Kanuni 10 Za Kutafasiri

You might also like

Download as pptx, pdf, or txt
Download as pptx, pdf, or txt
You are on page 1of 36

KANUNI 10 ZA KUTAFASIRI

MAANDIKO
TR MGINA LODI
UTANGULIZI
• Hoja za mwanzo:
• Hermeneutics- ni neno linalotokana na neno la
kiyunani hermeneuo lililo na maana ya “kutafsiri”

• Hatua mbili za somo la hermeneutics:


• 1. kutambua maana ya mwandishi kwa
waandikiwa. (wakati huo)
• 2. kutambua matumizi ya makala kwa wakati
huu.
HOJA ZA MWANZO
• A. JINSI YA KUSOMA BIBLIA.
• 1. soma Biblia kama kitabu chochote: kingereza ni Bible
lakini kiyunani ni Biblia ikiwa na maana ya “kitabu” Biblia
ni kitabu hivyo kama ilivyo vitabu vingine kukisoma
inataka utumie akili,.
• 1 Wakor 10:15, 2 Tim 2:7

• 2. Usisome Biblia kama kitabu chochote:


• Kwakuwa Biblia ni neno la Mungu hivyo alipaswi kusomwa
kama vitabu vingine kwakuwa hiki kitabu kina husisha hali
ya kiroho. 1 Wak 2:14, Math 11:25-26, Zab 119:18
Kwanini tusome Tafsiri ya Maandiko?
• Kanuni ni muhimu sana sio tu katika kusoma Biblia lakini katika
kila sehemu ya maisha:

• mfano; madereva wana kanuni..kutumia upande wa kushoto,


kutowapita madereva wengine kwenye mlima (ku overtake),
kuendesha polepole kwenye watu wengi, kuegesha gari kando
ya barabara. Kama vile tunavyo hitaji kanuni kwa madereva
ndivyo tunahitaji kanuni katika kutafasiri maandiko.

• Wahubiri husababisha ajali, wanaposhindwa kutumia kanuni..


Kwa sababu kila mtu anataka kuhubiri vile anajisikia yeye
kuhubiri. (Filipo na mtu wa kushi.. Mdo 8:30-31)
SURA YA KWANZA
KANUNI YA UTIIFU
• I. UTIIFU: (uhusiano kati ya hermeneutics na utiifu)
• Kutenda na kujua ni mambo yenye mahusiano makubwa, yale tunayo yajua
hutokana na mapenzi yetu ya kutenda: Yoh 7:17
• Yesu anafundisha kwa mifano kuzuia uelewa mpya kwa hawa watu kwakuwa
hawa kutii ukweli wa zamani. Mathy 13:10-15
• Ikiwa utatii yale tu uliyo kwisha fahamu basi kuelewa kwako kutaongezwa.
Mathy 13:12

• II. Kuelewa kwa wasiotii kuta punguzwa (Ebra 5:11-14); wavivu kusikia,
kwakutumia akili na neno (utii) wamejua kupambanua mema na mabaya. Rum
1:24-25; walibadili kweli kuwa uongo

• III. Kuelewa kwa wanao tii kutaongezwa: Mamajusi wanapewa nuru kwa kutii
(Mth 2:1-5), Daudi anapata baraka kuu kwa kutii na kuongezewa ufahamu.
Zaburi 119:97-101
SURA YA PILI
KANUNI YA UVUVIO
• 1. Maandiko yote yamevuviwa na Mungu: uvuvio= “kupumulia ndani
ya” waaandishi wake walipumuliwa ndani yao. (2 Tim 3:16)
• Hii ina maanisha kuwa waliongozwa na Roho (2 Pet 1:20-21).

• Hifadhi Iliyo Vuviwa: biblia haiifadhi maneno ya Mungu, mitume na


malaika tu, lakini ya shetani na hata manabii wa uongo, pia habari za
maanguko. Kusudi la Mungu kuwavuvia waandike hayo nisisi kuelewa
na kujifunza kitu katika hayo.

• Mfano Petro katika: Mathayo 26:33, -hifadhi hii ya maandiko


yamevuviwa maana Roho mtakatifu ana msaidia Mathayo kuandika hayo
lakini Petro hakuwa amevuviwa alipo yasema hayo, Petro aliyanena hayo
kutokana na ujasiri ulio pita kiasi, majivuno na kupofushwa .
• Hifadhi ya taarifa ilivuviwa ila taarifa yenyewe haikuwa na uvuvio
MAANDIKO YOTE NI YA MANUFAA
2 Tim 3:16
• Njia Tatu Ambazo Kwazo Maandiko Niya Manufaa.
• A. katika huduma: (kukemea, kukosoa, na kufundisha; (hata agano la kale :Rum
15:4)
• B. katika itikadi: sio yote lakini nyaraka zote zilikuwa kwa sababu za kiitikadi, misingi
ya itikadi za kimaisha, salamu, mambo binafsi na utamaduni. Hutusaidia kujifunza
itikadi nzuri za kuishia.

