Download as docx, pdf, or txt
Download as docx, pdf, or txt
You are on page 1of 9

MAWASILIANO NA LUGHA

Illi kuhakikisha mawasiliano kamilifu, ni sharti anayewasiliana ahakikishe vipengele


vifuatavyo
1) Kusudi maalumu: Hatuwasiliani katika obwe (vaccum) tupu. Ni lazima pawe na
kusudi maalum l,inalosababisha kuwepo na hitaji la kuwasiliana kama kupitisha
ujumbe fulani wa kidharura , kuelimmisha n.k

2) Hadhira maalum /teule : Ujumbe unapopitishwa huwa pana hadhari maalum au


teule inayolegwa na ujumbe ule . Ni sharti uangalie kama hadhira ni watoto au
watu wakubwa, wasomi au wasiosoma mwananchi wa kawaida au mwanasiasa n.k
( mmust understand the target audience )

3) Ubayana na usahihi ( Clarity and precision) ; sharti habari/ujumbe ziwe banyana


na ziwe na usahihi ndani yake. Kuandika porojo au propaganda ni kinyume cha
uandishi habari au uripota unaongozwa na sheria.

4) Ukamilifu; habari zikamike zisiwe nusunusu


5) Ziwe na mantiki (completeness and logic)
Ujumbe unaopatisha uwe na mfuatano unaonyesha, chanzo athari matokeo
suluhu/hitimisho
Vipengele hivi vinapofuatwa kwa njia inafaa, husaidia kuwepo na mawasilino .
Utaratibu ambao huwezesha viumbe kupashana habari

SARUFI YA KISWAHILI
Sifa za lugha
1) Lugha inahusisha sauti - kwa sababu lugha huhusisha sauti, huwa na uwezo
wa kutoa sauti.
2) Lugha ni kigezo kikuu cha mawasiliano hata ingawa hii sio njia tu pekee ya
kuwasiliana. Kuna nyingine nyingi- mavazi, sauti, ishara, mgusano na mtagusano
n.k
3) Lugha inahusisha sifa za unasibu
4) Lugha ni mali ya binadamu (wanyama hawana lugha )
5) Lugha inafuata taratibu fulani : sauti nasibu zenye kubeba maana
6) Lugha huhusisha shughuli ya kijamii
7) Watu hujifundisha lugha japo huzaliwa na uwezo wa kujifunza lugha
8) Lugha hukubalika kwa sababu ni kiungo hai
Mfano; msichana - Dem, Manyanga, Mbusi

Viambishi / mofu
Mofu au kiambishi nmi kipashio kidogo zaidi cha neno kilicho na maana ya kisarufi na
ambacho huambisha kwenye mzizi wa neno ili kuleta maana ikusudiwayo.
Mofu haiwezi kukatwakatwa zaidi kwani ikifanyiwa hivyo hupoteza maana.
Neno la lugha ya Kiswahili likiwa kamili huitwa leksimu
Leksimu ndio hubeba maana kuu na ndio hufasirika katika ubongo wa mzungumzaji
wa lugha husika .
Umilisi wa lugha haswa wa mzawa/mzaliwa wa lugha husika. Huielewi kutokana na
kufahamu maana yake kiisimu.
Leksimu hubeba mzizi na kiishio cha neno lenye maana kuu na ndio tunapata kwenye
kamusi za lugha husika kwa mfano; lima ni leksimu iliyojegwa na mzizi Lim na kisha a
Lim - a

1
cheka (Leksimu) (chek - a)
mzizi kiishio

andika (leksimu) (andik - a)


mzizi kiishio

haribu (leksimu) (harib - u)


mzizi kiishio

nadi (leksimu) (nad - i)


mzizi kiishio

samehe (leksimu) (sameh - e)


mzizi kiishio

Mzizi ni sehemu ya leksimu ambayo hubeba maana yake kuuu na sehemu hii
haibadiliki katu hata leksimu hiyo ikipanuliwaje .
Maneno yenye asili ya kibantu huishia /huchukua kiishio /a /kwenye mzizi ilhali maneno
yenye asili ya kigeni huchukua kiishio aidha /e/, /u/ au /i/
Kuna aina mbili za mizizi, ya leksimu.

