Professional Documents
Culture Documents
Kiswahili STD 4 - Kiongozi Cha Mwalimu
Kiswahili STD 4 - Kiongozi Cha Mwalimu
Kiswahili STD 4 - Kiongozi Cha Mwalimu
Darasa la Nne
ISBN: 978-9976-61-735-1
ii
iii
iv
1. Msamiati
Ni jambo muhimu kuhakikisha kuwa, wanafunzi wanafahamu maneno
yote mapya na kuyatumia katika sentensi. Msamiati ufundishwe kwa
kutumia vitu halisi, picha na vielelezo, maelezo, vitendo, maigizo na
onesho. Kwa hiyo, huna budi kutayarisha zana za kutosha za kufundishia
hasa zinazopatikana katika mazingira yako. Vidokezo vifuatavyo ni
muhimu:
(a) Kutumia vitu halisi
Ni muhimu utumie vitu halisi katika kufundisha msamiati kwa
kuwa wanafunzi wanapoona wanaelewa kwa urahisi.
2. Miundo
Muundo ni mpangilio wa maneno na uhusiano wake katika sentensi.
Katika muundo mmoja inawezekana kutunga sentensi kadhaa zenye
maana tofauti.
Katika kitabu cha mwanafunzi alama za “____” na “……..” zinatumika
kuonesha miundo. Alama ya “____” huonesha kuwa neno halijakamilika.
Alama ya “……” huonesha kuwa neno au maneno hayapo. Katika
miundo nafasi hizo zinatakiwa zijazwe. Nafasi ya “____” itajazwa na
sehemu ya neno na “……..” itajazwa kwa neno au maneno. Waongoze
wanafunzi kujaza nafasi hizo. Kwa mfano:
(a) Muundo
ana____ inaweza kujazwa na kuwa: analima, anasoma,
anaimba, anatembea na kuendelea.
vi
vii
viii
ix
xi
xii
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; mshereheshaji, mahafali, alfajiri,
wasili, alasiri, tumbuiza, adhuhuri na hitimu kwa kutumia
mbinu ya maelezo, vitendo, maigizo na nyimbo.
(b) Andika maneno hayo ubaoni kisha wanafunzi wayasome
na kueleza maana ya neno mojamoja.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo. Andika sentensi hizo ubaoni.
(d) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(e) Waambie wanafunzi watunge sentensi kwa kuandika.
(f) Sahihisha kazi za wanafunzi na kufanya masahihisho
darasani.
Somo la 9 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutaja vyombo mbalimbali vya usafiri
na sifa zake kwa mfano; baiskeli, ndege, pikipiki, gari, treni
na meli.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 7 kwa kutoa mfano
ulio katika kitabu cha mwanafunzi ukurasa wa 10. Unaweza
kuongeza mifano mingine.
(c) Waongoze wanafunzi waandike majigambo kwa kutumia
vyombo viwili vya usafiri.
Muhtasari
Vitendawili, nahau, na methali zinaonesha lugha ya kisanii katika
Kiswahili. Mwanafunzi atajifunza kutega na kutegua vitendawili,
kueleza maana ya nahau, kukamilisha methali, kueleza maana zake na
kufafanua ujumbe uliomo katika methali. Vilevile, mwanafunzi ataeleza
umuhimu wa vitendawili, nahau, na methali katika matumizi ya lugha
katika kuwasiliana.
Somo la 3 Vitendawili
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutega na kutegua vitendawili
wanavyovifahamu.
Mfano
Kitendawili – Tega
Kuku wangu ametagia mibani – Nanasi
Endapo mwanafunzi hatatoa jibu sahihi, mtegaji apewe mji.
(b) Waongoze wanafunzi kwa kutumia maelezo, picha na mifano
kutega na kutegua vitendawili.
(c) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 A ukurasa wa 14,
kutegua vitendawili kwa kutumia picha.
(d) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 B ukurasa wa 15 la
kutegua vitendawili namba 1 – 8. Angalia majibu yafuatayo:
1. kisogo 2. majani ya mti yaliyodondoka 3. bendera 4.
nyoka 5. kivuli 6. njia 7. moshi 8. chupa. (zingatia majibu
kulingana na mazingira wanayoishi wanafunzi).