• Injili zote na matendo ya mitume ni maandiko yaliyo kusudia kutoa mambo ya


kihistoria badala ya itikadi. Japo kuna uwezekano wa kuona itikadi ndani ya maisha
kwenye njili. Mfano hakuna misingi ya kiitikadi katika vifungu vifwatavyo. (Mk 11:2,
Mt 10:9, Yn 21:18, Mdo 4:32-33)
• Ni rahisi kuhusisha itikadi na vitabu vya historia katika matukio yanayo jirudia na sio
jambo la wakati mmoja.

• C. katika maisha binafsi: himizo na imarisho; sio kila andiko laweza tumika katika
itikadi lakini maandiko yote yanaweza tumika katika huduma lakini sio yote
yatatumika katika maisha ya mtu binafsi. Mfano katika kuzidai ahadi katika maandiko.
Je ni nani anaweza kuzidai ahadi hizi? (Mt 10:17, 11:22, 26:34, Yoh 21:18, Mdo 5:9b,
9:16)
SURA YA TATU
KANUNI YA MUKTADHA
• KANUNI YA MUKTADHA: 1. kuelewa muktadha wa
kihistoria: neno hili linatokana na neno la kingereza context ambalo
linatokana na maneno mawili ya kirumi “con” (pamoja) na “textus” (fuma)
hivyo maana ya neno context ni “fuma pamoja”. Maana ya kila mstari wa
maandiko imefumwa pamoja na muktadha wa kihistoria na wakawaida.
• Muktadha huu una mambo kama: mwandishi na tarehe, waandikiwa,
tamaduni, tatizo lililopelekea kuandikwa kwa kitabu. Huwezi elewa mstari
kama hujajua umefumwa katika hali gani ya kihistoria (picha kwenye kanga)
• Hatua 3 za kubainisha muktadha wa kihistoria , hasa katika nyaraka ni.
• 1. jibu maswali ya muandishi a) alikuwa nani? b) je aliandika lini.
• 2. jibu maswali juu ya wasomaji a) wakina nani? b) wamji gani? c) hali ya ya
maisha (wayahudi au mataifa, tajiri au maskini?
• 3. tambua shida ambazo muandishi aliandika kutatua
SURA YA TATU: MUKTADHA
2: kuelewa muktadha wa kimaandishi
• Muktadha wa kimaandishi tuna maanisha maneno na mistari na
vifungo vyote vinavyo izunguka makala. ni mawazo yanayo kuja
kabla na baada ya makala.
• Ukijaribu kutoa makala katika muktadha wake utaharibu kila kitu.
• Hatua 5 za kuchunguza muktadha wa kimaandishi
• 1. taja kichwa kikuu cha kitabu/sehemu uliyo chagua.

• 2. jibu maswali ya msingi ya sehemu. a) ni mistari gani ya Biblia


inahusiana na sehemu hio. b) kichwa kikuu cha kijisehemu hiki ni
kipi?. c) je kichwa cha kijisehemu chako ni sawa na kichwa kikuu
cha kitabu au sehemu ambapo kijisehemu chako kinatoka.
Hatua 5 za kuchunguza muktadha wa kimaandishi

• 3. jibu maswali yanayofuata yale ya msingi juu ya kijisehemu


• a) Kama kuna ahadi ni nini sharti lake “ikiwa” b) je kuna
matatizo, kuna suluhisho? C) ikiwa kuna mfano ni lipi funzo kuu
• 4. muhtasari wa kila aya ya kijisehemu (andika sentensi moja
au mbili kwa kila )
• 5. je jinsi mtu anavyo tumia makala yenyewe ni sawa na?
• a) mpangilio wa maneno ya makala? b) mambo ambayo
mwandishi anasema katika kijisehemu? c) kichwa cha kitabu
au sehemu.
• Mifano mitatu:
• 1: zaburi 91:11-12, 2. 1 Wakorintho 3:21 3. Efeso 5:1
Sura ya Nne
Kanuni Ya Yaliyomo
• 1. Katika kanuni hii inatuambia kuwa hatupaswi kupuuza neno hata moja katika
maandiko. Kusudi la kanuni hii ni kuchunguza maana ya maneno binafsi na
mahusiano yake kwa mengine.

