MAKALA VITABU12

You might also like

Download as pdf or txt
Download as pdf or txt
You are on page 1of 3

MASWALI KUHUSU VITABU YANAHITAJI MAJIBU

Na.Magabilo Masambu

Siku za hivi karibuni mpaka sasa tumeendelea kusikia taarifa


mbalimbali za matendo yanayokiuka maadili yetu kama taifa. Si
utamaduni wetu wala taifa halijawahi kufundisha mahala
kwasababu tukisoma miongozo mbalimbali ya elimu hakuna
sehemu tunaweza kuyapata mafundisho yenye kuvunja maadili
yetu, ni mambo ya kushangaza na ya aibu katika jamii zetu.

Nilizungumza na mzee John Mollel kupata maoni yake kuhusu


masuala haya kujitokeza zaidi nyakati hizi. Yeye kwa upande wake
akahusisha mambo haya na imani za kishirikina anasema
“haiwezekani baba mzazi kumlawiti mwanaye bila imani za
kishirikina, kwasababu siyo mambo ambayo tumekua tukiyaona
tangu utoto wetu” Wengine wanadai uasi juu ya Mungu ni mkubwa
pamoja na kwamba, tunazo nyumba nyingi za ibada. Wengine
wanadai ni mmomonyoko wa maadili kutokana na utandawazi,
mitazamo juu ya masuala haya ni mingi.

Lakini wakati haya yakiendelea mnamo tarehe 13 February 2023


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Adolf Mkenda
akajitokeza mbele ya waandishi wa habari akiwa na orodha ya
vitabu 16 alivyovipiga marufuku kwa mamlaka aliyopewa chini ya
kifungu cha 59 cha Sheria ya Elimu sura 353 ili visitumike katika
shule za umma wala binafsi. Akaeleza kuwa vitabu hivyo vina
maudhui yanayokinzana na mila, desturi na utamaduni wa
Mtanzania na vinahatarisha malezi bora ya watoto na vijana wetu.

Baadhi ya vitabu hivyo ni Diary of a Wimpy kid-cabin, Diary of a


Wimpy kid, Diary of a wimpy kid-Rodrick Rules, Diary of wimpy
kid-Last Straw, Diary of wimpy kid-Dog days, Diary of wimpy
kid-The ugly Truth. Vingine ni Is for TRANSGENDER, Is for LGBTQIA
na Sex Education a Guide to life. Prof.Mkenda hakuishia hapo tu
lakini pia akatoa namba za simu ikiwa vitabu kama hivyo
vitaonekana mahala popote basi watu waweze kutoa taarifa katika
kupitia zifuatazo 02622160270 au 0737962965. Mwisho
akamaliza kwa kuwaomba wazazi na walezi kufuatilia kwa karibu
kubaini kama aina ya vitabu hivyo vitatumika au vingine vyenye
maudhui kama hayo.
Taarifa hii ikanifanya nipate maoni ya baadhi ya watu, mmojawapo
ni Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi ndugu Joseph Selasini
ambaye kwa maoni yake kwanza, alieleza umuhimu wa nchi
kulinda ustaarabu wake kwa maana ya maadili kama, pili akawa na
maswali kadhaa ambayo anasema waziri alipaswa kuyajibu katika
maelezo yake.

Swali la kwanza vitabu hivyo viliingiaje nchini? Je, vilipitia uwanja


wa ndege au bandarini?, licha ya kuingia nchini viliingiaje
mashuleni? Je, ni shule gani za Serkali au binafsi? je, idara ya
ukaguzi Tanzania imekufa? Au wanakagua nini? Kama
wanakwenda kukagua huwa hawakaguwi vitabu vya kufundishia?
Je idara ya usalama wa taifa kazi yake ni kulinda viongozi tu? Je
wakati wa uingije wake TRA walipokea kodi bila kukagua na kama
walikagua waliruhusuje ikiwa vinakwenda kuharibu maadili ya
watoto wetu?

