhifadhiwa kwenye maandishi na kusambazwa kwa njia ya maandishi. Ngano
kwa kawaida hutambwa, lakini riwaya huandikwa. Nyimbo huimbwa lakini mashairi
andishi huandikwa.
(b) Fasihi simulizi huwasilishwa kwa hadhira hai. Fanani hukabiliana ana kwa ana
na
hadhira. Vitendawili, kwa mfano, hutegwa moja kwa moja kwa hadhira inayotarajiwa

o
kuvitegua papo hapo. Kwa upande mwingine, fasihi andishi kwa kawaida huwasilishwa
kupitia kwa maandishi. Mwandishi wa riwaya hana fursa ya kuonana na wasomaji wa
riwaya yake ana kwa ana.
(c) Hadhira ya fasihi simulizi ni tendi. Huchangia katika uwasilishaji kwa kuuliza na kujibu
maswali, kuimba ama kucheza na kupiga makofi kwa kushangilia. Huonyesha taathira
ya utungo utaowasilishwa kwa hisia zao kwa kucheka au kuhuzunika. Katika ngoma
ama utegaji na uteguaji wa vitendawili, hadhira ni washiriki. Hadhira ya fasihi andishi
kwa upande mwingine haiwezi kuwa tendi (ni tuli). Haiwezi kumwuliza mwandishi
maswali wala haiwezi kushiriki wakati mwandishi anapoandika. Hadhira hushirikishwa
katika kusoma kurasa za kitabu zilizokwisha kuandikwa.
(d) Hadhira ya fasihi simulizi ni pana kuliko ya fasihi andishi. Fasihi simulizi huweza
kupokewa na hata wale wasiojua kusoma na kuandika. Fasihi andishi huwafikia tu
wale wanaojua kusoma na kuandika.
(e) Fasihi simulizi ni mali ya jamii. Haimilikiwi na fanani mahususi, tofauti na fasihi
andishi ambayo ni mali ya mwandishi au waandishi binafsi. Visasili huhusishwa na,
jamii wala si mtu binafsi, ilhali riwaya au tamthilia ni mali ya mwandishi na ndiye
mmiliki wa maandishi hayo.
(£) Fasihi simulizi ina uwezo mkubwa wa kubadilika kimaudhui na kimtindo kutegemea
hadhira kuliko fasihi andishi. Fanani anaweza kubadilisha mtindo wa uwasilishaji,
badala ya kukariri, anaweza kuimba shairi. Anaweza kurahisisha lugha na kubadilisha
baadhi ya maudhui, akaongeza mengine ama kuyapuuza mengine. Msanii wa fasihi
andishi hana nafasi ya kuifanyia mabadiliko kazi yake baada ya kuchapishwa hadi pale
toleo jipya la kazi hiyo litakapotolewa. Kwa vile hakabiliani ana kwa ana na hadhira
yake, hawezi kujua maoni yao, hivyo hawezi kujirekebisha moja kwa moja.
(g) Yaliyomo katika fasihi simulizi huweza kusahaulika kwa urahisi, yakafisidiwa au
yakavurugika. Kwa sababu ya kuhifadhiwa ubongoni na kupitishwa kwa mdomo,
kudumu kwake hutegemea kumbukumbu ya wasanii mbalimbali. Pia, fanani anaweza
kufa au akarukwa na akili au hata akasahau mtiririko wenyewe. Ikiwa msanii atasahau
au kurukwa na akili, yaliyomo katika utungo asilia huenda yasidumu; yatabadilika.
Fasihi andishi ina uwezo zaidi wa kudumu kwani imehifadhiwa katika maandishi
ambayo huweza kusomwa na vizazi vingi kwa muda mrefu bila kufutika.
(h) Fasihisimulizi hutolewa katika vipindi (nyakati) na mahali maalumu. Ngano hutambwa
jioni kwenye nyumba za watu. Matambiko hufanyiwa katika sehemu maalumu. Miviga
kama vile upashaji tohara hutokea katika vipindi maalumu vya mwaka kama vile
wakati wa mavuno. Msomaji wa fasihi andishi hafungwi na mazingira ya wakati wala
mahali. Huweza kusoma wakati wowote na mahali popote.
(i) Uwasilishaji wa fasihi simulizi hutegemea viziada-lugha kama vile ishara za uso, mavazi,
miondoko, toni na hisia za hadhira. Katika fasihi andishi, mwandishi anategemea ujuzi
wake wa lugha kuwasilisha ujumbe wake kimaandishi. Hana nafasi ya kuwaigizia watu

o
sauti yake wala sauti za wahusika hazisikiki. Hata katika tamthilia, nafasi ya wahusika
wa hadithini huigizwa na wahusika wengine — wa mchezoni. Vivyo hivyo, mavazi ya
mwandishi hayawezi kuchangia katika uwasilishaji kwani hayupo pamoja na hadhira.
Ubora wa kazi yake hutegemea zaidi tamathali za usemi na ujuzi wa lugha.
D Fasihi simulizi ina historia ndefu (ni kongwe) kuliko fasihi andishi. Fasihi simulizi
ilianza pamoja na binadamu ilhali fasihi andishi ilianza baada ya kubuniwa kwa
maandishi. ;
(k) Wahusika katika fasihi simulizi kwa kawaida huwa binadamu, wanyama, mazimwi,
majini, miungu, mashetani na vitu visivyo hai. Wahusika wa fasihi andishi kwa kawaida
huwa binadamu, japo kuna baadhi ya kazi ambazo zina wahusika wanyama na hata
mizimu.
() Mwasilishaji wa fasihi simulizi anaweza kuwa mhusika mmojawapo katika kazi ya
kifasihi. Hata hivyo, mwandishi kwa kawaida si mhusika katika riwaya au hadithi
anayoandika. Isipokuwa katika kazi zilizosimuliwa katika nafsi ya kwanza (tawasifu)
ambapo mwandishi (msimulizi) hushiriki matukio ya hadithini.
(m) Fasihi simulizi haihitaji maandalizi kabla ya kutolewa. Majigambo, kwa mfano,
"hutungwa papo hapo na kuwasilishwa kwa hadhira. Aidha, ngano huwasilishwa bila
maandalizi na fanani huweza kufaragua masimulizi yake. Fasihi andishi hata hivyo
huhitaji maandalizi ya kutunga na kuandika kwa kipindi kirefu kabla ya kuchapishwa
na kuwasilishwa kwa hadhira.
(n) Fasihi simulizi ina tanzu na vipera vingi kuliko fasihi andishi. Semi, hadithi, ushairi,
maonyesho na mazungumzo yana vipera vingi ambatani ilhali fasihi andishi ina tanzu
kama vile riwaya, tamthilia, ushairi, novela na hadithi fupi ambazo hazina vipera vingi.

(o) Kurithishwa kwa fasihi simulizi kuna ubunifu kuliko kurithishwa kwa fasihi andishi.
Kufaulu kwa kazi ya fasihi simulizi hutegemea zaidi ubunifu wa fanani. Fanani ana
uhuru wa kubuni upya mtindo wa kuwasilisha kazi yake. Badala ya kutumia ngano,
fanani anaweza kutumia fani ya ushairi kama vile nyimbo. Fasihi andishi ikiandikwa
kwa mtindo fulani kama vile wa riwaya, huwa inabaki hivyo; itarithishwa vivyo hivyo
kwa vizazi vyote. Hata hivyo, baadhi ya riwaya huweza kuigizwa.

Athari za fasihi simulizi katika fasihi andishi


Fasihi simulizi imeathiri fasihi andishi kifani (kwa kuzingatia mbinu za uwasilishaji) na
kimaudhui (yaliyomo). Athari hizi zinaweza kuonekana katika mifano ifuatayo:

(a) Maudhui na dhamira


Kuna mfanano mkubwa kati ya maudhui katika fasihi andishi na fasihi simulizi. Masuala
Mengi ambayo yanashughulikiwa na tungo za fasihi andishi yamekwisha kujadiliwa
katika
fasihi simulizi. Kile ambacho fasihi andishi inafanya ni kuongeza masuala mapya kutokana
Na uchangamano wa jamii ya kisasa. Dhana ya majaaliwa, kwa mfano, hujitokeza sana
katika kazi za kinathari za fasihi simulizi. Katika baadhi ya ngano, tunapata watu ambao,
kupitia kwa majaaliwa, wanatajirika kimiujiza baada ya kuwa maskini. Majaaliwa ni uwezo
wa Mungu. Wazo la majaaliwa linajitokeza katika tamthilia kama vile Mfalme Edipode
ambapo Edipode (Mhusika mkuu) anajaribu sana kukimbia utabiri kwamba angemuua
baba yake na kumwoa mamake mzazi. Mwishoni mwa tamthilia, utabiri huu unatokea na
hivyo majaaliwa yanatimia. Maudhui ya asasi ya ndoa, nafasi ya wanawake katika jamii,
siasa, mapenzi na ushirikina ni mifano zaidi ya maudhui katika fasihi simulizi ambayo
yamejitokeza katika fasihi andishi.
Jukumu kubwa la kijamii la fasihi simulizi ni kuadilisha. Ngano, semi, nyimbo na mawaidha
ni baadhi ya tungo za fasihi simulizi zilizotumiwa kuadilisha. Ngano inayohusu kisa cha
fisi kumkosa ndama kwa kuila kamba iliyokuwa imemfunga ndama, ni mfano wa ngano
inayotahadharisha kujiepusha na tamaa na ujinga.
Dhamira hii ya kuadilisha inajitokeza katika tungo za fasihi andishi kama vile katika riwaya
ya Adili na Nduguze ya Shaaban Robert ambapo ndugu zake Adili wanageuzwa kuwa nyani
kama adhabu kwa kumdhulumu Adili. j

(b) Nyenzo na malighafi


Easihi simulizi na fasihi andishi hutumia lugha kuwasilisha mawazo ya binadamu. Fasihi
simulizi ndiyo ya kwanza kutumia lugha kiufundi kama malighafi yake. Lugha ilitumiwa kwa
njia ya methali na fani nyingine kama vile vitendawili, nyimbo na maghani. Vivyo hivyo,
fasihi andishi kama vile riwaya iliibuka kimaandishi kwa kutumia lugha kwa ufundi kama
malighafi. Tanzu za kimaandishi kama vile tamthilia, riwaya, hadithi fupi na hata mashairi
hutumia tamathali za semi kama vile methali, nahau, tashbihi na jazanda.

(c) Usimulizi
Msingi wa fasihi simulizi ni masimulizi. Kwa mfano, tendi, majigambo, ngano na rara
huwasilishwa kwa masimulizi. Fasihi andishi ni mwendelezo wa fasihi simulizi. Riwaya
kama vile Lila na Fila ya Kiimbila na Kipendacho Roho ya Pauline Kyovi zimeandikwa kwa
mtindo wa ngano za kimapokeo; hali inayoonyesha athari za tanzu za fasihi simulizi kwa
fasihi andishi. Katika tungo za kinathari za fasihi simulizi, fanani husimulia hadithi katika
nafsi ya tatu. Kazi nyingi za fasihi andishi za kinathari zimetumia nafsi hii hii ya tatu.

(d) Fani
Fani ni mbinu anazotumia msanii kuwasilisha maudhui. Kuna vipengele vingi vya fani
katika fasihi simulizi vinavyojitokeza katika fasihi andishi. Baadhi ya vipengele hivi ni:
(i) Ploti: Tanzu za kinathari za fasihi simulizi (ngano, visasili, mighani) huwa na ploti
sahili au nyepesi. Sifa hii pia inajitokeza katika baadhi ya riwaya za Kiswahili kama
vile Heri Subira ya Omar Babu na Siku Njema ya Ken Walibora ambazo ni nyepesi
kueleweka.
za
(ii) Wahusika: Fasihi simulizi pia imeathiri fasihi andishi kwa upande wa wahusika. Kama
tulivyotaja awali, fasihi simulizi hutumia wahusika kama vile binadamu, wanyama,
mizuka, mazimwi na viumbe visivyo hai. Fasihi andishi nayo hutumia wahusika wa
aina mbalimbali kuwasilisha ujumbe. Riwaya kama vile Shamba la Wanyama ya George
Orwell na Lila na Fila ya Kiimbila zina wahusika wanyama ambao wanatenda matendo
ya kibinadamu. Aidha, sifa za wahusika kushikilia nafasi zaidi ya moja katika tamthilia
inatokana na sifa za wahusika katika fasihi simulizi ambapo fanani na hadhira huweza
kuwa washiriki katika hadithi au kipera kinachowasilishwa.

| (iii) Nyimbo: Mtambaji wa ngano za fasihi simulizi hutumia nyimbo katika usimulizi.
Vivyo hivyo, baadhi ya kazi za fasihi andishi kama vile tamthilia hutumia nyimbo.
Katika tamthilia ya Kitumbua Kimeingia Mchanga, S. A.Mohammed anatumia nyimbo
kuwasilisha maudhui yake.
(iv) Fantasia: Fantasia ni sifa nyingine ambayo hupatikana katika ngano, visasili na
mighani. Sifa hii pia hupatikana katika baadhi ya tungo za fasihi andishi. Zipo
riwaya za Kiswahili ambazo zina matukio ambayo yamekiuka uhalisia. Kuwepo kwa
wahusika wasio wa kawaida kama vile wanyama, samaki, mizimu na mazimwi katika
fasihi simulizi na fasihi andishi ni mfano wa fantasia. Matendo yasiyo ya kawaida
yanapatikana katika baadhi ya riwaya. Mathalani, katika Rosa Mistika, Kezilahabi
amewasawiri wahusika Rosa na Zakaria wakiwa mbinguni mbele ya hukumu ya Mungu.
Haya ni mandhari yasiyo ya kawaida.
(v) Safari: Tungo za kinathari za fasihi simulizi huwasawiri wahusika wakisafiri nchi za
mbali. Ngano za mashujaa husawiri mashujaa wakisafiri mbali kutafuta masuluhisho
kwa matatizo yanayozikumba jamii zao. Baadhi ya riwaya pia huwa na kipengele cha
safari kama vile Kusadikika, ambapo wajumbe wanasafiri nchi mbalimbali kutafuta
suluhisho kwa matatizo yanayoikumba nchi ya Kusadikika.

(e) Utendaji
Fasihi simulizi ni tendi. Vivyo hivyo, upo uwezekano wa kutenda fasihi andishi kwa kutumia
mbinu za fasihi simulizi. Tamthilia huigizwa jukwaani, tendi nyingi huimbwa, ngonjera
huambatanishwa na vitendo, na riwaya pia huweza kuigizwa kama sinema.

Fasihi andishi ni utanzu unaojitegemea.” Jadili.


'Sifa kuu inayoitofautisha fasihi simulizi na fasihi andishi ni uwasilishaji.”
Jadili.
'Fasihi ni moja tu.' Jadili kwa kutoa mifano.
Fafanua sifa za kimsingi zinazoifanya fasihi simulizi kuwa hai zaidi kuliko
fasihi andishi.
-

Fasihi Simulizi

Utangulizi
Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo huwasilishwa kwa mdomo. Kama tulivyotangulia
kusema, fasihi simulizi hubuniwa na kuhifadhiwa katika akili ya binadamu.

Vipengele muhimu katika uwasilishaji wa fasihi simulizi


(a) Fanani/Msanii: Fanani ndiye anayetunga na kuwasilisha utungo wa fasihi simulizi
kama vile ngano, shairi ama kitendawili.
(b) Hadhira: Hawa ni wasikilizaji na watazamaji wa fasihi simulizi.
(c) Kipera cha fasihi simulizi: Kipera ni utungo wa fasihi simulizi uiiaswililishwa kwa
hadhira. Ngano, mighani na hekaya ni vipera vya hadithi ilhali methali, vitendawili
na misimu ni vipera vya utanzu wa semi.
(d) Mandhari/Mazingira: Mandhari ni mahali, hali na wakati ambapo sanaa ya fasihi
- simulizi hutendwa. Ngano hutambwa jioni ndani au nje nyumba za watu.
(e) Shughuli ya kijamii ambamo utungo huibuka: Utanzu wa fasihi simulizi hauibuki
vivi hivi tu. Lazima kuwe na tukio au kiini cha utanzu huo ambacho ni chemchemi yake.
Mbolezi, kwa mfano, zilitokana na kuwapo kwa majanga katika jamii yaliyopelekea
watu kutunga nyimbo ili kuimba katika hali hii. Vivyo hivyo, nyimbo zinazoimbwa
jandoni na harusini zilitungwa kuadhimisha shughuli husika.
(£) Lugha: Lugha ndiyo malighafi ya fasihi. Lugha katika fasihi simulizi huteuliwa kwa
usanii mkubwa ili kuleta mguso, mnato na mvuto kwa hadhira. Tamathali za usemi
kama vile methali, tashbihi, sitiari, tabaini, tanakuzi, kej eli, tashihisi na nahau
hutumika. Masimulizi ya fasihi simulizi hayategemei lugha ya maneno pekee bali
hutegemea pia viziada-lugha kama vile sauti za miguno, miondoko, ishara za uso na
viziada-lugha vingine.

5
ai

Sifa za fasihi simulizi


(a) Fasihi simulizi ina utendaji. Uwasilishaji wa fasihi simulizi hutegemea maneno na
vitendo. Mtambaji hutumia ishara za uso, miondoko ya mwili, miguno, toni na kiimbo
anapowasilisha hadithi. Vilevile, mtambaji anaweza kutumia tanakali za sauti kwa
kuiga milio ya viumbe fulani ili kusisitiza ujumbe wake.
Fasihi simulizi ni hai. Yaani ina hadhira hai. Kuna uhusiano wa ana kwa ana kati ya
fanani na hadhira yake. Katika uwasilishaji, fanani au msemaji anaweza kushirikisha
hadhira zaidi kwa kuwataka kujibu au kuitikia kwa kukariri kiitikio fulani. Iwapo
hadhira hairidhishwi na fanani, huweza kumpa maoni au mwitiko ambao utamwezesha
kuirekebisha na kuiboresha kazi yake papo hapo.

(c) Fasihi simulizi lazima iwe na mtendaji (fanani) kwa vile fasihi hii hutendwa. Mtendaji
anaweza kuwa mwimbaji kama ilivyo katika nyimbo, yeli/manju katika maghani,
mtambaji katika ngano au mpigaji ngoma katika ngomezi. Mtendaji katika fasihi
simulizi ana umuhimu wa kuuwasilisha utanzu wa fasihi simulizi na kuurithisha
kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Wakati mwingine fanani hubuni tungo za fasihi
simulizi na kuziwasilisha papo hapo. Katika majigambo, kwa mfano, anayejigamba
hubuni maghani na kuyawasilisha papo hapo.
(d) Fasihi simulizi huwa na mahali maalumu wa kutendea. Kwa mfano, sherehe za jando
huwa na mahali maalumu pa kufanyiwa. Matambiko hufanyiwa chini ya miti mikubwa
au pangoni na nyimbo huimbwa katika miktadha na mahali maalumu. Nyiso huimbwa
jandoni, kimai huimbwa katika shughuli za baharini kama vile uvuvi na ubaharia, na
mbolezi katika matanga.
(e) Fasihi simulizi ni mali ya jamii. Tanzu za fasihi simulizi zikishatendwa humilikiwa na
kila mwanajamii. Hakuna anayeweza kudai kwamba ndiye mmiliki wa ngano, methali,
vitendawili au tanzu nyingine za fasihi simulizi. Mathalani, methali ni tungo za jamii
wala si za mtu binafsi. Hata waliozikusanya na kuziandika vitabuni hawazimiliki.
(f) Wahusika katika fasihi simulizi huweza kuwa mazimwi, mizuka, wanyama, binadamu,
milima, mawe, ndege, miungu au vitu.
(g) Fasihi simulizi ina wakati maalumu wa kuwasilishwa. Ngano, kwa mfano, hutambwa
jioni baada ya shughuli za mchana. Nyiso huimbwa tu wakati vijana wanapokuwa
jandoni na ulumbi husemwa wakati watu wanapokutana kwa shughuli fulani rasmi.
(h) Fasihi simulizi huwa na athari ya utegemezi. Uhai wa fasihi simulizi hutegemea
uwezo wa fanani kuigiza. Wakati wa kutamba, fanani huiga vitendo vya mhusika
wa hadithini ili kuifanya kazi yake kuvutia. Kwa sababu vitendo haviwezi kuingizwa
katika maandishi, kule kutegemea fanani au mwasilishaji hufanya fasihi simulizi
kuwa chapwa inapoandikwa. Aidha, tanzu na vipera vya fasihi simulizi hutegemeana.
Hadithi hutegemea methali kutoa funzo. Vitendawili navyo hutegemea taswira katika
mafumbo.
(i) Fasihi simulizi ina historia ndefu. Fasihi simulizi ilianza pamoja na maisha ya
binadamu. Hata kabla ya kuvumbuliwa kwa maandishi, fasihi simulizi ilikuwepo.
(j) Fasihi simulizi huzaliwa, hukua na kufa. Fasihi simulizi huzuka au huzaliwa na jamii.
Hukua jinsi jamii inavyokua kwa kuongezewa tanzu mpya ili kufumbata matukio
mapya katika jamii. Hata wakati jamii inapokufa, fasihi simulizi nayo hufa kwa kukosa
kizazi cha kuiendeleza. Aidha, kwa vile fasihi simulizi huhifadhiwa bongoni, inaweza
kupotea fanani akifa au hata akirukwa na akili.
(k) Fasihi simulizi huchukua umbo mahususi. Tungo za fasihi simulizi zina maumbo
yenye sifa za kipekee. Ngano, kwa mfano, zina sifa ya mianzo na miishio ya kipekee.
Methali zina maumbo ambayo hayabadilishwi. Vitendawili navyo vina sifa ya mtindo
bainifu wa uwasilishaji.
(1) Fasihi simulizi hurithishwa na fanani kwa mdomo. Fanani ndiye huiwasilisha kwa
hadhira kwa kutumia fani kama vile methali, ngano, mawaidha au nyimbo. Kwa njia
hii, yeye hurithisha fasihi simulizi kwa vizazi na vizazi.
(m) Fasihi simulizi hubadilika kutegemea fanani, wakati na mazingira. Kila fanani ana
mtindo wake wa kuiwasilisha. Jinsi fasihi hii inavyopitishwa na mafanani mbalimbali
ndivyo inavyobadilika. Aidha, fasihi simulizi hubadilika kutegemea mazingira na
wakati. Tashbihi, kwa mfano, hubadilika kutegemea hali hizi. Mathalani weusi waweza
kulinganishwa na vitu mbalimbali kama vile -eusi kama makaa, -eusi kama mpingo
ama -eusi kama lami.

Dhima ya fasihi simulizi


(a) Huburudisha, huliwaza na kufurahisha.
Kwa kawaida, nyingi za tanzu za fasihi simulizi huwasilishwa usiku au jioni kama
njia ya kujiburudisha baada ya shughuli za kutwa. Aidha nyimbo za kazi huimbwa
kuwaondolea watu uchovu na ukinaifu wanapofanya kazi.

(b) Huhifadhi historia.


Fasihi simulizi hupokezwa kwa mdomo kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa njia
hii, historia ya jamii hupokezwa. Methali, nyimbo, hadithi, semi, miviga na tanzu zote
za fasihi simulizi huhifadhiwa katika jamii kwa kupokezwa.

(c) Hukuza uwezo wa kufikiri na kudadisi.

Tanzu kama hadithi, vitendawili, methali na mafumbo humhitaji binadamu kudadisi


mazingira yake na kufikiria kwa makini ili kupata jawabu, suluhisho mafunzo au maana
inayokusudiwa.
ai

(d) Fasihi simulizi ni nguzo ya kuunganisha watu.


Uwasilishaji wa fasihi simulizi huhitaji uhusika wa watu wawili au zaidi. Lazima watu
wawe pamoja katika kuimba ama kutega na kutegua vitendawili. Kule kuja pamoja
hufanya watu kujihisi kama kundi moja. Hivyo, umoja hujengeka.

(e) Hukuza lugha.


Lugha ndiyo malighafi ya fasihi simulizi. Kupitia kwa vipera kama vile ulumbi,
malumbano ya utani, misimu na utambaji wa hadithi, wanajamii hukuza uwezo wao
wa kutumia lugha kwa usanii katika mawasiliano.

(f) Hukuza uzalendo.


Kwa kushiriki katika miviga ya jando, harusi, ibada na matambiko, wanajamii
hujitambulisha na jamii. Huionea fahari jamii yao na hivyo uzalendo kujengeka.

(8) Hukuza ubunifu.

Katika kutamba hadithi, ulumbi na malumbano, wanajamii huimarisha vipawa vya


kubuni. Mtambaji bora ni yule anayeweza kuitamba hadithi upya kwa kutumia mtindo
mpya na hivyo kuipa hadithi uhai mpya. Kwa njia hii ubunifu kujengeka.

(h) Huwasaidia wanajamii kuielewa historia yao.


Mighani, visakale, tendi na rara huonyesha historia ya jamii husika. Masimulizi ya
mashujaa wa jamii hiyo, vita walivyopigana na hamahama za jamii hiyo huelezwa katika
baadhi ya vipera vya fasihi simulizi. Fasihi simulizi basi ni rekodi au kumbukumbu za
matukio katika jamii fulani.

(i) Fasihi simulizi huadilisha.


Katika hadithi, matendo mabaya hukashifiwa kwa kuadhibiwa kwa mhusika hasidi
(mui). Matendo mema huhimizwa kwa kuokolewa au kutuzwa kwa wahusika nguli.
Tanzu nyingine zinazoadilisha ni pamoja na methali, semi za tasfida, mawaidha,
nyimbo, miviga na baadhi ya vitendawili.
D Hutambulisha jamii na utamaduni wake.
Visasili, miviga na nyimbo husawiri imani na desturi za jamii husika. Kila jamii ina
upekee wake unaoandamana na utamaduni wake. Upekee huo hudhihirika katika
tanzu na vipera vya fasihi simulizi yake.
(k) Huelekeza jamii
Methali na ngano hutoa mwongozo kuhusu njia za kusuluhisha matatizo na zile za
kukabiliana na changamoto katika maisha. Mathalani, unaposema: Maji ukiyavulia
nguo huna budi kuyaoga, unampa mtu mshawasha wa kukabiliana na masuala magumu
aliyoanza kukabiliana nayo maishani mwake.

Co)
Mambo ambayo huchangia kubadilika kwa fasihi simulizi
Mojawapo ya sifa za fasihi simulizi ni hali yake ya kubadilika. Mabadiliko hayo husababishwa
na mambo yafuatayo:

(a) Hadhira
Fanani au mwasilishaji wa fasihi simulizi hukabiliana ana kwa ana na hadhira yake.
Hadhira inaweza kumwathiri akabadilisha mtindo wake wa uwasilishaji papo hapo.
Mtambaji anaweza kulazimika kutumia msamiati rahisi au mgumu kuliko ule uliokuwa
katika utungo wa awali ili kukidhi mahitaji ya hadhira yake kulingana na umri na
viwango vya uelewa wao.

(b) Muktadha wa wakati


Wakati huathiri yaliyomo, muundo na mtindo wa kazi ya fasihi simulizi. Kitendawili
kilichobuniwa wakati wa utawala wa Mzungu kinaweza kuwa na neno 'Mzungu', nacho
kilichobuniwa wakati wa Waarabu kikawa na neno 'Mwarabu'. Vitendawili vifuatavyo
vina maana sawa ingawa vimetumia maneno mawili tofauti: Mzungu amesimama kwa
mguu mmoja' — (mwavuli), “Mwarabu amesimama kwa mguu mmoja' — (mwavuli).

(c) Fanani
Kila fanani ana mtindo wake wa kisanii. Ana uwezo wa kuisimulia kazi kwa mtindo
mpya, na hivyo kuleta mabadiliko kifani. Kwa mfano, ngano moja inaweza kusimuliwa
kwa mitindo tofauti kulingana na mtindo nafsi wa mtambaji. Ploti hubaki kuwa ile
ile lakini pakawa na tofauti kuhusu yaliyomo na lugha.
Fanani husimulia anayokumbuka. Ikiwa kumbukumbu yake si nzuri, huenda
akasahau baadhi ya yaliyomo, hivyo kutoyarithisha kabisa. Kule kutorithisha huweza
kusababisha mabadiliko ya yaliyomo (maudhui) katika fasihi simulizi.

(d) Maendeleo katika maisha ya binadamu


Jinsi wakati unavyopita ndivyo maisha ya binadamu yanavyoendelea. Maendeleo ya
sayansi na teknolojia yanasababisha mwingiliano mkubwa katika jamii za binadamu.
Miingiliano hii huathiri maisha ya watu na vivyo hivyo mabadiliko katika fasihi
simulizi. Kwa sababu hii, jamii huenda ikaamua kurithisha tu yale inayoyaona
kuwa muhimu kwa kizazi kifuatacho na kuacha mengine. Kwa njia hii, tungo fulani
hubadilika kimaudhui na kutofautiana na tungo tangulizi za aina yake kwa kudondosha
baadhi ya maudhui au kuongeza mengine kulingana na hali inayomwathiri binadamu
katika maendeleo yake.
(e) Mazingira
Kadiri fasihi simulizi inavyoenea, hadhira yake pia hupanuka. Mambo ya msingi
yanayoathiri maisha ya binadamu hubaki yale yale licha ya mabadiliko katika
mazingira. Kifo, kwa mfano, hakibadiliki lakini visasili vinavyoeleza chanzo cha kifo
hubadilika kutegemea mazingira ya jamii mbalimbali.
aaa
Wahusika katika fasihi simulizi
miwa katika kazi ya kifasihi kuwasilisha
Wahusika ni viumbe wa kisanaa ambao hutu
masuala mbalimbali.
i makusudi ili kusawiri hali mbalimbali za
Wahusika huteuliwa na kufinyangwa na msani
maisha ya kijamii. Ikiwa msanii anataka kukashifu tamaa katika jamii, atamteua mhusika
mlafi kama vile fisi.

Aina za wahusika
Kuna aina mbalimbali za wahusika katika kazi za fasihi simulizi:

(a) Fanani
Fanani huhusika katika fasihi simulizi kwa kutunga utungo na kuuwasilisha kwa hadhira.
Ndiye msanii wa fasihi simulizi. Fanani anaweza kuwa msimulizi kama ilivyo katika ngano,
mwimbaji katika nyimbo, yeli au manju katika maghani, mtegaji katika vitendawili, mnasihi
(mtoaji nasaha) katika mawaidha, mpigaji ngoma katika ngomezi au mlumbi katika ulumbi.
Kwa kushiriki kwa njia hii, fanani huwa msimulizi na vilevile mhusika mshiriki katika
fasihi simulizi.
Yafuatayo ni majukumu ya fanani katika uwasilishaji wa fasihi simulizi:
(i) Ingawa fanani katika ngano si mmojawapo wa wahusika wa hadithini,
yeye huhusika katika uwasilishaji wa hadithi. Fanani haiwasilishi tu hadithi
bali huibadilisha kuwa sanaa tendwa kila anapoiwasilisha kwa hadhira hai.
Fanani hutenda mambo kama vile kuigiza sauti za wahusika wa hadithini pamoja
na kuashiria kwa uso (kutumia viziada-lugha) ili kufanikisha hadithi kwa kumsawiri
mhusika wa hadithi kama alivyo kwenye hadithi yenyewe.
(ii) Katika utegaji wa vitendawili, mtegaji (fanani) huhusika kwa kutoa kitendawili,
kupokea majibu na kuomba mji baada ya mteguaji kukosa jawabu.
(iii) Hutunga tungo na kuzisimulia au kuziwasilisha. Kwa mfano, anayejigamba hutunga
majigambo/vivugo na kuviigiza kwa hadhira hai.
(iv) Huwafunza vijana mbinu za kuiendeleza fasihi simulizi kupitia kwa uwasilishaji wake.
(v) Hutoa elimu kwa hadhira. Fanani ana jukumu la kuonya, kuarifu, kukashifu, kuelekeza,
kufahamisha, kukosoa na hata kuzindua hadhira yake.
(vi) Huendeleza utamaduni kwa kuupokeza kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kupitia kwa
utambaji wa ngano, mtambaji hurithisha mazoea ya utambaji na thamani za kijamii
zinazofumbatwa na ngano zenyewe kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
(vii)Hudumisha na kuendeleza lugha. Kadiri fanani anavyofinyanga lugha ndivyo
inavyopevuka na kukua. Fanani hubuni miundo mbalimbali ya lugha na kuipokeza.
Kwa jinsi hii huidumisha na kuiendeleza lugha.

o
(viii) Hushirikisha hadhira katika uwasilishaji wake. Kwa vile fasihi simulizi ni tendi na
ina hadhira hai, ni jukumu la mwasilishaji kuhakikisha kuwa hadhira yake inashiriki
vilivyo.

(b) Hadhira
Hadhira ya fasihi simulizi ni binadamu. Hawa ni wasikilizaji na watazamaji wa fasihi
simulizi.
Katika fasihi simulizi, wasikilizaji au watazamaji huchukua jukumu la uhusika pale ambapo
wanashiriki katika uwasilishaji kwa kuimba, kuuliza maswali kutegua vitendawili na kumpa
fanani ushauri kuhusu namna na wakati wa kuwasilisha utungo. Kwa kushiriki katika
nyimbo, hadhira inakuwa kama wahusika wa hadithini kwa kushiriki matendo ya wahusika
hao. Kwa hivyo, hadhira ya fasihi simulizi hutekeleza majukumu mawili: ni wasikilizaji au
watazamaji na pia ni wahusika washiriki katika fasihi simulizi.

(c) Wahusika wanyama


Wahusika wanyama hupatikana katika tungo kama vile hadithi. Kuna aina mbili za wahusika
wanyama:

(i) Wahusika wanyama watendao kama binadamu


Hawa ni wahusika wanyama ambao hupewa uwezo na sifa za kibinadamu. Wahusika wa
aina hii hupatikana katika ngano za kihurafa. Hutenda, husema, huoa, hushiriki katika
shughuli za kiuchumi kama vile kulima au kujenga mabwawa. Vilevile, hudhulumu
wanyama wengine jinsi binadamu awafanyiavyo binadamu wenzake. Katika ngano ya
“Sungura Mjanja', kwa mfano, wanyama wengine wanapoamua kuchimba kisima, Sungura
anatumia ujanja kuzinyonya nguvu za wanyama wenzake. Anakunywa maji kwa ulaghai
japo hakuchimba kisima.
Wahusika wanyama hupewa sifa mahususi kulingana na jamii. Zifuatazo ni baadhi ya sifa
zinazopewa wanyama katika jamii nyingi za Afrika Mashariki:
0 Fisi hupewa sifa ya tamaa, ujinga na woga.
0 Sungura hupewa sifa ya ujanja.
0 Simba ni mwenye nguvu na uwezo, lakini asiye na hekima.
o Ndovu ni mkubwa, mwenye fikira, lakini asiyeyapa mambo kipaumbele.
o Chui husawiriwa kama asiyeaminika, ambaye mara nyingi hulaghaiwa, pamoja
na kuwa mwenye hila.
eo Nyani na tumbili hupewa sifa ya ulaghai.
eo Mambani mnafiki na asiyeaminika.

WABEBA
eo Mbweha pia ni laghai.
eo Kinyonga husawiriwa kama asiyetandarukia mambo, asiye na msimamo na
anayebadilikabadilika.
o Kobe ni mwenda pole na mwenye makini. Wakati mwingine husawiriwa kama
mwenye hila.
Wahusika wanyama walio na sifa za kibinadamu hutumiwa kiistiara (kimafumbo) kukashifu
tabia hasi katika jamii. Katika mojawapo ya ngano, fisi anaamua kuila kamba inayomfunga
ndama kwanza ili amle ndama baadaye. Mwishowe fisi hadiriki kumla ndama kwa sababu
kamba inapokatika, ndama anatoroka. Hapa tunaonywa dhidi ya tamaa na kufanya mambo
bila tahadhari.
Ingawa wahusika wanyama hutenda kama binadamu, sifa zao za unyama hazipotei kabisa.
Sifa hizi hudumishwa kupitia kwa milio pamoja na miondoko yao.

(ii) Wahusika wanyama ambao hubaki kuwa wanyama tu


Hawa kwa kawaida hutokea pamoja na binadamu katika hadithi moja. Hutumiwa
kufanikisha shughuli za binadamu katika hadithi, jinsi wanavyotumika katika maisha ya
kawaida. Wanyama kama vile ngamia, farasi na punda hutumiwa katika kazi za uchukuzi.

(d) Wahusika binadamu


Wahusika binadamu hukuzwa kama binadamu. Wao hufinyangwa na kupewa sifa na
matendo mbalimbali kulingana na kisa kinachosimuliwa pamoja na dhamira ya kisa
chenyewe.
Wahusika binadamu wanaweza kuwa binadamu waliowahi kuishi (wa kihistoria) au wakawa
wa kubuni. Mifano ya wahusika wanaodhaniwa kuwa waliishi hupatikana katika mighani,
tendi na visakale. Katika baadhi ya hadithi, wahusika binadamu huonekana wakiingiliana
na wanyama na mazimwi katika shughuli mbalimbali. Katika hadithi nyingine walipewa
majina halisi kama vile Adili au walirejelewa kwa sifa zao, kwa mfano Mfalme Juha.
Wahusika wanapopewa majina kulingana na sifa zao, huwa ya kimajazi, na majina yenyewe
huchangia dhamira ya hadithi kwa jumla.

(e) Wahusika mazimwi


Mazimwi ni viumbe ambao si binadamu, si wanyama wala mashetani. Mazimwi huwa na
maumbile ya kiajabu. Yanaweza kuwa na jicho moja, vinywa viwili, vichwa saba au nusu
binadamu nusu mnyama. Pia wana uwezo wa kujibadilishabadilisha maumbo. Mara wana
Sura za binadamu wa kupendeza mara ni viumbe wasiotambulika.
Aghalabu huwa wahusika mahasidi, wenye tamaa iliyokithiri na tabia za kutisha. Wanaweza

Wanaweza kuumizana wenyewe kwa wenyewe. Wakati mwingine mazimwi yanaweza


kumhifadhi na kumtuza binadamu anayewapendeza.
(f) Wahusika vitu (viumbe visivyo hai)
Wakati mwingine hadithi, vitendawili, methali na mafumbo hutumia vitu kama vile vyungu,
magofu, vijaluba, vibuyu na mawe. Katika hadithi, vitu hivi husikika vikizungumza kama
binadamu. Mawe pia, katika baadhi ya hadithi, hutenda kama binadamu.
Katika jamii nyingi, wahusika ambao ni viumbe visivyo hai hubuniwa kwa misingi ya imani
za kidini.

(g) Wahusika mizimu


Wahusika mizimu ni roho za waliokufa ambazo huonekana zikitembea, kula na kuwaathiri
binadamu kwa matendo yao. :

(h) Wahusika miungu


Baadhi ya hadithi kama vile visasili huwa na wahusika miungu. Miungu huaminika kuwa na
uwezo mkubwa dhidi ya binadamu. Yale ambayo miungu inataka ndiyo hutendeka katika
maisha ya binadamu. Hadithi zilizo na wahusika miungu ni visasili na mighani. Kwa mfano:
0 asili ya kifo
0 asili ya kuumbwa kwa binadamu wa kwanza
0 asili ya kuumbwa kwa ulimwengu.

Tanzu za fasihi simulizi


Utanzu ni istilahi ya kifasihi ambayo hutumiwa kurejelea kundi la tungo ambazo
huwasilishwa kwa mtindo unaolingana (fani sawa), zina maudhui sawa au halihamasa
sawa. Methali na semi zimo katika utanzu mmoja kwa vile ni tungo fupi zinazotumika
kuwasilisha ujumbe uliofumbwa.
Tanzu za fasihi simulizi zinaweza kugawanywa katika makundi yafuatayo:
(a) Hadithi — Huu ni utanzu wa kinathari. Hadithi hujumuisha ngano za kubuni na
hadithi za kihistoria kama vile visasili, mighani na visakale.
(b) Ushairi simulizi — Utanzu huu unajumuisha tungo zinazotumia lugha ya mkato
yenye mpangilio maalumu wa maneno. Katika utanzu huu kuna nyimbo, maghani,
mashairi na ngonjera.
(c) Semi- Utanzu huu hujumuisha tungo fupi za kimafumbo zinazonuiwa kutoa mafunzo
maalumu kuhusu mwelekeo fulani wa maisha. Methali, vitendawili, nahau, misimu
na lakabu ni mifano ya semi.
(d) Maigizo —- Huuni utanzu wa sanaa ya maonyesho. Maigizo huwa na utendaji, uwanja
wa kutendea, watendaji na hadhira. Hujumuisha michezo ya watoto, michezo ya
jukwaani, ngonjera, majigambo au vivugo, miviga na ngoma. Katika kundi hilitunaweza
ai
kutia pia ngomezi ambayo japo baadhi ya wataalamu wanauchukua kama utanzu
unaojitegemea, ina uigizaji.
(e) Mazungumzo — Utanzu huu unahusu vipera vinavyotumia usemi au maongezi
kama
vile malumbano ya utani, ulumbi, maapizo na mawaidha. Hata hivyo vipera hivi pia
vimeainishwa kama vipera katika utanzu wa maigizo na baadhi ya waandishi.
Ni muhimu kutaja kuwa tanzu za fasihi simulizi huingiliana. Kwa mfano, mighani
na tendi zina maudhui sawa (zinahusu mashujaa au matukio ya kihistoria),
japo mighani ni hadithi na tendi ni tungo za kishairi. Aidha, majigambo
huweza kuainishwa kama ushairi lakini yakiigizwa yatawekwa katika utanzu
wa maonyesho.

1. Jadili mambo manne yanayochangia kubadilikabadilika kwa fasihi simulizi.


2. Andika sifa tano za fasihi simulizi.
3. (a) Eleza maana ya wahusika.
(b) Taja aina za wahusika ambao hupatikana katika hadithi za jamii yako.
4. Kuna umuhimu gani wa kufundisha fasihi simulizi shuleni?
5. Tunga ngano yenye wahusika wanyama.
6. Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali.

Zamani sana, mjukuu wangu, usidhani dunia ilikuwa na chochote. La


hasha!
Aliyekuwa anaishi katika ulimwengu mzima na juu ya mawingu alikuwa
Mulungu mwenyewe. Basi asubuhi moja Mulungu akatafakari na kuona kuwa
ni vyema kuumba kiumbe ambacho kitatamalaki ulimwenguni. Eeeh, mjukuu
wangu! Mulungu akamfinyanga binadamu kwa udongo uu huu uuonao.
Janadume lililojaa misuli likasimama kwa heba kuu. Kisha akalipulizia hewa
yake mapafuni mwake. Likaanza kupumua.
Kwisha hayo, Mulungu akapendezwa na alichokiumba lakini aliona
udhaifu fulani kwa nyamaume huyo. Alikuwa na upweke wa ajabu. Kwa
kumhurumia akautwaa ubavu wa nyamaume huyu, akauhuisha, akaupa
umbo
la kike; kisura chenyewe! Akamkabidhi, “Binadamu, mkeo huyu! Mwenzio
wa kupenda, sio wa kutumikisha.” Kwisha kuona jinsi walivyofurahi pamoja,
Mulungu akawapa na kishamba mle mle mbinguni.
Siku moja Binadamu na kisura wake waliamka asubuhi. Kutanabahi,
walikuwa duniani, jaala yao bila shaka imetimia. Mandhari hayo yalikuw
a
tofauti na paradiso walikokaa. Binadamu mabe ga yalimshuka. Alikuwa hajazoe
a
milima, mabonde, uyabisi wa ardhi na hewa, majabali ya kutisha, maeneo
makubwa ya maji ... Zaidi, hakuwa amezoea kujisaga kwa kazi.
Mulungu alimtazama Binadamu na kipenzi chake kutoka mbinguni.
Akawaonea huruma, akaona ni wajibu wake kushuka kuja kumfunza kiumbe
huyu stadi za kujitegemea maishani.
Mulungu aliandamana na Binadamu kiguu na njia hadi shambani.
Akamfunza kutifua udongo kwa majembe yakokotwayo na ng'ombe. Akamfunza
kufuga wanyama kama vile mbuzi, kondoo, ng'ombe na ndege kama vile kuku.
Akamkabidhi mapori yote na matunda ayatumie kwa manufaa yake. Binadamu
akaemewa. Hakujua kuparaga miti! Mulungu, kama mama aendeshavyo mtoto
tata, akamshika Binadamu mkono, akampandisha mtini.
“Basi hivyo ndivyo utakavyoyatunda matunda,” Mulungu akamwelekeza.
Mulungu akamwongoza Binadamu hadi bahari kuu. Akatwaa wavu na
mashua, akampa. Akawaamrisha papa na vidagaa, wakatii amri, wakaingia
wavuni. Binadamu akapata kitoweo cha siku kadha.
Mulungu akarudi mbinguni. Kabla ya kurudi akamuusia Binadamu atafute
mikakati ya kuyaboresha maisha yake. Binadamu hakuchelewa. Akavumbua
namna ya kusaga nafaka na kupika. Akavumbua mbinu za ujenzi, akajenga
nyumba wakajisetiri na mpenzi wake.
Binadamu aliamka siku moja na kumpata mkewe kajiinamia kwa jitimai.
Alipomwuliza kisa na maana, mama alisema kuwa tumbo lake lilikuwa na
jinyama lililokuwa likitembea! Binadamu akaangua kicheko kikubwa! Akasema
moyoni, “Kiumbe huyu ni limbukeni vipi?” Akakumbuka maneno ya Mulungu
kuwa kupitia kwa mkewe, ulimwengu mzima ungefurika watu. Binadamu
akamweleza mkewe agano la Mulungu. Naye mkewe, japo hakuyaelewa haya
vyema, akafurahi kwamba ndiye atakayeupa ulimwengu uhai.
Huo mjukuu wangu ndio uliokuwa mwanzo wa ulimwengu kutawaliwa
nabinadamu. Hivyo basi ndivyo hata wewe ulivyojipata ulimwenguni. Hadithi
yangu inaishia hapo.

Maswali
(a) Andika wahusika katika hadithi hii.
(b) Nini umuhimu wa hadithi za aina hii?
(c) Andika sifa za fasihi simulizi zinazojitokeza katika hadithi hii.
(d) Dondoa mbinu za kifasihi zilizotumiwa katika hadithi hii.
(e) Mtambaji wa hadithi hii amedokeza stadi (mbinu) mbalimbali za kuishi.
Andika zozote tano.
p
g'

Utanzu wa Hadithi

Utangulizi
Hadithi ni masimulizi yanayowasilishwa kwa lugha ya kinathari kuhusu watu, matukio
na mahali mbalimbali. Lugha nathari ni lugha iliyo na maelezo ya moja kwa moja katika
mfululizo wa sentensi zilizopangwa katika aya. Hadithi huweza kuwa ya kweli au ya kubuni.
Hadithi katika fasihi simulizi hutofautiana na hadithi za fasihi andishi, kwa sababu hadithi
za fasihi simulizi huwa na mtendaji na hadhira pamoja na pahali maalumu pa kutambia.

Sifa za hadithi
(a) Hadithi huwa na wahusika wa aina mbalimbali. Wahusika katika hadithi wanaweza
kuwa wahusika binadamu, wanyama, mazimwi, miti, mawe au miungu.

(b) Hadithi hueleza matukio kwa mpangilio wa moja kwa moja, kuanzia tukio la mwanzo
hadi la mwisho. Yaani, hadithi huwa na ploti sahili au nyepesi isiyo na mbinu
changamano kama vile hadithi ndani ya hadithi au mbinu rejeshi.
(c) Hutumia lugha ya kimaelezo au ya nathari.
(d) Hadithi huwa na mtendaji au fanani. Fanani anaweza kuiga wahusika katika hadithi
anayosimulia. Kwa mfano, anaweza kuiga jinsi fisi alivyokula. Anaweza kupandisha
au kushusha sauti kutegemea ukali wa kauli inayotolewa.
(e) Hadithi husimulia matukio ya kweli au ya kubuni yenye maadili. Hadithi za mazimwi,
kwa mfano, ni za kubuni. Aidha, hekaya na visasili ni hadithi za kubuni ilhali mighani
na visakale vina ukweli fulani.
(£) Kwa kawaida, hadithi hutambwa jioni baada ya shughuli za mchana, hususan baada ya
chakula chajioni au watu wanapongojea chakula chajioni kiive. Katika baadhi ya jamii,
utambaji hauruhusiwi mchana. Wanaojaribu kufanya hivyo hutishwa. Kwa mfano,
katika jamii ya Wagiriama, wanaohadithiana mchana hutishwa kuwa wataolewa na
fisi.
D

huwa hai. Yaani hushiriki


(8) Hadithi huwasilishwa kwa hadhira. Hadhira katika hadithi
na kuonana ana kwa ana na fanani. Aidha, hadhira katika hadithi inaweza kuwa
wahusika washiriki kwa kushiriki katika usimulizi.
(h) Hadithi huwa na pahali maalumu pa kutambia. Kwa kawaida hutambwa katika nyumba
za watu au chini ya mti fulani au uwanjani ambapo watu hukusanyika pamoja.
(i) Hadithi lazima iwe na mgogoro au tukio la kueleza. Mgogoro mkubwa unaojitokeza
ndio
katika hadithi za kimapokeo huwa kati ya uovu na wema. Mara nyingi wema
hushinda uovu ili kuwafunza wanajamii maadili. Aghalabu ngano ambazo husawiri
mazimwi yakiwatesa binadamu huishia kwa shujaa kuyaua mazimwi hayo na kurejesha
utulivu katika jamii husika.
za
J) Baadhi ya hadithi kama vile ngano, huwa na fomyula maalumu za ufunguzi na
kumalizia (Tazama kipera cha ngano ukurasa 25 — 28).

Dhima ya hadithi
Hadithi hutekeleza majukumu yafuatayo katika jamii:
katika hadithi ni kati
(a) Huielekeza jamii. Kama tulivyotaja hapo juu, mgogoro mkuu
vita
ya wema na uovu. Kwa kawaida wema huishia kushinda uovu. Hii huonyesha
vya jamii dhidi ya uovu. Kila hadithi huwa na funzo maalumu linalokusudiwa kutoa
mwongozo wa kimaadili kwa wanajamii.
ya kilimo,
(b) Hurithisha elimu ya jamii. Maarifa ya jamii ya kijadi kama vile sayansi
husimul iwa
uhunzi, mbinu za uwindaji, tiba, ukunga, sanaa ya uchongaji na ufinyanzi
katika ngano na kurithishwa kwa vizazi vya jamii.
kwa mdomo. Kwa sababu
(c) Hukuza uwezo wa kukumbuka. Fasihi simulizi hupokezwa
hii, watu hutarajiwa kuikumbuka hadithi ili kuweza kuitamba baadaye kwa wengine
na kwa njia hiyo kuipokeza kizazi baada ya kizazi.
(d)Huhalalisha baadhi ya desturi za jamii. Baadhi ya hadithi hueleza sababu ya kuwepo
Hueleza, kwa
kwa hali fulani. Visasili, kwa mfano, huhalalisha tabia na imani za kidini.
madhehebu
mfano, sababu za kuabudu milima, miti, majabali na sababu za kuwepo kwa
fulani. Baadhi ya visasili hueleza asili ya kifo kwa nia ya kuhalalisha kuwepo kwake.
wake.
Hadithi huonya, hushauri, huadibu na kunasihi jamii kupitia kwa wahusika
wa na
Wahusika katika hadithi husawiri tabia hasi na chanya. Tabia chanya huhimiz
hasi hupuuzwa na kulaaniwa.
Huhifadhi na kuendeleza historia ya jamii. Mashujaa na michango yao kwa jamii
hujulikana kupitia kwa hadithi za mighani ambayo hupitishwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine. Mashujaa waliopata kuathiri historia ya jamii zao ni kama Lwanda
u:
Magere wa Waluo, Fumo Liyongo wa Waswahili na Wangu wa Makeri wa Wakikuy
——

(8) Huhifadhi utamaduni wa jamii. Kupitia kwa hadithi ambazo hupitishwa kutoka kizazi
kimoja hadi kingine, tunaweza kuona mazoea, mila na utamaduni wa jamii hiyo.

(h) Ni kitambulisho cha jamii. Kila jamii huwa na hadithi zake ambazo husimulia tajriba
ya jamii hiyo. Kila jamii, kwa mfano, ina fasiri yake ya chanzo cha kifo. Ngano fulani
na mighani huhusishwa na jamii fulani. Mathalani, Wangu wa Makeri anahusishwa
na jamii ya Wakikuyu.
(i) Hukuza ujasiri wa kuzungumza hadharani. Hadithi hutambwa mbele ya hadhira.
Kadiri mtu anavyotamba ndivyo anavyoboresha uwezo wake wa kuzungumza mbele
ya watu.

(j) Huliwaza na kuburudisha baada ya shughuli za kazi. Hii ndiyo sababu hadithi
zilitambwa jioni. Zile zinazotambwa wakati kazi ikiendelea zilinuiwa kuondoa ukinaifu
na uchovu unaosababishwa na kazi.
(k) Hukuza ubunifu. Utambaji wa hadithi ni kipawa. Jinsi kipawa hiki kinavyopaliliwa
kupitia utambaji ndivyo kinavyokua.
(1) Hadithi huunganisha watu katika jamii. Watu wanapokuja pamoja kutambiana ngano
hujihisi kuwa jamii moja na ushirikiano hujengeka zaidi.

Usimulizi wa hadithi

Nafasi ya mtambaji/fanani katika uwasilishaji wa hadithi


Mtambaji huchukua nafasi mbili katika usimulizi wa hadithi:
(i) Ni mhusika mshiriki. Mtambaji wa hadithi huwa mshiriki katika hadithi kwa
kuonyesha matendo na hisia za wahusika katika hadithi kupitia kwa dayolojia igizi
au kupitia kwa ishara za usoni.
(ii) Ni msanii. Kwa kutamba hadithi, msimulizi huwa msanii katika fasihi simulizi.
Hutumia mbinu azijuazo kuibuni upya hadithi na kuifanya ivutie hadhira yake.

Sifa za mtambaj
Mtambaji wa hadithi huchukua nafasi muhimu sana katika kufanikisha uwasilishaji wa |
hadithi. Kwa sababu hii, mtambaji wa hadithi anafaa kuwa na sifa zifuatazo: |
(a) Mtambaji anapaswa kuwa na ubunifu wa kiwango cha juu. Aweze kuibuni upya hadithi
kila mara anapoitamba kwa hadhira mpya au katika muktadha mpya kwa njia ya
kuchangamsha. Ikiwa hadhira yake ni ya watoto ataongeza masuala ambayo yanapendwa
Zaidi na watoto kama vile ishara za uso, miondoko na mabadiliko ya sauti au mchezo wa
maneno na sauti. |
(b) Mtambaji anapaswa kuijua hadhira yake na mahitaji yake pamoja na kiwango chao cha
elimu au tajriba yao maishani. Hili litamwezesha kubadilisha mtindo wa uwasilishaji
ili kuwafaa wale anaowasimulia. Kama ni watoto, atatumia lugha rahisi na yenye
vichekesho vinavyopendwa na watoto. Aidha, sharti aelewe hulka za hadhira yake
kama vile nini huwachukiza, huwachangamsha au kuwavutia.
(o) Mtambaji anapaswa kuielewa na kuimudu lugha ya hadhira yake. Malighafi ya fasihi
simulizi ni lugha. Ni muhimu mtambaji afahamu kiwango kikubwa cha msamiati wa
lugha anayotumia ili aweze kuitumia lugha hiyo kwa wepesi katika utambaji.
(4) Anapaswa kuyaelewa mazingira ya hadhira yake na kutoa mifano inayofahamika na
hadhira kutoka kwayo. Ikiwa hadithi inahusu mfalme, na katika mazingira ya hadhira
yake pana rais, mtambaji anaweza kutoa mfano wa rais. Hili litawafanya wasikilizaji
wake kuelewa dhana ya ufalme. Inabidi pia afahamu masuala ibuka katika jamii ili
aweze kuyashughulikia katika masimulizi yake.
(e) Anapaswa kuwa jasiri wa kuweza kuzungumza hadharani. Mtambaji hastahili kuona
haya kuzungumzia masuala ya aibu inapobidi. Pia anahitajika kuwa na ukakamavu
wa kusimama mbele ya hadhira na kuihadithia.

(£) Anapaswa kuujua utamaduni wa hadhira yake ili kuepuka kutumia maneno au ishara
zinazoweza kuvuruga mawasiliano. Aweze kutoa ujumbe kwa njia inayokubalika na
utamaduni wa jamii.
ya kuunda au
(8) Mtambaji anapaswa kuwa na uwezo wa ufaraguzi. Ufaraguzi ni hali
kuigeuza kazi ya fasihi simulizi papo hapo na kuiwasilisha kwa hadhira. Mtambaji
basi anapaswa kuwa na uwezo wa kubadilisha sauti, kuigiza na kutumia viziada-lugha
kutegemea hadhira na muktadha.
(h) Mtambaji bora huwa mcheshi. Hili humwezesha kuichangamsha hadhira yake na
kunasa makini yao. Ucheshi hata hivyo hutegemea hadhira. Hadhira ya watu wazima
itafurahishwa na lugha inayoghushi kiucheshi kuliko hadhira ya watoto.
Gi) Mtambaji anapaswa kuwa na uwezo wa kuishirikisha hadhira yake kwa kuiuliza
maswali ya balagha na kuishirikisha katika nyimbo. Hili litakinga dhidi ya ukinaifu.
Pia litampa fursa ya kujirekebisha kutokana na mwitiko wa hadhira.
J) Anastahiki kuwa mbaraza anayeingiliana vyema na watu. Hili humfanya kuvutia
hadhira.

1. “Kufanikiwa kwa uwasilishaji wa hadithi hutegemea fanani.” Thibitisha.


2. Kwa nini hadithi zilitambwa katika jamii za Kiafrika? Toa sababu kumi.
3. Je, ni kina nani:
(a) wanaotamba hadithi katika jamii yako?
(b) wanaotambiwa hadithi katika jamii yako?
4. Toa mfano mmoja wa:
(a) hadithi ya kubuni (b) hadithi ya kihistoria.
Vipera vya hadithi
Hizi ni aina mbalimbali za tungo zinazosimuliwa kama hadithi katika fasihi simulizi. Vipera
vingi vya hadithi huingiliana na wakati mwingine ni vigumu kuchora mpaka kati ya kipera
kimoja na kingine. Kwa mfano, hurafa ni hadithi zenye wahusika wanyama. Hurafa inaweza
kueleza asili ya uhusiano wa wanyama au maumbile yao. Hapa hurafa itakuwa ngano ya
usuli. Aidha, mighani na visakale ni hadithi zinazohusiana kwa sababu zote ni hadithi za
mashujaa za kihistoria.
Utanzu wa hadithi unaweza kuainishwa katika makundi mawili makuu:

(i) Hadithi za kubuni


Hadithi za kubuni ni visa vilivyotungwa na jamii fulani na kupokezwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine. Lengo la hadithi hizi ni kuadilisha. Ngano kama vile hurafa, istiara, ngano
za usuli na ngano za mashujaa ni baadhi ya tungo katika kundi hili.

(ii) Hadithi za kisalua au kihistoria


Hadithi za kihistoria zina misingi katika historia ya jamii. Hadithi hizi husimulia matukio
yaliyowahi kutendwa na wahusika waliowahi kuishi. Hata hivyo, matukio haya ya kihistoria
huongezewa chumvi au ubunifu ili kuyafanya yavutie zaidi. Mifano ya hadithi za kihistoria
ni kama vile mighani, visakale, tarihi, kumbukumbu, shajara na mapisi.

Ngano
Ngano ni hadithi za kimapokeo ambazo hutumia wahusika kama vile watu, wanyama,
miungu, mashetani, mizimu, miti na vitu visivyo hai kuelezea au kuonya kuhusu maisha.