i. -Mizizi ambayo inaweza kuchukua viambishi au mofu mbalimbali kati yake


na kiishio.
ii. –Mizizi ambayo ni maneno kamili kiishio chake hubaki kuwa sehemu ya
mzizi wakati wa kulipanua. (kunyambua)
Ili kupanua leksimu na kuleta maana ikusudiwayo kisarufi basi huwa tunaweka mofu kabla/
baada ya mzizi.
Zinazowekwa kabla mzizi hujulikana kama; mofu/viambishi awali.
Zinazowekwa baada ya mzizi hujulikana kama; mofu/ viambishi tamati
Mfano:leksimu imba, imejengwa na mzizi –imb na kiishio –a ili tuweze
kutoa maana za kisarufi mbalimbali na zieleweke basi
tunatumia mofu/viambishi mbalimbali ili kuleta maana hizi.
Imba-(huleta maana kutenda). Tenda. (x alitekeleza moja kwa moja)
Imbia-Tendewa (fulani alifanyiwa)
Imbisha-mtu alifanya mwingine atende
Imbika- Uwezo wa kuimbwa upo
Imbiwa- Tendewa
Imbiana- Tendeana.
Imb - Mzizi
Alimwimbia Imb ndio mzizi Kwa sababu haibadiliki
A/li/mu viambishi /mofu awali
i/a viambishi/ mofu tamati
Maana ya kimsingi la neno huletwa na leksimu.
Maana ya kisarufi huletwa na mzizi, kiishio na mofu (kabla au baada ya mzizi)
Mofimu
Mofimu ni maana ya kisarufi inayobebwa na mofu.
Mfano: leksimu/neno-Samehe inaweza kutupatia maana ya kisarufi
waliosameheana
Onyesha mofu na mofimu: Waliosameheana
Wa-li-o-samehe-a-na

2
-wa- Nafsi ya tatu wingi
-li- Wakati (uliopita)
-o- Kirejeshi( urejeshi)
-Samehe- Mzizi
-an- viambishi tamati -an- kiendelezi
-a- -a- kiendelezi
Nafsi (binadamu- kiumbe chenye uhai)
I. Mimi- Sisi (Ni-Tu)
II. Wewe- Nyinyi ( U-M)
III. Yeye- Wao(A-WA)
*Ainisha/ changanua/bainisha/ onyesha sehemu za kisarufi au ainisha mofu na
mofimu za sentensi:

a) Lisilonifurahisha.
Mofu mofimu (maana)
-li- kipatanishi cha ngeli
-si- kikanushi(ukanusho)
-lo- kirejeshi
-ni- mtendwa/ shamirisho
-furahi- mzizi
-sh- kiendelezi
-a- kiishio
b) Sijamchezesha
Mofu mofimu
-si- kikanushi/ukanusho
-ja- kipatanishi
-m- mtendwa/shamirisho
-chez- mzizi
-esh- kiendelezi
-a- kiishio
Mofu Mofimu
-si- kikanushi
-ja- wakati timilifu
-m- mtendewa/shamirisho
-chez- mzizi
-e- viendelezi
-sh-
-a- kiishio
Wakati mfano
Li- uliopita Nilimchezesha
Ta-unaokuja Nitamchezesha
Na-uliopo Ninacheza
Me- timilifu Nimecheza
Ku- Mazoea Nakuchezesha

c) Asiyetuogofya ogopa
Mofu Mofimu
A- Nafsi ya tatu umoja
-si- kikanushi/ukanusho
-ye- kirejeshi/urejeshi

3
-tu- shamirisho
-ogo- mzizi
-fy- kiendelezi
-a- kiishio

Mtumiaji wa lugha yoyote, ili aweze kuwasiliana sharti aelewe nafasi ya


mofu/viambishi na mofimu zinazobebwa na mofu zile. Ili kutoa maana ya kisarufi
ambayo ndiyo ujumbe unaopitishwa wakati wa mawasiliano.
Mofu huwekwa kabla na baada ya mzizi.

AINA ZA MANENO YA KISWAHILI


Lugha ya Kiswahili ina aina nane kuu za maneno; ambayo hupatanishwa kwenye upatanisho
faafu kulingana na ngeli husika na kuweza kuwasiliana.
Mawasiliano hukwama upatanisho huu ukikosa kuzingatiwa. Maneno haya ni:
1) Nomino(jina)
2) Kivumishi
3) Viwakilishi
4) Vitenzi
5) Viunganishi
6) Vihusishi
7) Vielezi
8) Vihisishi

AINA ZA MANENO

Nomino
Ni neno linalotaja jina la kitu, mtu, mahali au jambo la udhahania.
Nomino tendaji katika sentensi huchukua sehemu ya kwanza ya sentensi ambayo huelezwa
na kiarifu au kitenzi.
Sehemu hii ya kwanza hujulikana kama kiima na aghalabu huchukuliwa na nomino au
kiwakilishi chake. Kuna aina mbalimbali za nomino.