(e) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 C ukurasa wa 15
kwa kuandika vitendawili vyenye majibu yafuatayo:
mhindi, mwiba, utelezi, konokono na ngoma.
10
Somo la 5 Nahau
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutaja nahau wanazozifahamu.
(b) Waongoze wanafunzi kubaini nahau kwa kukamilisha
maelezo waliyopewa.
Mfano Kandambili alitoka shamba kulima. Alifika nyumbani
alioga na kubadilisha nguo. Alikwenda kilabuni
kunywa pombe. Kandambili alilewa sana. Akiwa
njiani alianguka kila mara huku akiimba. Kandambili
alifanya nini? Kandambili alivaa miwani.
(c) Waongoze wanafunzi kutumia nahau kukamilisha maelezo
waliyopewa katika zoezi la 4 ukurasa wa 16 katika kitabu
cha mwanafunzi.
11
C. Kukamilisha methali
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutaja methali wanazozifahamu
(ii) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 5 C la
kukamilisha methali katika ukurasa wa 18 katika kitabu
cha mwanafunzi.
12
13
14
15
16
Somo la 4 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Rejea utangulizi sehemu ya namna ya kufundisha miundo.
(b) Andika ubaoni miundo unayotaka kufundisha kisha
wanafunzi wasome.
(c) Toa mifano ya sentensi zenye miundo unayofundisha.
Mfano Baba alimwambia mama, hatuna budi
kuwapeleka watoto shuleni.
(d) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 la kutunga sentensi
kwa kutumia miundo ukurasa wa 23 katika kitabu cha
mwanafunzi.
17
18
19
20
21
Kueleza matukio
Muhtasari
Katika sura hii wanafunzi wataweza kuelezea na kutumia nyakati
mbalimbali kueleza na kukanusha matukio katika sentensi kwa kutumia
wakati husika.
22
23
24
25
26
27
Mfano
(a) Aliondoka asubuhi na mapema – wakati uliopita
(b) Nitawaeleza wenzangu madhara ya wizi – wakati ujao
(c) Tabia ya wizi inapaswa kukomeshwa – wakati uliopo
28
29
Mavazi yetu
30
31
Somo la 4 Methali
Hatua za ufundishaji
(i) Waongoze wanafunzi kutaja methali wanazozifahamu.
(ii) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 3 ukurasa wa 40
katika kitabu cha mwanafunzi la kukamilisha methali.
32
B. Kukanusha sentensi
Hatua za ufundishaji
(a) Toa mifano kwa kukanusha sentensi.
Mfano Msichana alivaa sketi ya kubana
Msichana hakuvaa sketi ya kubana.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 4 B ukurasa wa 41
katika kitabu cha mwanafunzi.
33
34
35
Somo la 6 Vitendawili
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutega na kutegua vitendawili
wanavyovifahamu.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 5 ukurasa wa 44
kitabu cha mwanafunzi.
Somo la 7 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kusimulia habari kwa kufuata
mwongozo uliopo zoezi la 6 ukurasa wa 44 katika kitabu
cha mwanafunzi kwa mazungumzo.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 6 kwa kuandika.
(c) Waongoze wanafunzi kuandika habari hiyo kwa kuzingatia
mwongozo uliyotolewa katika kitabu cha mwanafunzi zoezi
la 6 ukurasa wa 44.
(d) Baada ya kusahihisha chagua habari iliyoandikwa vizuri na
wanafunzi waisome darasani kwa sauti.
36
Vinywaji vyetu
Muhtasari
Katika sura hii wanafunzi watajifunza maana ya vinywaji na aina zake,
vinywaji vyenye madhara na visivyo na madhara kupitia habari ya
Vinywaji vyetu. Pia, watajifunza msamiati, nahau, methali, kinyume
cha maneno na utungaji.
37
38
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati: mlevi, starehe, madafu, madhara, athiri,
togwa, wakazi, sharubati, kileo kwa kutumia mbinu ya
maelezo, vitu halisi, picha na maigizo.
(b) Andika maneno hayo ubaoni na waongoze wanafunzi kusoma
maneno hayo.
(c) Waongoze wanafunzi kueleza maana ya neno mojamoja.