Sifa za ngano
(a) Ngano huwa na fomyula maalumu - fomyula ya ufunguzi (mwanzo) na fomyula ya
kuhitimisha (mwisho). Mfano wa fomyula ya mwanzo ni:
“Hadithi! Hadithi!”
“Hadithi njoo!”
Mfano wa fomyula ya mwisho ni:
“Hadithi yangu inaishia hapo.” au “... wakaishi raha mustarehe.”
(b) Ngano ni hadithi za kimapokeo. Yaani, hurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
Watambaji mbalimbali huzipitisha ngano kwa vizazi tofautitofauti.
(c) Usimulizi wake huwa na urudiaji au ukariri mwingi wa maneno, sauti na vifungu vya
maneno, kwa mfano, “... zimwi likakimbia, likakimbia ...”.
RA
hai, mizimu,
(d) Ngano huwa na wahusika wanyama, binadamu, mazimwi, viumbe visivyo
miungu na hata mashetani. Wahusika hawa hupewa sifa za kibinadamu ili waweze
kutumiwa kuadilisha.
(e) Aghalabu ngano huwa na matumizi ya nyimbo ambazo ni kitulizo kwa hadhira.
Nyimbo huipunguzia hadhira mwemeo unaosababishwa na matukio ya hadithi na
pia kuwasilisha mafunzo muhimu. |

(£) Ploti yake huwa sahili. Ngano hazina matumizi ya mbinu nyingi kama mbinu rejeshi
ambazo huenda zikafanya ploti kuwa changamano.
(g) Ngano ni hadithi za mafunzo na ambazo humulika mtazamo wa jamii husika kuhusu
maisha. Ngano za kiayari, kwa mfano, huhimiza uaminifu.
ya
(h) Ngano huwa na matumizi mengi ya fantasia. Fantansia ni mambo ya ajabu au yasiyo
kawaida. Mfano wa fantasia ni binadamu kuruka kama ndege hewani, zimwi kumeza
watu na baadaye kuwatapika wote.
a
(i) Ngano huwa na kipengele au motifu ya safari. Mashujaa katika ngano za mashuja
husafiri nchi za mbali kutafuta masuluhisho kwa matatizo yanayozikumba jamii zao.
i
(j) Ngano huwa na upenyezi wa mtambaji. Upenyezi wa mtambaji ni hali ya mtambaj
kuingiza maneno yake au kutoa maoni kuhusu tukio au mhusika fulani katika hadithi.
kana
(k) Matukio katika ngano hayajikiti katika kipindi maalumu. Visa husimuliwa
kwamba vilitokea wakati uliopita bila kutaja wakati maalumu. Kwa mfano, “Zamani
sana ...” au “Hapo zamani za kale ...”

Fomyula katika ngano


Fomyula ni mtindo maalumu wa kufanya jambo. Fomyula katika ngano ni mtindo maalumu
wa kuanza na kumalizia ngano. Ngano za Kiafrika za kimapokeo huwa na fomyula maalumu
ya ufunguzi na ya kumalizia masimulizi:

(a) Fomyula ya ufunguzi:


Msimulizi: — Paukwa! |

Hadhira: Pakawa!
Msimulizi: —Hapo zamani za kale...
au
Msimulizi: —Paukwa!
Hadhira: Pakawa!
Msimulizi: Sahani!
Hadhira: Ya mchele!
Msimulizi: Giza!
Hadhira: La mwizi!
Msimulizi: Na kiboko je?
Hadhira: Cha mtoto mkorofi!
Msimulizi: Hapo zamani za kale...

Umuhimu wa fomyula ya ufunguzi


(i) Fomyula ya ufunguzi huvuta makini au usikivu wa hadhira. Mtambaji anaposema,
“Hadithi! Hadithi!” huwafanya wanaotambiwa kuwa tayari kusikiliza.
(ii) Hutambulisha au hutangaza mtambaji.

(iii) Huashiria mwanzo wa hadithi. Kwa mfano, katika jamii ya Wameru, mtambaji
husema “Jukia rugano” kumaanisha “Chukueni ngano,” kisha wanaotambiwa husema,
“Twajukia” yaani “Tumechukua” kuonyesha kwamba wamekubali kuhadithiwa na hapo
hadithi huanza.
(iv)Huweka mpaka kati ya ulimwengu halisi na ulimwengu wa hadithi. Huwatanabahisha
wasikilizaji kuwa sasa wameingia katika ulimwengu wa ubunifu. Kwa mfano,
mtambaji anaposema, Hapo zamani za kale, wasikilizaji wanasadikishwa kuwa mambo
yatakayotambwa ni ya kipindi cha zamani; hayawahusu moja kwa moja japo huenda
hadithi ikawa na wahusika wenye tabia kama zao.
(V) Fomyula ya ufunguzi hushirikisha au huleta hadhira na mtambaji pamoja. Mtambaji
anaposema: Hadithi! Hadithi! hadhira hujibu: Hadithi njoo! kuonyesha kwamba hadhira
iko pamoja na mtambaji.

(b) Fomyula ya kumalizia au ya kuhitimisha:


“ww Hadithi yangu inaishia hapo.”
“... Wakaishi raha mustarehe.”

Umuhimu wa fomyula ya kuhitimisha


(i) Fomyula ya mwisho huashiria mwisho wa ngano. Mtambaji anaposema Hadithi yangu
inaishia hapo, hadhira hujua kuwa ngano imeisha.
(ii) Hutangaza funzo kwa wasikilizaji. Ngano huweza kumalizika kwa methali au usemi
ambao ni muhtasari wa maadili katika ngano. Mtambaji anaweza kumalizia kwa
kusema, Kama ngano ni nzuri, uzuri wake ni wetu sote, kama ni mbaya ubaya wake ni .
wa yule tu aliyeibuni ngano yenyewe. Kiishio kama hiki kinasisitiza matendo mema;
kwamba ubaya haufai kuwaathiri wale ambao hawakuhusika kuusababisha.
(iii) Baadhi ya viishio huwapa wasikilizaji changamoto ya kuwa watambaji mashuhuri wa
ngano. Kimalizio kifuatacho kutoka kwa jamii ya Wakamba kinaapiza hadhira: Nivoya
wilingile na mwithe wa na kimbuva nakwa ngilingila na mwithe wa ilondu kwa maana ya
“Naomba ujizungushe kwa mkia wa bafe nami nijizungushe kwa mkia wa kondoo”.
Bafe ni aina ya nyoka mwenye sumu. Kondoo naye ana faida kwa binadamu. Hutupa
nyama na sufu. Hivyo, mtambaji anajiombea kuwa bora kuliko anayemsikiliza. Anampa
msikilizaji wake changamoto ya kujifunza kutamba ili aweze hata yeye kujizungusha
kwa mkia wa kondoo.
(iv) Fomyula ya mwisho humpisha mtambaji anayefuata. Tazama kimalizio kifuatacho cha
ngano ya Wakamba. “Wano wakwa wathelela vau. Nivoya ng'ombe syaku iye muthanga
na ndaka, nasyo syakwa iye nyeki ila nzeo”, yaani “Ngano yangu imeishia hapo. Naomba
ng'ombe wako wale mchanga na tope nao wangu wafaidi zile nyasi nzuri.” Kimalizio
hiki kinampa fursa mtambaji mwingine kuanza utambaji.
(v) Huitoa hadhira kutoka ulimwengu wa ubunifu na kuiashiria kuwa imerudishwa katika
ulimwengu halisi sasa.
(vi) Hupisha shughuli inayofuata ikiwa kipindi cha utambaji kimekwisha.
(vii)Ni kitulizo kwa hadhira ambayo sasa huacha kuwa makini. Huwaondolea wasikilizaji
taharuki kwa kuwapa suluhisho la mgogoro/mwisho wa mgogoro unaomkumba
mhusika mkuu. Kwa mfano: “Zimwi likasema likatwe dole gumba. Watu wote ambao
lilikuwa limemeza wakatoka.”

Fafanua maana ya ngano.


“Maadili ya ngano hufumbatwa katika fomyula yake.” Jadili.
Andika ngano fupi kutoka jamii yako.
SIANGA
(a) Tathmini umuhimu wa kuwatambia watoto ngano.
(b) Umepewa jukumu la kuwafundisha wanafunzi wa darasa la tatu kutamba
ngano. Fafanua mambo kumi utakayowaeleza wazingatie wanapotamba.

Aina za ngano
Ingawa wataalamu wamejaribu kuziainisha ngano, si rahisi kuzitenganisha kabisa. Ile
ambayo ingeonekana kuwa ngano ya usuli kwa kigezo kimoja inaweza kuwa ngano ya
mtanziko au hurafa kwa kigezo kingine. Ngano huweza kuainishwa kwa kutumia vigezo
vifuatavyo:

(a) Wahusika .
Ngano zinaweza kuainishwa kwa misingi ya wahusika wanaotenda matendo katika ngano
yenyewe. Kwa kufuata kigezo hiki, tuna ngano kama vile:
(i) Ngano za mazimwi na majitu
Hizi huwa na wahusika mazimwi au majitu.

(ii) Hurafa
Hurafa ni ngano ambazo wahusika wake ni wanyama lakini wanaowakilisha binadamu.

(iii) Hekaya
Wahusika wake ni binadamu wanaowakilisha tabia za binadamu wa aina hiyo katika
jamii. Kwa mfano, Abunuwasi katika Hekaya za Abunuwasi huwakilisha walaghai.
(iv) Ngano za mashujaa
Wahusika katika ngano za mashujaa ni binadamu waliotenda mambo ya kishujaa katika
jamii zao.

(b) Dhamira j
Kwa kuzingatia dhamira, ngano huweza kuainishwa kulingana na sababu, nia au lengo la
kutambwa kwake. Kwa kuzingatia kigezo hiki tunapata ngano zifuatazo:
(i) Ngano za kuadilisha
Kimsingi, ngano za kuadilisha hufunza tabia inayokubalika.
(ii) Ngano za usuli
Ngano hizi huonyesha asili ya tabia, maumbile, tabia, hali au mahusiano fulani.
(iii) Ngano za mtanziko
Ngano za mtanziko hulenga kukuza stadi ya kutathmini na kutoa uamuzi ufaao.
Ni muhimu kutaja hapa tena kuwa vigezo vya dhamira na wahusika ni mwongozo tu
wa kuainisha ngano ili kuzifanya zieleweke kwa urahisi. Aina hizi za ngano huingiliana.
Kwa mfano, ngano ya usuli inaweza kuwa na dhamira ya kuadilisha.

Ngano za mazimwi
Hizi ni ngano ambazo wahusika wake ni mazimwi. Mazimwi ni wahusika ambao wana uhai
lakini si binadamu, si wanyama, si miungu wala si mashetani. Kwa kawaida, mazimwini
wahusika walio na sifa za kutisha kiumbo, sura na matendo. Kwa mfano, zimwi linaweza
kuwa na urefu wa kufikia mbingu. Mazimwi ni zao la fikira za binadamu. Yaani ni viumbe
wa kufikirika tu.

Sifa za ngano za mazimwi

(a) SIA WAASI. Mazimwi husawiriwa kama wahusika mahasidi wenye tamaa na uovu

wenyewe li wenyewe. Msanii huwaumba mazimwi wkusadi kusha chuki ya


binadamu kwa maovu ambayo yanaweza kuangamiza jamii. Mazimwi ni viwakilishi
vya binadamu wanafiki, wenye tamaa na ubinafsi na wanaowadhulumu wenzao...
(b) Huwa na matumizi mengi ya fantasia.
Wahusika wake huweza kujigeuza
wakachukua sura ya binadamu; nusu
binadamu, nusu mnyama au wakachukua
umbo jingine la ajabu kama vile kuota mkia
au miguu mitatu.
(c) Mazimwi katika ngano za kimapokeo.
hutenda mambo kama binadamu na
huingiliana na binadamu katika shughuli
za kawaida. Huoa, hulima, hudhulumu
na wakati mwingine huweza kutuza
wanaowatii.
(d) Ngano za mazimwi hufunza maadili kama,
ilivyo katika ngano zote.
(e) Ngano za mazimwi pia huwa na motifu au
kipengele cha safari.

Mfano wa ngano ya mazimwi

Zamani sana katika kijiji cha Tima paliondokea sonara mmoja. Sonara huyu alikuwa
na mke mrembo ambaye alihusudiwa na walimwengu wote katika eneo hilo. Karibu
na kibanda chao palikuwa na msitu ambao ulisetiri mazimwi ya kila aina. Kila jioni
ungeyasikia mazimwi hayo yaking'ang'ania mawindo. Sonara na mkewe hawakwisha
kushangaa jinsi viumbe hawa walivyokithiri kwa tamaa.
Siku moja sonara aliondoka kijijini kwenda mbali kwa shughuli za ufuaji. Alimwacha
mkewe akiwa mjamzito. Mara tu baada ya kuondoka, uchungu wa uzazi ulibisha hodi.
Mama mtu akawa taabani, asiwe na mwombezi. Katika hali hii ya hamaniko, mama
mtu alishtukia kapata mkunga aliyeonekana mzuri na mpole ajabu. Mama akajawa na
furaha tele. Bahati iliyoje!
Mkunga akaingia kazini. Baada ya dakika chache, malaika, kitoto kichanga
kikahanikiza hewa ya asubuhi mbichi kwa kilio. Mama mtu alimshukuru mkunga kwa
usamaria wema. Laiti angalijua kuwa kajipagaza zigo lisilobebeka!
Mkunga huyo hakukawia. Akaingia ghalani, akachukua mtama, akasaga na kumpikia
mwanagenzi fuka. Mzazi, hamu ya kula hajapata bado, mkunga akamkabidhi bakuli la
uji. “Shika mke mzazi,” akasema. Hata kabla ya mama kutoa kauli, mkunga akabadilika
ghafla. Ile sauti ya upole ikabadilika kuwa mngurumo wa kutisha: “UKIKATAA, MIMI
NAENDA KUUNYWA!”. Kumbe yule mkunga alikuwa zimwi lililobugia uji pamoja na
bakuli! Mama alipoona hayo, vimbimbi vikamsimama kwa woga.
Kufikia jioni, njaa ilikuwa imemuuma mama na mtoto si haba. Yule mkunga-zimwi
akajigeuza binadamu na kuchinja mbuzi ili ampikie mama mzazi. Baada ya supu kuiva,
zimwi likaibeba pamoja na minofu na kumpelekea mama mzazi. Lakini hata kabla ya
kutua sufuria, lilikariri maneno yale yale: “UKIKATAA, MIMI NAENDA KUNYWA.”
Kwa kauli hiyo, likabugia nyama pamoja na sufuria. Mbuzi mzima akapata makao
ndani ya tumbo la zimwi! Mama na mtoto wake wakalala mataya yakigongana. Siku
tatu zilipita bila ya mama kupewa chakula chochote. Unyonge wa uzazi ukamvamia.
Kitoto nacho kikaendelea kudai haki.
Asubuhi moja Kasuku alipitia akitarajia kiamsha kinywa kama kawaida. Akampata
mke wa sahibu yake taabani. Baada ya mazungumzo mafupi na mama mtu, waliafikiana
kuwa ampelekee sonara ujumbe.
Kasuku alienda akatua juu ya mti uliokuwa karibu na kiwanda cha sonara. Akaimba:
Ewe sonara unayefua
Mke kajifungua
Unyonge wa uzazi wamliza
Tumbo la uzazi latekenya
Chango zamsokota
Kisa na maana
Chakula hapati
Mpishi hupikia tumbole
Zimwi huchumia chunguche
Kikawia hasara takufika
Ya kinda na mamaye.
Sonara alisikiliza wimbo huu kwa muda na ujumbe wake ukamgonga ndipo.
Akajihami na kufunga safari kurejea nyumbani. Alipofika, alimpata mkewe taabani,
mwili umenyong'onyea. Maghala yote yalikuwa yamefagiwa na zimwi lililokuwa
limejidai kuwa mfadhili na lililala nje ya ghala kwa mavuno ya shibe. Sonara alilidunga
mkuki likafia papo hapo. Ingawa Sonara alijuta kwa kutowazia hali ya mke wake tangu
awali, aliweza kuliangamiza zimwi. Hadithi yangu inaishia hapo.

Ukirejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


1. Taja wahusika katika ngano uliyoisoma. a
2. Fafanua sifa za:
(i) Zimwi (ii) Sonara.
3. Andika mafunzo yanayojitokeza katika ngano hii.
4. (a) Bainisha sifa za ngano za mazimwi zinazojitokeza katika hadithi
uliyoisoma.
(b) Eleza umuhimu wa wimbo uliotumiwa katika ngano hii.
5. Andika mfano wa ngano ya mazimwi kutoka jamii yako.

Oo
Hurafa

Hurafa ni ngano zenye wahusika wanyama ambao hupewa tabia za kibinadamu. Ni


hadithi za kiistiara kwa sababu huwakilisha matendo ya binadamu kwa njia fiche. Wasanii
huwatumia wanyama iliwasionekane kuwahujumu binadamu wenye tabia hasi moja kwa
moja.
Hurafa hupendwa sana na watoto kwa sababu huwa na ucheshi mwingi kutokana na tabia za
wanyama waliopewa sifa za kibinadamu. Hurafa ni kipera cha ngano kilicho maarufu sana
miongoni mwa Waafrika. Katika fasihi nyingi za Kiafrika, wahusika wanyama mashuhuri
sana ni sungura na fisi.
Ngano za hurafa zinaweza kugawanywa katika makundi mawili:
(i) Hurafa zinazoeleza asili ya tabia au mahusiano fulani ya wanyama.
(ii) Hurafa zinazoonyesha ujanja wa wanyama fulani kama vile sungura.

Sifa za hurafa
(a) Wahusika katika hurafa ni wanyama.

(b) Wanyama hupewa tabia za binadamu za kuweza kuzungumza na kufanya kazi


jinsi afanyavyo binadamu. Nafasi zinazochukuliwa na wahusika wanyama katika
hurafa husawiri tabia mahususi za baadhi ya wanajamii. Kwa mfano, ndovu na
simba huwakilisha wenye nguvu ambao hutumia uwezo wao kupata miradi yao na
kuwakandamiza wengine. Sungura naye huwakilisha binadamu ambaye hatumii nguvu
ila hutumia ujanja, werevu na mbinu bunifu za kujitoa katika matatizo. Fisi huwakilisha
binadamu mjinga mwenye tamaa na asiyeweza kutegemewa. Kinyonga huwakilisha
binadamu asiyechangamkia mambo na asiyeweza kutegemewa.
(c) Hurafa hutoa maadili na kuonya kwa njia ya kuchekesha na isiyoumiza. Kwa mfano,
mtu huweza kukashifu utawala dhalimu kwa kutumia kisa cha mnyama mkubwa
kushindwa na mnyama mdogo. Tabia hasi na uongozi mbaya huweza kukashifiwa
bila kuogopa kulaumiwa na kuadhibiwa. j
(d) Hurafa huwa na ucheshi mwingi. Ngano hizi hupendwa sana na watoto kwani
wanapoona wanyama wadogo kama vile sungura wakiwaadhibu wanyama wakubwa
kama vile ndovu, hujitambulisha na sungura na kuona kuwa hata yeye anaweza kutenda
kitendo cha ujanja na kuwaadhibu watu wakubwa.
(e) Hurafa hutoa matumaini kwa wanyonge kwamba japo kwa sasa huenda wakawa
wanadhulumiwa, wakitumia akili zao vyema wanaweza kufaulu kuyatatua matatizo
yao siku moja.
' Mfano wa hurafa
Zamani sana Paka na Mbwa waliishi peponi. Mungu alikuwa amewatunukia mapenzi
si haba. Nyumba yao ilikuwa imepambwa kwa vyombo vya dhahabu na vito vingine.
Bustani kubwa lilizunguka nyumba hiyo ya fahari. Matunda ya kila aina: si matikiti, si
maembe, si matufaha, si machungwa; yote yalijaa kochokocho mitini. Almuradi Paka na
Mbwa hawakupungukiwa na lolote. Wanyama wengine hawakuisha kuwaonea kijicho
wanyama hawa.
Siku moja, Malaika Mkuu mbinguni alikuwa na ujumbe kwa Mungu. Aliamka
asubuhi na mapema na kuwaita Paka na Mbwa ambao walikuwa wamejipambanua kama
watumishi waaminifu na kuwaambia, “Ndugu zangu, nina salamu muhimu ambazo
ningependa kuwakabidhi mmpelekee Mungu. Kwa vile ujumbe wenyewe ni mrefu,
nimeuandika na kuutia ndani ya bahasha hii. Basi nitakukabidhi ewe ndugu yangu Mbwa
bahasha hii. Ni sharti uitunze isije ikakuponyoka njiani.” Mbwa akachukua bahasha na
kuitia ndani ya mfuko wa shati lake. |
Kabla ya Paka na Mbwa kuondoka, Malaika Mkuu aliwaambia, “Pana jambo ambalo |
ningependa kuwatahadharisha nalo. Msizungumze na yeyote wala kula chochote hadi
mtakapofika kwenye kasri la Mungu.”
Maneno haya ya mwisho yalimwia Mbwa vigumu. Alijua kuwa yeye hakuwa
mzungumzaji kiasi hicho lakini kuambiwa asile chochote na hali safari hiyo ingewachukua
kutwa nzima! Alichojua, kama alivyojiwazia, ni kwamba hata Malaika Mkuu asingeweza
kuwa na stahamala ya kiwango hicho!
Safari ilianza saa moja asubuhi baada ya staftahi. Paka na Mbwa wakaandamana guu
mosi guu pili. Jua la utosi liliwapata hata kabla ya kufikia nusu ya safari. Njaa ilikuwa |
imeanza kuwauma, uchovu ukawa unawang'ata kama nge. Hata hivyo, walijipa moyo,
wakajiambia kuwa subira yao itavuta heri baada ya muda mfupi. |
Ghafla kama ajali, Sungura alitokea katika kichaka kilichokuwa karibu. Macho
ya Mbwa ndiyo yaliyokuwa ya kwanza kumtua sungura huyo. Moyo wake ukamzaini
kukitwaa kisungura hicho na kukonga roho yake. Mara alikumbuka onyo ambalo
walikuwa wamepewa na Malaika Mkuu. Mvutano mkali ulizuka katika nafsi yake, “Bwana
wewe una njaa, vipi utakiacha kitoweo ambacho kwa kweli kinakunyooshea mkono?”
Kwa upande mwingine dhamiri yake ilimuasa na kumwambia, “Mwenye pupa hadiriki
kula tamu, tuliza moyo wako, usikaidi amri ya mtumishi wa Mungu usije ukauma dole.”
Basi mjukuu wangu, Mbwa akawa hajifai kwa mgogoro huu wa nafsi. Mara uhayawani |
wake ulimvaa, akafyatuka kama mshale na kumhujumu Sungura. Akamla asimbakize
chochote! Kwisha kumla, akamwambia Paka, “Ndugu, tuendelee na safari, huenda hata Ji
wewe ukabahatika kuambulia angaa buli la maziwa.” |
Hatua chache mbele, Panya alitokea. Akajishaua mbele ya marafiki zetu hawa kana |
kwamba alitarajia posa kutoka kwa mmoja wao. Moyo wa Paka ulimpapa kwa tamaa ya

Oa
kutaka kulipiza kisasi kwa kiumbe huyu ambaye daima alizoea kuyahujumu maghala
ya mahindi. Paka akamtazama Panya kwa jicho la hasidi, akatayarisha mafumba yake
kwa vita. Lakini ghafla akakumbuka maneno ya Malaika Mkuu na kujiasa. Alimnyoshea
Panya kidole na kumwambia, “Laiti Malaika Mkuu asingekuwa amenionya dhidi ya kula
chochote, ningekufunza funzo la maisha.” Basi Panya akanusurika.
Sasa walikuwa wakilitazama kasri la Mungu. Kwa mbali, mbwa alikaza mboni zake
zaidi na kumwona Swara akija kwa madaha. Ziraili akamwingia, “Kaka Mbwa, natumai
unakumbuka walivyotwambia wahenga kuwa ngojangoja huumiza matumbo. Je, una hakika
gani kuwa baada ya kufikisha ujumbe utapewa hata tone la maji? Hamadi kibindoni bwana.
Faidi chajio ukionacho sasa.” Bila nadhari, Mbwa alimtwaa Swara na kumla shibe yake.
Jua lilipozama Paka na Mbwa walijipata nje ya lango la kasri. Mungu akatoka kwenye
chumba chake cha maongezi na kwenda kupokea salamu zake. Akamwuliza Mbwa, “Je,
safari ilikuwaje?” Mbwa akajibu, “Safari ilikuwa ndefu, lakini yenye mafanikio makubwa.
Niliweza kuwashika Sungura na Swara na kuwala. Njaa haikunidhili mno, ila bahasha
niliyopewa ilipotelea njiani.” Mungu akamjibu, “Subiri hapo nje ya lango. Nitakuita baada
ya kuzungumza na Paka.” Paka alipoulizwa, alijibu kwa sauti hafifu, “Safari ilikuwa ndefu
mno. Sikuweza kuzungumza na yeyote. Nilitaka kulipiza kisasi kwa Panya niliyekutana
naye ila sikuweza kwani Malaika Mkuu alikuwa ametuonya dhidi ya hayo.” Mungu
alimpa pole kwa hayo. Akamkaribisha ndani ya kasri na kumpa sharubati kwanza. Mbwa
akabaki nje akisubiri. Tangu siku hiyo, Mbwa daima husubiri nje naye Paka huishi ndani
ya nyumba. Hadithi yangu inaishia hapo.

Zoezi ZI

Ukirejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


1. Eleza aina ya ngano hii kwa kuzingatia:
(a) Wahusika (b) Dhamira.
Andika mafunzo yanayojitokeza katika ngano hii.
Toa sifa nne za hurafa zinazojitokeza katika ngano hii.
Simulia mfano wa hurafa kutoka jamii yako.

Hekaya
Hizi ni ngano ambazo kwa kawaida humsawiri mhusika akitumia ulaghai kupata matilaba
yake kutoka kwa wengine. Hekaya pia huitwa ngano za kiayari. Ayari ni mtu mwenye tabia
ya kulaghai. Mhusika huyu hujifanya kuwa rafiki wa mwingine kwa nia ya kujifaidi.
Katika ngano za kiayari au hekaya, kwa kawaida mhusika mdogo au mnyonge hutumia
akili kumshinda mhusika mwenye nguvu asiye na akili.
Katika jamii ya Waswahili, kwa mfano, hekaya nyingi zilihusu mhusika wa kubuniwa
aliyepewa jina la Abunuwasi. Katika jamii nyingine za Kiafrika, hekaya zilimhusu sungura
aliyewalaghai wanyama wakubwa kama vile ndovu. Wanyama wengine kama vile nyani,
mbweha, nyoka na mamba pia husawiriwa kama wahusika walaghai. Ngano za kiayari au
hekaya hutumiwa kuadilisha na kuonya dhidi ya matendo hasi kama vile udanganyifu,
usaliti, hadaa na matumizi mabaya ya cheo.

Mfano wa hekaya

Hapo zamani za kale, Abunuwasi alikuwa mshairi mashuhuri katika kasri la SIA
Abunuwasi alikuwa na punda wake aliyekuwa na sura nzuri mno.
Siku moja punda wa Abunuwasi alihisi kiu. Kwa sababu Abunuwasi hakutaka
kumpeleka punda huyo mtoni kwa kuchelea kwamba angeibwa na mahasidi, aliamua
kumnywesha maji mle nyumbani. Hata hivyo, Abunuwasi hakuwa na ndoo wala karai
ya kutilia maji na hivyo basi akamwendea jirani yake na kumwambia, “Bwana wee nifae
kwa jua nikufae kwa mvua. Punda wangu yu taabani kwa kiu. Nami mwenzio wajua |
tangu hapo wezi walikuja wakabwakura mali yangu. Sasa hata chano cha kutilia tonge |
sina. Naomba uniazime karai yako niitumie kisha nitairejesha mara moja.”
Jirani aliyatilia shaka maneno ya Abunuwasi. Alikuwa ameangukia mizungu ya mja
huyu mara nyingi. Hata hivyo, moyo ulimkumbusha kuwa hata adui hupendwa. Alitwaa
karai na kumkabidhi mgeni wake.
Juma lilipita, Abunuwasi akawa hajarudisha karai. Jirani, subira ikamkimbia.
Akamwendea Abunuwasi na kumwambia, “Ndugu yangu, nimepatwa na haja. Naomba
unikabidhi ile karai.”
>
Abunuwasi alijidai kuhizika. Hata hivyo akili yake nyepesi ilimwambia, “Huu ndio |
wakati.' Aliingia ndani, akatwaa karai ya jirani yake. Ndani ya karai hiyo alitia karai |
nyingine. “Kikembe cha karai kubwa,” aliiita. Alimkabidhi jirani ambaye alimkumbusha
kuwa alikuwa amemwazima karai moja tu. Abunuwasi alikenua akamwambia, “Ndugu,
muda si haba umepita, nayo karai yako imezaa karai ndogo. Sina nia ya kukudhulumu.
Nairudisha karai pamoja na mtoto wake.”
Jirani, ambaye kwa mara nyingine hakutambua mtego wa Abunuwasi, alimsifu
Abunuwasi kwa uaminifu wake. Akatwaa 'mama' na 'mwanawe' na kujiendea zake.
Baada ya mwezi mmoja Abunuwasi alimwendea jirani yake kuomba ile karai tena. |
Jirani alimwazima mara moja kwa kutarajia natija hata maradufu. Wiki mbili zilipita bila
jirani kupata neno lolote kutoka kwa Abunuwasi. Asubuhi moja akaenda kwa Abunuwasi
kudai mali yake. Abunuwasi alitoka nje, uso umejaa huzuni ya mamba. Akamwambia
jirani kuwa karai ilikuwa imekufa! Jirani alikasirika na kukataa kuwa karai ambayo
imetengenezwa kwa chuma inaweza kufa. Abunuwasi alimkumbusha, “Ndugu, kizaacho
Pia hufa.”
j

|
|
|
Ji
(35)
Jirani hakumwamini Abunuwasi. Alimshtaki. Hakimu, katika kuamua kesi alisema,
“Mantiki inadai kuwa ikiwa kifaa kinaweza kuzaa basi kufa ni faradhi”. Abunuwasi
wakashinda. Hadithi yangu inaishia hapo.

Ukirejelea hekaya uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


Thibitisha kuwa hii ni ngano ya kiayari.
Katika makundi, jadili mafunzo yanayojitokeza katika hekaya hii.
Onyesha tamathali za usemi zilizotumiwa katika ngano hii.
AAndika sifa za jirani wake Abunuwasi.
AA
AAA“Onyesha jinsi ngano hii ilivyoshughulikia maudhui yafuatayo:
(a) Tamaa (b) Usaliti (c) Unafiki (d) Mapuuza.
6. -Andika mbinu mbili ambazo wahusika wanatumia kukabiliana na dhuluma .
Na katika ngano hii.

Ngano za mtanziko
Katika ngano za mtanziko, mhusika hukabiliwa na hali ngumu ya kuamua baina ya mambo
au hali mbili au zaidi zinazomkabili; kimaadili, kisheria au kikanuni. Ngano za aina hii
mara nyingi huipa hadhira swali la kujadiliana. Hukuza uwezo wa kutathmini (kupima)
hali na kutoa uamuzi ufaao.

Mfano wa ngano ya mtanziko


(Katika enzi za mababu zetu, wanyama wote waliishi jinsi sisi binadamu tunavyoishi.
Waliweza kulima, kufuga, kuchota maji na hata kupika. Wanyama wote waliishi katika

kupindukia; na Simba, Chui au Duma walikuwa wakali sana.


Kulikuwa na milki mbili kubwa zaidi zilizopakana; Almasi iliyoongozwa na Simba, na
Dhahabu iliyoongozwa na Nyati. Milki hizi mbili zilitoshana kwa kila kitu — si ustawi wa
kielimu, si wa kiuchumi, si wa miundomsingi. Wanyama wote katika milki hizi waliishi
kwa mtagusano uliowawezesha kuishi kwa amani na umoja. Hili lilitiwa mbolea zaidi
na kwamba viongozi wao walikuwa marafiki wa kufa kuzikana.
Hata hivyo, baada ya muda Simba alianza kujiona kuwa alistahili kumiliki eneo
kubwa kuliko Nyati. Alianza kuota akiwa mfalme wa milki zote mbili. Katika ndoto zake
alimwona Nyati akinyenyekea mbele yake. Alifikiri kuwa wadhifa wake ungekuwa wa
juu zaidi kama angemiliki rasilimali za milki zote mbili. Mawazo haya yalimfanya Simba
kujaa chuki nyingi kila wakati walipokutana na Nyati.
Kama wasemavyo wahenga, kikulacho ki nguoni mwako. Simba alianza kumtembelea
Nyati kuuliza ushauri wa jinsi wangeweza kuunda muungano wa milki zao. Nyati aliliona
wazo la Simba kuwa zuri lakini akampendekezea rafikiye kuwa wachukue muda kutafakari
zaidi juu ya muungano huo. Wazo hili halikumfurahisha Simba kwani alimwona Nyati
kama kizingiti kwenye ngazi yake ya madaraka. Hapo ndipo Simba alipoanza kupanga
mikakati ya kumng'oa Nyati mamlakani.
Baada ya kuhakikisha kuwa mipango yake imekamilika, Simba aliamua kumvizia
Nyati na kumwangamiza. Hata hivyo, Nyati aliweza kuonywa na marafiki zake waliokuwa
kwenye utawala wa Simba kabla ya Simba kumvamia. Alipofahamu mipango hasi
ya Simba, Nyati pia aliamua kujihami ili kujikinga dhidi ya Simba. Pupa za Simba za
kuongoza zilimfanya amvamie Nyati katika milki yake. Simba alikuwa amesahau kuwa
mwenye pupa hadiriki kula tamu. Vita vikali kati ya milki hizi mbili vilizuka. Umoja
uliokuwepo ukageuka utengano; uhusiano wao ulikuwa umeingia nyufa.
Nyati alikataa abadan kumwachia Simba mamlaka kwa nguvu. Alihimiza kikozi
chake kupigana kwa vyovyote vile ili kuhifadhi uhuru wao, jambo ambalo walilifanya
kwa uwezo wao wote. Kama isemwavyo, fahali wawili wapiganapo nyasi ndizo huumia.
Wengi wa wanyama ambao hawakuwa na nguvu za kupigana kama vile panya, fuko na
vipepeo waliangamia. Pia wale wakongwe kama vile kobe na kasa waliangamizwa wote.
Vita hivi vilidumu kwa muda mrefu. Kwa kawaida, Nyati aliwapenda wanyama
aliowaongoza kwa moyo wake wote. Kila usiku alifikiri jinsi ya kuvimaliza vita hivi
ili kuepusha maafa zaidi katika milki yake) Hata hivyo alijipata na namna mbili tu za
kushughulikia jambo hili — aidha aendelee kupigana na kuwaangamiza wanyama wake
wote au akubali wito wa Simba wa kung'atuka mamlakani. Aliamua kuwaita washauri
wake kwenye makao makuu ya milki ili wajadili jinsi wangeweza kuinusuru milki yao.
Washauri wake walionekana kugawanyika mara mbili. Kundi moja lilisisitiza kuwa amani
haiji ila kwa ncha ya upanga ilhali lingine liliona kuwa heri nusu shari kuliko shari kamili.
Nyati aliwaza na kuwazua asijue la kufanya. Hadithi yangu inaishia hapo. za

WA

Ukirejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


(a) Thibitisha kuwa hii ni ngano ya mtanziko.
(b) Eleza madhara ya ubinafsi na tamaa kama yanavyojitokeza kwenye ngano
hii.
(c) Taja na ueleze sifa mbili mbili za wahusika wafuatao:
(i) Simba (ii) Nyati.
Fafanua ufaafu wa methali zozote nne zilizotumiwa katika ngano hii.
Je, kama ungekuwa Nyati ungefanya nini? Toa sababu za jibu lako.
zi
Ngano za usuli
ama mahusiano fulani,
Hizi ni ngano ambazo huelezea sababu za kuwepo kwa hali, tabia
hula mizoga. Ngano
kwa mfano, kwa nini mwewe hula vifaranga wa kuku au kwa nini fisi
nyingi za usuli aidha huelezea:
wahusika.
(a) chanzo au sababu ya urafiki au uadui kati ya makundi mawili ya
madoadoa
(b) sababu ya maumbile ya baadhi ya wanyama, kwa mfano kwa nini fisi ana
mgongoni.
au kwa nini
(c) chanzo cha tabia fulani, kwa mfano kwa nini paka hupenda kukaa mekoni
;
mbwa akawa mnyama wa kufugwa.
unafiki. Ngano
Ngano za usuli pia hufunza maadili kama vile kuonya dhidi ya usaliti au
wa
nyingi za usuli hasa zinazoeleza hali fulani za kimaumbile hazina misingi au ushahidi
wenyeji
kisayansi. Huwa ni ngano za kubuni na husimuliwa tu kulingana na hadhira na jinsi
wanavyoyaona na kuyaelewa mambo.

Mfano wa ngano ya usuli


mwake, Gunge
Hapo zamani za kale paliondokea shababi aliyeitwa Gunge. Tangu utotoni
ana wa kijiji
alisifika kwa weledi wake katika uchezaji wa ngoma iitwayo gungu. Wasich
wao alitaka
chake walipumbazwa na jinsi alivyozitawala nyanja za ngoma. Kila mmoja
utongoz aji. Gunge
kujinasibisha naye, jambo lililomfanya kuwa gwiji katika masuala ya
akawa kila mara anaonekana akifuatana na msafara wa hurulaini.
kila yanionapo
Siku moja Gunge alisema, “Naona macho ya waja hayeshi kunihujumu
ikiwa ni halali
nikitembea na waungwana hawa. Nitakwenda kwa Mungu nimuulize
kuwapenda wanawali wengi.”
kuwa alikuwa
Njiani, Gunge alikutana na mtu mfupi kama nyundo. Alipomweleza
ta Mungu
akienda kwa Mungu, yule mtu mfupi akamtuma kwake, “Ndugu, ukimpa
muulize iwapo ufupi ni mzuri.”
“Ndugu niulizie
Hatua chache mbele akakutana na mkulima. Mkulima akamwambia,
kidesturi.”
kwa Mungu kama ukulima ni kazi nzuri. Ikiwa ni nzuri nitaifanya kazi yangu
zie kwa Mungu iwapo
Tena, Gunge akakutana na mchawi. Pia mchawi akamtaka amuuli
alikutana na jitu. Jitu
uchawi ni kazi nzuri ili auendeleze kama mazoea. Mwisho, Gunge
likamtuma, “Ukikutana na Mungu muulize iwapo urefu ni mzuri.”
kwa Mungu.
Gunge aliwaahidi wote kwamba angewawasilishia maswali yao
barabara yoyote.
Akatembea hadi pale alipofikia pahali pasikokuwa na kijia wala
ka nini?”
Hapo akaketi akifikiri. Mara akasikia sauti laini ikimwuliza, “Unata
kuwa mfupi.”
Gunge akajibu, “Ningempata Mungu ningemwuliza iwapo ni vyema
mto au kutunda
Sauti ya Mungu ikajibu, “Ufupi ni mzuri ila tu pale unapotaka kuvuka
” Sauti ikamjibu,
matunda ya mkoma.” Kisha Gunge akauliza, “Je, ni vizuri kuwa mrefu?
a matunda ya
“Urefu ni mzuri sana, hasa wakati unapotaka kuvuka mto au kutund
mengi, lakini
mkoma.” Gunge akasema, “Samahani sana Muumba kwa maswali yangu
je, uchawi ni mzuri?' Sauti nene ya Mungu ikasema, “Uchawi ni mbaya mno, mchawi ni
hasidi mkubwa duniani na ahera. Huua watu wengi na husababisha majonzi makuu.”
Gunge akauliza tena, “Kilimo ni kazi nzuri?” Sauti ikamwambia, “Kilimo ni kazi nzuri
tena sana. Ndicho chemchemi ya uhai.” Gunge akanyamaza kidogo, kisha akauliza kwa
mashaka, “Je, ni halali kuwapenda wanawake wengi?” Sauti ya Mungu ikamjibu: “Si
halali kuwapenda wanawake wengi wasio wake zako. Hata hivyo, ni halali kuwapenda
wanawake wengi ikiwa wote ni wake zako.”
Tangu siku hiyo, Gunge akaamua kuwaoa wasichana wote aliowapenda. Hii ndiyo
sababu ya jamii ya Wanagungu kuoa wake wengi.

Ukirejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo. ;


1. Eleza sifa za ngano ambazo zinajitokeza katika utungo huu.
2. Thibitisha kuwa hii ni ngano ya usuli.
3. Taja na toa mifano ya tamathali tatu za usemi zilizotumiwa katika ngano hii.
4. Simulia ngano ya usuli kutoka jamii yako.

Ngano za mashujaa
Hizi ni ngano ambazo wahusika wake ni mashujaa. Ngano za mashujaa husimulia kuhusu
maisha ya mtu au watu waliotenda mambo ya kishujaa na kutukuzwa. Mashujaa hawa
hutenda vitendo vya kijasiri kama vile kusafiri kwenye nchi za majitu na kupigana na
majitu ili kuziokoa jamii zao.
Ngano nyingi za mashujaa huwa na motifu ya safari na husawiri mapigano kati ya wema
na uovu. Uovu kwa kawaida huwakilishwa na wafalme au viongozi dhalimu, mazimwi au
majitu. Hatimaye wema hushinda uovu kupitia kwa juhudi za mashujaa.
Ngano za mashujaa husimuliwa kuhimiza uzalendo na ujasiri miongoni mwa vijana.

Tofauti kati ya ngano za mashujaa na mighani ni kwamba mighani ni hadithi


za mashujaa wanaoaminiwa kuwa waliwahi kuishi, lakini ngano za mashujaa
ni hadithi za kubuni tu.

Mfano wa ngano ya mashujaa


Zamani za kale katika nchi ya Ustawi kulikuwa na ufanisi si haba. Raia wa Ustawi
walikuwa wakulima wenye bidii za mchwa. Wafalme na raia wa nchi hii waliongozwa
na sera ya, “Kinga na kinga ndipo moto uwakapo”. Wanaustawi wote, wake kwa waume,
wakwasi kwa mafukara waliungana mikono kuikweza Ustawi kutoka daraja moja la
Ustawi hadi jingine. Jamii ya Ustawi ikapanda mimea mingi kwa ajili ya chakula na kwa
kuuza katika nchi jirani. Si maharage, si mahindi, si pareto, vyote viliyapamba mashamba
ya Wanaustawi. Wafugaji nao hawakuachwa nyuma. Miroromo ya ng'ombe na milio ya
mbuzi, kondoo, bata na kuku ilisikika hata katika makaazi ya maskini. Almuradi kila

Mwanaustawi alipania kulizika tatizo la uhaba wa chakula katika kaburi la sahau.


Hali iliendelea hivyo hadi Mfalme Tuvu alipochukua hatamu za uongozi. Msiba baada
ya msiba uliwaandama Wanaustawi kama kivuli. Miaka miwili ya mwanzo ya uongozi
wa Tuvu ilishuhudia kiangazi ambacho kilikuwa hakijawahi kuonekana tangu kuumbwa
kwa ulimwengu. Wasemao wamesema hakuna msiba usiokuwa na mwenziwe. Kiangazi
hiki kiliandamizwa na mkurupuko wa magonjwa sugu. Raia wengi wakasalimishwa
amri na ukoma, ndui, surua na homa ya ubongo. Waganga na waganguzi wakakabiliana
na mahasimu hawa bila mafanikio. Nchi ambayo awali ilijaa vicheko vya heri ikajaa
vilio vya shari. Kasri la mfalme likawa kama mzinga wa nyuki. Washauri waliingia na
kutoka kwa majadiliano na Mfalme Tuvu kuhusu mustakabali wa Ustawi. Hata hivyo,
suluhisho halikupatikana. Mfalme akawa kama aliyekata tamaa. Utukufu na mamlaka
yake yakashindwa kabisa kuwaokoa raia aliowapenda kama mboni ya jicho lake.
Siku moja palitokea mganga aliyeweza kugangua janga la Ustawi. Alimwambia
Mfalme kuwa aliota kuwa maangamizi ya Ustawi yalisababishwa na hasira za mizimu
zilizosababishwa na udhalimu uliotendewa washauri wa mfalme aliyemtangulia Mfalme
Tuvu. Ilisemekana kwamba utulivu ungerejea tu kwa kuukata mkia wa jitu ambalo ndilo
lililokuwa likiwala Wanaustawi na kusababisha maafa. Habari hizi ziliuatua moyo wa
mfalme. Alijua kuwa lazima suala hili lingetandarukiwa. Wazo la kupambana na majitu
lilikuwa zito lililowatia kitetemeshi hata mashujaa. Hata hivyo, lisilobudi hutendwa.
Mfalme aliwaita mashujaa wote wa Ustawi ambao walifika na kupanga foleni mbele
yake kana kwamba wanangojea hukumu ya kifo.
“Palipo na suala linalotishia usalama wa nchi raia hawana budi kujitoa mhanga
kupambana. Hakuna atakayeweza kurejesha amani nchini ila Wanaustawi wenyewe.
Kwa miezi kadha sasa, Wanaustawi wamekuwa wakipukutika kama majani ya mti.
Jitu limemmeza raia baada ya mwingine, kiangazi na magonjwa yameshirikiana na jitu
kutupoka uzima. Suluhisho la jambo hili ni moja; lazima mmoja wenu ajisabilie kukiokoa
kizazi cha Ustawi!”
Maneno ya Mfalme yalikuwa machache na ya mkataa. Yalisababisha mzizimo kwa
kila mmoja aliyekuwepo. Kimya cha kaburi kilitanda huku Mfalme akimtazama shujaa
mmoja baada ya mwingine. Ni kweli kuwa kuilinda nchi lilikuwa suala la kimsingi, lakini
kupambana na majitu! Hatimaye jicho la Mfalme lilitua kwa Kitwana. Kitwana alikuwa
shujaaa ambaye alijipambanua kwa uzalendo. Kwa jinsi Mfalme alivyomtazama, Kitwana
alijua kuwa hilo halikuwa jambo la hiari. Adhabu ya shujaa kukaidi wito wa Mfalme
ilikuwa kifo kwa upanga wa shujaa mwenzake! Hali ya mtanziko ilitanda machoni mwa
Kitwana. Akatae wito wa mfalme auawe na shujaa mwenzake au akabiliane na jitu, aliue
au limuue?
“Nitakwenda,” hatimaye Kitwana alitamka baada ya sekunde ambazo kwake ilikuwa
kama karne nzima.
Jioni ya siku iliyofuata ilimpata Kitwana katika jumba la majitu. Akabisha hodi na
kufunguliwa na ajuza mmoja. Kitwana alimtazama ajuza huyo kwa imani na woga.Uso
wake ulijaa mabaka na viganja vyake havikuwa na vidole. Alikuwa kakonda na kubakia
mifupa. Kitwana alimweleza ajuza huyo sababu ya kuwa hapo. a
“Kijana, naona wewe ni jasiri kweli, ila nataka ujue kuwa hali uliyojitumbukiza
kwayo ni hatari mno. Nilipotoka Ustawi nilikuwa kipusa kweli, lakini nione kilichobakia
baada ya majitu kunifanya karamu yao kila mara wakosapo chakula. Nimewafazama
Wanaustawi wakibugiwa kwenye matumbo ya majitu haya mmoja baada ya mwingine.
Mimi wamenibakiza hapa kuwapikia. Karibuni majitu yatarejea. “Shika kibuyu hiki
na upande nacho juu ya dari. Wakati wa kutoroka, ukiona mazimwi yanakukaribia,
kigongeshe chini,” ajuza alimwambia na kumkabidhi kibuyu. “Harufu ya binadamu
itahanikiza, aliendelea ajuza, “lakini nitajua la kuwaambia. Ukisikia majitu yameanza
kupiga kelele, jua ya kwamba yamelala. Wakati huo twaa sime yako na uukate mkia wa
lile jitu kubwa. Nakutakia heri.” ;
Mazimwi yaliingia na baada ya muda kidogo, yakalala. “Waai! Waai!” majitu yalitoa
kelele zilizotikisa ulimwengu mzima. Kitwana hakupoteza muda. Aliukata mkia wa lile
jitu kubwa akauweka juu ya bega lake na kutifua vumbi; kwenda kuisalimisha jamii
yake. Majitu yalitimua mbio kumfuata Kitwana ambaye alikuwa na mbio kama za duma.
Kadiri alivyokimbia ndivyo majitu yalivyomkaribia. Akakumbuka kibuyu chake cha
wokovu. Akakigongesha chini. Moto mkubwa ukamtenga na majitu. Majitu yakaanza
kuupoza moto kwa mate yao hadi pale ulipozimika kabisa. Yakaendelea kumkimbiza
Kitwana ambaye sasa aliweza kuliona kasri la Mfalme. Jitu lililokuwa limekatwa mkia
likanyosha mkono wake uliofikia mbingu kumshika Kitwana. Ghafla bin vuu, Kitwana
akakigongesha kibuyu chake chini tena. Bahari kubwa likawatenga mahasimu hawa.
Jitu lililokatwa mkia likainua mkono na kuyaamrisha maji ya bahari kujigawa njia mbili.
Majitu yakapita bila kujua kuwa siku yao ya arubaini ilikuwa imefika. Muda wote huu
tayari Kitwana alikuwa ameingia kwenye kasri la Mfalme na kumkabidhi mkia.
Mfalme alitoka nje ya kasri, buruji ikapulizwa, watu wakakusanyika Mfalme
akamshukuru Kitwana kwa kuyaweka maslahi ya taifa mbele ya maslahi yake binafsi.
Akamkabidhi mganga mkuu ule mkia. Mganga akagongesha mkia chini. Moto mkubwa
ukazuka na kuyateketeza majitu ambayo ndio kwanza yalikuwa yakiwasili kwenye kasri.
Nchi ya Ustawi ikatwaa kijani kwa pigo hilo moja la mkia. Wanaustawi wote waliokuwa
wameliwa na majitu wakatoka kwenye moto uliokuwa unayateketeza majitu. Mfalme
akampa Kitwana wadhifa wa Jemadari Mkuu. AA
maameni
irejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.
1. Thibitisha kuwa ngano uliyoisoma ni mfano wa:
(a) ngano ya mashujaa.
(b) ngano ya mazimwi.
Eleza sifa za hadithi zinazojitokeza katika utungo huu.
Bainisha matumizi ya mbinu ya fantasia katika utungo huu.
Eleza maadili yanayowasilishwa katika ngano hii.
kaFafanua masuala ibuka matano ambayo yameshughulikiwa katika ngano hii.
wa
LI
Ngano za kimafumbo

Hizi ni ngano ambazo huwa na maana nyingine ya ndani/maana iliyofichika. Kuna aina
mbili kuu za ngano za kimafumbo.

(a) Istiara
Istiara ni hadithi ambayo maana yake ya juu inawakilisha maana nyingine iliyofichika.
Hurafa ni mfano wa istiara, ambapo wanyama huwakilisha binadamu.

(b) Mbazi
Mbazi ni hadithi fupi yenye mafunzo na inayotolewa kama kielelezo wakati wa kumkanya
au kumwelekeza mtu. Mbazi huwa na maana fiche na hutolewa katika vikao rasmi vya
kutoa mawaidha. Mbazi nyingi hupatikana katika Biblia hasa katika mafundisho ya
Yesu Kristo.

Mfano wa ngano ya kimafumbo

Mjukuu wangu, ni vyema kulipa wema kwa wema. Wazazi wako wamekulea kwa
kujisabilia, mbona unawahangaisha hivi kwa kufusha mioshi midomoni kila mara?
Pulika usikie hadithi niitambayo.
Zamani sana, Simba na Nyoka walikuwa wanapigana, Simba akitaka kumla Nyoka.
Hata hivyo, Nyoka aliweza kuhepa kabla ya Simba kumuua. Akapata hifadhi katika
nyumba ya Binadamu. Binadamu alimficha Nyoka ndani ya kabati. Simba akamtafuta
nyoka asimpate.
Mara tu nyoka alipogundua kuwa hasimu wake ameondoka, alitoka ndani ya kabati,
akamuuliza Binadamu, “Matendo mema hulipwa vipi?” Bila shaka, mjukuu wangu,
Binadamu alimjibu, “Jaza ya hisani ni hisani.”
Nyoka hakusema lolote. Alimkazia jicho Binadamu tu. Kwa kudhani kuwa
hajaeleweka, Binadamu akamfafanulia, “Kwa kawaida, wema hulipwa kwa fedha, lakini
kwa vile huna pesa, unaweza kunipa mnyama yeyote mara tu utakapofanikiwa katika
mawindo yako.”
Nyoka alitabasamu na kusema huku akipanua mataya yake, “Ndugu yangu, unajua
kuwa Nyoka hulipa wema kwa uovu? Nitakumaliza sasa hivi!”
Binadamu akamwambia Nyoka, “La! La! La! Hiyo si haki. Hebu tumuulize Nyuki.”
Nyuki alipoulizwa naye alisema kuwa binadamu hurina asali yake na kumfukuza kwa
mioshi kutoka kwa makazi yake. Binadamu hakuridhishwa na jibu la Nyuki. Akamwomba
Nyoka aulize Mwembe. Nao Mwembe ukasema, “Mimi sijawahi kutendewa haki na
Binadamu. Yeye hutunda matunda yangu msimu baada ya msimu. Anapoona kwamba
utasa umeniingia, yeye hunikata na kunitumia kujitengenezea makaa.” Binadamu
kijasho kikaanza kumtoka. Hata hivyo, akamwomba Nyoka aulize maoni ya Mnazi.”
Nao Mnazi ukasema, “Ni kweli kuwa wema hulipwa kwa ubaya. Binadamu huchukua
nazi zangu, akazikuna na kutumia tui apendavyo. Majani yangu nayo huyachukua'
kuezekea nyumba. Hata shukrani ya mbolea tu hajawahi kunipa.”
Nyoka akamwambia Binadamu, “Unaona sasa? Kigumba kwa nguruwe kwa
binadamu ki uchungu.” Binadamu akakubali. Hata hivyo akamwomba Nyoka ampe
fursa ya kumuaga mkewe. Nyoka akaridhia ombi la binadamu. Binadamu akaenda
kumwambia mkewe kisa chake. Mama mtu michirizi ya machozi ikatiririka njia nne nne.
Akaamua kwenda kuongea na Nyoka, “Bwana Nyoka, nimeona itakuwa bora nikikupa
mayai ule kabla ya kumla mume wangu.” Nyoka akaongozwa na tamaa kukubali. Mke
wa binadamu akachukua fuko lenye mayai na alipolifungua, Nyoka akaingiza kichwa
kuyatwaa mayai. Mara mke wa binadamu akavuta kamba iliyokuwa kwenye mdomo
wa fuko hilo na kufungia kichwa cha Nyoka ndani ya fuko. Kisha akachukua kisu
na kumkata Nyoka kooni. Maisha ya mumewe yakaokolewa. Hata hivyo, Binadamu
akakiona kitendo cha mkewe kuwa cha dhuluma. Akaamua kumtaliki mkewe. Wema
ukalipwa kwa uovu tena. Mjukuu wangu hadithi yangu inaishia hapo. ji

Ukirejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


1. Ni kwa vipi tunaweza kudai kuwa hii ni mbazi?
2. Andika wahusika katika hadithi hii.
3 Andika sifa za ngano ambazo zinajitokeza katika hadithi hii.
4. Hukuukirejelea hadithi hii, bainisha jinsi binadamu anavyoharibu mazingira.
5. Eleza changamoto kuu inayowakabili vijana kwa mujibu wa hadithi hii. |
Mighani
Mighani ni hadithi za kimapokeo zinazohusu mashujaa au maj agina. Kila jamii ulimwenguni
ina mtu au watu inaowatukuza kwa matendo yao ya kishujaa waliyowahi kutenda. Mighani
husimulia visa na mikasa ya mashujaa hawa wanaoaminiwa kuwa waliishi katika historia
ya jamii fulani. Hata hivyo, sifa za mashujaa hawa hutiliwa chumvi kiasi cha kuwafanya
waonekane kana kwamba si binadamu wa kweli.
Mighani husimuliwa kwa nia ya kueleza matendo ya mashujaa na kuwasifu. Aidha, mighani
ni sehemu ya historia ya jamii. Majagina wanaweza kuwa mashujaa wa vita, waganga
mashuhuri na waasisi wa dini waliojipambanua kwa matendo ya kipekee.
Baadhi ya mashujaa katika jamii ni kama vile Fumo Liyongo wa Wapate, Syokimau wa
Wakamba, Lwanda Magere wa Ujaluoni, Mekatilili wa Medza wa Wagiriama, Koome Njue
wa Wameru na Wangu wa Makeri wa Wakikuyu.

Sifa za mighani
(a) Mighani husimulia kuhusu watu na matendo yao ya kihistoria yaliyowahi kutokea.
Kwa mfano, inaaminiwa kuwa Fumo Liyongo ni shujaa wa Waswahili wa Pate aliyewahi
kuishi.

(b) Ingawa mighani huaminiwa kuwa ni matukio ya kweli, matukio yenyewe na uwezo
wa wahusika hupigwa chuku kiasi cha kuwafanya kuonekana kama si binadamu wa
kawaida. Kwa mfano, tunaambiwa kuwa Fumo Liyongo aliweza kuinua tani mia moja
za chuma.

(c) Mighani huaminiwa kuwa ya kweli na jamii husika.

(d) Kila jamii huwa na mighani yake mahususi ya mtu au watu waliotenda matendo ya
kukumbukwa. Mekatilili wa Medza wa Wagiriama, Lianja wa Wakongo, Wangu wa
Makeri wa Wakikuyu na Shaka wa Wazulu ni mifano ya mashujaa ambao walileta
mabadiliko makubwa katika jamii zao.
(e) Baadhi ya mighani huhusiana na visasili. Masimulizi ya Lwanda Magere, kwa mfano,
yanaeleza sababu ya Wajaluo kuabudu jiwe waliitalo “Mtemi Lwanda Magere'.
Inaaminika kuwa jiwe hili ni mwili wa Lwanda Magere.
(f£) Mashujaa husimuliwa kuwa na maumbile ya kiajabu. Huweza kuzaliwa wakiwa na
upungufu wa kiungo cha mwili, lakini wakawa na nguvu za ajabu.
(g) Mashujaa huangamizwa kwa njia ya kiajabu. Lwanda Magere, kwa mfano, aliuawa
kwa kuchomwa kivuli chake kwa mkuki. Naye Fumo Liyongo aliuawa kwa kuchomwa
sindano ya shaba kwenye kitovu. Katika Biblia, Samson aliishiwa na nguvu kwa
kunyolewa nywele tu!
Mashujaa huangamizwa na husalitiwa na watu wa karibu au jamaa zao. Fumo Liyongo,
kwa mfano, alisalitiwa na mwanawe, naye Lwanda Magere akasalitiwa na mkewe.
Samson, katika Biblia, alisalitiwa na mkewe.

(i) Mashujaa huangamizwa na watu wasiokuwa na uwezo kama wao. Kwa mfano, Fumo
Liyongo aliuawa na mwanawe, Samson katika Biblia alinyolewa na mkewe, naye
Goliathi akauawa na Daudi ambaye alikuwa kijana mdogo.

D Kwa kawaida, shujaa hukabiliwa na mgogoro mkubwa. Anaweza kuwa na mgogoro


kati yake na mfalme au jamii nyingine.
(k) Mighani, kama ngano za mashujaa, huwa na motifu ya safari. Aghalabu mashujaa wa
vita husafiri mbali kupigana vita ili kuziokoa jamii na watu wao.

Umuhimu wa mighani

(a) Mighani hutambulisha jamii. Kila jamii ina mighani yake mahususi inayohusu watu
na matukio yaliyowahi kutokea katika historia yao. Mighani ya Lwanda Magere
inawatambulisha Wajaluo; Fumo Liyongo, Waswahili; Koome Njue, Wameru;
Syokimau, Wakamba.

