Professional Documents
Culture Documents
Form ya mkopo
Form ya mkopo
Form ya mkopo
ROHO
MTAKATIFU
YALIYOMO
YALIYOMO ………………………………………………………………….3
TABARUKU. ……………………………………………………………………………………4
LENGO LA KITABU……………………………………………………………………………5
1 wathesalonike 5:19
Msimzimishe Roho;
Hesabu 11:26-29
[26]Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la
mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa
Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa
miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa
hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri
kambini.
[27]Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda
akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi
wanatoa unabii kambini.
[28]Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa
tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana
wangu Musa, uwakataze.
[29]Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa
ajili yangu; ingekuwa heri kama watu wote wa
BWANA wangekuwa manabii na kama BWANA
angewatia roho yake.
1 Samuel 19:23-24
[23]Basi akaenda Nayothi huko Rama, na roho ya
Mungu ikamjilia yeye naye, akaendelea mbele, huku
anatabiri, mpaka kufika Nayothi huko Rama.
[24]Naye akavua nguo zake, akatabiri mbele ya
Samweli, akalala uchi mchana kutwa na usiku kucha
siku ile. Kwa hiyo watu husema, Je! Sauli pia yumo
miongoni mwa manabii?
Ukisoma kwenye Hili andiko utaona jinsi sauli
alivyofurikiwa na Roho Mtakatifu kuanzia mbali
kabisa, hii inaonesha hakuzuiliwa wala hakukatizwa
mpaka Roho Mtakatifu alipomaliza Kazi yake ndani
yake na hivi ndivyo tunavyotakiwa kumpa nafasi
huyu MUNGU Roho Mtakatifu bila kuwaza Kuwa
Muda umeenda au nipo ofisini au wataniona ni wa
kiroho sana au watu watanifikiria mimi sina
utaratibu au sio mstaarabu.
1 wakorintho 2:4-5
[4]Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa
kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za
watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
[5]Ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu,
bali katika nguvu za Mungu. Hekima ya Kweli ya
Mungu
SURA YA PILI
DALILI ZA ROHO MTAKATIFU
1)Kunena kwa Lugha
Marko 16:17
[17]Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa
jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha
mpya;
Mfano;
Mwaka 2018 nikiwa kidato cha sita na nakaribia
kufanya mitihani ya Taifa nilienda DIT kwa rafiki
yangu Deo kumtembelea hivyo nililala hapo sasa
asubuhi yake nilipoamka nilisikia msukumo wa
ajabu wa kunena kwa Lugha hivyo nikaruhusu ile
hali yaani nikawa nanena kwa lugha tangu
nilivyoamka mpaka nikiwa naeleka Shuleni Tambaza
na nilivyofika maeneo ya pale faya mjini nikiwa
nataka kuvuka barabara gari ikasimama na dereva
akanionesha ishara ya kuniruhusu nipite na nikiwa
napita akatoa gari na kunigonga huku nikiwa
nanena kwa lugha unajua nini kilitokea sikuumia
wala kuchubuka na huku naendelea kunena kwa
lugha kwa sauti ya chini chini lakini nikiwa
nimemaanisha, Sikia shetani alipanga nipate ajali
lakini MUNGU akaepusha mauti Kupitia kunena kwa
lugha ndio maana Biblia inasema huwa tunaponena
ni Roho Mtakatifu akiwaombea watakatifu kwa
kuugua haleluya na mimi na wewe ni mmojawapo
wa watakatifu hivyo inaonesha kuwa tunaponena
kwa lugha tunatengeneza ulinzi kwa ajili yetu na
familia zetu.
Warumi 8:26
[26]Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu,
kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini
Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua
kusikoweza kutamkwa.
Mfano.