(d) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo. Andika sentensi hizo ubaoni
ukizingatia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(e) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 la msamiati ukurasa
wa 48 katika kitabu cha mwanafunzi.
39
40
41
Somo la 6 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Andika ubaoni mambo ya kuzingatia kama yalivyoandikwa
katika zoezi la 5 ukurasa 52 katika kitabu cha mwanafunzi.
(b) Waongoze wanafunzi kujadili mambo hayo yaliyoandikwa
ubaoni na majibu kuyaandika ubaoni.
(c) Waongoze wanafunzi kumalizia habari kwa kuzingatia
mwongozo uliopo katika zoezi la 5 ukurasa wa 52 katika
kitabu cha mwanafunzi.
42
Mimea yetu
Muhtasari
Maudhui ya majigambo ya Mimea yetu yatawafundisha wanafunzi
aina mbalimbali za mimea na faida zake kwa ufasaha. Pia, atajifunza
matumizi mbalimbali ya msamiati, nahau, methali na utungaji.
43
44
Somo la 5 Nahau
Hatua za ufundishaji
(a) Toa mfano uliopo katika zoezi la 3 katika kitabu cha
mwanafunzi ukurasa wa 56.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 3 la kutunga sentensi
moja kwa kila nahau.
45
46
47
Somo la 8 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo kuhusu somo utakalofundisha.
(b) Ongoza majadiliano kuhusu picha iliyopo katika ukurasa
wa 60.
(c) Waongoze wanafunzi kumalizia habari waliyopewa katika
zoezi la 6 ukurasa 60 katika kitabu cha mwanafunzi kwa
kuandika katika madaftari yao.
(d) Sahihisha kazi za wanafunzi kwa kuzingatia sifa sahihi za
mmea wa mhogo, alama za uandishi, mwandiko, nafasi
kati ya neno na neno na matumizi sahihi ya herufi kubwa.
48
49
50
51
52
53
Somo la 5 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo jinsi ya kuandika habari katika mtiririko mzuri.
(b) Uliza maswali yaliyopo zoezi la 4 ukurasa wa 70 katika
kitabu cha mwanafunzi na andika majibu ubaoni.
(c) Waongoze wanafunzi kuandika habari kwa kuzingatia
maswali na mwanzo waliyopewa. Nakili mwanzo huo ubaoni
au tumia kitabu cha mwanafunzi ukurasa wa 70.
(d) Sahihisha kazi za wanafunzi kwa kuzingatia, alama za
uandishi, mwandiko, nafasi kati ya neno na neno na matumizi
sahihi ya herufi kubwa.
54
Muhtasari
Katika hadithi ya Juhudi na Amani wanafunzi wataweza kueleza kazi
za kila siku kwa kuzingatia nyakati. Vilevile, wataweza kuandika
ratiba zao za siku wakihusisha shughuli mbalimbali za kila siku. Pia,
watajifunza misamiati, nahau, vitendawili na nyakati.
55
56
Somo la 4 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo kuhusu miundo. Tafadhali rejea katika kipengele
cha miundo katika utangulizi.
(b) Nakili miundo yote ubaoni iliyopo katika zoezi la 2 ukurasa
wa 73 katika kitabu cha mwanafunzi.
(c) Waongoze wanafunzi kusoma miundo ubaoni na kutoa
mfano uliopo kitabuni.
(d) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia miundo
hiyo kwa mazungumzo na andika sentensi hizo ubaoni.
(e) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(f) Waongoze wanafunzi kutunga na kuandika sentensi kwa
kutumia miundo katika madaftari yao.
57
58
D. Kutunga sentensi
Hatua za ufundishaji
(i) Toa maelezo jinsi ya kutumia maneno ya sehemu A
na sehemu B ili kukamilisha maana.
(ii) Nakili ubaoni zoezi la 4 D ukurasa wa 77 katika kitabu
cha mwanafunzi.
(iii) Tumia mfano uliopo katika zoezi 4 D.
(iv) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi hilo kwenye
madaftari yao.
E. Kuandika sentensi katika wakati uliopita
Hatua za ufundishaji
(i) Toa maelezo jinsi ya kuandika sentensi katika wakati
uliopita zingatia kiambishi cha wakati ‘li’ katika
kitenzi.