• 2. SHERIA TATU ZA KUCHUNGUZA MAANA ZA MANENO.


• A. yatazame maneno unayo tambua huyajui: unayo nafasi ya kutazama
maneno hayo katika kamusi ya biblia pia namna yalivyo tumika sehemu
zingine za maandiko. (Tunguja, Aba, mafarisayo)

• B. chunguza maneno/mafungu ambayo unadhani unayajua: unaweza kuwa


unalifahamu neno lakini bado unahitaji kuchunguza matumizi yake.(maana
ya imani. Rumi 14:23, Gal 1:23)

• C. uliza maswali yatakayo kulazimu kutafasiri na kutumia maandiko wakati


unaposoma: msomaji anapaswa kujiuliza kila wakati hii ina maana gani.
Sura ya Nne
Kanuni Ya Yaliyomo
• CHAMBUA UHUSIANO WA MANENO:
• A. bainisha majina na vitenzi katika sentensi.
• Majina: mtu-paulo, mahali-palestia, kitu-hekalu. (tafuta majina; Yn
12:35, Mk 9:19)
• Vitenzi: yapo majina mengine hutumika pamoja na vitendo. Kazi yake
ni kuonyesha vitendo. Mfano (Yesu alikitwaa kikombe, Kornelio
aliomba)
• Huonyesha pia uhusiano: (Yesu ni Bwana, tulikuwa tu wenye dhambi)
• B. kuunda sentensi za gari moshi. Unahitaji kuwa na “jambo linalo
zungumziwa “subject” pamoja na kitendo ili kuunda muelekeo. Jambo
linalozungumziwa pamoja na kitendo huvuta maneno mengine. Tuna
hitaji marafiki saba waminifu (nani, vipi,gani, nini, wapi, kwanini, lini)
Sheria Mbili Wakati Wa Kuuliza Maswali Ili
Kujua Jambo Linalo Zungumziwa Na Kitenzi
• Sheria 1: “Nani” au “Nini” hutumika kutaka
kujua jambo linalo zungumziwa. Hawa ndio
marafiki wawili watakao kusaidia kutambua
jambo linalo zungumziwa.

• Sheria 2: “Vipi” “Gani” “Wapi” “kwanini” au


“Lini” haya ndio maswali yatakuongoza
kutambua sehemu ambayo siyo jambo linalo
zungumziwa.
SURA YA TANO
KANUNI YA URAHISISHAJI
• Kutafasiri mistari ya maandiko katika hali rahisi iwezekanavyo peke
yake. Kupambanua lugha ya kawaida au ni ya mafumbo inayotumika.

• 1. Lugha ya kawaida: ni lugha isiyo na mafumbo wala kumaanisha


kitu kingine. (Mtend 20:7-12) hakuna maana ya ziada ya , chumba
cha orofani, taa, dirisha, usingizi mzito , maneno haya hayawakilishi
chochote. Kitu cha pekee hapa ni uponyaji wa Eutiko.
(japo kutumia kifungu kama mfano inakubalika) lakini usiseme
ndio maana ya muandishi.

2. Lugha ya Mafumbo: ni makosa kulazimisha tafasiri za kawaida katika


lugha ya mafumbo. (nikodemu; Yn 3:3, msamalia Yn 4:10; Yn 6:48; Mt
26:26.
SURA YA TANO
KANUNI YA URAHISISHAJI
• AINA ZA LUGHA YA MAFUMBO.
• 1.mifano na mafumbo: katika mfano kuna kuwa na funzo kuu moja la kiroho,
japo sehemu zingine zinaweza kutumika kama mfano (msamaria mwema,
somo ni jirani yangu ni kila mtu). Fumbo linakuwa na kweli kadhaa na mengi ni
viwakilishi (mfano; mchungaji mwema Yn 10; malango, mgeni, kondoo,
mchungaji, mwizi, mtumishi, mbwa mwitu)

• 2. methali na mifano ya maneno: kazi ya hizi ni kulinganisha kitu kimoja na


kingine mara nyingi hutumia neno “kama” Mt 13:33, mfano wa maneno
hulinganisha kitu kimoja na kingine bila kutumia neno “kama” Yn 6:35.
• 3. maneno yanayo ongeza chumvi: lengo ni kufanya hoja kuwa wazi na kuwa
ya kukumbukwa daima (Mt 23:24; Mt 19:24, Yn 21:25)

• 4. kufanya kanakwamba ni mtu: kupatia uhai vitu visivyo na uhai; (Mt


6:36,Zab 147:12) hapa “kesho” inatumika kama binadamu.
SURA YA SITA
KANUNI YA UPATANO
• 1. Huwezi kutumia andiko moja tu kujenga hoja inayo simama vyema. (mfano wa
kiti cha mguu mmoja). Unahitaji maandiko mengine yanayo sema kuhusu hoja unayo
shughurikia.

