Professional Documents
Culture Documents
INSHA ZA KIFALME~1
INSHA ZA KIFALME~1
DIBAJI
2
SURA YA KWANZA
SAIKOLOJIA YA UMRI
UMRI kwa fasili ya kawaida ni hesabu ya muda uliopita
tangu kiumbehai kianze kuwepo. Mintarafu, umri wa
binadamu na wanyama huanza kuhesabika mara baada
ya kuzaliwa!
Kama mtu alizaliwa mwaka 2011 basi mwaka 2021
atahesabika kuwa na umri wa miaka 10!
Kama hakuna mwingiliano wa tatizo lolote, Umri wa
binadamu na viumbe wengine hutakiwa kwenda
sambamba na mwonekano wa mwili, uwezo wa
akili/fikra, nafasi katika jamii hata uwezo kiuchumi.
Yaan kadiri umri wa kuzaliwa unavyosonga, basi
vilevile hutegemewa ukuaji huohuo uonekane katika
akili na nafasi ya mtu kijamii.
UMRI KATIKA SAIKOLOJIA
Katika saikolojia umri wa kiumbe hai hasa binadamu
hupimwa kwa kuzingatia mambo kadhaa anuai, siyo
idadi ya miaka tu!
Kwa hiyo unapotaja umri wako katika mukutadha wa
saikolojia ni muhimu kuzingatia aina husika ya umri!
AINA YA UMRI
Zipo aina nyingi za umri katika mukutadha za saikolojia,
na hapa nitachambua aina tano kama ifuatavyo!
3
1. UMRI WENDO (Chronological age)
2. UMRI WA KIMAUMBILE/KIBAIOLOJI
(Biological/physiological age)
4
Vilevile unaweza kumwona mtu ana mwonekano
kama kijana wa miaka 40, kumbe ni mzee na
yuko kwenye 60+
5
wameshakuwa wakubwa sana japo kimwili na kiakili
bado sana!
6
kijana na hupewa heshima kidogo kama vijana wengine
wasio wa umri au rika lake!
8
akili/ufahamu, hisia sahihi, mwonekano
unaoendana na umri pia mchango na utambulisho
sahihi kijamii!
9
psychological and physiological well being,
social functions and roles included!
UMRI NA KUZEEKA
Umri kusonga mbele siyo ugonjwa wala fedheha, ni sifa
ya kiumbe hai chochote, lazima kizaliwe, kikue
ikiwezekana kizeeke na mwisho ni lazima kife!
Kwa hiyo uzee wenye tija, ni ule unaobeba maendeleo
yote, yaan ya wendo, mwili, akili, hisia na kijamii! Siyo
kujaza mvi tu kumbe kichwani hamna kitu! Ni uzee
unaotambua majira na nyakati siyo una miaka 70
unahangaika na vitoto vya miaka 17!
CHANGAMOTO ZA UZEE!
10
Kadiri umri wako wa kuzaliwa unavyosonga, unaweza
kukutana na changamoto za uoni hafifu, kupoteza uwezo
wa kusikia, kuishiwa nguvu, kupoteza kumbukumbu na
magonjwa ya uzeeni!
KUHUSU KUPUNGUKIWA!
Saikolojia inatambua uwezekano wa mtu kupoteza
kumbukumbu kutokana na uzee, kuchoka, kuchakaa
ngozi nk!
Na hapa mtu mmoja alipata kuandika!
Yoshua bin Sira 3:12-13
“Mwanangu, umsaidie baba yako katika UZEE
WAKE, Wala usipate kumhuzunisha siku zote za
maisha yake. Akiwa amepungukiwa na UFAHAMU
umwie kwa upole wala usimdharau iwapo wewe u
mzima sana.”
11
kawaida unafanya kazi ambayo ni kipaji chako cha
kuzaliwa!
UNAKUFA KAZINI.
Kwa kawaida mtu hupaswa kufa akiwa anatumikia
kusudi lake! Kwa mfano kama kipaji chako ni kuimba
basi ukiwa na afya njema hakikisha unafariki katika
mazingira ya kazi yako!
12
ninyi bila shaka, atawapandisha kutoka nchi hii
mpaka aliyowaapia Ibrahimu, na Isaka na
Yakobo. Yusufu akawaapisha wana wa Israeli,
akisema ‘Bila shaka Mungu atawajia ninyi, nanyi
mtapandisha huko mifupa yangu. Basi Yusufu
akafa, mwenye miaka mia na kumi; wakampaka
dawa, wakamtia katika sanduku, huko Misri.”
WENGINE HAWACHAKAZWI SANA NA UZEE
Katika saikolojia hii huitwa “Individual differencies”
wengine huzeeka na kuhangaika wakati baadhi hudunda
tu kama miaka imeganda vile! Hii husababishwa kwa
kiwango kikubwa na mtindo wa maisha na nasaba!
Nabii Musa ni kielelezo cha hilo!
Kumbukumbu la torati 34:7 “Musa alikuwa mtu wa
miaka mia na ishirini alipokufa; Jicho lake
halikupofuka, wala nguvu za mwili wake
hazikupunguka.”
*Umeona? Pamoj na kuzeeka, hakupungukiwa nguvu
wala kupata shida ya macho!
13
SURA YA PILI
UFAHAMU UGONJWA WA KUTOSAMEHE
14
SASA Kama ulikuwa hujui, basi leo nakujulisha kuwa
“Kutosamehe ni ugonjwa” kama yalivyo magonjwa
mengine!
Kutokusamehe ni moja kati ya magonjwa mengi
yanayotafuna nguvu kazi ya familia, jamii na taifa!
Na kwa bahati mbaya sana watu wengi hawajui kuwa
hali ya kutosamehe ni ‘UGONJWA’ wa akili
KWANI UGONJWA NI NINI?
Kisayansi, ugonjwa ni hali yoyote ile inayoingilia
utendaji kazi wa kawaida wa mwili wa kiumbe hai.
Kutoka kwenye fasili hiyo, hali ya kutosamehe inapata
sifa ya kuwa ugonjwa, kwani hali ya kutosamehe
huingilia utendaji kazi wa kawaida na wa asili wa akili,
hisia na mwili, na hivyo kuorodheshwa kama moja
wapo ya magonjwa ya akili kwenye tafiti za saikolojia
hasa zile za tawi la Psychiatriology !
Kwa hiyo kutosamehe kwa kifupi ni tatizo la akili kama
nitakavyofafanua baadae!
TAFITI ZINASEMAJE?
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa (Johns Hopkin
Medical Research) kutosamehe (unforgiveness)
imetajwa kusababisha mabadiriko katika mapigo ya
moyo, shinikizo la damu, na kuzorota kwa mfumo wa
kinga za mwili (immunity) hali hii hufanyika kama
mwitikio wa mwili kutokana na kusongwa na hasira,
fadhaa, sonona na wasiwasi!
15
Asilimia 61 ya magonjwa kama kansa na shinikizo
yamehusishwa na kutosamehe!
Kwa upande mwingine utafiti wa Worthington na
Scherer (2004) unabainisha kuwa ugonjwa wa
kutosamehe kama aina ya mwikitikio utokanano na
mfadhaiko. Athali za ugonjwa huu ni nyingi, kama vile
hasira, huzuni, fadhaa, wasiwasi, mgogoro nafsia au
baina ya watu na wakati mwingine mgogoro wa kiimani.
Zaidi sana; Kujihisi hauko salama (Chronic stress
response) jaziba ya muda mfupi (short term intense
Response) na uwenda wazimu wa kujihisi unaonewa tu
kila wakati, ambayo kisaikolojia huitwa Paranoid
Personality Disorder, ni sehemu ya athali za ugonjwa wa
kutosamehe!
TIBA YA KUTOSAMEHE.
Kutosamehe ni ugonjwa unaotibika na kupona kabisa!
Ugonjwa huu unaweza tu kutibika na kupona endapo
mgonjwa atajulishwa na kufahamishwa yafuatayo!
KUUJUA UKWELI:
Unaumia na kuteseka kwa sababu hujui ukweli kuwa
wewe ndiye unayekosa usingizi na kujaa mawazo kwa
sababu umeshindwa kumsamehe mbaya wako!
Ukiujua ukweli wa “Mechanism” ya mateso na
sononeko la kumbeba mtu moyoni, utaapa kusamehe
kwa ajili ya kulinda amani ya moyo na furaha yako!
16
Yohane 8:32 “Tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo
kweli itawaweka huru.”
UKWELI NI HUU!
Kwa uchache
17
Ukisha jua hayo yote, utachukua hatua za makusudi na
juhudi za haraka kuwasamehe unaodhani walikukosea!
Kitendo cha kusamehe ni kama kutua mzigo mzito na
mkubwa mabegani mwako!
Dawa, sindano, dripu na mionzi ya kumaliza ugonjwa
huu ni wewe kuamua ‘KUSAMEHE BILA
MASHARTI’ Unasamehe bila masharti kwa sababu
unafanya hivyo kama hatua ya kujitibu wewe
mwenyewe!
Ukitaka kusamehe kwa masharti maana yake utakuwa
bado hujipendi na unatamani kuendelea kuteseka juu ya
waliokukosea wakati wao wanalala usingizi wa pono na
hawana muda na wewe!
NITAJUAJE KAMA NIMESAMEHE?
Njia rahisi ya kujua kuwa umesamehe ni pale
unapojisikia ‘fresh’ tu hata pale unapomwona
aliyekuumiza! Uzoefu unaonesha kwamba, wengi
hujisikia vibaya, mapigo ya moyo kwenda haraka na
kupata hisia za chuki au huzuni wanapowaona wabaya
wao! Sasa ukiona hali hiyo imeisha na haikusumbui tena
basi jua umeshasamehe na umepona kabisa ugonjwa
huo!