Aina za nomino
Nomino jumla-kawaida
Nomino za jamii-makundi
Nomino za pekee
Nomino za wingi
Nomino za dhahania
Nomino vitenzi-jina

Vivumishi
Fungu la maneno ambayo hutoa maelezo zaidi kuhusu nomino/ kiwakilishi chake
Aina
Vivumishi vya Sifa: -zuri, -zito, -baya n.k.
Vivumishi viashiria
Visisitizi-papa hapa, papo hapo
Vimilikishi- vinatumia mizizi angu, ake, ako
Virejeshi-hurejelea kitu kilichotajwa tayari.
Mfano; hiyo, hicho hilo

4
Viulizi-hutumia mzizi ngapi na gani
Idadi-hutumia majina ya idadi kamili
Mfano; moja, mbili, tatu
Na idadi isiyo kamili
Mfano; chache, -ingi.nk.

Viwakilishi
Hivi ni maneno ambavyo huwepo wakati nomino haijatajwa. Hufanya kazi ya kuwakilisha
kitu kinachorejelewa pasi kutajwa.
Mfano; Wake ametoweka badala ya, mtoto wake ametoweka
Kilichonifurahisha badala ya kitu kilichonifurahisha.
Kadri tulivyo na aina ya vivumishi; ndivyo tulivyo na aina ya viwakilishi isipokuwa;
1. viwakilishi ngeli
2. Viwakilishi vya nafsi

1) Viwakilishi vya ngeli; ni viambishi ambavyo hutokea mwanzoni mwa kitenzi na


hufanya kazi ya kupatanisha katika ngeli zote.
Mfano: kilichoibiwa-ki, ni kiambishi kinachowakilisha ngeli ya KI-VI
Aliyefika –a, kiambishi kinachowakilisha ngeli ya A-WA
2) Viwakilishi vya nafsi
Huwa katika makundi mawili; viwakilishi vya nafsi huru na nafsi tegemezi
Nafsi huru- Maneno kamili yanayojitegemea.
Mimi –Sisi Nafsi I
Wewe - Ninyi Nafsi II
Yeye -Wao Nafsi III
Nafsi tegemezi - Ni viambishi vinavyosimamia nafsi kwenye vitenzi.
Nafsi I- mimi nilifika
Kiambishi kinachosimamia/ wakilisha nafsi I umoja
Sisi tulifika
Kiambishi kinachowakilisha nafsi I wingi
Yeye aliondoka

Inawakilisha nafsi ya tatu umoja

Wao waliondoka

Kinawakilisha nafsi ya tatu wingi


Viambishi vinavyowakilisha dhana mbalimbali hupatikana mwanzo mwa kitenzi.
Kwa muhtasari; viwakilishi huwa aidha maneno kamili au ******** na viambbishi
vinapatikana kwenye vitenzi

Kitenzi/ kiarifa/kiarifu
Ni neno linalotupasha habari au linalotuarifu kinachotendwa au kutendewa nomina au
kiwakilishi chake.
Mfano; Mtoto anapikiwa chakula (anatendewa)
Mwanafunzi anaandika (anatenda)
Rudisha ni hodari (t)
Yeye si mwelekezi makini (t)
Kiatu ki sakafuni (t)
Wao wamekuwa wakipigana tangu Jana.

5
wangali uwanjani.

Kwa jumla tuna aina tatu za vitenzi:


i. Kitenzi halisi I
ii. Kitenzi kikuu T
iii. Kitenzi kisaidizi TS
iv. Kitenzi kishirikishi t vishirikishi kamilifu
Vishirikishi vipungufu

Kiunganishi
Ni neno au fungu la maneno linalounganisha wazo moja na lingine. K.m na, isipokuwa nk.