• Ukitumia andiko moja tu unaweza kupata dhana zisizo sahihi kama vile:
• Usiwahubirie wamataifa bali wayahudi tu (Mt 10:5) usibebe pesa/ nenda bila viatu
(Mt 10:27) watemee watu mate kabla hujawaombea (Mk 8:23)

• 2. MUWEKE PUNDA MBELE: hatuchagui yale tunayo penda tu kuhubiri,; isome biblia
kwa makini juu ya yale unataka kuzungumzia.
• Ukiamua yale unataka kuhubiri kisha kwenda kutafuta mistari ya Biblia kuunga mkono
mahubiri yetu, nisawa na kuweka gari mbele ya punda.

• (mfano: Branham: aliomba usiku kucha akapata wazo kuwa hakuna utatu bali Yesu
pekee, aliweka gari mbele ya punda, alipata wazo kisha kwenda kutafuta maandiko ya
kumuunga mkono wazo lake. Alipata tu Yn 14:9; na hakuwaza kuhusu Yn 14:1, Yn
14:21; 23; 24; 25-26) lazima kutafasiri maandiko kwa upatano wa maandiko
mengine
SURA YA SITA
KANUNI YA UPATANO
• 3. TENA IMEANDIKWA: (Mt 4:5-7) tunapo toa maandiko kwenye Biblia
iwe kwa kusudi la kutoa muangaza, shetani alitumia “imeandikwa
kutaka kumuongoza Yesu gizani.

• Kristo hakupinga mstari ule wa Ibilisi bali alihitaji kumuonyesha mstari


mwingine unaopatana na huo kwakumwambia pia “imeandikwa”

• (mfano: imeandikwa Lk 2:14; Mt 10:34- upatano ni Yesu alikuja kuleta


amani kwa kila atakaye mpokea sio kwa wanao mkataa, kumpokea
kutafanya watu kutuchukia)

• (Yn 9:39—Yn 12:47; alikuja kutafuta na kuokoa, lakini wanao mkataa


wata hukumiwa)
SURA YA SABA
KANUNI YA MAAGANO
• 1. Sheria Ya Agano La Kale Ni Sehemu Ya Agano: (agano ni mkataba baina ya makundi
mawili) ni mkataba wa pande mbili na kuna sheria ambazo pande zote mbili
wanatakiwa kukubaliana.
• Agano la kale: ilikuwa ni makubaliano kati ya Mungu na Israeli (amri zaidi ya 600
Kut 20- kumb 33)

• 2. Agano La Kale sio Agano letu: ilikuw kati ya Israeli na Mungu, wakristo
hawapo chini ya sheria ya kale (Rum 6:14, Yn 1:16-17, Gal 5:4): Yesu hakuja
kuharibu sheria ila kuitimiza, alikuja kutupatia haki kwa neema badala ya
matendo. Agano letu sio la kale bali jipya pamoja na Mungu (Rum 10:4)
• 3. Baadhi ya Masharti ya Agano la Kale hayafanywi upya katika Agano
Jipya: sheria ya agano la kale (1. utaratibu wa ibada 2. sheria za jamii)
zinapatikana katika vitabu vya walawi, kutoka, kumb, hesabu. Rangi gan?
Mavazi gani? Sadaka gani? Haya maswali yote yange jibiwa na sheria hii ya
utaratibu wa ibada. Chakula, hekalu , ukuhani na sadaka katika agano jipya
yame badilishwa kabisa. (1 Tim 4:1-5)
• hata sheria za jamii, ambazo zilikuwa zina simamia mahusiano katikati ya
mtu na mwenzake ni tofauti sana kwa sasa. (hutumpigi mzinzi mawe)
SURA YA SABA
KANUNI YA MAAGANO
• 4. Kanuni Za Maisha Maadilifu Za Agano La Kale zimerudiwa Upya Katika
Agano Jipya: tumekwisha angalia kuwa katika (Mathayo 5:17-20) Yesu hakuja
kuharibu sheria.
• Lakini: Yesu anasisitiza kanuni kuliko amri yenyewe kwakuwa kila amri ilikuwa
na kanuni nyumba yake:
• 1. katika amri ya kuua yeye alisema ni makosa kuchukia (Mt 5:21-24) 2.
Amri ya kuzini akasema tamaa ni mbaya (Mt 5:27-30) 3. katika amri ya viapo
alienda zaidi na kusema tutekeleze tuliyo ya ahidi (Mt 5:33-37)
• Neema haiondoi amri juu ya maadili na tabia, bali inaangazia kanuni iliyo
ndani ya sheria.