Kusamehe na kupona kwa hiyo ni pale unapopata ahueni
moyoni!
18
Kumbuka: kusamehe wakati mwingine siyo tukio la
mara moja! Ni mchakato kulingana na chanzo cha
maumivu yenyewe.
USHUHUDA WA MTEJA.
Mteja wangu mmoja aliniambia kuwa aliona dunia kama
kiwanja cha mateso na jehanamu kwake, kwani mtu
aliyekuwa amegoma kumsamehe na alikuwa
anamchukia sana ndiye alikuwa mgeni wake wa mara
kwa mara! Alishindwa kumfukuza wala kumwambia
kwamba hamtaki! Alilazimika kutabasamu japo moyo
ulikuwa unavuja damu, alimchinjia kuku mara kwa mara
huku moyoni akiomboleza! Alimfanyia mema yote
kinafiki tu!
Jamaa alikula na kunywa na kuondoka! Halafu baada ya
muda mfupi tu alirudi tena! Eeh, alikuja mara kwa mara
kwa sababu alikuwa hajui kuwa kabebwa moyoni?
What a pain? Usiyempenda ndiye mgeni wako wa mara
kwa mara! Maisha ya jehanamu ya duniani!
UFALME WA MUNGU UNASEMAJE?
Kimaumbile ya asili binadamu ameumbwa na uwezo
mkubwa wa kusamehe na kuachilia! Hili suala la kukaa
miaka 15 na zaidi bila kusamehe ni athali ya mazingira
tu, tumefundishwa tu lakini kwa hakika binadamu
hajaumbwa kuwa kiumbe wa aina hiyo!
19
Mtoto mdogo, ambaye hajavurugwa wala kuathiliwa na
mazingira ya migogoro huwa ana uwezo wa asili kabisa
wa kusamehe! Hata hivyo uwezo huo hupotea kadiri
miaka inavyosonga na kujifunza jinsi ya kutunza hasira
na uchungu kwa muda mrefu.
Mtoto mdogo huwa haoni kazi kusamehe hata
ungemfanyaje, kwa sababu kiasili suala la kusamehe
limefungwa kwenye muda!
Waefeso 4:26-27 "Mwe na hasira, ila msitende
dhambi; Jua lisichwe na uchungu wenu bado
haujawatoka." Wala msimpe nafasi ibilisi."
Kwa kawaida unaweza kukasirika kuanzia asubuhi
mpaka jioni, lakini zaidi ya hapo linaanza kuwa tatizo la
akili!
Kwa uwezo wao wa kusameheana na kuacha upendo
utawale Bwana Yesu aliwasifia watoto na kuwatolea
mfano!
Marko 10:13-16 “Basi wakamletea watoto wadogo ili
awaguse; wanafunzi wake wakawakemea. Ila
alipoona alichukizwa sana, akawaambia, ‘Waacheni
watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana
watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao. Amini
nawaambieni: Yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu
kama mtoto mdogo hatauingia kabisa.
Akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao,
akawabariki.”
20
Kwa hiyo watoto wadogo ndiyo mfano halisi wa
binadamu ambaye hajaumizwa! Jinsi tulivyo leo kwa
asilimia kubwa siyo asili yetu ni matokeo ya
kunyanyasika sana mpaka manyanyaso hayo yakaibadiri
asili yetu njema! Hata hivyo lipo tumaini kubwa, tumaini
hilo ni kwamba upo uwezekano wa kurudisha fikira na
mtazamo wako kwenye asili yake na kuwa binadamu wa
kusamehe na kuachilia bila masharti!
USHAURI WA BWANA YESU
Yesu Kristo alilsisitiza sana umuhimu wa kusamehe na
kuachilia! Suala la kusamehe alilipa uzito na msisitizo
wa kipekee SANA! Mintarafu, hali hii iliwafanya
wanafunzi wake wahoji sana juu ya kusamehe. Kwamba
unaweza kusamehe hata mara ngapi? Hata mara saba?
Yesu alijibu hata saba mara sabini! Rejea mathayo
18:21-22 (samehe 7×70)
*Tunaomba msamaha kwa Mungu kwa sababu hata sisi
tunasamehe watu wengine walio tukosea. Rejea Luka
11:4, 6:37
21
wenye huruma, MKASAMEHEANE kama na Mungu
katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”
Unakumbuka athali ya kutokusameha? Kwa hiyo
uchungu, ghadhabu, hasira, kelele na kila aina ya ubaya
unaokutesa, unaweza kuondoka kwa kusamehe!
Wakolosai 3:12-15 “Basi kwa kuwa mmekuwa
wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni
moyo wa REHEMA, utu wema, unyenyekevu, upole,
uvumilivu. Mkichukuliana, na KUSAMEHEANA,
mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake;
kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo hivyo na
ninyi. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndiyo
mlioitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa
shukrani.”
**Kwa hiyo, waliozaliwa mara ya pili kwa kumwamini
Yesu ni wateule na watakatifu wa Mungu! Hawapaswi
kuteseka kwa kubeba watu mioyoni mwao! Wanapaswa
kusamehe kwa maana kusamehe ni ishara ya ukomavu
na upendo ambayo ndiyo amri katika agano jipya!
Kutosamehe ni kukosa kujipenda mwenyewe na
kuwapenda wengine!
22
WENGINE WAMEKUKOSEA KWA UJINGA
WAO!
Ni muhimu kutambua kuwa wapo watu waliokukosea
kwa sababu tu ya ujinga wao, sio ujinga wako! na hivyo
wakakuachia maumuivu makali moyoni mwako! Kwa
hiyo kundi hilo la wajinga hupaswa kusamehewa kwa
kuwa ni wajinga tu! Hawajui athali ya maneno
wanayotunenea, au matendo yao kwetu!
Yesu alijua waliokuwa wanamtesa na kumsulibisha
msalabani walikuwa wajinga tu! Kwa hiyo ilikuwa
muhimu kuwasamehe!
Luka 23:34 “Baba uwasamehe kwa kuwa hawajui
walitendalo”
Kwa hiyo kuna watu unapaswa uwasamehe yaishe kwa
sababu walikukosea kwa kutokujua kwao madhala ya
waliyokufanyia! Na kwa kuwa ni wajinga basi
hawajaona hata umuhimu wa kukuomba msamaha,
hivyo wasamehe ili wewe uwe huru!
**Watu wa aina hii unapaswa siyo tu kwamba
uwasamehe lakini uwasamehe na kuwaelimisha na
kuwafariji ikiwezekana!
Rejea 2 Wakorintho 2:5-11
23
JE, ASIPOKUBALI MSAMAHA?
Ndiyo, kuna watu huwa wanakataa suluhu! Hawataki
yaishe! Wanapenda maisha ya ugomvi, migogoro na
kutunishiana misuli!
Bwana Yesu alishauri kushughulika nao kama
ifuatavyo!
Mathayo 18:15-17 “Na ndugu yako akikukosea,
enenda ukamwonye, wewe na yeye peke yenu;
akikusikia, umempata nduguyo. La, kama hasikii,
chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, ili
kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila
neno lithibitike. Na asipowasikiliza wao, liambie
kanisa: na asipolisikiliza kanisa pia, na awe kwako
kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.”
Kumfanya mtu kuwa “wa mataifa” siyo kumweka
moyoni wala kumbeba, bali ni kumsamehe na kuachana
naye!
Usijipe kazi ya kumbadirisha mpumbavu, kama
haeleweki achana naye na asikusumbue! Mtu wa mataifa
ni mtu ambaye hajastarabika, mshenzi na kafiri! Akija
kwako utampokea na kumfanyia ukarimu kwa heshima
na kiwango cha watu wa mataifa!
Kwani akija kwako mtu usiyemjua, huwezi
kumkaribisha? Utakuwa na kinyongo naye? Kama jibu
ni hapana, fanya hivyo kwa ndugu yako asiyetaka
suluhu!
24
KUSAMEHE NA KUSAHAU
Hii ni dhana tu isiyo na uhakika wala ulazima! Cha
muhimu ni kusamehe tu sauala la kusahau siyo lazima
wala muhimu kwa sababu ubongo huhifadhi matukio
yote mazuri na mabaya! Kwa hiyo unaweza
kuukumbuka ubaya uliotendewa na usiumie maana
ilishabaki kama historia tu!
Hata hivyo, kama unataka kujisahaulisha uwezekano
upo. Kwani kwenye saikolojia kuna dhana ya
kukumbuka na kusahau “Concept of memory and
forgetting” kuna kitu kinaitwa ‘Motivated forgetting’
kwa hiyo ni wewe tu, unaweza kutengeneza mazingira
ya kusahau msala au tukio lililopelekea wewe kuchukia
na kushindwa kusamehe!
25
SURA YA TATU
SAIKOLOJIA YA HASIRA NA UFALME WA
MUNGU
"A Rhapsody For Kingdom Anger Management and
Strategies"
MASWALI YA KUJIULIZA.
1. Umewahi kuwa na hasira?
2. Huwa unapata hasira Mara kwa Mara?
3. Ukiwa na hasira huwa unafanyaje?
4. Je, Kuna ndugu, jamaa au marafiki umewafuta kabisa
na hutaki hata kusikia habari zao kutokana na hasira?
5. kuna wakati hasira inajaa mpaka unahisi Koo
linauma/Kuwaka Moto?
6. Umewahi kujuta kwa kufanya maamuzi mabaya
kutokana na hasira?