Vihusishi
Ni neno au fungu la maneno linalounganisha uhusiano kati ya kitu na kingine, jambo na
linguine au mtu na mwingine.
Vihusishi vya wakati, kabla ya, mbele ya, mpaka, hadi n.k
Vihusishi vya mahal; mpaka, nyuma ya, mbele ya.
Vihusishi vya kiwango, mpaka, hadi, pomoni n.k

Vihisishi
Haya ni maneno yanayoonyesha hisia za kindani na zinazoleta mchomo wa moyo
hudhihirisha hisia mbalimbali.

Mfano: Salalaa! Masalale! N.k

Ili kuwepo na sentensi sahihi, basi maneno haya lazima yapangwe kwa mpangilio mahususi
wa kisintaksia.
Katika sintaksia, tunarejelea jinsi maneno yanavyo ungana na kuhusiana ili kuunda sentensi
zenye maana.
Sharia ya kisintaksia ni kuwa sentensi ianze na nomino au kiwakilishi chake ambacho huitwa
kiima ikifuatiwa na kitenzi au kiarifa muundo wa sentensi kisintaksia ni:
N/W+T
Hata hivyo, nomino au kiwakilishi hiki kinaweza kuambatanisha na maneno mengine
yanayolenga nomino au kiwakilishi hicho na maneno haya huwa ni kivumishi na kitenzi.
Baada ya nomino au kiwakilishi (kiima), sentensi hufuatwa na kiarifa au kitenzi ambacho pia
kinaweza kuambatanishwa na maneno mengine na maneno hayo huwa ni; kielezi pamoja na
nomino tendewa.
Sentensi hii, ili iweze kuleta maana kamili ni sharti iwe na upatanisho wa kisarufi unaofaa.

UAINISHAJI WA NGELI KISINTAKSIA


Sintaksia inarejelea jinsi maneno yanavyoungana na kuhusiana ili kuunda sentensi
zenye maana. Kwa hivyo , uanishaji wa nomino za Kiswahili kwa kutumia kigezo hiki
hufanywa kwa kuangalia namna vishio mbalimbali katika sentensi
vinavyochukuana/kukubaliana hali inayoitwa upatanisho wa kisarufi:
Mfano: Kijana amefariki.
Samba ameuwawa.
Kitu kikubwa kimenunuliwa.
Chuo kikuu kimefunguliwa.
Jitu lilo limemwangamiza.
Tunda kubwa limeazea mtini.

6
Ni wazi [kuwa kijana na samba wako katika ngeli moja ( kikundi kimoja ) kitu na chuo
kikundi kingine kimoja na jitu na tunda katika kikundi kingine tofauti
Makundi haya yamebainika kwa kuzingatia viambishi awali vinavyo tangulia kila kitensi. Hii
ni dhahiri kuwa, kigezo cha kisintaksia kinachotumikoa katika sarufi ndicho
kinachokubualika kuainisha ngeli na huzianmisha ngeli kwa kuzingatia viambishi awali
kwenye vitensi ili kuleta upatanisho wa kisarufi .
Kwa kuzingatia kigezo hiki tuna makundi yafuatayo ya ngeli.

UAINISHAJI WA NGELI KWA KIGEZO CHA KISINTASIA


1) Ngeli ya A- WA ( ngeli ya 1 and 2 )
Hii ni ngeli ambahyo huchukua upatanisho wa kisarufi ama ‘a’ au ‘yu’ – hali ya umoja
na ‘wa’ – hali ya wingi kwenye sentensi . Hujumulisha majina ya vitu vyenye uhai
a) Binadamu
b) Wadudu
c) Wanyama
d) Ndege k.v kasuku , kiwi

Ngeli ya U-I (Ngeli ya 3-4)


Huchukua upatanisho wa kisarufi, U- umoja na I- wingi
Ngeli hiii hujumlisha nomino za vitu visivyo na uhai.
Pamoja nza viumbue vya kimaajabu k.m miungu na watu wenye uwezo mkubwa . atayo
a) Baadhi ya viungo vya mwili mfano; mgongo, muundi n.k
b) Baadhi ya mimea
c) Baadhi ya vitu vya asili
d) Majina yaliyoundwa kutokana na vitenzi
e) Baadhi ya maneno yaliyokopwa kutoka lugha za kigeni

Mfano: Mgongo wake uniaumia sana - umoja


Migongo yao inaumia sana – wingi

Ngeli ya LI- YA (Ngeli ya 5-6)