Nilikua nyumbani nafua mwaka 2018 baada ya
kumaliza kidato cha sita lakini nikasikia kunena kwa
lugha kwa msukumo wa ajabu sana na mimi
nikisikiaga hii hata nikiwa chooni huwa ninanena tu
kwa lugha hivyo nikaruhusu ile hali ya kunena kwa
lugha baada ya kumaliza kufua nikaenda kufunua
ndoo ya Maji ilikua imekaa vibaya yaani imegeuzwa
juu chini ile kuiinua tu nikamkuta nyoka akiwa
amejipanga kung’ata tayari nikakimbia kwa mstuko
mkubwa lakini baada ya Muda nikarudi nikamkuta
yule nyoka kama ameganda vilevile hivyo nikampiga
na jembe kisha nikamchoma moto sikia Roho
Mtakatifu alileta msukumo huu kwa sababu
Kikawaida nisingeweza kujua kilichopangwa na adui
lakini yeye anajua dakika kumi zijazo shetani alikua
amepanga nini hivyo akaleta hii hali ndio maana
Biblia inasema huwa tunanena mambo ya sirini na
Mungu wetu, haleluya Mungu ashukuriwe kwa
zawadi hii ya kunena kwa lugha.
1 Wakorintho 14:2
Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu,
bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye;
lakini anena mambo ya siri katika roho yake.
2.Lugha ya binafsi.
• Kuongea na Mungu
• Kujijenga kibinafsi
1 Wakorintho 14:4
[4]Yeye anenaye kwa lugha hujijenga nafsi yake; bali
ahutubuye hulijenga kanisa.
• Kupambana na hila za adui.
3.Lugha za malaika.
1 Wakorintho 13:1
[1]Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za
malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo
na upatu uvumao.
Waebrania 1:7,14
[7]Na kwa habari za malaika asema, Afanyaye
malaika wake kuwa pepo, Na watumishi wake kuwa
miali ya moto.
[14]Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa
kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
1 Wakorintho 14:2
[2]Maana yeye anenaye kwa lugha, hasemi na watu,
bali husema na Mungu; maana hakuna asikiaye;
lakini anena mambo ya siri katika roho yake.
Kuna kunena kwa lugha kwa kupeleka maombi
mbinguni hii ni wewe na Roho Mtakatifu tu
Warumi 8:26
[26]Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu,
kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini
Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua
kusikoweza kutamkwa.
Maana ya kigugumizi
Kigugumizi (kutoka kitenzi “kugugumia”, kwa
Kiingereza: “stuttering” au “stammering” ni shida ya
baadhi ya watu katika kusema:
Mhusika anajua la kusema, lakini maneno
yanamtoka tofauti, kwa mfano kuna:
• marudio ya fonimu, sehemu
ya maneno au sentensi
• mkwamo kabla ya maneno fulanifulani
• urefushaji wa sauti (hhhhhhhhhham badala
ya ham)
• kusimama
• kusema kitu tofauti na kilichokusudiwa
• kusita au kuhangaika ili kusema kitu
“laba laba laba laba laba laba laba laba laba laba
laba”
Ukiona hii ya kurudia rudia hasa baada ya kuomba
kwa muda fulani ujue sio kwamba wewe ni
mchanga kiroho ila Mungu anataka akuvushe
Mahali au kuna tatizo anataka ulishinde ndo
anakupa hii yaani hii ni kama funguo au kodi au
“password” tatizo tunatumia Sana hekima za
kibinadamu sikia kuna jambo unavushwa kuna
viwango unaingizwa huko kurudia rudia ndio
funguo yako sikia ukikuta simu yenye password ya
1111111 je utaandika moja tu na kusema nyingine
zinajirudia hapana utaandika zote Ili ukamilishe
password, sikia kule kurudiarudia ndio
kunakokamilisha funguo yako rohoni kwa sababu
sio wewe uliyetunga hayo maneno bali ni Roho
Mtakatifu hivyo yeye anakupa maneno hayo, hivyo
maneno yamepangiliwa na Roho Mtakatifu kabisa
na anaelewa anafanya nini
Matendo ya mitume 2:4
[4]Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza
kusema kwa lugha nyingine, kama Roho
alivyowajalia kutamka.
Haleluya Utukufu kwa YESU wetu
1 Wakorintho 2:14-15
[14]Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei
mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni
upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa
yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.
[15]Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala
yeye hatambuliwi na mtu.
Ayubu 32:8
[8]Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi
za Mwenyezi huwapa akili.
Zaburi 59:8
[8]Na Wewe, BWANA, utawacheka, Utawadhihaki
mataifa yote.
Mithali 1:26
[26] Mimi nami nitacheka siku ya msiba wenu,
Nitadhihaki hofu yenu ifikapo;
Waefeso 5:19
[19]Mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za
rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana
mioyoni mwenu;
Wakolosai 3:16
[16]Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu
katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana
kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku
mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
Malaki 4:2
[2]Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la
haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake;
nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama
wa mazizini.