(b) Mighani huelezea na kuhifadhi historia ya jamii kwa kuipitisha kutoka kizazi kimoja
hadi kingine. Pia hutaja mashujaa, vita walivyopigana, lini na dhidi ya nani.
(c) Hutumiwa kama sifo kusifu mashujaa kwa matendo yao. Mighani, kwa mfano, ya
Fumo Liyongo inamsifu Liyongo.
(d) Ni kumbukumbu kwa mashujaa kuonyesha kuwa jamii inatambua na kuthamini
mchango wao.
(e) Huhimiza uzalendo. Hadithi za mashujaa huwafanya watu kujitambulisha na mashujaa
hao na hivyo kukuza hisia za kizalendo. Vijana huhimizwa kupigania jamii zao kama
mashujaa hao walivyofanya.
Huonya dhidi ya matendo kama vile usaliti na kupuuza mambo madogo madogo. Shujaa
aghalabu husalitiwa na mtu wa karibu, hivyo tunapotambiwa mighani, tunafunzwa
kutahadhari na watu wa karibu walio na hila —- Kikulacho ki nguoni mwako.
Hupitisha thamani na amali za jamii kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kama
tulivyotangulia kutaja, baadhi ya mighani huoana na visasili. Kwa mfano, mwili wa
Lwanda Magere unapogeuka jiwe, jiwe hilo linakuwa takatifu kwa jamii ya Waluo.
Mighani hii inapotambwa, watu huelewa thamani inayohusishwa na jiwe hilo.
Kama tanzu nyingine za fasihi simulizi, mighani hutumiwa kuburudisha. Huburudisha
baada ya shughuli za mchana.
Huhimiza ujasiri na kutokata tamaa. Watu wanapoona jinsi mashujaa walivyopigania
nchi zao, wao hupata moyo wa kutokata tamaa.
Kama tanzu nyingine za fasihi simulizi, mighani hukuza ushirikiano. Watu hujumuika
pamoja kutambiwa mighani na hujihisi kundi kuwa moja.
Mfano wa mighani
Mojawapo ya mighani ambayo imesimuliwa kwa miongo mingi katika jamii ya Waswahili
ni mighani ya Fumo Liyongo. Liyongo alikuwa jagina wa jamii ya Wapate ambaye aliishi
Ungwana wa Mashaha, eneo la Shaka, katika jimbo la Ozi. Liyongo anasifika kama
shujaa wa vita-ambaye katu hakunywea mbele ya mahasidi wake hata kama mahasidi
hao wangekuwa na silaha kali kiasi gani. Inasimuliwa kwamba Liyongo alikuwa na tambo
ambalo liliwafanya watu kumwogopa. Alikuwa mrefu kiasi kwamba hata Wagalla ambao
waliaminiwa kuwa warefu sana walimfikia magotini tu. Liyongo alikuwa na nguvu
zisizomithilika. Inasimuliwa kwamba aliweza kuinua tani mia moja za chuma! Na hilo
lisionekane kubwa sana kwani Liyongo aliwahi kuusukuma mtumbwi uliojaa watu na
mizigo kutoka upande mmoja wa bahari hadi ule mwingine huku yeye amejikita kwenye
ufuo. Ama kweli shujaa huyu alikuwa na misuli ambayo haikuweza kushindwa na jambo
hata likawa na uzito wa nanga. Alikuwa simba ambaye kutembea kwake usiku kulikuwa
kama kutembea mchana.
Si kimo tu ambacho kiliwafanya waja kumwogopa Liyongo bali pia mtazamo wake.
Wengi walizimia mara tu alipowakodolea macho, na wengine kushikwa na kitapo
alipowatokea ghafla. Umaarufu wa Liyongo katika uwanja wa vita ulimvutia sana
Mfalme Daudi Mringwari, kakake Liyongo. Mfalme aliusifia ujagina wa Liyingo kwa
Wagalla ambao walikuwa mabingwa vitani. Wagalla hawakuyaamini maneno ya Mfalme
hadi pale alipoagiza Fumo Liyongo kusafiri kutoka Shaka hadi Pate ili Mfalme apate
kuwasadikisha Wagalla kuwa avumaye baharini papa, kumbe wengine wapo! a
Basi Liyongo akashika tariki kuelekea Pate, kwenda kuitika wito wa Mfalme.Kutoka
Shaka hadi Pate ni safari ya siku nne kwa miguu, naye Liyongo alidiriki kufika Pate
baada ya siku mbili. Kuwasili kwa Liyongo Pate kuliandamana na shani kuu. Liyongo
alipokaribia Pate alipuliza panda mara tatu zikipasuka, nao mji mzima ukatanabahi kuwa
Liyongo keshawasili. Umati mkubwa ukakusanyika kwenye baraza la mfalme kujionea kwa
macho yao mja huyu wa kugandisha damu kwenye mishipa, ikawa ni kama waliostaajabu
ya Musa na sasa wenda kushuhudia ya Firauni. Mara tu Liyongo alipotia guu kwenye
kizingiti cha kasri la Mfalme, alitua mizigo aliyokuwa amebeba, nalo! Mizigo hiyo ilijaza
nyumba nzima. Wagalla wakahizika, wakaamini kuwa kweli Liyongo ni jabari. Ujagina
wa Liyongo ukawatuma Wagalla kutaka kuunga udugu naye, angaa wajinasibishe naye.
Wakamwomba Mfalme awaruhusu wapate mbegu ya Liyongo. Mfalme akaridhia ombi
lao na kumwoza Liyongo kimanzi wa Kigalla. Liyongo na kidosho huyu wakazaa mvulana
ambaye alikuzwa vyema, akainukia kuwa ghulamu mwenye heba na nguvu.
Walisema wasemao kuwa mti huanguka kwa tundaze. Umaarufu wa Liyongo ndio
uliomchongea kwa Mfalme ambaye kadiri siku zilivyosonga ndivyo mshale wa wivu
ulivyomfuma na woga wa kunyang'anywa ufalme ukaukuza zaidi mgogoro kati ya ndugu
hawa. Mfalme akataka kumwangamiza Liyongo alakulihali. Liyongo akagundua feli ya
Mfalme na kutorokea nyikani ambako aliishi na Wasanye, Wadahalo, Waboni na Watwa.
Ari ya kutaka kumwangamiza Liyongo ilimsukuma Mfalme kula njama na Wasanye na
Wadahalo. Akawaahidi kuwapa reale mia ili kumletea kichwa cha Liyongo. Ukatili ulioje!
Kwa kujua uwezo wa Liyongo, ilibidi Wasanye na Wadahalo kujifanya kuwa marafiki
wa Liyongo ili watekeleze mradi wao. Wakapanga kutunda makoma kutoka mtini na
kula kikoa, wakitarajia kuwa zamu ya Liyongo ikifika atapanda mtini, wapate kumuua,
bila kujua kuwa akili ya Liyongo iliyokuwa inashika kama sumaku ilikuwa imekwisha
kugundua hayo! Zamu ya Liyongo ilipofika alichukua mshale wake akayaangua matunda
kikwi kwa mshale uo huo. Maadui wakala shibe yao huku wakiugulika. Wakampasha
Mfalme habari kuwa Liyongo ni jabali ambalo mijusi hawawezi kulikwea.
Mfalme hakufa moyo. Wanasema kuwa mbwa hafi maji akaribiapo ufuo. Naye
Mfalme alihisi kuwa alikuwa karibu kama pua na mdomo katika kuizika historia ya
Liyongo katika kaburi la sahau. Akatayarisha shambulizi jingine, mara hii akihakikisha
kuwa ametumia akili kweli kweli. Akawatuma wale wale wajumbe aliokuwa amewatuma
awali kumwambia Liyongo kuwa mjini ku salama; kwamba angeweza kurejea nyumbani. |
Liyongo, pamoja na uwekevu wake akaanguka kwenye mtego huu. Akarejea mjini |
ambako aliviziwa na askari wa Mfalme akicheza gungu na mwao, ngoma ambayo Liyongo
akiisakata kwa faka kuu, na ambayo alikuwa mahiri kwayo.Liyongo akatiwa kizuizini,
akawa anangojea hukumu ya kifo.
Liyongo alihesabu siku gerezani akisubiri mauko yake. Hakungoja jinsi kondoo
angojeavyo kutiwa sime shingoni na kudhulumiwa sufu yake! La hasha! Liyongo aliwazia
mkakati wa kujiopoa. Akaona kuwa njia ya pekee ya kuepuka mauti yaliyomkodolea
macho ni kutoroka gerezani. Akamwandikia mamake shairi ambalo lilimtaka kuoka
mkate wa wishwa na kuitia tupa ndani ili Liyongo apate kifaa cha kukerezea minyororo.
Mamake Liyongo hakukawia kufanya hivyo. Japo mama mtu alijua kuwa tendo hilo
lilikuwa hatari, uchungu wa uzazi ulimtuma kujisabilia kwa mwanawe.
Liyongo akakata pingu na kuvunja lango la gereza. Kwa viganja vyake akarejesha
uhuru wake na kurudi tena nyikani.
Tamaa ya utukufu na uluwa ni kama kiu ya maji, haikatiki hadi pale mtu ayapatapo
maji, akakinai na hata kupiga mbweu. Hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Mfalme. Alipogundua
kuwa Liyongo katoroka, aliamua kutumia mshale wake wa mwisho uliokuwa kwenye
riaka.Mara hii alihakikisha kuwa amelenga ndipo. Alimwendea mwanawe Liyongo na
kumrai amuulize babake ni kitu gani ambacho kinaweza kumuua, kwani Mfalme tangu
hapo alikuwa ametanabahi kwamba Liyongo hafi hata kwa mzinga hatari. Shababi
akaahidiwa uwaziri na kuozwa binti ya Mfalme. Wazo la kuozwa huyu hurulaini
likaupujua utu wa rijali huyu. Akafunga safari hadi Shaka ambako Liyongo, japo alijua
njama ya mwanawe alimwambia kuwa angeweza kufa tu kwa kudungwa kwa sindano |
ya shaba kitovuni. Kijana aliposikia hayo alifurahi na kurudi kwa Mfalme kumpasha
habari. Mfalme alifurahi na kumtuza kijana zawadi maridhawa. Akampa sindano ya |
shaba na kumtaka akamuue baba yake.Kijana akarudi kwa baba yake, akamwotea akiwa
usingizini na kumchoma kwa ile sindano.
j
W. |

|
ji
(r)
Liyongo alikurupuka kwa ghamidha kutoka usingizini, akachukua upinde na
kuelekea kisimani akijua kuwa hatima ya maisha yake ilikuwa imefika; anakufa kifo
cha mwana alompa uhai yeye. Alipofika kisimani, Liyongo alitia mshale kwenye upinde
huku anauelekeza mjini na kukata roho huku waliokuja kumtazama wakidhani bado yu

kwenda kuchota maji kisimani. Wakamlilia jagina wao huku wakimmiminia sifa,
wakamrai azungumze nao ila hawakuambulia lolote. Mama mtu alipiga moyo konde
na kwenda kisimani, roho mkononi, zingizi ya uzazi ikimkeketa si haba akampembejea
mwanawe kuondoka kisimani. Hewa ya mandhari hayo ikahanikiza mashairi. Mama
akaimba, akaghani, akakariri ... Kimya. Hatimaye mwili wa Liyongo ukasalimu amri
baada ya siku kadha, mwamba uliokuwa tayari umeanza kuoza ukaanguka. Maskini mama
mtu akakitazama kifo kikimpoka mwana alokuwa tegemeo la jamii. Wingu la huzuni
likatanda eneo zima. Mbolezi za akina mama zikapamba kutwa hiyo ya kiza, wakawa
kama wanawakiwa, wakamlilia shujaa wao kwa beti ali ali:

“Liyongo silaha yetu Mui walisikitika


kwa w'ute khasimu zetu Hakuna wa kutosheka
alikuwa ngao yetu!” kwa Liyongo kutoweka
Wut'e wakinena haya. Imeanguka paziya.

Ukirejelea mighani uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.


1. (a) Andika sifa za mighani zinazojitokeza katika utungo huu.
(b) Changanua utungo huu kifani.
2. (a) Kwa nini jamii ziliwatambia vijana mighani?
(b) Toa mfano wa mighani kutoka jamii yako.

Visakale
Visakale ni masimulizi ya kimapokeo ya matukio yaliyotendeka zamani. Matukio haya
yanaweza kuwa ya kweli lakini yakaongezwa ubunifu na kuyafanya yaonekane kama ya
kubuni tu. Visakale husimulia masuala kama vile:
(a) vita
(b) hamahama za jamii
(c) majanga ambayo jamii ilikabiliana nayo kama vile njaa, na maambukizi ya magonjwa.
Wahusika katika visakale ni binadamu. Visakale na mighani hulingana kwa kuwa vinahusu
matukio ya kihistoria. Mighani huangazia mashujaa katika jamii ilhali visakale husimulia
matukio mengine yote ya kihistoria katika jamii. Hamahama za jamii ya Waisraeli kutoka
Misri, kupitia jangwani hadi Nchi ya Agano (Kanaani) katika Biblia ni mfano mwafaka wa
kisakale.

aa Ji
Visasili
Visasili ni hadithi za kale ambazo huelezea imani na mtazamo wa jamii kuhusu asili ya
ulimwengu na mwenendo wake. Hufungamana sana na masuala ya kiimani au kidini na
mitazamo ya jamii kuhusu asili ya miviga kama vile tohara, ndoa na unyago na utaratibu
uliozingatiwa katika desturi hizo. Visasili huelezea pia chanzo cha kifo, asili ya jamii
fulani na asili ya maumbile mbalimbali ya kiasili kama vile milima na mito. Aghalabu,
visasili huaminiwa kuwa ukweli usiopaswa kuuliziwa maswali. Kimsingi, visasili hutumiwa
kuhalalisha desturi, miiko na madhehebu ya jamii iliyovizaa. Wahusika katika visasili
huweza kuwa binadamu au miungu. Visasili vinaweza kuainishwa katika makundi mawili:
vya usuli na vya kidini, kutegemea majukumu yake.
Visasili hutofautiana na ngano za usuli. Ngano za usuli hueleza sababu za hali, maumbile au
mahusiano ya kawaida katika jamii ilhali visasili hueleza chanzo au asili ya hali, maumbile
na mienendo ulimwenguni.
Visasili hujikita katika imani fulani za kidini ilhali ngano za usuli ni zao la ubunifu tu.
Visasili huaminiwa kuwa vya ukweli lakini ngano za usuli hubuniwa na jamii katika kujaribu
kueleza sababu za hali, maumbile au mahusiano.
Visasili huwa na wahusika miungu na mandhari yasiyo ya kawaida. Wahusika binadamu
katika visasili ni mashujaa au majagina kama vile Gikuyu na Mumbi kwa Wagikuyu au Sera
na Mwambo kwa Waluhya.

Sifa za visasili
(a) Visasili ni hadithi za kinathari ambazo zinaaminiwa kuwa ni masimulizi ya kweli
kuhusu tukio linalosimuliwa kama lilivyotukia zamani za kale.
(b) Husimulia mambo ya kiimani au kidini kama yanavyoaminiwa na jamii.
(c) Hukubaliwa na jamii husika na kuaminiwa kuwa vya kweli. Kwa mfano, Wakikuyu
huchukuliwa kuwa ni kizazi cha Gikuyu na Mumbi.
(d) Huwa na misingi ya kihistoria. Tangu jadi, kwa mfano, jua hupatwa. Jamii hujaribu
kueleza na kuhalalisha kupatwa huku kwa jua.
(e) Visasili huweza kuwa na wahusika binadamu mashujaa, miungu, wanyama, mawe na
vitu vingine.
(£) Matendo ya wahusika katika visasili hukitwa katika ulimwengu wa asili au mwanzo
wa ulimwengu ambao ulikuwa tofauti na ulimwengu wa kisasa au katika ulimwengu
mwingine wa mbinguni au wa kufikirika tu.

Umuhimu wa visasili
(a) Hutumiwa kuhalalisha baadhi ya desturi na imani katika jamii fulani, kwa mfano
sababu za kuabudu miti, mawe, milima na miungu wengine.
(b) Huelezea asili ya mambo, kwa mfano asili ya kifo, maisha na tamaduni mbalimbali
kama vile uwindaji.
(c) Nikitambulisho cha jamii. Kila jamii huwa na visasili ambavyo hufungamana na imani
za jamii husika. Chanzo cha kifo, kwa mfano, hufafanuliwa kwa njia tofauti tofauti
kutegemea imani ya jamii. Tofauti hizi hutambulisha upekee wa kila jamii.
(d) Huonyesha na kuhifadhi historia, imani na utamaduni wa jamii. Imani hizo hupitishwa
kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
(e) Hupunguza athari za baadhi ya majanga kwa watu. Kwa mfano, watu hukubali kifo
kwa sababu kimehalalishwa; kwamba kila binadamu lazima afe. Wanaamini kuwa si
kosa lao kufa na hivyo hupunguza uchungu baada ya kufikwa na kifo.
(£) Huadilisha. Kila kisasili hutoa maadili. Katika baadhi ya jamii, kinyonga alisababisha
kifo. Wenye imani hii huonya dhidi ya kufanya mambo polepole.
(g) Ni nyenzo ya kudhibiti tabia na matendo ya watu. Yapo baadhi ya maeneo kama vile
mibuyuni ambayo huchukuliwa na jamii zingine kuwa madhabahu au pahali patakatifu
pa ibada, hivyo ni mwiko kucheza katika maeneo haya. Wanajamii huonywa dhidi
ya kukata miti humo. Aidha, jamii nyingine huamini kuwa mibuyuni ni makao ya
mashetani, hivyo wanajamii huonywa dhidi ya kwenda humo.

Mfano wa kisasili

Mulungu ndiye aliyemuumba binadamu. Kwa vile Mulungu ni mwema daima aliwaambia
malaika wake, “Nisingependa binadamu wawe wakifa kabisa. Ningependa binadamu akifa
awe anafufuka.” Basi akawaumba binadamu na kuwaweka katika eneo jingine mbali na
alikoishi yeye Mulungu.
Karibu na nyumba ya Mulungu, paliishi kinyonga na ndege aitwaye Mnana. Katika
mtagusano wao na Mulungu, Mulungu aliweza kung'amua kuwa ndege huyo alipenda
kutia chumvi maneno na hata kusema mambo kinyume na alivyoambiwa. Akamtambua
kuwa kiumbe asiyeweza kuaminiwa. Kwa upande mwingine, kinyonga alikuwa mwadilifu
na mwenye busara. Hakusema uongo.
Mulungu alipoona kuwa wakati umefika wa kumpasha binadamu ujumbe wa uzima
alimwita kinyonga na kumwambia, “Nenda katika eneo ambamo nimewaweka binadamu.
Waambie kuwa yeyote atakayekufa atafufuka.” Kinyonga alisujudu na kusema, “Ndiyo,
Mulungu.” Hata hivyo, kinyonga alitembea polepole kama kawaida yake. Mnana alibaki
nyumbani kwa Mulungu. Kinyonga akahesabu hatua zake polepole akihofia kuumiza
ardhi ya wenyewe. Alipofika alikuwa yu hoi, nguvu zimemwishia. Aliwakuta binadamu
wamekusanyika pamoja. Taratibu akaanza kutoa ujumbe wake, “Nime ... nime ...
nimeambiwa ...” lakini hakudiriki kusema aliloambiwa.
Mnana alimwomba Mulungu udhuru wa kuondoka. Mulungu akamridhia, naye
akaruka moja kwa moja. hadi alikoishi binadamu. Alimkuta kinyonga katika harakati
zake za kusema 'nime ... nime ... nimeambiwa” huku watu wakingoja kwa matarajio
makuu kusikia alichoambiwa. Mnana alipofika, kinyonga alikuwa amechoka kiasi cha
kusahau ujumbe wenyewe. Kinyonga alipomwona Mnana akamuuliza, “Tuliambiwa nini
na Mulungu?” Naye Mnana bila kuchelewa akasema, “Tuliambiwa kuwa binadamu wakifa
wataangamia na kudidimia kabisa kama mizizi ya mshubiri.” Kinyonga akashangaa na
kusema, “Lakini tuli ... tuli ... tuliambiwa kwa ... kwamba ... bin ... bin-adamu wakifa
... wa ... Wata ...watafufuka tena ...” Hata hivyo kinyonga alikuwa amechelewa. Watu
walikuwa wametawanyika wakaelekea makwao, nyuso wameziinamisha.

- Andika sifa za visasili zinazojitokeza katika hadithi hii.


Eleza tofauti kati ya hadithi hii na ngano ya usuli.
Taja maudhui matano yanayojitokeza katika hadithi hii.
Andika maadili ya hadithi hii.
NABUWN
Eleza tofauti kati ya mighani na visasili.

Vipera vingine vya hadithi


Vigano
Vigano ni hadithi fupifupi zinazosimulia kuhusu matendo mabaya katika jamii na wakati
uo huo kuelekeza au kuonya dhidi yayo. Aghalabu vigano huandamana na methali kwa
lengo la kufafanua linalokusudiwa au kuthibitisha funzo la methali fulani.

Sifa za vigano
(a) Vigano ni hadithi fupifupi.
(b) Vigano husimulia kisa kimoja tu.
(c) Wahusika katika vigano ni binadamu au wanyama.
(d) Vigano hukusudia kuadilisha hasa kwa kutumia methali au kuthibitisha na kusisitiza
katika methali.

Tarihi
Tarihi ni rekodi za matukio ya kihistoria. Katika tarihi, matukio hupangwa kulingana na
jinsi yalivyofuatana kiwakati. Tarihi huwasilishwa kwa njia ya masimulizi bila kutolewa
ufafanuzi.
Ingawa tarihi hazichukuliwi kama tungo za kisanaa, baadhi yazo hutumia mbinu za kifasihi
na hivyo kuzifanya zichukuliwe kama fasihi. Kwa kawaida, tarihi hutokea katika maandishi.
Kwa kiasi fulani, sifa hii hufanya tarihi kutofautiana kidogo na fasihi simulizi. Aghalabu
tarihi husimulia kuhusu familia za kifalme. Mfano wa tarihi ni Habari za Wakilindi, Tarihi
ya Kilwa na Tarihi ya Pate.

OO
Kumbukumbu
ambamo
Kumbukumbu ni maelezo ya kitawasifu au kiwasifu ambayo husimulia matukio
ambayo
msimulizi amehusika binafsi au jamii yake. Mfano wa kumbukumbu simulizi
iliwahi kuandikwa ni Uhuru wa Watumwa ya James Mbotela.

Soga/Visoga
ta
Hizi ni hadithi fupi za utani au ucheshi. Soga hutumiwa kukejeli jambo kwa kufumba
Soga kwa
ukweli wake katika kicheko. Hivyo, hukashifu tabia fulani kwa njia ya ucheshi.
kawaida hutolewa katika vikao vya kupitisha muda.

Mfano wa soga
miguu kwenda
Mama mmoja alikuwa amebeba mzigo mzito huku akitembea kwa
eka alikokuwa
sokoni. Msamaria mwema alisimamisha gari na kujitolea kumpel
u mgongoni,
anaelekea. Mama huyu aliketi kwenye kiti cha nyuma huku mzigo wake
kacheka na
hautui. Dereva alipomwuliza sababu ya kutoutua mzigo, mama aliche
na zigo jingine
kusema, “Gari lenyewe naliona dogo mno. Kulipagaza uzito huu wangu
itakuwa dhuluma kubwa. Acha nilipunguzie uzito.”
husu magari.
Kisa hiki kinaonyesha kwamba mama huyu ni limbukeni wa mambo yanayo
garini.
Haelewi kwamba hata asipouweka mzigo chini, uzito utabakia mlemle

1. Eleza tofauti kati ya soga na vigano.


2. Andika soga ya aya mbili.

Mbinu za uchambuzi wa hadithi


Katika kuchanganua hadithi yoyote ile, mambo yafuatayo huzingatiwa:

1. Dhamira
mwisho. Ni sababu
Dhamikra ni wazo kuu linalojitokeza katika hadithi kuanzia mwanzo hadi
dhidi ya ubinafsi,
kuu ya kusimulia hadithi fulani. Hadithi inaweza kudhamiria kuonya
kwa dhamira.
unafiki au tamaa. Aghalabu, maadili katika hadithi hujitokeza kupitia

2. Maudhui
. Mfano wa
Maudhui ni masuala ambayo hushughulikiwa na mtambaji katika hadithi
.
maudhui ni tamaa, usaliti, ulaghai, ubinafsi, umaskini na uongozi
3. Fani
Fani ni mbinu zote ambazo mtambaji hutumia kufanikisha utambaji wake. Fani hujumuisha
matumizi ya lugha na tamathali zake, wahusika, ploti, uigizaji, urudiaji, nyimbo na vipengele
vingine kama vile kupanda na kushuka kwa sauti.

Fani katika hadithi


Katika kufanikisha uwasilishaji wake, mtambaji hutumia vipengele vifuatavyo vya fani:

1. Ploti
Huu ni mfuatano wa matukio kulingana na jinsi yanavyosababishana. Kwa kawaida, ploti
ya hadithi nyingi huwa na mtindo sahili au wa moja kwa moja. Haina matumizi mengi ya
mbinu rejeshi na vipengele vingine ambavyo huenda vikaifanya hadithi kuwa changamano.
Kwa kawaida ploti ya hadithi huwa na mgogoro mmoja ambao ndio unaosukuma hadithi
mbele. Hata hivyo, kuna baadhi ya hadithi ambazo huwa na ploti changamano. Ploti za
aina hii huwa na migogoro miwili au zaidi.
Kimuundo, ploti ya hadithi huwa na sehemu tatu kuu:
(a) Mwanzo: Mwanzo wa hadithi huweza kujumuisha fomyula ya ufunguzi wa hadithi
kama ilivyojadiliwa awali. (Tazama fomyula katika ngano ukurasa 26 — 28) Ngano za
kimapokeo huchukua mianzo kama iliyokwisha jadiliwa katika fomyula.
(b) Katikati au mwili: Sehemu hii ndiyo hutoa habari zote zinazohusiana na hadithi.
Mgogoro unaomkabili mhusika mkuu hukuzwa hapa. Kwa kifupi, hadithi yenyewe
husimuliwa hapa.
(c) Mwisho: Katika hadithi, mwisho hujumuisha fomyula za kumalizia. Aghalabu hadithi
nyingi za kimapokezo huishia kwa '... wakaishi raha mustarehe” au “Hadithi yangu
inaishia hapo'. Sehemu hii pia huonyesha utatuzi/mwisho wa mgogoro unaomkumba
mhusika mkuu.
Mambo yanayozingatiwa katika uchambuzi wa ploti ya hadithi
(a) Wahusika: Je, hadithi ina wahusika wangapi?
(b) Mgogoro: Kuna migogoro mingapi inayomkabili mhusika mkuu?
(c) Utatuzi: Juhudi zinazotumiwa na mhusika mkuu kukabiliana na mgogoro au tatizo
linalokabili ni gani?
(d) Mtiririko: Matendo yanafuatana na kusababishana vipi kuanzia mwanzo hadi
mwisho?
(e) Kuna matukio yepi makuu au ya kimsingi? Matukio hayo yanahusiana vipi?
(£) Ni nini upeo wa juu wa hadithi yenyewe? Kwa mfano, katika baadhi ya ngano za
mazimwi, upeo wa juu ni kuuawa kwa zimwi na kurejea kwa amani katika jamii.
(g) J e, hatimaye kuna suluhisho gani kwa tatizo linalomkumba mhusika mkuu?
(h) Hadithi inachukua muundo wa aina gani? Ina mwanzo, katikati na mwisho?

(3)
2. Mandhari
Mandhari ni mazingira ya mahali, wakati na hali inayozunguka tukio fulani. Kwa sababu
ya ufupi wa hadithi, mara nyingi mandhari hayafafanuliwi kwa kina.
Katika kuchanganua mandhari ya hadithi tunajiuliza maswali yafuatayo:
mandhari ya
(a) Tukio linatokea wapi? Matukio katika ngano, huweza kutokea katika
kifantasia au kiajabu kama vile ndani ya matumbo ya majitu, katika ulimwengu wa
mazimwi au mazingira ya kawaida.
(b) Tukio linatokea katika hali gani? Je, ni katika hali ya njaa, kiangazi, shibe, vita au
majonzi?
za
(c) Tukio lilitokea lini? Je, ni zamani za kale, usiku au mchana? Aghalabu hadithi
kimapokeo hujikita katika muda mrefu uliopita.

3. Wahusika
za binadamu
Wahusika ni viumbe vya kisanaa ambavyo mtambaji hutumia kuwakilisha tabia
katika jamii husika. (Rejelea wahusika katika fasihi simulizi kurasa 15 — 18.)
maana
Katika usimulizi wa hadithi, mpaka kati ya wanyama na binadamu hufutwa. Hiiina
u.
kuwa wanyama huweza kusawiriwa wakizungumza na kujadiliana na binadam
yafuatayo:
Katika kuchanganua wahusika katika hadithi, mhakiki anastahiki kujibu maswali
Kwa kujibu swali hili
(a) Hadithi inamhusu nani? Je, ni fisi, sungura au shujaa wa vita?
utakuwa unamtambulisha mhusika mkuu.
mawe?
(b) Je, wahusika ni wa aina gani? Ni binadamu, mazimwi, mimea au
ni shujaa
(c) Je, mhusika mkuu amesawiriwa vipi? Ni nguli au ni hasidi? Mhusika nguli
a hasidi
au jasiri asiyeogopa ambaye kwa kawaida hutetea maadili ya jamii. Mhusik
naye ni adui au mpinzani wa nguli au anayepigana na maadili ya jamii.
au mafunzo
(d) Je, mhusika huyu anawakilisha hali gani katika jamii? Anatoa maadili
gani?
(e) Je, kuna wahusika wengine wangapi katika hadithi na wana sifa gani?
o kati yao?
(£) Wahusika wengine wanaingiliana vipi na mhusika mkuu? Je, kuna mgogor
atendayo?
(g) Je, ni misukumo (motisha) au hali gani inayomfanya mhusika mkuu kutenda
kilisha hali gani?
(h) Wahusika wana mchango au umuhimu gani katika hadithi? Wanawa
Wanasaidia vipi kuiendeleza hadithi?
ni mhusika
(i) Je, wahusika hawa ni wa aina gani? Ni bapa? Ni duara? (Mhusika bapa
asiyebadilika; kama ni mui hubaki mui hadi mwisho. Mhusika duara hubadilika.)
a wengine
(j) Je, mhusika huyu hufanya nini na husema nini kujihusu? Je, wahusik
wanasema nini kumhusu?
ai

4. Lugha |
Lugha huchukua nafasi kubwa sana katika hadithi na fasihi simulizi kwa jumla kwani
ndiyo malighafi ya fasihi simulizi. Katika usimulizi wa hadithi, fanani aghalabu hutumia
lugha yenye: |
(a). sentensi fupifupi. Sentensi fupi ni rahisi kueleweka na pia hazina uchovu wa kufasiri |
dhana nyingi kama ilivyo katika kauli moja ndefu. Aidha, sentensi fupi hujenga
taharuki upesi na huondoa uchovu au ukinaifu.
(b) tamathali za usemi. Hizi hutumiwa kujengea taswira au picha ya matukio
yanayosimuliwa akilini mwa msikilizaji. Taswira (picha) huweza kujengeka kwa
kusikiliza sitiari, tashbihi na tanakali za sauti.
(c) vichekesho. Hivi hutumiwa kuteka makini ya wasikilizaji na pia kuwafanya wasisahau
yanayosimuliwa.
(d) nyimbo. Nyimbo hushirikisha hadhira na hazisahauliki kwa urahisi. Pia, nyimbo
huupa usimulizi uhai na kuondoa uchovu unaotokana na masimulizi makavu. Aidha |
nyimbo huwazindua waliokuwa wakisinzia wakati wa masimulizi. Mawazo makuu pia |
hupitishwa kupitia nyimbo katika hadithi. |
(e) takriri. Hiki ni kipengele cha lugha kinachohusu kurudiarudia maneno fulani au
vifungu vya maneno ili kuyasisitiza. Kwa mfano, badala ya kutumia viwakilishi vya
nomino, fanani hurudia majina ya wahusika. Kibwagizo katika wimbo pia hukaririwa.

Zoezi la kwanza la kuchambua

Hapo zamani za kale, Nyani na Mamba walikuwa marafiki wa kufa kuzikana. Watoto wao
walipendana na kufaana kama ndugu wa toka nitoke. Familia ya Mamba iliishi mtoni
nayo ya Nyani iliishi katika msitu uliokuwa maili thelathini kutoka mtoni. Kila mara
marafiki hawa walitembeleana na kusaidiana kwa hali na mali. Kwa vile Mamba alikuwa |
mvuvi mashuhuri, aliweza kumwauni Nyani na aila yake kwa samaki wa aina mbalimbali. |
Nyani naye alimpelekea Mamba matunda na nafaka kutoka shambani mwake. |
Urafiki wao ulikita mizizi na kunawiri zaidi wakati Mamba alipokuja kwa Nyani
kumposea mwanawe binti. Ukwe uliutilia viungo uhusiano wa Nyani na Mamba
wakawa wanagandana kama kupe na mkia wa ng'ombe. Wakatenda mengi pamoja.
Wakazungumza ya kupwa na ya kujaa. Hakuna hata mmoja wao aliyeutilia shaka |
uaminifu wa mwenzake. Wake zao nao walifuata kaida ya maji kufuata mkondo.
Walikuwa masahibu wa chanda na pete. ;
Msimu mmoja wa mapukutiko ulishuhudia mabadiliko ya kudumu katika maisha ya
Nyani na Mamba. Wakati huo, bahari ilichafuka si haba. Kazi ya Mamba ya uvuvi ikaanza
kukabiliwa na majabali ya kila aina. Kila mara Mamba alipokwenda uvuvini, alirudi
akichekelewa na nyavu zake. Hakuambulia chochote. Njaa ilianza kubisha hodi katika
familia ya Mamba. Hali hii ilitishia kuutia ufa urafiki kati ya Mamba na Nyani. Mamba
alivamiwa na pepo ambaye hata yeye alishindwa kumfahamu. Kila mara alipomwona

55 |

(5) Ji|
alivyojaribu
Nyani au watoto wake alitamani kumdakia na kumla mzima mzima. Kadiri
ri, “Una njaa
kujiasa dhidi ya fikira hii mbovu ndivyo moyo wake ulivyoendelea kumshau
wanawe za kuwa
bwana, familia yako itaangamia. Je, huoni rafiki yako na familia yake
anajiita rafiki
kitoweo? Utaendelea kula wishwa hadi lini? Mbona huyo Nyani ambaye
karafuu alizokuwa
yako sasa amekata guu humu? Mbona haji tena kukutazama? Hata
na akasadiki kuwa
akikuletea ameacha kuleta.” Mamba akaanza kumshuku rafiki yake
Nyani alikuwa mla naye tu.
abu nyota,
Usiku mmoja baada ya kula mate na kujilaza kitandani mwake akihes
ili apate kujiokoa
wazo lilimjia. Alikata shauri kumlaghai rafiki yake wa miaka mingi
yake alikwenda kwa
yeye na familia yake kutoka katika kinamasi cha njaa. Asubuhi
agana nilipata
Nyani akiwa amejiinamia kwa jitimai. Alisema, “Rafiki yangu, jana tulipo
a mahututi. Alisema
tanzia. Mjumbe kutoka kijijini aliniarifu kuwa baba yangu ni mgonjw
majonzi makuu.
kwamba baba ananitaka nyumbani upesi.” Habari hizi zilimtia Nyani
Nyani hangeweza
Alimwahidi Mamba kwamba wangeandamana pamoja. Kwa vile
uchefu na manyezi kila
kutembea majini, ilibidi abebwe na Mamba. Alipatwa na kichef
hivyo, Mamba
alipotazama bahari iliyojitandaza mbele yao kwa mbwembwe. Hata
kana na urafiki na mazoea
alimhakikishia kuwa wangefika salama. Naye kwa imani iliyoto
ya miaka mingi, alitulia.
ni mwa
Safari ilikuwa ndefu na yenye machovu yaliyomfanya Nyani kulala mgongo
mbarika Nyani,
Mamba. Walipofika kwenye vina vya maji, Mamba aliamua kumpasulia
kumbe uzuri wako wa
“Rafiki yangu, nimekuwa nikidhani wewe ni rafiki wa dhati,
huku maghala
mkakasi? Mimi na wanangu tumetafunwa na njaa kwa miezi kadha sasa
kama nimepata
yako yakishiba na kutapika chakula. Hujadiriki hata siku moja kuja kujua
ia hali yangu,
hata senti moja ya kusagia mkunguni. Jana usiku nilipokuwa nikiwaz
basi hali ya
nilioteshwa katika ndoto kwamba kama ningepata moyo wako na kuula,
hata hivyo lisilo
uhitaji ingeniishia. Moyo wangu unaniuma sana kukufanyia tendo hili,
budi hutendwa.”
Hata hivyo,
Nyani alipigwa na butwaa nusura moyo wenyewe ujikabidhi kwa Mamba.
pole sana ikiwa
akili yake nyepesi ilifanya kazi. Alimwambia Mamba, “Ndugu yangu,
/
umekuwa unadhani sikujali. Kwa kweli, hata ungeniomba
moyo wangu siku hizo ningekupa tu. Unajua tena sisi
Nyani, Tumbili na Kima tuna mioyo mingi. Hata
hivyo, nasikitika kuwa Mungu alituambia kuwa
daima mioyo yetu itakaa mitini. Hii ndiyo sababu
tukajenga nyumba zetu juu ya miti. Basi ndugu
mpenzi, badala ya kuendelea na safari hii, turudi
pale mtini nikupe moyo wangu pamoja na mitatu
ya wanangu kusudi uwalishe wanao na mkeo.” 4
Mamba akaingia mtegoni. Wakarudi hadi ufuoni.
Kwa vile Mamba hakuweza kutoka majini, alibaki
ufuoni akimngojea rafiki yake amletee mioyo.
Mamba alitunga macho yake kwenye ujia alioufuata Nyani akiomba pasitokee |
lolote la kumchelewesha Nyani. Matumbo yalimnguruma kwa njaa. Roho ikampapa |
kwa tumaini. Alingoja, akangoja, akangoja ... wiki, mwezi, mwaka ... Nyani hakurudi.
Mamba akajua amepwaguliwa na Nyani. Akaapa kumtafuta kwa udi na ambari. Huo
ukawa mwisho wa urafiki kati ya Nyani na Mamba.

ia
Kwa kurejelea ngano uliyoisoma, jibu maswali yafuatayo.
1. Hii ni ngano ya aina gani? Thibitisha.
2. Fafanua sifa za wahusika wafuatao:
(a) Mamba (b) Nyani.
3. Andika na utolee mifano, sifa za kimsingi za hurafa ambazo zimejitokeza
katika kisa hiki. |
Andika maadili ya kisa hiki. ; '
Onyesha mbinu tano za lugha zinazojitokeza. YAI |

Zoezi la pili la kuchambua


Hapo zamani za kale, paliondokea mtu mmoja kwa jina Mzee Kata. Mzee Kata alikuwa>
na wake wawili. Mke wa kwanza aliitwa Neema na wa pili Nduli. Kila mmoja wa wake
hawa alikuwa na mtoto mmoja. Neema alikuwa na mtoto wa kike kwa jina Majaliwa. |
Majaliwa alikuwa ameumbwa akaumbika. Uso wake ulihimili macho meupe mfano
wa theluji. Meno yake ya juu yalipangika kwa njia ambayo iliyafanya kuacha mwanya
ambao ulifanya tabasamu yake kuwa na mvuto wa sumaku. Urembo wa Majaliwa, kama
walivyosema wengi, ungemtoa nyoka yeyote pangoni.
Kwa upande mwingine, Kutu, bintiye Nduli, alikuwa mwenye sura mbaya ya |
kutisha. Uso wake usiopendeza ulimfanya kuonekana kama ajuza wa miaka mia moja! |

mara kwa kumkumbusha kuwa hakufaa kuringa. “Sura kama kiboko,” wangemtania. |
Tofauti za kiumbo kati ya Majaliwa na Kutu zilizua uhasama mkubwa kati ya |
ndugu hawa, sikwambii mama zao. Hali hii ilizidishwa zaidi na nongwa za kila siku |
zilizotokana na ukewenza. Familia ya Mzee Kata ikawa medani ya vita vya wenyewe
kwa wenyewe.
Hali ya mtafaruku iliendelea kuikosesha nyumba ya Mzee Kata amani. Asubuhi |
moja, Mzee Kata aliamka kama kawaida na kuelekea katika kibanda cha mke wake wa ji
kwanza. Kama kawaida yake, alijikohoza kama ishara ya kutangaza kufika kwake. Daima |
hakupenda kuzungumza na wakeze asubuhi na mapema. Aliamini kuwa wangemletea |
nuksi. Kinyume na siku nyingine, Mzee Kata hakuitikiwa. Ilibidi kujikaribisha nyumbani |
mwake. Mara tu alipovuka kizingiti cha kijumba hicho, alitupa macho yake juu ya |
kitanda cha mayowe ambapo mke wake alijinyosha twaa kakauka kama ukuni; hana
Pumzi. Weupe wa macho yake na mapovu yaliyomtoka kinywani yalimhakikishia Mzee

(s7)7 ||

(57)
| |
|
Kata kuwa Neema kampungia mkono. Harufu kali ya sumu ilihanikiza hewa kumwarifu
Mzee Kata kuwa mkewe kafa kwa kutendwa na mkemwenza.
Maisha ya Majaliwa yalichukua mkondo mpya baada ya tanzia hii. Mama wa kambo
sasa alipata mwanya wa kumhini Majaliwa. Kazi zote za nyumbani aliachiwa yeye, huku
Kutu akiachwa huru kucheza. Majaliwa alipewa chakula haba; wengine wakila biriani
yeye alipewa wali wa kawaida. Mavazi yake yaligeuka matambara. Siku zilivyozidi
kusonga ndivyo mateso yalivyoongezeka. Mama wa kambo alizidisha wivu wake kwa
Majaliwa. Hata Majaliwa alipovunja ungo na wachumba kuja kumposa, mama wa kambo
aliwafukuzia mbali. Wengine walihimizwa kumposa Kutu. Wachumba waliochachawa
kutaka kumwoa Majaliwa wakidai kuwa hawamtaki Kutu kwa sababu ya kiburi chake,
walinyeshewa matusi, wakahizika na kujiendea zao.
Siku moja, alitokea kijana mmoja maskini. Alikuja amevalia gwanda jeusi
lililojiinamia kwa uchovu. Viatu alivyovaa vilikuwa vimejichokea kwa kupiga lami. Kofia
iliyokuwa kichwani pake ilitosha kumhakikishia mama wa kambo kuwa huyu alikuwa
fakiri. Mama mtu alikubali mara moja posa ya kijana huyu kwa Majaliwa akijua kuwa
angeadhibika. Aliamini amemtokomeza Majaliwa ndani ya lindi la ulitima. Mzee Kata
naye hakusita kumwoza Majaliwa kwa kijana huyu maana aliiona hii kama fursa ya
pekee ya kumwepushia vitimbi vya mama wa kambo.
Majaliwa aliandamana na mume wake hadi kijiji cha Peponi ambako kijana huyu
aliishi. Waliingia katika nyumba ya msonge ambamo Majaliwa alitarajia kuanza maisha
ya ndoa. Walitayarisha chajio, wakala na kulala.
Asubuhi, Majaliwa aliamshwa na nyimbo za ndege. Alipofumbua macho, alijikuta
kalala ndani ya chumba kikubwa chenye sakafu ya vigae. Ukuta wa chumba hicho
ulikuwa wa rangi ya zari. Mapambo ya dhahabu yalitundikwa ukutani. Kumbe kijana
aliyemwoa hakuwa maskini kama ilivyodhaniwa! Alikuwa mwana wa mfalme! Na hili
lilikuwa kasri hasa! Majaliwa hakuweza kuamini! Alikuwa ameamkia maisha ambayo
hakuwahi kuyawazia.
Alipoingia sebuleni alimpata mama yake mpenzi, akiwa na tabasamu ya milele usoni.
Walikumbatiana kwa shauku kuu. Kumbe kijana huyo alikuwa ametumwa na mamake
Majaliwa! Mumewe Majaliwa alishuhudia kwa mbali, machozi ya mama mtu na mwanawe
yakilovya vifua vyao na kuyeyusha simanzi iliyokuwa imeyaandama maisha yao. Tangu
Usiku hiyo, watatu hawa waliishi kwa raha mustarehe. Hadithi yangu inaishia hapo.

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea ngano uliyoisoma.


1. Jadili athari za ukewenza katika familia.
2. Fafanua sifa za wahusika wafuatao:
(i) Mzee Kata (ii) Nduli.
3. Utungo huu unaweza kuainishwa kama ngano? Toa sababu.
4. Taja na utolee mifano, mbinu za lugha zilizotumiwa katika utungo huu?
4

Utanzu wa Semi

Utangulizi
Semi ni kauli fupi za kisanaa zenye maana na mafunzo yaliyofichika. Semi hutoa mafunzo
kwa njia ya kufumba. Mafunzo katika semi hutokana na imani ya jamii ambayo imezibuni.
Mifano ya semi ni methali, vitendawili, misemo, nahau, misimu, lakabu, mafumbo,
chemshabongo na vitanza ndimi. Semi pia huitwa tungo fupi au tungo banifu.

Sifa za semi
(a) Semi hufumba ujumbe wake. Kwa mfano, maana ya ndani ya nahau 'piga kalamu' ni
“kufuta kazi' ilhali maana ya juu ni “kuchapa au kugonga kalamu'. Methali pia huwa
na maana iliyofumbwa. Aidha, vitendawili hufumba jibu.
(b) Hutumia picha (taswira) na ishara kupitisha ujumbe wake. Mtu anaposema, “kwetu ni
jehanamu', ile picha ya jehanamu inajichora akilini mwa msikilizaji. Jehanamu hapa
inaashiria mahali pabaya penye mateso. mengi.
(c) Maana ya semi hupatikana katika jamii iliyozibuni. Methali Mgaagaa na upwa hali
wali mkavu, kwa mfano, itaeleweka na jamii za pwani. Vilevile katika tashbihi, weupe
au weusi hulinganishwa na vitu mbalimbali kutegemea jamii na mazingira yake.
Mathalani, watasema -eupe kama maziwa au -eupe kama theluji; -eusi kama mpingo,
-eusi kama lami au -eusi kama makaa kutegemea vifaa vinavyopatikana katika jamii
husika. |
(d) Huwasilisha ujumbe mrefu kwa maneno machache. Mfano ni methali Juhudi si pato
ambayo imefupisha ujumbe mrefu kuwa mtu huweza kufanya bidii sana na akakosa
kufanikiwa. Semi huwasilisha ujumbe kwa njia ya mkato tofauti na hadithi ambazo
ni masimulizi marefu.
(e) Semi ni tanzu tegemezi. Hii ina maana kwamba semi hutokea kuambatana au
kutegemea tanzu nyingine. Kwa mfano, methali hutolewa katika muktadha wa
mazungumzo ya kutoa mawaidha, au mwishoni mwa hadithi kama funzo la hadithi.

3
Lakabu, misimu, misemo na nahau pia hupatikana katika utanzu wa mazungumzo.
Umuhimu wa semi
(a) Semi huelimisha. Vitendawili, methali, mafumbo na nahau zote hutoa mafunzo
ya aina fulani. Methali Mwenda pole hajikwai hutoa maarifa ya kufanya mambo
bila pupa. ;

(b) Hukuza uwezo wa kufikiria. Vitendawili, methali na mafumbo humhitaji mtu kufikiria
ili kupata ujumbe uliofumbwa. j

(c) Hutambulisha jamii na wanajamii. Kila jamii huwa na semi mahususi zinazohusu
shughuli zake. Misimu, kwa mfano, hutumiwa na kundi fulani katika jamii. Methali
mkulima ni mmoja walaji ni wengi inatambulisha jamii inayojihusisha na kilimo, ilhali
samaki mmoja akioza na mtungo pia inatambulisha jamii ya wavuvi. Vitendawili, misimu,
nahau na mafumbo pia hutofautiana kutegemea jamii. Kitendawili kimoja kinaweza
kuwa na majibu tofauti kutegemea jamii na mazingira yake.
(d) Hukuza utangamano katika jamii. Wakati wa kutegeana vitendawili, kwa mfano,
watu huja pamoja. Aidha, misimu hujenga uhusiano wa karibu miongoni mwa watu
wanaoitumia. Lakabu nazo hutumiwa na watu walio na uhusiano wa karibu.

Huburudisha. Baada ya shughuli za kazi, watu hujumuika pamoja katika vikao vya
kujiburudisha ambapo hutegeana vitendawili na hushiriki katika vitanza ndimi ili
kutuliza bongo na kusisimka pamoja.
Huhifadhi utamaduni. Semi hufumbata desturi za jamii. Zinapopitishwa kutoka kizazi
hadi kingine, utamaduni huo hurithishwa na kuhifadhiwa.

Husawiri mitazamo ya jamii kuhusu masuala fulani. Je, jamii inachukia nini? Inahimiza
nini? Kupitia kwa methali, bidii ya mja haiondoi kudura, tunafahamishwa kwamba
jamii hii inaamini kuwa binadamu yumo chini ya uwezo wa Mungu. Nahau, lakabu,
vitendawili na mafumbo pia hufumbata tajiriba ya jamii.
Hutasfidi lugha. Nahau, misemo, misimu na lakabu hutumiwa badala ya msamiati
mkali/wenye aibu. Badala ya kusema kuzaa tunasema kujifungua.
Hukuza lugha. Semi huyapa maneno maana mpya au maana ya ziada. Misimu
huweza kukubaliwa na kuwa nahau rasmi za lugha. Kwa njia hii, msamiati wa lugha
hupanuliwa.

1. Toa mifano mitano ya semi kutoka jamii yako.


2. Andika majukumu ya semi ulizotoa katika swali la 1.
3. Toa mifano mitatu kuthibitisha kuwa semi ni aina ya sanaa.
au

Vipera vya semi

Methali
Methali ni semi fupifupi za kimapokeo zenye kueleza fikira, maarifa, hekima na mafunzo
yanayotokana na uzoefu wa jamii mahususi. Methali hutumia taswira na mafumbo.
Chukulia, kwa mfano, Fimbo ya mbali haiui nyoka. Utungo huu ni mfupi, na unatumia neno
fimbo kama fumbo la suluhisho.
Methali ni utanzu tegemezi. Kama tulivyotangulia kutaja, kutumika kwake hutegemea tanzu
nyingine. Methali hutokea katika mazungumzo mazito kama vile katika kutoa mawaidha
au kama kielelezo na kifupisho cha hadithi. Si utanzu unaoweza kujisimamia kama tanzu
nyingine kama vile hadithi, ushairi au mazungumzo.

Sifa za methali

(a) Methali ni kauli fupi ambazo hutolewa kwa mtindo wa kishairi kinyume na jinsi kauli
za kawaida zinavyowasilishwa.
(b) Methali: Ushikwapo, shikamana; Aliye juu, mngoje chini, mathalani, zina sifa za kishairi:
kuwa na vipande vyenye mizani inayolingana na kwamba ni mshororo mmoja.
(c) Maudhui katika methali huchotwa kutoka kwa jamii zinamozaliwa. Maudhui hutokana
“na tajiriba na mambo yanayoathiri jamii.
(d) Huwa na muundo maalumu wenye sehemu mbili, kwa mfano Asiyesikia la mkuu,
huvunjika guu au Pilipili usiyoila, yakuwashiani?. Sehemu ya kwanza hudokeza wazo
na sehemu ya pili hulikamilisha kwa kukubali au kukataa.
(e) Hujengwa kwa tamathali nyingine za usemi na mbinu za lugha kama vile kinaya,
taswira na takriri. Methali Kukopa arusi kulipa matanga imejengwa kwa tamathali
ya sitiari. Arusi ni sitiari ya kukopa kuonyesha kuwa mtu anapokopa huhisi vizuri.
Matanga ni sitiari ya kulipa kuonyesha kwamba watu huona ugumu kulipa deni
walilokopa. Arusi ni jambo la furaha ilhali matanga ni jambo la huzuni.
(f) Methali hueleweka na jamii iliyozibuni, kwa mfano Kikiharibika cha fundi kikiongoka
cha Bwana Swedi kwa Waswahili, na methali ya Kikamba Yakua yiisawa ngathi ni aka
(Ng'ombe akizeeka nundu huliwa na wanawake). Katika jamii ya Wakamba, sehemu
fulani za nyama huliwa na wanaume, nundu ikiwa moja yazo. Hata hivyo ng'ombe
anapozeeka sana, utamu wa nundu huisha na wanawake wanakubaliwa kuila wakati
huo tu. Methali hizi mbili zina maana sawa. Hata hivyo, methali hizi hazitaeleweka
kwa watu wa jamii tofauti na iliyozibuni.
(8) Methali zina sifa ya utegemezi na huingiliana na tanzu nyingine za fasihi.
(i) Hutumiwa mwishoni mwa ngano kufupisha maadili ya ngano hiyo.
marafiki anaweza kuitwa
(ii) Hutumiwa kubuni lakabu. Mtu ambaye huwasaliti
“kikulacho' kutokana na methali Kikulacho ki nguoni mwako.
tamthilia ili kuongeza
(iii) Hutumiwa katika tanzu za kimaandishi kama vile riwaya na
ladha katika usimulizi.
mvuto.
(iv) Hutumiwa katika mazungumzo ya kawaida na ulumbi kuleta
(v) Hutumiwa katika nyimbo na mashairi.
daawa. Mshtakiwa
(vi) Hutumiwa katika hotuba rasmi au hata mahakamani katika
ishi
anaweza kujitetea kwa kurejelea methali Mavi ya kale hayanuki. Naye mlalam
kapoa. Aidha,
anaweza kusisitiza msimamo wake kwa kudai Mwenye kovu sidhani
mbio zako zimefika
mahakimu wanaweza kutumia methali kama vile Mshtakiwa,
ukingoni kutoa hukumu.
(vii) Hutumiwa katika kutoa mawaidha.
o imebuniwa.
(h) Methali huelezea ukweli ambao unakubalika na jamii ambam
mu wa kutolewa. Methali
(i) Tofauti na vitendawili, methali hazina muktadha maalu
anaweza kutumia
hazitengewi vikao vya kutolewa kama vitendawili vifanyiwavyo. Mtu
au usio rasmi.
methali wakati wowote anapozungumza katika muktadha rasmi
i, hakuna anayeweza
(j) Methali ni mali ya jamii. Kama tanzu nyingine za fasihi simuliz
kudai kumiliki methali.
hulka, itikadi, tamaduni na
(k) Methali huambatana na mazingira ya jamii iliyozizaa,
mea mazingira
tajiriba zake. Busara fulani inaweza kuwasilishwa kwa njia tofauti kutege
kana na jamii zilizo
ya jamii. Methali zifuatazo, kwa mfano, zina maana sawa ila zinato
na mazingira tofauti:
(i) Ulingo wa Kwae haulindi Manda.
(ii) Kamba ya mbali haifungi kuni.
(iii) Fimbo ya mbali haiui nyoka.
leza majukumu
(1) Methali zina matumizi mapana. Methali moja inaweza kutumiwa kuteke
Baada ya dhiki faraja
mbalimbali kama vile kuonya, kuelekeza na kufunza. Methali
inaweza kutumiwa:
(i) kuonya dhidi ya kukata tamaa
(ii) kuhimiza mtu asife moyo, avumilie, fanaka yaja
(iii) kutoa maoni tu kuhusu hali ya ukosefu
(iv) kushauri mtu awe na subira.
na na maana halisi
(m) Methali huwa na maana ya ndani na ya nje. Maana ya nje hutoka
ndani yenye fumbo
ya maneno yaliyoiunda. Vilevile, methali hupewa maana ya
lililofumbwa na maneno yanayoiunda.
Dhima ya methali
(a) Huelimisha. Methali hutumiwa katika hafla mbalimbali kama vile sherehe za jandoni
na arusi kupitisha maarifa ya kijamii kwa vijana. Methali Abebwaye hujikaza, kwa
mfano, inaelimisha wanajamii kuwa unapopata usaidizi fulani, nawe pia jikaze kutia .
bidii; usingoje kila mara kusaidiwa. Methali pia huelimisha kuhusu historia, siasa,
uchumi na utamaduni wa jamii. Methali Sheria ni msumeno, hukata mbele na nyuma
inaelimisha kuwa sheria haichagui. Aidha, Biashara haigombi inaelimisha kuwa ni
busara kwa muuzaji kuwabembeleza wateja wake.

(b) Huadilisha. Mbali na kuelimisha, methali hufunza maadili. Mstahimilivu hula mbivu
ni methali inayofunza uvumilivu. Nayo methali Tamaa mbele mauti nyuma hukashifu
tabia ya kuwa na uroho mwingi.

(c) Husawiri mitazamo na falsafa za jamii fulani kuhusu masuala mbalimbali. Je, jamii
inapenda nini? Inachukia nini? Inathamini nini? Methali Ucha Mungu si kilemba cheupe
huonyesha jamii inachukia unafiki. Vilevile, methali Uzuri wa mwanamke ni tabia
inaonyesha jinsi jamii inavyothamini mke mwadilifu.

(d) Hutambulisha jamii. Kila jamii ina methali zake zinazoitambulisha. Mathalani, Sie
munda sisuta sie emurwe (Kilicho tumboni ndicho kilicho akilini) ni methali kutoka jamii
ya Waluhya inayoonyesha umuhimu wa chakula. Ng'ombe akivunjika mguu malishoni
hujikokota zizini inatambulisha jamii ya wafugaji.

(e) Huongeza ladha (urembo) katika mazungumzo na maandishi. Mazungumzo au


maandishi yenye matumizi mazuri ya methali huvutia. Katika baadhi ya jamii,
mwenye busara hutambuliwa kwa ukwasi wake wa lugha, matumizi ya methali ikiwa
ni mojawapo ya vigezo vya kupima ujuzi wa lugha.
Huburudisha. Katika jamii nyingine, methali hutengewa vipindi vya kutolewa na
makundi yanayoshindana. Hii ni njia mojawapo ya kutuliza bongo.
Hurithisha utamaduni wa jamii. Methali ni zao la utamaduni wa jamii husika na
hupitishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Kwa njia hii, wanajamii na vizazi vyao
huweza kurithi utamaduni wao.
Hufariji. Methali huwatuliza na kuwaliwaza watu wanapokabiliana na matukio au
hali zinazohuzunisha. Methali Kuinamako ndiko kuinukako au Hakuna refu lisilo na
ncha zinamfariji mtu aliye na matatizo kwa kumjuza kwamba hata hali ikiwa mbaya,
mambo hutengenea.
Hukuza uwezo wa kufikiri. Mara nyingi methali zinapotamkwa hazionyeshi waziwazi
maana inayokusudiwa. Mtu anahitajika kufikiri kwa makini na kuoanisha msamiati
uliotumiwa katika methali na hali ya maisha ili kupata maana ya ndani.
(j) Hukuza ushirikiano na mshikamano wa kijamii. Katika baadhi ya jamii, methali
zilitengewa vikao vya kuchambuliwa kwa kushindana. Watu walijumuika pamoja
na
katika mashindano haya. Si ajabu kuwa kuna methali nyingi zinazohimiza udugu
umoja, baadhi yazo ni: Ndugu mui heri kuwa naye; Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu;
Jifya moja haliinjiki chungu na Kidole kimoja hakivunji chawa.

1. Andika majukumu ya kijamii ya methali zifuatazo:


Zindiko la mwoga ni kemi.
(ii) Usiache kunanua kwa kutega.
(iii) Chombo hakiendi ikiwa kila mtu anavuta makasia yake.
(iv) Aibu ya maiti aijuaye mwosha.
(v) Elfu huanzia moja.
2. Toa mifano ya methali kumi kutoka kwa jamii yako kisha uzifasiri kwa lugha
ya Kiswahili.

Uainishaji wa methali
Methali huainishwa kutegemea:

1. Muktadha
methali hizo.
Ili kuelewa methali, ni muhimu kujua mazingira, tamaduni na hali zilizozizaa
Methali ambazo zimezaliwa katika muktadha au mazingira sawa huweza kuwekwa katika
kundi moja. Methali Mpanda ovyo hula ovyo, Mke ni nguo mgomba kupalilia na Ukipanda
zinahusu
pantosha utavuna pankwisha huweza kuwekwa katika kundi sawa kwa sababu
muktadha wa kilimo.

2. Maudhui
kama
Maudhui na fani ndiyo hutawala methali. Maudhui katika methali ni mengi na mapana
zilivyo jamii na shughuli zake. Methali ambazo huwa na maudhui sawa huwekwa katika kundi
moja. Baadhi ya maudhui yanayojitokeza katika methali za Kiswahili ni ya:
(a) malezi, kwa mfano:

(i) Mcha mwana kulia hulia mwenyewe.


(ii) Samaki mkunje angali mbichi.
(iii) Asiyefunzwa na mamake hufunzwa na ulimwengu.

j
(b) kazi, kwa mfano:
(i) Kazi mbi si mchezo mwema.
(ii) Mchagua jembe si mkulima.
(iii) Kazi ya bakuli husiri.
(iv) Kazi isiyo faidi kutenda si ada.
(c) ushirikiano, kwa mfano:
(i) Kidole kimoja hakivunji chawa.
(ii) Jifya moja haliinjiki chungu.
(iii) Umoja ni nguvu utengano udhaifu.

3. Mtindo au fani

Mbali na maudhui, methali hutawaliwa na fani pia. Fani katika methali hudhihirika katika
muundo, tamathali za semi na taswira inayoibuliwa. Methali ambazo huundwa kwa kutumia
fani sawa huweza kuwekwa katika kundi moja. Methali zifuatazo zimeundwa kwa kutumia
kweli kinzani.