7. Hasira imewahi kukugarimu kama vile kutozwa faini,
kufungwa au kutengwa na jamii?
8. Je, Kuna faida au Hasara kwenye hasira?
26
HASIRA ni sehemu ya hisia kali za ndani zimpatazo mtu
hasa anapokutana na upinzani fulani.
Hakuna binadamu asiyekasirika, kwa Sababu hasira ni
hisia za kawaida za kuzaliwa nazo (Inborn).
Hata hivyo uwezo na kiwango cha kutawala hisia za
hasira hutofautiana kati ya mtu mmoja na mwingine.
Mwanafalsafa wa zamani Aristotle aliwahi kusema
"Kukasirika kila mtu anaweza, lakini Kukasirika
kwa sababu sahihi, kwa mtu sahihi, kwa Kiwango
sahihi na kwa wakati sahihi Ni vigumu kwa kila
mtu."
Lengo la sura hii ni kukufanya uwe na Uwezo wa
kuhimili hasira zako! Na ukikasirika basi iwe ni kwa
sababu sahihi, wakati sahihi, kwa Kiwango sahihi na
kwa mtu sahihi! Ili usijikute kwenye matatizo.
Ukiwa na Uwezo mkubwa wa kudhibiti hasira zako
utaonekana mtu mwema na muungwana kwa mwenzi
wako, familia yako na jamii kwa ujumla!
• Kama mshauri wa masuala ya kisaikolojia,
nimekutana na wateja kadhaa wanaosumbuka na
hasira, Wengi walikiri kuwa, kutokana na kuwa
na hasira za ghafla na za mara kwa mara hujikuta
wameleta fujo na madhara makubwa. Zaidi Sana
wengine imewapelekea kuepukwa na ndugu,
jamaa na marafiki kadhaa! Mmoja aliniambia
27
"Kwenye vikao vyetu vya ukoo wananijua, Mara kwa
Mara huwa wanaepuka kubishana na Mimi."
Hata hivyo hali hiyo ilionekana kumuumiza Sana!
Fikiria, wafanya kazi wenzako (Staff member)
wanakuogopa kwa hasira zako za kiwenda wazimu,
unajisikiaje!
Ukifahamu kwamba watu wanakwepa hata kukudadisi
Mambo ya kawaida kwa sababu ya hasira zako Kama za
mkizi, unajisikiaje?
AINA ZA HASIRA KISAIKOLOJIA
Kisaikolojia zipo aina kadhaa za hasira, aina hizi
zimechambuliwa kutokana na kisababishi cha hasira
yenyewe Kama Ifuatavyo.
1. Hasira ya haki. Hii kwa kimombo tunaita
Righteous Anger. Hii ni hasira chanya, Ni hasira
inayositahili na kuhitajika! Ni hasira ambayo
huinuka ukiona kitu/Jambo Fulani haliendi Sawa
Sawa, mfano ukaona mtu anaonewa na
kunyanyaswa, hasira hii hupelekea kukupa nguvu
hata za kujitoa mhanga ili umsaidie! Kwa hiyo
hii ni hasira Nzuri!
MFANO WA HASIRA YA HAKI
(Yesu aliwahi kucharaza viboko na kupindua meza za
watu waliokuwa wamegeuza nyumba za ibada kuwa
sehemu ya harambee na biashara maarufu Kama pango
la wanyang'anyi)
28
Soma Luka 19:45-46 au Marko 13:15-17
Kuna siku niliingilia Kati kuzuia mwizi asiuawe kwa
kupigwa mawe! Akili zangu zilikuja kujua kuwa
nilikuwa kwenye hatari ya Kufa Mimi Mwenyewe,
nikiwa tayari nimemwokoa mtu huyo aliyesadikika kuwa
kibaka !
2. Hasira kutokana na kuzidiwa au kuelemewa
na Mambo mengi, inaitwa ‘overwhelmed
anger!’
Mfano kutopata usingizi vizuri, kuwa na ratiba
iliyosonga sana, kukosa muda wa mazoezi na
kuburudika au kuwa na njaa!
3. Hasira za kutaka kuendesha/kutawala hii kwa
kimombo inaitwa Manipulative anger,
Ni hasira inayolenga kuwatisha watu ili wakuogope
uwaendeshe unavyotaka! Neno maarufu la mtaani
naweza kusema "Kupiga mkwara"
Baadhi ya viongozi madikteta, hutumia hasira hii ili
afanye anavyotaka bila kufuata katiba, utaratibu wala
sheria.
4. Hasira itokanayo na mapito!
Hii ni hasira kutokana na matukio aliyopitia mhusika
kama vile kusalitiwa na mpenzi, kufiwa, kunyanyaswa
kingono nk. (Post traumatic stress Disorder)
29
5. Hasira kwa kiasi fulani huweza kisababishwa na
hali ya kimaumbile/kifiziolojia kwa mfano
kiwango cha sukari kuwa chini sana mwilini,
kukosa mlinganyo sawia wa homoni na kemikali
kwenye ubongo kutokuwa sawa! (Hormonal na
brain chemical imbalances.
6. Sababu nyinginezo ni hofu ya maisha na
usalama, Mfano uchumi mbaya, ukosefu wa
ajira, changomoto za kimaisha kwa ujumla !
HABARI NJEMA
Pamoja na sababu zote nilizotaja hapo na zile uzijuazo
Mwenyewe, wanasaikolojia wote tunakubalina kuwa
hasira inaweza kudhibitiwa/kuzuiwa au kupunguzwa
UNAFANYAJE?
• Isome hasira yako vizuri bila
kujipendelea/kujihurumia
• Ukisha ielewa vyema, Epuka
vitu/Hali/vichochezi vya hasira yako.
• Ufundishe ubongo wako kubaini mapema
Mazungumzo, hali au mazingira yanayoweza
kukupelekea kwenye hasira.
HASIRA KWENYE UFALME WA MUNGU IKO
HIVI
Tuliozaliwa mara ya pili na kufanyika kuwa watoto wa
Mungu kwa kumwamini Yesu Kristo (Yohane 1:12)
30
Tunayo nafasi nzuri zaidi ya kuishinda hasira na kuwa
wenye furaha.
Kwa sababu gani?
Unapozaliwa kwa mara ya pili, unakuwa kiumbe kipya
na unabeba vinasaba na hali ya baba wa mbinguni.
Maana imeandikwa "Kama Yeye alivyo, ndivyo na sisi
tulivyoona humu Ulimwenguni" (1 Yohane 4:17b)
MUNGU YUKOJE?
Zaburi 103:8 " Bwana amejaa huruma na neema, Haoni
HASIRA upesi, Ni mwingi wa fadhili."
Sifa ya Mungu wetu ni hiyo
KWA NINI HASIRA HAIFAI?
Pamoja na faida moja ya hasira kama tulivyoona kule
juu, bado hasara inaonekana kuwa ni kubwa Sana.
• HASIRA HAITENDI HAKI. Mtu mwenye
hasira kamwe hawezi kutenda haki, kwa sababu
vitendo vingi huvifanya akiongozwa na hasira
kuliko akili.
Yakobo 1:19-20 "Hayo mnajua ndugu zangu
wapenzi: Basi kila mtu awe mwepesi wa kusikia, Bali
Si mwepesi wa kusema, Wala KUKASIRIKA kwa
Maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya
Mungu."
31
Kwa hiyo kwenye hasira hakuna Haki. Viongozi wengi
Wenye hasira hushindwa kutenda haki kwa
wanaowaongoza! Kamata kamata na vitisho ni dalili za
kiongozi mwenye hasira.
• HASIRA HULETA UGOMVI na uasi! Bila
hasira ugomvi na uasi utatoka wapi?
Mithali 29:22 "Mtu wa hasira huchochea ugomvi, na
Mtu mwenye ghadhabu huasi Sana."
• HASIRA HUTENDA MABAYA. Kuna watu
wanaozea kwenye magereza mbalimbali
kutokana na kufanya unyama kwa msukumo wa
hasira tu, wanajutia hasira yao.
32
Mhubiri 7:9 "Usifanye haraka KUKASIRIKA
Rohoni mwako, Maana hasira kukaa kifuani mwa
wapumbavu."
• Hasira huondoa ulinzi.
Mdomo hukiponza kichwa, ndivyo hasira pia iwezavyo
kukuponza, mtu Asiye na hasira ni vigumu kujikwaa
katika kusema au kutenda.
Mithali 25:28 "Asiye tawala Roho yake ni mfano wa
mji uliobomolewa, usio na kuta.
JINSI YA KUFANYA
Jipatie hekima na ufahamu. Ndiyo maana nipo hapa
kukufundisha, ukipata UFAHAMU wa kutosha juu ya
jambo fulani ni rahisi kukabiliana nalo kwa ufasaha!
Mithali 29:11 "Mpumbavu hudhihirisha Hasira Yake
yote, Bali mwenye Hekima huizuia na kuituliza."
Umeona? Mwenye hekima huizuia na kuituliza hasira!
Kwa hiyo uwezo wa kuituliza na kuizuia hasira yako
unategemea Kiwango cha hekima na uelewa wako!
Pia Mithali 14:29 "Asiye mwepesi wa hasira
anafahamu nyingi. Bali mwenye Roho ya hamaki
hutukuza upumbavu."
Zaidi ya hayo Mithali 16:32 "Asiye mwepesi wa hasira
Ni mwema kuliko shujaa, na Mtu aitawalaye roho
Yake kuliko mtu atekaye mji."
33
SAMEHE KWA FAIDA YAKO!