Yohana 11:35
Yesu akalia machozi.
Waebrania 5:7
Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule,
awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti,
maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi,
akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;
Luka 19:41
Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia,
Nini hutokea pale watu wakilia ni kutembea katika
viwango vikubwa vya kimiujiza ,pia kutembea katika
kibali na kuinuliwa kiungu katika Maisha yetu
6)KUUGUA ROHONI
Hii ni dalili inayoonesha kuwa kwa akili Yako
umeshindwa kuombea jambo kiusahihi na jambo la
lazima ndo Roho Mtakatifu anaingia Kati kuugua
rohoni mwako na hali hii huwa inaambatana na
suala la kukosa amani hii ni dalili kuwa jambo sio
jema ila linahitaji muombaji sana pia huwa anakupa
kuugua kwa ajili ya watakatifu wengine ili wasipotee
katika Jina la Yesu.
Warumi 8:26-27
[26]Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu,
kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini
Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua
kusikoweza kutamkwa.
[27]Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho
ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama
apendavyo Mungu.
7)KUTETEMEKA
Hii ni hali inayoashiria ni uwepo wa Mungu wa
kiwango cha juu sana eneo hilo
1 Wafalme 19:11-12
[11]Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za
BWANA. Na tazama, BWANA akapita; upepo mwingi
wa nguvu ukaipasua milima, ukaivunja-vunja
miamba mbele za BWANA; lakini BWANA
hakuwamo katika upepo ule; na baada ya upepo,
tetemeko la nchi; lakini BWANA hakuwamo katika
lile tetemeko la nchi;
[12]Na baada ya tetemeko la nchi kukawa na moto;
lakini BWANA hakuwamo katika moto ule; na baada
ya moto sauti ndogo, ya utulivu.
8)KUPIGA KELELE
Hii ni alama mojawapo inayowakilisha ushindi
Warumi 8:26
[26]Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu,
kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini
Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua
kusikoweza kutamkwa.
Yoshua 6:2,4-5
[2]BWANA akamwambia Yoshua, Tazama, nimeutia
Yeriko katika mkono wako, na mfalme wake, na
mashujaa wake.
[4]Na makuhani saba watachukua tarumbeta saba
za pembe za kondoo waume, mbele ya hilo
sanduku; na siku ya saba mtauzunguka mji mara
saba, nao makuhani watapiga tarumbeta zao.
[5]Kisha itakuwa watakapopiga hizo pembe za
kondoo waume kwa nguvu, nanyi mtakaposikia
sauti ya tarumbeta, watu wote watapiga kelele kwa
sauti kuu; na ukuta wa mji utaanguka chini pale
pale, na hao watu watapanda, kila mtu akiendelea
mbele kukabili.
Yoshua 6:10
[10]Yoshua akawaamuru watu, akasema Msipige
kelele, wala sauti zenu zisisikiwe, wala neno lo lote
lisitoke kinywani mwenu, hata siku ile
nitakapowaamuru kupiga kelele, ndipo
mtakapopiga kelele.
Yoshua 6:16,20
[16]Hata mara ya saba makuhani walipozipiga
tarumbeta, Yoshua akawaambia watu, Pigeni kelele;
kwa maana BWANA amewapeni mji huu.
[20]Basi watu wakapiga kelele, na makuhani
wakazipiga tarumbeta; hata ikawa, hapo watu
waliposikia sauti ya tarumbeta hao watu wakapiga
kelele kwa sauti kuu sana, na ule ukuta wa mji
ukaanguka nchi kabisa, hata watu wakapanda juu,
wakaingia katika mji, kila mtu akiendelea kukabili
mbele; wakautwaa huo mji.
Mi Sijui unapitia nini ila ninachokijua kelele inaweza
kukutoa hapo ulipo najua kibinadamu hakuna
anayependa kelele kwa sababu Kikawaida hazina
Maana ila kwenye ulimwengu wa roho ina Maana
kubwa Sana kwa sababu roho zinajua Maana ya
kelele na zinapambanuliwa na kujulikana zina
Maana gani ashukuriwe huyu Mungu kwa kuwa
yeye anachuja na kuelewa kelele
Waebrania 1:14
Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa
kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?