• 5. Agano la kale sio Amri ya Mungu kwetu, lakini ni chimbuko la mafundisho


kwetu: zipo amri kwenye Ak Mungu aliwapatia wapi na sisi haitutaki kuzitii
lakini inatutaka kujifunza kitu hapo (mf; Nuhu kujenga safina: Mwanzo 6:14)
• Tuna hitaji agano la kale kuelewa agano jipya; kwakuwa limerejelewa zaidi
ya 1100.
SURA YA SABA
KANUNI YA MAAGANO
• 6. Ahadi Katika Agano Jipya Ni Tofauti Lakini Bora Zaidi Kuliko A hadi
Za Kale:
• Katika agano la kale walitakiwa kutii sheria 600 na hawakuweza kutii
hivi walikataliwa (Ebr 8:9)
• Katika agano jipya Mungu ameahidi kutukubali kupitia imani yetu kwa
Kristo na hii ni ahadi kubwa zaidi ya hii ya kukubalika kwa kupitia kwa
kuzitii sheria 600.
• Katika agano la kale ana ahidi kanaani lakini katika jipya ana ahidi
mbingu.
• Aliwaahidi watawashinda adui zao , lakini katika agano jipya anasema
tunaweza kuonekana dhaifu lakini tuzaidi ya washindi. (Rum 8:36-37)
• Aliahidi mafanikio ya kifedha hapa duniani, yeye ametuambia tuwarithi
pamoja na Kristo.
SURA YA NANE
KANUNI YA UFALME
• Kusudi la kanuni hii ni kutofautisha hali iliyopo na hali ijayo ya ufalme wa
Mungu.
• 1. Ufalme wa Mungu ulianza lini?: tunajifunza tangu mwanzo kabla hata ya
uumbaji Mungu alikuwa ameshatawala.
• Nyakati za agano la kale: ulikuwa utanguliza wa ufalme wa Mungu (kupitia
kwa wafalme na manabii) mpango wa huu ufalme ukuwa kwanza kwa
wayahudi lakini waliukataa (Mt 8:11-12)
• Ufalme wa Mungu uliingia pindi Yesu alipokuja duniani. (Yohana alikuja
kuandaa njia. Mt 3:2)
• 2. Mahusiano ya Ufalme wa Mungu na ufalme wa Mbinguni: Agano jipya
inasema kuwa ni kitu kimoja, ilibadilishwa “mbingu na Mungu”(Mt 8:11;
Lk 13:28-29, Mt 11:11, Lk 8:28, Mt 13:11, Lk 8:10)
• 3. ni kwa namna gani ufalme wa Mungu “upo tayari lakini “bado” haupo?.
Ufalme ulikuja na Yesu tayari, lakini bado hauja kamilika.
SURA YA NANE
KANUNI YA UFALME
• 1. Wokovu: wakati uliopita (tulikuwa wenye dhambi) wakati uliopo (utakaso
unaendelea) wakati ujao (pindi hatutakuwa katika mwili wa dhambi).

• 2. ufahamu wetu: tunafahamu kwa sehemu tu lakini tuna utazamia ukamilifu


katika ufahamu (1 Kor 13:12)

• 3. thawabu: tunabarikiwa hapa duniani lakini baraka ya kuketi na Bwana


mbinguni bado twaingoja (Mt 19:27-29, Ufu 22:12)

• 4. Afya: tuna lindwa na kupokea uponyaji (Yko 5:15) lakini bado miili yetu ni
dhaifu, lakini katika utimilifu wa ufalme huo hapatakuwa na huu udhaifu (ufu
21:4)
• 5. Mali: yeye hushughurikia mahitaji yetu (Mt 6:33) ukristo sio njia ya kujipatia
utajiri (1 Tim 6:5) utajiri tunao ahidiwa ni wa zaidi ya haya ya dunia (Lk 8:14)
SURA YA NANE
KANUNI YA UFALME
• 6. Mateso: kwa kiasi fulani baada ya kumpokea Kristo kwa kiasi fulani tunapata pumziko, lakini huu
ufalme ulikuja na mateso mapya (Mt 10:34 kuchukiwa) pia katika kupewa nidhamu na yeye kuna
mateso (Ebr 12:5-6) lakini kuna wale watakao vumilia mateso hadi mwisho nao wataponywa (Mt
24:13; Ufu 12:11)