Kusamehe ni njia moja nzuri na rahisi Sana kumaliza
hasira! Kama Kuna mtu alikukosea na kukusababishia
hasira hizo, basi dawa nzuri ni kumsamehe!
Ukimsamehe moyo wako utafunguka na hautasikia
hasira juu yake!
Mithali 19:11 "Busara ya Mtu huiahirisha hasira
Yake. Nayo ni fahari Yake KUSAMEHE makosa."
EPUKA UKARIBU NA MTU MWENYE HASIRA
KALI.
Hasira wakati Mwingine inaambukizwa! “contagious”!
Inaambukizwa, kuenea na kusambaa! Ukiwa na urafiki
na Mtu mwenye hasira ni rahisi kuiga tabia zake! Ndiyo
maana Kuna makabila hapa Tanzania yanajulikana
kabisa kwa hasira na mapanga! Kwa nini? Wanaigana
tu! Hii huitwa "imitation"
Mithali 22:24-25 "Usifanye Urafiki na mtu mwenye
hasira nyingi, Wala usiende na Mtu wa ghadhabu
nyingi. Usije ukajifunza njia zake na kujipatia nafsi
yako mtego."
Hali hii inanikumbusha kipindi fulani nikiwa
mwanafunzi, kijana mmoja rafiki yangu (mwenye asili
ya hasira hasira) alinishawishi tukampige mkwara
mwalimu mmoja tuliyekuwa tunaamini ni mnoko sana
pale shuleni!
34
Nilikubali na tukaenda, tulichokifanya kidogo Mimi
nifukuzwe shule!
JE, TUSIKASIRIKE KABISA?
Waefeso 4:26-27 "Mwe na hasira, ila msitende
dhambi; Jua lisichwe na uchungu wenu bado
haujawatoka." Wala msimpe nafasi ibilisi."
• Kukasirika kwa muda mrefu ni kumpa shetani
nafasi ya kufanya uhalifu kwa kutumia Mikono
au Mdomo wako."
Kumbuka hasira imetajwa Kama matendo ya mwili
yasiyo na kibali kwa Mungu! Mwenye hasira hawezi
kuingia mbinguni!
Wagalatia 5:19-20 "Basi matendo ya mwili Ni
dhahiri, ndiyo Haya. Uasherati, ufisadi, uchawi,
uadui, ugomvi, wivu, HASIRA, Fitina faraka uzushi
husuda etc.
NI IPI SULUHU YA KUDUMU?
Hakikisha Roho Mtakatifu anakaa ndani yako na
kukuongoza, Yeye Ni kinyume na hasira!
Wagalatia 5:22-23 "Lakini tunda la Roho Ni
UPENDO, furaha, Amani, uvumilivu, utu wema,
fadhili, uaminifu, upole, kiasi juu ya Mambo hayo
hakuna sheria."
*Tafakari, chukua hatua !
35
SURA YA NNE
HOFU NI UGONJWA
HOFU ni hali ya kuwa na hisia hasi, hisia hizi
huambatana na woga, wasiwasi, mashaka, mfadhaiko,
msononeko,na kukata tamaa au kutoamini!
Katika maisha ya kila siku faida za HOFU ni chache
sana au hazipo ukilinganisha na kinyume chake yaani
"UJASIRI"
36
zote uzijuazo zimesheheni watu waliokataa kuwa waoga!
Zinazungumzia watu majasiri!
MUNGU ANASEMAJE?
37
1Yohane 4:18 "Katika pendo hamna hofu, lakini
pendo lililo kamili huitupa nje hofu, kwa maana
HOFU INA ADHABU"
TABIA ZA HOFU.
38
Kumbukumbu la torati 20:8 “Tena maakida na
waseme zaidi na watu, wawaambie, ni mtu gani aliye
hapa tena mwenye hofu na moyo mnyonge? Aende
akarudi nyumbani kwake, isije mioyo ya nduguze
ikayeyuka mfano wa moyo wake.”
39
MUNGU AKITAKA KUKUTUMIA
ANAOKUONDOLEA HOFU KWANZA
40
KWA NINI HOFU NI DHAMBI?
UMEONA KITU?
41
UJASIRI SIYO UKATIRI WALA KIBURI
42
muda wa kufanya tathmini juu ya vita hivyo
wanavyopigana bila kujua vimeisha au mapambano
yanaendelea!
BADILIKA!
Unaogopa kiongozi wa mtaa
Unaogopa mkuu wa idara
Unaogopa kasisi
Unaogopa mama/baba mkwe
Unaogopa mawifi/shemeji zako
Unaogopa Wachawi
Unaogopa shangazi/baba mdogo
Unaogopa waganga wa kienyeji
Unaogopa mijusi, bundi,njiwa
Unaogopa serikali
Unaogopa kufa
Unaogopa kuoa/kuolewa
Unaogopa kuanzisha biashara
Unaogopa kuweka hadharan msimamo wako
Unaogopa nini?
Kama unahangaika na hofu na inakukera, basi chukua
hatua ya imani leo! Kuwa chochote MUNGU
Alichokusudia uwe.
43
SURA YA TANO
44
Ndiyo kabisa! Kwa habari ya unajisi huwezi kunajisika!
Na ndiyo maana hata mimi siwezi kukuhukumu kwa
suala la chakula na vinywaji! Kwa Maana aliyezaliwa
mara ya pili hawi chini ya maagizo na makatazo ya hapa
na pale yasiyokuwa kwa jinsi ya Kristo.
Hapa Mtume Paulo anasema
Wakolosai 2:16 "Basi Mtu asiwahukumu ninyi katika
vyakula au VINYWAJI au kwa sababu ya sikukuu
au mwandamo wa mwezi au sabato."
Tena kwa asili kabisa hakuna kitu najisi hata kimoja
(Warumi 14:14)
Kumbuka baada ya uumbaji kukamilika, Mungu aliviona
vyote alivyiviumba kuwa ni vyema na vya kupendeza,
hakuona unajisi! (Mwanzo 1:25)
KAMA NI HIVYO, JE POMBE NI SAWA?
Ufunuo wa wazi wa kibiblia unamtaka mtu aliyezaliwa
Mara ya pili, aishi kwa kutumia AKILI zake vizuri na
ipasavyo!
1Wakorintho 15:34 "Tumieni akili Kama ipasavyo,
Wala msitende dhambi Maana wengine hawamjui
Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe."
Ikiwa biblia inatambua na kuthamini matumizi ya Akili,
naamini utaelewa sawia ninachoenda kukizungumzia
mapema iwezekanavyo!
45
HALALI LAKINI HAIFAI
Hapa panahitaji utulivu kidogo! Kuna Mambo mengi
sana hayafai kabisa kiafya japo ni halali. Kwa mfano
uvutaji wa sigara kwa sheria za Tanzania ni halali kabisa
japo haufai. Mpaka wazalishaji wa sigara huweka onyo,
kwamba uvutaji wa sigara ni hatari kwa Afya! Ni hatari
japo imethibitishwa na tbs! Kwa nini hawaachi
kuzitengeneza? Wanataka Akili yako ifanye kazi!
Ukiacha kuvuta hawawezi kuzalisha zingine!
Sasa sikia neno lisemavyo!
1Wakorintho 6:12 "Vitu vyote ni halali kwangu,
Lakini si vyote vifaavyo. Vitu vyote Ni halali kwangu
Lakini Mimi sitatiwa Chini ya Uwezo wa kitu
chochote."
Yawezekana Ni halali kabisa, sawa, lakini je
inafaa?
Yawezekana Ni halali, lakini Swali je, imeletea
uraibu? Umekuwa tegemezi kwa bidhaa hiyo?
Unaweza kuongezea 1Wakorintho 10:23-26
Kwani sumu Kama benofos siyo halali? Ni halali. Je
inafaa? Ndiyo inafaa kwa kuua wadudu shambani . Je,
ukiinywa? Ni uamzi wako, maana siyo najisi sawa lakini
kwa hakika inaua!
Inaweza ISIWE najisi lakini ikawa na Athali
hasi/mbaya.
46
Kwenye uhalali na kufaa, ndipo panadai
uwekezaji wa Akili yako na utashi ili uamue
vyema!
UMUHIMU WA KUTAMBUA NAFASI YAKO
Hili ni Suala wazi Sana, Mtu anayejitambua vyema na
anafahamu aina ya majukumu yake huamua ikiwa awe
mnywa POMBE au la.
48
Umeuona mbadala wa POMBE? Ni Kujazwa Roho
Mtakatifu !
49
Wagumu kuelewa Paulo aliwashauri hivi
Tito 2:3 "Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na
mwenendo wa Utakatifu; Wasiwe wasingiziaji,
wasiwe Wenye kutumia mvinyo nyingi, Bali
wafundishao mema."
Zaidi Mtume Paulo aliutaja ulevi katika kundi moja na
ugomvi, uchawi, uasherati, ufisadi, uchawi, uadui,
ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda,
ulevi, ulafi nk!
Soma hapa Wagalatia 5:19-20
50
Na ndiyo maana Kuna Mambo mengi hujitokeza baada
ya kulewa kama vile
Mithali 23:29-35 "Ni Nani apigaye yowe? Ni Nani
aliyae ole? Ni Nani mwenye ugomvi? Ni Nani
mwenye mguno? Ni Nani aliye na JERAHA zisizo na
sababu? Ni Nani aliye na macho mekundu? Ni wale
wakaao kwenye mvinyo, waendao kutafuta divai
iliyochangamka......." Tafuta usome pote!
ZAIDI ya hayo?
Mithali 20:1 "Mvinyo hudhihaki, kileo huleta ugomvi
na akosae kwa vitu hivyo hana hekima."