Ufunuo 19:10
Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili
nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi
ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda
wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda
wa Yesu ndio roho ya unabii.
Ufunuo 22:8-9
[8]Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona
mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona
nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika
yule mwenye kunionyesha hayo.
[9]Naye akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni
mjoli wako, na wa ndugu zako manabii, na wa wale
wayashikao maneno ya kitabu hiki. Msujudie
Mungu.
2 Wafalme 6:15-17
[15]Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule
mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje,
kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari,
wameuzingira mji ule. Mtumishi wake
akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?
[16]Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi
ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.
[17]Elisha akaomba, akasema, Ee BWANA, nakusihi,
mfumbue macho yake, apate kuona. BWANA
akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona;
na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na
magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.
Matendo 12:7
Mara malaika wa Bwana akasimama karibu naye,
nuru ikamulika mle chumbani, akampiga Petro
ubavuni, akamwamsha, akisema, Ondoka upesi.
Minyororo yake ikamwanguka mikononi.
Maombolezo 1:12-13
[12]Je! Si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia,
Angalieni, mtazame Kama kuna majonzi yo yote
mfano wa majonzi yangu, Niliyotendwa mimi,
Ambayo BWANA amenihuzunisha kwa hayo Siku ya
hasira yake iwakayo.
[13] Toka juu amepeleka moto mifupani mwangu,
Nao umeishinda; Ametandika wavu aninase miguu,
Amenirudisha nyuma; Amenifanya kuwa mtu wa
pekee, Na mgonjwa mchana kutwa.
Mwanzo24:40
Akaniambia, BWANA, ambaye naenenda machoni
pake, atapeleka malaika wake pamoja nawe,
atafanikisha njia yako; nawe umtwalie mwanangu
mke katika jamaa zangu, na wa nyumba ya
babangu.
1 Petro 1:8
[8]Naye mwampenda, ijapokuwa hamkumwona;
ambaye ijapokuwa hamwoni sasa, mnamwamini; na
kufurahi sana, kwa furaha isiyoneneka, yenye
utukufu,
1 wathesalonike 1:6
Nanyi mkawa wafuasi wetu na wa Bwana, mkiisha
kulipokea neno katika dhiki nyingi, pamoja na
furaha ya Roho Mtakatifu.
Warumi 14:17
Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali
ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.
Matendo ya mitume 13:52
Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.
Mtume Paulo pia anaiita “furaha yote”
Warumi 15:13
Basi Mungu wa tumaini na awajaze ninyi furaha
yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana
kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mtakatifu.
Zaburi 118:24
[24]Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA, Tutashangilia
na kuifurahia.
Zaburi 144:1-15
[1]Na ahimidiwe BWANA, mwamba wangu,
Anifundishaye mikono yangu vita, Vidole vyangu
kupigana.
[2]Mhisani wangu na boma langu, Ngome yangu na
mwokozi wangu, Ngao yangu niliyemkimbilia,
Huwatiisha watu wangu chini yangu.
[3]Ee BWANA, mtu ni kitu gani hata umjue? Na
binadamu hata umwangalie?
[4]Binadamu amefanana na ubatili, Siku zake ni
kama kivuli kipitacho.
[5]BWANA, uziinamishe mbingu zako, ushuke,
Uiguse milima nayo itatoka moshi.
[6]Utupe umeme, uwatawanye, Uipige mishale
yako, uwafadhaishe.
[7]Uinyoshe mikono yako toka juu, uniponye,
Unitoe katika maji mengi, katika mkono wa wageni.
[8]Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao
wa kuume ni mkono wa uongo.
[9]Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, Kwa
kinanda chenye nyuzi kumi nitakuimbia.
[10]Awapaye wafalme wokovu, Amwokoa Daudi,
mtumishi wake, na upanga wa uovu.
[11]Uniponye, unitoe, Katika mkono wa wageni.
Vinywa vyao vyasema visivyofaa, Na mkono wao wa
kuume ni mkono wa uongo.
[12]Wana wetu na wawe kama miche Waliokua
ujanani. Binti zetu kama nguzo za pembeni
Zilizonakishwa kwa kupamba hekalu.
[13]Ghala zetu na zijae Zenye akiba za jinsi zote.
Kondoo zetu na wazae Elfu na makumi elfu
mashambani mwetu.