• 7. Ulinzi: mara nyingi tunaona wazi wazi ulinzi wa Mungu kwetu, lakini hakuna mahali imeahidiwa
kuwa kwa wakati huu nguvu ya uharibifu haitakuwepo kabisa. Lakini katika wakati ujao Mungu ana
ahidi ulinzi (Isa 54:17)

• 8. Hukumu ya waumini: hata saa waumini wana hukumiwa (Yn 15:2, 1 Kor 11:30) lakini haitaishia
hapo bado ipo itakayo kuja (2 Kor 5:10)
• 9. Hukumu ya wenye dhambi : hata sasa huku yao tayari wameshatenganishwa na Mungu, pia
kuna matokeo ya dhambi zao kama hukumu ya dhambi. Lakini huku kuu inakuja (Ufu 20:12-13, Lk
16)

• 10. Hukumu ya shetani: shetani alishahukumiwa kwa kutupwa chini (Lk 10:18b-19) lakini pia
Kalvari alihukumiwa (Yn 12:31) lakini bado hajahukumiwa jumla (Efe 2:2) amehukumiwa kwa
kiwango fulani (Eze 28:11-19)
• 11. Mapenzi ya Mungu: ufalme wa MUNGU upo na kwa kiasi fulani mapenzi yake yapo lakini
hayajakua kwa ukamilifu ndio maana bado tunaomba (Mt 6:10)
SURA YA TISA
KANUNI YA MIFANO
• Tambua somo moja katika mfano: tambua muktadha wa kihistoria na
milima ya hoja za mafumbo.
• 1. ASILI YA MIFANO: ilikujua asili ya mifano lazima tujibu maswali ya
fwatayo.
• A.mfano ni nini?: ni hadithi fupi, rahisi na yenye maana ya kiroho. B.
kwanini Yesu alifundisha kwa mifano:
• 1. kwa sababu ya usalama: kwakuwa alikuwa aki laani mafarisayo na
wenye mamlaka alitakiwa kutumia lugha ambayo wasingeweza
kumshitaki. 2. alihitaji kufananisha ukweli: njia nzuri ya kujifunza ni
kuhusisha kitu na kingine, ukweli mpya unapaswa kujengwa juu ya
ukweli wa zamani. 3. kwa sababu inashinda pingamizi za watu: mfano
alio pewa Daudi na Nathani ilikuwa njia ya kumfanya Daudi asiwe na
pingamizi pindi atakapo ambiwa makosa yake. (2 sam 12:1-4) 4.
alifundisha kwa mifano kama aina ya hukumu: waliifanya mioyo kuwa
mizito, walipewa neno lakini hawakutaka kusikia kanuni ya mbinguni ni
“tumia au uipoteze” (Mt 13:10-15)
SURA YA TISA
KANUNI YA MIFANO
• C. Jinsi Wengine Wanatumia Mifano Kwa Kuifanya Kuwa Mafumbo (Kuifanya Iwe
Ya Kiroho Zaidi): kufanya mfano kuwa fumbo ni kosa kubwa sana, usifanye mfano
kuwakilish mambo tunayo fikiria.
• Hatua tatu za kutafasiri Mfano:
• A. Bainisha muktadha wa kihistoria wa Mfano: tambua hali ya asili ya huu mfano
kutolewa (jibu maswali; Yesu aliwatolea mfano kina nani, na kwanini aliutoa huo
mfano: katika mfano wa msamari (Lk 10:25-37) alimtolea nani= mwalimu wa
sheria, kwanini aliutoa: mwanasheria alikuwa akimjaribu Yesu, pia alitaka
kujihakikishia mwenyewe.
• B. Tambua milima michache ya hoja za mafumbo katika mfano: mfano katika
mfano wa “Msamaria mwema” kuna milima mitatu ya hoja: 1.mtu aliye jeruhiwa
(akiwakilisha wale wenye mahitaji) 2. Msamaria mwema (akiwakilisha jirani
anayejali) 3. kuhani na mlawiiiii (wakiwakilisha majirani wasio jali).
• C. Tambua somo kuu linaloelezwa na Mfano: usitafute somo zaidi ya moja katika
mfano. Katika “msamaria mwema” somo ilikuwa “kuwa jirani mwema kwa wale
walio na mahitaji”
SURA YA TISA
KANUNI YA MIFANO
• Tofauti ya kutafsiri na kutumia Mifano: kutafasiri mfano ni
kueleza maana yake, baada ya kutafsiri mfano mhubiri au
mwalimu anapaswa kuutumia.
• Mfano: “Msamaria mwema” mhubiri/mwalimu anapaswa
kutumia somo la mfano huu, kwa kugusia wa watu wenye
shida. Walio poteza mali zao, Wakristo wanatakiwa kuwa
majirani wema kwao.
• kufanya mfano kuwa fumbo ni hatari kwa sababu
hakuonyeshi maana asilia ya ujumbe ambao Yesu
alifundisha.
• Usifanye kuwa fumbo, tafasiri kwanza mfano kisha tumia
makala yenyewe.
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII
• Lengo ni kutafsiri unabii kwa roho ya
unyenyekevu, kwa kuzingatia muktadha wa
kihistoria,lugha ya mafumbo na sheria ya
utimilifu kwa wingi.
• vitabu na vifungu kuhusu unabii ni baadhi ya
sehemu ya Biblia ambazo ni vigumu sana
kuelewa.
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• KAZI NA HUDUMA YA NABII.