(a) Simba mwenda pole ndiye mla nyama.


(b) Kuinamako ndiko kuinukako.

4. Jukumu
Methali huweza kuainishwa kulingana na majukumu yake. Je, methali inasifu, inakashifu,
inahimiza, inaonya ama inafariji? Methali zifuatazo hutumiwa kuonya:
(a) Mwenye pupa hadiriki kula tamu.
(b) Asiyeangalia huishia ningalijua.
(c) Usione kwenda mbele kurudi nyuma si kazi.

5. Maana
(a) Methali zenye maana sawa zinaweza kutiwa katika kundi moja, kwa mfano:
(i) Damu ni nzito kuliko maji.
Meno ya mbwa hayaumani.
(ii) Mtoto wa nyoka ni nyoka.
Mwana wa mhunzi asiposana, huvukuta. j
(b) Methali zenye maana zinazokinzana pia zinaweza kuainishwa pamoja, kwa mfano:
(i) Mvumilivu hula mbivu.
Ngoja ngoja huumiza matumbo.
(ii) Mtu pweke ni uvundo.
Manahodha wengi chombo huenda mrama.
1. Huku ukitoa mifano kutoka jamii yako, eleza vigezo vitano vya kuainisha
methali.
2. Weka methali zifuatazo katika makundi kulingana na vigezo vya maana.
(i) Ucha Mungu si kilemba cheupe.
(ii) Bila chambo hunasi samaki.
(iii) Mbaazi ukikosa maua husingizia jua.
(iv) Aliyekupa wewe kiti ndiye aliyenipa mimi kumbi.
(v) Samaki mmoja akioza na mtungo pia.
(vi) Ukitaja nyoka shika kigongo.
(vii) Tumbili akiisha miti huja mwilini.
(viii) Paka hawekewi kitoweo kulinda.
(ik) Kitema kuni temato.
(2) Mchuma janga hula na wa kwao.

Fani katika methali


Methali hujengwa kwa tamathali za usemi na mbinu nyingine za kifasihi. Baadhi ya mbinu
hizi ni:

1. Sitiari
Sitiari ni mbinu ya kulinganisha kitu na kingine bila kutumia maneno ya kulinganisha kama
vile kama, mfano wa na mithili ya. Methali zinazoundwa kwa sitiari ni pamoja na:
(i) Mgeni ni kuku mweupe. Hapa mgeni anafananishwa moja kwa moja na kuku mweupe
kuonyesha mgeni hutambulika haraka akiwa kundini.
(ii) Ahadi ni deni. Ahadi inafananishwa na deni kuonyesha kuwa ni sharti mtu kutimiza
ahadi aliyoiweka.

2. Takriri

Takririnimbinu ya kurudiarudia maneno au sauti kwa nia ya kusisitiza. Methali zenye


takriri ni kama vile:
(i) Ngoja ngoja huumiza matumbo. Neno ngoja limerudiwa.
(ii) Haba na haba hujaza kibaba. Neno haba limerudiwa.

3. Tashbihi

Tashbihi ni tamathali ya usemi inayolinganisha vitu kwa kutumia maneno ya kulinganisha


kama vile mfano wa, kama na mithili ya. Mifano ya methali zinazotumia tashbihi ni:

|
au

(i) Kawaida ni kama sheria. Kawaida imefananishwa na sheria kuonyesha kuwa jambo la
kawaida ni kaida.
(ii) Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza. Lisilojulikana linalinganishwa na kiza.

4. Tanakali za sauti .

Hizi ni miigo ya sauti zinazotolewa na kitu au zinazotokea tendo linapotendeka. Methali


zinazotumia tanakali za sauti ni kama vile:
Chururu si ndo ndo ndo! "ndo! ni mlio unaotokea maji yanapodondoka.
“Chururu' ni mlio unaotokea maji yanapotiririka.

5. Taswira

Taswira ni picha zinazojengeka akilini mwa mtu baada ya kusoma, kutazama au kusikia
maelezo fulani. Taswira hizi hutokana na tajiriba pamoja na mazingira ya mtu. Ifuatayo
ni mifano ya methali zinazotumia taswira.
(i) Mti mkuu ukigwa wana wa ndege huyumba. Hapa, taswira au picha ya mti ulioanguka na
wana wa ndege kwenye viota inaonyesha jinsi kiongozi akifa au akipatwa na matatizo,
anaowaongoza pia huingia mashakani.
(ii) Mpanda farasi wawili hupasuka msamba. Taswira ya mtu apandaye farasi wawili na
kuathirika vibaya inajitokeza.
Kumbuka kuwa tamathali nyingine huweza kutumiwa kujenga taswira. Tashbihi na sitiari,
kwa mfano, zinaweza kuibua taswira ya jambo linalofananishwa.

6. Kweli kinzani

Katika kweli kinzani, maana ya maneno hukinzana kijuujuu (husikika kuwa haiwezekani)
lakini ikichunguzwa kwa undani kuna ukweli fulani uliofichika. Ifuatayo ni mifano ya
methali zinazotumia ukinzani:
(i) Wagombanao ndio wapatanao. Ukinzani unajitokeza kwamba kugombana na kupatana
ni vitendo tofauti na haviambatani. Watu hawawezi kugombana na wakati huo huo
wakawa wanapatana. Hata hivyo, ikichunguzwa kwa undani, ukweli wa kauli hiyo
unadhihirika. Watu waliowahi kukosana, baadaye huweza kuibuka kuwa marafiki
wakubwa.
(ii) Ukupigao ndio ukufunzao. Anayekupiga hakufundishi. Lakini, kwa ndani kuna
ukweli kwamba kila ambacho kinakuadhibu ndicho kinachokupa funzo la kudumu,
hutakirudia.

7. Chuku
Chuku ni mbinu ya kuongezea sifa za kitu zaidi ya kilivyo. Mifano ya methali zinazotumia
chuku:
(i) Usipoziba ufa utajenga ukuta. Hatari ya kupuuza “ufa' imetiliwa chumvi.
na kukejeliwa
(ii) Mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi. Mzigo wa mwingine unapigwa chuku
kwa kulinganishwa na kanda la usufi ambalo ni jepesi sana.

8. Taashira au ishara
:
Katika taashira, kitu kimoja huashiria kingine. Mifano ya methali zenye taashira
kubwa baada
(i) Kimya kingi kina mshindo mkuu. Methali hii inaashiria kutokea kwa jambo
ya utulivu au kimya.
Mgeni
(ii) Kuku mgeni hakosi kamba mguuni. Kamba mguuni pa kuku ni ishara ya ugeni.
hakosi kujulikana katika kundi la wenyeji.

9. Dhihaka, stihizai au kejeli


Kwa mfano:
Hii ni mbinu ya kufanyia mzaha au kudharau tabia au mienendo isiyofaa.
fimbo
(i) Hawi Musa kwa kuchukua fimbo. Methali hii inadhihaki anayefikiria kuwa kubeba
kutampa mamlaka ya mtu mwingine.
i kwa mavazi.
(ii) Ucha Mungu si kilemba cheupe. Inadhihaki wanaojidai kuwa waumin
Methali hizi zinakashifu unafiki wa kidini.

10. Tashihisi au uhaishaji


sifa za
Tashihisi ni mbinu ya kukipa kitu sifa za kibinadamu au kitu kisicho hai kupewa
kitu kilicho hai. Kwa mfano:
u aliye hai
(i) Adhabu ya kaburi aijuaye ni maiti. Hapa maiti amepewa uwezo wa binadam
kufahamu mambo.
mu hali ya
(ii) Siri ya mtungi aijuaye kata. Kata inapewa sifa ya kibinadamu ya kufaha
mtungi ya kuwa na siri.

11. Balagha
Balagha ni maswali yasiyohitaji majibu. Maswali haya humchochea mtu kufikiri.
(i) Pilipili usoila yakuwashiani?
(ii) Mavi usoyala wayawingiani kuku?
kuambiwa
Methali hizi zimeundwa kwa mbinu ya swali ambalo linamhitaji mwenye
kufikiria.

12. Tanakuzi
, sehemu moja
Hii ni mbinu inayotumia maneno au kauli zinazopingana. Katika tanakuzi
ya methali huwa na maana inayopingwa na sehemu ya pili.
ad
(i) Tamaa mbele mauti nyuma.
(ii) Mpanda ngazi hushuka.
Maneno yaliyokolezwa wino yana maana zinazopingana.

13. Kinaya
Kinaya ni kinyume cha matarajio au cha kauli inayosemwa au cha hali ilivyo. Kwa mfano:
(i) Kigumba kwa nguruwe kwa mwanadamu ki uchungu. Baadhi ya watu huwadhulumu
wengine na wao wanapodhulumiwa hulalamika.
(ii) Kikiharibika cha fundi kikiongoka cha Bwana Swedi. Jambo likiharibika mwenye
kulishughulikia ndiye hulaumiwa lakini likitia fora pongezi hazimwendei ila
humwendea mkubwa wake.

Muundo wa methali

Methali kwa kawaida huwa na muundo wenye sehemu mbili. Sehemu ya kwanza hudokeza
wazo, nayo ya pili hulikamilisha. Mifano:
(i) Baada ya kisa/mkasa.
(ii) Debe shinda/haliachi kutika.
(iii) Dawa ya moto/ni moto.

Uchambuzi wa methali
Maswali yafuatayo yatakusaidia katika kuchambua au kuhakiki methali:

(a) Methali imerejelea vifaa gani au inahusu nini? Kwa mfano, inarejelea wanyama,
binadamu ama vifaa vya nyumbani? Methali Hindi ndiko kwenye nguo na wendao uchi
wapo inarejelea vifaa vifuatavyo:
(i) Nchi - Hindi |
(ii) Rasilimali — Nguo
(iii) Watu — Waendao uchi/wahitaji/maskini.

(b) Methali imebuniwa kwa kutumia tamathali gani au mbinu gani za kifasihi? Kwa mfano:
(i) Haba na haba hujaza kibaba.
(ii) Haraka haraka haina baraka.
Methali hizi zimeundwa kwa mbinu ya urudiaji au takriri. |
Methali (i) imerudia neno haba na sauti ba ilhali (ii) imerudia neno haraka na sauti |
ka. |
pole ndiye mla nyama inaibua taswira
(c) Methali inaibua taswira gani? Methali Simba mwenda ni sharti uwe na subira.
kufanikiwa
ya utulivu, makini na subira; kwamba ukitaka
Methali Mtu pweke ni uvundo inaonyesha
(d) Methali inakupa wazo gani kuhusu jamii?
kuwa jamii husika inachukia utengano.
inayopingana na hii? Methali
(e) Je, kuna methali nyingine inayokaribiana kimaana au
zina maana sawa; nazo: Bidii
Wino wa Mungu, haufutiki na Bidii ya mja haiondoi kudura
ainame zinapingana kimaana.
ya mja haiondoi kudura na Mtaka cha mvunguni sharti
dha gani? Kwa mfano:
(£) Je, methali imejikita katika mazingira ama mukta
Mjini)
(i) Jogoo wa shamba hawiki mjini. (Mashambani/
(ii) Mgaagaa na upwa hali wali mkavu. (Pwani)
(iii) Ucha Mungu si kilemba cheupe. (Dini)
gani? Inanuia kuonya, kushawishi, kufahamisha
(8) Je, dhamira ya methali yenyewe ni inaelimisha; Uzuri wa
ea bila habari
au kukashifu? Kwa mfano Mali bila daftari hupot
refu lisilokuwa na ncha inaliwaza.
mkakasi ndani kipande cha mti ina kejeli ilhali Hakuna

katika kundi moja kulingana


1. Andika methali mbilimbili zinazoweza kuwekwa
na vigezo vifuatavyo vya kuainisha methali.
(b) Maudhui (c) Jukumu
(a) Mtindo
(d) Muktadha wa mahali (e) Maana
na zifuatazo:
2. Andika methali nyingine mbili zenye fani sawa
(a) Zingwizingwi lipe nguo utaona mashauo.
(b) Mwenye shibe hamjui mwenye njaa.
(c) Tabia ni ngozi ya mwili.
(d) Ikinona sana hujikaanga yenyewe.
(e) Mla ni mla leo, mla jana kalani?
3. Andika fani zilizojenga methali zifuatazo:
(a) Ganda la mua la jana chungu kaona kivuno.
(b) Asiyejua maana haambiwi maana.
.
(c) Aliyekupa wewe kiti ndiye aliyenipa mimi kumbi
(d) Chema chajiuza kibaya chajitembeza.
utapatwa na neno.
(e) Ukiona neno usiseme neno, ukisema neno
(£) Mapenzi ni kikohozi, hayafichiki.
(g) Kufa kikondoo ndiko kufa kiungwana.
(h) Kunguru mwoga hukimbia ubawa wake.
(i) Meno ya mbwa hayaumani.
(j) Mgala muuwe na haki umpe.
ai

Vitendawili
Kitendawili ni kauli yenye fumbo ambalo hutolewa kwa hadhira hai ili ilifumbue. Jibu la
kitendawili ndilo fumbo lenyewe.

Sifa za vitendawili
(a) Kwa kawaida, vitendawili ni semi fupifupi zinazotumia lugha ya mkato. Kwa mfano: |
'Pa' funua 'pa' funika. (Jibu: Nyayo wakati wa kutembea.) |
|
|
(b) Vitendawili hutolewa kwa hadhira ili vifumbuliwe. Hivyo, hadhira yake ni hai na tendi.
|
(c) Hutumia lugha ya picha au taswira na vina ukwasi wa tamathali za semi. |
Jj!
(d) Vitendawili huhitaji watu au makundi mawili ili kukamilisha uwasilishaji wavyo. Mtu |
wa kwanza hutega, na mwenzake hutegua.
(e) Vitendawili huwa na muundo au fomyula maalumu ya uwasilishaji. Kwa mfano:

Mtegaji: Kitendawili! |
Mteguaji: Tega!
Mtegaji: — Nyumba yangu haina mlango.
Mteguaji: Yai.

(£) Vitendawili huwasilishwa kwa mtindo wa majibizano kati ya mtegaji na mteguaji.


Mteguaji akishindwa kutegua, huhitajika kutoa mji ndipo kupewa jibu na mtegaji.

(g) Kitendawili ni fumbo au swali lililofichika ambalo huhitaji jibu. Kwa mfano, Mzungu
katupwa jalalani. (Jibu: Machicha ya nazi.) Machicha ya nazi ndilo fumbo lililofumbwa.
(h) Fumbo au jibu la kitendawili hufahamika tu na jamii ambamo kitendawili hicho
kimezaliwa. Kitendawili kinaweza kuwa na majibu mawili kutegemea mazingira ya
jamii. Kwa mfano, vitendawili vifuatavyo huweza kuwa na jibu zaidi ya moja:
(i) Wanangu wawili hushabihiana. Majibu: Tui na maziwa; Unga na majivu.
(ii) Mwarabu kasimama kwa mguu mmoja. Majibu: Uyoga; Mwavuli.
(i) Vitendawili ni sanaa ambayo kwa kiasi kikubwa hutegemea uwezo wa mtu kutambua j
na kuhusisha au kulinganisha vitu katika mazingira yake. Kwa mfano, ili kufumbua
fumbo la kitendawili Mbili mbili hadi pwani, lazima mtu awaze kuhusisha vitu viwili |
ambavyo daima hufanya jambo pamoja. (Jibu ni Macho.) Macho hutazama pamoja,
hulala pamoja, hulia pamoja.
|
() Vitendawili huingiliana na tanzu na vipera vingine vya fasihi simulizi. Kwa mfano, |
ngano. za mtanziko hutumia vitendawili, hasa katika fomyula ya ufunguzi wa ngano. |

|
|
ya vikao
Aidha, vitendawili hutangulia vikao vya kusimulia hadithi au hutegwa baada
hivyo.
(k) Vitendawili hubadilika kutegemea wakati au kipindi cha kihistoria na maendeleo
ya jamii. Kitendawili kimoja kinaweza kuundwa au kutolewa kwa maneno tofauti
kulingana na kipindi cha wakati kinapotumiwa. Kwa mfano:
(i) Mwarabu wangu nimemtupa biwini. (Jibu: Machicha ya nazi).
.
(ii) Mzungu katupwa jalalani. (Jibu: Machicha ya nazi).
o vina
Maneno tofauti (Mwarabu na Mzungu) katika vitendawili hivi viwili ambavy
jibu moja yanaonyesha viliathiriwa na nyakati tofauti za kihistoria.
na methali
(1) Vitendawili ni sanaa inayotendwa kwa hivyo hujisimamia yenyewe tofauti
kutolewa.
ambazo kwa kawaida ni sanaa tegemezi. Hutengewa vikao maalumu na
zote za maisha ya
(m) Kimaudhui, vitendawili hushughulikia masuala katika nyanja
ali
binadamu na mazingira yake. Maudhui haya hutofautiana katika jamii mbalimb
ingawa baadhi yao kama vile maudhui ya njaa, imani na usafiri huingiliana. Kwa mfano:
Kamba yangu ndefu lakini haiwezi kufunga kuni. (Jibu: Njia.)
Hapa kamba na kuni ni vifaa vya kawaida katika jamii nyingi za Kiafrika.
(n) Vitendawili vinaweza kuwa sahili (rahisi) na vingine changamano.
Mungu.)
Mfano wa kitendawili sahili ni: Anatuona lakini hatumuoni. (Jibu:
ngozi na
Mfano wa kitendawili changamano: Tunda lake la ajabu; juu nyama, katikati
ndani mchanga. (Jibu: Firigisi.)
nyingine watoto na
Vitendawili ni semi maarufu sana miongoni mwa watoto. Katika jamii
wazima walishindana
watu wazima hushiriki. Miongoni mwa Wakamba, kwa mfano, watu
katika uteguaji wa vitendawili hata kuliko watoto.

Dhima ya vitendawili
mazingira
(a) Vitendawili huelimisha. Vitendawili hujumuisha masuala mengi katika
kuhusu
ya jamii. Hali hii inavifanya kuwa na uwezo mkubwa wa kuelimisha watu
kutoa mji.
mazingira yao. Aidha, mtu akikosa jibu la kitendawili haadhibiwi zaidi ya
kupata jibu
Akishataja tu hupewa jibu. Kwa hivyo, katika vitendawili, kukosa jibu au
ni njia za kuelimisha.
utegaji
(b) Huburudisha. Vitendawili huwapumzisha na kuwapumbaza wanaoshiriki katika
na uteguaji wavyo. Hili ni jukumu lililohifadhiwa vitendawili tangu jadi.
twa
(c) Hufundisha kaida na maadili ya jamii. Vitendawili huwa na utaratibu fulani unaofua
njia moja ya
na ambao washiriki wanapaswa kuuheshimu na kuuzingatia. Hii ni
miwe.
kuadilisha kuwa kila jambo maishani lina kaida zake ambazo ni lazima ziheshi
ishwa.
Kukosa jibu la kitendawili si sababu ya kulaaniwa lakini ni njia ya kufaham
(d) Hukuza ubunifu na stadi ya kufikiri haraka. Mteguaji wa kitendawili sharti afikiri na
kuoanisha yaliyotajwa na mazingira yake ili kupata jawabu. Vitendawili hukuza ari
ya kufikiria na kudadisi mazingira. |
(e) Vitendawili hudhihaki na kukejeli watu, hali au tabia hasi katika jamii. Hukashifu
matendo hasi na kusifu yale chanya. Kitendawili Rudi nyuma nikuonyeshe (ambacho jibu
lake ni Mavi ya mlevi) kinatumia stihizai kukashifu ulevi na kuhimiza usafi. Mzungu
katupwa jalalani. (Jibu: Machicha ya nazi.) Hapa mzungu anadhihakiwa, pengine kwa
sababu za kihistoria za kudharau Waafrika na hatimaye kufurushwa kwao.
(f) Husawiri mitazamo na itikadi ya jamii kuhusu hulka fulani. Kitendawili Nyumbani
kwetu kuna papai lililoiva sana lakini nashindwa kulichuma (Jibu: kaka au dada),
kinaonyesha kuwa ndoa kati ya dada na kaka haziruhusiwi; ni mwiko.
Hukuza uwezo wa kukumbuka. Vitendawili hutumiwa kama chemshabongo ya kujaribu
uwezo wa mtu kukumbuka na kuhusisha mambo.
Huleta umoja na ushirikiano katika jamii. Watu hujumuika pamoja wakati wa
kutegeana vitendawili. Kwa njia hiyo utangamano huimarika.
Hutambulisha jamii. Kila jamii huwa na vitendawili vyake vinavyoonyesha mazoea,
hali, tajriba na mazingira ya jamii husika.
Huchochea tabia ya udadisi. Uzoefu wa kutafuta kiini cha kitendawili hujenga tabia
ya kutaka kufichua jambo lililofichika. Kwa kujaribu kupata jibu la fumbo katika
kitendawili, wanajamii huimarisha ari yao ya kutafiti mambo ili kubaini kiini chake.
(k) Vitendawili hukuza na kusambaza ujuzi wa lugha. Vitendawili vina ukwasi mkubwa
wa lugha na tamathali za semi. Kwa hivyo, ni nyenzo kuu ya kukuza na kusambaza
masuala ya lugha katika jamii.

Fani katika vitendawili


Vitendawili, kama vipera vingine vya fasihi simulizi, ni sanaa inayotumia lugha kiufundi
kuwasilisha ujumbe. Baadhi ya vipengele vya kifani katika vitendawili ni:

Muundo

Kama tulivyotaja awali, vitendawili huwa na fomyula au muundo maalumu wa uwasilishaji:


(i) Kitangulizi cha kitendawili ambacho hutolewa na mtegaji.
Mtegaji: Kitendawili!
(ii) Hadhira humpa ruhusa ya kutega. Mteguaji: Tega!
(iii) Mtegaji hutoa kitendawili: Mtegaji: Fatuma mchafu.
(iv) Jibu hutolewa na mteguaji. Mteguaji: Nguruwe. (kosa)
N
(v) Jibu likikosekana mtegaji huomba mji. Mtegaji: Umenoa. Nipe mji.
(vi) Mteguaji hutoa mji. Mteguaji: Ninakupa Migingo.
(vii) Mtegaji akipewa mji hutoa jawabu sahihi. Mtegaji: Nilienda Migingo, watu wa
Migingo wakaniambia nikija niwasalimu. Jibu lake ni ufagio.

Mtindo
Vitendawili hutolewa kwa mtindo wa majibizano. Majibizano haya huwa kati ya mtegaji
na mteguaji au mtegaji na hadhira ya wasikilizaji. Utaratibu ulioelezwa katika muundo
huzingatiwa na mtegaji na mteguaji/hadhira.

Lugha

1. Sitiari
Aghalabu, vitendawili hutumia sitiari. Kwa mfano:
(i) Fatuma mchafu — (Ufagio). Hapa Fatuma ni sitiari ya ufagio.
(ii) Saa yetu kadiri inavyotembea ndivyo inavyopunguza nguvu — (Moyo). Saa ni sitiari
ya moyo.
(iii) Jani la mgomba laniambia habari zinazotoka ulimwenguni kote — (Gazeti/jarida).
Jani la mgomba ni sitiari ya gazeti/jarida.

2. Tashihisi/Uhaishaji
Wakati mwingine, vitendawili hutumia mbinu inayoipa kitu kisicho hai sifa za kibinadamu.
Kwa mfano:
(i) Akizungumza kila mtu hubabaika — (Radi). Hapa, radi imepewa sifa ya kuzungumza
kama binadamu. Sauti kali ya radi huwaogofya binadamu.
(ii) Amenifunika kote kwa blanketi lake jeusi — (Giza). Giza limepewa sifa ya binadamu
ya kumfunika mwingine.
(iii) Daima nasababisha mafarakano — (Ukewenza). Hapa, ukewenza umerejelewa
kwa nafsi ya kwanza.

3. Taashira
(i) Faiza akiniona ajificha — (Mzee kobe). Kinachoashiriwa na kujificha kwa Faiza ni
Kobe.
(ii) Chonge la nyoka huuma hata walio mbali — (Ugonjwa). Chonge la nyoka linaashiria
ugonjwa.

4. Stihizai/dhihaka/kejeli
Vitendawili vinavyobuniwa kwa dhihaka hutumiwa kukashifu mienendo hasi katika jamii.
Pia hueleza sifa ya kitu kwa njia ya kebehi (dharau). Kwa mfano:
di
(i) Akivaa miwani hafanyi kazi vizuri — (Mlevi). Kitendawili hiki kinakashifu ulevi. |
(ii) Babangu amevaa koti la chuma - (Mzee kobe).
(iii) Upara wa Mwarabu unafuka moshi — (Chai ya maziwa). |
(iv) Uzi mwembamba umefunga dume kubwa — (usingizi).

5. Kweli kinzani
Vitendawili vya aina hii huundwa kwa hoja mbili ambazo zinapingana. Mifano:
(i) Ajenga ingawa hana mikono — (Ndege). Ndege hana mikono kama binadamu,
hata hivyo yeye hujenga kiota.
(ii) Ana meno lakini hayaumi — (Kichana). Meno ya kichana hutumiwa kuchana wala
si kuuma.
(iii) Hufa ikifufuka — (Bahari kupwa). Maji ya bahari kupwa (kutoka ufukweni) ni |
kurejea.

6. Tanakali za sauti |
Kuna vitendawili vinavyoundwa kwa tanakali za sauti. Kwa mfano:
(i) 'Chubwi' — (Jiwe likianguka ndani ya maji). |
(ii) 'Prrr mpaka Makka' — (Utelezi). |
iii) 'Pa' funua pa' funika — (Nyayo wakati wa kutembea).

7. Takriri
| Baadhi ya vitendawili huundwa kwa kurudia neno au sauti. Kwa mfano:
(i) Aliwa yuala, ala aliwa — (Papa).
(ii) Amezaliwa Ali, amekufa Ali, na amerudi Ali — (Nywele).
(iii) Mama kazaa mtoto, mtoto kazaa mtoto na mtoto kazaa mtoto — (Kuku na yai).

8. Taswira
Baadhi ya vitendawili vimeundwa kwa jinsi ya kuibua taswira au picha mbalimbali. Kwa |
mfano: j |
(i) Nimemwona Bi Kizee akijitwika machicha — (Mvi). |
(ii) Ameingia shimoni akiwa uchi, akatoka amevaa nguo nzuri — (Mbegu).
Mtu anaposikiliza vitendawili kama hivi, anajenga picha akilini mwake. Katika picha hiyo |
ndimo mna jawabu la kitendawili chenyewe. |

9. Utata

Baadhi ya vitendawili huweza kufasiriwa kwa njia zaidi ya moja. Tunasema kitendawili
cha aina hii kina utata. Utata katika vitendawili husababishwa na hali kwamba jibu |
la kitendawili hutokana na mazingira. Watu tofauti huweza kuwa na majibu tofauti
kwa kitendawili hicho hicho kutegemea hali ambayo inawazunguka. Kwa mfano: |
(i) Inachurura inaganda — (Asali au gundi).

(ii) Gari la kila mtu — (Miguu au jeneza au kifo).

10. Vitendawili vinavyohusiana na methali


(i) Ukichukua mama chukua na mtoto — (Sagio/jiwe dogo la kusagia linalopitishwa juu
ya jiwe kubwa).
Methali: Ukivuta sagio uchukue kabisa na jiwe dogo la kusagia.
(ii) Mzee amekufa na vyombo vimevunjikavunjika — (Kifo cha kiongozi husababisha
matatizo).
Methali: Mti mkuu ukigwa wana wa ndege huyumba.

Mifano ya uchambuzi wa vitendawili kifani


Eleza mbinu za lugha zilizounda vitendawili vifuatavyo:
(a) Ndege wengi baharini — (Nyota angani).
Kitendawili hiki kimejengwa kwa:
(i) Taswira: Mtu anapokisoma anajenga picha ya ndege wengi baharini.
(ii) Istiari: Ndege ni sitiari ya nyota. Bahari ni sitiari ya anga.
(b) Natembea shambani — (Wembe wa kunyolea ukiwa kichwani).
Kitendawili hiki kimejengwa kwa:
(i) Taswira: unapata picha ya mtu akitembea.
(ii) Tashihisi: wembe kupewa uwezo wa kutembea.
(c) Pambo juu ya jiwe — (Upara).
Kitendawili hiki kimejengwa kwa:
(i) Taswira: Picha ya pambo likiwa juu ya jiwe inamjia mtu akilini.
(ii) Sitiari. Pambo ni sitiari ya nywele; jiwe ni sitiari ya upara.
(iii) Dhihaka/stihizai: Upara unakejeliwa kwa kuitwa pambo.
(d) Hulia huku akiunganisha — (Cherehani).
Kitendawili hiki kimejengwa kwa:
(i) Tashihisi: Cherehani kupewa uwezo wa kulia.
(ii) Taswira: Picha ya anayelia akiunganisha inajitokeza.
(e) Hukopa lakini halipi — (Kifo).
Kitendawili hiki kimeundwa kwa:
(i) Ukinzani: Kutolipa ilhali amekopa.
(ii) Tashihisi: Kifo kimepewa uwezo wa kukopa na kukataa kulipa.
(iii) Kinaya: Tunatarajia akikopa alipe.
(£) Kisiki chetu hakikui — (Mbilikimo).
Kitendawili hiki kimejengwa kwa:
(i) Stihizai/kejeli: Mtu kulinganishwa na kisiki kisichokua.
(ii) Sitiari: Kisiki ni sitiari ya mbilikimo.
(iii) Taswira: Picha ya kisiki cha mti kujitokeza.

Kufanana na kutofautiana kwa methali na vitendawili


Methali na vitendawili hufanana kwa vile:
(i) ni tungo fupi.
(ii) huwa na maana fiche.
(iii) hutumia lugha inayojenga taswira.
(iv) hupata maana kulingana na jamii.
(v) hufumbata ukweli fulani wa kijamii.
(vi) huweza kutumiwa katika shughuli rasmi kama vile katika maamuzi ya kesi na utoaji
hotuba.
(vii)huweza kutekeleza majukumu sawa kama vile kuonya, kuburudisha au kunoa bongo.

Methali na vitendawili hutofautiana kama ifuatavyo:


Vitendawili

(i) Kimuundo, vitendawili huwa (i) Methali kwa kawaida haina fomyula
na fomyula mahususi ya mahususi ya uwasilishaji.
uwasilishaji.
(ii) Huwa na fumbo ambalo lazima (ii) Fumbo halifumbuliwi papo hapo.
lifumbuliwe na hadhira papo Huwasilishwa kwa mwenye kutumia
hapo. methali.
(iii) Vitendawili huwa maarufu zaidi (iii) Methali hutumiwa zaidi kama semi za
miongoni mwa watoto/vijana. kuonyesha hekima hasa miongoni mwa
wazee na watu wazima.

(iv) Kwa kawaida vitendawili (iv) Si lazima methali zitengewe vikao


hutolewa katika vikao maalumu. maalumu. j

(v) Vitendawili kwa kawaida huwa (v) Si lazima methali zitolewe hadhira
na hadhira tendi inayotoa maana tendi. Huweza kutolewa kama funzo au
yake. changamoto kwa hadhira inayosikiliza au
kusoma.

(vi) Huwasilishwa kwa majibizano kati (vi) Huwasilishwa kwa kauli moja tu na
ya mtegaji na mteguaji. msemaji.
“Vitendawili ni aina ya sanaa. Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano mwafaka.
Andika tamathali za semi zilizojenga vitendawili vifuatavyo:
(a) Sanduku la babu latufurahisha. (Gitaa)
(b) Wanisikia tu wala hawanijui. (Mtangazaji wa redio)
(c) Mshale wangu umekita katika nyama nawatafuta wazee waje kunitolea.
(Mvulana akishampata mchumba)
(d) Mgongo wa bibi mchafu. (Chungu)
(e) Nina mawe yangu madogo lakini yanamaliza mlima. (Macho)

“Dhima ya vitendawili ni kuburudisha tu.' Jadili.


4. Andika mifano miwili miwili ya vitendawili vinavyoundwa kwa mbinu
zifuatazo:
(a) Tasfida (b) Takriri (c) Dhihaka/stihizai
(d) Kinaya (e) Taswira (f) Ukinzani

Misimu

Misimu ni semi za muda ambazo hubuniwa na kutumiwa katika mazingira maalumu na


katika kipindi maalumu cha wakati. Misimu huitwa pia simo. Misimu inaweza kupata
mashiko katika jamii na kukubaliwa kama msamiati au semi rasmi za lugha.

Sifa za misimu

(a) Misimu ni semi au msamiati ambao huzuka na kutoweka baada ya muda fulani.
na
(b) Hutumiwa na wanajamii katika mawasiliano yao katika kipindi fulani cha wakati
mahali fulani.
misimu
(c) Hutumiwa na kundi fulani la watu kufanikisha mawasiliano. Kwa mfano, kuna
ya vijana, ya wafanyakazi katika vyombo vya usafiri na hata ya watoto.
(d) Ingawa misimu huzuka na kutoweka baada ya muda, baadhi ya misimu hudumu na
kukubalika kama semi au msamiati sanifu wa lugha husika. Kwa mfano, neno chai (kwa
maana ya hongo) lilianza kama msimu, kisha likashika na kukubalika kama msemo
sanifu.
mahali
(e) Misimu hupata maana yake kutoka kwa watumiaji pamoja na muktadha wa
na wakati. Kwa mfano, neno sare ni msimu uliopata maana katika sekta ya usafiri wa
matatu likimaanisha kubebwa bila malipo. Aidha, pauni ya Uingereza ilipokuwa na
thamani ya shilingi ishirini za Kenya, noti ya shilingi ishirini ilirejelewa kama paundi.
Baada ya mabadiliko ya wakati na kiuchumi, ilikuja kurejelewa kama mbao. Huenda
neno hili litabadilika tena au lisalie hivyo. ;
(f) Misimu si semi sanifu, hivyo haipaswi kutumiwa katika miktadha rasmi.

(8) Misimu huundwa kwa mbinu mbalimbali kama vile kutohoa maneno au kugeuza
mpangilio wake, kwa mfano risto (hadithi) kutoka neno 'story' la Kiingereza.

Dhima ya misimu
Misimu hutumiwa kutekeleza majukumu mbalimbali katika jamii, kama ifuatavyo:
(a) Ni kitambulisho cha kundi fulani la watu. Misimu ya mabaharia, kwa mfano,
huwatambulisha na kuwatofautisha mabaharia na vikundi vingine vya wafanyakazi
katika vyombo vya baharini kama vile makuli.
(b) Misimu huhifadhi siri za wanaoitumia. Watu hutumia misimu ili kulinda siri zao
zisijulikane.
(c) Hutumiwa kuibua hisia mbalimbali miongoni mwa wazungumzaji. Kwa mfano, waasisi
wa misimu chungwa na ndizi nchini Kenya wakati wa kura ya maoni kuhusu katiba
mpya mwaka 2005 waliitumia misimu hii kunadia wito wao wa kupinga au kuunga
mkono katiba hiyo.
(d) Hukuza ushirikiano, uzalendo na uaminifu miongoni mwa wanaoitumia. Lugha ni
nyenzo kuu ya kuwaunganisha watu, hivyo wanajamii wanapotumia misimu sawa,
hujiona kuwa na mionjo, hali na maazimio sawa.
(e) Huongeza haiba au ladha katika lugha, hivyo kuondoa ukinaifu unaotokana na kutumia
msamiati uliozoeleka miaka nenda miaka rudi.
(£) Hutumiwa kupunguza makali katika lugha au kutasfidi lugha. Badala ya kutumia neno
la aibu au msamiati unaoibua masikitiko, watu hubuni misimu kuelezea jambo kwa
njia nyepesi isiyoumiza.
(8) Hukuza lugha zaidi. Wakati mwingine misimu hukubalika kama msamiati rasmi,
misemo, methali au nahau katika lugha fulani. Kwa mfano, maneno matatu na daladala
ni misimu iliyoibuka kurejelea magari ya uchukuzi wa umma nchini Kenya na Tanzania
mtawalia. Kwa sasa, maneno haya yanakubalika kama msamiati rasmi wa lugha ya
Kiswahili.
Huhifadhi utamaduni na historia ya jamii. Kwa vile misimu tofauti hutumiwa katika
vipindi mbalimbali vya wakati, kuwapo kwake huakisi maendeleo, ukuaji, historia na
mabadiliko katika jamii husika.
Ni kielelezo cha mpangilio (mfumo) wa jamii fulani, kijamii na kiuchumi. Kwa vile
misimu hutambulisha matabaka katika jamii, tunaweza kutambua ni matabaka gani
yanayounda jamii hiyo.
Hutumiwa kuondoa urasmi katika mazungumzo. Vijana, kwa mfano, wanapotumia
misimu badala ya semi sanifu, huondoa urasmi na kudumisha uhusiano wa kirafiki.
YA

(k) Hukuza uwezo wa kufikiri na kutathmini au kudadisi. Ili kuelewa misimu fulani, ni
lazima ufikirie na kutathmini chanzo cha msamiati huo. Mathalani Mukoloni (mama)
ni mfano wa msimu wa nyumbani. Ili kuuelewa, inabidi ufikirie zaidi na kupima ni
nani aliye na tabia za kudhibiti watoto zaidi kati ya mama na baba.

Uainishaji wa misimu
Misimu hutofautiana kutegemea:
(a) Wahusika. Kuna misimu ya vijana, mabaharia au wanafunzi. Neno beste hutumiwa
na vijana kumaanisha rafiki.
(b) Matilaba. Kuna misimu ya kuendeshea biashara. Neno kung'ara linamaanisha kuvaa
nguo inayopendeza na sare linamaanisha kubebwa kwenye matatu bila kulipa nauli.
(c) Vifaa. Kuna misimu ya vyakula, pesa na vyombo vingine. Maneno nyake ni nyama na
ashu (kwa kuboronga neno ashara) ni shilingi kumi.
(d) Mahali. Kila eneo huibua misimu yake. Gari la uchukuzi kwa umma nchini Kenya ni
matatu na Tanzania ni daladala.
(e) Wakati au kipindi. Misimu hubadilika kulingana na wakati au kipindi. Kwa mfano,
wakati wa uchaguzi wa 2002 nchini Kenya, kulizuka neno unbwogable lililomaanisha
wasioshindwa/wasiotishika na likatoweka katika muktadha wa baada ya hapo.

Lakabu
Lakabu ni jina la msimbo au jina la kupanga ambalo mtu hujibandika ama hubandikwa
kutokana na sifa zake za kimaumbile, kitabaka, kitabia au kimatendo. Lakabu aghalabu
huwa neno moja au fungu la maneno lililo na maana fiche au ya kisitiari. Sifa zinazodokezwa
katika lakabu zinaweza kuwa za kusifu, kudhalilisha au kukosoa.

Sifa za lakabu
(a) Lakabu si jina halisi la mtu. Ni jina tu la kupangwa.
(b) Lakabu aghalabu huwa neno au fungu la maneno lililo na maana iliyofumbwa.
(c) Lakabu huoana na sifa za mhusika. Inaweza kusifu, kukej eli au kufanyia tashtiti tabia
hasi ya mhusika. Lakabu Baba wa Taifa, moja kwa moja inaashiria sifa nzuri za mhusika
na kumsifu. Kwa upande mwingine, lakabu kama Kagumu inaashiria tabia ya uchoyo.
(d) Lakabu hupatikana katika tanzu na vipera vingine vya fasihi simulizi kama vile sifo,
malumbano ya utani na majigambo (vivugo), ambapo wahusika hujipa majina ya
kupanga ya kujitapa.
(e) Lakabu huundwa kwa lugha ya picha au taswira na sitiari, kwa mfano, lakabu Nyayo
ya Rais mstaafu Moi inatumia sitiari. Inamfananisha na nyayo za mtu, hivyo kutupa
taswira ya mtu anayefuata falsafa ya mwingine.
(£) Ingawa lakabu si jina halisi la mtu, huweza kudumu na kufanya jina halisi la mtu
kusahaulika.
Dhima ya lakabu
(a) Hutumiwa kusifia matendo chanya ya mhusika.
(b) Hukashifu au hukejeli matendo mabaya ya mhusika.
(c) Ni kitambulisho cha mhusika. Husawiri tabia au hali ya mtu fulani kwa maneno
machache.
(d) Hutumiwa kama ishara ya heshima. Katika jamii ambamo kumtaja mkazamwana kwa
jina lake halisi ni mwiko, baba mkwe huibua lakabu ya kumrejelea mkazamwanawe.
(e) Hutumiwa na baadhi ya wahusika kuficha utambulisho wao. Baadhi ya waandishi
hujibandika majina ya uandishi ili kuficha majina yao halisi.
(£) Hutumiwa na wahusika kujigamba na kujinaki. Katika majigambo, anayejigamba
hujipa lakabu ili kujinaki na kuonyesha ubingwa wake.
(g) Hutumiwa kuhifadhi siri. Wakati mwingine watu humpa mtu fulani lakabu ili
wanapomrejelea isijulikane ni nani.
(h) Hukuza uhusiano bora hasa miongoni mwa watani. Katika kufanyiana utani watu
huweza kubandikana majina.
(i) Hutumiwa kuondoa urasmi katika mahusiano ya kijamii.

Eleza tofauti kati ya misimu na lakabu.


Andika mifano mitano ya misimu na mitano ya lakabu.
Toa mifano mitano ya lakabu katika jamii yako kisha ueleze asili yake.
Au
Toa mifano mitano ya misimu inayopatikana katika mazingira na miktadha
ifuatayo:
(a) siasa (b) pesa (c) shuleni
(d) vijana (e) vyakula.

Vitanza ndimi
Vitanza ndimi ni kauli au sentensi zenye maneno ambayo yana mfuatano wa sauti
zinazotatanisha kimatamshi. Vitanza ndimi huundwa kwa maneno yenye sauti
zinazokaribiana sana kimatamshi. Kimsingi, katika jamii nyingi za Kiafrika, watu hufurahia
kucheza na maneno kama njia ya kujiburudisha. Watoto, kwa mfano, wana mazoea ya
kucheza na maneno na sauti katika michezo na nyimbo zao.

Sifa za vitanza ndimi


(a) Kimsingi, vitanza ndimi ni mchezo wa maneno na sauti.
(b) Huundwa kwa maneno ambayo yana sauti zinazokaribiana kimatamshi. Maneno haya
huweza kuwa na maana nyingi au yenye kukaribiana kimaana.
YA

(c) Ukuruba wa maneno kisauti na kimaana huyafanya matamshi ya maneno kuutatiza


ulimi.
Mifano ya vitanza ndimi:
(i) Wataita wataita Wataita wa Taita.
(ii) Waite wale wana wa Liwali wale wali wa Liwali.
(iii) Cha mkufuu mwanafuu ha, akila hu, cha mwanafuu mkufuu hu, akila ha. (methali)

Dhima ya vitanza ndimi

(a) Vitanza ndimi hukuza matamshi bora. Mtu anapotamka kwa haraka na kwa usahihi,
hutia makali stadi zake za kimatamshi. Kupitia hali hii, uzoefu wa kutamka vyema
hujengwa.

(b) Hukuza uwezo wa kufikiri kwa haraka. Baadhi ya vitanza ndimi hutatanisha kwa
sababu ya ukuruba wa maana. Mtu huhitajika kuwaza haraka ili kuteua neno sahihi
la kutamka katika muktadha wa maneno fulani.

(c) Kuburudisha. Kimsingi, vitanza ndimi vilinuiwa kuibua ucheshi na kuchangamsha


hadhira.

(d) Hukuza ubunifu. Anayebuni vitanza ndimi anahitajika kuwa na ujuzi mpana wa lugha
na ubunifu ili kuteua maneno yanayokaribiana kimatamshi na kimaana.

(e) Hukuza lugha. Vitanza ndimi vilivyobuniwa katika vipindi mbalimbali huhifadhiwa
na kupitishwa kwa vizazi vijavyo kama mifano katika kipera cha vitanza ndimi.

(£) Huhifadhi utamaduni na kuurithisha. Maarifa ya kipera cha vitanza ndimi


yasingehifadhiwa na kurithishwa kama vipera vingine vya fasihi simulizi, tusingevisoma
leo.
(8) Ni kitambulisho cha jamii. Vitanza ndimi huakisi mazoea ya jamii husika. Kila jamii
ina vitanza ndimi vyake mahususi.
(h) Hujenga uhusiano bora wa kirafiki. Ucheshi unaoibuliwa na vitanza ndimi hujenga
uhusiano bora miongoni mwa washiriki.

Mafumbo na chemshabongo
Mafumbo ni kauli zenye maana iliyojificha. Mafumbo hutumia lugha fiche au ya kiistiari
pamoja na tamathali nyingine za usemi. Humtaka anayeambiwa kudadisi mazingira yake
na kufikiria ili kupata maana. Mafumbo huchemsha bongo za wale wanaoshiriki katika
kuyafumbua. Ingawa vitendawili ni aina ya fumbo, tunadai kwamba mafumbo kwa kawaida
ni semi ndefu kuliko vitendawili. Mafumbo hutumika sana sana katika mazungumzo na
huundwa kutegemea mazingira. Kwa mfano, watu wanapozungumza wanaweza kumtaja
mtu fulani kwa ubaya wake kisha mtu mwenyewe akija, mmoja wao akawatahadharisha
wengine kwa kusema 'Chungeni msikanyage nyoka'. Watachunguza mazingira yao au
wafikirie ili kubaini maana ya fumbo la nyoka.
Kuna mafumbo ambayo huitwa chemshabongo. Chemshabongo ni maswali ambayo
humtaka mtu kutumia akili na ujuzi kuyajibu. Maswali mengi ya aina hii ni ya kimapokeo,
mengine hubuniwa na msemaji ili kukidhi mahitaji ya hadhira mahususi. Baadhi ya
chemshabongo, kwa hakika, ni hesabu tu. Nyingine hutolewa kwa njia ya mraba ambao
unahitaji kujazwa kwa maneno mwafaka. Tazama mfano ufuatao:
|
Nina kilo moja ya mchanga na kilo moja ya pamba. Kipi kizito zaidi, mchanga au
pamba?
Jibu: Vyote vina uzito sawa kwa vile uzito wavyo ni sawa (kilo moja).

Sifa za mafumbo
Mafumbo huwa na sifa zifuatazo:
(a) Ni semi ambazo hufumba jambo.
(b) Huhitaji mtu kuwaza ili aweze kubaini fumbo lenyewe.

(c) Shughuli, maumbile au vitu vilivyo katika mazingira ya jamii kama vile mifugo, njia
za usafiri na nyenzo za biashara vinaweza kufumbiwa.
(d) Baadhi ya mafumbo hufananisha kitu kilichotajwa katika fumbo na mazingira halisi.
(e) Baadhi ya mafumbo huwa marefu na mengine huwa mafupi. Tazama mfano ufuatao:

Watu watatu walikuwa wakivuka mto. Mmoja alivuka pasi


kukanyaga maji wala kuyaona. Wa pili aliyaona maji akayavuka
bila kuyakanyaga. Wa tatu aliyaona akayakanyaga huku
akiyavuka. Ni kina nani hawa?

Jibu:

(i) Wa kwanza - mimba/mtoto aliyekuwa tumboni mwa


mamake.

(ii) Wa pili — mtoto aliyebebwa mgongoni na mamake.


(iii) Wa tatu - mama mwenyewe.
(£) Mafumbo huhitaji mantiki ili kuyatambua. Tazama mfano ufuatao:

Nina vitu vitatu: kuku, nguchiro na mtama. Nimefika mtoni


nami nataka nivivushe vitu hivi. Mashua yangu ina uwezo wa
kunivusha mimi na kitu kimoja tu. Vyote lazima vivushwe. Siwezi
kumwacha nguchiro na kuku kwa sababu nguchiro atamla kuku.
Naye kuku akiachwa pamoja na mtama ataula. Nitafanyaje?

Jibu:
(i) Utavusha kuku kwanza.
(ii) Rudi, uchukue mtama uuvushe.
(iii) Chukua kuku, urudi naye ng'ambo ya kwanza na kumwacha
hapo.
(iv) Mvushe nguchiro.
(v) Mrudie kuku umvushe.

Fumbo hili, pamoja na kumhitaji mtu kutumia uhalisi wa mambo, anahitajika kutumia
mantiki ili kulifumbua. Mfumbuaji anahitaji kujua:
(i) Nguchiro hula kuku - hawezi kuwaacha pamoja.
(ii) Kuku hula mtama - hawezi kuacha kuku na mtama pamoja.

Dhima ya mafumbo
(a) Hukuza uwezo na wepesi wa kufikiri. Ili kufumbua fumbo ni lazima mtu afikiri kwa
makini na wakati mwingine kwa upesi.
(b) Hustawisha ubunifu. Fumbo hufumbuliwa kwa kuoanisha yaliyomo katika fumbo, tajiriba
na mazingira. Hivyo, mtu hutumia kiwango fulani cha ubunifu ili kupata maana. Aidha,
shughuli ya kufumba mafumbo huwahitaji watu kuwa wabunifu.
(c) Hukuza maarifa ya kukabiliana na changamoto na kutumia mantiki kusuluhisha mambo.
Tazama mfano:
za Li zikate mah

Mfalme ana watoto wawili wa kiume na anataka mmoja wao amrithi.


Kwa sababu hataki kupendelea yeyote, anawapa changamoto ya kukimbia
hadi mji wa mbali kwa farasi wao. Yule ambaye farasi wake atafika
mwisho ndiye atakayemrithi. Ndugu hawa wanazembea jangwani
kwa siku kadha kwa sababu kila mmoja anataka kufika wa mwisho.
Hatimaye wanakutana na mzee mwenye busara ambaye anawapa wasia.
Wanapanda farasi upesi na kutoka mbio ili wafike kwenye mji wa mbali
walioagizwa na baba yao. Je, Mzee mwenye busara aliwaambia nini?
Jibu: Wabadilishane farasi.
Nahau
Nahau ni fungu la maneno ya kawaida lenye maana ambayo haitokani moja kwa moja na
maana za maneno yaliyoziunda. Nahau Piga kalamu si kuchapa kalamu bali ni “kufuta mtu
kazi'. Mifano mingine ya nahau ni:
Piga maji — lewa
Kujitia hamnazo —- kujifanya hujui
Kukata kamba — kufa
Kukunja jamvi — kumaliza shughuli
Kwenda nguu —- kukata tamaa
Piga vijembe — kusema kwa mafumbo
Kumwaga unga — kuachishwa kazi
Ndege mbaya — bahati mbaya
Kupata jiko — kuoa
Shingo upande — bila kutaka

Sifa za nahau
(a) Nahau huundwa kwa lugha ya mkato iliyo na ujumbe mzito wa mafumbo. Kwa mfano
Kidudu mtu ina maana ya mfitini.
(b) Nahau mbili au zaidi zinaweza kuwa na maana moja. Ifuatayo ni mifano:
Kupata jiko
Kuoa
Kuasi ukapera
Jamvi la wageni
Bao la mkahawani Sa
Kunja jamvi
j Maliza shughuli
Funga virago
(c) Nahau moja inaweza kuwa na maana zaidi ya moja. Kwa mfano:
Kushika mguu —
kuomba radhi

kutoa shukrani

kupiga mbio
Kufunga virago —
kumaliza shughuli

kuondoka
(d) Maneno katika nahau hupoteza sifa zake za kawaida na kuchukua maana nyingine
iliyo tofauti kabisa. Kula chumvi, kwa mfano, ni kuzeeka wala maana haihusiani na
maana ya maneno 'kula' au 'chumvi'.
(e) Nahau huundwa kwa maneno mawili au zaidi. Soma mifano ifuatayo:
Shingo upande — bila kupenda
Kufua dafu —- kufaulu
Bega kwa bega — pamoja
Mtoto wa kikopo — mhuni
Kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa — kudanganya, kumpa mtu sifa asizostahili.
(f) Nahau huweza kuundwa kwa mitindo mbalimbali au kwa maneno ya kategoria
mbalimbali kama vile:
(i) Kitenzi na nomino — piga chuku
—- andika meza
—- tafuna maneno
(ii) Kitenzi na kitenzi —- kufa kupona
—- kufumba na kufumbua
— pata shika
—- ruka akitoja
(iii) Kitenzi na kielezi — jikaza kisabuni
— tokea pwani
—- kufa kikondoo
(iv) Nomino na nomino — askari kanzu
— donda ndugu
—- domo kaya
(v) Nomino na kitenzi — mguu haumshiki
— damu kumkauka
— akili kumruka
(vi) Nomino navivumshi — —nyota njema
— bahari kubwa
— ndege mbaya

Dhima ya nahau
(a) Nahau hukuza lugha. Nahau huyapa maneno maana tofauti na maana ya kawaida.
Kwa njia hii, hupanua msamiati wa lugha.
(b) Nahau huipa lugha ladha. Badala ya kutumia maneno yaliyozoeleka kurejelea mambo
ya kawaida, nahau hutumika kukoleza ladha ya lugha. Badala ya mtu kusema fulani
amezeeka sana, anasema fulani amekula chumvi ya kutosha.
(c) Nahau pia hutumiwa kupunguza ukali wa jambo linalorejelewa. Badala ya kusema
fulani ana tabia ya uasherati tunasema ana jicho la nje.
(d) Nahau huweza kutumika pia kuhifadhi siri ili wanaotengwa wasielewe. Si watu wote
wanaoelewa maana ya nahau zote. Unaposema fulani amekuwa kidudu mtu huenda
mwingine asielewe kuwa unamaanisha amekuwa mfitini.
F- |
Misemo
Misemo ni semi ambazo zinabeba ukweli wa kijumla. Hutumiwa kuelezea mambo
mbalimbali yanayokubali ukweli huo. Misemo hutumiwa kutoa ujumbe kwa muhtasari.

Mifano zaidi ya misemo: |


(i) Binadamu ni udongo — kumaanisha binadamu aliumbwa kwa udongo na hufa na |
kurudi udongoni anapozikwa.
(ii) Mwili haujengwi kwa mbao — kumaanisha mtu lazima ale ili apate kujenga mwili au
kunenepa. Hauwezi ukajengwa kwa mbao.
(iii) Umaskini si kilema — kumaanisha kuwa mambo hubadilika. Ukizaliwa katika umaskini
si lazima uishi na ufe ukiwa maskini.
(iv) Lila na fila havitangamani — kumaanisha ubaya na wema hauendi pamoja. !
(v) Ndio kwanza mkoko ualike maua —- kumaanisha ndio mambo yamezidi kushika kasi.
(vi) Mgomba haupandwi changaraweni ukamea. — kumaanisha jambo jema halifanywi
mahali pabaya likapendeza.

Baadhi ya misemo hutumiwa kama methali. Kwa mfano, tunasema, “Umoja ni nguvu,
utengano ni udhaifu.”

1. Andika mifano miwili miwili ya mafumbo:


(i) ambayo ni chemshabongo.
(ii) ambayo hujitokeza katika mazungumzo.
Fafanua tofauti kati ya mafumbo na vitendawili.
Andika mifano mitano ya mafumbo kutoka jamii yako.
“Ufunzaji wa vitanza ndimi hauna nafasi katika mtaala.” Jadili.
Kwa kutoa mifano miwili, eleza sifa nne za nahau.
BIN
AU Huku ukitoa mifano mwafaka, tofautisha kati ya misemo na nahau.
u
Utanzu wa Ushairi Simulizi

Utangulizi
Ushairi simulizi ni utanzu unaojumuisha tungo zote zenye mapigo ya kimuziki. Mawazo,
hisia na hoja katika utanzu huu huwasilishwa kwa njia ya mdomo kwa kutumia lugha ya
mkato yenye mpangilio maalumu wa maneno katika mishororo. Ushairi simulizi huimbwa,
hughaniwa au kukaririwa. Ni muhimu kutaja hapa kuwa ushairi simulizi hutofautiana
na mashairi ambayo yameandikwa kwa lengo la kuwasilishwa mbele ya hadhira katika
mashindano ya tamasha za muziki au yanayowasilishwa katika hafla maalumu.

Sifa za ushairi simulizi


(a) Ushairi simulizi huwasilishwa kwa njia ya mdomo mbele ya hadhira kwa kukaririwa,
kughaniwa au kuimbwa. Nyimbo, kwa mfano, huimbiwa watu. Hata hivyo, baadhi
ya mashairi simulizi huimbwa na watu bila kuhusisha hadhira. Nyimbo za kazi mara
nyingi hazina hadhira.
(b) Hubuniwa papo hapo na kuwasilishwa kwa hadhira au tungo za awali huwasilishwa
kutoka kwa kumbukumbu za mwasilishaji.
(c) Tungo za mashairi simulizi hutolewa zikiambatana na ala za muziki. Uimbaji wa
nyimbo huambatana na ala kama vile njuga na marimba. Aidha, anayejigamba huweza
kutumia ala kama vile mkuki anapojigamba.
(d) Ushairi simulizi ni sehemu ya utamaduni wa jamii na hupitishwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine. Nyimbo za jandoni (nyiso) na tendi, kwa mfano, hupitishwa kutoka
kizazi kimoja hadi kingine.
Ushairi simulizi hutumia lugha yenye mvuto mkubwa; yenye mapigo yaliyopangwa
kwa muwala na urari:
Utungo wa ushairi simulizi huweza kuwasilishwa na mtu mmoja kama ilivyo katika
majigambo au kundi la watu kama ilivyo katika nyimbo nyingi na ngonjera.
Ushairi simulizi, kama tanzu nyingine za fasihi simulizi, hubadilika kulingana na
anayeuwasilisha, hadhira na wakati. Wimbo mmoja unaweza kuimbwa kwa mahadhi
mbalimbali kulingana na mwimbaji. Mwasilishaji anaweza kubadilisha wimbo au shairi
wakati wa kuimba, kukariri au kughani kutegemea hadhira yake.
(h) Hadhira huweza kushiriki katika uwasilishaji wa mashairi simulizi. Mwimbaji, kwa
mfano, anaweza kuishirikisha hadhira yake katika uimbaji kwa kupiga makofi.
(i) Uwasilishaji wa mashairi simulizi, kwa kawaida, huandamana na uigizaji. Mwimbaji,
kwa mfano, huambatanisha maneno yake na vitendo kama vile ishara za uso, ishara
za mkono, miondoko mbalimbali na upigaji makofi.
(j) Ushairi simulizi hufungamana na shughuli au muktadha maalumu. Mathalani, nyimbo
hufungamana na shughuli tofauti tofauti kama vile:
(i) Hodiya — nyimbo za kazi.
(ii) Kimai>— nyimbo za uvuvi au shughuli za majini.
(iii) Mbolezi — nyimbo za kuomboleza au za matanga.
(iv) Wawe - nyimbo za kilimo.
(k) Ushairi simulizi una miundo mbalimbali. Unaweza kuwa na beti zilizo na kibwagizo.
Kila ubeti unaweza kuwa na idadi tofauti tofauti za mishororo kama vile 2, 3, 4, 5, 6,
7 na zaidi.
(1) Ushairi simulizi unaweza kuwa na urari wa vina na mizani au ukakosa kuwa nao. Kilicho
muhimu zaidi ni mapigo ya kimuziki yanayofanya utungo huo uweze kuimbika.
(m) Ushairi simulizi, kama tanzu nyingine za fasihi simulizi hutumia lugha ya kitamathali.
Kunaweza kuwa na misemo, nahau, methali, ishara na taswira, jazanda na istiara.

Uainishaji wa ushairi simulizi


Mashairi simulizi yanaweza kuainishwa kwa kutumia vigezo mbalimbali kama vile:

1. Maudhui
Kwa kuzingatia maudhui, tunaweza kupata mashairi yenye maudhui ya:
(a) mapenzi. Hupitisha jumbe za mapenzi.
(b) kutuliza. Kuna nyimbo za bembea au bembelezi ambazo hutuliza watoto.
(c) kuomboleza. Mbolezi huimbwa wakati wa msiba.
(d) kusifu. Sifo huimbwa kusifu mashujaa au waliofaidi umma na kustahiki kutambuliwa.
(e) siasa. Nyimbo za siasa huwasilisha jumbe za kisiasa.

2. Muktadha au mahali pa uwasilishaji


Kwa kufuata kigezo cha muktadha, kuna mashairi au nyimbo kama vile:.
(a) nyiso (Nyimbo za jandoni).
(b) mbolezi (Nyimbo za matanga zinazoimbwa kwenye mazishi au maombolezi).
nyimbo za harusi.
nyimbo za matambikoni ambazo hutolewa wakati wa kutoa kafara au sadaka kwa
mizimu labda baada ya janga.
nyimbo za kazi.