Ukijidhalilisha, kuaibisha kwa sababu tu ya
pombe jua wazi huna hekima !
51
POMBE INALETA UMASIKINI NA
KUTELEKEZA MAJUKUMU.
Kama mshauri, Nimeshauri wanafunzi wengi Sana wa
sekondari, msingi na vyuo vya Kati, ambao masomo yao
yameathirika Sana kutoka na ulevi wa wazazi wao!
Ndoa nyingi na familia zinaomboleza kwa ajili ya
Pombe!
Halafu mtu mmoja "anasisitiza" pombe ilibarikiwa
kabisa kwenye harusi ya kana ,,,,,aibu!
ELEWA KUWA
1 Timotheo 5:8 "LAKINI mtu yeyote asiyewatunza
walio wake, yaan wale wa nyumbani mwake, hasa
ameikana imani. Tena ni mbaya kuliko asiye amini."
Pombe imewafanya watu wangapi waikane imani kwa
kutokujali wenzi na familia zao? Mimi ni zao la jamii hii
ya Tanzania, utanidanganya nini juu ya Pombe?
Wanandoa wangapi wamezini kisa Pombe?
Familia ngapi zimevurugika kisa Pombe?
Kuna Vijana wangapi wamepata magonjwa ya
zinaa na UKIMWI Kama matokeo ya ngono
zembe kwenye clab za Pombe?
Makasisi wangapi wamedhalilika na kudhalilisha
kanisa kisa Pombe?
52
SIKIA WEWE KIZIWI NENO LA BWANA
Mithali 21:17 "Mtu apendaye anasa atakuwa
masikini, apendaye MVINYO na mafuta hatakuwa
tajiri."
Hapa Tanzania, familia nyingi ziko kwenye mstari wa
umasikini wa kutupwa, hasa vijijini kutokana na Pombe
tu! Kama hujui, jua hivyo kuanzia Sana!
Katika kiwango cha umasikini wa mtu mmoja mmoja na
familia unaweza kugundua kuwa umaskini
unasababishwa na Pombe kwa asilimia zisizopungua 75.
Usitake Sana kubishania Mambo ya kipumbavu! Kwani
huna ndugu, jamaa, rafiki, jirani, classmates etc aliyepata
majanga na kuharibu kabisa hatima Yake kutokana na
Pombe?
KWA NINI MAKANISA BAADHI YANAPIGIA
CHAPUO POMBE?
1. Akili za kinabii Tito
Yesu alilewa, na sisi tulewe jamani ! kwa maana
imeandikwa hivyo katika Luka 7:33-35
Nilishangaa watu wakimcheka nabii Tito
kwamba anapotosha, wakati kwa masikio yangu
nimesikia kwenye mahubiri zaidi ya Mara kumi
Makasisi wakihubiri hivyo kuanzia kwenye dini
yangu?. Kwa hiyo kina TITO Wapo kila Kona,
kila dini na kila dhehebu, sema wengine
53
wanaheshimika, wengine wanadharaulika, lakini
akili yao moja!
Yesu hakuwahi kuwa mlevi, aliitwa hivyo na
wapinzani wake wakuu, hasa mafarisayo
2. Mtume Paulo aliagiza tunywe pombe!
Ila Nyinyi watu, Paulo aliagiza wapi?
Aliagiza hapa!
1 Timotheo 5:23 "Tokea Sasa usinywe maji tu, Lakini
tumia MVINYO kidogo kwa ajili ya tumbo lako, na
magonjwa yanayokupata Mara kwa Mara."
Jamani, hata kwa akili za usiku ni kweli Paulo anaagiza
hapo tunywe pombe? Hata kwa Akili zangu za darasa la
kwanza Mwishoni mwa miaka ya 90 kule shule ya
msingi Kawekunelela-Ushetu Kahama, ningeelewa
hivyo?
Kwamba, Wakristo wote tunaumwa tumbo? Na
tunapatwa na magonjwa Mara kwa Mara ambayo tiba
yake ni kwunywa pombe?
Pombe Kama dawa haina shida, Maana hata majani ya
bangi hutengenezwa dawa na kemikali nyingi zifaazo
kwa tiba! Kama daktari kakwambia hivyo sawa, Lakini
usihalalishe uraibu wako kwa kigezo cha dawa wakati
huna ugonjwa unaotibika kwa Pombe.
4. Inaleta furaha ya moyo!
Zaburi 4:7 na zaburi 104:15
54
Elewa wazi kuwa, Hii ilikuwa njia nzuri kwa watu wa
agano la kale kujiliwaza kwa Sababu Roho Mtakatifu
alikuwa bado hajamwagwa! Leo hatutegemei Pombe
kufurahi, badala yake tunafuraha Kama matokeo ya
kuongozwa na Roho Mtakatifu!
Wagalatia 5:22 "Lakini tunda la Roho Ni UPENDO,
furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili,
uaminifu, upole na kiasi.
Unasaka furaha kwenye Pombe? Fikiri
kiungwana!
Ndiyo maana nimetangulia kusema kule juu na
Hapa nakumbusha tena
Waefeso 5:18 "Tena msilewe kwa mvinyo ambamo
man ufisadi Bali mjazwe Roho Mtakatifu."
Zaidi ya hapo Nisemeje?
4.Kuondoa mawazo!
Mithali 31:6-7 "Mpe kileo yeye aliye karibu na
kipotea, kaMpe divai yeye aliye na uchungu nafsini,
Anywe akausahau umasikini wake, asiikumbuke
Tena taabu Yake."
Kwa kawaida shida, dhiki, umasikini na uchungu nafsini
havitoki kwa kunywa Pombe. Zaidi vinakupa unafuu wa
muda mfupi “temporary relief” na Pombe ikiisha
55
matatizo unayakuta yanakusubiri! Wanasaikolojia wote
wanaomjua Mungu na WAPAGANI hawawezi
kukushauri kunywa Pombe kumaliza.matatizo yako!
MWISHO Kama umesoma na kuelewa Basi fanya uamzi
wako Mwenyewe!
56
SURA YA SITA
UKWELI KUHUSU URAIBU (ADDICTION)
MASWALI YA KUJIULIZA
1. Umetumia tumbaku, ugoro, pombe, bangi,
mirungi, sembe nk?
2. Umekuwa muumini mwaminifu sana wa
kutazama picha na video za ngono?
3. Umekuwa ukikaa na kuperuzi mitandao ya
kijamii muda wote napengine huelewi nini hasa
unakitafuta lakini huwezi kujizuia?
4. Vipi kuhusu mawazo, fikra na hisia za ngono,
zinakujia mara kwa mara?
5. Huwezi kushiriki tendo la ndoa bila kutumia
“booster” kwanza?
6. Unajichua? Unapiga punyeto?
7. Unathamini mpira, kiasi kwamba unaweza
kutoroka saa ya maziko au ratiba yoyote muhimu
ili ukaangalie mpira?
8. Unakaa kwenye runinga muda mrefu mpaka
wakunyang’anye rimoti?
9. Vipi, kuhusu kujiona mnafiki, na kujihukumu
wewe mwenyewe kutokana na ‘tabia’ yako
Fulani chafu ya gizani iliyokushinda kabisa
kuiacha?
10. Nini kinatawala sehemu kubwa ya maisha yako?
57
JIBU LOLOTE JUU YA MASWALI HAYO
LIKUPE KIU NA HAMASA YA KUSOMA SURA
HII KWA TAFAKARI.
60
kila kitu ni halali kabisa, lakini hatupaswi kutawaliwa
na chochote!
1wakorintho 6:12 Vitu vyote ni halali kwangu, lakini
si vyote vifaavyo; vitu vyote ni halali kwangu, lakini
mimi sitatiwa chini ya uwezo wa kitu chochote.
Kimsingi baada ya uasi wa wazazi wa kwanza pale
Edeni, miongoni mwa athali alizozipata mwanadamu ni
pamoja na kutawaliwa na viumbe, mimea, mpaka hisia
zake mwenyewe! Kifupi itoshe kusema kwamba
alishindwa kutawala na kujitawala, ndiyo chanzo cha
uraibu!
Ndiyo chanzo cha kuanza kutawaliwa na tumbaku,
bangi, vinywaji na kadharika. Pamoja na viwanda
vinavyotengeneza sigara kuweka onyo kali kuwa
‘uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya,’ lakini bado kuna
ongezeko kubwa la uvutaji wa sigara!
Kwa kifupi ni muhimu kuwapandikizia watoto wetu na
vijana mawazo ya kwamba hawajazaliwa watawaliwe na
kitu chochote! Wamezaliwa ili watawale kila kitu mpaka
hisia zao!
Kwa sababu, mtu asiyetawala hisia zake tayari ni tatizo!
Neno la Mungu linasema katika
Mithali 25:28 Asiyetawala roho yake ni mfano wa mji
uliobomoka, usio na kuta.
Na mithali 16:32 Asiye mwepesi wa hasira ni mwema
kuliko shujaa, na mtu aitawalaye roho yake kuliko
mtu atekaye mji.
61
Kwa ufupi biblia inamsifia mtu mwenye kutawala hisia
na tamaa zake kwamba ni zaidi za shujaa, lakini vilevile
imeweka wazi kuwa mtu asiyetawala roho yake ni kama
mji uliobomoka usio na kuta!
62
ya sekunde chache au muda huo huo, Kwa sababu hiyo
hazina athali yoyote kwa mtu!
Pili kuna kumbukumbu za muda mfupi hizi huitwa
(short term memory) hudumu kwa muda mfupi na
baadaye husahaulika kabisa!