• -Mnenaji aliyewakilisha sauti ya Mungu
• -Nabii alingojea mpaka neno la Bwana lilipomjia.
• -Baada ya kupokea neno, huja mbele za watu na kutangaza
kile Bwana alimwambia “Ndivyo asemavyo Bwana”
• -Nabii aliwasaidia watu kutabiri (Isa 9:6) na kutangaza
mambo kwa wakati uliopo (2 Sam 12:7)hatakama ni jambo
la wakati ujao nabii hutangaza kama ni jambo la wakati huu
kuonyesha uhakika wa jambo hilo.
• =Madhumuni: kuwasaidia watu kumjua Mungu na mapenzi
yake kwao. pia ni kujenga, kuhimiza, na kufariji (1 Wak 14:3)
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• MIONGOZO MITANO YA KUTAFSIRI UNABII


• A. Bainisha muktadha wa Kihistoria wa Unabii
• -hatuna kitabu cha unabii kutoka (1800 kk. Ibrahimu- hadi
1000kk. Daudi)
• -vitabu 16 vya unabii vya Agano la Kale viliandikwa kati ya
760 na 460 KK. katika ya miaka hii kulikuwa na mabadiliko ya
kisiasa,kiutawala,kiuchumi na kijamii.
• -kulikuwa na ukosefu wa utii wa sheria ya musa na agano,
watu walikuwa wanahamahama, na mipaka ya kitaifa
ilikuwa inabadilika.
• -hivyo Mungu aliwainua manabii na walitoa unabii kwa
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• Ilituweze kuelewa vitabu vile 16 vya unabii katika


Agano la Kale, unahitaji kuelewa kwa undani
muktadha wa kihistoria. ili kuubainisha muktadha wa
kihistoria jiulize maswali haya:

• 1.Unabii ulitolewa kwa kina nani (Israele au Yuda)?


• 2. Unabii ulitolewa lini (kabla au baada ya utumwa)?
• 3. Unabii ulitolewa kwa nini (ulikusudia kuwaonya
watu, kutubu, au ulikuwa ni ujumbe wa kutia moyo)?
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• B. Tambua Lugha Ya Mafumbo Katika Unabii


• -kuna wakati unabii unapaswa kutafsiriwa kwa lugha ya mafumbo.
(vifungu vingi katika Danieli, Ezekieli na Zakaria vimejaa lugha ya
mafumbo pia Ufunuo katika Agano Jipya)
• -katika ufunuo kuna mafumbo ambayo hayawezi tafsiriwa kawaida lazima
yatafsiriwe kama mafumbo. Mfano wa Msomi fulani wa Agano Jipya.
• -nyota 7 (1:16)= malaika 7 (1:20)
• -vinara 7 (1:13)= makanisa 7 (1:20)
• -mana iliyofichwa (2:17)= Kristo katika utukufu (Ebr 9:4)
• sio kila mtu anakubaliana na maana hizi za mafumbo haya. lakini jambo la
muhimu katika kutafsiri lugha ya mafumbo na mifano ni kulinganisha
vifungu na sehemu zingine za maandiko, mifano mingi ya Ufunuo
inapatikana sehemu nyingine za maandiko hasa katika Agano la Kale.
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• C. Amua Ikiwa Unabii Utatimia Kwa Kawaida Au Kwa Mafumbo.