Mtindo wa uwasilishaji
Mashairi simulizi huchukua mitindo ya uwasilishaji ifuatayo:
(a) maghani. (Hutolewa kwa kauli bila kuimbwa.)
(b) nyimbo. (Huwasilishwa kwa mahadhi ya kupanda na kushuka.)
shairi. (Utungo unaokaririwa.)
tendi au rara. (Husimuliwa kwa mapigo ya kishairi.)
ngonjera. (Huwasilishwa kwa kujibizana.)

Mwasilishaji
Majigambo. (Huwasilishwa na anayejigamba.)
Kwaya. (Uimbaji wa watu wengi pamoja.)

Umuhimu wa ushairi simulizi


Ushairi simulizi, kama kipengele cha fasihi simulizi, una umuhimu wa kijumla, licha ya kuwa
kuna vitanzu mbalimbali vinavyotekeleza majukumu tofauti. Majukumu ya ushairi simulizi j
hutofautiana kutoka jamii hadi jamii. Hata hivyo, kuna majukumu ya kijumla kama vile:
(a) Ushairi simulizi hutumiwa kupitisha maarifa au mafunzo ya jamii fulani. Nyimbo za
jandoni, za harusi na dini hutumiwa kupitisha mafunzo maalumu.
(b) Ni nyenzo ya kuhifadhi na kupitisha utamaduni na historia ya jamii kutoka kizazi
kimoja hadi kingine. Kwa mfano, tendi zinazosifu mashujaa huendeleza historia ya
jamii hiyo kwa kuonyesha matukio kama vile vita. Nyimbo za jandoni (nyiso) husawiri
utamaduni wa jamii kuhusu jando na kuuhifadhi.
(c) Hukashifu tabia hasi kwa nia ya kuhimiza urekebishaji wa tabia hizo. Nyiso, kwa
mfano, hukashifu woga, hivyo vijana waoga huhimizwa kujirekebisha. Maghani na
nyimbo za kisiasa hukashifu tawala dhalimu.
(ad) Ni nyenzo kuu ya kukuza umoja na uzalendo miongoni mwa wanajamii. Kupitia kwa
nyimbo zinazosifu mashujaa wa vita, huhimiza vijana kuzionea fahari jamii zao na
kujitoa mhanga kuzitumikia. Aidha, wanajamii wanapojumuika pamoja kuimba au
kughani katika hafla fulani, hujihisi kuwa kitu kimoja, hivyo uzalendo hujengeka.
Ni nyenzo ya kutakasa hisia. Kupitia kwa mashairi au nyimbo, watu hutoa hisia za
moyoni na kutakaza nyoyo zao. Mfano mwafaka ni nyimbo na mashairi ya mapenzi
ambayo kwayo mtu humtolea mpenzi wake hisia. Rara nafsi pia hutumiwa kutekeleza
jukumu hili.
(£f) Huelimisha, hukosoa na kurekebisha jamii. Nyimbo hutoa maadili ya kuonya na
kuelimisha wanajamii. Nyimbo au mashairi ya sifo, tendi, hata mbolezi huonyesha
matendo mazuri ya anayeimbwa na kukashifu wanaoenda kinyume na matakwa ya
jamii.

(8) Husawiri mfumo wa jamii fulani kisiasa, kiuchumi na kijamii. Baadhi ya nyimbo
huonyesha shughuli za kiuchumi za jamii kama vile ufugaji. Hodiya (nyimbo za kazi)
huonyesha shughuli mbalimbali kama vile uwindaji, kilimo, uvuvi. Majigambo pia
husawiri mifumo ya jamii kisiasa na kijamii.
(h) Huonyesha falsafa na imani za jamii husika kuhusu masuala fulani. Mbolezi huonyesha
imani za jamii kuhusiana na kifo. Majigambo husawiri falsafa ya jamii kuhusu ushujaa.
(i) Ni nyenzo kuu ya kuhamasisha wanajamii. Nyimbo za kisiasa na kizalendo zimetumiwa
na tawala kama nyenzo ya kueneza propaganda za kisiasa.
G) Hukuza ubunifu. Anayekariri, kuimba au kughani mashairi huhitajika kubuni mbinu
zifaazo za uwasilishaji. Kwa kufanya hivi, uwezo wake wa kubuni hukuzwa.
(k) Hukuza usanii wa lugha. Wanaotunga na kuimba mashairi hujizoesha kutumia lugha
kwa ufundi mkubwa ili kutosheleza urari wa mizani na vina.
(1) Husaidia wanajamii kukabiliana na hali ngumu na kuwahimiza wasikate tamaa. Kwa
mfano, mbolezi hufariji na kusawiri kifo kama faradhi. Kwamba humfika mja yeyote,
hivyo hisia za mwemeo hupungua. Aidha, nyimbo huhimiza waliokwenda vitani au
wanaofanya kazi wasikate tamaa.
(m) Ushairi simulizi hustarehesha na kufurahisha wanajamii. Tungo za ushairi simulizi
huvutia hisia, huburudisha na kusisimua mwili na akili.

—..—
1. (a) Andika miktadha mitano katika jamii yako ambamo nyimbo huimbwa
au mashairi hukaririwa.
(b) Taja aina za mashairi au nyimbo ambazo huimbwa katika miktadha
uliyoitaja.
2. Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali.
Umeanguka mwamba
Jabali tuloegemea
Lilotupa kimbilio
Mahasidi kutishia
Mti mkuu umegwa
Wana wa ndege wawapi?
Bila shaka hangaiko
'Metukumba makinda
Angalikuwa pamwe nasi
Maulana Mungu wetu
Swali hilo tungemuuliza
Mbona kaacha mauko
Ngome yetu kuvamia?
Ela mwenyewe Mwenza
Ajua hatima yetu
Lilobaki kumwamini
Riziki kutuangushia

(a) Andika muktadha ambamo utungo huu unaweza kutolewa.


(b) Huu ni utungo wa aina gani kimaudhui? Thibitisha.
(c) Taja sifa za ushairi simulizi katika utungo huu.
(d) Andika mbinu za kifasihi zilizotumiwa katika utungo huu.

- Vipera vya ushairi simulizi


Ushairi simulizi una vipera vitatu: nyimbo, maghani, ngonjera.

Nyimbo
Nyimbo ni tungo za kishairi zenye mahadhi ya kupanda na kushuka kwa sauti, muwala na
mapigo ya kimuziki na huwasilishwa kwa kuimbwa. Nyimbo hutambuliwa kwa sifa tatu:
(i) huwepo kwa hadhira inayotumbuizwa
(ii) muziki unaoimbwa kwa sauti
(iii) matumizi ya ala.

Sifa za nyimbo
(a) Sifa bainifu ya nyimbo ni kwamba hutolewa kwa mahadhi ya kupanda na kushuka
kwa sauti.
(b) Nyimbo hutumia lugha ya mkato yenye mpangilio maalumu wa silabi, mishororo na
beti zenye mapigo ya kimuziki.
(c) Nyimbo hutumia lugha nzito yenye kuibua taswira na hisia nzito kama za mapenzi,
huzuni na furaha.

(d) Nyimbo zinapoimbwa, mara nyingi huandamana na ala za muziki kama vile ngoma,
baragumu, msewe na zumari.
(e) Katika jamii za Kiafrika, nyimbo hufungamana na muktadha fulani. Kuna nyimbo
za kazi, harusi, jando na unyago, kuzaliwa kwa mtoto, kumpa mtoto jina, ibada na
matambiko.

(£) Baadhi ya vifungu katika nyimbo hurudiwarudiwa. Vifungu hivi huitwa vibwagizo,
viitikio au mikarara ya nyimbo.

(8) Nyimbo nyingi huandamana na uchezeshaji wa viungo kama vile mabega kupiga
makofi na mapigo ya miguu. j
(h) Kimsingi, nyimbo ziliimbwa na makundi ya watu kwa hadhira hai. Hata hivyo, kuna
nyimbo zinazoimbwa na mtu mmoja kwa hadhira yake au hata bila hadhira.

Umuhimu wa nyimbo
(a) Nyimbo hutambulisha jamii kwa kusawiri shughuli na maisha ya jamii iliyozibuni.
Mathalan, nyimbo katika jamii ya wakulima zitasheheni msamiati unaohusu shughuli
za kilimo kama vile kuvuna, kupanda na kupalilia.
(b) Nyimbo humwezesha binadamu kutakasa hisia zake. Kupitia kwa nyimbo, binadamu
hutoa hisia za moyoni kama vile kujutia kosa ulilofanya, mapenzi ama huzuni.
Mbolezi humsaidia aliyeathiriwa kutoa hisia za huzuni. Nyimbo za mapenzi, kama
vile chombezi, humwezesha mpenzi kumfichulia mwenzake hisia zake za moyoni.
(c) Ni mbinu mojawapo ya kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii. Rekodi za
. matukio muhimu katika jamii huweza kuhifadhiwa kwa nyimbo na kupitishwa kwa
vizazi.

(d) Nyimbo hutumbuiza. Hutumiwa kama burudani kufurahisha, kustarehesha na


kusisimua.

(e) Hupitisha amali na mambo ambayo jamii inayathamini. Amali hizo hurekodiwa katika
nyimbo mbalimbali kama vile za kazi na kurithishwa vizazi vya jamii hiyo. Mawaidha
na thamani za jamii hukaririwa katika nyimbo kama nyenzo za kuzirithisha.
(f) Nyimbo hutumiwa kuhamasisha watu na kuchochea hisia za kuchamgamkia jambo
fulani. Nyimbo za kisiasa, kwa mfano, huweza kuchochea hisia za kuungana pamoja
kutetea haki au kuunga mkono jambo fulani.
(8) Nyimbo huakisi ukwasi wa tamaduni za jamii. Umbuji (ufasaha wa kujieleza) na
ujumi (mvuto au uzuri wa kazi ya sanaa) wa jamii hujitokeza katika nyimbo. Uteuzi
wa maneno, ishara na ujumbe katika nyimbo huonyesha ukwasi wa jamii hiyo kifani.
(h) Hukuza ubunifu miongoni mwa wanajamii. Uimbaji ni kipawa na nyimbo hupalilia
kipawa hiki.
Soma ubeti ufuatao kisha ujibu maswali:
Siku hiyo ya nuru
Tulokata pingu
Kuyabwaga mazigo
Silisili tukakata
Beberu tukatimua
Istiimari tukaua
Uhuru tukarejesha
Hadhi yetu kufufua
Bendera mlingotini ikapepea,
juu ya kilele cha mlima
Ishara ya kujitawala.
1. Nyimbo hufungamana na muktadha. Andika muktadha ambapo wimbo huu
unaweza kuimbwa.
2. Nyimbo huakisi ukwasi wa tamaduni za jamii. Jadili kauli hii kwa kurejelea
ubeti huu wa wimbo.
Taja sifa nyingine tano za nyimbo zinazojitokeza katika wimbo huu.

Aina za nyimbo
Kila jamii ina nyimbo zake ambazo hutofautiana na nyimbo za jamii nyingine. Baadhi
ya nyimbo ambazo hupatikana katika jamii za Kiafrika ni pamoja na:

Bembea/Bembelezi/Pembejezi
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa ili kuwabembeleza watoto walale au watulie wanapolia.

Sifa za bembea
(a) Bembea huimbwa taratibu kwa sauti na mahadhi ya chini.
(b) Huimbwa na wazazi au walezi wa watoto kuwaliwaza na kuwabembeleza watoto walale
au wanyamaze wakati wanapolia.
(c) Huwa fupi.
(d) Bembea hutofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine kulingana na thamani za jamii
hiyo.
(e) Huimbwa kwa kurudiarudia maneno au kibwagizo. Wakati mwingine hata wimbo
mzima huimbwa kwa kurudiwarudiwa.
(£) Hutumia lugha shawishi na wakati mwingine hutolewa ahadi za kununuliwa watoto
zawadi.

Majukumu ya bembea
Majukumu yanayotekelezwa na nyimbo zabembea nipamojana:

(a) Kutumbuiza na kuongoa watoto. Bembea humpumbaza na kumfanya mtoto alale au


anyamaze anapolia.

(b) Hutumiwa kama sifo kumsifu mtoto ambaye ni mtulivu. Husifu pia somo ya mtoto
huyo au wazazi wake.
(c) Husawiri mfumo wa kiuchumi wa jamii husika. Ikiwa baba ni msasi, mtoto atatajiwa
kuwa baba ni msasi jasiri au baba yuko karibu kutoka usasini.

(d) Husawiri mahusiano katika jamii. Kupitia kwa bembea, mlezi huweza kuibua migogoro
iliyomo kati yake na wazazi wake au wazazi wa watoto, hivyo kuonyesha uhusiano
kati ya waajiri na waajiriwa.

(e) Hutakasa hisia ambazo mwimbaji huweza kuwa nazo.


(f) Humwelimisha mtoto, hata katika umri huu mchanga, kuhusu mambo na shughuli
mbalimbali katika jamii na umuhimu wake au thamani yake kwa jamii. Soma mfano
ufuatao wa bembelezi iliyotafsiriwa kutoka lugha ya Kikamba.

Lulu, mwanangu tulia,


Wiwi mtoto lala, mvua imekuja
Si uongo hata na miti huichangamkia mvua,
hakuna haja ya kuelezwa,
Lulu mwana tulia,
Wiwi mtoto lala, mvua imekuja.

Wimbo huu unaonyesha thamani ya mvua kwa jamii hii. Kila mtu duniani
huichangamkia mvua kwa sababu ndiyo chanzo cha kila kitu kilichoumbwa na Mungu.
(8) Husawiri falsafa au mtazamo wa jamii kuhusu jinsia na matarajio ya jamii kwa jinsia
fulani. Katika bembea, mlezi anaweza kutaja kuwa machozi ni ya kike iwapo anatuliza
mtoto wa kiume. Majukumu yake (mtoto wa kiume) kwa jamii pia huweza kutajwa.
Mlezi huweza kumtajia mtoto wa kike kwamba msichana anatarajiwa kuwa mlezi
mwema wala si kilizi.

(h) Huwaonya watoto dhidi ya tabia hasi. Watoto huonywa dhidi ya kulia ovyo kwa sababu
kulia hukumbusha mtu mambo mabaya.
Mfano wa bembea

Ewe malaika wangu


Uloshuka toka mbinguni
Mbingu kapasua kwa heri
Siku nipokukopoa
Ulinitia furaha iliyopasua kifua
Tabasamu kipajini pako
Ilinitia tumaini, ikanisahaulisha zingizi
Ikayeyusha madhila, ya utasa wa miaka kumi
Ikapeperusha mbali cheko la ukewenza
Sasa napolia, wanitonesha jeraha
Waniregesha Misri, kwa vitimbi vya Firauni
Kwa vitisho vya muhebi
Talaka kuahidiwa, hadi mbingu
Lipofungua milango ya heri.
Silie mwana silie, walimwengu watakusuta
“Tangu hapo tanabahi
Vidume humu mwenu
Kulia havikuumbiwa
Machozi na kekevu ni za kike fahamu
Jogoo halii, daima huwika
Nikikuona kigugumika hivi wanitia hangaiko
Tumaini kuzima
Udhaifu kiandama, moyo kitia hamaniko
Atanipigania nani
Watesi king'ang'ania changu kujitwalia?

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea wimbo uliosoma.


(a) (i) Je, mtoto anayeongolewa wimbo huu ni wa kike au kiume?
(ii) Toa sababu tatu kuthibitisha jibu lako.
(b) (i) Mwimbaji ni nani au ana uhusiano gani na anayeimbiwa?
(ii) Thibitisha kwa kutoa mfano kutoka kwa wimbo wenyewe.
Andika sifa tatu za jamii ya mwimbaji kama zinavyojitokeza katika wimbo huu.
- Andika mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu.
Andika majukumu sita ya wimbo wa aina hii katika jamii.
Mbolezi
Mbolezi ni shairi au wimbo wa kuomboleza. Huimbwa wakati wa maafa au katika hafla ya
kuadhimisha makumbusho ya mtu. Nyimbo zinazoimbwa na Wakristo wakati wa Pasaka
kukumbuka mateso ya Yesu Kristo ni mfano wa mbolezi za kidini. Mbolezi pia huimbwa
baada ya kushindwa, kwa mfano, katika vita.

Sifa za mbolezi
(a) Mbolezi hutofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine kutegemea imani ya jamii
kuhusu kifo pamoja na hadhi ya aliyekufa.
(b) Huimbwa kwa nia ya kufariji waliofiwa.
(c) Husifu aliyekufa. Kwa kawaida, mbolezi hutoa sifa chanya au nzuri za aliyekufa. Watu
mashuhuri katika jamii huweza kutungiwa mbolezi zao mahususi zinazowasifu na
kutaja michango yao kwa jamii.
(d) Hufungamana na muktadha maalumu. Mbolezi huimbwa tu wakati wa matanga au
wakati wa kuomboleza jambo fulani. j
(e) Huimbwa kwa toni ya huzuni na pengine uchungu hivyo kuibua hisia za ndani za
mwombolezaji.
(£) Huimbwa kwa mwendo wa utaratibu.

Majukumu ya mbolezi
(a) Mbolezi husawiri msimamo wa jamii kuhusu kifo. Wapo wanaoamini kuwa kifo
husababishwa na maovu au pepo fulani na ambao hukashifu kifo. Watu wengine
hutambua kifo kama mlango wa kuingia katika uzima wa milele (kidini).
(b) Nikumbukumbu na sifo kwa aliyekufa. Husawiri tabia za aliyekufa kwa nia ya kumsifu
na kumkumbuka.
(c) Hufariji waliofiwa na kuwasaidia kukabiliana na uchungu au uzito wa kumpoteza
mpendwa wao.
(d) Ni njia ya kutakasa moyo na hisia za aliyefiwa. Aliyefiwa huweza kutumia mbolezi
kutoa hisia zake za huzuni. Kwa njia hii, anaweza kupunguza uzito wa kumpoteza
mwenzake.
Mfano wa mbolezi
Wa

“Kama kesho itapambauka


Jua la kinjano kuchomoza
Kuangazia siku mpya
Siku iso tumaini
Siku bila mimi mama mtu
Kumbuka ewe kipenzi
Usiache chozi kufurika
Kuyeyusha makini yako inuka, mwanangu inuka
Silie daima, yote yatatengenea.”

Mpenzi mama ulolala usingizi usio na mzindushi


Nalikumbuka vyema hili ni beti uloniandikia
Kitandani ukiwa, ukiuguza donda
Donda walokusababishia walimwengu mahasidi
Ela nataka ujue, kamwe yote si shwari kama uliponambia
Hayawezi kuwa shwari kwa mlezi kikembe
Hayawezi tengenea kwa yatima alozungukwa
Na waja wenye tamaa kila kitu kurithi
Hayawezi kuwa shwari kumtazama mwenzio,
ulotwambia tumwite baba na kumstahi,
ati ni amri ya Muumba.

Akitoka na muhebi, pumbao apate yeye


Wafurahia ulochuma wewe.
Najitahidi mpenzi mama
Ukakamavu kujipa
Machozi kuyafuta
Ela hino kumbuka
Kuondoka kwako huko
hatukukutarajia, japo hukuisha kunikumbusha
Ziraili liingia ja mwewe
Na kukwiba mithili ya kifaranga
Mama yake akitazama.

Jibu maswali kwa kurejelea wimbo uliousoma.


1. (a) Andika sifa za mbolezi zinazojitokeza katika utungo huu.
(b) Andika mbinu za kifasihi zilizotumiwa na mwimbaji.
Fafanua masuala ya kijamii ambayo yameibuliwa katika wimbo huu.
(a) Tunga mbolezi ya beti tatu.
(b) Andika majukumu matano ya mbolezi katika jamii yako.
Nyiso
Nyiso ni nyimbo ambazo huimbwa jandoni (kwa wavulana) na unyagoni (kwa wasichana).
Kila jamii hata hivyo, ina desturi zake ambazo huzingatiwa kama kigezo cha kuvusha vijana
kutoka utotoni na kuingia utu uzima. Tohara ni moja ya vigezo hivyo. Nyiso hupatikana
katika jamii ambazo huthamini tohara.
Katika baadhi ya jamii, nyiso huimbwa usiku wa kuamkia siku ya kupasha tohara. Aidha,
maudhui katika nyiso hutofautiana kutoka jamii hadi nyingine. Maudhui yanaweza kuwa
ya kuonya dhidi ya kutoa siri, kuwaandaa kwa uchungu watakaohisi au kukejeli waoga.

Majukumu ya nyiso

(a) Nyiso hutumiwa kuwaandaa kihisia wanaotahiriwa kwa kuwapa ari ya kupitia kijembe
cha ngariba.

(b) Huwajuza wanaotahiriwa kuhusu majukumu mapya na matarajio ya jamii yao kwao.
Huwafahamisha kuwa wamevuka hatua muhimu na kuwaandaa kiakili kwa majukumu
ya utu uzima.

(c) Huonyesha furaha ya vijana kujivunia hatua ya kutoka utotoni na kuingia utu uzima.
(d) Huhimiza ujasiri na kukebehi woga.
(e) Huhimiza uzalendo na kuonea fahari utamaduni wa jamii. Wanaoshiriki jandoni
hujitambulisha na jamii yao zaidi, na hivyo uzalendo huimarika.

(£) Nyiso hutoa nasaha kwa vijana. Huwafahamisha kuhusu matarajio ya uchungu,
majukumu yao ya kiutuuzima, huasa dhidi ya woga na kuwasia umuhimu wa kuhifadhi
siri watakazopewa.

(8) Huburudisha waliohudhuria shughuli hii.


(h) Huleta umoja miongoni mwa wanajamii. Vijana waliotahiriwa wakati mmoja
hujitambulisha kama ndugu.

Mfano wa nyiso

Ewe kilizi
Ulozowea kujificha
Nyuma ya mama kujikinga, dhidi ya milio
ya radi ilo juu mbinguni
Jua kesho ni siku ya siku
Siku ya kujua mbichi na mbivu
Kutofautisha jogoo na vipora,
ngariba taposhika, chake kijembe
Ndipo utakapojua bayani
Ukoo wetu si wa kunguru
Ikiwa hu tayari
Kisu kukidhihaki
Sithubutu kamwe, wanjani kuingia
sije kuniaibisha miye, amiyo na akraba nzima!

Kwa kurejelea wimbo uliosoma, jibu maswali yafuatayo.


Nani anayeimba wimbo huu? Thibitisha.
Taja sifa za nyiso zinazojitokeza katika utungo huu.
Andika mbinu tatu za kifasihi zilizotumiwa katika wimbo huu.
Fafanua majukumu matano ya nyiso.
MELI
Andika ubeti mmoja wa nyiso kutoka kwa jamii yako.

Nyimbo za kisiasa
Hizi ni nyimbo ambazo huimbwa katika shughuli au miktadha ya kisiasa. Nyimbo za kisiasa
huwa na maudhui mapana kama vile mapambano, propaganda, kuzindua, kuhamasisha,
kukejeli, kuhimiza au kutia ari.

Majukumu ya nyimbo za kisiasa


(a) Nyimbo za kisiasa hukuza umoja wa kisiasa miongoni mwa washiriki. Wakati wa
kupigania uhuru, nyimbo hizi zilitumiwa kama nyenzo za kuwaunganisha watu.
(b) Huzindua na kuhamasisha watu. Huwapa watu, kwa mfano wafanyakazi, ari ya
kupigania haki zao. Nyimbo za kisiasa huwatanabahisha watu kuhusu haki zao na
kuwahimiza kupigana dhidi ya unyanyasaji.
(c) Husawiri mfumo wa kisiasa na kijamii wa jamii husika na maoni ya wananchi kuhusu
mfumo huo. Je, wanaupenda au wanaupinga? j
(d) Husawiri migogoro iliyopo katika jamii. Je, ni ya unyanyasaji, uongozi mbaya,
unyonyaji, ubinafsi, usawa, uhuru?
—(e) Hutumiwa kueneza propaganda za kisiasa. Baadhi ya nyimbo za kisiasa huimbwa ili
kusawiri uzuri wa utawala fulani. Kwa mfano, KANU Yajenga Nchi, ni wimbo wa kisiasa
ulionuia kuwavutia watu kukipenda chama hiki cha kisiasa.
Ai
(£) Huhimiza uzalendo na mshikamano wa kitaifa. Nyimbo za taifa ni mfano wa nyimbo
za kisiasa ambazo hutumiwa kuwahimiza raia kuionea fahari nchi yao na kuishi kwa
udugu.
(8) Huweza kutumiwa kama rekodi ya matukio ya kihistoria katika jamii fulani. Baadhi
ya nyimbo za kisiasa huzungumzia mapambano dhidi ya ukoloni na historia ya
mapambano hayo.
(h) Hutumiwa kukashifu uongozi mbaya.
(i) Hutumiwa kama sifo kuwasifia viongozi waadilifu na mashujaa wengine wa kisiasa
kama vile Harry Thuku, Dedan Kimathi, Arap Moi, Kenyatta na Jaramogi Odinga
nchini Kenya.

() Huburudisha, hutumbuiza na kustarehesha watu katika shughuli za kisiasa au za


kitaifa.

(k) Hutumiwa kuliwaza na kuwapoza wahasiriwa wa migogoro ya kisiasa.

Mfano wa wimbo wa kisiasa


mala

Mabeberu watu wabaya


Walimfunga Kombozi
Nia yao ikiwa moja
Kudidimiza jamii yetu
Katika lindi la istiimari
Ela hawakufua dafu
Mabarobaro waliingia msituni
Bunduki wakashika
Kupigana, kupigania 'wiyathi'

Beberu lipoona
Vita vimechacha
Tamaa iliwatoka
Wakasalimu amri
Uhuru wakatoa
Hawakutoa kwa hiari
Hilo usisahau
Wazalendo walipigana '
Kwajino na ukucha
Uhuru tukapata
Kombozi akashika sukani
Hadhi yetu tukarudishiwa.
Tumia wimbo uliosoma kujibu maswali yafuatayo.
1. (a) Thibitisha kuwa huu ni wimbo wa kisiasa.
(b) Andika majukumu matano ya nyimbo za aina hii.
(c) Bainisha matumizi ya mbinu zifuatazo katika wimbo huu.
(i) Majazi (ii) Urudiaji (iii) Nahau

2. Tofautisha kati ya nyimbo za taifa na nyimbo za vita.

Nyimbo za sifa (sifo)


Nyimbo za sifa pia huitwa sifo. Ni nyimbo ambazo hutoa sifa za mtu fulani. Sifo husifu
michango na mafanikio ya watu katika jamii. Ni muhimu kutaja kuwa nyiso, mbolezi na
nyimbo za arusi huweza kutumiwa kama sifo.

Sifa za sifo
(a) Sifo husifu na kutukuza watu ambao wamefanya jambo fulani. Kwa mfano, husifu
maarusi, waliohitimu jandoni, viongozi wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, walioshinda
mashindano ya michezo au wenye kumiliki vitu, vipawa na hali fulani.
(b) Sifo hutumia sitiari kwa ufanifu mkubwa. Huwafananisha wanaosifiwa na wanyama
ili kuonyesha sifa fulani bora. Kwa mfano, kiongozi anaweza kufananishwa na simba
kuonyesha ujasiri wake au kurejelewa kiistiari kama Mkuki uwakao au Ngao yetu.
(c) Sifo hutumika katika miktadha mbalimbali ya kijamii kama vile miviga.
(i) Huimbwa kwenye jando kuwasifu mashujaa na kuwapongeza kwa kuingia katika
utu uzima.
(ii) Huimbwa kwenye mazishi kama taabili/taabini kuwasifu na kuwakumbuka
waliokufa.
(iii) Huimbwa kwenye harusi kuwasifu maarusi.
(iv) Huimbwa katika sherehe za kutawazwa kwa viongozi au wafalme.
(v) Kuna sifo za kidini ambazo humsifu Mungu na mtume. Kwa mfano, Kasida ya
Hamziya inamsifu Mtume Mohammed.
(d) Sifo pia huweza kuimbwa na mtu au watu binafsi wakijisifu. Sifo ya aina hii huitwa
majigambo au vivugo.
(e) Sifo huakisi thamani ya jamii husika. Kila jamii ina thamani yake. Kuna jamii zinazothamini
ujasiri wa kivita, nyingine usuli mwema au nasaba tukufu, ufugaji wa mifugo wengi, kilimo
au harusi.
(£) Sifo hupigia chuku sifa za anayesifiwa.
Majukumu ya sifo
Sifo husifu matendo chanya ya viongozi au watu mashuhuri katika jamii.
Hutangaza mafanikio au mchango wa mtu au watu wanaosifiwa kwa jamii. Anayeimba
sifo hutaja mambo ambayo anayesifiwa alitenda au ametenda.
Hukuza uzalendo. Sifo huwahimiza vijana kuiga matendo mazuri ya wanaosifiwa. Kwa
njia hii, watu hujifunza kuionea fahari jamii na kuwa tayari kuitolea mchango wao.
Kuweka kumbukumbu au rekodi ya matukio ya kihistoria. Wimbo unaomsifu shujaa
wa vita, kwa mfano, huonyesha vita alivyopigana, alipigana na nani na lini.
Huonyesha msimamo na mitazamo ya jamii fulani kuhusu masuala mbalimbali. Wimbo
unaosifu uzalendo wa mtu fulani vilevile unaweza kuonyesha chuki kwa usaliti.
Hutambua mchango wa watu mbalimbali kwa jamii. Sifo hutaja majina ya wanaosifiwa
kwa nia ya kuwatambua na kutambulisha juhudi zao.
(g) Huburudisha. Sifo nyingi hutumbuiza, hutuliza na hupumbaza akili.
Mfano wa sifo
aa

Lau sifa zingekuwa milki


Ungeumiliki ulimwengu mzima
Ungeufumbata kwa viganja vyako
Viganja ambavyo daima vi wazi
Kumwaya fadhila ya matone
Matone ja mvua ya masika

Lipi ambalo hukutenda


Kuikwamua jamiiyo?
Umevinjari misitu na nyika ngapi?
Miguuyo ambayo daima hailalamiki kukanyaga miiba,
miiba mikali ja nyembe
Suluhisho kitafuta kuiauni aila?

Nani asokumbuka siku ulipozaliwa?


Mbingu hazikushuka
Kwa vishindo ngurumo?
Likajiri kutangaza, mezaliwa mkombozi?
Nani asoajabia ukarimu wako utotoni?
Kutoa vyako vya tunu kuwakabidhi wahitaji?
Je, waja mmeghafilika, jinsi alipotanga na jua

Tulipotekwa na adui
Mifugo wote kutwaliwa
Tukabaki kuuma vyanda
Je, hakupambana na majagina
Mifugo wetu kurudisha
Utu wetu kukomboa
Haiba yetu kurejesha?

Wafalme wangapi wameweza


Hata katika aushi yao yote
Kutekeleza alofanya
Kwa miongo mitatu aloishi?
Miji mingapi ilosimama
Kwa fahari vilimani kutangaza yako bidii
Maendeleo kudumisha?

Kwa milizamu ya maji yalotoka mabombani?


Makoo hawakuingia vyuoni
Vitabu kubukua wakiandamana na wenzao vipora,
ambao awali wakiumiliki
Uga huu peke yao?
Nani wa kutolewa, kama kifani chako?

Zoezi Zi

Ukirejelea mfano wa sifo uliosoma, jibu maswali yafuatayo:

Thibitisha kuwa huu ni wimbo wa sifo.

Fafanua muundo wa jamii hii kijamii na kiuchumi?


Huku ukitoa mifano, eleza sifa za aliyetungiwa utungo huu?
Andika mabadiliko ambayo anayesifiwa ameiletea jamii hii.
Bainisha mbinu zozote za lugha zilizotumiwa na uonyeshe umuhimu wazo
katika uwasilishaji wa maudhui.
Nyimbo za kazi (hodiya)
Nyimbo za kazi pia huitwa hodiya. Hizi ni nyimbo ambazo huhusishwa na kazi kama vile
kutwanga nafaka, kupalilia, kuinua gogo na kuvuna. Kuna aina nyingi za nyimbo za kazi
kama zilivyo kazi zenyewe. :

Sifa za hodiya
(a) Huimbwa wakati watu wanapofanya kazi. Kila aina ya kazi huwa na aina yake ya
nyimbo. Kuna nyimbo za wawindaji, za wakulima (wawe), nyimbo zinazohusishwa
na shughuli za majini (kimai) na pia za vita.
(b) Huimbwa na kundi la wafanyakazi au mtu mmoja wakati anapofanya kazi yake binafsi.

Majukumu ya hodiya
(a) Huhimiza watu kutia bidii na kuendeleza kazi bila kufa moyo.
(b) Hukashifu uvivu na utegemezi. Baadhi ya nyimbo za kazi hukashifu wasiopenda kazi.
(c) Hurahisisha kazi kwa kupunguza fikira za uchovu. Watu wanapofanya kazi wakiimba,
kazi huonekana kuwa nyepesi na muda huonekana kupita kwa kasi.
(d) Husawiri imani, mitazamo na thamani za jamii husika kuhusu kazi. Jamii inathamini
kazi gani? Uzembe na bidii kazini huchukuliwaje? Kazi inapewa nafasi gani?
(e) Huonyesha changamoto au matatizo ambayo wafanyakazi hukabiliana nayo katika
kazi zao. Je, wanahofia nini kazini? Wana matumaini gani katika kazi zao?

(f) Hujenga ushirikiano. Watu wanapoimba wakifanya kazi pamoja hujenga ushirikiano.
Ushirikiano pia huhimizwa katika baadhi ya nyimbo za kazi.

Mfano wa wimbo wa kazi

Viongozi walisema Pasiwe wa kutuvuta


Turudi mashambani Misri kuturudisha
Makonde kushughulikia Kwa pato la kufutia chozi
Mimea kupalilia. Ukame tatwandama
Tutie ghera ndugu Mashamba tukiachilia
Tujifunge masombo Mmomonyoko kuyatwaa
Udongo tutifue Tutabaki mikunguni
Samadi tutie, Kutegemea wahisani.
magugu tung'oe
Kilimo tuimarishe.
Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea wimbo uliosoma.
l; Wimbo huu huimbwa katika muktadha wa kazi gani?
2. Ni majukumu gani ya nyimbo za kazi yanayotekelezwa na wimbo huu?
3. Katika makundi, jadili ni changamoto zinazokabili wafanyakazi katika kazi
zifuatazo:
(a) Uvuvi (b) Uwindaji
(c) Kilimo (d) Ufinyanzi.

Nyimbo za mapenzi
Hizi ni nyimbo ambazo huwa na maudhui au ujumbe wa kimapenzi.

Sifa za nyimbo za mapenzi


(a) Nyimbo za mapenzi kwa kawaida huelezwa kwa maneno matamu yenye hisia
nzitonzito.
(b) Zinaweza kuwa sifo, yaani zikaimbwa kumsifu mpenzi fulani.
(c) Huwa na maudhui mbalimbali kulingana na lengo la mwimbaji. Mathalani:
(i) kumsifu mpenzi. Huweza kusifu umbo lake au hulka yake.
(ii) kuonyesha kusalitiwa au wivu.
(iii kuomba uchumba au huba.
(iv) wimbo wa mke kwa mume/mume kwa mke.
(v) kutaka udugu, kwa mfano, kutoka kwa familia ya mume kwa mke au familia ya
mke kutaka udugu kwa mume.
(vi) nyimbo za harusi.
(vii) kutambua uhusiano mzuri na mpenziwe na kumbembeleza mpenzi. Mfano wa
nyimbo za aina hii ni chombezi.

Majukumu ya nyimbo za mapenzi


Nyimbo za mapenzi hutekeleza majukumu yafuatayo:
(a) Kusifu tabia au umbo la mpenzi. Hutaja tabia chanya na umbo zuri la mpenzi.
(b) Kutakasa hisia za anayeimba. Mwenye mapenzi anaweza kutumia nyimbo kutoa hisia
zake za huzuni, furaha au kupumbazika. Kwa kufanya hivi, anaweza kupunguza uzito
wa hisia alizonazo.
(c) Huburudisha. Nyimbo za mapenzi huburudisha anayezisikiliza.

Aa.
4
(d) Hukuza ubunifu. Nyimbo za mapenzi hubuniwa kwa umbuji na ujumi wa hali ya juu
ili kuibua hisia za mapenzi, huzuni au huruma.
(e) Ninyenzo ya kupitisha maarifa au elimu ya jamii. Nyimbo za harusi hutumiwa kutoa
mawaidha ya unyumba kwa maarusi wapya. Aidha, matarajio ya jamii na majukumu
yao wapya kama bibi nabwana hupitishwakwanyimbo.

Mfano wa wimbo wa mapenzi

Tina analia, Tina analia


Chozi lausaliti undani wake
Undani ambao ameuficha kwa miaka na mikaka
Undani ambao japo anachelea kutangaza asije akaonekana
apendaye chongo ...
Itabidi kuutoa, kuumwaga mtama

Na kiini cha chozi hili ni kwamba imewadia


Imewadia siku ya siku Kanisani kwenda,
Kujitia pingu |
Kujitia pingu, pingu za aushi .
Je, hakuyataka haya? . |
Hakupania yapakata kama mwanagenzi,
apakatavyo malaika mikononi pake?
Kwani basi analovya, kidari kwa maji chumvi?
Shavu lake laini, kuwa kijivu kwa shaka?
. Ama ni yano mapenzi yalomlemea?
Mapenzi alopalilia kwa miaka na dahari?

Kipi kinokwinamisha,
kwa tewengu kukubwaga?
Ama ni majukumu kuhofia mwenzetu? aa |
Ni aidha za ulezi?
Ni hofu ya kutelekezwa?
Jikoni kuachwa jukumu la kawaida?
j |

Ama ni ugeni kwa nasaba uso asili unokuuguza? j


Je, ni mazoea unochelea kuacha? |
Ama ni uzito wa nanga ya huba?
Kipi, sema ewe mwenzangu, sema.

Nikahi ni sitara
Usumbufu kuepuka vipanga na mwewe
Ndoa huneemesha na jina kukupa ukatukuka kimwana
Shujaa ukapata wa kukulinda
Miliki ni hakikisho kutoka kwa dume hata katika mauko,
Penzi halali kupata, na warithi kuambulia,
wa kiume kukufaa
Silie mwana silie,
watutia simanzi
Waitia ndoa doa, nuksani kukuandamia.

Wavyele mpeni baraka


Mashangazi mtemeeni mate
Viganjani kumiminia pumzi zenu za neema
Ndoa yake kutengenea
Maumbu acheni
Kulengwa na machozi
Mwanmliza zaidi, unyonge kumtia
Baba mtu mshike kondooyo,
mwongoze kidesturi, madhabahu karibia,
mkabidhi mkweo, mwenzi wake wa maisha.

Ndiye takayekuwa fahali, simba atakuwa kikaida


Amri tatoa yeye, malkia kufuata,
utashi wake tatimizwa, ndivyo sheria inenavyo
Bila yeye kutamka mtamba haandamwi na sahibu
Tampenda ewe kinda, tanyenyekea bila kulalama
Penzi talinda wewe, wengine sije paramia
Kukupoka mwamba wako!

Zoezi

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea wimbo uliosoma:

Ainisha utungo huu kimaudhui.


Kwa mujibu wa wimbo huu, jadili kwa kutoa mifano nafasi ya mwanamume
katika jamii hii.
- Toa mifano ya tamathali za usemi zilizotumiwa katika utungo huu.
Fafanua majukumu ya utungo wa aina hii katika jamii yako.
Nyimbo za watoto (chekechea)
Nyimbo za watoto pia huitwa nyimbo za chekechea. Nyimbo hizi huimbwa na watoto wakati
wa kucheza ili kuifanya michezo ipendeze au wanapofanya shughuli zao za kitoto. Aidha,
katika shule za malezi, maarufu kama shule za chekechea, watoto hufunzwa na kuimba
nyimbo hizi. Nyimbo za watoto hubainishwa kwa mchezo mkubwa wa maneno na urudiaji
wa vifungu mbalimbali.

Umuhimu wa nyimbo za watoto


(a) Hutumiwa kama burudani. Ni nyenzo muhimu ya kujipumbaza na kupitisha wakati.
(b) Hukuza ubunifu miongoni mwa watoto. Watoto hujifunza kubuni nyimbo ambazo
zinaoana na michezo yao.
(c) Hukashifu tabia hasi. Watoto hutumia nyimbo hizi kuwakosoa na kuwakashifu walio
na tabia mbaya kama vile uchoyo.
(d) Hukuza utangamano. Watoto wanapokuja pamoja kucheza na kuimba, hawajali tofauti
zao za kinasaba na hukua kama watu wa jamii moja.
(e) Hutambulisha jamii. Kila jamii ina nyimbo za watoto ambazo hufungamana na
utamaduni pamoja na thamani za jamii hiyo.

Mfano wa wimbo wa watoto

Kitoto kivivu aiya aiya


Kikienda skuli aiya aiya
Saa tatu hazijafika aiya aiya
Ndicho hicho chalia njaa aiya aiya
“Ticha naona njaa aiya aiya”
Mwalimu hadiriki kuandika lolote aiya aiya
Kitoto machozi yatoka aiya aiya
Hadi ruhusa kipewe aiya aiya
Kitazame kilo ndani ya chupa aiya aiya
Ndipo kitulie aiya aiya.

Zoezi /1|

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea wimbo uliosoma: .


1. Andika maadili yanayojitokeza katika wimbo huu.
2. Taja mbinu za lugha zilizotumiwa katika wimbo huu.
3. Andika miktadha mitatu ambamo nyimbo za watoto hupatikana.
Jadiiya
Jadiiya ni nyimbo za kitamaduni ambazo zinaimbwa na kupokezwa kwa mdomo kutoka
kizazi kimoja hadi kingine. Kila jamii ina jadiiya ambazo hupokezwa kwa vizazi vyake.
Kimaudhui, nyimbo hizi husimulia mambo mengi hasa yaliyotukia katika historia ya jamii
kama vile matendo ya shujaa fulani, mateso, njaa na ucheshi.

Muhtasari wa aina za nyimbo


Baadhi ya nyimbo zifuatazo hazikufafanuliwa. Tumeziorodhesha tu kwa faida ya
mwanafunzi na mtafiti.
Ji Mbolezi. Huimbwa wakati wa kuomboleza mambo kama vile katika matanga, mazishi,
janga au kushindwa vitani.
Nyimbo za dini. Huimbwa katika shughuli za kidini kama vile katika ibada.
Nyimbo za vita. Huimbwa wakati wa vita ili kuwashajiisha wapiganaji au kusisitiza
ushujaa na uzalendo. Huwatambua mashujaa wa zamani kwa nia ya kuhimiza uzalendo.
Huweza pia kuimbwa baada ya kumalizika kwa vita ili kutaja matokeo ya vita.
4. Nyimbo za mapenzi. Huimbiwa wapenzi. Huhusu ulimbwende au usaliti.
Bembea/Bembelezi. Huimbiwa watoto kuwafariji au kuwabembeleza walale au
waache kulia. f
Nyiso. Huimbwa wakati wa jando na unyago.
Nyimbo za watoto/za chekechea. Huimbwa na watoto wanapocheza au wakiwa
shuleni.
- Tumbuizo. Huimbwa kwa madhumuni ya kutumbuiza au kuliwaza watu katika
sherehe kama vile ngomani na harusini.
Nyimbo za kuzaliwa kwa mtoto. Huimbwa kuonyesha au kuadhimisha kuzaliwa
kwa mtoto.
. Sifo/Tukuzo. Huimbwa kumsifu mtu fulani kwa mchango wake katika jamii.
- Hodiya/Chapuzo. Hizi ni nyimbo za kazi kwa jumla. Huimbwa kuchapua kazi.
- Kimai. Kimai ni nyimbo zinazohusu mambo ya majini au shughuli za majini kama
vile uvuvi na ubaharia.
. Wawe/Vave. Huimbwa wakati wa shughuli za kilimo.
- Kongozi. Nyimbo za kuaga mwaka katika jamii ya Waswahili.
. Nyimbo za usasi. Huimbwa na wasasi wanapokwenda au kutoka usasini.
- Nyimbo za taifa. Huimbwa kusifia au kutambulisha taifa fulani.
- Jadiiya. Jadiiya ni nyimbo za jadi ambazo hupokezwa kutoka kizazi kimoja hadi
kingine.
Uainishaji huu wa nyimbo huingiliana. Wimbo ambao ni mbolezi huweza
pia kutumiwa kama wimbo wa mapenzi au hata sifo.

Maghani
Maghani ni ushairi ambao hutolewa kwa kalima badala ya kuimbwa. Tofauti kati ya maghani
na nyimbo ni kwamba maghani hayaimbwi. Hata hivyo, kimaudhui maghani ni sawa na
nyimbo. Hushughulikia masuala ya kijamii kama vile kazi, maombolezi au siasa, kama
ilivyo katika nyimbo.

Sifa zaidi za maghani


(a) Maghani ni tungo za kishairi. Hii ina maana kuwa yana sifa za kishairi za kuwa na
mapigo ya kimuziki na maneno mateule yenye muwala.
(b) Maghani, husimulia matukio kwa kirefu hasa yanayotambwa.
(c) Maghani hutungwa papo hapo na kusemwa au kutongolewa mbele ya hadhira.
(d) Hutungwa kwa ufundi mkubwa.
(e) Maghani huweza kutolewa na mtu mmoja au kundi la watu.

Aina za maghani
Maghani ni ya aina mbili kuu:

(a) Maghani ya kawaida


Maghani ya kawaida ni tungo za kishairi ambazo hutongolewa kuhusu masuala ya kawaida
kama vile mapenzi, njaa, masikitiko, kazi, majonzi au dini. Maghani ya kawaida hughanwa
tu bila kusimuliwa.

(b) Maghani simulizi


Maghani simulizi ni maghani ya kihadithi ambayo husimulia sifa za mtu, kitu, mnyama,
historia au tukio fulani. Maghani simulizi hutolewa yakiambatana na muziki pamoja na
ala kama vile njuga, zeze au marimba.
Mtambaji wa aina hii ya maghani huitwa yeli au manju. Manju au yeli kwa kawaida huwa
bingwa wa kupiga ala fulani ya muziki. Utanzu wa maghani unaweza kuainishwa katika
vitanzu vifuatavyo vya sifo, tendi, rara na rara nafsi.

Sifo
Haya ni mashairi ya sifa ambayo hughaniwa kumsifu mtu fulani kutokana na matendo
yake ya kishujaa.

D
Sifa za sifo
(a) Sifo huwasifu watu, wanyama, mimea na hata vitu visivyo hai.
(b) Sifo hutoa sifa chanya na hasi. Sifa hasi hutolewa kwa nia ya kukashifu vitendo vibaya.
(c) Huingiliana na kutegemeana na tanzu nyingine za fasihi simulizi. Sifo huweza
kutumiwa katika miviga kama vile mazishi kusifu aliyekufa kwa matendo yake ya
kipekee. Pia, huweza kutumiwa katika harusi na tohara kuwasifu wanaohusika katika
shughuli hizo.

Aina za sifo

Sifo zinaweza kuainishwa katika vitanzu mbalimbali kama vile majigambo au vivugo,
pembezi na tondozi.

(i) Majigambo au vivugo


Hizi ni tungo za kujisifu, kujitapa au kujigamba. Anayejigamba huwa mwanasanaa (mshairi)
ambaye anaelewa kwa undani analozungumzia. Majigambo hutofautiana na aina nyingine
za sifo kwa kuwa katika majigambo, anayejigamba huzungumza kujihusu yeye mwenyewe.

Sifa za majigambo
Sifa bainifu za majigambo ni kwamba:
(a) Hutungwa na kughanwa na mhusika mwenyewe.
(b) Hutungwa kwa usanii mkubwa. Anayejigamba hutumia mfanano, sitiari, vidokezi,
ishara na urudiaji.
(c) Anayejigamba hujitungia kivugo kufuatia tukio mahususi katika maisha yake. Anaweza
kuongea kuhusu siku za jandoni, ndoa au kuoa, kutoka vitani, kushinda mchezo, kesi
au jambo fulani gumu.
(d) Kwa kawaida, majigambo au vivugo hutungwa na kughanwa na wanaume.
(e) Huwa na matumizi ya chuku. Anayejinaki hujisifu kupita kiasi kwa kutaja mafanikio
au mchango wake. Anaweza pia kutoa ahadi ya kuleta mafanikio makubwa hata zaidi
ya yale ambayo tayari ameiletea jamii yake.
(£) Majigambo hutolewa kwa nafsi ya kwanza kwa sababu anayejigamba ni mshairi
mwenyewe.
(g) Anayejigamba huweza kubeba baadhi ya vifaa vyake vya kazi au vinavyoonyesha
jambo analojisifia. Aidha, anaweza kuvaa maleba yanayooana na kazi au jambo ambalo
anajisifia.
ai

(h) Kwa kawaida majigambo hutungwa papo hapo. Hata hivyo, mengine huandikwa ili
kughanwa baadaye katika hafla fulani kama vile harusi. Ni muhimu kutaja hapa kuwa
haya ni mabadiliko katika sanaa hii.
(i) Anayejisifu huweza kutaja usuli wake wa kinasaba. Katika baadhi ya jamii, anayej igamba
huhitajika kutaja na kuisifu nasaba au ukoo wake — upande wa baba na mama kwa
majina yake halisi.
G) Wanaojigamba mara nyingi huwa walumbi au washairi wanaoelewa kwa kina
wanalolitongoa.
(k) Maudhui makuu katika majigambo ni ushujaa.

Umuhimu wa majigambo
(a) Hukuza ubunifu. Kadiri mtu anavyotunga na kughani majigambo ndivyo
anavyoimarisha uwezo wake wa kubuni mitindo mipya ya utunzi na uwasilishaji.
(b) Hukuza ufasaha wa lugha.Watunzi wengi wa majigambo huwa walumbi.
(c) Ni nyenzo ya burudani. Majigambo huongoa waliohudhuria sherehe ambapo
yanatolewa.
(d) Hudumisha utu na utambulisho wa mwanaume katika jamii. Kwa sababu ya uchokozi
uliokuwepo katika jamii, ilikuwa muhimu kwa wanaume katika jamii kuwa jasiri,
wakakamavu na mashujaa waliokuwa tayari kutetea jamii zao. Kupitia kwa majigambo,
wanaume walidhihirisha nafasi zao katika jamii.
(e) Ni nyenzo ya kufanya watu waheshimiwe. Hudumisha ari ya kuwafanya wanaume
kutaka kuwa mashujaa. Mtu alipofanya kitendo cha ushujaa alijigamba na
kuheshimiwa. Kwa sababu hii, kila mtu alitaka kufanya jambo la kishujaa ili ajigambe
na kuheshimiwa.

Mfano wa majigambo

Ndimi Kisoi, dume la ukoo mtukufu


Ulojipambanua kwa mabingwa
Wachezaji hodari wa ngoma
Ndimi dume liloingia nyanjani
Makoo yakatetemeka
Yakang'ang'ania, gozi kusakata nami.

Kijiji kizima kilinijua


Wazee walinienzi
Wakamiminika kiamboni
Mabinti kunikabidhi.
Kwa kurejelea shairi ulilosoma, jibu maswali yafuatayo:
1. Eleza sifa za majigambo zinazojitokeza katika utungo huu.
2. Andika mbinu za lugha zilizotumiwa katika utungo huu.

(ii) Tondozi
Tondozi ni tungo ambazo hughanwa kuwasifu watu, wanyama au vitu kama milima,

mashuhuri, wapenzi, marafiki, watani, wake/waume, watoto au hata adui zao.


Wanyama na vitu ambavyo hutungiwa tondozi sanasana ni mifugo, wanyama wa porini
na miti mikubwa. Vitu na wanyama hawa hupewa sifa kiistiara zikikusudiwa binadamu.

Mfano wa tondozi

Kipungu kipungu
Nani kama yeye?
Hashindiki kwa nia
Hashindiki kwa shabaha
Hulenga mbinguni
Hutia ghera kufikia peo
Peo zisofikika kwa wanokata tamaa
Kipungu, kipungu, hachi tufani za anga.

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea utungo uliosoma.


1. Kwakutoa mifano kutoka kwa utungo huu, thibitisha kuwa utungo wenyewe
ni aina ya sifo.
2. Kipungu anapewa sifa gani katika tondozi hii?

(iii) Pembezi au pembejezi


Pembezi ni aina ya tondozi ambayo hutolewa kusifu watu fulani pekee. Kwa kawaida,
husifu watu wenye kujipambanua kwa matendo yao ya kishujaa na kujitolea kwao. Pembezi
hutungiwa watu kama vile:
(i) watawala au viongozi (ii) walezi wazuri (iii) mashujaa wa vita
(iv) waganga mashuhuri (v) wapenzi waliopigania pendo lao.
Mfano wa pembezi

Nani kama wewe mama?


Nani anokufana 'mwaitu'
Subira uliumbiwa
Bidii nd'o jina lako la pili
Moyo wenye heba
Msimamo usoyumba
Anoelekeza kwa imani
Anoadhibu kwa mapenzi makuu
Mzazi, mlezi na rafiki wa dhati
Tangu siku za kusimama dede.

Tumia shairi ulilosoma kujibu maswali yafuatayo.


1. Andika sifa za sifo zinazojitokeza katika utungo huu.
2. (a) Ninani anayezungumza (nafsineni) katika pembezi hii?
(b) Anamsifu nani?
3. Tunga pembejezi ya ubeti mmoja.

Tendi

Tendi huitwa pia ushairi wa ushujaa. Utendi ni ushairi mrefu wa kimasimulizi unaotumia
mtindo (lugha ya) wa kiwango cha juu na ambao nguli wake ni jagina au shujaa mwenye
sifa za kiuunguungu.
Tendi husimulia matukio ya kihistoria yenye uzito au umuhimu wa kijamii na kitaifa.
Husimuliwa kwa mfano, kuhusu mwanzilishi wa dini au shujaa wa vita.

Tendi hujumuisha sifo zinazoonyesha mafanikio ya mashujaa na mbolezi zinazoonyesha


anguko la shujaa au hata tawala. Huweza pia kutoa mawaidha kuhusu masuala ya kijamii,
kama vile jinsi ya kuishi na wanajamii wenzako, masuala ya unyumba, uhusiano wa
binadamu na Mungu au miungu. Tendi za mwanzomwanzo zilitungwa na wasanii kutokana
na visasili na mighani ya jamii husika. Tendi hizi simulizi, baadaye, ziliigwa na waandishi.
Hivi sasa tendi nyingi zimeandikwa.

<<
Sifa za tendi

(a) Tendi husimulia matukio muhimu ya kihistoria au kijamii kama vile vita vya ukombozi,
safari ndefu au watu mashuhuri.

(b) Utendi ni masimulizi yenye ulumbi na lugha ya kiwango cha juu. (Ulumbi ni sanaa ya
kutumia lugha kwa upekee.)

(c) Ingawa tendi huhusu matukio ya kweli, tendi nyingi huchanganya historia na visasili
(imani za kidini za kijamii kuhusu asili ya matukio ya kijamii). Matukio na sifa za
wahusika husimuliwa kwa kupigwa chuku kiasi kwamba wanaonekana kutokuwa watu
wa kawaida.

(d) Kimsingi, utendi husimulia kuhusu ushujaa au mashujaa. Huonyesha migogoro


iliyowakumba mashujaa hao na jamii kwa jumla.

(e) Utendi unaweza kughanwa au ukaimbwa kishairi. Uwasilishaji wake pia unaweza
kuandamana na ala za muziki.

(£) Tendi hutolewa katika mazingira maalumu. Ikiwa utendi utawasilishwa hadharani,
hafla ambamo unatolewa huwa ama rasmi au ukahusiana na miviga kama vile harusi
na matambiko.
Tendi hupokezwa kutoka kizazi hadi kingine.
Kwa kawaida tendi ni tungo ndefu.
Tendi hutungwa papo hapo, hivyo huathiriwa na muktadha wa utungaji. Hata hivyo,
sanaa ya utendi imebadilika na sasa huhifadhiwa vitabuni kimaandishi.
Baadhi ya tendi muhimu katika jamii za Waafrika ni:
(i) Utendi wa Fumo Liyongo (ii) Utendi wa Sundiata
(iii) Utendi wa Al-Inkishafi (iv) Utendi wa Mwanakupona
(v) Utendi wa Adamu na Hawa (vi) Utendi wa Shaka Zulu
(vii) Utendi wa Tambuka viii) Utendi wa Shufaka.
(ir) Utendi wa Mwindo (2) Utendi wa Lianja.

Mfano 1 wa utendi

34. Uwene wangapi watu wakwasi, 35. Malimwengu yote yawatiile,


walo wakiwaa kama sham'si, na dunia yao iwaokele;
Wa muluku zana za adharusi, Wachenenda zitwa zao zilele,
dhahabu na fedha wakhiziniye. mato mafumbuzi wayafumbiye.
37. Nyumba zao mbake zikinawiri, 45. Sasa walaliye moya shubiri, |
kwa taa za kowa na za sufuri; pasipo zuliya wala jodori,
Masiku yakele kama nahari, Ikawa miwili kutaathari, |
haiba na jaha iwazingiye. dhiki za ziyara ziwakusiye. |

50. Madaka ya nyumba ya zisahani, 59. Wapi wa Kiungu wayaza kumbi, j


sasa walaliye wana wa nyuni,
Jj
na Mashekhe mema wa Kisarambi? |
Bumu hukoroma kati nyumbani; Walaliye nyumba za vumbi-vumbi, |
zisiji na koti waikaliye. ziunda za miti ziwaaliye. j
|
60. Wa wapi ziuli wa Pate Yunga, 61. Kwali na mabwana na mawaziri, |
wenye nyuso 'ali zenye mianga? wenda na makundi ya asikari, |
Wangiziye nyumba za tanga-tanga, Watamiwe nati za makaburi, |
daula na 'ezi iwaushiye. pingu za mauti ziwafundiye.

62. Kwali na makadhi wamua haki, 63. Aimi! Wawapi wake zidiwa,
wahakiki zuo wakihakiki, Zituzo za mato, wasiza ngowa?
Waongoza watu njema tariki; Wasiriye wote kuwa mahuwa;
wesiwe kwa wote waitishiye. sasa ni waushi waliushiye.

(Kutoka: Tenzi Tatu za Kale, Mulokozi (Mh.), TUKI, uk. 89 - 96.)


AM mm mm ———————

Kwa kurejelea utendi uliosoma, jibu maswali yafuatayo.


1. Andika sifa za utendi zinazojitokeza katika utungo huu.
2. Yaliyomo katika utendi huu yanakatisha tamaa! Thibitisha.
3. (Ya) Andika wahusika katika utendi huu.
(b) Fafanua sifa za wahusika uliotaja katika (a).

Mfano 2 wa utendi

5. Niweleze kwa utungo Kimo kawa mtukufu


hadithi yake Liyongo mpana sana mrefu
niweleze na mazingo majimboni yu marufu
mambo yalomzingiya. watu huya kwangaliya.
11. Wagala wakabaini 12. Mfalume kawambiya
“Huyu Liyongo ni nyani Wagala kiwasifiya
Kwetu hayusilikani “Huwegema watu miya
wala hatuyasikiya.” wasiweze hukimbiya.”

13. “Ni mwanamume swahihi 14. Ghafula kikutokeya


kama simba una zihi mkoyo hukupoteya
usiku na asubuhi tapo likakuwiliya
kutembea ni mamoya.” ukatapa na kuliya.

15. Mato kikukodoleya 41. “Twaitaka mbeu yake


ghafula utazimiya nasi kwetu tuipeke
kufa kutakurubiya kwa furaha tumuweke
kwa khaufu kukungiya. apate kutuzaliya.”

225. “Liyongo silaha yetu 226. Mui walisikitika


kwa wut'e khasimu zetu hakuna wa kutosheka
alikuwa ngao yetu!” kwa Liyongo kutoweka
wut'e wakinena haya. imeanguka paziya.
(Kutoka: Tenzi Tatu za Kale, Mulokozi (Mh.), TUKI, uk. 23-25, 29, 57.)

Andika sifa za utendi zinazojitokeza katika utungo huu.


Fafanua sifa za mhusika wa utendi huu.
Onyesha matumizi ya vipengele vifuatavyo vya kifani katika utungo huu.
(a) Usimulizi (b) Sitiari (c) Taswira
(d) O Tashbihi (e) Chuku (f) Taashira/Ishara

Rara

Rara ni hadithi fupi na nyepesi za kishairi zinazopitishwa kwa mdomo. Rara huzungumzia
tajiriba ya maisha kwa kutamba hadithi kwa mtindo pendwa au kwa njia ya kusisimua.
Wakati mwingine, hughanwa kwa kuandamana na ala za muziki.

