Professional Documents
Culture Documents
Mada Ya Uzalendo
Mada Ya Uzalendo
MAISHA
1. UONGOZI.
Uongozi ni mfumo wa kiutawala unaotoa fursa kwa Mtu au kikundi kidogo cha Watu
kuwatawala walio wengi katika Jamii,Taasisi,Jumuiya na hata katika vikundi vya
kijamii .Uongozi katika mfumo wa Maisha unaweza ukawa wa kidemokrasia,Udikiteta au
uongozi wa kichifu.Uongozi wa kidemokrasia unatoa fursa kwa wanachi kuchagua
viongozi/uongozi kwa kupiga kura za siri au za wazi baada ya wahusika wanaotaka
kugombea nafasi kuweka nia , kugombea na kuchaguliwa na wananchi.Aidha uongozi
wa kidikteta niwa mabavu,unyanyasaji ambao haukubaliki kwa jamii.Nchi ya Tanzani
uongozi wake niwa kidemokrasia ambapo Rais,Wabunge na Madiwani uchaguliwa kila
baada ya miaka Mitano.
WAJIBU WA KIONGOZI
2.3 Njia za Kudhibiti Ukiukwaji wa Maadili Njia zifuatazo zinaweza kutumika kudhibiti
ukiukwaji wa maadili:-
Uzalendo ni hali ya mtu kuwa na moyo wa kuipenda nchi yake, kulinda raslimali za
Taifa, kuenzi Tunu za Taifa (Utu, Amani, Mshikamano na Umoja), kuwajibika, kuwa
mwadilifu, kufanya kazi kwa bidii na kutetea maslahi ya Taifa kwa gharama yeyote.
Maendeleo ya Taifa lolote duniani yanategemea zaidi namna wananchi walivyo tayari
kujitolea kwa ajili ya Taifa lao na kushiriki kikamilfu katika mchakato wa kujiletea
maendeleo yao wenyewe, ikiwa ni pamoja na kujinasibisha na utekelezaji wa shughuli
za Serikali kwa kuzingatia vipaumbele vya Taifa, pamoja na kuunga mkono juhudi za
Serikali yao kuwajengea mazingira wezeshi ya kujiletea maendelo endelevu. Aidha,
Uzalendo unaanza kwa kutambua utu na asili ya utu ambavyo vimebebwa na Tunu za
Taifa zinazo tambulisha taifa na utaifa wa watu wake.
Kwa tafsiri ya kawaida, tunu ni kitu adhimu, ni kitu cha pekee na pia ni utambulisho.
Tunu za Taifa ni masuala ya msingi ambayo hulitambulisha Taifa na utaifa wa watu
wake. Aidha, utendaji kinyume na tunu hizo hupelekea nchi kuingia matatani. Hivyo,
masuala yamustakabali wa nchi na ustawi na ufanisi wa watu wake hutawaliwa na
mfumo ambao sehemu zake ndizo TUNU za Taifa husika na viongozi wa juu katika
utawala wa nchi ndio wasimamizi na walinzi wakuu wa tunu za nchi yao. Hivyo viongozi
na wananchi wakizitambua, wakaziheshimu na kuwajibika ipasavyo katika kulinda tunu
za nchi, huingia katika daraja la uzalendo.
Dhana ya uimarishaji Uzalendo hapa nchini ilianza tangu miaka ya 1960 ambapo
jitihada mbalimbali zilifanyika ikiwa ni pamoja na: Maandalizi na utekelezaji wa falsafa
na sera kama vile Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na Azimio la Arusha ambazo
zilikuwa na lengo la kuimarisha umoja, upendo, ushirikiano na mshikamano miongoni
mwa wananchi wa Tanzania licha ya tofauti zao za asili, maeneo wanayotoka, rangi,
kabila na dini. Aidha, jitihada nyingine ni:- kuanzishwa kwa Jeshi la Kujenga Taifa;
Chuo cha Kivukoni kilichofundisha na kuzalisha Makada wa Siasa ya Ujamaa na
Kujitegemea, kufundishwa kwa somo la uraia katika Shule za Msingi na Sekondari na
Somo la Elimu ya Maendeleo (Development Studies) katika Vyuo Vikuu.