• 1. Kutimizwa kwa kawaida hakubadiliki.
• -Mika alitoa unabii kwamba Masiya angezaliwa Bethlehemu (Mika
5:2) unabii huu ulitimizwa kwa kawaida neno kwa neno. hapakuwa na
lugha ya mafumbo, Bethlehemu ilikuwa na maana ya Bethlehemu.
• 2. Unabii unaweza pia kutimizwa kwa mafumbo.
• -huu unabii hutimizwa katika picha kubwa (Mfano: shati na Koti)
Mfano: Malaki anatabiri ujio wa Yohana kama nabii Eliya.(mal 4:5-6)
miaka mia nne baadae Yohana alianza huduma yake. lakini hata yeye
Yohana hakukiri kuwa yeye ni Eliya (Yn 1:21) pia Yesu anazungumzia
huu unabii (Mt 17:10-13)
• -huu ni unabii uliotimizwa kwa mafumbo (Lk 1:17) Eliya alikuja kweli
kwa lugha ya mafumbo (yani nabii aliye kuwa na uwezo kama Eliya)
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• D. Bainisha Ikiwa Sheria ya Kutimia Kwa Wingi inatumika.


• -unabii unaweza kutimizwa kwa hatua kadhaa, au kwa zaidi ya mara
moja (sheria ya kutimia kwa wingi) Mfano: Isaya alitabiri- (Isa 9:6)

• -katika unabii wa Isaya tunaona kuwa ulikuwa wa kutimia kwa hatua;


wakati mtoto anazaliwa uwezo haukuwa mabegani mwake na
hautakuwa begani mwake mpaka atakapokuja “mara ya pili” hivyo
sheria ya kutimia kwa wingi inatumika katika unabii huu.

• -Manabii hawakufunuliwa zaidi katika kuja kwake mara ya pili


walizungumzia tu Masiya kuja na kuteseka .
• Mfano: Hosea 11:1, Mathayo 2:15 (katika Mathayo andiko linaonyesha
utimilifu wa unabii)
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• E. Onyesha Roho Ya Unyenyekevu Unaposoma


Unabii.
• -katika kutafsiri unabii tunahitaji sana kuwa
wanyenyekevu kwakuwa niwazi yapo mengi ambayo
hata kwa kutumia mbinu na kanuni za kibinadamu
hatuwezi kufunua siri za Mungu.

• -ogopa sana kuto onyesha hali ya mashaka katika


kutafsiri baadhi ya sehemu ngumu za maandiko.
usilisemee neno.
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• Muhtasari
• Muhtasari wa miongozo mitano, kwa kutumia mfano wa Mathayo 24:4-8
• A. Muktadha wa Kihistoria
• jibu maswali haya.
• 1. ulitolewa kwa kina nani? kwa wanafunzi
• 2. lini? muda mfupi kabla ya kusulubiwa
• 3. kwanini? Yesu alikuwa amesema hekalu litabomolewa, wanafunzi
wake waka muuliza itakuwa lini, ipi dalili ya kuja kwako, na mwisho wa
dunia (Mt 24:3) hivyo alitoa unabiii kujibu maswali yao.
• B. Lugha ya mafumbo.
• -”uchungu wa kuzaa” hapa Yesu analinganisha wakati dhiki na utungu
wa mwanamke akizaa. hapa ni kuwa dhiki za 24:4-7 zinaonyesha dalili za
mwanzo wa wakati hup.
SUYA YA KUMI
KANUNI YA UNABII

• C. Amua Ikiwa Unabii Utatimizwa kwa kawaida au kwa


Fumbo.
• -sisi tunao amini kutawala kwa Kristo kwa miaka elfu
tunatarajia kutimia kwa hali ya kawaida.
• D. Tambua Ikiwa Sheria Ya Kutimia Kwa Wingi Inatumika.
• -kwa hali fulani inatumika kwakuwa Kristo wa uongo, vita,
njaa na mitetemeko ya ardhi kwa vizazi vingi tangu wakati
wa Kristo imedhihirika.
• E. Dhihirisha Roho ya Unyenyekevu Unapotafsiri Unabii.
• -hatuwezi kukubaliana na kila mtu katika kuyasoma na
kuyaelewa maandiko hivyo inataka unyenyekevu.

You might also like