Rara nyingi pendwa husimulia matukio ya kubuni, ingawa kuna chache zinazosimulia
matukio ya kweli. Zinaweza kusimulia kuhusu mahusiano mbalimbali kama vile kati ya
waajiri na waajiriwa, uhaba wa kazi, suala la usalama, masuala ya kijinsia na msongamano
wa magari.
ai

Sifa za rara

(a) Hadithi katika rara huwasilishwa katika beti, kila ubeti ukishughulikia suala bainifu.
Maana ya kila ubeti huwa wazi.

(b) Huwasilishwa kwa mtindo igizi kwa kuandamana na ala za muziki na utendaji wa
matukio.

(c) Hupatikana katika fani au mitindo tofauti tofauti. Hii ni kwa sababu waliozighani
walijifunza na kuzipitisha kwa njia ya mdomo na kuingiza mabadiliko.

(d) Rara nyingi simulizi zilihusu koo tawala japo za kisasa zimeanza kusimulia masuala
ibuka na ya kawaida, kama vile mahaba, kwa lugha isiyo rasmi.
Kwa kawaida, rara simulizi hutolewa kwa toni ya kitanzia.
Rara husisimua. Kwa kawaida rara huwa na mwanzo wa kiupeo unaoteka hisia za
msikilizaji na kumsisimua kwa lugha yenye mguso.
Rara nzuri zaidi huwa na ufumbaji na udokezaji wa masuala badala ya kuyaelezea kwa
ukamilifu na uwazi. Zinaweza kutumia sitari badala ya kutaja jambo moja kwa moja.
Rara pia huwa na ucheshi wenye kinaya.

(h) Nyingi za rara husimulia mambo ya kubuni. Hata hivyo, kuna baadhi ya rara ambazo
husimulia visa vya kweli.

Mfano wa rara

Alichukua mkoba wake


Akanipa kisogo
Kana kwamba hakunijua
Kana kwamba hakusema, “Hadi mauko”.

Hakujali penzi letu


Hakujali wana
Ambao ndiye alowapa uhai.

Alijua nilimpenda
Ila hata hilo alijipa kujipurukusha
Akayoyomea
Akamezwa na ulimwengu.
Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea utungo uliosoma.
1. Bainisha mzungumzaji (nafsineni) katika utungo huu.
2. Mzungumzaji analalamikia nini?
3. Eleza toni ya rara hii.
4 Bainisha sifa za rara zinazojitokeza katika utungo huu.

Rara nafsi
Huu ni ushairi wa kinafsi ambao hutungwa na mtu kuelezea hisia, matatizo na fikra zake
mwenyewe. Kwa kawaida, rara nafsi huwasilishwa kwa njia ya uimbaji unaoandamana na
ala za muziki. Hushughulikia masuala yanayoathiri hisia za mtu binafsi kama vile mapenzi,
usaliti, talaka na kifo. Mashairi mengi yanayohusu mahaba ni rara nafsi. Rara nafsi
hubainisha tabia za anayeghani, historia yake, imani na mionjo yake ya maisha. Ushairi
rasmi wa makiwa na sifo ni aina za rara nafsi.

Katika baadhi ya rara, mzungumzaji huzungumza moja kwa moja na hadhira au


anayeandikiwa rara hii. Anaweza, kwa mfano, kuzungumza na mkewe, mwanawe,
mpenziwe, au hata Mungu au miungu.
Rara nafsi hutolewa katika miktadha mbalimbali ya kijamii kama vile:
(a) Katika mazishi —- kumsifu aliyeaga dunia.
(b) Katika harusi —- kuwasifu maarusi. (Biarusi pia anaweza kughani rara pale ambapo
ameshinikizwa kuolewa ili kukashifu tendo hilo.)

(c) Katika baadhi ya jamii, rara nafsi zilighanwa katikati ya utambaji wa ngano, wakati
wa kazi kama vile mavuno au utwangaji wa nafaka au katikati ya sala.
Mfano wa rara nafsi
ka

Muda umefika wa pingu kutiwa


Kutiwa silisili, kwani si utashi wangu
Ukoo waniuza, mithili ya kondoo sokoni
Mwambieni shangazi kwaheri nampigia
Hata angataka kuniopoa hawezi
Kwani mahari imetolewa
Mifugo kikwi nduguye amepokea
Kwaheri mama, kwaheri dada.
Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea utungo uliosoma.
1. Ni nani anayezungumza katika rara nafsi hii?
2. Andika changamoto zinazomkumba mzungumzaji.
3. Eleza toni ya rara nafsi hii.
4. Taja sifa zozote mbili za maghani zinazojitokeza katika utungo huu.

Ngonjera
Ngonjera ni tungo za kishairi ambazo huwa na muundo wa kimazungumzo.Mazungumzo
katika ngonjera ni ya kulumbana au kujibizana. Mhusika mmoja husema au huuliza jambo
na mhusika mwingine hujibu au kuendeleza mazungumzo.
Katika ushairi simulizi, ngonjera huendelezwa (kwa kawaida kwa njia ya wimbo) pale mtunzi
mmoja husema jambo ambalo linaendelezwa na wenzake kwa njia hiyo hiyo - ya wimbo.
Katika baadhi ya jamii za Kiafrika, kuna nyimbo za harusi za aina ya ngonjera ambapo
upande wa bwana harusi huimba kuhusu jambo ambalo hujibiwa na upande wa bibi harusi.

Umuhimu wa ngonjera
(a) Hukuza ubunifu. Majibizano kati ya wanaobishana humfanya kila mmoja atake
kuonekana bora zaidi katika ubunifu.

(b) Huimarisha stadi ya kuongea na kukuza ujasiri wa kuzungumza hadharani.

(c) Huburudisha. Dhana zinazowasilishwa katika majibizano husisimua hadhira.

(d) Hutia hadhira hamu ya kutenda jambo fulani au kuwasilisha maarifa fulani.

Mfano wa ngonjera

Upande wa Bwana Harusi


Sasa Susa
Utapikiwa na nani?
Jiko tumelitwaa
Utapakuliwa na nani?
Kijiko tumetwaa
Upande wa Bibi Harusi
Hatuna shida
Makoo tunao chungu tumbi
Mchukueni huyo
Tumewakabidhi
Nyie dhaifu
Msio na wa kuwatunza
Msio na wapishi!
AA AA IA AAA EIA aa ” - a A Wa aw

Kwa kurejelea utungo uliosoma, jibu maswali yafuatayo.


1. Thibitisha kwa kutoa mifano kuwa huu ni utungo wa aina ya ngonjera.
Eleza umuhimu wa utungo wa aina hii katika jamii.
Eleza mbinu za kifasihi zilizotumiwa katika utungo huu.
Fafanua uhusiano kati ya pande mbili zinazoshiriki katika ngonjera hii.
Eleza, kwa kutoa mifano kutoka kwa ngonjera hii, sifa za ushairi simulizi.

Mashairi mepesi
Haya ni mashairi ya kawaida ambayo hupatikana katika ushairi simulizi na ambayo
hukaririwa. Hujumuisha mashairi mafupi ya kihisia, kimapenzi, ya kuwasifu na kuwakosoa
watu, kuelekeza au hata kufahamisha kuhusu suala fulani. Kuna mashairi ya kisasa, kama
vile ubaguzi wa kijinsia, ukiukaji wa haki za watoto na ufisadi, ambayo yamehifadhiwa
kwenye maandishi.

Mfano wa shairi

Wa zamani waliamba, mwacha mila hujituma — Vazi hino kuazima, kamwe halitegemeki
Vipi wewe tauamba, utamaduni wa zama? Utakuwa ja kulima, wa shamba asomiliki
Kokote utapotamba, hutopata ila mama Mwenyewe kiliandama, mkulima hujidhiki,
Utamaduni ndo mama, mwingine ni wa kuomba. Kutafutala kukodi, kwanihanapakwegema.
AA AAA
AAA IIIA

Eleza ujumbe wa shairi hili.


2. Tunga shairi la beti tatu kuhusu masuala yafuatayo:
(a) Ufisadi (b) Shujaa wa kidini (c) Vitavyaukombozi.
3. Katika makundi, jadilini sababu kumi za mtaala wa elimu kusisitiza tamasha
za muziki katika shule na vyuo.
Utanzu wa Maigizo |

Utangulizi
Maigizo au drama ni sanaa ya mazungumzo yanayoambatana na matendo. Katika maigizo,
wahusika waigizaji huigiza tabia, maneno na matendo ya watu wengine katika jamii kwa
nia ya kuburudisha na kupitisha ujumbe fulani. Maigizo au uigizaji hupatikana katika tanzu
nyingine za fasihi simulizi ya Kiafrika. Katika hadithi, kwa mfano, utambaji huandamana
na matendo. Uigizaji pia hupatikana katika vipera vya ushairi simulizi kama vile ngonjera,
majigambo, tendi na mazungumzo kama vile soga, ulumbi na malumbano ya utani.
Vipera vya maigizo ni kama vile: michezo ya jukwaani, michezo ya watoto, vichekesho,
miviga, matambiko na ngomezi.

Sifa za maigizo
(a) Maigizo hutolewa au huigizwa mbele ya hadhira. Lazima kuwa na mwigizaji (fanani)
na mtazamaji (hadhira) ili uwasilishaji wa utanzu huu ukamilike.
(b) Uigizaji huhitaji uwanja maalumu wa kutendea au mandhari.
(c) Maigizo hufungamana na shughuli za kijamii kama vile utambaji wa hadithi na sherehe
za miviga kama jando, harusi na matanga. |
(d) Katika maigizo, sharti kuwe na tendo la kuigizwa. Wahusika huiga tabia au matendo
ya watu na viumbe wengine kwa nia ya kuelimisha, kukashifu na kuburudisha.
(e) Waigizaji huvaa maleba yanayooana na hali wanazoigiza.
(£) Maigizo huiga hali ya maisha ya jamii kisiasa, kiuchumi na kitamaduni kwa nia ya
kuonyesha mafanikio, udhaifu na migogoro katika nyanja za maisha.
(g) Maigizo huwa na muundo mahususi wa mtiririko wa matukio. Huanza kwa utangulizi |
wa mchezo (unaohusu kutambulisha mgogoro), ukuzaji wa mgogoro wenyewe, kilele |
cha mchezo (mgogoro) na mwisho (usuluhishaji wa mgogoro).
(h) Maigizo yanaweza kuambatana na ngoma pamoja na uimbaji wa nyimbo au ukariri
wa tungo za kishairi.
Umuhimu wa maigizo
(a) Maigizo huburudisha watazamaji na waigizaji wenyewe. Watu hutumbuizwa na
kupumbazwa na maigizo kama vile ya ngoma za kitamaduni na vichekesho.
(b) Maigizo huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii. Desturi za jamii kama vile
upashaji tohara, matambiko, majigambo, ngoma, miviga na michezo ya watoto
hudumishwa kupitia kwa maigizo.
(c) Ni kitambulisho cha jamii. Kila jamii ina sanaa yake ya maigizo ya shughuli za jamii
husika. Miviga kama vile mazishi na harusi hutofautiana kutoka jamii moja hadi
nyingine. Michezo ya watoto huwa mahususi kwa watoto wa jamii fulani.
(d) Hukuza umoja na ushirikiano. Watu wanapokuja pamoja kushiriki katika maigizo
hujitambulisha kama jamii moja.
Ni nyenzo ya kupitisha maarifa na amali za jamii. Kupitia kwa michezo ya jukwaani,
matambiko, ngoma, miviga na vipera vingine vya maigizo, maarifa na amali za jamii
hupitishwa. i
Husawiri mitazamo ya jamii kuhusu masuala mbalimbali. Baadhi ya uigizaji hufanyia
tashtiti vitendo vinavyochukiwa na wanajamii kama vile woga, wizi na usaliti.
(8) Husifu tabia chanya na kukashifu tabia hasi. Baadhi ya vichekesho hukashifu matendo
ya kijinga.
Hukuza uzalendo. Kupitia kwa maigizo kama vile miviga, vijana hujitambulisha na
jamii zao na kuzionea fahari. Baadhi ya miviga kama vile maigizo ya kutawazwa kwa
viongozi husifu waliotoa mchango mkubwa kwa jamii zao. Vijana na wanajamii hupata
kielelezo bora cha kuiga.
Huimarisha na kupalilia ubunifu. Kwa mfano, watoto wanaposhiriki katika michezo
ya watoto, hujifunza kubuni michezo wakiwa wachanga na pia kujifunza sanaa ya
uigizaji.
GJ) Hukuza kipawa cha uongozi. Waigizaji wanapochukua majukumu ya uongozi katika
michezo huweza kujifunza stadi za uongozi.
(k) Ni njia ya kuimarisha urafiki. Mathalan, mizaha au utani katika malumbano ya
utani yanapoigizwa hukuza urafiki, uhusiano bora na stahamala kati ya watu, koo na
makabila yanayolumbana. Pia, waigizaji wa michezo ya jukwaani wanapoigiza pamoja
hujenga uhusiano wa kirafiki.
(D) Huongoza jamii kupambana na mazingira wanamojipata. Kutegemea imani ya
wanajamii, matambiko yanaweza kuondoa matatizo katika jamii kama vile njaa,
ugonjwa na ukame kwa kuomba Mungu au miungu.
(m) Huelimisha. Kupitia kwa maudhui na hulka za waigizaji, hadhira hupata fursa ya
kujitathmini na kushauri nafsi zao kuiga ama kukashifu hulka hizo.
Sifa za mwigizaji bora

Kufanikiwa kwa uigizaji, kwa kiasi kikubwa, kunawategemea waigizaji. Mwigizaji bora
huwa na sifa zifuatazo:

(a) Ni jasiri. Ili aweze kuigiza bila woga mbele ya watu, ni sharti awe na ujasiri.
(b) Ni mbunifu. Huweza kutumia mbinu mbalimbali za uigizaji ili kuufanya uigizaji
kuvutia, kuondoa ukinaifu na kusisitiza ujumbe.

(c) Ni mwenye ujuzi wa kutumia ishara za uso, za mwili na miondoko ambayo inaoana
na hali anayoigiza. Ikiwa anaigiza hali ya huzuni, ishara za usoni zionyeshe hali hiyo.

(d) Ni mwenye ujuzi na ufasaha wa lugha. Aweze kutumia lugha ipasavyo kuwasilisha
mawazo kwa njia mwafaka na inayovutia.

(e) Anaielewa hadhira yake ili abadilishe mtindo wa uigizaji kulingana na kiwango na
matakwa yao.

(£) Anapaswa kuvaa maleba yanayooana na nafasi anayoigiza. Ikiwa anaigiza mzee, avae
mavazi ya kizee. Ikiwa anamwigiza mtu mwenye cheo, avae mavazi yanayooana na
hadhi hiyo.

(g) Aweze kubadilisha toni na kiimbo kulingana na hali tofauti tofauti za matukio
anayoigiza. Tukio la huzuni, kwa mfano, liwasilishwe kwa toni ya huzuni. Tukio la
kuudhi pia liwasilishwe kwa toni ya kukashifu.

(h) Hushirikisha hadhira kwa kuuliza maswali ya balagha ili kuondoa uchovu wa kutazama
na kusikiliza tu uigizaji na kumsaidia kuboresha uwasilishaji.

(i) Sharti aelewe utamaduni wa hadhira yake ili asitumie maneno na ishara ambazo
zinakinzana na imani yao.

J Ni mfaraguzi. Anapaswa kuwa na uwezo wa kubadilisha uigizaji wake papo hapo


kutegemea hadhira yake na kutoa mifano inayofahamika kutoka kwa mazingira ya
hadhira yake.

(a) Eleza maana ya maigizo.


(b) Fafanua nafasi ya mwigizaji katika uwasilishaji wa maigizo.
(c) Katika makundi, igizeni sherehe ya harusi katika jamii yenu.
Vipera vya maigizo
Utanzu wa maigizo una vipera vifuatavyo:

Michezo ya jukwaani
Hii ni aina ya michezo ambayo huigizwa jukwaani au mahali wazi. Mchezo wa jukwaani
huigizwa moja kwa moja mbele ya hadhira hai. Uigizaji wa michezo ya jukwaani huonyesha
kisa cha mgogoro fulani wa kijamii. Mgogoro huu unaweza kuwa kati ya wanajamii au
mgogoro kati ya mhusika na nafsi yake. Michezo inayoigizwa jukwaani inaweza kuwa ya
kawaida au ikawa michezo bubu (michezo isiyoambatana na sauti).

Umuhimu wa michezo ya jukwaani


(a) Huburudisha na kupumbaza baada ya shughuli za kazi. Ufundi wa kucheza/kuigiza
huburudisha watazamaji na wachezaji pia.

(b) Huimarisha uwezo wa kuzungumza hadharani. Jinsi mtu anavyoigiza ndivyo


anavyokuza ukakamavu wake wa kukabiliana na hadhira.

(c) Hukuza ubunifu. Waigizaji huhitajika kuiga tabia, hali au sauti za wahusika wa
hadithini. Pia, huhitajika kubuni mbinu mpya za uigizaji ili kuivuta hadhira.

(d) Ninyenzo ya kukuza umoja. Watu wanapokuja pamoja kutazama michezo, urafiki na
utangamano hujengeka.
(e) Hukuza uwezo wa kukumbuka. Mwigizaji huhitajika kukumbuka maneno halisi ya
mhusika wa mchezoni ili ayawasilishe kwa hadhira jinsi yalivyo.
(f) Hukosoa jamii. Watu wanaofanya kinyume na matarajio ya jamii kama vile wivu,
uchoyo au wizi hutungiwa mielezo inayosawiri matendo yao kwa nia ya kuwakosoa
kwa kudhihaki.

Vichekesho
Vichekesho ni michezo mifupi ambayo hupitisha ujumbe kwa namna ya kuchekesha.
Vichekesho vinaweza kujitegemea kama kipera cha maigizo au vikategemeana na
kufungamana na tanzu au vipera vingine vinavyoibua kicheko kama vile ngano na ulumbi.

Sifa za vichekesho
(a) Vichekesho huigizwa.
(b) Huwasilishwa kwa lugha sahili au nyepesi iliyojaa taswira zinazoweza kutambuliwa
na hadhira.
(c) Hutumia mbinu ya kejeli, kinaya au tashtiti kwa ufanifu mkubwa.
(d) Hushughulikia masuala ya kijamii kwa njia nyepesi, lakini inayonuiwa kuadilisha au
kurekebisha tabia.
(e) Vichekesho huwa vifupi.
(£) Vichekesho havihitaji uchambuzi wa makini au wa ndani ili kuvielewa au kupata
maana.

Umuhimu wa vichekesho

(a) Hutumiwa kukashifu matendo hasi au ya kijinga.


(b) Huburudisha na kusisimua.
(c) Huadilisha. Kila kichekesho hunuia kutoa funzo fulani.
(d) Kama aina nyingine za maigizo, hukuza ujasiri, ubunifu na uwezo wa kukumbuka.
Mifano ya vichekesho katika runinga nchini Kenya ni Vioja Mahakamani na Vitimbi.

Majigambo/Vivugo
Ingawa majigambo huainishwa kama kipera cha ushairi, yanaweza kuigizwa. Ikiwa
yatasimuliwa au yatakaririwa yakiambatanishwa na matendo basi yanaweza kuainishwa
katika utanzu wa maigizo. Majigambo, aghalabu yaliambatana na ngoma. Katikati ya ngoma,
aliyejigamba anajitokeza na kujigamba na kisha kurudia kucheza ngoma. Aliyejigamba
anabeba zana zake za vita, kama vile mkuki na ngao, ambazo alizitumia kuonyesha jinsi
alivyotenda matendo ya kishujaa aliyojigambia. Aidha, alivaa maleba kuambatana na jambo
alilojisifia.
(Kwa maelezo zaidi, rejelea Majigambo ukurasa 112 — 114.)

Michezo ya watoto/chekechea
Hii ni michezo ambayo huigizwa na watoto katika shughuli zao za kila siku. Watoto huigiza
mambo wanayoyaona katika mazingira yao kama vile upishi, ukulima, sherehe za kijamii,
kama vile arusi, shughuli za kiuchumi kama vile biashara na kilimo.

Sifa za michezo ya watoto


(a) Huigizwa na watoto.
(b) Michezo ya watoto hutofautiana kulingana na jamii walimokulia. Kila jamii ina michezo
mahususi inayooana na shughuli za jamii hiyo.
(c) Maudhui ya michezo ya watoto hufungamana na shughuli za kitamaduni, siasa na
uchumi katika jamii zao, kama vile upishi, arusi, matanga au ususi.
(d) Michezo ya watoto inaweza kuhusisha pia nyimbo za watoto.
(e) Michezo ya watoto huwa na miondoko mingi kama vile mchezo wa mwajificho (kibe)
kuruka kamba inayozungushwa na kuigiza.

Umuhimu wa michezo ya watoto


Michezo ya watoto huwa na majukumu yafuatayo:
(a) Kukuza kipawa cha uigizaji miongoni mwa watoto.
(b) Kukuza ubunifu. Watoto hutazama yanayoendelea katika jamii zao na kuyabunia
michezo. Kadiri wanavyoendelea kuigiza ndivyo wanavyoimarisha vipawa vyao vya
kubuni.
(c) Ninyenzo za kukashifu matendo hasi ya watu wazima. Watoto huweza kuigiza michezo
ya kulalamikia unyanyasaji wa watoto na wazazi au walezi wao.
(d) Hutambulisha na kusawiri falsafa ya jamii kuhusu malezi na majukumu ya wanajamii.
Katika mchezo wa Baba na Mama, kwa mfano, nafasi ya mume na mke katika jamii
hiyo hudhihirishwa. Watoto hujifahamisha majukumu yao pindi wawapo watu wazima.
Mtoto wa kike ataingia kuchota maji, kupika na kutafuta kuni na wa kiume kujenga
nyumba, kulima au kuwinda.
(e) Huwapa watoto ukakamavu na kuwawezesha kujiatfrini wakiwa wangali wachanga.
(f) Hukuza utangamano. Watoto hucheza pamoja bila kujali tofauti zao za kitabaka, hivyo
basi, kujifunza mapema kuwakubali wenzao.
(g) Huimarisha uwezo wa kukumbuka. Watoto hukumbuka matendo na maneno
waliyoyasikia watu wazima wakisema na kuyaigiza.
(h) Huwawezesha kupata mikakati au maarifa ya kukabiliana na hali mbalimbali katika
maisha. Kwa kucheza mchezo wa mwajificho (kibe), watoto hujihami na mikakati ya
kumtafuta aliyejificha au kujificha wasionekane.
(i) Huburudisha. Watoto hujiburudisha kwa kuigiza michezo yao.

Ngonjera
Kama tulivyotaja, ngonjera ni mashairi ambayo hukaririwa, huimbwa au kughanwa kwa
njia ya kujibizana. Ili majibizano hayo yawe sehemu ya maigizo, ni lazima yaambatane na
vitendo au utendaji.
Ngonjera isiyoambatana na maigizo/ishara za mikono na uso haiwi maigizo, huwa shairi
simulizi tu.
(Rejelea sehemu ya Ushairi Simulizi kwa maelezo zaidi na mfano wa ngonjera uk. 121.)
Ngoma
Katika fasihi simulizi, neno ngoma linaweza kuwa na maana kadha. Kwanza, ni chombo
cha muziki. Pili, ni sherehe kama vile jando au harusi, na tatu ngoma ni uchezeshaji wa
viungo vya mwili kuambatana na mdundo au mwondoko maalumu. Maelezo tunayonuia
hapa ni ya maana ya tatu ya ngoma.
Ngoma hutofautiana kulingana na jamii zilimozaliwa. Kila jamii ina ngoma yake mahususi.
Kwa mfano, jamii ya Wabukusu wana Isukuti; Wakamba, Wathi na Kilumi ilhali Waswahili
wana Chakacha.
Ngoma huweza kuchezwa ikiandamana . wa
na sherehe maalumu au ikachezwa bila WA UU
kufungwa katika sherehe yoyote kwa 3 iz.uu
LI AA AUA
NAI
nia ya kustarehesha na kufurahisha.
Aina hii ya ngoma huchezwa popote ili
kuburudisha watu. Ngoma hutofautiana
kulingana na dhamira ya ngoma na
wachezaji wake. Kuna ngoma za harusi,
za kufukuza mapepo, za kuaga mwaka,
na za unyago na jando. Kwa kufuatia
mkabala wa wachezaji, kuna ngoma
za wanawake, ngoma za vijana na pia
ngoma za wazee.

Sifa za ngoma
(a) Ngoma huandamana na muziki au ala za muziki kama vile ngoma. Aidha, wachezaji
ngoma huvaa maleba maalumu. Mara nyingi, maleba huteuliwa kulingana na mafunzo
yanayonuiwa kupitishwa pamoja na kaulimbiu ya kikundi chenyewe.
(b) Ngoma kwa kawaida huchezewa mahali wazi, kwenye kumbi za kuigizia michezo au
mahali popote palipo na nafasi ya kutosha kuchezewa.
(c) Katika ngoma, kuna wahusika wa aina mbili: watendaji (wachezaji) na watazamaji
(hadhira). Ili sanaa ya ngoma ikamilike, makundi haya mawili yanastahiki yawepo
kwa wakati mmoja.

Dhima ya ngoma
(a) Kuburudisha. Watu hutazama ufundi wa uchezeshaji viungo kufuatia midundo ya
ngoma inayoandamana nao kwa nia ya kujiburudisha.
(b) Ni kitambulisho cha jamii. Kila jamii huwa na aina zake za ngoma.
(c) Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii husika. Kila aina ya ngoma hufumbata
desturi za jamii hiyo. Kwa kuzipitisha ngoma hizi kutoka kizazi kimoja hadi kingine,
jamii hudumisha utamaduni wake.
(d) Huleta utangamano katika jamii. Watu wanapojumuika kucheza ngoma, hujihisi kitu
kimoja na urafiki au udugu hujengeka.
(e) Huelimisha. Kupitia kwa nyimbo zinazoandamana na ngoma, jamii huweza kupitisha
mafunzo au maarifa maishani. Maudhui katika nyimbo hizi ni mapana na hulenga
kuadilisha pamoja na kuburudisha.
(f£) Hukuza ubunifu. Uchezaji ngoma ni ufundi unaohitaji kuchezwa kwa mtindo wake
kulingana na mdundo wa muziki. Wachezaji hubuni mbinu za kucheza ngoma upya.
Pia mashindano mbalimbali ya uchezaji wa ngoma hizi huimarisha zaidi vipawa vya
ubunifu. y
(g) Hukuza uzalendo. Ngoma za kitamaduni huwafanya wanajamii kuionea fahari jamii
yao, hivyo uzalendo kujengeka.

Miviga
Miviga ni sherehe za kitamaduni ambazo hufanywa na jamii yoyote katika kipindi maalumu
cha mwaka. Mara nyingi, miviga kama vile jando hufanywa katika kipindi baada ya mavuno.
Miviga ya mazishi, kwa mfano, hufanywa kabla ya wakati fulani wa siku kutegemea imani
ya jamii. Aidha, miviga ya kuwapa watoto majina huathimishwa muda fulani baada ya
mtoto kuzaliwa.
Sanaa ya maigizo katika baadhi ya miviga hujitokeza pale mwanajamii anapoingizwa katika
kundi fulani kutoka kundi jingine. Uhamishwaji huu huandamana na majukumu mapya
pamoja na madaraka. Kwa mfano:
(i) Kutoka katika kundi la watoto kuingia kundi la watu wazima (jando au unyago).
(ii) Kutoka kundi la makapera kuingia kundi la waliooa (arusi).
(iii) Kutoka kwa uraia kuingia jeshi (askari).
(iv) Kutoka kwa uraia kuingia kwa utawala (kutawazwa kuwa kiongozi).
(v) Kutoka uhai kuingia ufu (mazishi).
Aghalabu miviga huwa na hatua tatu:
(i) Kumtoa mtu rasmi kutoka kundi moja la wanajamii.
(ii) Kumfundisha majukumu yanayohusiana na wadhifa mpya.
iii) Kumwingiza rasmi katika kundi jingine.

Hatua hizi huandamana na uigizaji. Kule kukabidhiwa madaraka au majukumu mapya


huwekwa katika umbo la vitendo vilivyopakwa uzuri wa kisanaa ili kumzoesha mwenye
madaraka mapya majukumu yake kwa urahisi.
Sifa za miviga
(a) Miviga huandamana na matendo au kanuni fulani (viviga). Hufuata utaratibu maalumu
na huwa na sababu maalumu.
“(b) Miviga huandamana na matendo fulani. Katika matambiko, kwa mfano, kuna kunuiza
maneno. Katika ibada, kuna kusimama na kupiga magoti wakati wa sala. Katika sherehe
za ndoa na sherehe za kutawazwa kwa viongozi, kuna ulaji viapo.
(9) Miviga huongozwa na watu mahususi ambao huendeleza shughuli za miviga. Kuna
wale ambao huendesha ibada za ndoa na wengine kutoa kafara.
(d) Miviga huandamana na utoaji mawaidha. Mawaidha haya hutolewa kwa njia nyingi
kama vile kwa hotuba, kwa nyimbo au kwa maigizo.
(e) Maleba maalumu huvaliwa na wanaohusika ili kuwatofautisha na hadhira. Katika
jamii nyingi, bwana na bibi harusi huvaa mavazi maalumu. Aidha, viongozi wa kidini
huvaa mavazi maalumu. Askari wanaojiunga na kikosi fulani pia huvaa maleba yao.
(f) Shughuli za miviga aghalabu hufanyiwa mahali sherehe hiyo inapofanyiwa. Katika
baadhi ya jamii, sherehe za jando hufanyiwa maporini. Matambiko pia hufanyiwa
porini, kwenye madhabahu, milimani au mapangoni. Shughuli za kufukuza mashetani
huweza kufanywa mibuyuni.
(8) Miviga huambatana na utamaduni wa jamii husika. Huandamana na uimbaji, uchezaji
ngoma, mawaidha, ulumbi na ughanaji wa mashairi kitamaduni. Vivugo (majigambo)
huweza kuwasilishwa katika miviga kama vile jandoni ili kuwahimiza vijana kuwa
jasiri na kutoa mchango wao kuiendeleza jamii.

Dhima ya miviga
(a) Huelimisha wanajamii. Wakati wa jando, vijana huelimishwa kuhusu mambo
yanayohusu utu uzima na mikakati ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za
maisha.
(b) Huonyesha matarajio ya jamii kwa vijana/wanajamii. Katika mafundisho yanayotolewa
katika miviga, matarajio ya jamii hubainika. Kupitia kwa sherehe za harusi, matarajio
ya jamii kuhusu wake/waume hupitishwa.
(c) Ni kitambulisho cha jamii. Kila jamii huwa na miviga yake mahususi. Sherehe za
mazishi ama za kumpa mtoto jina huendeshwa kwa namna fulani na jamii fulani. Pia
huonyesha mpangilio wa jamii husika.
(d) Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii. Miviga hupitishwa kutoka kizazi kimoja
hadi kingine ili kuhifadhi utamaduni.
(e) Hukuza uzalendo. Huwahimiza wanajamii kuzionea fahari tamaduni za jamii yao.
Vijana wanapojumuika pamoja katika miviga kama vile sherehe za jando hujitambulisha
na jamii yao na uzalendo huimarika.

(ai)
(f£) Huhimiza na kukuza umoja miongoni mwa wanajamii wanapojumuika pamoja katika
sherehe kama vile harusi, matambiko ama mazishi.

(g) Miviga huwasaidia wanajamii kukabiliana na hali ngumu katika maisha kama vile
kufiwa.

(h) Ni njia ya kupitisha maadili na thamani za jamii kwa vijana. Hufunza umuhimu wa
kazi, suala la unyumba, uzazi na malezi kwa jumla.
(i) Ni mizani/kigezo cha kuonyesha kuvuka kutoka daraja moja la maisha hadi jingine.
Mathalani kupitia sherehe za jando, wavulana huhisi kuwa wakati umewadia wa kuacha
utoto na kuingia katika utu uzima. Harusi pia ni kivuko cha kutoka useja/ujane na
kuingia katika maisha ya ndoa.
(Jj) Huonyesha imani za kidini za jamii. Kila jamii ina imani zake za kidini na viviga
vinavyoambatana nazo. Kupitia kwa miviga, tabia zinazohusishwa na imani zao
huonekana. ;

Hasara za miviga
(a) Baadhi ya miviga kama vile kutiwa unyagoni kwa wasichana na kurithi mke wa mtu
aliyeaga zimepitwa na wakati. Huhatarisha maisha na afya ya wanajamii.
(b) Baadhi ya miviga hukinza malengo ya kitaifa. Kwa mfano, kutia unyagoni kwa lazima
na ukeketwaji wa watoto wa kike ni ukiukaji wa haki za binadamu.
(c) Hujaza watu hofu. Kwa mfano, miviga inayohitaji kafara ya binadamu katika baadhi
ya jamii huogofya. Aidha, sherehe za kufukuza pepo huhofisha.
(d) Baadhi ya miviga huhusisha ushirikina. Mazishi katika jamii nyingine huandamana
na ushirikina ambao huweza kusababisha uhasama baina ya koo.
(e) Baadhi ya sherehe za miviga hugharimu kiasi kikubwa cha pesa/mali na kuiacha familia
katika hali duni kiuchumi. Sherehe za kuomboleza katika jamii nyingine huandamana
na matumizi ya fedha nyingi.

Matambiko
Tambiko ni sadaka au ada inayotolewa kwa Mwenyezi Mungu, miungu, pepo au mizimu
moja kwa moja au kwa Mungu kupitia kwa miungu. Yapo matambiko yalitolewa na wazee
maarufu waliopewa jukumu hilo. Matatizo yaliyoshinda mababu zetu yalipelekwa kwa
miungu ili iwasaidie kuyatatua. Baadhi ya matatizo haya yalikuwa magonjwa, ukame, kukosa
kupata watoto au mafuriko. Wakati mwingine, matambiko yalifanywa kutoa shukrani au
kuomba radhi. Iliaminiwa kuwa baadhi ya matatizo yalisababishwa na hasira za miungu.
Ili kuomba radhi, matatizo haya yalipelekwa kwa miungu mbalimbali kutegemea tatizo
lenyewe, mathalani, kwa mungu wa jua, wa mvua au wa milima.
Aghalabu matambiko yaliambatana na kafara ambazo zilibadilika kutegemea jamii na tatizo
lilitolewa kafara. Kwa hivi leo, matambiko yanaendelea kufa.
Sifa za matambiko

(a) Matambiko ni sanaa inayotendeka.


(b) Matambiko hayatolewi na mtu yeyote bali hutolewa na wazee maarufu walioteuliwa.
(c) Matambiko hufanyika mahali maalumu kama vile chini ya miti mikubwa, makaburini
au porini kutegemea jamii husika.
(d) Matambiko yaliandamana na sala na ni utanzu wa maigizo unaoendelea kufa.
Ngomezi
Ngomezi ni sanaa ya ngoma. Ni aina ya fasihi ambayo
huwasilishwa kwa kutumia milio ya ngoma badala ya midomo.
Ngomezi huingizwa katika kundi la fasihi simulizi kwa sababu
mapigo na ishara za ngoma huwakilisha ujumbe fulani. Kila
mpigo wa ngoma huwa na fasiri/maana mahususi ambayo
inajulikana na jamii husika. Kwa mfano, mapigo matatu
ya ngoma au debe katika jamii fulani huweza kumaanisha
amezaliwa mtoto. Katika jamii za Kiafrika, ngomezi ilitumiwa
kuwasilisha aina mbalimbali za jumbe kama vile vita, ujumbe
wa dharura kutoka kwa watemi, kuzaliwa kwa mtoto, kutokea
kwa janga kama moto, uvamizi, msiba au kifo, au arusi.

Sifa za ngomezi
(a) Kila mdundo wa ngoma huwakilisha kauli mahususi kwa lugha ya jamii ambamo
ngomezi imezuka.
(b) Ngomezi hutegemea mapigo, wizani na upatano unaotokana na ngoma inayopigwa
kuwasilisha ujumbe. j
(c) Fasiri (maana) hujikita na kutokana na jamii husika. Jamii ndiyo huyapa mapigo ya
ngoma maana yake. Maana ya mapigo hayo basi hueleweka tu na wanajamii walioubuni
mpigo huo wa ngoma.
(d) Kila mpigo wa ngoma hufuata mtindo wa kishairi. Kila mpigo huwakilisha silabi au
mizani katika lugha tamkwa. Hii ndiyo sababu lugha ya ngomezi ikachukuliwa kuwa
lugha ya kishairi. Katika jamii ya kisasa, matumizi ya ngomezi huweza kupatikana
kupitia:
(i) kengele zinazotumiwa kupigia hodi kwenye majumba.
(ii) kamsa/milio kwenye magari kama ambulensi. Magari ya kawaida pia hutiwa vifaa
ambavyo hutoa milio pindi magari hayo yakiguswa.
iii) toni katika rununu huwakilisha aina mbalimbali za taarifa/ujumbe.

Oo
Majukumu ya ngomezi
Ngomezi ina majukumu yafuatayo:
(a) Ninyenzo ya kupitisha ujumbe wa dharura kuhusu matukio ya dharura kama vile vita.
Hutumiwa kutoa matangazo rasmi.
(b) Nikitambulisho cha jamii. Huonyesha ufundi wa jamii wa kutumia vyombo vya muziki.
Kila jamii huwa na ngomezi zake mahususi. Ujumbe wa kuzaliwa kwa mtoto huweza
kupitishwa kwa mapigo tofauti tofauti ya ngoma kutegemea na jamii.
(c) Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii kutoka kizazi hadi kingine.
(d) Ninyenzo ya kukuza uzalendo. Wanajamii hufunzwa kuionea fahari mbinu hii yao ya
kuwasiliana.
(e) Hukuza ubunifu. Jinsi wanajamii wanavyokabiliwa na aina tofauti tofauti za ujumbe
ndivyo wanavyojifunza/wanavyobuni mitindo mipya ya kuwasilisha ujumbe kwa
ngoma, hivyo kuimarisha ubunifu.
(f) Ni njia rahisi ya kuwasilisha ujumbe bila kutegemea sauti ya mtu.
Hata hivyo, ngomezi huweza kutatiza hasa pale wanajamii wanaposhindwa kufasiri ujumbe
au wanapofasiri ujumbe visivyo.

. Andika mifano mitano ya maigizo katika jamii yako.


Eleza tofauti kati ya ngoma na ngomezi.
3. Jadili dhima ya vipera vifuatavyo vya maigizo katika jamii yako:
(a) Vichekesho
(b) Miviga
(c) Michezo ya kuigiza
“Maigizo hayapaswi kuainishwa kama utanzu unaojitegemea. Jadili.
“Maudhui na fani ya maigizo hutegemea mwigizaji. Thibitisha.
6. “Majigambo yanaweza kuainishwa kama utanzu wa sanaa ya maonyesho.”
Thibitisha.
7

Utanzu wa Mazungumzo

Utangulizi
Mazungumzo ni maelezo ya mdomo kwa lugha ya kawaida kuhusu suala lolote. Mazungumzo
huwa fasihi pale ambapo yanadhihirisha usanii wa aina fulani; pale ambapo yanaeleza
ukweli kwa namna ambavyo hayaunukuu tu moja kwa moja, bali yanaueleza kwa ubunifu.
Katika kuzungumzia tukio la kawaida, mtu anaweza kuifinyanga lugha kwa ufasaha na kwa
njia isiyo ya kawaida. Mazungumzo ya aina hii huwekwa katika kundi la fasihi simulizi.
Mazungumzo yanayotokea katika miktadha rasmi hutengewa vikao maalumu. Pia, kuna
mazungumzo yasiyo rasmi. Katika jamii za Kiafrika, mazungumzo rasmi hupatikana katika
miktadha mingi kama vile:
(i) kwenye sherehe za jandoni (mawaidha)
(ii) kwenye harusi (hotuba na mawaidha)
(iii) maabadini (mahubiri na sala)
(iv) kwenye mazishi (hotuba na taabili/taabini)
(v) mikutano ya kisiasa (hotuba)
(vi) shughuli za posa (hotuba)
(vii) kortini (ulumbi).
Mazungumzo pia hupatikana katika vipera vingine vya fasihi simulizi kama vile utegaji na
uteguaji wa vitendawili, maigizo na hata utambaji hadithi.

Vipera vya mazungumzo


Mazungumzo ya kifasihi yanaweza kuainishwa katika vipera vya: malumbano ya utani,
ulumbi, hotuba, mawaidha, soga na maapizo.

Malumbano ya utani
Malumbano ya utani ni majibizano kati ya watu wawili au makundi mawili ya watu kwa
nia ya kutaniana. Ni mazungumzo yanayofanywa kwa kutumia maneno ya mzaha ili kuleta
ucheshi. Watu hutaniana kwa kutumia lugha kwa ufundi na mtiririko maalumu. Kuna aina
mbalimbali za utani: ;

Cs)
(i) Utani wa mababu/mabibi na wajukuu
(ii) Utani wa marafiki
(iii) Utani wa koo, makabila au mbari
(iv) Utani wa mawifi na mashemeji
(v) Utani wa marika
(vi) Utani wa maumbu.

Sifa za malumbano ya utani


(a) Malumbano ya utani hufanywa na watu wawili au makundi mawili ya watu
wanapokutana. Hata hivyo, kila utani una misingi na mipaka yake.
(b) Watu wenye uhusiano mzuri ndio hutaniana.
(c) Watani hufanyiana mizaha ambayo inadhibitiwa na masharti yanayotawala uhusiano
wao. Baadhi ya makabila hutaniana hata kwenye mazishi.
(d) Malumbano ya utani huweza kuwa kati ya makabila, marafiki, wajukuu na mababu,
wajukuu na mabibi, maumbu, bwana na bibi arusi na hata mataifa.
(e) Katika malumbano ya utani, mbinu ya chuku hutumiwa kwa ufanifu sikuliya Mbinu
hii hunuiwa kusisitiza sifa fulani au kukejeli sifa fulani hasi. Malumbano ya utani
yanaweza hata kuwa na masimango. Mtani humdhihaki mwenzake kwa kumkumbusha
wema aliomtendea.
(f) Huchukua njia ya ushindani, kila mmoja akijaribu kumpiku mwenzake.
(8) Wakati mwingine, watu hutania wasiokuwepo. Utani wa aina hii huandamana na
uigizaji wa kuchekesha.
(h) Wakati mwingine malumbano ya utani yanaweza kuhusisha uigizaji. Hii ndiyo sababu
baadhi ya wataalamu wakakitia kipera hiki katika utanzu wa maigizo.

Umuhimu wa malumbano ya utani


(a) Malumbano hupunguza urasmi miongoni mwa wanajamii, hivyo kuhimiza kujieleza
kwa uwazi/bila kuficha.
(b) Huimarisha urafiki. Ni watu walio na uhusiano mwema tu ndio wanaoweza kutaniana.
(c) Hukuza utangamano miongoni mwa watu na makabila mbalimbali hasa yanapokuja
pamoja kutaniana.
(d) Hutambulisha jamii kwa kutaja baadhi ya sifa zake katika utani. Kwa mfano, miongoni
mwa Wakamba, ukoo wa 'Kitondo' unataniwa kuwa ni wachoyo kiasi cha kubania
chakula kilichooza.

(e) Hukosoa na kukashifu tabia hasi. Baadhi ya malumbano ya utani hudhihaki ulafi,
uchoyo, wivu na tabia nyingine mbaya.
(f£) Huburudisha. Ucheshi katika malumbano ya utani huburudisha na kuchangamsha.
(g) Huelimisha. Kupitia kwa malumbano ya utani, watu hupana maarifa ya kukabiliana
na hali mbalimbali katika maisha.

Mifano ya malumbano ya utani |

(i) Utani wa kikabila: Wakamba, ukoo wa Akanga hutaniwa kuwa


wanapenda nyama kiasi cha kula kijusi cha mbuzi!
(ii) Wakikuyu hutaniwa kuwa wanapenda pesa sana kiasi kwamba maiti
ikisikia mlio wa sarafu inaweza kufufuka.
(iii) Utani wa kijamii: Babu humtania mjukuu wa kike kwa kumwita mke
wake ilhali bibi/nyanya humtania mjukuu wa kiume kuwa ni mume
wake.
(iv) Utani katika mazishi (katika baadhi ya jamii): Afadhali umekufa
tukakuzika, sasa maghala yetu yatasalimika.
(v) Utani wa vijana (kugowana/mchongoano): Wewe ni 'mshamba' kiasi
kwamba ukiona picha yako kwenye kioo unasema ni pacha wako.

Ulumbi
Huu ni uhodari wa kutumia lugha kwa ufundi wa kipekee. Ni utumiaji wa lugha kwa mvuto
na ufasaha. Ulumbi humwezesha mtu kulielezea jambo la kawaida kwa namna ambavyo
linaonekana kuwa geni kabisa na kuwashawishi watu kulikubali au kulipenda. Kuna aina
mbili za ulumbi: rasmi na usio rasmi.
Ulumbi rasmi huweza kupatikana katika miktadha mbalimbali kama vile:
(i) kortini, ambapo mawakili hutoa hoja zao kutetea wanaowawakilisha.
(ii) kanisani/msikitini wakati wahubiri wanapotoa sala/mahubiri.
(iii) mijadala ya kisiasa ambapo wanasiasa wenye vipawa vya ulumbi huvitumia
kuwapiku wanasiasa wenzao na kuwashawishi raia kuwapigia kura.

(iv) katika sherehe za harusi au mazishi, kwa mfano, katika kutoa taabini/taabili
(hotuba kumhusu marehemu).
(v) katika kuapiza na katika kufukuza pepo.
(vi) katika utoaji wa risala. j
(vii) ulumbi usio rasmi hupatikana ambapo watu hutumia lugha kwa ufasaha hata katika
kuapiza/kulaani au hata katika mazungumzo ya kupitisha muda na marafiki. |

Sifa za ulumbi
(a) Ulumbi ni usemaji au uzungumzaji wa kifasihi. Mlumbi hutumia lugha kwa njia
inayovutia na kushawishi hadhira yake. |
(b) Ulumbi hubainika katika miktadha ya kutoa hotuba au katika hali ambapo mtu
anahitajika kutetea msimamo wake katika vikao, au hata katika mijadala rasmi.
(c) Hukuza ukakamavu wa kuzungumza hadharani. Mlumbi hupenda kuzungumza na
hupenda kujisikia akizungumza mbele ya watu.
(d) Hutumia vipengele anuwai vya lugha kama vile sitiari, maswali ya balagha, methali,
nahau, taswira na viziada-lugha kama vile toni, kiimbo na kidatu ili kuishawishi hadhira
au kutilia mkazo wazo fulani na kutetea misimamo yao. Hutumia lugha kutegemea
muktadha na hadhira yake.
Ce) Katika baadhi ya jamii, walumbi walitumiwa kuzungumza kwa niaba ya viongozi kama
vile machifu, wanaoomba posa au kwa niaba ya ukoo au mwanajamii aliyedhulumiwa.
Walumbi wengi aghalabu huwa na vipawa vya uongozi na huinukia kuwa viongozi wa
jamii zao.
(£) Utoaji hotuba kwa umbuji ni jambo ambalo limetambuliwa katika jamii nyingi. Ulumbi
husisitizwa sana katika matabaka ya juu kama kitambulisho cha tabaka hilo. Katika
baadhi ya jamii, watu katika tabaka tawala walifunzwa kutumia msamiati wenye
haiba, matumizi ya ishara, toni na sauti zifaazo. Hili lilinuiwa kuimarisha stadi za
ulumbi. Hata katika jamii ya kisasa, viongozi hufunzwa naa kufanyizwa mazoezi ya
kutoa hotuba kwa ufasaha (ulumbi).
(g) Walumbi hutumia chuku kwa ufanifu mkubwa. Hata hivyo, lazima wadumishe adabu.
(h) Ulumbi huweza kuwa na urudiaji mwingi wa maneno, virai na vishazi ili kusisitiza.
Katika sala, kwa mfano, unaweza kupata matumizi ya takriri na usambamba
yanayonuiwa kuvuta usikivu wa Mungu/miungu au kusisitiza jambo fulani.

Mfano wa ulumbi wa kisala

Ewe baba yetu uishie juu mbinguni


Mungu mwenye enzi
Mungu wa Burahimu na Isaka
Baba mwenye rehema
Baba usio kifani
Ewe muumba wa vyote
Ewe mneemesha wa wote
Baba wa mayatima
Mume wa wajane...

Kifungu hiki kinarejelea wazo moja tu; mlumbi anaitetea dua — anatambua uwezo wa Mungu.

Umuhimu wa ulumbi

(a) Hukuza uwezo wa kujieleza hadharani. Kadiri mtu anavyozungumza hadharani ndivyo
anavyojiboresha kama mlumbi.
Ni nyenzo ya kukuza ujuzi na ufasaha wa lugha. Jinsi mtu anavyoitumia lugha kwa
umbuji ndivyo anavyokuza umilisi wake na umahiri wake wa kuisarifu lugha.
Ni msingi wa kuteua viongozi. Uwezo wa mtu kuwashawishi wanajamii kukubaliana
na mtazamo wake humfanya kutambuliwa kama mwenye uwezo wa kuongoza jamii.
Walumbi wana uwezo mkubwa wa kuishawishi hadhira.
Huhifadhi utamaduni wa jamii. Ulumbi ni sanaa jadiiya, yaani imekuwepo katika jamii
kwa muda mrefu ikipokezwa vizazi na vizazi.
Ni nyenzo ya kuburudisha wanajamii na kuwaelimisha bila kuwachosha. Walumbi
huweza kupitisha maarifa mbalimbali kwa wanajamii kwa njia yenye mvuto.
Hukuza uzalendo. Vijana wanapowasikiliza walumbi wakitongoa lugha, huionea fahari
lugha yao na kujitambulisha zaidi na jamii zao.
Huweza kutumiwa kuwasilisha ujumbe muhimu au ulio na athari kubwa au ambao
una makali na usio rahisi kueleza.
Ni kitambulisho cha utabaka. Katika baadhi ya jamii, ulumbi ulihusishwa zaidi na
tabaka tawala au watu wenye vyeo vya juu na haiba/heshima katika jamii zao. Katika
jamii hizi, ulumbi ni kigezo cha kuainisha matabaka.
(i) Ulumbi ni msingi wa kuheshimiwa katika jamii. Walumbi huheshimiwa kwa sababu ya
matumizi yao ya lugha yenye ujumi na umbuji katika kuyafafanua masuala ya kijamii.

Mfanowaulumbiusiorasmi

“La, hasha kimwana! Hatukukaidi wala si upepo, mabinti, ila ni wawindaji, lakini si wa
wanyama. Naomba kuyafasiri niliyoyagomba. Kwa ruhusa nitasema hivi; kwamba thawabu
ya mja ni sawasawa na jitihada na suna zake. Siku nyingi tumewinda. Na silalamiki kwa
kuwa adinasi, kiada huwinda mengi katika sayari hii kwa kadiri ya haja na hekima yake.
Hana budi, hata hivyo, kuutumia ubongo wake kwa nafasi sawasawa na namna ambavyo
Jalia alivyomkirimu. Naam, kwa maana wenye hekima hunaswa kwenye hila zao. Kwa
kuwa mpaka wa hadaa na yakini u katika ridhaa ya mwanadamu aliyejawa choyo, husuda,
hitilafu na mpungufu wa karama. Nawaomba kwa hivyo warembo mmakinike, pasiwe kwenu
faraka. Bali mhitimu katika nia moja na ushauri mmoja katika ombi letu. Naitwa Dzombo...
(Kutoka: Kipendacho Roho, Pauline Kyovi, OUP, uk. 10.)

Jibu maswali yafuatayo kwa kurejelea utungo uliosoma.


1. Eleza sifa za ulumbi zinazojitokeza katika utungo huu.
2. Fafanua tofauti kati ya ulumbi na malumbano ya utani.
3. Toa mfano wa ulumbi usio rasmi.
4. Andika mfano wa malumbano ya utani kati ya:
(a) marika (b) mke na mume.
- Taja manufaa matatu matatu ya:
(a) ulumbi (b) malumbano ya utani.
Hotuba
Hotuba ni maelezo au taarifa ambayo hutolewa mbele ya hadhira kuhusu mada fulani,
Kwa kawaida, hotuba ni mazungumzo rasmi na hutolewa katika vikao rasmi kama vile:
(a) hafla za kisiasa (Hotuba za wanasiasa).

(b) kanisani/msikitini (Mahubiri).

(c) sherehe za kitamaduni kama vile vikao vya posa.


(d) kortini (Kabla jaji hajatoa hukumu, anaweza kutanguliza hotuba).
(e) kwenye mazishi (Taabili/taabini na risala za rambirambi).

(f) katika harusi. Mawaidha yanayotolewa kwa maarusi huchukua muundo wa hotuba.
(g) katika tamasha za muziki na ukariri wa mashairi au mashindano ya utoaji hotuba.

Sifa za hotuba

(a) Kwa kawaida, hotuba hutolewa na watu maalumu au walioteuliwa kuzungumza kama
vile viongozi au wawakilishi wao na watu wengine wenye hadhi katika jamii. Hata
hivyo, baadhi ya hotuba hutolewa katika miktadha isiyo rasmi. Katika makazi ya watu,
hotuba za waadhi/mawaidha/nasaha huweza kutolewa wakati wa chajio au baada ya
chajio.

(b) Watu wanaoteuliwa kutoa hotuba aghalabu huwa na umilisi mkubwa wa lugha.
Walumbi ni watoaji hotuba stadi. Siku hizi, viongozi pia hufunzwa stadi za kutoa
hotuba za hadharani.
(c) Hotuba hutolewa kwa nafsi ya kwanza.

(d) Mtoaji hotuba anaweza kutumia viziada-lugha kama vile ishara za uso na mikono ama
miondoko ili kufanya hotuba ivutie hadhira. Maswali ya balagha pia hutumika.
(e) Hotuba huteuliwa mada mahususi wala haizungumzii jambo lolote lile.

Umuhimu wa hotuba

(a) Huadilisha na kuasa. Hotuba zinazotolewa jandoni au katika harusi kwa kawaida
hunuiwa kutoa nasaha.

(b) Huelimisha. Hotuba za jandoni, kwa mfano, huwapa vijana maarifa ya kukabiliana na
maisha.

(c) Huimarisha ukakamavu wa kuzungumza hadharani. Kadiri watu wanavyotoa hotuba


ndivyo wanavyoimarisha umilisi wao wa lugha na ujasiri wa kuzungumza hadharani.
Aa

(d) Hukuza ufasaha na umilisi wa lugha.


(e) Hupalilia kipawa cha uongozi. Kwa kawaida, mahatibu huteuliwa. Kadiri mtu
anavyolichukua jukumu la kuhutubu katika hafla mbalimbali ndivyo anavyojitayarisha
kuchukua nyadhifa kubwa zaidi za uongozi.

Mawaidha
Haya ni mazungumzo ambayo hutolewa ili kumpa mtu ushauri au nasaha kuhusu jambo
fulani. Mawaidha hutoa mwongozo na maelekezo ya kukabiliana na changamoto katika
maisha na jinsi ya kuhusiana na wanajamii.

Sifa za mawaidha

(a) Mawaidha hutolewa katika miktadha rasmi kama vile jandoni, katika harusi, kwenye
mazishi, darasani na kanisani. Hata hivyo, mawaidha yanaweza kutolewa katika
miktadha isiyo rasmi. Mzazi anaweza kumpa mwanawe mawaidha nyumbani wakati
wa chajio.
(b) Katika jamii nyingi, wazee na watu walio na vyeo vikubwa na waliochukuliwa kuwa
na hekima ndio waliopewa jukumu la kuwatolea vijana mawaidha. Hata hivyo, vijana
pia wanaweza kutoa mawaidha kwa vijana wenzao ambao wanahitaji ushauri au hata
vijana wakatoa mawaidha kwa wazee.
(c) Mwenye kutoa mawaidha hulielewa jambo analousia kwa undani. Sharti awe na ujuzi
wa kutosha katika mada anayozungumzia.
(d) Mwenye kutoa mawaidha hutumia lugha inayoathiri hisia za wanaousiwa. Inaweza
kuwa na tamathali za usemi kama vile methali.
(e) Mawaidha huingiliana na vipera vingine vya fasihi simulizi. Kwa mfano, methali
hufumbata mawaidha. Pia, utambaji ngano, miviga kama vile jando na harusi,
huandamana na utoaji wa mawaidha. Aidha, yapo mashairi ya waadhi (nasaha/
mawaidha). Hali kadhalika, anayetoa mawaidha anaweza kutumia mbazi (ngano za
kimafumbo) ili kusisitiza ushauri anaotoa.

(f) Maudhui katika mawaidha ni mapana. Huweza kugusia masuala kama vile dini,
uongozi, ujasiri, amali, elimu na taaluma, unyumba, mahusiano ya kijamii, malezi na
afya.
(g) Mawaidha yanayotolewa katika miktadha rasmi huwa na muundo maalumu wenye
sehemu tatu kuu: :

(i) Utangulizi
Katika sehemu hii, anayetoa mawaidha huanza kwa kauli ya kuvuta makini ya hadhira.
Anaweza kuanza kwa kutoa kiini cha mawaidha, kwa mfano, 'Utu uzima huenda na
uwajibikaji ...”
(ii) Mwili

za usemi kama vile methali. Wasia, maonyo na maelekezo hutolewa kutegemea lengo.
(iii) Hitimisho
Mwasilishaji huonyesha msimamo wake kuhusiana na suala analousia. Kwa kawaida,
anayetoa mawaidha huishirikisha hadhira kwa kutaka kujua msimamo au maoni yao
kuhusu suala alilowausia. Hadhira inaweza kutaja changamoto zinazohusiana na
mawaidha yanayotolewa.

Majukumu ya mawaidha
(a) Jukumu la kimsingi la mawaidha ni kuelekeza. Mawaidha hutoa mwongozo wa jinsi
ya kukabiliana na matatizo au jinsi ya kutenda jambo fulani.
(b) Huelimisha. Mawaidha huwapa wanajamii maarifa ya kuendeshea maisha. Huwajuza
wanajamii kuhusu majukumu yao ya kijamii na matarajio ya jamii zao kwao.
Mawaidha yanayotolewa kwa maarusi, kwa mfano, huwajuza wanaohusika kuhusu
yale wanayowajibika kutenda kwa mke au mume na kwa jamii kwa jumla.
(c) Huadilisha. Wanaopewa mawaidha hujifunza maadili kama vile usafi, unyenyekevu,
utulivu na kusamehe.
(d) Hutambulisha jamii. Kila jamii huwa na aina yake ya mawaidha kulingana na thamani
zake. Pia, mawaidha hutolewa kwa namna mbalimbali kutegemea jamii.
Mfano wa mawaidha

1. Owa sandame hadaa, moyo ukahadaiwa


Owa anaye kufaa, mke mwenye kusifiwa
Owa upate kuzaa, kama ulivyozaliwa
Owa ukijaaliwa, mupendane na mkeyo
2. Owaaliye na kheri, muandamane kwa dini
Owa yai la johari, litiye nuru nyumbani
Owa mdomo mzuri, ukupambie lisani
Owa ungiye nyumbani, mupendane na mkeyo
3. Owa moyo wa imani, usozumbua mafuja
Owa usiowe duni, anayeitwa kioja
Owa mtenda ya dini, ndiye mke mwenye haja
Owa utungiwe koja, mupendane na mkeyo
4. Owa siowe tambara, linukiyalo vibaya
Owa mwanamke jura, umfunze yenye ndiya
Owa usiowe sura, kutaka kuzangaliya
Owa mzuri tabiya, mupendane na mkeyo
10. Owa akukubaliye, akuizao siowe
Owa upendane naye, zamani sizo ujuwe
Owa akuridhiyaye, mujikubali wenyewe
Owa mukae mutuwe, mupendane na mkeyo
12. Owa utukuze cheo, najina lipate kuwa
Owa upate mkeo, aambiwe meolewa
Owa kama waowao, moyo usiliye ngowa
Owa ujuwe kukuwa, mupendane na mkeyo
(Kutoka: Malenga wa Mvita, Ahmed Nassir, OUP, uk. 158 — 159.)
UA UE

uu umumumumumumu——————————— )
1. (a) Eleza sifa za mawaidha zinazojitokeza katika utungo huu.
(b) Utungo huu au mawaidha haya yanaweza kutolewa katika muktadha au
shughuli gani katika jamii.
(c) Kwa kurejelea utungo huu, eleza mawaidha yanayotolewa kuhusiana na
ndoa.