Lakini kuna kumbukukmbu za kudumu au za muda
mrefu yaani (long term memory) ambazo huhifadhiwa
na kukaa kwa muda mrefu! Kumbukumbu hizi
zinazokaa kwa muda mrefu huitwa “Subconcious mind”
au “unconscious mind” na kwa maana hiyo huweza
kuathili kabisa tabia ya mtu husika bila hata yeye
kujitambua, kwa kuwa huingia kwenye mfumo wa
maisha ya kawaida ya tabia, hisia na hulka za mhusika.
Sasa basi, kama mtu ataijaza akili yake mambo mabaya
kwa muda mrefu, matokeo yake ataanza kufanya mambo
ya kijinga na huo ndiyo hasa utakuwa utaratibu wa
maisha yake ya kila siku!
Mtu aliyezoea kuangalia picha au video za ngono kwa
mfano, hufikia hatua hata asipoangalia tena lakini
akizichota picha na videoz kwenye kumbukumbu za
muda mrefu (subconscious mind) na kuzileta kwenye
kumbukumbu inayofanya kazi kwa wakati huo (working
memory) huweza kuziona kana kwamba ni mubashara
(live) na rangi na sauti zake.
63
maana hiyo zimefanyika kuwa utaratibu wa kawaida
katika kuratibu maisha yao!
MUUNDO WA BINADAMU
Binadamu kamili ni mwili, nafsi na roho. Ili unielewe
vizuri zaidi ngoja niweke hivi! Binadamu ni ROHO
inayoishi kwenye MWILI wenye NAFSI.
Ambapo ili uelewe sawasawa zaidi naweza kukuonesha
hivi;
Mwili+Roho+Nafsi=Binadamu aliyekamilika
Mwili-Nafsi-Roho=Maiti
Mwili+Roho-Nafsi=Kichaa wendawazimu
64
kuwa utaratibu wake wa maisha ya kila siku.
Umenielewa?
Kama umenielewa tuendelee mbele kidogo, Roho
ikishahifadhi mambo ya hovyo hovyo, itakuwa
inaiamrisha nafsi yako na nafsi kwa sababu ilisharuhusu
siku nyingi basi na yenyewe itauamrisha mwili
utekeleze kwa lazima hata kama hautaki. Ndiyo chanzo
cha mtu kujichua bila kutaka, au kuvuta ugoro, sigara, na
kufanya ngono uzembe zenye majuto baadae!
Kuna watu wengi sana wanatamani kuacha mazoea
fulani fulani, lakini imeshindikana kwa sababu tayari
mambo au tabia hizo zilishaingia kwenye (subconscious
mind) MOYO/ROHO na ndiyo maana hawezi kuacha
kujichua, hawezi kuacha kuvuta sigara au kunywa
pombe au kutumia dawa za kulevya nakadharika! Bila
usaidizi wa kiroho pamoja na ule wa kisaikolojia ni
jambo gumu sana kujinasua!
Kama umenielewa itakuwa rahisi sana kwako kuelewa
mafundisho na mantiki za kibiblia hasa kwenye kitabu
cha;
Mithali 5:23 “Linda moyo wako kuliko yote
uyalindayo maana ndiko zitokazo chemchemi za
uzima.”
Kumbe MOYO, kama nilivyotangulia kusema ni ghala
au stoo ya kuhifadhia akiba. Kwa hiyo ni stoo
inayohifadhi taarifa mbaya na nzuri. Kama mtu
amehifadha mambo mema ndipo zitatoka chemchemi za
uzima!
65
Kwa kutambua umuhimu huo wa moyo, ndiyo maana
umeshauriwa kuulinda ipasavyo!
Na ikiwa umehifadhi picha na video za ngono basi hizo
ndizo zitaendesha maisha yako!
Kama unafikiri nadanganya linganisha na Ufafanuzi wa
Yesu Kristo mwenyewe kwenye
Mathayo 12:33-35 “Ufanyeni mti kuwa mzuri na
matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa
mbaya kwa matunda yake mabaya; kwa maana kwa
matunda yake mti hutambulika. Enyi wazao wa
nyoka, mwawezaje kunena mema mkiwa wabaya?
Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo
wake. Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema,
na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya.”
Kama hujaamizi kuwa Moyo (mind) wako ndiyo hazina
inayohifadhi taarifa njema na mbaya linganisha tena na
Mathayo 15:18-19 ‘Bali vitokavyo kinywani vyatoka
moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi kwa
maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, izinzi,
uasherati, wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano.”
Unapoona ujinga unazidi kuongezeka, hata miongoni
mwa watu wazima ni lazima uchunguze na kutafakari
hata vitu wanavyovipa nafasi kubwa kwenye mioyo yao
na bongo zao!
YESU ALIONYA KUJILINDA NA CHACHU
Mathayo 16:5-12 Nao wanafunzi wakaenda hata
ng’ambo, wakasahau kuchukua mikate. Yesu
akawaambia, “Angalieni, jilindeni na chachu ya
66
mafarisayo na masadukayo” wakabishana wao kwa
wao wakisema, ni kwa sababu hatukuchua mikate.
Naye Yesu akafahamu, akawaambia, “Mbona
mnabishana ninyi kwa ninyi, enyi wa imani chache,
kwa sababu hamna mikate?. Hamjafahamu bado,
wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa wale elfu
tano, na vikapu vingapi mlivyoviokota? Wala ile
mikate saba kwa wale elfu nne, na makanda mangapi
mliyookota? Imekuwaje hamkufahamu ya kuwa si
kwa sababu ya mkate naliwaambia? ILA JILINDENI
NA CHACHU YA MAFARISAYO NA
MASADUKAYO, Ndipo walipofahamu ya kuwa
hakuwaambia kujilinda na chachu ya mikate, BALI
MAFUNDISHO YA MAFARISAYO NA
MASADUKAYO.
Yesu anawatahadharisha na kuwaonya wanafunzi wake
wajihadhari na mafundisho ya mafarisayo na
masadukayo! Kwa nini wajihadhari? Ili ujue mafarisayo
walikuwa watu wa aina gani rejea katika
Mathayo 23:1-36 ukisoma hapa, utagundua mara moja
kuwa Mafarisayo kwa ujumla walikuwa wanafiki!
Walipenda kukaa viti vya mbele kwenye sherehe na
ibada, mafisadi, waongo na watu wasiojua kitu yaani
vipofu!
Kwa hiyo, Yesu aliwaonya kwa tafsiri ya kiingereza
(KJV) imeandikwa [take heed] of what you hear! maana
yake [be selective] yaani chagueni vya kusikiliza!
67
KWA NINI MAFUNDISHO MABAYA
ALIFANANISHA NA CHACHU?
68
moja huwa naachana nacho, nahii nidhamu nimeijenga
kwa muda mrefu!
Kwa hiyo, vyote kwa pamoja yaani Mwili, roho na nafsi
vinatakiwa kuwa safi! Havitakiwi kuchafuliwa na jambo
lolote, hasa habari na picha au video zisizofaa.
Tumeshashauriwa kuwa
“linda moyo wako kuliko yote uyalindayo maana
ndiko zitokazo chemchemi za uzima’
lakini pia ni jambo zuri na la kheri kama tukilinda na
viungo vinavyorekodi taarifa mbalimbali na kuzituma
kwenye Moyo. Katika hili neno la Mungu linashauri
hivi;
1Wathesalonike 5:23 Mungu wa amani mwenyewe
awatakase kabisa; Nanyi NAFSI zenu na ROHO
zenu na MIILI yenu, mhifadhiwe mwe kamili, bila
lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu
Kristo.
Kwa hiyo nafsi, roho na mwili ni lazima vitakasike, na
kitu kikitakasika maana yake kitumike inavyopaswa!
Mtume Paulo aliuona uhitaji huu alipowaandikia
wakristo Wathesalonike, anawahimiza na kuwaombea
kwamba Mungu wa amani, Awatakase kabisa katika
maeneo hayo matatu ambayo nimeyazungumzia hapo
juu yaan mwili, nafsi na roho!
69
USHAURI WA KIBIBLI
Marko 9:42-50 “Jicho, mkono, mguu nk
kikikukosesha, kata au ng’oa”
kwa hiyo ni bora kuliong’oa jicho lako kwa habri ya
pornograph!
Zaburi 119:37 “Unigeuze macho yangu, nisitazame
visivyofaa, unihuishe katika njia yako”
70
SURA YA SABA
SHABAHA YA URAFIKI
Urafiki ni hali ya uhusiano, mapatan na /ushirikiano wa
karibu kati ya watu wawili au zaidi wenye malengo
yanayofanana. Urafiki hulenga hasa kusaidiana,
kufarijiana, kutiana moyo, kushauriana, kukosoana nk!
Upo urafiki wenye faida na urafiki wenye hasara. Na
kwa mujibu wa saikolojia ya jamii, marafiki kwa sehemu
kubwa huweza kuathiriana kwa namna moja au
nyingine! Rafiki anaweza kuwa chachu ya mafanikio
kwako au chachu ya kukudumaza kama tutakavyoona
baadaye.
UFALME WA MUNGU UNAUTAZAMAJE
URAFIKI?
Ufalme wa Mungu unautazama urafiki kwa jicho
chanya! Kwamba kuwa na rafiki au marafiki ni jambo
jema na la kheri, hata hivyo umeweka tahadhari na
angalizo juu ya aina ya marafiki, kwani rafiki anaweza
kukubomoa au kukujenga.
SHABAHA YA URAFIKI
Shabaha ua lengo mahususi la urafiki ni kusaidiana,
kutiana moyo, nguvu, kushauriana nk
Rejea hapa!