[14]Ng’ombe zetu na wachukue mizigo, Kusiwe na
kushambuliwa. Wala kusiwe na kuhamishwa, Wala
malalamiko katika njia zetu.
[15]Heri watu wenye hali hiyo, Heri watu wenye
BWANA kuwa Mungu wao.
Ayubu 4:12-16
[12]Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu
likasikia manong’ono yake.
[13]Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya
usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo
wanadamu.
[14]Hofu iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha
mifupa yangu yote.
[15]Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na
nywele za mwili wangu zilisimama.
[16]Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua
sura zake, Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu;
Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,
Kutoka 28:30
Nawe utie hizo Urimu na Thumimu katika kile kifuko
cha kifuani cha hukumu; nazo zitakuwa juu ya moyo
wa Haruni, hapo atakapoingia ndani mbele ya
BWANA; na Haruni atachukua hukumu ya hao wana
wa Israeli juu ya moyo wake mbele ya BWANA
daima. Mavazi mengine ya Ukuhani
Urimu na thumimu
Katika Agano la kale Mungu alikuwa akitumia njia
kuu tatu aidha kuwasilisha ujumbe au leta majibu
au kuthibitisha jambo..Njia ya kwanza ni manabii,
njia ya pili ni ndoto, na njia ya tatu ni Urimu na
thumimu.
Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha 1Samweli 28:4
pale ambapo Mfalme Sauli alipokwenda kuuliza kwa
Bwana kuhusu vita iliyokuwa inamkabili mbele yake
dhidi ya wafilisti, Kama watashinda au La, lakini
Bwana hakumjibu kwa njia yoyote kati ya hizo tatu..
1Samweli 28:4 “Nao Wafilisti wakakusanyika,
wakaenda kufanya kambi huko Shunemu; naye Sauli
akawakusanya Waisraeli wote, nao wakapiga hema
katika Gilboa.
5 Basi alipowaona hao majeshi ya Wafilisti, huyo
Sauli akaogopa, na moyo wake ukatetemeka sana.
6 Lakini Sauli alipouliza kwa Bwana, Bwana
hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala
kwa manabii”.
Hesabu 27:21
Naye atasimama mbele ya Eleazari kuhani, naye
atamwulizia kwa hukumu ya ile Urimu mbele za
BWANA; kwa neno lake watatoka, na kwa neno lake
wataingia; yeye na wana wa Israeli wote pamoja
naye, mkutano wote pia.
Tunaona tena, wakati mfalme Sauli alipopishana na
mwanawe kuhusu kuvunjwa viapo ambavyo
alivyoweka, alitaka Mungu ahukumu katikati yao ni
nani mwenye makosa, Hivyo alitumia Urimu na
Thumimu kuomba uthibitisho huo.
Mwanzo 26:1-2,6,12-13
[1]Ikawa njaa katika nchi hiyo, mbali na njaa ile ya
kwanza iliyokuwa siku za Ibrahimu. Isaka
akamwendea Abimeleki, mfalme wa Wafilisti, huko
Gerari.
[2]BWANA akamtokea, akasema, Usishuke kwenda
Misri, kaa katika nchi nitakayokuambia.
[6]Isaka akakaa katika Gerari.
[12]Isaka akapanda mbegu katika nchi ile, akapata
mwaka ule vipimo mia kwa kimoja, BWANA
akambariki.
[13]Na mtu huyu akawa mkuu, akazidi kusitawi,
hata akawa mkuu sana.
• Baraka zitakufuata
Kumbukumbu la Torati 28:1-2
[1]Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu
wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake
yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako,
atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
[2]na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata
usikiapo sauti ya BWANA, Mungu wako.
• Hautakosea njia au kufeli.
Huwezi ukachumbia au kuchumbiwa alafu
ukaachwa au ukaacha
Zaburi 32:8
Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;
Nitakushauri, jicho langu likikutazama.
Isaya 30:21
na masikio yako yatasikia neno nyuma yako,
likisema, Njia ni hii, ifuateni; mgeukapo kwenda
mkono wa kulia, na mgeukapo kwenda mkono wa
kushoto.
✓USICHOCHEE MAPENZI
✓KIJANA ALIYEOKOKA NDANI YA BABILONI
✓MAHALI PA SIRI PA MUNGU
✓UELEWE ULIMWENGU WA ROHO