2. (a) Taja miktadha mitano ambamo hotuba hutolewa katika jamii yako.
(b) Eleza majukumu manne ya mawaidha katika jamii yako.
3. Hotuba na mawaidha hufanana. Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano
mwafaka.

Soga
Soga ni mazungumzo yanayonuiwa kupitisha wakati. Mazungumzo haya huchukuliwa
kama fasihi yanapotolewa kwa usanii fulani yakimithilisha uhalisia badala ya kuunakili.
Katika soga, jambo la kawaida linalozungumziwa hupigwa chuku na kufanywa lionekane
kana kwamba halina uhalisia.

Soga ni utanzu wa zamani sana ingawa umeathiriwa na mabadiliko ya kisasa na kuchukua


sura mbalimbali kama vile za vibonzo na maigizo ya soga katika runinga. Soga pia huweza
kuwa hadithi fupifupi. Kwa maelezo zaidi ya soga, rejelea utanzu wa hadithi.

Maapizo
Maapizo ni maombi maalumu ya kumtaka Mungu/miungu/mizimu kumwadhibu mhusika
hasidi, mkinzani au mwovu. Hivyo, maapizo ni dua ya laana au maombi mabaya kutoka
kwa mtu ambaye anahisi ametendewa uovu au amesalitiwa na mwingine.
Sifa za maapizo
(a) Maapizo yalitolewa kwa watu ambao walienda kinyume na matarajio ya jamii zao.
Mifano ya watu hawa ni wabakaji, wezi, wauaji na waliowatusi wazazi, wazee au ukoo.
Wazazi pia huweza kutoa maapizo kwa wana wao ili kuwaonya dhidi ya hulka mbaya
kama vile utumiaji wa vileo. Huenda mzazi akasema, Nimelaani unywaji wa pombe
katika familia hii. Atakayeonja hata tone na aandamwe na ufukara usoisha!
(b) Katika baadhi ya jamii za Kiafrika, maapizo yalitolewa kabla ya ulaji viapo. Mtoaji kiapo
anaweza kusema, Ambaye amefanya tendo hili chuma hiki kimwingie kwenye mboni ya
jicho, asiuone mwangaza wa jua tena!
(c) Maapizo yanaweza kutolewa moja kwa moja na yule aliyeathirika. Mtu anapopoteza
kitu chake anaweza kuapiza ili kumtisha aliyekiiba arudishe. Kwa mfano, mtu anaweza
kusema, Aliyeiba mbuzi wangu apeperuke na huo mchanga, zizi lake lisipate kulala mbuzi
hata mmoja! Katika baadhi ya jamii, watu mahususi waliteuliwa kutoa maapizo, hasa
wakati wa ulaji kiapo. Watoaji kiapo ndio pia walioapiza.
(d) Kidini, Mungu, miungu au mizimu huweza kutoa maapizo kuhusu mustakabali wa
mhusika fulani. Aidha, maapizo ya kidini yanaweza kutolewa kama laana baada ya
mhusika kukaidi amri za Mungu au miungu. Kwa mfano, katika tamthilia ya Edipode
iliyoandikwa na Sofokile, miungu waliapiza kuwa Edipode angemuua baba yake na
kumwoa mamake mzazi. Maapizo ya aina hii huathiri, si jaala ya mhusika tu bali ya
jamii pia. Katika kisa cha Edipode, kwa mfano, waliyoapiza miungu yalitimia. Edipode
alikuja kumuua babake bila kujua (alikuwa ametoroka asimuue babake). Aidha, alimwoa
mamake bila kujua. Katika Biblia, Mungu anawalaani Adamu, Hawa na nyoka baada
ya kukaidi amri yake. Laana hii inaaminika kuwa imedumu hadi kizazi cha sasa.
(e) Maapizo huaminiwa kuwa yataleta maangamizi kwa jamii, hivyo wanajamii hushauriwa
kuyaepuka kwa kutenda mema.
(f£) Maapizo hutumia lugha fasaha (ulumbi). Watoaji maapizo katika ulaji wa viapo
aghalabu huwa walumbi.
(g) Maapizo hutumia lugha kali inayonuiwa kujaza woga ili kuonya dhidi ya maovu.

Umuhimu wa maapizo
(a) Kimsingi, maapizo hutumiwa kama nyenzo ya kuwaonya wanajamii dhidi ya matendo
hasi.
(b) Hutambulisha jamii. Kila jamii ina namna yake ya kuapiza na mitindo tofauti ya kutoa
maapizo.”
(c) Hukuza umoja katika jamii. Kuwapo kwa kaida na miiko sawa huwafanya watu kujihisi
kuwa kitu kimoja.
(d) Huadilisha. Wanajamii hujifunza kutenda mema ili kuepuka laana.
Mfano wa maapizo

Ikiwa kweli wewe ni mkazamwanangu,


Nami ndiye nilompa uhai mwana unoringia,
Anokufanya upite ukinitemea mate,
Chakula kuninyima, wajukuu kunikataza ushirika,
Miungu nawaone chozi langu, wasikie kilio changu,
Mizimu nawaone uchungu wangu,
Radhi zao wasiwahi kukupa,
Laana wakumiminie,
Uje kulizwa mara mia na wanao,
Usiwahi kufurahia hata siku moja pato lao,
Watalokupa likuletee simanzi badala ya furaha,
Wakazawanao wasikuuguze katika utu uzima wako!

Kwa kurejelea utungo liosoma, jibu maswali yafuatayo:


Msemaji ni nani katika utungo huu?
Fafanua sifa tatu za anayeelekezewa maapizo haya.
. Andika mfano mmoja mmoja wa maapizo katika miktadha ifuatayo.
(a) Dini (b) Familia
(c) Kijijini (d) Darasani
Eleza majukumu ya maapizo ambayo yanajitokeza katika utungo huu.
D

Ukusanyaji na Uhifadhi wa
Fasihi Simulizi

Utangulizi
Sifa za fasihi simulizi ni kwamba huzaliwa, hukua, huishi na huweza kufa. Kadiri jamii
inavyobadilika, fasihi simulizi nayo inabadilika na kuathiriwa na maendeleo ya binadamu
kisayansi, kijamii na kiteknolojia. Vipera vipya vya fasihi simulizi huzaliwa kutokana na
athari za utandawazi, hukuzwa na kupewa uhai katika mazingira mapya. Aidha, vipera
vya zamani kama vile matambiko na ngomezi huweza kufa au kupewa sura mpya. Kwa
sababu hii, kuna umuhimu wa kuhifadhi tanzu za fasihi simulizi ili zisipotee. Lakini kabla
ya kuzihifadhi, ni lazima kwanza zikusanywe. Katika kukusanya data ya fasihi simulizi,
anayenuia kuikusanya huenda ilipo jamii anayolenga kukusanya data kutoka kwao.
Ukusanyaji wa data ya fasihi simulizi hufanywa ili kuendeleza na kutekeleza malengo
muhimu yanayokusudiwa na anayekusanya.
Mkusanyaji wa data huhitajika kufuata hatua zifuatazo za utafiti: j
(a) Kujiandaa/Maandalizi — Hapa anatakiwa kuzingatia yafuatayo:
(i) Mada ya utafiti — anatafiti kuhusu nini? Je, ni uwasilishaji mbolezi?
(ii) Mawanda ya utafiti — Kama ni kitendawili, je, anatafitia fani? Aina?
(iii) Walengwa — Atatafiti katika jamii gani? Wakamba? Wajaluo? Je, walengwa ni
wa umri gani? Wazee? Vijana?
(iv) Kipindi cha utafiti — Utaanza lini na unatarajiwa kumaliza lini?
(v) Kuomba kibali cha utafiti kutoka kwa taasisi husika, k.v. Wizara ya Elimu.
(vi) Mbinu za ukusanyaji na kuhifadhi data — Je, atatumia hojaji? Mahojiano?
Maandishi? Je, vifaa hivi vi tayari? Je, ikiwa ni hojaji, atazituma kwa posta au
ataziwasilisha kwa walengwa wenyewe? |
(vii) Gharama ya utafiti — Je, atatumia kiasi gani cha pesa? Nani atafadhili utafiti?
(b) Utafiti na ukusanyaji wa data — Mtafiti anaweza kukusanya data kupitia kwa hojaji,
mahojiano, kushiriki ama kutazama?
(c) Rekodi ya data — Mtafiti anaweza kurekodi data kupitia kwa maandishi, hunasa sauti
ya mhojiwa au fanani wa ngano, n.k. Vifaa hivi sharti viwe tayari kabla ya shughuli ya
utafiti kuanza.
(d) Kuchunguza upya data/maelezo yaliyotolewa na walengwa na kuyanakili jinsi yalivyo
ili kuyachanganua baadaye.
(e) Uchanganuzi na kufasiri kwa data — Hapa mtafiti huchanganua data kulingana na
vigezo vya uchanganuzi alivyoweka awali, na kulingana na mada yake. Matokeo ya
uchanganuzi hutumiwa kutoa hitimisho na mapendekezo kuhusu mada ya utafiti.
Uchanganuzi unaweza kutumia maelezo pekee au tarakimu/takwimu pamoja na
maelezo.

Ukusanyaji wa kazi za fasihi simulizi


Kama zilivyo sanaa nyingine, fasihi simulizi ni sanaa na hutegemea usanii wa jamii husika.
Fasihi simulizi hupewa umbo na thamani yake na jamii iliyoizaa. Hii ina maana kuwa fasihi
simulizi ina sifa na dhima maalumu katika jamii yake. Kwa sababu hizi, haifai mkusanyaji wa
kazi za fasihi simulizi kulinganisha fasihi simulizi ya jamii moja na sanaa ya jamii nyingine.
Ni vyema kwa mkusanyaji kuchukulia jamii kama ilivyo na kuichunguza ili aelewe umbo,
thamani na dhima ya fasihi hiyo katika jamii husika.
Fasihi simulizi inaweza kukusanywa kwa njia mbalimbali, mathalan:

1. Kusikiliza
Mkusanyaji anaweza kusikiliza wasanii katika jamii fulani wakitamba, kusimulia au
kuimba tungo zao.

2. Kushiriki
Mkusanyaji anaweza kujiunga na jamii kwa kushiriki katika ngoma, soga na masimulizi
ya hadithi na tanzu nyingine. Hapa, anayekusanya data ya fasihi simulizi haulizi
maswali bali hujirekodia anachokibaini katika ushirika huo.

Umuhimu wa kushiriki
(a) Kwa kushiriki katika fasihi simulizi, mtafiti huja karibu zaidi na jamii na hupata habari
za kuaminika moja kwa moja.
(b) Kushiriki ni njia bora ya kukusanya habari kutoka kwa watu ambao hawajui kusoma
na kuandika, ama wale ambao huona vigumu kujieleza moja kwa moja.
(c) Ni rahisi kwa mtafiti kuuliza maswali kuhusu kipera kinachowasilishwa. Mathalan,
anaweza kuuliza kuhusu kipindi ambamo wimbo fulani uliimbwa au hadhira mahususi
ambayo ilitambiwa aina fulani ya ngano.
(d) Mtafiti anaweza kunakili/kunasa anayosikiliza au anayotazama, hivyo kuhifadhi sifa
za kiimbo, toni na ishara.
(e) Mtafiti hupata taathira na hisia halisi ya yanayowasilishwa kwa vile anakabiliana ana
kwa ana na watendaji na hivyo kuelewa zaidi mada ya utafiti.
(f) Mtafiti anaweza kuthibitisha yale aliyokusanya kupitia kwa hojaji na mahojiano kwa
kuyahakiki.
(g) Kushiriki hukuza utangamano kati ya mtafiti na wanajamii. Ni rahisi kwa mtafiti
kupata majibu ya masuala anayotafiti kwa kushiriki na kutangamana na wanajamii.
Udhaifu wa kushiriki ”)

(a) Mbinu hii huchukua muda mrefu. Kushiriki katika utendaji huchukua muda zaidi
kuliko kuuliza maswali katika mahojiano.
(b) Huenda mtafiti akatekwa na yaliyomo na kusahau kurekodi.
(c) Ugeni wa mtafiti huweza kuleta wasiwasi miongoni mwa washiriki na wakakosa
kutenda kama kawaida.
(d) Uchanganuzi wa data inayokusanywa kwa njia hii ni mgumu na ni rahisi kwa mtafiti
kuacha masuala muhimu.
Hii ni njia ghali ya utafiti kwani inamhitaji mtafiti kusafiri mbali ili kushiriki katika
utendaji. Pia baadhi ya vifaa vya kuhifadhia data yenyewe kama vile kanda za video
huwa ghali au huenda zikakosa nguvu za umeme.

Kurekodi
Mkusanyaji anaweza kusikilizana na wasanii na kuwarekodi katika vinasasauti, kanda
za video, filamu au kuwapiga picha.

Kutazama
Mkusanyaji wa fasihi simulizi anaweza kukusanya data ya fasihi simulizi kwa
kushuhudia kwa macho fasihi fulani ikiendelezwa. Hapo, atashuhudia mwenyewe bila
kushiriki. Baadaye anaweza kuandika ili kuhifadhi. Mbinu hii hutumiwa zaidi katika
utafiti wa kipera cha maigizo.

Umuhimu wa utazamaji
(a) Ni rahisi kwa mtafiti kurekodi kwa vile hashiriki katika utendaji.
(b) Mtafiti hupata habari za kutegemewa zaidi hasa pale anapotumia kinasasauti kurekodi
moja kwa moja.
(c) Mtafiti anaweza kukaa mahali asipoonekana na kushuhudia utendaji halisi. Kwa sababu
washiriki hawajui kuwa wanatazamwa, utendaji wao hautaathiriwa na chochote;
utakuwa wa kawaida. Data ya aina hii inategemeka zaidi.

Udhaifu wa utazamaji
Wanajamii wanaweza kumshuku mtafiti kuwa anawapeleleza na hivyo kusitisha uwasilishaji
wao.

5. Kutumia hojaji
Hojaji ni fomu yenye maswali yaliyochapishwa ili kukusanya habari fulani. Hojaji
huandaliwa na mkusanyaji wa data na kutumwa au kupelekwa kwa mhojiwa au
atakayeijaza. Akikamilisha kuijaza unaituma au kupelekwa tena kwa mhoji. Hojaji ni
za aina mbili:
(a) Hojaji funge
Hii ni aina ya hojaji ambayo inamfunga mhojiwa kwa majibu fulani tu. Kila swali huwa
na orodha ya majibu na mhojiwa huhitajika kuweka alama tu kwa lile analoona kuwa
jibu sahihi.

Mfano wa hojaji funge:

Weka alama 4/ | kwenye visanduku vinavyowakilisha majibu


yako.

(i) Mawaidha hutolewa na kina nani katika jamii yako?


(a) Wazee | (b) Vijana IA

(ii) Vitendawili hutolewa wakati gani katika jamii yako?


(a) Jioni | (b) Mchana LO

Aina hii ya hojaji haimpi mhojiwa fursa ya kutoa maoni yake.

(b) Hojaji wazi au huru


Aina hii ya hojaji huwa na maswali ambayo yanahitaji majibu ya maelezo. Anayejibu
hupewa fursa ya kutoa maoni yake.

Mfano wa hojaji huru


HA AI WA AA aa KAWA

Unadhani kuna umuhimu gani katika kuhifadhi fasihi simulizi?

Sifa za hojaji
(a) Hojaji huwa na maswali ambayo hujibiwa na kundi linalolengwa katika jamii. Mtafiti
anaweza kulenga watambaji ngano au walumbi.
(b) Hojaji inaweza kutumiwa moja kwa moja na mkusanyaji wa fasihi simulizi kwa
anayehojiwa. Katika hali hii, mtafiti humwelekeza mtoaji wa habari kuhusu namna
ya kujibu. j
(c) Hojaji inaweza kutumwa kwa mhojiwa bila kuwepo kwa mtafiti. Mhojiwa hujisomea
na kujijazia hojaji bila mwongozo wa mtafiti. (Aina hii ya hojaji ndiyo iliyozoeleka
zaidi.)
Umuhimu wa hojaji
(a) Hojaji ni njia ya ukusanyaji data iliyo na gharama ya chini zaidi.
(b) Mtafiti anaweza kufikia idadi kubwa ya watoaji habari kwa kipindi kifupi kwa sababu
hojaji nyingi zinaweza kutumwa hata kwa njia ya posta.
(c) Inaweza kutumika katika mahojiano kama mwongozo. Mhoji anaweza kuitumia katika
mahojiano kufidia udhaifu wa mhojiwa.
(d) Humpa mhojiwa muda wa kuwazia maswali na kuyafanyia uchunguzi kabla ya kuyajibu.
(e) Hojaji, kwa kawaida, hazina athari za mtafiti kwa sababu, aghalabu mtafiti hayupo
zinapojazwa. Mhojiwa hujaza habari za kweli bila kushinikizwa kuchukua mtazamo
fulani kutokana na kuwepo kwa mtafiti.
(£) Hojaji inaweza kubadilishwa kulingana na kiwango cha wajazaji au wahojiwa.

Udhaifu wa hojaji

(a) Maswali yenye utata husababisha fasiri mbalimbali ambazo hufanya matokeo
yasitegemeke.
(b) Huenda watu wakakosa kuijaza hojaji kwa kikamilifu kwa sababu mbalimbali kama
vile kuhofia lawama au wakakataa kujaza kabisa.
(c) Hojaji ikiwa ndefu sana huenda baadhi ya watu wakakataa kuijaza.
(d) Hojaji wazi huwa ngumu sana kwa mtafiti kuchanganua data. Uchanganuzi huchukua
muda mrefu.
(e) Huenda wahojiwa wasijaze mambo ya kweli. Si rahisi kwa mtafiti kuthibitisha iwapo
habari zilizojazwa ni za kweli.
(£) Wahojiwa wanaweza kuchelewa kutuma hojaji zao, hasa hojaji zilizotumwa kwa posta.
(g) Baadhi ya wazee, japo wana habari za kutegemewa, hawajui kusoma na kuandika. Kwa
sababu hii, hawawezi kujaza hojaji isipokuwa wanaposaidiwa na watafiti au wasaidizi
wa watafiti.
(h) Kwavile mtafiti hakabiliani na mhojiwa ana kwa ana, hawezi kupata sifa za uwasilishaji
wa vipera vya fasihi simulizi kama vile toni na kidatu.

6. Mahojiano
Katika mahojiano, mkusanyaji wa fasihi simulizi hukabiliana ana kwa ana na watu
anaonuia kupata maarifa kutoka kwao. Mkusanyaji atakuwa ameandaa maswali
atakayouliza katika kikao rasmi. Mkusanyaji pia anaweza kushiriki katika mahojiano
yasiyo rasmi bila kunakili majibu papo hapo. Maelezo yanayotolewa yanaweza
kuhifadhiwa katika kanda ya kunasa sauti. Siku hizi, mahojiano huweza kufanywa
hata kwa simu.
Umuhimu wa mahojiano
(a) Kwa vile mtafiti anatazamana ana kwa ana na mhojiwa, ni rahisi kupata habari za
kina na za kutegemeka.
(b) Mbinu (sifa) za uwasilishaji kama vile toni, ishara za uso na kiimbo hubainika kwa
mtafiti, hivyo kuimarisha uelewa wake.
(c) Mtafiti anaweza kumfafanulia mhojiwa maswali na kumwezesha kupata data ya
kuaminika zaidi.

(d) Kwa vile mtafiti anamhoji mlengwa moja kwa moja, anaweza kurekodi majibu ya
mhojiwa au kuyaandika. Kwa njia hii, yaliyosemwa kuhusu mada husika huhifadhika
na si rahisi kupotea.

(e) Mtafiti anaweza kuyabadilisha maswali au mtindo wa kudadisi au kuhoji kulingana


na kiwango cha elimu cha mhojiwa. Kwa kufanya hivyo, anaweza kupata mwitiko
(majibu) bora zaidi.

(f) Kwa sababu wanatazamana ana kwa ana, mtafiti anaweza kung'amua wakati mhojiwa
anapotoa habari zisizo za kweli na kwa hivyo kuzichuja.

(g) Mtafiti anaweza kupata habari za kibinafsi na data zaidi kwani si rahisi kwa mhojiwa
kukataa kabisa kujibu maswali.

Udhaifu wa mahojiano
(a) Mahojiano yanahitaji stadi za mawasiliano za kiwango cha juu. Ikiwa mtafiti hana
stadi hizi, huenda akaathiri majibu ya wahojiwa kutokana na jinsi anavyoyafinyanga
maswali.

(b) Urasmi unaotokana na vikao vya mahojiano huenda ukatatiza mawasiliano kati ya
mbhoji na mhojiwa.
(c) Ukosefu wa muda wa kutosha wa mahojiano. Mahojiano huchukua muda mrefu na
huenda mtafiti akakosa kupata muda huo.
(d) Mhojiwa huenda asimwamini mtafiti, akahisi kuwa anapelelezwa, na kukataa kutoa
habari.

(e) Kiwango cha elimu cha mtafiti huenda kikawahofisha na kuwatia wahojiwa hisia za
unyonge na kuwafanya kutotoa habari za kutegemewa.
(f) Wahojiwa wengine huenda wakampa mtafiti habari za uongo ili kumfurahisha.
(g) Matatizo ya kutafsiri, ikiwa data imeandikwa kwa lugha tofauti, huenda yakaathiri
mahojiano.
(h) Mahojiano ni njia ghali ya kutafiti kutokana na gharama ya usafiri kwenda nyanjani.
|
|
|
Vifaa vya kukusanya na kuhifadhi fasihi simulizi
Ukusanyaji wa fasihi simulizi huhitaji vifaa vya kuhifadhi ujumbe. Vifaa hivi ni pamoja na:

(i) Kalamu na karatasi (maandishi)


Mkusanyaji wa data ya fasihi simulizi anaweza kutazama au kushiriki na baadaye akaandika
aliyoyashuhudia. Aidha, anaweza kuandika wakati maelezo, masimulizi au sanaa yenyewe
inapoendelezwa iwapo anatazama. Hata hivyo, vifaa hivi vya kukusanya fasihi simulizi vina
udhaifu kwani uzuri wa kazi ya sanaa (ujumi) hupotea kwa sababu sauti, toni, mageuzo,
vitendo na viziada-lugha vinavyoambatana na fasihi simulizi haviwezi kurekodiwa na
kufahamika ipasavyo kimaandishi.

Umuhimu wa maandishi
(a) Data kama vile hadithi huhifadhiwa kama ilivyotambwa, hivyo si rahisi kusahauliwa.
Mashairi na ngano nyingi zimeandikwa vitabuni.
(b) Huweza kufikia vizazi vingi kwa sababu kuandikwa huifanya fasihi simulizi iweze
kudumu.
(c) Si ghali kama zilivyo baadhi ya mbinu za kuhifadhi kama vile video.
(d) Si rahisi kufisidiwa au kupotea, hasa zikiandikwa katika vitabu. Hadithi, methali na
vitendawili vingi vimehifadhiwa kwa njia hii.

Udhaifu wa maandishi
(a) Kuna baadhi ya mambo kama vile kiimbo, toni, ishara, hisia na mapigo ya muziki
ambayo hayawezi kuandikwa kama yalivyowasilishwa na fanani, na kwa hivyo hupotea.
(b) Aidha, kwa vile maandishi si hai, hayawezi kutenda wala kusema. Ule uhai asilia wa
fasihi simulizi hufifishwa na kupotezwa na maandishi.
(c) Baadhi ya watafiti huenda wakaandika yale ambayo wanahitaji kwa wakati mahususi
na kupuuza mengine. Kwa mfano, ikiwa mada yake ni 'Wahusika katika ngano za
kimapokeo”, huenda akajihusisha na wahusika na kupuuza vipengele vingine kama
vile fanani. Haya huipujua fasihi simulizi.
(d) Kuandika fasihi simulizi huifanya kukosa ile taathira asilia kwani kunaipokonya
hadhira yake ile fursa ya kushirikiana ana kwa ana na fanani. Hivyo, hata mtu akitaka
kuulizia jambo, hana fursa ya kuuliza.
(e) Kuiandika fasihi simulizi huidhibiti na kupunguza hadhira yake na kuathiri vibaya
usambazaji wake. Fasihi inapoandikwa inawafikia tu wale wanaojua kusoma.

(ii) Vinasasauti/tepurekoda
Vinasasauti hupata sauti, toni na mahadhi ya tungo za fasihi simulizi. Vinaweza kutumiwa
katika mahojiano au mtu anaposhiriki au kutazama fasihi simulizi ikiigizwa. Ingawa ni bora
kuliko kalamu na karatasi, vinasasauti vina udhaifu kwa vile haviwezi kurekodi matendo
na miondoko ya wasanii.
Umuhimu wa vinasasauti/tepurekoda
(a) Sauti ya mhojiwa/fanani huweza kuhifadhiwa.
(b) Sifa ya uhai wa fasihi simulizi huhifadhiwa kwani kinasasauti hunasa sifa kama vile
za kidatu, toni na kiimbo cha mtambaji.
(c) Mkusanyaji wa fasihi simulizi anaweza kurudia kusikiliza uwasilishaji au mahojiano
iwapo hakuelewa. Sifa hii haipatikani katika maandishi.

Udhaifu wa vinasasauti/tepurekoda
(a) Kinasasauti huhitaji nguvu za umeme au betri hivyo basi, hakiwezi kutumiwa katika
sehemu zisizo na huduma hizi. Aidha, nguvu za umeme zikikosekana kabla ya utafiti
kukamilika utafiti utaathirika. Mtafiti atalazimika kuanza tena utafiti wake.
(b) Kinasasauti hakiwezi kumnasa mtambaji wala uigizaji wake. Watu wanaotumia kazi
iliyorekodiwa basi hukosa ile taathira ambayo inaibuliwa na kukabiliana ana kwa ana
na mtambaji.
(c) Baadhi ya wahojiwa au mafanani huenda wasitambe vyema ikiwa wanajua kuwa
wanarekodiwa. Mtafiti anaweza kukosa kupata data ya kutegemewa kama alivyotarajia
kuipata.

(ili) Kamera
Tofauti na vinasasauti, kamera inaweza kuchukua picha ambazo zinaonyesha kipengele
kimoja tu bila kuonyesha misogeo au miondoko wala sauti. Hata hivyo, kamera zinaweza
kuonyesha maleba.

(iv) Video
Video zinaweza kuchukua picha na pia kunasa sauti na miondoko. Ni njia nzuri ya kukusanya
fasihi simulizi isipokuwa ni ghali.

(v) Sinema au filamu


Filamu pia huonyesha picha za miondoko na sauti kama video. Kama ilivyo katika video,
filamu huwa ghali.

Umuhimu wa filamu na video

(a) Filamu na video hunasa picha na sauti, hivyo kuhifadhi uigizaji, ishara na kiimbo.
(b) Uhalisi wa mandhari ambamo kazi ya kifasihi inajikita huonekana na watumizi wa
kazi iliyohifadhiwa kwa filamu au video.
(c) Huipa kazi ya fasihi simulizi uhai na taathira zaidi kuliko kazi zilizohifadhiwa kwa
maandishi, kamera na kinasasauti.

Cs)
Udhaifu wa filamu na video
(a) Hii ni njia ghali ya kuhifadhi data.
(b) Data iliyohifadhiwa katika vifaa vyororo vya kompyuta na hata vinasasauti huweza
kufisidiwa, hivyo kutofaidi waliolengwa.

Njia nyingine za kisasa ambazo hutumiwa kuhifadhia na kuendeleza fasihi simulizi ni


pamoja na:

(i) diski za kompyuta.


(ii) magazeti. Baadhi ya tanzu za fasihi simulizi kama vile hadithi huandikwa mara nyingine
katika magazeti.
(iii) michezo ya kuigiza inayopeperushwa moja kwa moja kupitia kwa runinga na redio
na mashirika ya uigizaji. Michezo hii, pia, hutumiwa kuhifadhi na kuendeleza fasihi
simulizi.
(iv) tamasha za muziki zinazofanywa shuleni na katika majimbo kila mwaka. Tamasha
hizi husaidia kusambaza na kuhifadhi fasihi simulizi.

Umuhimu wa kukusanya na kuhifadhi fasihi simulizi


(a) Fasihi simulizi ni hifadhi ya mitazamo ya kitamaduni ya jamii. Ili kuweza kuifasiri na
kuielewa vyema, mwanafunzi wa fasihi simulizi anahitaji kutagusana na jamii ambayo
ni chanzo cha fasihi hiyo na utamaduni wake. Ukusanyaji utampa mwanafunzi wa
fasihi simulizi fursa ya kuingiliana na jamii iliyozaa fasihi husika. Kufanya hivyo
kutamwezesha mwanafunzi kuelewa utamaduni na fasihi yake kwa jumla.
(b) Ukusanyaji humpa mwanafunzi wa fasihi simulizi nafasi ya kushuhudia na kuathiriwa
moja kwa moja na utendaji wa fasihi simulizi. Kwa njia hii, mwanafunzi hupata kuona
vipengele hai vya fasihi simulizi kama vile uigizaji, toni na kiimbo ambavyo husaidia
kuielewa kwa kina.
(c) Ukusanyaji husaidia kurekodi na kuhifadhi tamaduni za jamii mbalimbali kwa nia ya
kuzipitisha kwa vizazi vijavyo. Mojawapo ya tamaduni hizi ni fasihi simulizi ambayo
kwa hakika hubeba tamaduni nyingine kama vile imani na falsafa za jamii fulani.
(d) Ukusanyaji huiendeleza fasihi simulizi. Kwa kurekodi vipera vya fasihi simulizi kama
vile ngano, hekima ya jamii pamoja na historia, itikadi, desturi na mtazamo wa kijumla
wa jamii kuhusu maisha huhifadhiwa na kupitishwa kwa vizazi vijavyo.
(e) Ukusanyaji wa fasihi simulizi husaidia kuziba pengo la utafiti lililopo. Tanzu nyingi za
fasihi simulizi hazijafanyiwa utafiti wa kutosha ili kuzihifadhi. Ukusanyaji utasaidia
kuziba pengo hili.
(f) Ukusanyaji zaidi wa data za fasihi simulizi hutumiwa kama kiunzi (msingi) cha
uchunguzi wa kiulinganishi wa fasihi simulizi za jamii mbalimbali. Kwa mfano, habari
kuhusu muundo wa utambaji ngano katika jamii moja huweza kutumiwa kama msingi
wa kuchunguza muundo wa utambaji ngano katika jamii nyingine. Mifanano au tofauti
katika miundo ya fasihi simulizi husaidia kuelewa jamii fulani na utamaduni wake.
(8) Ni muhimu kukusanya fasihi simulizi ili kueleza kwa nini, kwa mfano, utungo mmoja
wa fasihi simulizi ukawasilishwa kwa njia tofauti katika miktadha tofauti? Kwa nini
uwasilishaji una upekee wake kulingana na jamii? Jambo hili huwawezesha watafiti
na wasomi kwa jumla kuelewa sifa za tungo za fasihi simulizi.
(h) Utafiti wa fasihi simulizi humwezesha mwanafunzi kupata maarifa au stadi za kufanya
utafiti katika taaluma nyingine za kijamii kama vile sosholojia.
(i) Utafiti wowote ule husaidia kurekebisha mawazo potovu kuhusu suala fulani. Utafiti
kuhusu fasihi simulizi humpa msomi mwanga kuhusu masuala changamano katika
taaluma hii na kusahihisha dhana za awali ambazo huenda zinapotosha. Kwa mfano,
utafiti wa aina hii utamwezesha mtafiti kujua ni tanzu gani zilizokuwa katika jamii
za awali kabisa.
GJ Uchunguzi katika fasihi simulizi umewawezesha wasomi kutambua kuwa tungo nyingi
zilizoandikwa zilitokana na simulizi za tungo za fasihi simulizi. Kwa mfano, inaaminiwa
kuwa tanzu za kinathari kama vile hadithi fupi, novela na riwaya ni mwendelezo wa
hadithi za kimapokeo. Tanzu hizi zimechota maudhui na vipengele vya fani kutoka kwa
hadithi za kimapokeo kama vile ngano.

Matatizo yanayomkabili mkusanyaji wa fasihi simulizi


Baadhi ya matatizo ambayo humkabili mkusanyaji wa data za fasihi simulizi ni pamoja na
yafuatayo:
(a) Gharama ya utafiti. Huenda gharama ikawa kubwa kiasi cha mtafiti kutoimudu. Mtafiti
huenda akakosa pesa za kusafiria kwenda katika jamii mbalimbali au kununulia vifaa
kama vile tepurekoda.
(b) Mtazamo hasi wa wanajamii kuhusu ujazaji wa hojaji huenda ukawafanya wengi wao
kutojaza hojaji hizo.
(c) Wanajamii wengine huweza kushuku kwamba mtafiti anawapeleleza na wakakataa
kutoa habari.
(d) Baadhi ya mafanani au wahojiwa huenda wakadai walipwe kabla ya kutoa habari
zozote. Ikiwa mkusanyaji hana pesa, basi utafiti wake utakwamizwa.
(e) Mbinu nyingine za utafiti kama vile hojaji huhitaji watu wanaojua kusoma na kuandika.
Ikiwa watu wanaohojiwa hawajui kusoma na kuandika matokeo ya utafiti huenda
yasiwe ya kutegemewa.

(3)
(f) Vizingiti vya kidini. Hivi hutokea pale ambapo baadhi ya wahojiwa wanaamini kwamba
matendo ya fasihi simulizi kama vile matambiko na uimbaji wa taarabu, yanaenda
kinyume na imani yao ya kidini, na hivyo kukataa kuhojiwa.
(8) Kupotea au kufisidiwa kwa vifaa vya kuhifadhia data. Vifaa kama vile vinasasauti,
video na santuri za kompyuta huweza kupotea au kuharibika kutokana na hali mbaya
ya anga. Yote yaliyokuwa yamehifadhiwa vilevile yatapotea.
(h) Uchache wa wazee au wataalamu wa fasihi simulizi. Fasihi simulizi ilikuwa maarufu
sana miongoni mwa wazee na pengine watu wa umri wa makamo. Kukosekana kwa
wazee wanaoweza kutamba ngano ama kueleza vipera vingine kama vile vitendawili
hutatiza mkusanyaji wa fasihi simulizi, na kwa hivyo huenda data ya kutegemewa
isipatikane.
(i) Vikwazo kutoka kwa watawala. Watawala huenda wakakataa kutoa idhini ya kufanya
utafiti. Baadhi ya taasisi fadhili pia huenda zikakataa kudhamini utafiti katika fasihi
simulizi.
G) Wadhamini mara nyingi ndio huamua mambo yanayochunguzwa, mahali pa
kuchunguziwa na mawanda au upeo wa uchunguzi wenyewe. Aidha, fasiri ya ufafanuzi
wa data mara nyingi lazima ilingane na maslahi ya wadhamini. Ikiwa mtafiti atatoa
fasiri isiyowiana na mapendeleo ya wadhamini, huenda mapendekezo yake yakafutiliwa
mbali na pengine udhamini wa utafiti zaidi kusitishwa. Aidha, matokeo ya utafiti mara
nyingi huwa mali ya mdhamini ambaye huweza kuyatumia kuikandamiza jamii ya
mtafiti.
(k) Mtafiti huenda asiwe na wakati wa kutosha kuwahoji watu wengi. Muda ukikosekana
hatapata habari za kutosha kuhusiana na mada yake.
(Ii) Matatizo ya mawasiliano na uchukuzi. Ikiwa mkusanyaji analazimika kwenda mbali
kukusanya habari, hasa katika sehemu kame, itakuwa vigumu kufika huko kwa sababu
ya ukosefu wa vyombo vya usafiri kama vile magari.
(m) Matatizo ya kibinafsi. Anayekusanya fasihi simulizi anaweza kushindwa kuidhibiti
hadhira. Badala ya kuwauliza maswali, wahojiwa wanaweza kuwa ndio wanaomuuliza
mtafiti maswali. Kutojua lugha ya wahojiwa au kukosa mlahaka mwema na wahojiwa
kunaweza kuathiri ukusanyaji wa kazi za fasihi simulizi.
(mn) Ukosefu wa usalama. Huenda mkusanyaji wa fasihi simulizi akavamiwa. Aidha, baadhi
ya watu si karimu na huenda wakamshuku mtafiti na kumvamia.

(o) Tafsiri za data pia ni tatizo jingine. Fasihi simulizi huendelezwa kwa lugha za kijamii.
Kupata msamiati unaofaa kufasiri lugha changizi/chanzi hadi lugha pokezi ni tatizo.
Changamoto zinazoukabili ukusanyaji na uhifadhi wa
fasihi simulizi
Pamoja na matatizo yanayomkabili mkusanyaji moja kwa moja, kuna vikwazo ambavyo
vinakabili ukuaji wa fasihi simulizi:
(a) Ukosefu wa utafiti wa kutosha. Ingawa mengi yameandikwa kuhusu fasihi simulizi,
kuna vipera ambavyo bado havijaandikiwa sana.
(b) Uchache wa wataalamu wa kuitafitia na kuiendeleza. Wasomi wengi hupuuza utafiti wa
fasihi simulizi. Utafiti mwingi kuhusu fasihi umefanywa katika tanzu za fasihi andishi,
hususan riwaya, tamthilia, ushairi na hadithi fupi, lakini fasihi simulizi haijatafitiwa
vya kutosha.
Ukuaji wa kazi za kimaandishi. Kwa mfano, ngano nyingi za kimapokeo zimeandikwa,
hivyo hakuna haja ya utambaji; mtu anaweza kujisomea. Hili limefanya stadi ya
utambaji kufifia.
(d) Maendeleo ya kiteknolojia na kisayansi. Fasihi simulizi ilikuwa nyenzo ya kuburudisha
baada ya kazi, lakini kwa sasa teknolojia inatoa njia za kisasa za kujiburudisha kama
vile vipindi katika runinga.
(e) Kuhamia mijini kwa wanajamii wengi na kutangamana na watu wa jamii tofauti
kumefanya uhifadhi wa tamaduni za jamii na urithishaji wake kutowezekana.
(f) Mtaala wa elimu kupuuza lugha za kiasili ambazo ndizo zinazohifadhi na kurithisha
fasihi simulizi ya jamii mbalimbali. Kutofunzwa kwa lugha hizi katika madarasa ya juu
kwa jumla kunatinga ukuaji wa fasihi iliyosimuliwa au kuandikwa kwa lugha za kiasili.
(28). Kuna baadhi ya watu ambao wanaihusisha fasihi simulizi na ukale, hivyo kutoona
haja ya kuitafitia wala kuirithisha vizazi vya sasa.
(h) Fasihi simulizi ilihifadhiwa akilini. Kwa sababu hii, anayeihifadhi anaweza kuibadilisha,
anaweza kufa na kutoweka nayo au akili yake inaweza kufifia na kubetua kiini cha
simulizi hiyo.

Jinsi jamii ya kisasa inavyojaribu kuendeleza fasihi simulizi


Ingawa fasihi simulizi imepata changamoto kubwa kutokana na ukuaji wa tanzu za
kimaandishi, zipo shughuli ambazo zimefanywa kuchangia katika kuiendeleza:

(a) Tamasha za muziki. Wanafunzi hukariri, hughani na kuimba mashairi katika tamasha
za muziki.

(b) Sherehe za harusi, jando, mazishi na matambiko ambayo ni mifano ya miviga bado
zipo. Vipera vya mazungumzo kama vile mawaidha huendelezwa kupitia kwa sherehe
hizi.
(c) Utegaji na uteguaji vitendawili kupitia redio na runinga.
(d) Michezo ya kuigiza katika runinga, redio.
(e) Tamasha za drama huendeleza utanzu wa maigizo, mazungumzo na ushairi simulizi.

(f) Sarakasi zinazofanywa na wasanii huhifadhi kipera cha vichekesho na kukipokeza.


(g) Ngoma za kienyeji kama'vile Isukuti zinazochezwa katika hafla kama vile za kisiasa
na harusi.
(h) Watafiti, ingawa wachache, wanatafiti na kuandika au kurekodi vipera vya fasihi
simulizi. Mikusanyiko ya visasili, mighani na ngano imeandikwa kwenye vitabu. Tendi
na rara nyingi pia zimeandikwa vitabuni. Methali na vitendawili vimekusanywa na
kuhifadhiwa kwenye kamusi.
(i) Utambaji wa hadithi bado hufanyika katika baadhi ya jamii, hasa katika sehemu za
mashambani.

ia “Kuiweka fasihi simulizi katika maandishi, vinasasauti na video ni kuifisha.'


Jadili kauli hii kwa kutoa mifano mwafaka.
“Gharama ya utafiti ndilo tatizo kuu linalomkumba mtafiti wa nyanjani wa
fasihi simulizi.” Jadili.
Jadili nafasi ya vifaa vifuatavyo vya ukusanyaji na uhifadhi wa data katika
ukuaji wa fasihi simulizi:
(a) Hojaji (b) Video (c) Kalamu na karatasi.
(a) Eleza tofauti kati ya hojaji na mahojiano.
(b) Andika mifano miwili miwili ya:
(i) Hojaji funge
(ii) Hojaji huru.
Umepewa jukumu la kutafiti kuhusu michezo ya watoto katika jamii yako.
(a) Taja eneo ambalo utafanyia utafiti. L
(b) Fafanua mbinu ambazo utatumia kukusanyia data huku ukionyesha
sababu za uteuzi wako.
Kuna umuhimu gani wa kufundisha mbinu za ukusanyaji na uhifadhi wa
fasihi simulizi katika shule za upili?
Muhtasari wa Tanzu za Fasihi Simulizi

If
1
SU Si
ya Ka
S ”
Soga
9
yA , alumb, a
ano Yi t:
WA, Ja
ai

YA

yA Visakale E £

KA 9
ya AS IIS >
Z|SAA ZUIA
Ngano za usuli Ya ka 5 ?
afumbo |
5 i-
Ai
Zao
” AA AB / N ahau
- ZI
AI y SI S 13 4S7,

$/ fil No S
s > (ai
9 jv

$
S fe) 3 zA

|
di simulizi ALI
Na ya zani
NA N YA > 09 3
io
VAI
Nyimbo

>
wa
z
>$
> KA 3 YA GY
icheks Sho
ana fsi o. YA
E wa Aa Yap

LI “5 — 0
3 ua) Pembezi a. z S Ss AA Jah.
5 o 8 Yi
WALA Ja (50 3 6. WA
fa
$ YA < Z .

“ za
ka >
Mazoezi ya Marudio

1. Tofauti kuu kati ya tanzu na vipera vya fasihi simulizi ni ya kifani.” Thibitisha.
2. (a) “Fasihi simulizi ni utanzu ambao hauna budi kubadilika.” Jadili.
(b) Andika sifa sita zinazoipambanua fasihi simulizi.
3. “Kuna mfanano mkubwa kati ya fasihi andishi na fasihi simulizi.” Thibitisha.
4. (a) Fafanua maana ya hadithi.
(b) Eleza umuhimu wa aina zifuatazo za ngano katika jamii yako:
(i) Ngano za mtanziko (ii) Ngano za usuli (iii) Ngano za kiayari.
(c) Ngano zilitambwa usiku kwa sababu gani?
5. Taja aina za wahusika katika hadithi za kimapokeo.
6. Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata:

Hapo zamani za kale paliishi mzee aliyekuwa tajiri sana. Kwa jina alijulikana kama
Mzee Mali. Mzee Mali alikuwa na mashamba si haba. Fauka ya hayo, alikuwa mfugaji
mashuhuri. Alikuwa na mifugo wengi. Wengi mno wajukuu wake; wengi kama nyota
angani.
Mzee Mali hakuwa tajiri wa mali tu; alikuwa na moyo uliosheheni imani na
ukarimu. Alikuwa na mkono wazi kwa wanakijiji wote. Hata hivyo, maisha ya mzee huyu

kiburi na inda. Mama huyu kwa jina Husuda, alimiliki hiana iliyomfanya hata kuwahini
watoto wake mwenyewe mahitaji ya kimsingi.
Siku moja, kifunguamimba wa Mzee Mali alikwenda malishoni. Akiwa huko,
macho yake yalitua juu ya unyoya mmoja mweupe pepepe mfano wa theluji. Kijana
alivutiwa na weupe wa unyoya huo na akataka kuuchukua. Lakini, akienda kuuchukua,
unyoya ulimhepa na kuelekea kulia.
Kijana aliufuata unyoya, akaufuata, akaufuata. Hatimaye, unyoya ulifika katikati
ya msitu na kujikita ardhini. Kando ya unyoya huo, palisimama yai kubwa la mbuni. Yai
lilisafisha koo kwa kikohozi kama cha mtu aliye na homa ya mkunguru, likamwambia,
“Rafiki yangu, msituni humu mnatisha, tafadhali nichukue, nipeleke nyumbani
kwenu uniepushie hatari inayonikodolea macho.” Kijana aliposikia yai likinena,
kijasho chembamba kilimtiririka tiriri na moyo kumdunda ndundundu. Kwa hakika,
aliweza kusikia mpigo wa moyo wenyewe masikioni. Mandhari hayo yalimpa mwemeo
mkubwa. Hebu jifikirie ukiwa katikati ya msitu mkubwa, mfano wa Msitu wa Kauleni
ulio karibu na Mto Ngamiza; miti mingi mikubwa zaidi ya mivule imekuzunguka, kisha
yai likuzungumzie na kukurai ulipeleke nyumbani! Mjukuu wangu utafanyaje?
Fikira za kila aina zilifurika akilini mwa kijana huyo. Moyo ulimwambia,
“Ukithubutu kuchukua yai hili utajichongea kwa mama yako. Kumbuka jinsi alivyo katili
na mchoyo.” Fikira nyingine ikamwambia, “Usiache uovu wa mama yako kuubadhiri
wema wako. Lichukue yai hili; liokoe.” Fikira hizi ziliendelea kupigania nafasi akilini
mwake na kuupa moyo wake ulemavu wa muda. Hatimaye alikata kauli kulibeba yai hilo
alakulihali. Alilitwaa na kulipakata mikononi kama kitoto kidogo akaelekea nyumbani.
Kijana alipofika nyumbani alimkuta mama ameketi nje. Mara tu alipoliona
yai hilo, alifoka, “Umeokota wapi yai wee?” Kijana alijaribu kumweleza mamake
alivyolifikia yai hilo, lakini kumbe alikuwa kayasukumia maelezo ndani ya masikio ya
kiziwi! Alijaribu, akajaribu kumsihi mama yake amkubalie aliweke yai lake ndani ya
nyumba, lakini wapi! Hatimaye alichoka na kubaki kumkodolea macho tu. Mama mtu
alimwamuru kulitupa yai hilo katika kichaka kilichokuwa karibu na nyumbani kwao.
Laiti angalijua! Mama alifurahi kwamba mwanawe kalitupa yai na kumwonya dhidi
ya vitendo vya kitoto. “Wewe unajua hata kizimba cha kuku hakiwatoshi kuku wetu,
waniletea yai liso faida niliweke wapi?” Kijana alinyamaza tu.
Usiku ulipofika familia ya Mzee Mali haikulala. Pepo za chamchela zilitisha
kung'oa mapaa ya nyumba. Majinamizi yalimwandama mama mtu. Lile yai lilimjia
na kumsuta kwa kuliita yai la kuokotwa. Hata kulipopambazuka, ulimwengu mzima
ulishuhudia mabadiliko makubwa katika familia ya Mzee Mali. Mifugo wote walikuwa
wamelala chini - mizoga. Mimea yake yote ilikuwa imekauka japo mimea katika
mashamba jirani ilitwaa rangi ya kijani kibichi. Mke wake naye alikuwa ameambulia
ugonjwa wa ngozi na kifafa.
Mzee Mali alijikongoja kutoka ndani ya kibanda chake, ambacho usiku wa
kuamkia mkesha wake kilikuwa kasri. Alimwita kitindamimba wake kwa mashauriano.
Kijana alimweleza kadhia ya lile yai. Baada ya kutia na kutoa, Mzee aliamua kwenda
kulisihi yai lirudi. Alishika kiguu na njia hadi alipoelekezwa na mwanawe.
Lile yai lilikuwa pale alipoelezwa. Alipoliona, alijaribu kulitwaa. Yai lilipoona
linachukuliwa, lilichupa na kukimbia kwa kasi ya umeme huku nyuma likiacha Mzee
Mali kaduwaa. Mzee alijuta kwa kutomkanya mkewe dhidi ya uchoyo wake.
Hata hivyo, wajukuu zangu, Waswahili husema, “Maji yakimwagika hayazoleki.'
Mzee Mali alikuwa amechelewa. Alibaki kutazama kivumbi kilichotifuliwa na yai lile
huku akiimba wimbo kulisihi:

Ewe yai rudi


Rudi, najuta kumwoa mke afriti
Rudi kwa imani ya mwanangu
Rudi uiopoe mali yangu
Naahidi nitaujenga ukuta nilioshindwa kuuzibia ufa.

Nalo yai lilizidi kukimbia likimjibu:

Mke wako alinitusi


Akaniita yai
Yai la mbuni
Lililookotwa njiani
Na kitoto kikembe
Lisofaa kujengewa
Kizimba kuhifadhiwa
Kula chumo la husuda
Husuda la muhebi.

Mzee aliendelea kunasihi kwa wimbo ule ule, akaimba, akaimba, akaimba mpaka
koo likakauka. Kila mara alijibiwa kwa wimbo ule ule. Baadaye wazo lilimjia mzee huyu
kumtuma kifunguamimba msituni. Kifunguamimba alienda pale pale na kulipata yai
lake. Aliliangukia miguuni kwa wimbo:

Ewe sahibu yangu


Tulokutanishwa na jaala
Nyoyo zetu zikaungana
Kwa upendo wa udugu
Rudi nakunasihi
Rudi nakuomba
Rudi nakunyenyekea
Rudi uiokoe aila
Rudi umwondoshee baba simanzi
Rudi kwa pendo la baba.
Kwa wimbo huu, hisani ya yai iliyeyusha hisia za kisasi zilizokuwa moyoni.
Likakubali kutwaliwa na kijana. Wakapanda milima na kuteremka mabonde hadi
nyumbani. Kijana akaliweka yai kibandani alimokuwa mama. Mara tu yai lilipowekwa
chini, kibanda kiligeuka kuwa jumba lenye madirisha ya dhahabu. Mifugo wote wa
Mzee wakafufuka. Ngozi ya mama mtu iliyojaa mabaka sasa ikawa laini kama ya mtoto
mchanga, kifafa kikatoweka. Hali ya furaha ikarejea katika familia hii. Hadithi yangu
inaishia hapo.

Maswali
(a) Eleza funzo linalotokana na ngano hii.
(b) Eleza sifa za ngano zinazojitokeza katika utungo huu.
(c) Taja wahusika katika ngano hii.
(d) Andika mbinu nyingine za kifasihi zilizotumiwa katika ngano hii.

7. (a) Tathmini umuhimu wa aina zifuatazo za hadithi katika jamii:


(i) Mighani (ii) Soga (iii) Visasili.
(b) “Mighaini na visasili hufanana na kutofautiana. Jadili.
8. Jadili vipengele vitano vya kuzingatia katika uchanganuzi wa hadithi.
9. Jadili majukumu ya nyimbo katika uwasilishaji wa ngano.
10. (a) Huku ukitoa mifano, thibitisha kwamba semi ni utanzu wa fasihi simulizi.
(b) Onyesha, kwa kutoa mifano, matumizi ya vipengele vifuatavyo vya kimtindo
katika vitendawili:
(i) Sitiari (ii) Urudiaji
(iii) Mchezo wa maneno (iv) Tanakali za sauti
(v) Dhihaka/Kejeli/stihizai (vi) Taswira
(vii) Ukinzani.
11. 'Dhima ya pekee ya vitendawili ni kuburudisha'. Jadili.
12. (a) Eleza fani iliyovijenga vitendawili vifuatavyo:
(i) Afuma hana mshale - (Nungunungu).
(ii) Amekaa kimya na watoto wamemzunguka pande zote — (Mgomba).
(iii) Huwezi kukwea mti wangu - (Unyasi).
(iv) Mfalme analindwa na askari watano — (Kiganja).
(b) Taja mazingira mawili rasmi ambamo vitendawili hutolewa katika jamii yako.
13. Andika mifano miwili miwili ya methali zinazoweza kuainishwa pamoja kwa kuzingatia
vigezo vifuatavyo vya uainishaji:
(a) Maudhui ya malezi
(b) Maudhui ya maonyo
(c) Mbinu ya kinaya.
14. Eleza tofauti kati ya methali na vitendawili ukizingatia:
(i) Muundo (ii) Jukumu.
15. Andika mifano miwili miwili ya methali zilizoundwa kwa tamathali za semi zifuatazo:
(a) Kweli kinzani (b) Sitiari (c) Urudiaji/takriri
(d) Maswali ya balagha (e) Stihizai/dhihaka/kejeli.
16. (i) Andika fani zilizounda methali zifuatazo:
(a) Msiba wa kujitakia hauna kilio.
(b) Maji ya kifuu bahari ya chungu.
(c) Maneno matamu humtoa nyoka pangoni.
(d) Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.
(e) Chelewa chelewa utapata mwana si wako.
(f£) Kigumba kwa nguruwe kwa binadamu ki uchungu.
(g) Ujana ni moshi ukienda haurudi.
(h) Mla cha uchungu na tamu hakosi.
(i) Pambo la jeneza lamfaani mfu?
(j)) Siri ya nyani kamwulize kima.
(ii) Andika methali mbili mbili zinazotumiwa:
(a) Kuhimiza kutokata tamaa.
(b) Kufariji wakati wa msiba.
(c) Kusifu tendo jema.
(d) Kuhimiza udugu.
(e) Kuonyesha umuhimu wa mtu kuthamini vitu vyake.
(f£) Kuonyesha kuwa jambo jema huja baada ya jitahada.
(g) Kuonya dhidi ya kuamini marafiki sana.
(h) Kuonyesha kuwa binadamu hupendelea nafsi zao kwanza.
17. Eleza dhima ya vipera vifuatavyo vya semi katika jamii yako:
(a) Lakabu (b) Misimu (c) Vitanza ndimi.
18. Huku ukirejelea jamii yoyote ya Kiafrika, andika miktadha ambamo ushairi simulizi
ulijikita.
19. (a) Taja aina tano za nyimbo.
(b) Eleza majukumu ya nyimbo zifuatazo:
(i) Sifo (ii) Hodiya.
20. Fafanua sifa za aina zifuatazo za maghani simulizi:
(a) Tendi (b) Rara.
21. 'Maigizo huchukua nafasi muhimu katika fasihi simulizi.” Thibitisha.
22. Tathmini sifa muhimu za fanani katika kufanikisha fasihi simulizi.
23. Fafanua umuhimu wa maigizo ya watoto na vichekesho.
24. Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali:
Aa
Ewe Mainga wa Ndumi
Siwe uloambia akina mama
Siku tulopiga foleni
Chakula cha msaada kupata
Turudishe vifaranga kwenye miji
Wageuke vijusi tena
Njaa isiwaangamize?

Siwe ulopita
Matusi ukitema
Chumvi na sukari kuturushia ja samadi?
Uhitaji wetu ukatutuma
Kuokota vihela uloturushia
Ukatununua, kura ukapata?
Sasa miaka mitano imetimia
Waja tulaghai tena
Mainga wa Ndumi huna lolote safari hii
Ubunge umekudondoka ukitazama
Wanyonge tumeamua
Kwingine kujaribu

Maswali
(a) Huu ni wimbo wa aina gani? Kwa nini?
(b) Andika mbinu za lugha zilizotumiwa katika utungo huu.
(c) Ni nani anayezungumza (nafsineni) katika utungo huu?
(d) Fafanua toni ya utungo huu.
(e) Fafanua umuhimu wa nyimbo za aina hii.

25. Andika ubeti mmoja mmoja wa aina zifuatazo za nyimbo:


(a) Mbolezi zinazohusiana na vita
(b) Rara nafsi ya kimapenzi.
26. Fafanua sifa za mawaidha kwa kuzingatia:
(a) Hadhira (b) Fanani (c) Maudhui (d) Fani.
27. Taja miktadha mitano ambamo ulumbi hutumika katika jamii yako.
28. (a) Eleza tofauti kati ya ngoma na ngomezi.
(b) Andika aina tano za miviga katika jamii za Kiafrika.
(c) Toa mfano mmoja mmoja wa aina zifuatazo za malumbano ya utani:
(i) Yakiukoo (ii) Kati ya maumbu
(iii) Ya bibi na mjukuu (iv) Ya marika.
29. Eleza umuhimu wa ukusanyaji wa data za fasihi simulizi.
30. Kwa nini ni muhimu kufunza fasihi simulizi katika shule za sekondari?
31. Soma utungo ufuatao wa fasihi simulizi kisha ujibu maswali yanayofuata.

'Nilipokukopoa,
Cheko la mwivu wangu lilipaa sana
Ukewenza ukamshawishi kuchukua buruji kueneza habari.
“Njooni mwone jana la ajabu”.
“Hajawahi kuonekana kama huyu
tangu kuumbwa kwa ulimwengu”
Ndivyo walisema walokubeza
Kijiji kizima kilimiminika mwangu nyumbani
Kuyatuma maozi kukutazama weye
Uso na thamani walikwona,
Wakaupa unyonge moyo wangu toto,
Wakanituma kuola viungo vyako
Wakanitanabahisha upungufu ulokulemaza!
Chozi chungu likapukutika
Likalovya changu kidari
Likanavya chako kipaji
Tabasamu ukatoa kunihakikishia
“Mimi si mjalana!
Katu sivyo wasemavyo walimwengu!”
Neno lako hili likanipa tulivu
Nikaamua alakulihali kupambana na yangu jumuiya
Ilosema kwa moja kauli utokomezwe, chakani utupwe.
Tazameni mahasidi mloteka
Teko la dharau mlonimwaiya
Mkanitia ukiwa usomithilika!
Oleni! Tungeni macho!
Mwana mlioambaa ja ukoma
Mlomwinga ja nyuni wala mtama, tazameni
Mekuwa malaika, anowaauni
Kiguru mlomtajia hakimzuwii kufuma mishale!
Maadui wamwonapo hutetema kama jani

Mepigana vita visohisabika


Na wetu mahasimu waliotupoka na mifugo.

Jamii yetu sasa metawala kote


Umekuwa nahodha mwenye kubwa saburi
Akili yako nyepesi sumaku kweli kweli
Hupakata yote ya neema na shwari
Mwili wako japo lemavu,
Mesheheni nguvu za majagina mia moja!
Naposhika zana, maadui elfu huanguka!
umtfifaa jamii hii, ilotaka kuangamiza
Majagina wote, wakusujudia
Walokufurusha wamebaki hizika
Watukuka ewe shibli
Mfano wa Shaka Zulu
Alowaonjesha kivumbi wapinzani
Kuwayeyusha kama barafu.

Limwengu mzima wakujua, mwana


Alozawa kishika mkuki
Ulosema na miungu, alfajiri lipoukumbatia ulimwengu
Ela mwana jihadhari usaliti wao waja
Wasije kutosa lindini kwa nduli kukukabidhi.

Maswali

(a) Ainisha utungo huu kimuundo na kimaudhui.


(b) Andika sifa za mighani ambazo zinajitokeza katika utungo huu.
(c) Jadili fani katika wimbo huu.
(d) Jadili sifa za jamii iliyoizaa kazi hii.
(e) Ni nani anayeimba wimbo huu (nafsineni)?
pa
32. Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata:

£ Hapo zamani za kale katika kitongoji cha Shwari, paliishi Sungura na Fisi. Sungura
na Fisi walikuwa marafiki wa chanda na pete. Walizama na kuibuka pamoja katika
bahari mbalimbali za maisha. Marafiki hawa walizilea aila zao pamoja. Walifanya
kazi kwa ujima mashambani na kushiriki vunoni pamoja. Mvua nayo ilinyesha
msimu baada ya mwingine. Makonde yao yakanawiri na maghala yao yakaanza
kulalamikia shibe. Pia walichunga mifugo wao pamoja.
Watoto wa Sungura na Fisi walicheza pamoja bila kujali tofauti zao za kimaumbile.
Waliamka alfajiri na mapema kwenda kuchunga mifugo wa wazazi wao. Kadiri siku
zilivyosonga, ndivyo gundi iliyougandisha udugu kati ya familia hizi ilivyoendelea
kunata. |
Hata hivyo, siku za neema zilipisha shari. Mvua ilikataa katakata kukitembelea

Mwishowe ikakauka kabisa.