Hata hivyo, pamoja na jitihada hizo historia inaonesha kuwa, tangu miaka ya 1990 hadi
sasa, hali ya uzalendo hapa nchini imedorora. Hii inadhihirika kutokana na: Uwepo wa
baadhi ya Watanzania wanaokwepa kulipa kodi,Ukosefu wa uwajibikaji kwa baadhi ya
Watanzania; Kukithiri kwa vitendo vya rushwa, baadhi ya Watanzania wanao saliti Taifa
letu kiuchumi na kisiasa, ubadhirifu wa mali za Umma ikiwemo utakatishaji wa fedha;
Baadhi ya Watanzania kutotunza siri za nchi; Ubinafsi na kutumia madaraka ya Umma
kwa maslahi binafsi kwa baadhi ya watu wanaopewa dhamana ya kuongoza; Baadhi ya
Watanzania kudharau maadili ya Taifa letu; Kuanza kujitokeza kwa vikundi katika jamii
vyenye viashiria vya misimamo mikali ya kupinga jitihada za serikali za kuwaletea
wananchi wao maendeleo
4.0 Hitimisho
Kuna msemo wa lugha ya Kiswahili unaosema kuwa "Kuishi kwingi ni kuona mengi":
maana halisi ni kuwa mtu aliyemtangulia mwenzake kiumri anakuwa na uzoefu mkubwa
sana kwa sababu mambo ambayo amekwisha kuyaona ni mengi katika kuishi kwake.
Kupitia uzoefu huo ndivyo mtu huyo anapata mbinu nyingi za kumwezesha yeye
kukabiliana na nyakati zote katika maisha yake.
Haina maana ya kwamba mtu mwenye umri mdogo, kwa sababu ya kuwa na uzoefu
mdogo wa kimaisha, basi anapaswa kukosa busara na hekima za kumwezesha yeye
kuishi vizuri.
Mtoto au kijana anaweza kuwa na hekima kama ya mzee kwa kujifunza stadi za maisha
ambazo ni kama zifuatazo
1. Stadi binafsi
2. Stadi za kijamii
3. Stadi za maamuzi sahihi[3]
Stadi binafsi
Hizi ni mbinu au kanuni ambazo zinamwezesha mhusika kuwa na uwezo mkubwa wa
kujitambua, kwanza kiundani zaidi, kwa maana ya hisia, uwezo, madhaifu na nafasi
yake katika jamii. Stadi binafsi ni muhimU sana kwa sababu zinamwezesha mhusika
huyo kujijengea hali ya kujiamini kutokana na kuitambua thamani yake katika jamii
inayomzunguka.
Ili kuwa bora katika stadi binafsi mhusika anapaswa kuwa na uwezo katika vitu
vifuatavyo: kujitambua, kutambua mahitaji na kuweka malengo katika maisha.
Stadi za kijamii
Hizi ni stadi ambazo humjenga na kumwezesha mhusika kujua naamna ya kuishi na
watu kwa upendo na amani na kujenga ushirikiano ulio bora. Vifuatavyo ni vipengele
muhimu ambavyo vinamthibitisha mtu kuwa stadi za kijamii:
1. mawazo chanya
2. ubunifu wa kimawazo
3. maono ya mbeleni
4. uwezo wa kufanya maamuzi
Vyanzo vya stadi za maisha
Watu hujifunza/kuiga stadi za maisha katika sehemu, makundi au watu mbalimbali ila
sehemu au vitu ambavyo ndio msingi wa stadi za maisha ni hizi zifuatazo.
Familia zetu
Hapa tunajifunza na kuiga vitu kutoka kwa wazazi au ndugu zetu kwa sababu tunaishi
nao kwa muda mreefu, hususani katika kipindi cha ukuaji wetu ambacho ndicho
kipindi vichwa vyetu vinapodaka na kukariri mambo mengi
Taasisi za kielimu
Hapa mara nyingi ni kupitia maarifa tunayopata kwa kufundishwa
na wakufunzi hususadi shuleni, vyuoni na kadhalika.
Jamii zetu
Tofauti na familia kuna kundi jingine kubwa ambalo linatuzunguka, hivyo lenyewe pia
lina mchango katika kutujenga kifikra na kuendeleza stadi zetu za kimaisha.
Imani/Dini
Imani tofautitofauti zimekuwa zikitoa mafunzo mengi ya kidini ambayo yamekuwa
yakihusika katika kuwajenga waumini wake. Kwa mfano imani ya Kikristo imekuwa
ikifundisha juu ya amri kuu ya upendo, kitu ambacho ni stadi muhimu inayowezesha
mtu kuishi vizuri na watu katika jamii yake.