(ii) Toa mfano uliopo katika zoezi la 4 E ukurasa wa 77
katika kitabu cha mwanafunzi.
(iii) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 4 E, katika
ukurasa wa 77-78 katika kitabu cha mwanafunzi katika
madaftari yao.
59
Somo la 7 Vitendawili
Hatua za ufundishaji
(a) Wakumbushe wanafunzi namna ya kutega na kutegua
vitendawili.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 5 ukurasa 79 katika
kitabu cha mwanafunzi, kwa kuonesha picha au vitu halisi
ambavyo ni majibu ya vitendawili. Wape nafasi ya kutega
kitendawili chenye jibu husika hatua kwa hatua.
(c) Ongeza majibu kadiri uwezavyo ili wanafunzi waandike
vitendawili kwenye madaftari yao.
60
61
62
63
Somo la 4 Nahau
Hatua za ufundishaji
(a) Nakili nahau ubaoni na kuwaongoza wanafunzi kutoa
maana ya nahau zote zilizopo katika zoezi la 3 ukurasa wa
82 katika kitabu cha mwanafunzi.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 3 ukurasa wa 82
katika kitabu cha mwanafunzi la kutunga sentensi mbili
kwa kila nahau.
64
65
E. Kukamilisha sentensi
Hatua za ufundishaji
(i) Toa maelezo kuhusu upatanisho wa kisarufi.
(ii) Nakili ubaoni kisanduku kilichopo katika zoezi la 4 E
ukurasa wa 84 katika kitabu cha mwanafunzi.
66
67
68
Kuandika hadithi
69
70
Somo la 4 Nahau
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo jinsi yakuoanisha nahau na maana zake.
(b) Nakili ubaoni zoezi la 3 ukurasa wa 89 katika kitabu cha
mwanafunzi. Waongoze wanafunzi kuzisoma nahau zote.
(c) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 3 la kuoanisha nahau
na maana zake kwenye madaftari yao.
Majibu i. (c), ii. (a), iii. (d), iv. (f), v. (b)
71
72
73
74
75
76
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; kibanda, kasi, jeruhi, kando,
chakavu na okoa
(b) Andika maneno hayo ubaoni na waongoze wanafunzi kusoma
maneno hayo.
77
Somo la 4 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo kuhusu somo kwa kurejea utangulizi kipengele
cha miundo.
(b) Nakili miundo yote ubaoni iliyopo katika zoezi la 3 ukurasa
wa 95 katika kitabu cha mwanafunzi na waongoze wanafunzi
kusoma miundo hiyo.
(c) Toa mfano kwa kutumia swali la kwanza la zoezi la 3.
(d) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia miundo
hiyo kwa mazungumzo na andika sentensi hizo ubaoni.
(e) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(f) Waongoze wanafunzi kutunga na kuandika sentensi nyingine
kwenye madaftari yao.
Somo la 5 Nahau
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo ya namna ya kupata maana ya nahau.
(b) Nakili ubaoni zoezi la 4 ukurasa wa 95 katika kitabu cha
mwanafunzi au tumia vitabu kuwaongoza wanafunzi kusoma
nahau zote.
(c) Toa mfano kwa kutumia swali la kwanza kutoa maana ya
78
Somo la 7 Vitendawili
Kutegua vitendawili
Hatua za ufundishaji
(a) Toa mfano wa kitendawili na wanafunzi wategue.
(b) Toa nafasi kwa wanafunzi kutega na kutegua vitendawili.
(c) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 6 ukurasa wa 96
katika kitabu cha mwanafunzi kwenye madaftari yao.
Majibu 1.nzi 2.nanasi 3. maboga 4. moto 5. macho.
6. kitanda 7. nywele 8. ardhi/mawingu
9. mwangwi 10. mate
79
80
81
82
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati familia, dawa, madhara, asilani, makini
na kinywaji.
83
84
85
86
87
Muhtasari
Sura hii itamsaidia mwanafunzi kujifunza utungaji kwa kufuata
maelekezo ya kutenda jambo hatua kwa hatua. Mfano, atajifunza
kupika chai hatua kwa hatua.
88
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati epua, chemka, upishi, vifaa, na viungo.