Selesini aliendelea kuhoji kwanini shule hazikutajwa, je watoto


walipewa vitabu na nani? Kama vilikutwa mashuleni kwanini hizo
shule hazikutajwa ili kuondoa sintofahamu? Je wakati watoto
wanavitumia uongozi wa shule na walimu kwa ujumla hawakujua
kama havistahili? Mwisho ndugu Selesini akatoa ushauri kwa
Serikali kwamba kuna umuhimu wa kubaini wale wote waliohusika
kuhakikisha vitabu hivyo vinatumika mashuleni wanajulikana na
hatua kali zichukuliwe dhidi yao na akaongeza kuwa wao kama
chama cha NCCR-Mageuzi wanapinga vikali masuala hayo
kwasababu yanakwenda kuharibu maadili na utamaduni wa
kitanzania.

Kwa maoni yangu nadhani bado kuna jambo kubwa la kufanyika


taarifa juu ya kufungia vitabu tu haitoshi kama alivyohoji ndugu
Selasini hapo ni jambo zito hilo. Lazima tathimini na uchunguzi wa
kina ufanyike kubaini athari za vitabu hivyo, vimeshaathiri watoto
kwa kiasi gani? Tangu vimeanza kutumika vina muda gani? Je
madhara yake ni makubwa kiasi gani ili tusije kuwa tunahangaika
na matawi, wakati mizizi ilisha mea zamani pengine inawezekana
tuhuma za baadhi ya shule kuhusika na uchafu huo ni matokeo ya
vitabu hivyo.

Kutaja majina ya shule ilikuwa na tija zaidi kwasababu ingesaidia


wazazi kuhamisha watoto wao katika shule hizo, kwasababu
maadili na malezi ni muhimu zaidi kuliko biashara ya mtu.
Hatuwezi kukubali watoto wetu waharibike kwa kufanikisha
biashara za mtu, kutotaja majina ya shule maana yake wazazi
wataendelea kupeleka watoto wao katika shule hizo bila kujua.
Kama shule inafikia hatua ya kufundisha au kukubali vitabu vya
aina hiyo vitumike, maana yake watoto wameshafundishwa mengi
zaidi. Kwahiyo pamoja na uchunguzi wa vitabu, ufanyike uchunguzi
wa kidaktari juu ya watoto wote wanaosoma kwenye shule
zilizokutwa na vitabu hivyo.

Kama tutaona haya kuyakemea mambo haya waziwazi maana


yake tunaandaa taiba la ajabu sana, tutapoteza nguvu kazi ya taifa
hili, hatutakuwa na vijana wenye uwezo wa kuijenga nchi kwa hapo
baadaye, na hapa walegwa zaidi ni watoto wa kiume, tukatae
ujinga huu kwa vitendo ni bora tule nyasi kuliko kukubali taifa
liangamie.

Mwisho nimshukuru waziri mwenye dhamana kwa hatua


alizochukua, lakini hatua zaidi zinahitajika. Kwa upande wa wazazi
nao ni muhimu kulinda watoto wetu, tusiamini sana shule
wanakosoma kwasababu matendo haya sasa yanafanywa popote,
tuliyokuwa tunawaamini nao siku hizi wanatuhumiwa, hata
nyumbani tusiaminiane sana maana unyanyansaji wa kijinsia
umekuwa ukifanywa na watu wa karibu kabisa, ambao huwezi
kuamini unakuja kushtuka mtoto alishaharibiwa.

Lakini kama jamii lazima tutafakari kwa kina tumepatwa na nini?


Kwanini matukio haya yanaongezeka kwa kasi zaidi? Tunataka
kuifanya nchi hii kuwa Sodoma na Gomora? Hatuoni kama
tunamkosea Mwenyezi Mungu? Tunalalamika mvua hakuna kwa
maasi kama haya neema itatoka wapi? Mashirika yachunguzwe
ikiwa ni pamoja na fedha wanazopewa tukiacha holela tu
tutaangamia.

0689157789
magabilomjalifu@gmail.com
DAR ES SALAAM-TANZANIA

You might also like