TAARIFA BOTI YA MIKOKO

You might also like

Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 1

DOKEZO SABILI

CE

TAARIFA KUHUSU KUHUDHURIA KIKAO CHA MAREKEBISHO YA


BOTI AINA YA MV MIKOKO 3 TSC/DAR 103 MKOANI TANGA.

Husika na somo tajwa hapo juu, Ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu


Tanzania ilinunua boti mpya ya Mikoko Tanga yenye namba za usajili
TSC/DAR.103 kwa Kampuni ya utengenezaji Boti inayoitwa Sam & Anzai
Boat Builders Co.Ltd mnamo tarehe 29/06/2019 kwa lengo la kuthibiti
matumizi mabaya ya rasilimali za Taifa kwa kuhakikisha Doria inafanyika
kwa ukamilifu pasipo kizuzi chochote Mkoani Tanga.
Aidha muda mfupi baada ya Boti hiyo kukabidhiwa kwa Wakala ilibainika
kuwa na hitilafu na mapungufu kadhawakadha yaliyopelekea watumiaji wa
Boti kushindwa kufanya kazi ya Doria kama ilivyotarajiwa.
Kwakuwa Mtengenezaji na Muuzaji wa Boti hiyo alitoa hati ya ubora na
matengenezo (Warranty Certificate) kwa muda wa mwaka mmoja toka
kununuliwa kwa Boti hiyo,Wakala ulifanya mawasiliano nae ili kurekebisha
hitilafu hizo zilizojitokeza.Pamoja na mawasiliano hayo mtengenezaji wa
Boti hiyo hakuweza kufanya kazi hiyo kwa wakati,kupelekea kuandaa
kikao cha pamoja kati ya Kampuni hiyo pamoja na Wakala wa Huduma za
Misitu.
Hata hivyo baada ya kufanya kikao kifupi na kutembelea eneo ilipo boti
hiyo,mtengenezaji na Muuzaji wa Boti hiyo alirekebisha hitilafu zote
zilizokuwa zimeainishwa katika ripoti ya ukaguzi iliyojumuisha pande zote
mbili.
Pamoja na Dokezo hili, naomba kuwasilisha muhutasari wa kikao hicho
unaotoa ufafanuzi zaidi.
Naomba kuwasilisha,

Peter Tesha
AFISA UGAVI
08/06/2020

You might also like