Hii ni ngeli ambayo huchukua upatanisho wa kisarufi wa Li- Umoja na YA katika hali ya
wingi.
Ngeli hii huashiria sifa za ukubwa za nomino zinazohnusika ( ukubwa usio wa kawaida) .
Makundi mengine ya nomino zinazojumlishua kaitka ngeli hii ni;
a) Baadhi ya maneno kutoka lugha za kigeni
b) Baadhi ya sehemu za mwili
c) Baadhi ya majina ya kijamii
d) Majmina yanayoonyesha nyadhifa wzanazoshikilia watu katika jamii mfano;
Umoja Wingi
Hekalu Mahekalu
Jitu Majitu
Jichwa Majichwa
Ganda Maganda
Neno Maneno
Ziwa Maziwa

Ngeli ya KI- VI (7-8)


Hii ni ngeli ambayo upatanisho wake lwa kisarufi ni KI- umoja na VI- wingi.

7
Nomino za Kiswahili kwa kutumia kigezo hiki , hufanywa kwa kuangalia namna
vipashio mbalimbali katika sentensi vinavyochulua na kukabiliana hali inayoitwa
upatanmisho wa kisarufi
Mfano: kijana amefariki
Simba ameuwawa
Kitu kikubwa kimenunuliwa
Chuo kikuu kimefunguliwa
Jitu lilo limemwangamiza
Tunda kubwa limeozea mtini

Ni wazi kuwa kijana na samba wako katika ngeli moja ( kikundi kimoja )
Kitu na chuo kikundi kingine kimoja na jitu na tunda katika kikundi kingine tofauti Makundi
haya yamebainika Kwa kuzingatia viambishi awali vinavyotangulia kila kitensi. Hii ni
dhahiri kuwa, kigezo cha kisintaksia kinachotumika katika sarufi ndicho kinachokubalika
kuanisha ngeli nza huzianisha ngeli kwa kuzingatia viambishi awali kwenye vitenzi ili
kuleta upatanisho wa kisarufi. Wza ama ‘a’ au ‘yu’ – hali ya umoja na ‘wa’ – hali ya wingi
kwenye sentensi . Hujumlisha majina ya vitu vyenye uhai.
a) Binadamu ‘
b) Wadudu
c) Wanyama
d) Ndege k.k

Mfano: Nyuki mdogo amemdunga mtoto – umoja


Nyuki wadogo wamewadunga watoto – wingi

Ngeli ya U- I (Ngeli ya 3-4)


Huchukua upatanmisho wa kisarufi, U- umoja na 1- wingi.
Nomino katika ngeli hii huwakilisha vifaa vya kawaida
Mfano- kalenda shati vile vile, nomino zifuatazo hujumlishwa
a) Nomino za majina yaliyotolewa / yaliyoazimwa kutoka lugha za kigeni
Ofisi- Office
Koti – Court
Baiskeli- bicycle
b) Majina ya vifaa vya kazi
Ndoo, nyundo, ngozi
Mfano: Nguo yake imeraruka vibaya sana - umoja
Nguo zao zimeraruka vibaya sana

Ngeli ya U-ZI (1-2)


Upatanisho wa kisarufi : u – umoja na zi - wingi ( kwenye vitenzi
Makundi ya nomino katika ngeli hii.
a) Nomino zinazowakilisha majina ya vitu vyenye umbo refu na jembamba.
Mfano: Ulimi, ufito, unywele, ujia n.k
Uzi ule no wa mama – Umoja
Nyuzi zile ni za mama – wingi
Uzi ule umoeshona vizuri – umoja
Nyuzi zile zimeshona vizuri

8
Ngeli ya U (14)
Upatanisho wa kisarufi katika hali ya umoja na wingi kwenye vitensi huchukua kiambishi
awali U
a) Nomino za n geli hii ni vitu vya kidhahania vinavyofikirika tu.
Mfano: Utukufu, uchangamfu, umaskini
b) Umoja wa sehemu ya vitu vidogo
Mfano: Ufito, ushanga
c) Baadhi ya majina ya nchi

Mifano: Ulaya Uholanzi, Urusi na Uchina


Ugojwa huo ulimlemea sana – umoja
Ugojwa huo uliwalemea sana – wingi
Umasikini wake unaogofya

Ngeli ya YA
Huchukua upatanisho wa kisarufi YA katika hali ya umoja na wingi:
Huwakilisha nomino za vitu visivyoweza kuhesabika, vitu vyenye umajimaji
Mifano: marashi, manemane, maziwa n.k.

You might also like