(b) Andika maneno hayo ubaoni na wanafunzi wayasome na
kutoa maana ya neno mojamoja.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo. Andika sentensi hizo ubaoni, zenye
makosa zirekebishe.
89
90
91
92
93
Kuandika barua
Shughuli za kutendwa na mwanafunzi
(a) Kujifunza jinsi ya kuandika barua ya kirafiki
(b) Kueleza muundo wa barua ya kirafiki
(c) Kueleza umuhimu wa barua za kirafiki
(d) Kuandika barua ya kirafiki
Muhtasari
Uandishi wa barua ni jambo muhimu kwa mawasiliano katika jamii.
Katika sura hii mwanafunzi atajifunza muundo na jinsi ya kuandika
barua ya kirafiki, ambapo itamsaidia katika maisha yake ya kila siku.
94
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; ziara, kujikimu, kukengeuka
na ndoto.
(b) Andika maneno hayo ubaoni na kuyasoma kisha eleza maana
ya neno mojamoja.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo.
(d) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi na
kuzisahihisha.
(e) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 ukurasa wa 39
katika kitabu cha mwanafunzi.
95
96
97
Somo la 5 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutaja vipengele muhimu vya barua
ya kirafiki. Tumia mfano wa barua ya kirafiki.
(b) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 4 ukurasa wa 117
katika kitabu cha mwanafunzi. Sahihisha barua walizoandika
wanafunzi kwa kuzingatia muundo wa barua ya kirafiki,
uumbaji wa herufi, nafasi kati ya neno na neno, matumizi
ya alama za uandishi na herufi kubwa.
98
Muhtasari
Katika sura hii mwanafunzi ataweza kuhadithia na kuandika hadithi.
Pia, mwanafunzi atajifunza aina mbalimbali za ndege na majina yao.
Vilevile, atajifunza kubuni mambo muhimu katika kuandika hadithi.
99
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; kale, tenga, hamaki, laumu,
uchungu na nyanyasa
(b) Andika maneno hayo ubaoni, waongoze wanafunzi kusoma
maneno hayo na kueleza maana ya neno mojamoja.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo. Andika sentensi hizo ubaoni.
Mfano Hapo kale kunguru na bata walikuwa marafiki.
(d) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
100
101
Somo la 5 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo mafupi kuhusu miundo.
(b) Andika miundo ifuatayo ubaoni.
....... walipokuwa ........
....... huku na huko ......
kila siku .........
........ lakini .......
........ kwa sababu .......
(c) Waongoze wanafunzi kusoma miundo iliyoandikwa ubaoni.
(d) Toa mifano ya sentensi zenye miundo unayotaka kufundisha.
mfano i. Kila siku .........
Kila siku kunguru huruka juu ya mti.
ii. ........ huku na huko .........
Alitazama huku na huko hakumuona ng’ombe wake.
(e) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 4 ukurasa wa 124
katika kitabu cha mwanafunzi.
102
103
Somo la 7 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Waongoze wanafunzi kutaja mambo ya kuzingatia katika
uandishi.
(b) Waongoze wanafunzi kujibu kwa mazungumzo maswali ya
mwongozo katika zoezi la 6 ukurasa wa 126 katika kitabu
cha mwanafunzi.
(c) Waongoze wanafunzi kuandika hadithi kwa kuzingatia
mwongozo wa maswali yaliyotolewa zoezi la 6 ukurasa wa
126 katika kitabu cha mwanafunzi.
104
105
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; kinga, samba, maradhi,
maambukizi, lishe na kusinyaa ulioko katika ukurasa wa
129 katika kitabu cha mwanafunzi.
(b) Andika maneno hayo ubaoni wanafunzi wayasome na
waeleze maana ya neno mojamoja.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia maneno
hayo kwa mazungumzo. Andika sentensi hizo ubaoni.
Rekebisha makosa yaliyojitokeza katika sentensi hizo.
(d) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 2 katika ukurasa wa
129 katika kitabu cha mwanafunzi.
106
107
108
Somo la 5 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Toa mfano wa kusoma shairi kwa wanafunzi kwa kutumia
shairi lenye ubeti mmoja.
