Professional Documents
Culture Documents
Kanuni Za Umoja PDF
Kanuni Za Umoja PDF
KANUNI
UMOJA WA TUNAJALIANA
1. SIFA ZA MWANACHAMA
a) Mwanachama kulipa ADA mara moja anapojiunga;
b) Mwanachama anafanya MAJERESHO ya michango iliyotolewa na Chama kwa niaba yake
ndani ya Mwezi (1) Mmoja;
c) Mwanachama asipohudhuria vikao (3) vitatu mfululizo, anapoteza uanachama wake na
haki zake zote, isipokuwa kama ana sababu za msingi kwa kutoa taarifa RASMI;
d) Endapo Mwanachama ataamua kujitoa kwa hiyari yake mwenyewe kwenye chama,
atapoteza haki zake zote.
2. ADA
a) ADA ya mwanachama ni Tshs 600,000/= (LAKI SITA);
b) Kutakuwa na nyongeza ya thamani ya mwanachama ya Tshs 200,000/= (LAKI MBILI) kwa
kila mwanzoni mwa mwaka;
c) Aidha kutakuwa na RIBA ya asilimia 10 kwenye nyongeza ya thamani ya mwanachama
kwa kila baada ya MIEZI MITATU (3) kupita. Vilevile, kila baada ya Miezi MITATU (03)
mingine kupita kutakuwa na ongezeko ASILIMIA 10 nyingine;
d) Mtu asipolipa ADA anakuwa si MWANACHAMA.
3. SHUGHULI ZA KIUCHUMI
a) Kukopeshana kwa riba ya ASILIMIA 10 (sio zaidi ya miezi mitatu na sio zaidi ya asilimia 80
ya fedha zake zote zilizo kwenye mfuko wa chama). Aidha kutakuwa na ongezeko la RIBA
ya ASILIMIA 10 kwa kila MIEZI MITATU (03) kupita;
b) Kama mwanachama anayetaka kukopa atakuwa na DENI, atakatwa tofauti kufidia DENI
lake la awali;
c) Shughuli nyingine itakayoamuliwa na KIKUNDI kupitia VIKAO halali;
d) Kutakuwa na nyongeza ya Tshs 200,000/= LAKI MBILI kila mwaka kama ongezeko la
thamani ya kila mwanachama.
6. WATEGEMEZI WA MWANACHAMA
a) Wategemezi wa mwanachama ni wale ambao wameainishwa na kutambuliwa na
KATIBA.
8. MAWASILIANO
a) Mwanachama anawajibika kutoa TAARIFA ya TUKIO lolote liwe la SHIDA ama RAHA
kupitia njia rasmi za mawasiliano kama kupiga simu kwa kiongozi ama viongozi;
b) Kutuma ujumbe mfupi kwa kiongozi ama viongozi, kutuma barua pepe kwa kiongozi ama
viongozi;
c) Kutuma ujumbe kupitia kikundi cha WHATSAPP