Fisi alikesha kitandani kwa tafakuri kuu. Hali ya baadaye ya familia hizi mbili
ilimsononesha. Alihofia kuwaona wanao wakigeuka magofu. Asubuhi moja baada
ya yeye na familia yake kula mate usiku uliotangulia, alimwendea Sungura na
kumtaka washauriane kuhusu mkakati wa kukabiliana na hali mbaya iliyowasibu.
Baada ya kutia na kutoa, wazo zuri lilimjia Sungura. “Ndugu yangu, janga hili
la njaa ni tokeo la hasira za mizimu. Mababu zetu walikosa nasi hatuna budi
kuangukiwa na laana za mizimu. Jana usiku, mizimu ilinijia usingizini. Iliniambia
kwamba njia ya pekee ya kujiopoa na familia zetu ni kwa kuituliza kwa kuitolea
kafara. Tukifanya hivyo, mvua itanyesha mara moja na tutaweza kuyanusuru maisha
ya watoto wetu.”
Kipaji cha Fisi kilinawiri kwa furaha. Hata hivyo, tabasamu yake haikudumu.
Alizama tena katika fikira. Baada ya kutafakari kwa muda, alimuuliza Sungura,
“Ndugu yangu, mifugo wetu wote wamesalimishwa amri na ukame. Maghala yetu
hayana chochote. Hata kuwalisha watoto wetu ni tatizo. Je, tutatoa wapi kafara?”
Sungura alijibu kwa huzuni, “Mizimu yenyewe haitaki mifugo wala nafaka.
Inataka damu. Damu ya binadamu pekee ndiyo inayoweza kufuta dhambi za mababu
zetu.”
“Na binadamu wenyewe watatoka wapi?” Aliuliza Fisi.
“Hilo ndilo tatizo. Mizimu inataka tuwatoe sadaka mama zetu na vifunguamimba
wetu. Leo usiku, wanataka kila mmoja wetu amuue mama yake na kumtoa kama
sadaka kwenye mbuyu ulio karibu na mto.” Sungura alisema.
| Maneno ya Sungura yaliyafanya masikio ya Fisi kuvuma kwa uchungu wa
fikira ya kumpoteza mamake. Alimpenda mama yake kwa dhati. Aidha, alijua
kuwa haikuhalisi binadamu kumuua mwenzake. Hata hivyo, nafsi yake ilimnasihi
kwamba alihitaji kufanya uamuzi wa dharura. Jioni hiyo, sime yake ilifanya
kazi. Alikata koo la mama yake mpenzi huku machozi ya majonzi yakimtiririka.
Aliuchoma mwili wa mama yake pale mbuyuni huku akiimba:
Enyi mizimu mtoao vipaji,
Nimewapeni roho ya kipenzi mama yangu,
Itumeni mvua kuineemesha ardhi.
Fisi aliondoka huku akijituliza kuwa hata Sungura naye amemchinja mama yake.
Usiku huo, mvua ya gharika ilinyesha. Mashamba ya Sungura na Fisi yakajaa
chakula mara moja. Zizini, ng'ombe wakasikika wakikoroma na ardhi ikavaa vazi
la kijani kibichi. Wakati wote huo Sungura hakuonekana nyumbani. Fisi alidhani
kwamba huzuni ya kumpoteza mama yake imemlemea, hivyo akaamua kwenda
mbuyuni kumtafuta. Hata kabla hajakivuka kizingiti cha mlango, alikumbana ana
kwa ana na mama yake Sungura. Malaika yalimsimama mwilini, mate yakamkauka
kwa mshangao! “Kumbe Sungura hakumtoa kafara mama yake? Kumbe maneno yote
ya Sungura yalikuwa ulaghai ili mimi Fisi nimtoe kafara mama yangu na kuiauni
jamaa ya Sungura!” Moyo wa Fisi ulifungwa kwa fundo kubwa la chuki na kisasi
kwa Sungura. Huo ukawa mwisho wa urafiki wao.

Maswali
(a) Andika sifa tano za ngano zinazojitokeza katika hadithi hii.
(b) Hii ni ngano ya aina gani?
(c) Andika maadili yanayojitokeza katika ngano hii.
(d) Jadili mbinu za kifasihi zilizotumiwa katika ngano hii.
33. Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali yanayofuata:
Zimepita siku ayami
Siku chungu tangu giza lipotanda
Wakati lipotazama kwa kiwewe na shauku
Pumzizo kipania, roho kupigania
Ziraili alipokakamaa aushiyo kufakamia.

Nalikwita kwa sauti


Ela penzi hukunitika
Machoyo litunga mbele
Kumkabili huyu nduli
Nikabaki kunyong'onyeya
Jaala kitumainia,
mtima kijiinamia
Hatima kungojea.
Ya mwisho lipopumua,
alfajiri ya kiza kikuu
Nalidhani wanichezea,
mizaha yako kawaida
Lijaribu kupulizia
Hewa toka langu pafu,
tumaini kiniambia pumzi zangu takuhuisha
Sikujua hizo likuwa juhudi za mfa maji muhebi.

Macho libaki kutunduiya, tabasamuyo kitaraji


Kumbe mwenzangu kaniacha!
Ukiwa ulinivaa, ukungu ukatwandama
Pa kuegema, sikujua fundo chungu linisakama
Tabibu alipoingia na kutangaza rasmi mauko.

Ilikuwa kana kwamba ndo jana lipofunga nikahi.


Kumbukizi zilinijia kwa chozi teletele
Japo kifo ni faradhi ndwele hino halieleweki
Ama jicho la hasidi,
limekuangaza jamani?

Koja hili ninalokuwekea,


kando ya kasri hili la shakawa
Ni hakikisho toka kwangu, nitatamba sana na njia
Kutafuta alotwendea kinyume kutupoka,
mauko kutuleteya.

Maswali

(a) Utungo uliosoma ni mfano wa mbolezi. Thibitisha.


(b) Wimbo huu unasawiri msimamo gani wa jamii husika kuhusu kifo?
(c) Andika tamathali na mbinu za lugha zilizotumiwa katika shairi hili.
(9) Nani nafsineni/mzungumzaji katika utungo huu?

Oo
11

Majibu ya Mazoezi ya Marudio


Fani ni jumla ya mbinu ambazo msanii Msimulizi (nafsineni) — majigambo
hutumia kuwasilisha maudhui. Tanzu na hutolewa na mwenye kujigamba ilhali
vipera vya fasihi simulizi hutofautiana kwa katika pembejezi mtu husifiwa na
sababu ya matumizi tofauti ya vipengele vya mwingine.
fani kama vile: Mandhari - mandhari yanaweza
- Mtindo —- mtindo ni jinsi msanii kuwa mahali, wakati au hali ambamo
anavyotumia lugha kuwasilisha kazi ya kifasihi imezaliwa. Tanzu za
ujumbe. Kwa mfano, ingawa mighani fasihi simulizi hutofautiana kutegemea
na tendi zina maudhui sawa kwamba mandhari. Kwa mfano, bembea ni
ni masimulizi kuhusu mashujaa/ nyimbo ambazo huimbiwa mtoto
majagina, kimtindo mighani anayelia (hali ya huzuni) ilhali nyimbo
husimuliwa kwa mtindo wa nathari za chekechea huimbwa na watoto
ilhali tendi husimuliwa kwa mtindo wanapocheza. Hadithi, vitendawili na
wa kishairi. Aidha, ngano huwasilishwa mawaidha hutolewa katika vikao rasmi,
kwa lugha ya nathari ilhali mashairi lakini methali huweza kutolewa katika
hutumia lugha teule yenye mdundo na mazungumzo ya kawaida.
mapigo ya sauti.
Tanzu na vipera vya fasihi simulizi
- Muundo - hili ni umbo au sura ya kazi pia hutofautiana kimaudhui. Kwa
ya kifasihi. Semi ni utanzu wenye kauli
mfano, mighani husimulia masuala ya
fupifupi ilhali hadithi ni utanzu wa
kihistoria/ya kishujaa navyo visasili
masimulizi marefu. Vitendawili vina
husimulia mambo ya kidini/kiimani.
fomyula ya uwasilishaji yenye ufunguzi,
mwili na mwisho ilhali methaliina 2. (a) Mambo yanayosababisha kubadilika
muundo wa mshororo wa kishairi. kwa fasihi simulizi:
- Tamathali za usemi — methali hutumia Hadhira. Kubadilika kwa hadhira
tamathali mbalimbali za usemi ilhali husababisha kubadilisha kwa mtindo
lakabu hutumia sitiari sanasana. wa kuwasilisha. Kwa mfano, mtu
- Wahusika — katika ngano kuna wahusika akitambia watoto ngano ataisahilisha
binadamu, wanyama, mazimwi na lugha kulingana na kiwango chao na
viumbe visivyo hai. Wahusika hawa akitamba ngano hiyo hiyo kwa watu
hutumiwa kutofautisha kati ya aina za wazima, atapevusha lugha.
ngano. Kwa mfano, hurafa ni ngano Wakati. Wakati/kipindi huathiri fani
zenye wahusika wanyama ilhali hekaya na yaliyomo katika kazi ya kifasihi. Kila
ni ngano zenye wahusika binadamu. kipindi huwa na masuala yanayokiathiri.
- Ploti — ploti ni mpangilio wa matukio Masuala haya huwasilishwa kupitia
kulingana na jinsi yanavyosababishana. tungo za kifasihi. Aidha, wasanii wa
Utanzu wa hadithi, kwa mfano, una vipindi tofauti huwa na mitindo tofauti
ploti ilhali utanzu wa semi hauna ploti. ya kutumia lugha.
AA...
Fanani. Kila fanani ana mtindo wake kuzaliwa upya kwa fasihi simulizi
wa kuwasilisha fasihi simulizi. Hadithi (kimaudhui na kifani), kukua kwake na
moja inaweza kusimuliwa kwa mitindo hata kufa kwake. Uhifadhi kimaandishi
tofauti kulingana na yule anayeisimulia. wa fasihi simulizi unaua uhai wake.
Kumbukumbu za fanani. Kumbukumbu Jamii fulani inapokufa, hakuna watu
zinaweza kufifia au kupungua. Haya wa kuirithisha. Kwa sababu hii fasihi
yakitokea, hubadilisha yaliyomo na simulizi hufa.
mkondo wa utanzu wa fasihi simulizi. - Fasihi simulizi ni mali ya jamii. Tanzu
Kizazi kinaweza kuibadilisha fasihi zake zote zikishatendwa humilikiwa na
simulizi kwa kurithisha tu yale ambayo jamii nzima na kupokezwa vizazi vyake.
yanachukuliwa kuwa muhimu na - Huwa na wakati maalumu wakupokezwa.
kuacha mengine.
Hadithi hutambwa jioni. Sherehe za
Maendeleo ya kisayansi na teknolojia. jando na unyago ziliadhimishwa wakati
Kufuatia maendeleo ya kisayansi fulani maalumu.
na kiteknolojia. Fasihi simulizi sasa - Huchukua umbo mahususi. Methali,
inawasilishwa redioni, katika runinga
vitendawili, ngano na majigambo yana
na vyombo vingine vya kisasa. Aidha
maumbo yake maalumu.
fasihi simulizi inarithishwa kupitia kwa
- Ina historia ndefu. Fasihi simulizi
vyombo vya kisasa kama vile runinga
na filamu. Uhifadhi wake umebadilika ilikuwepo tangu mwanzo wa maisha ya
binadamu.
na sasa inahifadhiwa kimaandishi au
katika kanda za video, vinasasauti na - Fasihi simulizi ina sifa ya kuwa na
kompyuta. ; pahali mahususi pa kutendea. Sherehe
(b) Zifuatazo ni sifa za fasihi simulizi: za jando hufanyiwa jandoni, matambiko
hufanyiwa pangoni au kwenye miti
Fasihi simulizi huwasilishwa kwa
mikubwa.
hadhira hai. Kuna uhusiano wa ana kwa
ana kati ya fanani na hadhira. - Fasihi simulizi huhifadhiwa akilini.
Kwa sababu ilihifadhiwa akilini, ilikuwa
Huwa na utendaji. Anayejigamba, kwa
mfano, huigiza akibeba zana za kazi
muhimu kuirithisha kutoka kizazi
anayojisifia. Aidha, fanani anaweza kimoja hadi kingine ili kuidumisha.
kutumia viungo vya mwili akachezesha - Fasihi simulizi huwasilishwa kwa
mabega, kufumba macho au kukunja mdomo. Kwa sababu ilihifadhiwa
uso. akilini, iliweza kurithishwa tu kupitia
Fasihi simulizi ina sifa ya kuwa kwa mdomo.
na mtendaji/fanani. Fanani ndiye Fasihi andishi ina mfanano mkubwa na fasihi
husimulia, hutamba, huimba au simulizi:
kuwasilisha kazi ya fasihi simulizi.
- Fasihi andishi na fasihi simulizi
Ina uwezo mkubwa wa kubadilika.
hushughulikia masuala sawa
Tanzu za fasihi simulizi hubadilika
yanayotokana na migogoro kati ya
kutegemea hadhira, wakati, mandhari
binadamu na tajiriba mbalimbali katika
na hata teknolojia. Hadithi moja
mazingira yake, kwa mfano utawala,
inaweza kutambwa kwa njia tofauti
ubinafsi, mapenzi, woga, utabaka,
kutegemea mazingira.
jinsia, ndoa, ushujaa.
Huwasilishwa kwa namna tofauti
tofauti, kwa mfano, ngano hutambwa - Aina zote mbili hutumia lugha kwa
ilhali vichekesho huigizwa. ubunifu kuwasilisha maudhui.
Fasihi simulizi huzaliwa, hukua na - Tanzu za fasihi andishi zilitokana na
hata kufa. Mabadiliko ya mazingira na fasihi simulizi. Kwa mfano, riwaya,
maendeleo ya binadamu husababisha novela na hadithi fupi ni mwendelezo
Wa

wa hadithi za kimapokeo. Mashairi - Huadilisha.


yaliyoandikwa yanatokana na ushairi - Huburidisha.
simulizi. (iii) Ngano za kiayari:
Fasihi zote mbili zina vipengele viwili - Huonya dhidi ya usaliti.
vikuu: fani na maudhui. - Hutumiwa kukashifu uongozi
Jukumu kubwa la aina zote mbili za dhalimu au matendo maovu.
- Hufanyia tashtiti au hukejeli
fasihi ni kusawiri maisha, kupumbaza,
wanaotumia nguvu badala ya akili
kuadilisha, kuelimisha, kukuza lugha, na hekima.
kuhifadhi na kuendeleza utamaduni wa - Huburudisha.
jamii. (c) Sababu za kutamba ngano usiku:
Fani zinafanana. Tanzu za kinathari Ngano zilitambwa usiku kwa sababu
za fasihi andishi zinafanana na tanzu ndio wakati ambao jamaa wengi
za kinathari za fasihi simulizi. Kwa walikuwa wamejumuika nyumbani
mfano, baadhi ya riwaya zina wahusika baada ya kazi.
wanyama. Utambaji ulikuwa njia nzuri ya kupitisha
Aina zote mbili za fasihi zina utendaji. wakati wakingoja chajio.
Fasihi andishi inaweza kuigizwa Vikao vya utambaji vilitumia ngano
jukwaani. Kwa mfano, tamthilia kutoa mawaidha kwa wanajamii kwa
huigizwa jukwaani. Aidha, riwaya jumla. Wanajamii waliweza kujumuika
zimeigizwa kama filamu. pamoja jioni kuliko mchana.
Fasihi zote huzaliwa, hukua na hufa Wakatihuu ulihakikisha kuwa wanajamii
kutegemea mabadiliko ya wakati. hawapotezi wakati wa kazi.
Sifa ya utambaji hupatikana katika
Aina za wahusika katika hadithi za kimapokeo:
fasihi simulizi na fasihi andishi. Ngano,
Wahusika binadamu
kwa mfano, ina mtambaji. Riwaya ina
Wahusika wanyama na ndege
sauti ya msimulizi ambayo inaweza
kufananishwa na mtambaji. Mazimwi au majitu
Mizimu
4. (a) Hadithi ni masimulizi ya kweli au ya
kubuni kwa lugha ya nathari kuhusu Vitu visivyo hai, kwa mfano mawe, miti
watu, wanyama, matukio au hali Miungu na mashetani
mbalimbali. Funzo - ngano inaonya dhidi ya uchoyo.
(b) Nafasi ni sawa na umuhimu. Uchoyo wa mke wa Mzee Mali uliiletea
Gi) Ngano za mtanziko: familia maafa.
-. Hukuza uwezo wa kupima mambo Sifa za ngano zinazojitokeza:
na kuamua/kuteua lililo muhimu. - Ina fomyula ya ufunguzi na
- Hukuza uwezo wa kujadiliana na hitimisho. Inaanza kwa 'Hapo
kufikia uamuzi mwafaka. zamani za kale', na kuishia kwa
- Huonya dhidi ya kutenda bila “Hadithi yangu inaishia hapo'.
kuwaza kwa kina. - Inawahusika wa aina mbalimbali;
- Huadilisha. wahusika binadamu —- Mzee Mali
na familia yake.na wahusika vitu
- Huburudisha.
— yai na unyoya.
(ii) Ngano za usuli: Ina matumizi ya fantasia —
-
-. Huelezea sababu za mazoea au hali
yai linazungumza, unyoya
fulani.
unatembea, utajiri unatokomea
- Huonya dhidi ya tabia hasi kama mara moja na kurudi mara moja.
vile usaliti.
j y

Ina tashihisi. Wahusika wasio - Hutumiwa kama sifo. Husifu


binadamu wanapewa sifa mashujaa katika jamii.
za binadamu, kwa mfano Yai - Huhimiza uzalendo.
linazungumza.
- Huadilisha.
Inaadilisha. Inaonya dhidi ya - Hupalilia ujasiri miongoni mwa
uchoyo.
vijana.
Ina matumizi ya nyimbo. Hukuza utangamano.
-
Ina matumizi ya takriri. Maneno -
Huonya dhidi ya matendo hasi
fulani yamerudiwarudiwa, kwa kama vile usaliti.
mfano akaimba, akaimba. (ii) Umuhimu wa soga:
(c) Wahusika katika ngano hii: -. Hukashifu matendo hasi kwa njia
Mzee Mali ya ucheshi.
Husuda, mke wa Mzee Mali - Huburudisha.
Kifunguamimba - Huadilisha.
Yai (iii)
Umuhimu wa visasili:
Unyoya. - Hudhibiti na kuhalalisha baadhi
(d) Mbinunyingine za kifasihi zilizotumiwa: ya desturi katika jamii.
Majazi — Mzee Mali, Husuda -. Hueleza asili ya mazoea au jambo
fulani.
Tashihishi — Yai linapewa sifa za
kibinadamu za kuzungumza. - Hutambulisha jamii.
-. Huhifadhi utamaduni na historia
Ndoto —Majinamizi kumwandama
mke wa Mzee Mali. ya jamii.
- Huadilisha.
Mjadala nafsia/uzungumzi nafsia
—Kifunguamimba anajizungumzia - Huburudisha.
mawazoni. (b) Kufanana kwa mighani na visasili:
Chuku —- Husuda anashikwa na Mifanano kati ya mighani na visasili:
kifafa cha mara moja. - Mighani na visasili ni hadithi za
Sitiari — Kusukumia maelezo ndani kihistoria.
ya masikio ya kiziwi. - Zote hazina mianzo maalumu.
Usambamba - Rudi nakunasihi, - Zote zina matumizi ya fantasia.
rudi nakuomba - Aghalabu binadamu huhusiana na
Taswira — Picha ya kasri na kibanda miungu, shetani au pepo.
cha Mzee Mali, picha ya ngozi Tofauti kati ya mighani na visasili:
ya mke wa Mzee Mali, picha ya
| MIGnani PU;
mifugo waliokufa na ile ya mimea kua G
aa

iliyokauka. Husimulia kuhusu |Husimulia asili ya vitu.


Takriri —- Akaimba, akaimba, mashujaa.
akaimba; akaufuata, akaufuata. Husimulia historia |Husimulia mianzo
Wimbo pia una takriri. Neno rudi ya vitu au mambo
linarudiwarudiwa. ulimwenguni.
7. (a) Umuhimu wa mighani katika jamii: Wahusika wakuu ni Wahusika ni vitu
majagina. tofauti kama vile
Hutambulisha jamii.
miungu, wanyama,
Huhifadhi historia ya jamii.
binadamu.
Huelimisha/huipa jamii maarifa Hueleza sifa za Hueleza mianzo ya
ya kukabiliana na'changamoto na majagina. desturi.
kutambua inda na hila.
Vipengele vitano vya kuzingatia katika Huendeleza hadithi.
Huangazia maadili katika hadithi.
uchanganuzi wa hadithi:
Huburudisha.
Dhamira. Hili ni wazo kuu linalotawala
10. Semi ni utanzu wa fasihi simulizi kwa
katika hadithi. Ni lengo au nia
inayokusudiwa na hadithi. Dhamira sababu zifuatazo:
inaweza kuwa kuadilisha, kuonya, Zinatumia lugha kwa ubunifu. Kwa
kuasi, kuelimisha au kukashifu. mfano, methali hujengwa kwa tamathali
Maudhui. Hayani mambo yanayoelezwa nyingine za usemi kama vile kinaya na
katika hadithi. Kwa mfano, katika kejeli. Mifano:
mighani maudhui yanaweza kuwa sifa . Zingwizingwi lipe nguo utaona
kwa mashujaa; katika hekaya kuna mashauo —- kejeli/dhihaka.
maudhui ya ujanja/ulaghai. o Simba mwenda pole ndiye mla
Ploti. Huu ni mtiririko wa vitushi au nyama — kweli kinzani.
matukio katika hadithi kulingana na Semi hutumia lugha yenye taswira.
jinsi yanavyosababishana. Ploti katika Semi pia huwa na fanani. Kwa mfano,
hadithi ni ya moja kwa moja. vitendawili hutolewa na fanani.
Mandhari. Mandhari katika hadithi ni
Semi huwa na hadhira. Vitendawili
mazingira ya wakati, hali au kimaeneo.
hutolewa kwa hadhira ambayo hushiriki
Mandhari yanaweza kuwa ya kuogofya,
kwa kujibu. Aidha, methali, nahau na
yenye misitu na majitu au ya mawazoni.
misemo husemwa kwa hadhira fulani.
Wahusika. Wahusika katika hadithi
ni wa aina nyingi. Wanaweza kuwa Semi zina sifa za kuwa na utegemezi.
binadamu, wanyama, mazimwi au vitu
Hutegemea sanaa au tanzu nyingine
visivyokuwa na uhai. za fasihi simulizi kama vile hadithi au
Usimulizi. Hadithi inaweza kusimuliwa mashairi.
katika nafsi ya kwanza au ya tatu. Semi, kama fasihi simulizi nyingine,
Muundo. Hadithi huwa na muundo huwa na uwanja wa kutolewa. Kwa
maalumu wa ufunguzi, mwili na mfano, vitendawili hutolewa katika
hitimisho. vikao.
Lugha. Lugha katika hadithi ni ya moja Semi, kama fasihi simulizi nyingine,
kwa moja (sahili). Hata hivyo inaweza huzaliwa, hufa na hukua. Methali,
kuwa na tamathali kama vile methali, lakabu na misimu huzaliwa. Misimu
nahau, tashihisi au istiari. hukua na kuwa semi rasmi kama
Majukumu ya nyimbo katika uwasilishaji wa vile methali. Aidha, huweza kufa na
ngano: kusahaulika.
Nyimbo hutumiwa kuwasilisha ujumbe Humilikiwa na jamii. Methali
mzito katika hadithi. huhusishwa na jamii wala si mtu binafsi.
Hutenganisha matukio yanayojumuisha Hubadilika. Yaliyomo katika semi kama
hadithi. vile vitendawili hubadilika kulingana na
Huisisimua hadhira na kuiondolea maeneo na wakati ambapo vinatumiwa.
ukinaifu wa masimulizi makavu. Aidha, semi hubadilika kutegemea jamii
Huishirikisha hadhira katika utambaji. zilimozaliwa.
Hurefusha hadithi. Majibu sahihi yakubaliwe. Mifano ya
Ni kipumuo. Hupunguzia hadhira vitendawili ambavyo vinatumia:
uchovu au huzuni. Sitiari:
Huipa hadithi toni fulani. Kwa mfano, - Mamangu hachoki kunibeba
wimbo wa huzuni huipa hadithi toni ya —- Kitanda (Mama ni sitiari ya
huzuni. kitanda.)
Aa ——.

-. Bibihatui mzigo wake —- Konokono 11. Ingawa kimsingi vitendawili hutumiwa


(Bibi ni sitiari ya konokono.) kuburudisha, hasa watoto, vina majukumu
-. Nyumba yangu haina mlango -Yai mengine ya kijamii:
(Nyumba ni sitiari ya yai.) - Huwajuza wanajamii kuhusu mazingira
Gi) Urudiaji: yao kwani vitendawili huundwa kwa
-. Bakbandika bak bandua - Nyayo mambo yanayozunguka jamii.
(Neno bak limerudiwa.) - Hudhihaki na kukejeli watu, hali na
- Huku ng'o na kule ng'o - Giza tabia hasi katika jamii.
(Neno ng'o limerudiwa.) - Hukuza ubunifu. Wanajamii hujifunza
(iii) Mchezo wa maneno: kulinganisha vitu katika mazingira
Ukiona 'njigi' utadhani 'njege' na ukiona yao ili kuunda vitendawili na kubaini
'njege' utadhani 'njigi' —- Maziwa na majibu.
tui (Kuna kuchezea 'njege' na 'njigi'.) - Hukuza uzalendo. Watu huonea fahari
Maneno haya yana sauti ambazo vitendawili vya jamii yao.
zinakaribiana. - Huhimiza utangamano.
(iv) Tanakali za sauti: - Huimarisha uwezo wa kukumbuka.
- Hukuza stadi ya kufikiri harakaili kupata
- Huku 'i!', kule 'pi! — Mkia wa
jibu. Hutumiwa kama chemshabongo.
kondoo atembeapo. - Huhimiza tabia ya kudadisi/kuuliza
-. Prr! hadi Makka - Utelezi. maswali kuhusu chanzo cha jambo.
-.
Tang! Yaanguka - Sarafu. - Hukuza lugha.
(v) Dhihaka/kejeli: 12. (a) (ii) Kweli kinzani/ukinzani -
- Mtani wangu hata akiishi majini hatutarajii mtu/kitu kufuma bila
hatakati — Chura. mshale.
-. Wafu wanakokotana - Jahazi na (ii) Taswira — picha ya watoto
tanga. kumzunguka mtu.
-. Warembo wangu wamevaa sare — Sitiari > mgomba kulinganishwa
Kumbikumbi. moja kwa moja na mtu/mnyama.
- Mama mtu mweusi mtoto Tashihishi - mgomba kupewa sifa
mwekundu - Pilipili. ya kukaa na kuwa na watoto.
(vi) Taswira: (iii) Dhihaka — unyasi kuitwa mti ilhali
- Adui tumemzingira lakini ni mdogo mno.
hatumwezi —- Watu wanaoota Chuku — unyasi unapewa sifa za
moto. ukubwa wa mti.
- Wanatazamana tu lakini (iv) Sitiari — kiganja kinafananishwa
hawaamkiani —- Ardhi na mbingu.
moja kwa moja na mfalme.
- Wazee wamesimama na vijana Chuku — kiganja kinapewa sifa ya
wanapita — Mawe na maji.
ufalme na hali ni kidogo.
- Nyama nje, ngozi katikati na
Tashihisi — kiganja kupewa sifa
mchanga ndani — Firigisi ya kuku.
za binadamu za kuwa mfalme na
(vii) Ukinzani:
kulindwa.
- Useja wangu mrefu lakini hautiliki (b) Mazingira rasmi ya kutoa vitendawili:
shingoni — Siafu.
- Katika kutoa hotuba.
-. Nameza lakini sishibi —- Mate.
- Katika vikao rasmi vya kutamba
-. Nina shamba langu kubwa lakini ngano, labda mwishoni au
nikilivuna halijai hata kofi —
mwanzoni.
Nywele.
WAA

- Katika vikao rasmi vya utoaji —- Ukupigao ndio ukufunzao.


wa mawaidha. Mtu mkaidi, -. Mwenye kelele hana neno.
kwa mfano, anaweza kupigiwa (b) Sitari:
kitendawili ili kumkashifu kwa - Ahadi nideni.
tabia yake.
- Kukopa harusi kulipa matanga.
-. Vitendawili pia hutolewa katika
(c) Urudiaji/Takriri:
vikao rasmi vya mashindano.
- Bandubandu huisha gogo.
13. (a) Majibu sahihi yakubaliwe. Mifano ya
—-. Chelewa chelewa utapata mwana
methali zinazoainishwa pamoja kwa
kuzingatia maudhui ya malezi: si wako.
- Mcha mwana kulia hulia (d) Maswali ya balagha:
mwenyewe. -. Maviusoyala wayawingiani kuku?
-. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo. -. Pilipili usiyoila yakuwashiani?
-. Udongo uwahi uli maji. (e) Stihizai/Dhihaka/Kejeli:
Samaki mkunje angali mbichi. - Zingwizingwi lipe nguo utaona
(b) Kuonya dhidi ya tabia hasi: mashauo.
- Aliyekupawewekiti ndiye aliyenipa - Kichwa cha nyoka hakibandikwi
mimi kumbi. mtungi.
- Usione kwenda mbele kurudi - Kichwa cha kuku hakistahimili
nyuma si kazi. kilemba.
- Asiyesikia la mkuu huvunjika guu. - Maskini akipata matako hulia
(c) Methali zinazoonyesha kinaya: mbwata.
- Hindi ndiko kwenye nguo na Stihizai/Kejeli — inamkejeli mtu
waendao uchi wako.
16. (i)
aliyejisababishia matatizo.
- Asante ya punda ni mateke. Chuku - maji kwenye kifuu ni
14. Tofauti kati ya methali na vitendawili kwa kidogo sana, ilhali yanaonekana
kuzingatia: kama bahari kwa chungu.
(i) Muundo - Vitendawili vina fomyula (c) Tashihisi - maneno yanapewa
maalumu ya uwasilishaji. Kwa mfano: uwezo wa kumtoa nyoka pangoni/
Fanani: Kitendawili! maneno humbadilisha mtu.
Hadhira: Tega!
(d) Kinaya —- mkakasi unapendeza
Fanani: Huku ng'o na kule ng'o!
kwa sura ya nje, lakini kwa ndani
Hadhira: Giza. ni kipande tu cha mti.
Kwa upande mwingine, methali kwa Urudiaji/takriri — neno chelewa
(e)
kawaida huwa mshororo mmoja ambao
limerudiwa.
una vipande viwili au kimoja. Kwa
mfano, Mwenye nguvu/mpishe, Haba na (£) Kinaya —- binadamu anamdunga
haba/hujaza kibaba. nguruwe kwa kigumba na hali yeye
akifanyiwa hivyo anaona uchungu.
(ii) Jukumu - Kwa kawaida, jukumu la
kimsingi la vitendawili ni kuburudisha Binadamu anawatendea wengine
ilhali kimsingi, methali hutumiwa maovu ilhali yeye akitendewa
kuelimisha, kuonya na kuadilisha. maovu hayo ataona vibaya.
15. Majibu sahihi yakubaliwe. Mifano ya methali (g) Istiari — moshi unatumiwa
zinazoundwa kwa: kurejelea ujana.
(a) Kweli kinzani: (h) Tanakuzi - tamu na chungu ni
- Kuinamako ndiko kuinukako. maneno ya kinyume.
AA.
(i) — Swali la balagha Usiache ubaharia kwa unahodha.
—- Kejeli/Dhihaka - inakejeli Bura yangu siibadili na rehani.
watu ambao hupenda (£) Jambo jema huja kwa kufanyiwa kazi:
kumzika maiti kwa jeneza la
Ukiona vyaelea jua vimeundwa.
kifahari ilhali hawakumsaidia
Ukitaka kuvua nguo huna budi
akiwa hai. Pia inakejeli
kuchutama.
hali ya kumsaidia mtu
wakati ambapo mtu huyo Mtaka cha mvunguni sharti
ameathirika sana na msaada ainame.
huo hauna faida kwake tena. (8) Kuonya dhidi ya kuamini marafiki sana:
ND Tashihisi — nyani na Kikulacho ki nguoni mwako:
kima kupewa uwezo wa Ibilisi wa mtu ni mtu.
kuzungumza na binadamu Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa
—. Sitiari — nyani na kima ni nawe.
sitiari ya marafiki wa karibu (h) Kukashifu tabia ya binadamu ya
au watu wenye uhusiano wa kujifikiria kwanza jambo jema
karibu. linapotokea:
(ii) Methali sahihi zikubaliwe. Kwa mfano: Kila mwamba ngoma ngozi
(a) kuhimiza kutokata tamaa: huivuta kwake.
- Kulima mavune, kuvuna vicheko. Mchuna ngozi huvutia kwake.
—. Papokwa papo kamba hukata jiwe. 17. (a) Dhima ya lakabu:
—. Kibuzi na kibuzi hununua jahazi. Kusifu tabia njema — mwenye tabia
-> Kenda karibu na kumi. nzuri hubandikwa jina zuri.
(b) Kufariji: Kukashifu tabia hasi — mwenye
” Riziki ya mwanadamu imo tabia hasi hubandikwa jina baya.
maishani. Kutambua mchango wa mtu kwa
- Mauti ni faradhi. jamii.
-—. Kifo hakimjui mfalme. Hutambulisha mhusika - Lakabu
- Kifo na kiumbe, kiumbe na kifo. ni muhtasari wa sifa za mhusika.
Kusifu tendo jema: Kutasfidi lugha - Mtu
” Jina jema hung'aa gizani. anayeheshimiwa hubandikwa
- Wema hauozi. jina la heshima.
-. Mcheza kwao hutuzwa. Huficha utambulisho wa mtu.
(ad) Kuhimiza udugu: Watani hubandikana majina
—. Ndugu mui heri kuwa naye. kuondoa urasmi na kukuza
-Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa uhusiano wa karibu.
nawe. (b) Dhima ya misimu:
”. Ndugu chungu, jirani mkungu. Huhifadhia siri.
(e) Umuhimu wa kuthamini vitu vyako: Hukuza uhusiano bora.
-” Usiache mbachao kwa msala Kukuza utangamano na
upitao. uzalendo. Watu huonea fahari
” Kuku akiacha wana ana mayai kundi lao kwa kuwa na msimbo
tumboni. unaowaunganisha.
- Kibaya chako si chema cha Hutambulisha kundi.
mwenzio. Hutasfidi lugha —- Badala ya
- Mwacha kiwi hanacho na chake kutumia msamiati wa aibu au
kimpotele. wenye makali misimu hutumiwa.
AAA
WA

- Hukuza lugha zaidi. Misimu Bembea—Nyimbo zakumbembeleza


huweza kukubaliwa kama mtoto.
msamiati rasmi wa lugha. - Sifo— Nyimbo za kusifu.
- Huongeza ladha katika lugha. - Hodiya — Nyimbo za kazi.
Maneno yale yale hupewa maana - Wawe- Nyimbo za kazi za kilimo.
tofauti. - Kimai— Nyimbo za kazi ya uvuvi.
- Huhifadhi historia na utamaduni - Nyimbo za mapenzi.
wa jamii. Misimu huweza
- Nyimbo jadiiya.
kubuniwa kufuatia matukio
muhimu ya kijamii. (b) Majukumu ya
- Huondoa urasmi katika (i) Sifo:
mazungumzo. - Husifu tabia chanya (nguni).
- Husawiri mpangilio wa jamii fulani - Huonyesha mchango wa
kiuchumi na kijamii. anayesifiwa.
(c) Vitanza ndimi: - Huwezakutumiwa kama rekodi ya
- Huboresha matamshi. matukio ya kihistoria, kwa mfano
- Huburudisha. Ucheshi huibuliwa wimbo unaomsifu shujaa fulani.
kwa kushindwa kutamka ipasavyo. - Hutambulisha msimamo wa jamii
- Huimarisha uwezo wa kufikiri kuhusu baadhi ya masuala.
haraka. - Huonyesha mahusianao katika
- Hukuzaubunifu. Msanii huhitajika jamii.
kuteua kiubunifu maneno - Huhimiza uzalendo.
yanayokaribiana kimatamshi. - Huburudisha.
- Hukuza ufasaha wa lugha (ii) Hodiya/Nyimbo za kazi:
kutokana na umilisi wa makosa - Huadilisha kwa kuhimiza bidii.
ya kimatamshi katika lugha. - Hukuza utangamano/ushirikiano.
- Hutambulisha jamii. - Hutambulisha jamii na shughuli
18. Jamii inayorejelewa itajwe kwanza. Miktadha zake za kiuchumi.
ambapo ushairi simulizi ulitolewa unaweza - Hukashifu tabia hasi, kama vile
kuwa: uvivu.
Kazini — Nyimbo za kazi. - Huonyesha imani na mtazamo wa
Kwenye miviga jandoni, harusini, jamii kuhusu kazi.
mazishi. - Huonyesha matatizo ambayo
Sherehe za kutawazwa kwa viongozi wafanyakazi hukumbana nayo
kama vile watemi. kazini.
Shughuli za posa. - Huwatia moyo wanaofanya kazi
Panapotolewa mawaidha. wasikate tamaa.
Vitani. 20. (a) Sifa za tendi:
Shughuli za ibada na utoaji kafara. - Tendi ni tungo ndefu za kishairi
Katika sherehe za makumbusho. zinazosimulia matukio muhimu
Katika sherehe za kisiasa. ya kihistoria.
19. (a) Aina za nyimbo: - Tendi husimulia maisha ya
-. Mbolezi— Nyimbo za kuomboleza. mashujaa kama vile waanzilishi
wa madhehebu.
-. Nyimbo za dini.
—-. Tendinyingi huchanganya historia
—- Nyimbo za siasa.
na visasili (mambo ya kidini/
- Nyiso —- Nyimbo za jandoni au
kiimani). -
unyagoni.
Aa ——...

- Baadhiyatendi hulenga kuadilisha. Huonyesha thamani na mitazamo ya


— Huhusishwa na muktadha (hali) jamii kuhusu masuala mbalimbali.
fulani wa kijamii kama vile ufalme Husifu tabia chanya na kukashifu tabia
au vita. hasi.
- Kwa kawaida, hutolewa katika Ni nyenzo ya kupalilia kipawa cha
miktadha rasmi au inayohusiana uongozi kupitia kwa uigizaji.
na viviga. Huimarisha urafiki, kwa mfano
Tendi, kama ushairi mwingine, malumbano ya utani.
hutumia lugha ya kiwango chajuu Uigizaji huimarisha uwezo wa
cha usanii. kukumbuka.
- Mambo yanayosimuliwa katika Huadilisha. Watazamaji hujifunza
tendi hupigwa chuku. kujihusisha na wahusika nguli na
- Hupokezwa kutoka kizazi kimoja kupuuza wahusika hasidi.
hadi kingine. Hukuza ujasiri wa kuzungumza
(b) Sifa za rara: hadharani.
- Nihadithi fupi nyepesi za kishairi 22. Sifa za fanani katika fasihi simulizi:
ambazo husisimua. Ni jasiri.
- Huweza kuwasilishwa kwa Ana uwezo wa kutumia lugha kwa
kuandamana na ala za muziki. ufasaha kulingana na hadhira, hivyo
-. Rara nyingi simulizi zilihusu koo kuiwezesha hadhira kuelewa maudhui
tukufu/zilizotajika kama vile za anayowasilisha.
wafalme au viongozi wa kijamii Ni mbunifu. Huuwasilisha utanzu kwa
na kidini. mitindo ya kuivutia hadhira.
- Kwa kawaida rara hutolewa kwa Ni mcheshi. Huchekesha hadhira yake.
toni ya kitanzia (huzuni). Ni mwigizaji bora. Huiga toni,
-. Masuala hufumbwa na kudokezwa sauti na kiimbo kulingana na suala
tu. analowasilisha.
> Lugha yake hujaa utendaji wa Huchota mifano kutoka kwa mazingira
matukio. ya hadhira yake.
> Raranyingihushughulikia masuala Hushirikisha hadhira katika kazi yake.
ya kawaida na ibuka kwa mtindo Huelewa utamaduni wa hadhira yake na
usio rasmi. kuulinda.
- Baadhi ya rara huwa na ucheshi 23. Umuhimu wa maigizo ya watoto:
wenye kinaya. Hukuza udugu na ushirikiano miongoni
- Rara nyingi husimulia mambo mwa watoto. Watoto hucheza pamoja
ya kubuni japo zipo nyingine bila kujali tofauti zao za kijamii.
zinazosimulia mambo ya kweli. Hukuza ubunifu. Watoto hubuni
21. Umuhimu wa maigizo katika fasihi simulizi: michezo yao.
Huburudisha. Huimarisha uwezo wa kukumbuka.
Hukuza kipawa cha ubunifu. Watoto huhitajika kukumbuka matendo
Hutambulisha jamii — kila jamii ina aina ya watu wanaowaiga.
yake ya maigizo. Ni kitambulisho cha jamii. Watoto
huigiza yale wanayoyaona katika jamii
Huhifadhi utamaduni na historia ya
zao.
jamii. '
Hupitisha maarifa.
Huimarisha ushirikiano.
Ni kiburudisho na njia nzuri ya watoto
Hupitisha maarifa.
kupitisha muda.
Huwafunza watoto majukumu yao ya Kuzindua.
utu uzima. Kutangaza kaulimbiu za vyama vya
Hupalilia kipawa cha uongozi. Watoto upinzani au vyama tawala.
wanapochukua nyadhifa za kuwaelekeza - Kueneza propaganda za kisiasa.
wengine michezoni, wao huimarisha —- Kusifu viongozi waadilifu.
stadi za uongozi. - Kuimarisha uzalendo miongoni
Hukuza kipawa cha uigizaji. Watoto mwa wanajamii.
hujizoesha kuigiza wakiwa wadogo. - Kuadilisha.
Huwapa watoto ujasiri na kujiamini. - Kukuza umoja miongoni mwa
Kadiri wanavyoigiza ndivyo wanajamii. Kwa mfano, nyimbo
wanavyokakamaa na kujiamini zaidi. za taifa huhimiza umoja.
Umuhimu wa vichekesho: - Huonyesha migogoro kati ya
Huburudisha. watawala na watawaliwa.
Hukashifu tabia hasi. - Hutambulisha jamii kwa
Hukuza ubunifu. kuonyesha mfumo wake wa
Hukuza ujasiri wa kuzungumza kisiasa.
hadharani. - Huonyesha matarajio ya
Huadilisha. Vichekesho hufunza watawaliwa kwa viongozi.
uvumilivu na umuhimu wa kuwaza
Huonyesha historia ya jamii
kabla ya kutenda.
husika.
24 Ni wimbo wa kisiasa. Umetaja kura na - Huburudisha.
ubunge.
25. (a) Mbolezi ionyeshe huzuni. Tazama mfano:
(b) Mbinu za lugha zilizotumiwa: Ni
—- Sitiari — vifaranga ni istiari ya Walisema walosema
watoto. Kitali hakina macho
- Maswali ya balagha —- ubeti wa Huvizia wapendwa
kwanza — Siwe uloambia akina Kikafakamia
mama ... njaa isiwaangamize?
Kwenye kinywa kisochoka
Ubeti wa pili — Siwe ulopita Chumvi
Kwa mara nyingine hasidi
na Sukari kuturushia ja samadi?
ametudhalilisha
Uhitaji wetu ukatutuma ... kura
Amewapukutisha wanetu
ukapata?
Majagina kupiga busu la sime
- Tashbihi - Chumvi na sukari
Jeshi letu sasa ni mateka
kuturushia ja samadi?
Wasaliti wamewapa mahasimu
-. Tashihisi— uhitaji wetu ukatutuma
(uhitaji umepewa uwezo wa Cheko la kutucheka
kutuma). Ni kilio ni kilio, ni kilio Tungamo. g
- Usambamba- siwe uloambia akina (b) - Rara ionyeshe shairi jepesi
mama ... siwe uliopita ... linalohusu mapenzi. Liandikwe
(c) Mnyonge/mpigakura mwanamke ndiye kwa mtindo wa masimulizi, japo
anayezungumza. ni shairi. i
(d) Wimbo una toni ya kusuta. Nafsineni/ Tazama mfano:
mzungumzaji analalamikia usaliti wa
Nalitazama jua likichwa,
mbunge wao na kumsuta kwa vitendo
Matumaini yangu yakizama pamoja
hasi.
na miale miekundu
(e) Umuhimu wa nyimbo za siasa:
Nalidhani lilikuwa jinamizi tu
- Kukashifu uongozi dhalimu.
Kwamba ulikuwa kesha n'acha (d) Fani:
Walikuwa wameisha n'ambia Mawaidha yanayotolewa katika
walimwengu miktadha rasmi huwa na sehemu tatu
Ela nilikataa katakata walosema kuu ambazo ni utangulizi, mwili/kati/
Nikajitia kuamini waloamba yalikuwa yaliyomo na hitimisho.
uzushi 27. Miktadha ambamo ulumbi hutumiwa:
Hadi siku hii nilopokea waraka, Katika mijadala bungeni.
Waraka ambao ulikuwa jeneza la kuziki Katika hotuba za kisiasa.
Pendo letu la miongo miwili. Katika mahubiri maabadini na mitaani.
Linaweza pia kuonyesha masikitiko Katika mijadala shuleni.
baada ya kusalitiwa au kusifu mpenzi. Kortini, wakili anapomtetea mshtakiwa/
mshtaki.
Tazama mfano: Katika shughuli za kijamii kama vile za
Siku uliponambia, 'Yamekwisha' posa.
Nilidhani ulikuwa utani Katika hotuba kwenye mazishi.
Nilitaka kukusahau Katika sala/dua.
Ela moyo ulikataa Katika utoaji wa maapizo.
La, moyo haukukataa, Katika malumbano ya utani.
Kwani moyo wenyewe Katika majigambo/vivugo.
Mwenzio sikuwa nao, 28. Tofauti kati ya ngoma na ngomezi:
Ulikuwa kesha wiba -. Ngoma ni uchezeshaji wa viungo
Miaka kumi ilopita vya mwili kwa kufuata mdundo wa
muziki au mpigo wa ala ya muziki
26. Sifa za mawaidha kwa kuzingatia: kama vile ngoma.
(a) Hadhira: - Ngomezi ni fasihi ya ngoma
Mawaidha hutofautiana kulingana na ambapo mapigo ya ngoma
hadhira. Kuna mawaidha yanayotolewa huwasilisha ujumbe wenye maana
maalumu. Kwa mfano, katika
kwa wasichana, wavulana, wazee,
baadhi ya jamii mapigo matatu
vijana, walezi, wazazi au maarusi pekee.
ya ngoma katika jamii fulani
(b) Fanani:
huashiria kuzaliwa kwa mtoto wa
Mawaidha hasa hutolewa na watu kiume na mawili mtoto wa kike.
wenye umri mpevu. Kwa mfano, wazee (b) Aina za miviga:
huwatolea mawaidha vijana. Walio na - Jando/Unyago
maarifa zaidi katika taaluma huwapa - Harusi/Ndoa
mawaidha wale wanaohitaji ushauri.
-. Matanga
(c) Maudhui: -. Mazishi
Maudhui ya mawaidha ni mengi - Sherehe za ulaji viapo
na hutegemea muktadha ambamo
-. Matambiko
yanatolewa na lengo la kutolewa.
- Sherehe za kutawazwa kwa
Mawaidha hushughulikia maudhui
viongozi gi
kama vile malezi, dini, uongozi, siasa,
-. Sherehe za kuzaliwa kwa mtoto
ndoa na mapenzi/unyumba, jinsi ya
- Shughuli za posa
kukabiliana na ujana.au mahusiano ya
- Ibada
kijamii.
- Arusina ndoa
Maudhui mengine yakubaliwe.
- Shughuli kufukuza pepo
Aa
WA

- Shughuli kabla ya kuanza kazi Ni muhimu kutafiti kuhusu fasihi


fulani kama vile ujenzi. simulizi ili kusahihisha mawazo potofu
kuhusu baadhi ya tanzu na vipera vya
(i) Malumbano ya kiukoo: Mifano
fasihi simulizi.
ya wanafunzi ihakikiwe. Tazama
mfano ufuatao: 30. Umuhimu wa kufunza fasihi simulizi katika
shule za sekondari:
Ukoo wenu ni wa waoga kiasi kwamba
Fasihi simulizi huadilisha.
mtu akiona kivuli chake mchana
hukimbia akidhani anafukuzwa! Kupitisha thamani za jamii kwa vizazi.
(ii) Malumbano kati ya maumbu: Kuwapa wanafunzi maarifa ya
kukabiliana na chamgamoto za maisha.
Mifano ya wanafunzi ihakikiwe. Kwa
mfano:
Kuwatambulisha wanafunzi kwa
mazingira yao.
Wewe unajifanya jasiri na juzi
baba alikukemea kidogo tu Kupitisha utamaduni na historia ya
ukaanza kutetemeka kama kondoo jamii kwa wanafunzi.
aliyenyeshewa. Kuwaonya na kuwakosoa wanajamii.
(iii) Malumbano ya bibi na mjukuu: Kukuza utangamano na mshikamano .
Mifano ya wanafunzi ihakikiwe. Kwa wa kijamii.
mfano: Kukuza stadi za lugha kama vile
Ee mume wangu, mbona walala kusikiliza na kuzungumza.
mapema hivi? Utawezaje kulilinda Ni nyenzo ya burudani — kwa mfano,
boma letu ikiwa wewe ndiwe wa kupitia maigizo, nyimbo na vitendawili.
kwanza kujizika kitandani? Hueneza matarajio ya jamii kwa vijana/
(iv) Malumbano ya marika wanajamii.
Mifano ya wanafunzi ihakikiwe. Kwa Hujenga tabia ya kudadisi/kuchunguza/
mfano: kuuliza maswali kuhusu mambo. Kwa
Wewe ni mweusi kiasi kwamba mfano, kupitia kwa vitendawili, mtu
ukiingia chumbani taa zinazimika! hujifunza kuchunguza na kufananisha
vitu ili kupata jawabu.
29. Umuhimu wa ukusanyaji wa data za fasihi Hupanua ujuzi wa masuala ibuka kupitia
simulizi: kwa masimulizi, mashairi na semi
Husaidia kurekodi fasihi simulizi, hivyo zinazohusu mambo mbalimbali.
kuirithisha kwa vizazi vijavyo. 31. (a) Kimuundo ni shairi. Unaweza pia
Husaidia kuibua sifa za kimsingi za kuchukuliwa kama utendi (shairi la
vipera vya fasihi simulizi kwa kuviona ushujaa) kwa sababu unazungumzia sifa
vikitendwa. za shujaa na vita alivyopigana.
Husaidia kulinganisha fasihi simulizi za Kimaudhui ni sifo/wimbo wa sifa —
jamii mbalimbali na kuonyesha tofauti unamsifu shujaa.
zake.
Matokeo ya utafiti wa nyanjani kuhusu
(b) (i) Matukio ya ajabu kama vile:
-. Kusema na miungu alipozaliwa.
fasihi simulizi hutumika kuziba
- Anayesema ana nguvu za kipekee
mapengo ya utafiti yaliyopo.
japo ni kilema.
Ukusanyaji na uhifadhi huendeleza
fasihi simulizi kwa vizazi vijavyo. - Anayesema kazaliwa akishika
Utafiti kuhusu fasihi simulizi unaweza mkuki.
kuonyesha mabadiliko katika maudhui (ii) Matumizi ya chuku kama vile:
na fani za fasihi simulizi na kuvifunza - Maadui elfu kufa anaposhika
vizazi vya sasa na vya kesho. silaha.
(iii) Ni wafugaji — Kutupoka mifugo.
la kiganja chake.
Anayeimba ni mama. Anasema
(iii) Utungo unahusu shujaa wa vita — nilipokuopoa.
amepigana vita vingi visivyohesabika.
(iv) Anayesemwa amezungukwa na Ina mwanzo maalumu, “Hapo
migogoro — mahasidi waliochukua zamani za kale' na mwisho
maalumu - “Huo ukawa mwisho
mashamba na wasaliti.
wa urafiki wao.” j
(v) Utungo umechanganya historia na
Ina wahusika wanyama - Sungura
mambo ya kidini — anazungumza na
na Fisi.
miungu anapozaliwa — haya ni mambo
ya kiimani. Ploti ni nyepesi — inatiririka moja
kwa moja.
(ce) Yi) Kejeli/stihizai — anaitwa jana la' Kuna dayolojia kati ya Fisi na
ajabu. Sungura.
(ii) Chuku: Kuna fantasia — mvua inanyesha
- Kijiji kizima kuja kuona na mazao yanajaa mara moja.
mtoto. Inaadilisha — tusiwaamini marafiki
- Maadui elfu kufa kwa wanafiki.
anayesemwa kushika silaha. Ina sehemu tatu: mwanzo “Hapo
”. Mwili kuwa na nguvu za zamani ...”, kati, na mwisho ... huo
majagina mia moja. ukawa mwisho wa urafiki wao ...
(iii) Ritifaa — anazungumza na
Kuna matumizi ya wimbo - wimbo
mahasidi ambao hawapo kana wa Fisi.
kwamba wapo.
(b) Hurafa. Ina wahusika wanyama:
(iv) Tashbihi: Sungura na Fisi.
-”> Maadui wamwonapo
Ni ngano ya kiayari. Sungura
hutetemeka kama jani.
anamhadaa Fisi.
> Kuwayeyusha kama barafu.
Ni ngano ya usuli. Inaeleza chanzo
(v) Sitiari: ” cha uadui kati ya Fisi na Sungura.
> umekuwa nahodha.
Ngano inaonya dhidi ya kuamini
- Akili yako sumaku. marafiki bila kutafakari zaidi.
(vi) Usambamba: Inaonya dhidi ya usaliti. Urafiki
- Likalovya changu kidari.
kati ya Sungura na Fisi unakatika
-. Likanavya chako kipaji.
kwa sababu ya usaliti wa Sungura.
(vii) Taswira:
”. Mama alivyolia na kujilovya (d) (i) Uhuishi au tashihisi:
machozi na kumlovya -> Maghala yanatajwa
mwanawe. kulalamikia shibe (kujaa
- Alivyopigana na utawala chakula).
”. Mvua inapewa uwezo wa
kizima kinavyomiminika kuwa na hiari ya kukataa
kwake nyumbani.
Waume huoa wake wengi —
Anasema, Uke wenza ukamhimiza (ii)
kuchukua buruji kueneza habari. na Fisi awali waliishi kwa utulivu,
Vilema walitupwa kichakani - walipata neema na mavuno mengi.
Ilosema kwa moja kauli utokomezwe (iii) Nahau. Kula mate —- kukaa bila
chakani utupwe. chakula.
(iv) Ndoto. Sungura alidai kuwa aliota. Unaonyesha nguvu za Muumba —
(v) Dayolojia — Fisi na Sungura kifo ni faradhi.
wanazungumza. Unaonyesha imani kuhusu chanzo
(vi) Maswali ya balagha - kumbe cha kifo - uchawi.
Sungura hakumtoa kafara mama (b) —-— Ni washirikina. Mshairi anasema
yake? atabaki kusaka aliyesababisha
(vii) Kinaya - Sungura ambaye ni rafiki ndwele ya mpenziwe.
ya Fisi kumtaka Fisi kumuua Wanaamini kifo husababishwa
mama yake na hali yeye Sungura na matendo ya watu wabaya.
hamuui mama yake. Anasema Ama jicho la hasidi
(viii) Uzungumzi nafsi — Fisi limekuangaza, jamani?
anazungumza na nafsi yake: Wanaamini katika nguvu za
“Kumbe Sungura hakumtoa kafara majaliwa — “kifo ni faradhi'.
mama yake? Kumbe maneno yake
Ritifaa —- mpenzi anazungumza na
yote yalikuwa ulaghai ili mimi Fisi
aliyekufa kana kwamba yu pale.
nimtoe kafara mama yangu na
kuiauni familia ya Sungura!” Taswira — shairi zima limejaa picha
ya huzuni/ukiwa.
33. (a) Ni mbolezi kwa sababu:
Balagha —- Kumbe mwenzangu
Imetumia lugha hisishi — inaibua
kaniacha?
hisia nzito za huzuni.
Tashihisi —- Ukiwa ulinivaa.
Mshairi anataja Ziraili — Malaika
wa kifo — kifo kimetokea. Kejeli/stihizai—kaburilinarejelewa
Toni ya huzuni inadhihirika katika kama kasri la shakawa.
shairi zima. Kwa mfano, mshairi (vi) Mbinu rejeshi —- mwimbaji
anasema alivaliwa na ukiwa. anakumbuka siku ya kufunga
Ni ushairi/wimbo kwa sababu ndoa.
umegawika katika beti. (vii) Sitiari — kifo kinafananishwa moja
Unataja sifa nzuri za marehemu. kwa moja na nduli.
Mshairi anazungumza moja kwa (d) Mjane/aliyefiwa.
moja na marehemu.
Marejeleo

Akivaga, S. 8: Odaga, A. (1982). Oral


Literature:A School Certificate Course.
Nairobi: Heinemann
Allen, J. de Vere (1977). Al-Inkishafi:
Catechism ofa Soul. Nairobi: East Afric
an Literature Bureau.
Bukenya na wengine (1997). Oral Liter
ature, A Senior Course. Nairobi: ME
TA
Finnegan, R. (1971). Oral Literature in Afric
a. Ozford: Ozford University Press.
Hichens, W. (1972). Al-Inkishafi: The
SoulsAwakening. Nairobi: OUP.

Knappert, J. (1979). Myths and Legends of


the Swahili. Nairobi: EAEP.
Kyovi, P. (2010). Kipendacho Roho.
Nairobi: OUP.

Miruka, 0. (1999). Studying Oral Literature


. Nairobi: Acacia Publishers.
Mkota, A. (2009). Kamusi ya Methali: Maan
a na Matumizi. Nairobi: Vide-Muwa Publi
shers.
Msokile, M. (1992). Kunga za Fasihi na Lugha
. Dar es Salaam: Educational Publishers
and Distributors.
Mugenda, 0.8 Mugenda, G. (1999).
Research Methods: Ouantitative and Ouali
tative Approaches. Nairobi:
Acts Press.

Mulokozi, M.M. (1996). Fasihi Simul


izi ya Kiswahili. Dar es Salaam: Chuo
Kikuu cha Tanzania.
— (1999). Tenzi Tatu za Kale. Dar
-es Salaam: TUKI.

Myers, J. 8: Simms, M. (1985). The Long


man Dictionary of pogtic terms. White
Plains: Longman.
Murray, P. (1978). Literary Criticism:A
Glossary of Major Terms. New York: Long
man Inc.
Nassir, A. (1971). Malenga wa Mvita
. Nairobi: OUP.

Rukwaro, R. (2007). Fundamentals


of Social Research. Meru: Eureka Publi
shers.
Syambo, B Mazrui, A (1992). Uchambuz
i wa Fasihi. Nairobi: EAEP.

TUKI (1976). Fasihi Simulizi ya Mtanzani


a: Vitendawili 1. Dar es Salaam: TUKI.
— (1983). Makala za Semina ya Kimat
aifa ya Waandishi wa Kiswahili Ill-F
asihi. Dar es Salaam: TUKI.

Wamitila, K.W.(2003). Kichocheo cha


Fasihi Simulizi na Andishi. Nairobi:
Focus publishers.
Sawa yai
SE Kaa TAWALA Ba AA

Simuliz
aa | ” gi - ” UA IA

kwa shule
za Upili

FaniyaFasihiSimulizi kwa Shuleza Upili kimeandikwa


kwanengo Ma kumfafanulia. mwanafunzi, tanzu.na vipera
vya fasihi.simulizi kwa njia Angavi-nanyepesi;

Mdhitajiyote yasilabasi yashuleza upili yameshughulikiwa


kwakina:

Madazimejadiliwa kwa lugha rahisi namifanoanuwai ya.


uchanganuzi kutolewa:

Yapomaswali yaliyotolewamwishonimwa mada, Maswali;


haya Yandtahiniistadi zote, za ufumbuzi Mwishoni.mwa
kitabu kumetolewa majibu” yatbaadhilya maswali ya
mazoezi. ;

Assumpta” K-Matei ni mwalimu mwenye tajriba pana


katika ufundishaji wa? Kiswahili; Pia 'ameandika vitabu
kadha'vyakufunzim lugha nafasihuya Kiswahili:

OKFORD
. i

UNIVERSITY PRESS ;

www.onford.co.ke 73654

You might also like