Mfano
Leo tumekusanyika, malaria kuongelea,
Njia kutaja nataka, jinsi unavyoenea,
Nyasi na pia vichaka, makazi kukaribia,
Safisheni mazingira, mbu kutozaliana.
109
110
Muhtasari
Katika sura hii wanafunzi watasoma shairi la Haki ya elimu kwa mtoto
litakalowasaidia kuzijua na kuzielezea haki zao. Pia, watajifunza kutunga
shairi kwa kuzingatia vina na mizani.
111
112
Somo la 4 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo namna ya kutumia miundo katika sentensi.
(b) Nakili ubaoni miundo yote iliyopo katika zoezi la 3 ukurasa
wa 137 katika kitabu cha mwanafunzi.
(c) Waongoze wanafunzi kusoma miundo ubaoni.
(d) Toa mifano iliyopo kitabuni na waongoze wanafunzi kutunga
sentensi kwa kutumia miundo hiyo kwa mazungumzo na
andika sentensi hizo ubaoni.
(e) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(f) Waongoze wanafunzi kufanya zoezi la 3 la kutunga na
kuandika sentensi nyingine kwa kutumia miundo hiyo katika
madaftari yao.
113
Majibu 1. B 2. C 3. D 4. A 5. C 6. D
114
115
Somo la 8 Utungaji
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo kuhusu kanuni na taratibu za utungaji wa shairi
la kimapokeo. (Shairi linalozingatia urari wa vina na mizani)
(b) Andika ubeti ufuatao ubaoni.
Kibeta ni shule yetu, ipo Kishanje sikia,
Makini walimu wetu, darasani fundishia,
Tunza mazingira yetu, afya kuizingatia,
Taaluma zingatia, kuienzi shule yetu.
116
117
118
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
(a) Fundisha msamiati ufuatao; Kaskazini, Kusini, Mashariki,
Magharibi, shaka, mchoyo, nyenyekea, msitu, zama na
chomoza kwa kutumia mazingira halisi na vitendo.
(b) Nakili zoezi la 2 ubaoni ukurasa wa 144 katika kitabu cha
mwanafunzi.
119
Somo la 4 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Nakili miundo yote ubaoni iliyopo katika zoezi la 3 ukurasa
wa 144 katika kitabu cha mwanafunzi.
(b) Waongoze wanafunzi kusoma miundo ubaoni na toa mfano
kwa kila muundo kama ilivyooneshwa kitabuni.
(c) Waongoze wanafunzi kutunga sentensi kwa kutumia miundo
hiyo kwa mazungumzo na andika sentensi hizo ubaoni.
(d) Angalia usahihi wa sentensi walizotunga wanafunzi.
(e) Waongoze wanafunzi kutunga na kuandika sentensi nyingine
katika madaftari yao.
120
121
122
123
Muhtasari
Katika sura hii wanafunzi watajifunza namna ya kutamba ngonjera na
kuandika habari fupi baada ya kusoma ngonjera ya Wajibu wa mtoto
katika familia. Pia, wanafunzi watasoma majigambo na kuweza kueleza
umuhimu wa viungo vya mwili.
124
(c) Toa muda mfupi kwa kila mhusika kusoma sehemu yake.
125
Somo la 3 Msamiati
Hatua za ufundishaji
Somo la 4 Nahau
Hatua za ufundishaji
(b) Toa mfano kwa kutumia swali la (i) na la (ii) katika zoezi la
3 ukurasa wa 152 katika kitabu cha mwanafunzi.
126
Somo la 5 Miundo
Hatua za ufundishaji
(a) Nakili ubaoni miundo yote iliyopo katika zoezi la 4 ukurasa
wa 153 katika kitabu cha mwanafunzi.
Somo la 6 Methali
Hatua za ufundishaji
(a) Toa maelezo ya namna ya kukamilisha methali.
Kuishi kwingi,……………..
Kuishi kwingi, ni kuona mengi.
127
Hatua za ufundishaji
Hatua za ufundishaji
128
Hatua za ufundishaji
Hatua za ufundishaji
129
Hatua za ufundishaji
Somo la 8 Utungaji
Hatua za ufundishaji
130
(c) Toa muda mfupi kwa kila mhusika kusoma sehemu yake.
131
132