Mhubiri 4:9-10 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja,
maana wapata ijara njema kwa kazi yao. Kwa maana
71
wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake.
Lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala
hana mwingine wa kumwinua!”
Shabaha ya urafiki ni kuinuana na kutiana moyo! Ni
kusaidiana na kushauriana.
Hii ndiyo ilimfanya Bwana Yesu aboreshe zaidi mfumo
wa kimahusiano kati yetu na yeye ili aweze kutusaidia
zaidi na kwa karibu zaidi. Yaan kutoka hali ya
mahusiano ya kitumwa na kujenga hali ya mahusiano ya
kirafiki zaidi!
Yohane 15:15 “Siwaiti tena watumwa; kwa maana
mtumwa hajui atendalo Bwana wake; lakini ninyi
nimewaita RAFIKI, Kwa kuwa yote niliyoyasikia
kwa baba yangu nimewaarifu.”
*Kumbe ile hali ya kujulishana na kufahamishana
mambo na kila kinachoendelea ni tabia ya urafiki hai.
Huwezi ukawa na rafiki wa kweli na wa dhati ambaye
hakushirikishi kwa lolote katika mambo yake. Huyo siyo
rafiki, labda ni jamaa tu!
Hata katika namna za ibada, Bwana Yesu alitushauri
tusali vikundi vikundi vyenye kupatana kama marafiki!
Mathayo 18:19-20 “Tena nawaambia, ya kwamba
wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo
lolote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu
aliye mbinguni. Kwa maana walipo wawili watatu
wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo
hapo katikati yao.”
72
Huo ndiyo aina ya urafiki unaopaswa katika Ufalme wa
Mungu! Urafiki kwa ajili ya mambo yauhusuo Ufalme
wa Mungu yaani urafiki chanya!
VIGEZO VYA KUWA MARAFIKI.
Suala la kuwa marafiki wa kweli huwa halitokei kwa
bahati tu! Ni mchakato wa asili ambao huweza
kukamilika baada ya wawili hao kuwa wamefanana na
kuendana katika mambo kadhaa kama ifuatavyo!
MFANANO/SIMILARITY.
Katika saikolojia, kigezo kikubwa cha watu kuwa
marafiki ni mfanano. Rejea Gestalt Psychologists
Principles of grouping.
Kufanana huku kuko kwenye kuendana kimawazo na
mitazamo siyo sura na mwonekano!
Yoshua bin Sira 13:14 “Kila kiumbe hupenda
kilichofanana nacho, na kila mwanadamu humpenda
aliyefanana naye. Wanyama wote huandamana wa
aina kwa aina, vilevile mwanadamu ataambatana na
mmoja wapo wa aina yake.”
Huu ndiyo ukweli unaoishi, ni suala gumu kuwa kwenye
urafiki na mtu usiyeendana naye kimawazo! Na ndiyo
maana watu wenye hekima wa zamani sana walipata
kusema hivi.
Mithali 27:17 “Chuma hunoa chuma, ndivyo mtu
aunoavyo uso wa rafiki yake.”
73
Kwa hiyo kama wewe ni chuma basi siyo rahisi kunoana
na ubao! Urafiki wa kweli hufanana katika vigezo vingi!
Kama rafiki yako siyo chuma halafu wewe ni chuma
uwe na uhakika urafiki huo hautadumu, ni kama ngoma
ya watoto tu, haitakesha!
KUPATANA/CONNECTEDNESS
Bila kupatana katika mambo mengi, urafiki huweza kufa
kabisa, kwa hiyo kupatana ndiyo kigezo ambacho
huufanya urafiki udumu na kudumu kwa muda mrefu.
Amosi 3:3 “Je, watu wawili waweza kutembea
pamoja, wasipokuwa wamepatana?.”
Urafiki bila mapatano kwa hakika kabisa hauwezi
kudumu!
IDADI YA MARAFIKI
Hakuna kigezo maalumu cha idadi ya marafiki, hata
hivyo hekima inashauri bora uwe na rafiki mmoja wa
maana, halafu wengine wawe kwenye lile kundi la jamaa
tu!
Kuwa na Idadi kubwa ya marafiki wakati mwingine ni
kuongeza idadi ya maadui, Uzoefu unaonyesha kwamba
maadui wakubwa wa mtu ni watu wa karibu, ni wale
ambao kwa kipindi fulani wamewahi kuwa marafiki!
74
Yoshua bin Sira 6:6 “Wale wenye amani nawe na
wawe wengi. Bali rafiki wa kukushauri mmoja kati
ya elfu.”
75
Kwa nini kila sehemu inasisitizwa kutokumwamini
rafiki? Watu wengi wamesalitiwa na rafiki zao wa karibu
sana!
NJIA YA KUDUMISHA URAFIKI
Katika safari ya urafiki huwa kuna mambo mabaya na
sintofahamu kadha wa kadha hutokea. Sasa yanapotokea
hayo ni muhimu kwa wahusika kuhojiana bila woga ili
kupata ukweli na kuonyana kindugu hali hii husaidia
sana kuboresha, kukomaza na kuupa thamani urafiki kwa
kiwango kikubwa sana!
Yoshua bin Sira 19:13-17 “Mhoji rafiki yako, labda
hakulitenda. Hata iwapo amelitenda yawezekana
asizidi kulitenda. Mhoji jirani yako, labda
hakulisema. Hata iwapo amelisema yawezekana
asiliseme tena. Basi mhoji rafiki yako mara nyingi
huwa masingizio tu, wala usiliamini kila neno. Aidha
kuna atelezaye kwa ulimi, wala si kwa moyo kwa
maana yu nani asiyekosa kwa ulimi wake? Basi mhoji
jirani yako kabla ya kumtisha, uipishe torati yake
aliye juu.”
Changamoto kubwa kwa baadhi ya rafiki zetu kwenye
hili huwa ni moja! Ukimhoji badala ya kukuelewesha
kwa upendo, anakufanya adui mara moja na kukuepuka!
76
Mathayo 18:15-17 “Na ndugu yako akikukosea,
enenda ukamwonye, wewe nay eye pake yenu.
Akikusikiliza umempata nduguyo. Lakini kama
hasikii, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au
wawili, ili kwa vinywa vya mashahidi wawili au
watatu kila neno lithibitike. Na asipowasikiliza wao,
liambie kanisa; na asipowasikiliza kanisa, na awe
kwako kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.”
77
TAFUTA WENYE UWEZO WA KUKUSAIDIA!
Ikiwa una njaa na kiu ya kuwa mtu mwenye hekima,
basi ni busara zaidi kutafuta marafiki watakaokusaidia
kuwa na hekima unayoihitaji!
Mithali 13:20 “Enenda pamoja na wenye hekima,
nawe utakuwa na hekima. Bali rafiki wa wapumbavu
ataumia.”
Karibu katika Ufalme wa Mungu, Ujipatie rafiki mmoja
wa kwali asiye mnafiki, Bwana Yesu,!
78
SURA YA NANE
UHUSIANO WA AFYA YA AKILI NA IMANI
Kupitia uzoefu nilioupata kwa kujifunza historia ya
mwanadamu na maendeleo ya dini, afya ya akili, biblia,
kutafakari na uhalisia wa kinachoendelea kwenye
ulimwengu wa dini na madhehebu, nimeng’amua na
kuhitimisha kuwa “Upo uhusiano mkubwa sana kati ya
afya ya akili na Imani”
KIVIPI?
Mtu amabaye afya yake ya akili siyo bora na thabiti
yupo hatarini zaidi kuamini hoja za
kizushi/kijinga/kipumbavu!
Ni rahisi kuamini propaganda za kidini na mafundisho
ya kipumbavu yenye sura ya dini! Na vilevile mtu
ambaye afya yake ya akili ni bora na thabiti anao uwezo
wa kufikiri, kutafakari na kung’amua kuamini
mafundisho hayo, kuyakataa au kuamini vinginevyo!
Kwa kifupi kabisa, afya ya akili inaanza kutengenezwa
kipindi cha mimba na hata baada ya kuzaliwa! Uchaguzi
mzuri wa vykula kwa mama huimarisha ukuaji wa
ubongo wa mtoto akiwa tumboni, kwa upande mwingine
mjamzito hushauriwa kuacha matumizi ya baadhi ya
dawa, pombe, sigara, bangi nk kama njia ya kulinda afya
ya akili ya mtoto tumboni!
Baada ya kuzaliwa, lishe nzuri na bora ni muhimu sana
kwa ukuaji na maendeleo ya ubongo wa mwanandamu
79
mpaka miaka 5 hivi. Baada ya hapo ubongo wa
mwanadamu hustawi ama kudumaa kutokana na aina ya
mafundisho anayopata, mila, desturi na utamaduni wa
jamii husika! Mafundisho na utamaduni bora huweza
kuchochea ubunifu na kukuza fikra halikadhalika
mafundisho na tamaduni duni hudumaza ubongo. Hata
hivyo matumizi makubwa ya pombe, bangi na dawa za
kulevya huweza kuharibu ubongo wa mwanadamu kwa
kiwango kisichomithilika!
AKILI NDOGO HUDANGANYIKA KIRAHISI
Tito 3:3 “Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa
hatuna AKILI. Tulikuwa waasi,
tumedanganywa…………”
Mtume Paulo anamwambia Tito, tatizo la wao kuwa
waasi, wauaji nk hapo zamani lilisababishwa na kukosa
akili tu! Kwa kukosa akili walidanganyika! Leo hii
vijana wadogo kabisa kwa kukosa akili wanajiunga na
imani za kipumbavu zenye kuleta maangamizi, ukatiri na
maafa kwa familia na jamii zao wenyewe!
NI LAZIMA KUSAILI KILA FUNDISHO
Watu wenye kujiridhisha na ukweli wa mafunmdisho
kwa tafiti na tafakari, biblia imewataja kama
waungwana!
Matendo ya Mitume 17:10-11 “Mara hao ndugu
wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao
walipofika huko wakaingia katika sinagogi la
wayahudi, Watu hawa walikuwa WAUNGWANA
80
kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea
lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza
maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo
ndivyo yalivyo.”
Mwandishi Luka anawatazama watu hawa wa Beroya
kama waungwana kwa sababu mbili muhimu!
Kwanza, waliipokea injili kwa uelekevu wa moyo, na
pili, wakayachunguza maandiko kila siku, waone
kwamba mambo hayo waliyofundishwa ndivyo yalivyo!
Kumbuka kinyume cha uungwana ni ushenzi! Kwa hiyo
kukubali fundisho la kiimani kwa shingo upande au bila
kulisaili ni dalili za wazi kuwa wewe si muungwana! Ni
dalili za kuwa mshenzi! Usipende tu kupiga kelele
ameeeee! Sema babaaa! Bila kusaili
kinachozungumzwa!
Fundisho lolote linalokunyima fursa ya wewe kufikiri,
kutafakari na kung’amua ni fundisho hatari na ni sumu
kwa ubongo wako! Ndiyo maana daima huwa niko
kinyume na mafundisho yenye dogma ndani yake!
Historia imesheheni watu waliowahi kuanzisha vikundi
vya imani za kidini zilizopata uungwaji mkono na watu
wengi, lakini mwisho wa siku wengine walichomwa
moto ama kunyweshwa sumu au kutapeliwa fedha na
mali na viongozi waanzilishi wa vikundi hivyo.
Ukifuatilia kwa karibu sana unaweza kugundua kuwa
dini na madhehebu mengi pamoja na kupingana lakini
wanafanana katika vipengele vingi! Kila dini kwa mfano
81
hutengeneza shuhuda za kusisimua na kustaajabisha
kama njia ya kupamba ama kusindikiza fundisho Fulani
la kidini. Kwa mfano katika dini ya kikristo, fundisho
lolote linalokosa uungwaji mkono kwenye biblia
hutengenezewa shuhuda maridadi pamoja na
kutangazwa kama dogma ya kiimani lengo likiwa ni
kuhalalisha uzushi huo!
Leo hii, maeneo mengi ya dunia yanaomboleza na
kusikilizia maumivu na uchungu mkubwa wa
kulazimishwa kuishi kinyume na dhamiri zao kutokana
na makundi ya wanamgambo wa kidini kuchukua
udhibiti wa maeneo yao! Mauaji ya kutisha naukatili wa
kinyama kote duniani kwa kiasi kikubwa hutekelezwa na
watu wenye masilahi ya kidini!
82
ROHO MTAKATIFU NI KAMA “SOFTWARE”
KWENYE UBONGO!
Mungu aliahidi kumtuma Roho wake mtakatifu kwa
malengo anuai, kama ilivyobainishwa na manabii wa
kale katika
Ezekileli 36:26-27
Yoeli 2:28
83
dhahabu na wa fedha, na wa shaba,Na kukata vito kwa
kutiwa mahali, na kuchora miti; Na kufanya kazi ya
ustadi iwayo yote.”
Lakini hapa pia Mfalme Suleimani alidokeza kuwa dawa
ya ujinga na upumbavu ni kuwa na roho wa Mungu
Mithali 1:22-23
NI SEHEMU YA KAZI ILIYOMLETA YESU
Pamoja na mambo mengine, Kristo Yesu alikuja kutupa
akili!
1 Yohane 5:20 “Nasi twajua kwamba, mwana wa
Mungu amekwisha kuja, naye ametupa AKILI
kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, Nasi tumo ndani
yake yeye aliye wa kweli, yaani ndani ya mwana
wake Yesu Kristo, Huyu ndiye Mungu wa kweli, na
uzima wa milele.”
KWA NINI ENEO LA AKILI LIMEANGAZIWA
SANA KWENYE BIBLIA?
Neno la Mungu linaweka mkazo wa kipekee kwenye
“Akili” maarifa na ufahamu kwa sababu vitu hivyo
vikienda likizo kuna uwezekano wa kupokea imani
potofu!
Tazama hapa kwa mfano!
Hosea 4:6 “Watu wangu wanaangamizwa kwa
kukosa maarifa; kwa kuwa wewe umeyakataa
maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani
84
kwangu mimi; kwa kuwa umeikataa sheria ya
MUNGU wako mimi nami nitawasahau watoto
wako.”
Pia katika Isaya 5:13 “Kwa sababu hiyo watu wangu
wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na
maarifa.”
85
UBONGO UNATANUKA PALE UNAPOTUMIWA
Waebrania 5:14 “Lakini chakula kigumu ni cha watu
wazima, ambao AKILI zao kwa KUTUMIWA,
zimezoezwa kupambanua mema na mabaya.”
Kwa hiyo, akili inapotumika ndipo utaanza kuwa mtu
mzima kichwani! Na hapa Paulo anashauri hivi
1Wakorntho14:20 “Ndugu zangu msiwe watoto
katika AKILI zenu, lakini katika uovu mgeuzwe
watoto wachanga bali katika AKILI zenu mkawe
watu wazima”
MATUMIZI YA AKILI HADI KWENYE NYIMBO
NA MAOMBI
1Wakorintho 14:15 “Imekuwaje basi? Nitaomba
Kwa roho tena nitaomba Kwa AKILI pia; Nitaimba
Kwa roho, tena nitaimba kwa AKILI pia.”
1Petro4:7 “Lakini mwisho wa mambo yote
umekaribia, basi iweni na AKILI, Mkeshe katika
sala”
Umeona kitu? Hata kukesha kutanguliwe na matumizi ya
akili! Maana bila akili tumeshuhudia watu wakifanya
maovu hukohuko kwenye mikesha ya maombi!
MAFUNDISHO UNAYOPATA YANA AKILI
NDANI YAKE?
Elimu dunia huanzia chekechea mpaka chuo kikuu! hapo
katikati vipo vyeti, diploma, shahada za awali, uzamili,
86
udhamifu mpaka uprofesa “professorship”! Hata
uprofesa utakuta viwango e.g associate professor mpaka
full professor! Hata elimu ya Ufalme wa Mungu huanza
na mambo mepesi mpaka yale ya juu au kwa lugha
nyepesi naweza kusema mambo yale magumu!
Kwa mfano
Yesu alilazimika kuacha kufundisha baadhi ya mambo
kwa sababui wanafunzi wake walikuwa wachanga bado
kiakili na kiimani. Soma hapa
Yohane 16:12-13 “Hata bado nikali ninayo mengi ya
kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa,
Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli,
atawaongoza awatie kwenye kweli yote………..”
JE, kanisa lako linakupa fursa ya kukua kiimani na
kiakili? Au viongozi tu ndiyo wanaosoma na
kujiendeleza, wewe huna cha maana ukijuacho kuhusu
imani yako na Ufalme wa Mungu kwa ujumla na
umebaki kuwa muhanga wa kutoa michango tu
wanayoipanga na kuiamua?
UNA HAKI YA KUYAJUA MAMBO MAGUMU
1Petro 2:2 “Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa
yatamanini maziwa ya AKILI Yasiyoghushiwa ili
kwa hayo mpate kuukulia wokovu”
Haya maziwa ya akili ni mafundisho ya juu, ya
kukufanya ukue kiakili na kiimani!
87
JUHUDI ZA KIDINI NI LAZIMA ZITAWALIWE
NA AKILI
Najua unampenda Mungu sana! Kumpenda Mungu ni
lazima kudhibitiwe na kutawaliwa na matumizi ya akili.
Kwa maana tumeshaona pale juu kwamba akili ni paji
ama kipawa kutoka kwa Mungu, kwa hiyo kutumia akili
siyo dhambi bali ni utii kwa mwenye kutuluzukia kipawa
hicho cha akili!
Warumi 10:2 “Kwa maana nawashuhudia kwamba
wanajuhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika
maarifa.”
Watu wa Rumi walikuwa na juhudi kubwa sana kwa ajili
ya Mungu kama ilivyo kwa madhehebu takribani yote,
hata hivyo akili/maarifa yalikuwa yamewekwa pembeni!
IMANI POTOFU NI TATIZO LA AKILI SIYO
IMANI
Kuna watu mpaka leo wanafundishana na kushikiria
mambo yaliyotolewa ufafanuzi zaidi ya miaka 2000
iliyopita na yakaeleweka! Tatizo hapo siyo shetani wala
imani aslani! Hilo ni tatizo la akili!
88
na mabaki hutolewa nje kama kinyesi! Alisisitiza
kuwa hakuna chakula kinachoweza kuingia
moyoni!
89
usaili matokeo yake ni hayo! Unakuwa msukule
ulioenda shule na ukapata vyeti na ajira!
90
Ukweli huo bado upo mpaka leo, kwani hekima
ndiyo ufunguo pekee wa maisha! Na ndiyo
maana leo ukimwomba Mungu kwa imani na
bidii, anakupa Roho mtakatifu aliye chanzo cha
hekima yote! Luka 11:13
91
Paulo hakuishia kwa wakolosai tu, sala hii pia
aliwaombea Wafilipi!
92
RUKWA NA AKILI KWA AJILI YA
MUNGU, KUWA NA HEKIMA KWA AJILI
YA KANISA!
93